Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

HOJA YA MDAU: Amri ya Rais JK kuhusu Wahamiaji Haramu nchini lazima ifanyiwe kazi haraka

$
0
0
Kwanini ? Vibali vyote vya kuishi wageni visifutwe na kusajiliwa upya.
Msako lazima uwe na kasi kubwa tena uanzie mji mikubwa kama Dar,Arusha...

Kuanzia mwezi julai 2013 kiongozi mkuu wa nchi yetu rais Dk.Jakaya Kikwete katoka agizo kuwa raia wote wa kigeni ambao ni wahamiaji haramu wamepewa siku 14,kuondoka au kujisalimisha katika vyombo vya dola.

Agizo hili la rais lina lengo zuri tu kwa watanzania na usalama wa watanzania,lakini utekelezwaji wake umekuwa hauna kasi,kwani idadi ya wahamiaji haramu walio jisalimisha ni ndogo kulingana na waliopo nchini,na kati ya hao walijisalimisha ni wahamiaji waliopo nje ya miji mkubwa sio katika miji mikubwa kama Dar ,Arusha na
kwingineko !

Cha kushangaza kwamba kuna baadhi ya wahamiaji haramu au halali wanakiuka kwa namna moja au nyingine sababu zinazowafanya kuwepo nchini Tanzania.

mfano raia wa kigeni aliyekuja nchini kwa kufanya kazi fulani na akapewa kibali kwa ajili hiyo anakiuka kwa taratibu za uhamiaji na kuanza kuwa mfanyi biashara ya baa au dangulo fulani! au pengine kujiingiza katika biashara ambayo mzawa anaweza kuifanya, na huku vyombo vya usalama vikimwangalia !

Hivi kuna uhalali wa kisheria Raia wa kigeni asiye na hata asili ya Tanzania kumiliki nyumba au Ardhi ?

Watanzania wengi wamekuwa wakilalamika juu ya ongezeko la raia wa kigeni hususan raia wa nchi za ulaya,Asia na nchi za kiarabu kumiliki au kununua nyumba na ardhi nchini ,mfano wachina wanamiliki majumba au ardhi uenda wakawa wanakiuka sheria fulani za nchi,na watanzania wanao wauzia nyumba wageni hao nao pia wanajisaliti au kuisaliti nchi.

Ukiwikaji wa sheria za ajira ! mchina anapofanya ya kuuza duka na mitumba au kubeba zege !  Mzungu anapokuja kutalii na baadaye 
kupata ajira ya muhudumu wa hotel ! hili nalo neno?
Bendi za muziki zinapo ajiri wanenguaji kutoka nje ya nchi!

Ndio maana watanzania walio wengi wanaona kuwa hipo haja kwa serikali
kuvifuta vibali vyote vya wageni na kuanza zoezi la kuvitoa upya na kuvihakiki kwa kupitia Wizara ya mambo ya ndani.

Kama Rais JK kesha toa agizo tangu mwezi julai mbona utekelezaji wake
una mwendo wa pole ? wakati kiongozi mkuu wa nchi,ambaye ndiye amri
jeshi mkuu kishaagiza siku 14 tu kila muhamiaji haramu aondoke sasa
tena msako kwanini? usianze katika kutekeleza agizo la mkuu wa nchi.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Mbariki Rais JK

Waziri Mkuu Pinda afanya ufunguzi wa maonysho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China leo jijini Dar

$
0
0
Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kulia) akikata utepe leo kuashiria ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo waweze kufanya biashara na watanzania. Kulia kwa waziri mkuu ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na kushoto kwake ni Balozi wa China nchini LV Youqing.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alijaribu jembe la kupandia nafaka wakati alipotembelea banda la kiwanda cha Qingyuan Manchu Autonomous County cha nchini China wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.Wanaomtazama ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda (kushoto) na Balozi wa China nchini LV Youqing (kulia).
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia malighafi zinazotumiwa na kampuni ya Beijing New Building Material kutengenezea nyumba alipotembelea banda hilo leo wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara ya Kimataifa wa Kampuni hiyo Alec Lu na wapili kulia ni Makamu Meneja Mkuu Fred Yu.
Mfanyakazi wa kiwanda cha Changzhou Amec Group cha nchini China Yan Xing Long (kulia) akimueleza Waziri Mkuu Mizengo Pinda jinsi mashine ya kuchanganya kokoto iliyotengenezwa na kiwanda hicho inavyofanya kazi wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia mfano wa nyumba zinazojengwa na kampuni ya Beijing New Building Material alipotembelea banda hilo wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na watatu kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara ya Kimataifa wa Kampuni Alec Lu.
Baadhi wa watu mbalimbali walioshiriki ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne ambayo yamefunguliwa leo yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo yaweze kufanya biashara na watanzania.Picha na Anna Nkinda – Maelezo

