WAHANDISI wazalendo wametakiwa kujipanga ili kuweza kuchangamkia fursa za uwekezaji katika miradi mbalimbali ya bandari nchini.
Akizungumza wakati wa warsha iliyoandaliwa na Chama cha Wataalamu Washauri wa Wahandisi ‘Association of Consulting Engineers Tanzania’, (ACET), Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit C.V. Kakoko amesema wakati umefika kuchangamkia fursa zilizopo bandarini.
Amesema kwamba japo malengo ya TPA kwenye warsha hiyo ni kuwafahamisha uwepo wa miradi mikubwa ya maendeleo hivyo kuchukua nafasi hiyo ili kuendeleza bandari kwa huduma zao kupitia miradi iliyopo na kuwaasa wachangamkie fursa zilizopo.
“Bandarini kuna fursa ya kazi za ujenzi wa miundombinu katika nyanja zote kama ujenzi wa mitambo, umeme, mafuta, gesi na TEHAMA,” amesema Mhandisi Kakoko.
Amesisitiza kwamba changamoto kubwa kwa sasa ni pamoja na kutochukua hatua za makusudi za kuchangamkia fursa kwa makampuni ya ujenzi ya ndani, uwezo mdogo wa makampuni ya wahandisi, wataalam wachache wenye weledi pamoja na vikundi vya taaluma kutoshirikiana.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akizungumza wakati wa warsha iliyoandaliwa na Chama cha Wataalamu Washauri wa Wahandisi ‘Association of Consulting Engineers Tanzania’, (ACET) iliyofanyika jijini Dar es Salaam.