Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110114 articles
Browse latest View live

INTRODUCING Msamiati's "Moja Moja" Official Music Video


Introducing "SLOW DOWN" by Crown Jay x The Green (G.O.G) Akonshaz Music

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM Mwl. Raymond Mwangwala atikisa Jang'ombe

$
0
0
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mwl. Raymond Mwangwala amewasihi wananchi wa jimbo la Jang’ombe hasa vijana kumchagua kwa kura za ndio mgombea wa tiketi ya CCM Ramadhan Hamza Chande. 
 Wito huo ameutoa leo alipokuwa akimnadi na mgombea wa CCM Jimbo la Jang’ombe huko katika Mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika Tawi la Kidongo Chekundu Unguja. Amemtaja mgombea huyo wa CCM kuwa ni mgombea pekee mwenye sifa na vigezo vya kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo katika Jimbo hilo. 
 Mwl. Raymond amesema viongozi mbali mbali wa CCM katika Jimbo la Jang’ombe wametekelea kwa ufanisi miradi ya maendeleo na kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto sugu za jimbo. Pia ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya saba inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ametekeleza kwa ufanisi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2016 hatua ambazo zinastahiki kuungwa mkono na wananchi wote hasa wa Jimbo hilo. 
 Katibu Mkuu huyo wa UVCCM Raymond, amebainisha kwamba mafanikio hayo yatakuwa endelevu endapo wanachama na wananchi wa Jang’ombe watamchagua mgombea anayetokana na Chama Cha Mapinduzi chenye sera imara na historia ya kuwatumikia wananchi wa rika zote hasa vijana. 
 Katika maelezo yake Katibu Mkuu huyo alisema kupitia Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 2018/2019 zimetengwa jumla ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kusaidia kundi la Vijana hatua ambayo inatakiwa kuthaminiwa na kundi hilo. 
 Alisema mbali na fedha hizo pia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayotokana na CCM inajenga viwanja vya kisasa vya michezo kwa kila Wilaya Zanzibar kwa lengo la kuwawezesha vijana wajiajiri kupitia sekta ya michezo mbali mbali. 
 Aidha alisisitiza kuwa CCM ina matarajio makubwa ya kushinda kwa asilimia kubwa katika uchaguzi huo kutokana na Wananchi hasa kuiamini na kuiunga mkono tasisi hiyo kwani ushahidi wa tathimini hizo umeonekana wazi katika Chaguzi za Majimbo mbali mbali ya Tanzania bara ambayo chama hicho kimeshinda kwa kishindo. 
 “Mgombea wetu anauzika ana mvuto na pia ana sifa ya utendaji na uchapakazi uliotuka hivyo nakuombeni wananchi wa Jimbo la Jang’ombe hasa Vijana Wenzangu Octoba 27, mwaka huu tumchague ndugu Ramadhan Hamza kwa kura nyingi za ndio”, alisema Mwl. Raymond. 
 Aliongeza kuwa Vyama vya upiunzani kwa sasa havina sera na vimepoteza dira ya kisiasa kwa kutawaliwa na migogoro na visasi vya wenyewe kwa wenyewe hali inayovikosesha sifa ya kuongoza nafasi yoyote katika jamii.
 WANACHAMA wa CCM na wananchi kwa ujumla walioudhuria katika mkutano wa kampeni za CCM wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi
 KATIBU Mkuu wa UVCCM Mwl.Raymond Mwangwala akiwahutubia wananchi katika kampeni za kumnadi mgombea wa CCM nafasi ya Uwakilishi Ramadhan Hamza Chande  katika Mkutano uliofanyika uwanja wa Tawi la CCM Kidongo Chekundu.
Mgombea uwakilishi tiketi ya CCM Jimbo la Jang’ombe  ndugu Ramadhan Hamza Chande(kushoto) akiomba kura za ndio katika mkutano huo ambao mgeni rasmi ni Katibu Mkuu wa UVCCM Mwl.Raymond Mwangwala(kulia) huko uwanja wa Kidongo chekundu.

RIDHIWANI KIKWETE AWATAKA VIJANA KUTOJIHUSISHA NA MADAWA YA KULEVYA

$
0
0
Na Shushu Joel,Chalinze
VIJANA wengi nchini wamejikuta wakikumbana na changamoto nyingi katika utafutaji wa maisha katika jamii zao na kupelekea kundi jingine kujiunga katika matumizi hatari ya utumiaji wa madawa ya kulevya na hivyo hata taifa kukosa vijana wa kuitumikia serikali yao.