Article 6

TAARIFA MBALIMBALI TOKA TFF LEO Septemba 10, 2013

$
0
0
KIMONDO KUCHEZA MBOZI, KURUGENZI WAMBI FDL
Timu za Kimondo SC ya Mbeya na Kurugenzi ya Mafinga zitatumia viwanja vya Mbozi na Mafinga kwa ajili ya mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoanza Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).
 Kimondo SC sasa itatumia Uwanja wa CCM Vwava ulioko wilayani Mbozi badala ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wa jijini Mbeya. Nayo Kurugenzi itatumia Uwanja wa Wambi ulioko Mafinga mkoani Iringa badala ya Uwanja wa Makambako ulioko mkoani Njombe.
 Mechi za fungua dimba FDL msimu huu zitakuwa kati ya Burkina Faso na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro, Mkamba Rangers na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, Majimaji na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na Kimondo na Kurugenzi kwenye Uwanja wa CCM Vwawa katika mechi za kundi B.
 Septemba 14 mwaka huu Tessema na Green Warriors zitaoneshana kazi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Siku inayofuata (Septemba 15 mwaka huu) Transit Camp na Polisi Dar (Mabatini mjini Mlandizi) wakati mechi nyingine za kundi hilo la A zitakuwa kati ya Villa Squad na African Lyon (Karume) na Ndanda FC na Friends Rangers (Nangwanda Sijaona, Mtwara). 
Kundi C ni Polisi Mara na Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United na Mwadui (Kambarage, Shinyanga) wakati Pamba na Toto Africans zitamenyana Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

 PONDAMALI AFUNGIWA MIEZI 3, FAINI MILIONI 1/-
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini ya sh. milioni moja na kumfungia miezi mitatu kocha wa makipa wa timu ya Coastal Union kwa kuwatukana washabiki wanaominika kuwa wa Simba.
Pondamali alifanya kosa hilo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu yake na Yanga iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
 Mwamuzi Martin Saanya na mwamuzi msaidizi namba moja Jesse Erasmo waliochezesha mechi kati ya Yanga na Coastal Union nao wamefungiwa mwaka mmoja kila mmoja kwa kutoimudu mechi hiyo.
 Nayo Yanga imepigwa faini ya sh. milioni moja (sh. 500,000) kwa kila kosa kutokana na washabiki wake kuwarushia waamuzi chupa za maji baada ya Coastal Union kusawazisha bao katika mechi hiyo. Pia waliwarushia chupa waamuzi hao wakati wakirejea vyumbani baada ya pambano hilo. 
Vilevile Coastal Union imepigwa faini ya sh. 100,000 baada ya kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting). Timu hiyo ilichelewa kwa dakika 23. Kikao kinatakiwa kuanza saa 4 kamili asubuhi.

TEMEKE YAIZAMISHA RUKWA 5-1 COPA COCA-COLA
Temeke imejiweka katika nafasi nzuri ya kucheza robo fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo (Septemba 10 mwaka huu) asubuhi kuizamisha Rukwa mabao 5-1. 
Hadi mapumziko katika mechi hiyo ya kundi B hatua ya Fainali za Taifa iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam, washindi walikuwa mbele kwa mabao 3-0.
 Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Constantine Katepa aliyefunga dakika ya 28, Patrick Ambrose dakika ya 36 huku Hamisi Kajole akipiga mawili dakika ya 43 na 71. Bao la nne lilifungwa dakika ya 46 na Ramadhan Juma.
 Rukwa ambayo kwa matokeo hayo imeshatolewa ilipata bao lake dakika ya 51 kupitia kwa Francisco Nkanga. Timu nyingine katika kundi hilo ni Geita na Ilala. 
Robo Fainali ya michuano hiyo itaanza keshokutwa (Septemba 12 mwaka huu). Kila kundi linatoa timu mbili kucheza hatua hiyo katika mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Coca-Cola.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

safarihub launched in London to promote Tanzania's tourism abroad

$
0
0
Safarihub is a UK based travel company with the main objective to make Tanzania the prime destination for tourists travelling to Africa. 
Being one of the few Tanzanian tour operators to have an office in London, Safarihub considers this as a major advantage for actively and effectively promote  Tanzania's touristic marvels throughout Europe  by easily accessing exhibitions and potential customer bases. Safarihub's future plans are to open offices in Asia, America and UAE. 
The company has been founded by London based Tanzanian business man Navraj Hans who has partnered with British investors Chris Riley and Dilip Navapurkar. 
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe was full of praise for Safarihub during its official launch last Friday, he emphasised on the importance of promoting Tanzanians touristic assets on an international level “Tanzania is the crown jewel of Africa, and more has to be done to promote this splendid country”.
Said Navraj Hans: "This is a new business which help promote Tanzania as a leading tourist destination by actively marketing in the UK and Europe. 
"We are looking to becoming  one of the leading Tanzanian safari providers in Europe by 2015, our website is 
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe pose for a group photo with the Safarihub company members during the launching ceremony in London. Others are Navraj Hans (second right) who has partnered with British investors Chris Riley(left)  and Dilip Navapurkar (second left). Right is an ogfficial from the Tanzania High Commission in London
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe is shown some of the many promotional material lined up by Safarihub company
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe cuts a ribbon to officially launch Safarihub Company in London
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe shakes hands with Mr Navraj Hans as his British partners Chris Riley (right)  and Dilip Navapurkar look on. 
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe inaugurates Safarihub
Tanzanian's High Commissioner to the UK Ambassador Peter Kallaghe congratulates Mr Navraj Hans during the brief ceremony

Canaco scoop Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment Awards

$
0
0
The Acting Commissioner for Minerals, Eng: Ally Samaje (left), presenting the award on behalf of the President HE Jakaya Kiwkete to President and Chief Geologist of Canaco Tanzania Limited, Denis Dillip at the Ministry of Energy and Minerals in Dar es salaam. At the center is the board chairman of the company, William Haji. 
Canaco emerged the First Winner of The  Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment  Awards in Tanzania on the category of  Mineral and Petroleum Exploration Projects.
The award ceremony which was presided by President Kikwete, was organized by the Ministry of Energy and Minerals through the Extractive Industries Stakeholders Forum (EISF).  The Extractive industry companies were classified in four categories; Large scale mining, Medium scale mining, Oil and gas companies and Exploration (minerals, oil and gas)  companies.
The event was hosted by Tanzania Ministry of Energy and Mineral and was held at Hyatt Hotel in Dares Salaam.Commenting on the Award, The President and Chief Geologist of Canaco Tanzania Limited, Denis Dillip said "We are delighted for being the 1st winner on the CSRE awards presented by HE President Jakaya Kikwete. 
"We thank the President, Ministry of Energy and Minerals, Handeni District and other stakeholders for  taking their time to recognising our outstanding efforts toward building a bright community that will continue to benefit from our Gold exploration project specifically Handeni and other coming new projects . 
"We believe such exceptional achievements are within our reach when we stand tall on a foundation of personal integrity, hard work and unwavering determination. Canaco Tanzania Limited and its team stand firm to continue hold this trophy for next coming round."
 Canaco Tanzania Limited emerged the overall winner in their category, however on individual awards the company scooped the following;
  1.          First Winner in Empowerment Programs for the communities.
  2.         First Winner in the Local Procurement Programs for the communities.
  3.          First Winner in Water  Programs for the communities.
  4.          Second Winner in Local Employment Programs for the communities.
  5.          Second Winner in Education Programs for the communities.
  6.          Second Winner in Infrastructure Programs for the communities.

EAC ELECTION OBSERVER MISSION TO THE 16th -18th SEPTEMBER PARLIAMENTARY ELECTIONS IN THE REPUBLIC OF RWANDA

$
0
0
 Kenya’s Former Minister of EAC, Hon Musa Sirma makes arrival statement of the EOM as EAC Deputy Secretary General in charge of Political Federation Hon Charles Njoroge and Hon Abubakar Zein Abubakar EALA team leader looks on
Group photo opportunity, members of EAC Election Observer 

ARRIVAL STATEMENT
 The East African Community is pleased to announce the arrival of its Observer Mission for the Parliamentary Elections in the Republic of Rwanda scheduled to take place on 16th – 18th September 2013.

The Mission is in the country at the invitation of the Government of Rwanda and the National Electoral Commission. It is led by Hon. Musa Sirma, Former Minister for EAC Affair’s, Republic of Kenya and comprises 40 members drawn from the East African Legislative Assembly, Electoral Management Bodies (EMBs)’ Civil Society Organisations (CSOs), and National Human Commissions from 4 EAC countries namely Burundi, Uganda, Tanzania and Kenya. 