Kukithili kwa vitendo vya uvutaji wa bangi vijiweni kunasababishwa na wazazi walio wengi kwa kutojenga tabia ya kuwakanya watoto wao pindi wanapokuwa wadogo na hata inapotokea watoto wao kupewa hadhabu ya viboko na walimu au watu wengine wazazi wamekuwa wakiwaijua juu wale waliojitokeza kuwakanya watoto hao.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Chalinze katika mahafari ya shule hiyo mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete amewataka vijana kutokaa vijiweni na watu walioshindikana kwani watawashawishi vibaya na hata kuwataka waweze kujiunga katika makundi ambayo si mazuri.

Alisema kuwa vijana wengi wamekuwa wakishawishiwa na watu wenye nia mbaya na vijana ili kuwaona tu na wao wanaharibika kwa kufuata matendo mabaya wanayoyafanya kwenye mitaa ikiwemo ubakaji,uvutaji wa madawa ya kulevya na hata kwenye wizi.

Kikwete aliongeza kuwa serikali inawategemea kwa kiasi kikubwa ili muweze kuja kuisaidia katika Nyanja mbalimbali pindi mtakapokuwa wakubwa kwani uongozi ni mchezo wa kupokezana.

“Mimi mbunge wenu nawahakikishieni serikali ya awamu ya tano imekuwa imejiwekea mikakati mikubwa ya kuhakikisha vijana wote wanamaliza masomo yao na wanafaulu ni lazima waende shule bila cha kusingizia kukosekana kwa ada,hivyo nawatakeni wanafunzi wote katika jimbo la chalinze kuhakikisha kila mmoja wenu anafaulu ili kuja baadae kuisaidia serikali na Taifa kwa ujumla.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Chalinze katika mahafari ya shule hiyo.




Baadhi ya wananfunzi.

MSANII HAWA KUFANYIWA UPASUAJI INDIA

$
0
0

Na Khadija Seif, Blobu ya Jamii
Mwanamuziki wa kike nchini anaejulikana kwa jina la Hawa  aliyeshirikishwa kwenye wimbo wa "Nitarejea" wa Mwanamuziki Naseeb Abdul 'Diamond platinumz' amefanikiwa kupata vipimo vya awali nchini India.
Hawa ambaye hivi karibuni alikua akiomba msaada kwa watu mbalimbali  ikiwemo kwa Diamond ili aweze kupata matibabu ya ugonjwa ambao ulikua ukimsumbua muda mrefu huku wengi wakimtupia lawama kuwa amejiingiza Kwenye ulevi wa kupindukia.
Akithibitisha hayo Meneja wa Daimond Platinum, Hamis Tale maarufu kama Babu Tale ameeleza kuwa wamefika salama nchini India na kufanikiwa kupata vipimo vya awali.
Tale ameweka wazi kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika 
"Asante Mungu tumefika salama India na tumefanya vipimo vyote upya salama na jibu lililotoka kwa wataalamu kwa asilimia 95% awajaona tatizo linalohusiana na ini kwa mgonjwa ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini ivyo basi kutaitajika kufanyika upasuaji mkubwa ambao utakua na uangalizi mkubwa wa wataamu then wametuakikishia baada ya hapo mgonjwa atapata nafuu na inawezekana izo 5% zilizobaki itakua poa na tatizo la ini alitokuwepo kikubwa tunaomba mtuombee dua na msiache kumuombea pia @diamondplatnumz apatenguvu ya kuendela kumsaidia kwa maana kutoa ni moyo. Kikubwa sana naomba tumuombee Hawa coz anaingia kwenye upasuaji mkubwa na hii ni atua ya yeye kua salama. Mungu tusimamie"

Hivyo basi tale amesema kuwa Hawa amefanya kipimo cha moyo nakugundulika kuwa ndio chanzo kilichokua kikipelekea mwili kujaa maji.

Wataalamu wanaendelea kuhakikisha Hawa anapata matibabu na taratibu zinaendelea vizuri ili aweze   kufanyiwa upasuaji mkubwa ambao utahitaji uangalizi sana. Pia Meneja huyo ameshukuru sana juhudi ambazo zinaonyeshwa kwa msanii daimond kwa kumsaidia mwana Dada huyo ili kuhakikisha anarudi katika hali yake ya kawaida na kuwasihi watu kumuombea dua sana katika kipindi hiki.