The overall objective of the Mission is to promote democracy and governance in the respective EAC Partner States, which includes Rwanda. Specific objectives include:
-    Assess whether the conditions exist for the conduct of parliamentary elections that allow the people of Rwanda to freely express their will;
-    Assess and determine whether the elections are conducted in accordance with the constitutional and legal framework governing elections in Rwanda;
-    Determine whether the outcome of the electoral process as a whole reflect the will of the people of Rwanda; and
-    Assess whether the elections meet the benchmarks set out in the 2002 Durban Declaration on the Principles 

Governing Democratic Elections in Africa by the African Union, the EAC Principles of Election Monitoring and Observation

The Mission’s advance team arrived on 5th September 2013 followed by the rest of the Observers on 9th September 2013. The Missions will remain in the country until 20th September 2013.

The Members of the Mission are attending a pre-deployment training and holding consultative sessions with stakeholders from 10th – 13th September 2013. On 14th September 2013, teams will be deployed to all provinces and districts of Rwanda where they will continue interacting with stakeholders and observe the concluding stages of the election campaign. 
On polling days, Monday 16th to Wednesday 18th September 2013, the EAC observer teams will observe the voting and counting processes at the polling stations. On Thursday 19th 2013, all EAC teams will reconvene in Kigali for debriefing session, after which the Mission will issue an interim statement on its preliminary findings on the electoral process. 

The EAC Election Observer Mission is committed to working closely with all the relevant stakeholders in Rwanda and other election observer groups. They will act in an impartial, objective and transparent manner at all stages of the electoral process.

Issued this 10th of September 2013
Hon. Musa Sirma,
Mission Leader


Katibu Mkuu wa ccm,Ndugu Kinana awakuna wakazi wa kahama kwa hotuba yake,avuna wanachama zaidi

$
0
0
Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea kadi kutoka vyama vya upinzani baada ya wananchi wengi kuridhika na hotuba yake nzuri, katika mkutano huo zaidi ya wanachama 560 wamejiunga na CCM kutoka vyama vya upinzani.


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kahama wakati mkutano wa hadhara uliofanika leo mjini Kahama.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye akiwa na mbunge wa Msalala Ezekiel Maige wakishiriki kucheza ngoma ya wakazi wa Isaka kabla ya kuhutubia kwenye mkutano wa Hadhara.
 Sehemu ya Umati uliofurika kusikiliza hotuba za viongozi mahiri wa CCM, Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye leo kwenye viwanja vya CDT mjini Kahama.

JK azindua miradi ya maji na umeme Sengerema

$
0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Katika kijiji cha Katunguru/Nyamtelela wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe. 
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya utekelezaji wa mradi wa umeme wa MCC unaotekelezwa katika mikoa ya Mwanza na Geita wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilyani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.

 Mwakilishi wa Serikali ya watu wa Marekani Bwana Karl Fickenscher akitoa hati ya kukabidhi mradi wa MCC I kwa waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Katikati akishuhudia ni Afisa mtendaji Mkuu wa Millenium Challenge Account-(MCC)Tanzania Bwana Bernard Mchomvu.
 Mwakilishi wa Millenium Challenge Account nchini Tanzania Bwana Karl Fickenscher akipanda mti wa kumbukumbu muda mfupi baada ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua mradi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambazia umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa,Wilayani Sengerema leo. Kushoto ni Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na kulia ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MMK MEDIA GROUP

$
0
0
Kampuni ya MMK MEDIA GROUP
Inayomiliki SWAHILI TV,SWAHILI RADIO ONLINE, SWAHILITV.BLOGSPOT.COM na DMK11.BLOGSPOT.COM Inatangaza nafasi za kazi kwa watu wa masoko na matangazo.
Wenye uzoefu na wanaojituma.
Maombi ya kazi yatumwe katika 
email
career@mmkmediagroup.com

Katibu Mkuu mpya wa Ofisi ya Waziri Mkuu,Bw. Florence Turuka awasili rasmi kazini

$
0
0
Aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu,Bw. Peniel Lyimo (kushoto) akimtambulisha rasmi Katibu Mkuu mpya wa Ofisi ya Waziri Mkuu,Bw. Florence Turuka alipowasili rasmi Ofisini kwake jana tarehe 10 Septemba, 2013.
Katibu Mkuu mpya wa Ofisi ya Waziri Mkuu,Bw. Florence Turuka (aliesimama) akizungumza na Wakurugenzi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (hawapo pichani) baada ya kuwasili rasmi katika Ofisi hiyo jana tarehe 10 Septemba, 2013.

Baadhi ya Wakurugenzi katika Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza kwa Makini Katibu Mkuu Bw. Florence Turuka (hayupo pichani) alipowasili rasmi kuanza kazi katika Ofisi tarehe 10 Septemba,2013 Asubuhi.

DSE PUBLIC AWARENESS CAMPAIGN FOR THE ENTERPRISE GROWTH MARKET

$
0
0
The Dar es Salaam Stock Exchange (“DSE”) would like to inform the general public that it has established a new segment at the DSE. This new segment, namely the Enterprise Growth Market is meant to facilitate long term capital raising for Small and Medium Enterprises (“SMEs”) in the Country. This program is schedule to run for a period of nine months and will involve the use of various media outlets with the intent to reach into the wider audience for both issuers and investors.

DSE understands that SMEs are considered among the key vehicles for wealth creation and, therefore, have the potential to make substantial contribution towards real economic growth, depending on their growth orientation. The DSEs’ decision to embark on this major campaign hinges on the DSE’s profound role in providing the required long-term financing to the identified feasible (with great potential for growth) projects.

DSE also understand that well nurtured SMEs have a positive impact on the country’s economic development initiatives since their activities are both inclusive and have a wider outreach in creating the multiplier effect in the economy. However, one of the major constraints facing SMEs is access to finance. Therefore, an initiative to provide capital financing solution to SMEs is of utmost importance.

As you are aware, SMEs, due to their nature have unique financial needs. However, so far efforts to provide access to finance by SMEs have focused mainly on commercial banks, microfinance institutions and government/donor funded programs. These funding sources provides mostly short term financing and, in some cases, have not been sustainable. To that effect, SMEs have not been able to obtain long-term funding for growth. There is, therefore, a need to identify additional sources of funds that will provide long term financing.

As one of the key stakeholders in the implementation of the government policy on SMEs, the DSE has worked with other stakeholders to put in place institutional framework in order to address the constraint to long-term financing. Introduction of the Enterprise Growth Market (EGM) on the DSE market segment will serve entrepreneurs and managers of enterprises by facilitating the availability of capital to start or expand their projects.

With is campaign, the DSE will inform entrepreneurs on this window of opportunity and therefore through this, the DSE will be able to have a closer working relationship with the widespread SMEs in the country and can easily share with these entities about the financing opportunity available at the DSE’S Enterprise Growth Market Segment. Through this campaign, existing and potential investors will also be informed on the existence of this new investment opportunity.

WAIGIZAJI KUPEWA MAFUNZO

$
0
0
Mdhamini mkuu wa mafunzo ya Uigizaji na utayarishaji wa Filamu kwa wasanii wa mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na asasi ya TCDA na shirikisho la filamu Tanzania (TAFF) Fredrick Mwakalebela.
=====  =====  ======
WAIGIZAJI KUPEWA MAFUNZO

Na Denis Mlowe,Iringa

SHIRIKISHO la Filamu Tanzania(TAFF) kwa kushirikiana na asasi isiyo ya Kiserikali ya Tanganyika Centre For Development and Advocacy (TCDA) wameandaa mafunzo ya uigizaji na utayarishaj wa filamu kwa wasaniin wa mkoa wa Iringa na maeneo ya jirani.

Akizungumza na Daraja letu mkurugenzi wa asasi hiyo, Jackson Kiyeyeu alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapa upeo na ujuzi zaidi wasanii wa Iringa katika kuweza kuandaa filamu bora na kuwa na ujuzi wa katika uigizaji.

Alisema mafunzo hayo yatakuwa ya mwezi mmoja na yatatolewa na wasanii wakali wa filamu Tanzania akiwemo msanii nguli  Haji Adam maarufu kama Baba Haji akiambatana na walimu wa sanaa kutoka Dar es Salaam.

Kiyeyeu alisema wahitimu wa mafunzo hayo watapatiwa vyeti vinavyotambulikana shirikisho la filamu Tanzania na wasanii bora 10 watapatiwa fursa ya kushiriki filamu ya No Option itakayochezwa na wakali wa Bongo Movie.

“ Mafunzo yatatolewa kwa watu wote kuanzia elimu ya shule ya msingi hadi kidato cha sita na vyeti vitakavyotolewa vitawawezesha kufanya kazi za filamu popote pale Tanzania na ni wakati wa wasanii sasa kuwa na elimu ya ugizaji na utayarishaji wa filamu kuliko ilivyo sasa wengi wao kutokuwa na elimu.” Alisema Kiyeyeu

Mafunzo ya ugizaji na utayarishaji wa filamu yatakakuwa ni mara ya kwanza kwa mkoa wa Iringa yamedhaminiwa na aliyekuwa katibu mkuu wa TFF Fredrick Mwakalebela aliyetoa asilimia 75 ya ada za mafunzo hayo kwa wasanii wa Iringa.

Kwa upande wake Daraja Letu lilipozungumza na Mwakalebela alisema  lengo ni kuwasaidia wasanii wa Iringa kuweza kuwa na ufahamu wa uigizaji na utayarishaji wa filamu bora Tanzania na kuwakomboa vijana katika umaskini.

Alisema sanaa ya uigizaji wa filamu una faida kubwa sana katika kuondokana na tatizo la ajira kwa vijana natoa wito wajitokeze kwa wingi na kuwataka wadau kuweza kuwasaidia vijana katika kuondokana na tatizo la umasikini katika kuwaidia kutimiza ndoto zao.

“Kutokana na kupenda sanaa  na michezo kwa ujumla ameguswa sana na wazo la TCDA kuweza kunipa mawazo yao hivyo sikuwa na budi kuweza kuwadhamini katika hilo nachoomba wadau wengine waweze kujitokeza kuwasaidia wasanii wa Iringa kuweza kutambulika kitaifa na kimataifa katika tasnia ya Filamu.” Alisema Mwakalebela

Alisema Iringa kuna wasanii wengi wanaojitahidi kupambana kwa uwezo wao binafsi kufanya sanaa kwa kile anachofikiria bila elimu ya sanaa ya ugizaji na utayarishaji wa filamu.

Mwakalebela alisema wasanii watakaofanya vizuri katika mafunzo hayo watashirkishwa katika filamu mbalimbali ambazo zinaandaliwa na wasanii wakubwa kutoka jiji Dar es salaam kwa lengo la kuwainua mbeleni waweze kujitegemea.

Dkt. Kawambwa kufungua kongamano la vyuo vikuu Arusha leo

$
0
0
Na Mwandishi wetu,Arusha

Vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu nchini vinatarajia kuhudhuria kongamano la tano la vyuo vikuu linaloanza leo jijini Arusha.

Kongamano hilo la siku mbili limetayarishwa na Kamati ya Makamu wakuu wav you vikuu nchini na wakuu wa taasisi za elimu Tanzania (CVCPT) kwa ushirikiano na wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na wadau wengine wa maendeleo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chuo Kikuu Mzumbe ambacho ndio mwenyekiti wa CVCPT kwa sasa, mgeni rasmi katika ufunguzi wa kongamano hilo anatarajia kuwa waziri wa elimu na mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa.

Mada kuu ya mkutano wa mwaka huu ni jinsi gani vyuo vikuu vinaweza kushirikiana na wadau wengine kama viwanda na makampuni ili kujenga elimu ya juu endelevu Tanzania.

“Mtazamo wa mwaka huu ni jinsi gani taasisi za elimu ya juu zinavyoweza kushirikiana na wadau wengine kama kampuni na viwanda na kuangalia jinsi gani ushirikiano huu unaweza kuimarishwa,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mada hiyo imechaguliwa mahsusi kwa kuzingatia changamoto zinazokabili vyuo vikuu kwasasa hasa jinsi ya kushirikiana na taasisi nyingine kutayarisha wahitimu ambao wako tayari kufanya kazi kwa ufanisi baada ya kuhitimu vyuo vikuu.

Kongamano hilo litawakutanisha wadau wa vyuo vikuu pamoja na wawakilishi wa sekta mbalimbali kwa nia ya kuimarisha mitaala ya vyuo hivyo ili kuwawezesha wanafunzi kupata maarifa yanayotakiwa kwenye soko la ajira.

Kongamano hilo linataka kukumbusha vyuo kuwa vina wajibu mkubwa katika swala zima la utafiti na ubunifu ili kufikia maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kuongeza ushirikiano na sekta mbalimbali.

CVCPT ilianzishwa mwaka 2005.

Wajumbe wa CVCPT ni makamu wakuu wa vyuo vikuu pamoja na wakuu wa taasisi za elimu binafsi na vya umma pamoja na katibu mtendaji wa TCU.

Kama mwenyekiti wa sasa wa CVCPT, Chuo kikuu Mzumbe kimekua kikitayarisha kongamano hilo kwa mwaka wa pili mfululizo sasa.

MSAFARA WA KATIBU MKUU CCM WAWASILI WILAYA YA SHINYANGA VIJIJINI

$
0
0
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ,Mbunge wa Jimbo la Swola ndugu Ahmed Salum na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakicheza na nyoka aina ya chatu wakati wa mapokezi katika kata ya Didia, Luhambo wilaya ya Shinyanga Vijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akisalimiana na wanachama wa chama cha Mapinduzi waliokuja kumpokea alipowasili  Wilaya ya Shinyanga Vijijini.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Ndugu Hamisi Mgeja akisalimia wakazi wa Luhambo Didia wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika wilaya ya Shinyanga Vijijini.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa kata ya Didia na kuwashukuru kwa mapokezi mazuri waliyowapa.

MAKAMANDA TOKA JKT SACCOS WATEMBELEA MAGEREZA SACCOS, JIJINI DAR

$
0
0
Meneja wa Magereza Saccos, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Godfrey Kavishe (wa kwanza kushoto) akiwatembeza Maafisa na Askari toka JKT Saccos katika jengo la Saccos ya Magereza walipotembelea leo Septemba 11, 2013 jijini Dar Es Salaam.
Afisa Mikopo wa Magereza Saccos, Mrakibu wa Magereza Nahman Koko (wa pili kushoto) akiwatambulisha Maafisa na Askari toka JKT Saccos kwa askari Stafu Sajini Naftal Shango(wa kwanza kushoto) anayeshughulika na Usajili wa wanachama walipotembelea Magereza Saccos leo Septemba 11, 2013 jijini Dar Es Salaam.
Meneja wa Magereza Saccos, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Godfrey Kavishe (katikati waliovaa sare) akitoa maelezo ya utangulizi kuhusu Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara kwa Maafisa na Askari toka JKT Saccos walipotembelea leo Septemba 11, 2013 jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya Maafisa na Askari toka JKT Saccos wakiongozwa na Meja Haule (wa kwanza kulia) wakimsikiliza Meneja wa Magereza Saccos, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Godfrey Kavishe (hayupo pichani) wakati akitoa maelezo ya utangulizi kuhusu Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara walipotembelea leo Septemba 11, 2013 jijini Dar Es Salaam (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Abdi K_Mtoto wa kike (Official Video)

BG TANZANIA KUIMARISHA USALAMA BARABARANI MKOANI LINDI

$
0
0
Mhandisi Dk. Ezekial Mganilwa, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (aliyesimama ) anamualika mgeni rasmi Mheshimiwa Saidi Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Mchinga (aliyevaa shati nyeupe). 
Mheshimiwa Saidi Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Mchinga akizindua mafunzo ya uendeshaji Piki Piki huku akimpa mkono Mkuu wa masuala ya Sera na Ushirika wa kampuni ya BG Tanzania, Fred Kiboya
Mhandisi Dk. Ezekial Mganilwa, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji akimpa mkono Mkuu wa masuala ya Sera na Ushirika wa kampuni ya BG Tanzania, Fred Kiboya.
Leo tunashuhudia uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani unaofadhiliwa na BG Tanzania katika mkoa wa Lindi, kusini mwa Tanzania. Baada ya kupewa kazi ya kufanya utafiti kuhusu ajali za barabarani na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), kampuni ya gesi ilibaini fursa za kushirikiana katika kuimarisha maadili ya usalama barabarani miongoni mwa wakazi wa Lindi .

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kilibaini visababishi vinne vya mara kwa mara vya ajali za barabani mkoani Lindi ambavyo ni:waendesha pikipiki wasiozingatia maadili ya uendeshaji; mwendo kasi wa waendesha pikipiki;kuendesha huku umelewa; na ukosefu wa alama au ishara za barabarani. BG Tanzania imeazimia kupunguza kiwango cha ajali kwa kufadhili utoaji wa mafunzo ya usalama barabarani.Hii inaenda sambamba na juhudi za mkoa katika kupunguza ajali za barabarani.

Mkuu wa masuala ya Sera na Ushirika wa kampuni ya BG Tanzania, Fred Kiboya, alihudhuria kwenye sherehe na alisema “Hili ni tukio muhimu kwa BG Tanzania. Kama kampuni tunaamini katika usalama, na tunataka kuhakikisha kuwa, uwepo wetu kusini mwa Tanzania unajenga jamii salama na zenye mafanikio zaidi.Tunaendesha programu ya aina hii Mtwara Mjini, ambapo waendesha pikipiki 600 wanapatiwa mafunzo, na sasa tunarudia zoezi mkoani Lindi.”

Mkoani Lindi, waendesha pikipiki mia mbili watanufaika katika awamu ya kwanza ya programu hii. Kila mmoja atapewa mafunzo ya zaidi ya siku kumi ambapo siku sita zitakuwa kwa ajili ya mafunzo ya nadharia na siku nne zitakuwa kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Hii itajumuisha utambuzi wa alama na ishara za barabarani, nadharia za uendeshaji wa kujihami,uendeshaji unaofaa, mkao sahihi katika uendeshaji na udhibiti.

Baada ya kumaliza mafunzo kwa ukamilifu, washiriki watapewa cheti cha umahiri katika uelewa wa usalama barabarani pamoja na leseni ya uendeshaji. Kundi la washiriki limechukuliwa kutoka katika kata za mchinga, Kitomanga, Rutamba, Nyangao na Milola.

Gharama za mafunzo ni Sh. 220,000/-kwa kila mshiriki,hii ikimaanisha kwamba ,kwa ujumla, BG Tanzania imewekeza Shilingi 44,000,000/- kwa ajili ya mafunzo na upatikanaji wa leseni katika awamu hii. Awamu ya pili,ambayo itajumuisha waendesha pikipiki wengine 200 itapangwa baadaye.

Mgeni rasmi kwenye tukio alikuwa Mheshimiwa Saidi Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Mchinga ;ambapo Mhandisi Dk. Ezekial Mganilwa, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji aliiwakilisha taasisi yake. Bwana Machumu Leonard, Afisa wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Lindi alihudhuria akiiwakilisha Ofisi ya Kamishina wa Polisi wa Mkoa pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa ACP Mwakanjiga

MSAFARA WA KINANA WAWASILI SHINYANGA VIJIJINI

$
0
0
 Mbunge wa Jimbo la Swola Ahmed Salum akiwasalimu wakazi wa Luhambo Didia wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana.

Katibu Mkuu wa CCM Taifa akiwashukuru wakazi wa Luhambo Didia kwa mapokezi mazuri.

Article 14

$
0
0
Africa Anzen Foundation (AAF) (Anzen means safety in Japanese), a local NGO established by a team of concerned Tanzanian and Japanese people, in collaboration with the Tanzania Traffic Police Force and the Embassy of Japan, on Monday launched the Anzen Unten campaign (which means safe driving in Japanese), with the purpose of raising awareness of Traffic Safety in Tanzania.

The inauguration ceremony for the Anzen Unten campaign was held at Serena hotel on 09 September, in the presence of Mr. Augustine Shio, Acting Permanent Secretary, Ministry of Home Affairs, Mr. Mohamed Mpinga, Deputy Commissioner of Police and H. E. Mr. Masaki Okada, Ambassador of Japan.

During the ceremony an original campaign song, Anzen Unten (‘Endesha kwa Uangalifu’), was performed by Barnaba, Recho and Tony, who is a Japanese volunteer based in Tanzania, dispatched by Japan International Cooperation Agency (JICA).

In addition, the ceremony was the world premiere of the Anzen Unten Movie, directed by the internationally recognized film director, Mr. Ben Suzuki. Mr Suzuki personally introduced the movie on the occasion.

On 10 September, Mr. Suzuki and the Tanzanian Traffic Police Force held road safety workshops at Kigogo Primary School and Mkwawa Primary School, using the Anzen Unten song and movie. Both the movie and song will be utilized for road safety education nationwide and as part of the National Road Safety Campaign of the Tanzanian Traffic Police Force.

The Anzen Unten song and movie is available at:

- Anzen Unten music with lyrics: http://www.youtube.com/watch?v=qXWHHLyzg0s
- Anzen Unten Facebook page: http://www.facebook.com/AfricaAnzenProject

From left, Ambassador Okada, Mr. Shio (Acting Permanent Secretary, Ministry of Home Affairs) and Mr. Mpinga, Deputy Commissioner of Police at the Inauguration Ceremony of Anzen Unten Campaign on 9 September.
 Mr. Ben Suzuki(centre), film director, with Anzen Unten Movie cast at the Inauguration Ceremony of the Anzen Unten Campaign on 9 September Road safety workshops.
Barnaba explains the importance of traffic safety at Kigogo Primary School.
From left. Mr. Shinya Tomonari, Chairperson of Africa Anzen Foundation, Tony (JICA volunteer) and Barnaba show the Anzen Unten movie at Kigogo Primary School on 10 September.
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images