RATIBA YA KUAGA MIILI YA WATUMISHI WATANO WA WIZARA YA KILIMO WALIOFARIKI KWA AJALI YA GARI MANYONI MKOANI SINGIDA

HABARI ZA UN KUTOKA NEW YORK, MAREKANI, LEO

VOA SWAHILI: Duniani Leo October 22, 2018


DC KINONDONI AKUTANA NA WAFANYABIASHARA SOKO LA MWENGE

$
0
0
1
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo akizungumza na wafanyabiashara wa soko la Mwenge alipokutana nao kwenye ukumbi wa Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam leo kulia ni Kazi Maduhu Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni na kushoto ni Mweka hazina wa Manispaa hiyo Bw. Max Tabonwa.
2
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo akimsikiliza Kazi Maduhu Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni wakati akitoa ratiba ya kikao cha mkuu huyo wa wilaya ya wafanyabiashara, kushoto ni Mweka hazina wa Manispaa hiyo Bw. Max Tabonwa.
3
Mmoja wa wamiliki wa majengo katika eneo la soko la mwenge akichangia hoja katika mkutano huo.
4
Baadhi ya wafanyabiashara wakiwa katika mkutano huo.
5
Mmoja wa wafanyabiashara akizungumza katika kikao hicho.

RELI TV: Tanzania na Rwanda kujenga Reli ya SGR,Rwanda waomba kuja Kujifunza kupitia Mradi wa JPM

DIRA YA MWALIMU NYERERE - UTANGULIZI, SEHEMU YA KWANZA

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA WENYEVITI WA TAASISI TANO ZA BODI ZA SERIKALI

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

UZINDUZI WA WIKI YA ASASI ZA KIRAI TANZANIA JIJINI DODOMA OKTOBA 22, 2018

Balozi wa Tanzania China Azitaka Taasisi za Umma Kuchangamkia Masoko China

$
0
0
Na Beatrice Lyimo - MAELEZO, CHINA 

Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki amezitaka Taasisi zenye dhamana ya kutafuta masoko ya bidhaa mbalimbali nchini ikiwemo TANTRADE , Bodi ya Kahawa, Bodi za Chai, Korosho, Nafaka na Mazao mchanganyiko kushiriki kwenye maonesho mbalimbali yatakayofanyika nchini China ili kutafuta masoko mapya ya bidhaa zao.

Balozi Kairuki ameyazungumza hayo alipokutana na ujumbe wa Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi walipotembelea nchini China kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu baina ya China na Tanzania katika tasnia ya habari na mawasiliano.

"Uzoefu wa hivi karibuni umekuwa wa kukatisha tamaa kutokana na Ubalozi kutafuta fursa mbalimbali kwa ajili ya bidhaa za Tanzania kutangazwa lakini wadau wameshindwa kushiriki" ameongeza Balozi Kairuki.

Aidha, Balozi Kairuki amesema kuwa kumekuwepo na ongezeko la matumizi ya kahawa miongoni mwa Watu wa Jamhuri ya China na kahawa ya Tanzania ni miongoni mwa kahawa zinazopendwa sana na watu hao hivyo hiyo ni nafasi ya kupata soko la uhakika nchini humo endapo itafanyika kampeni mahususi ya kuitangaza kahawa ya Tanzania.

Vilevile amesema kuwa Madini mbalimbali na vito kutoka Tanzania yana nafasi ya kupata soko nchini China endapo patakuwepo na mifumo mizuri ya kisasa ya kuendesha mnada ya madini.Mbali na hayo, Balozi Kairuki ametaja baadhi ya matarajio ya Ubalozi wa Tanzania nchini China katika kipindi cha miaka minne ijayo ikiwepo kuongeza idadi ya sasa ya watalii toka China kutoka 30,000 hadi 100,000 ifikapo mwaka 2020.

Aidha, amesema kuwa Ubalozi unatarajia kuongeza uwekezaji kutoka China hususani kwenye ujenzi wa viwanda ikiwa na lengo la kati ya sasa hadi 2021 kuvutia viwanda 100 ili kufanya ongezeko la uwekezaji kutoka dola za Kimarekani Bilioni 3.6 za sasa hadi kufika dola za Kimarekani bilioni 7 ifikapo 2021.

"Pia Ubalozi unatarajia kuongeza idadi ya fursa za mafunzo kwa Watanzania katika fani mbalimbali hususani uhandisi ikiwa na lengo kuu la kuhakikisha watanzania 1,000 wapate mafunzo ya uhandisi ifikapo mwaka 2021.

Dkt. Abbasi ameambatana na baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Habari na Uhusiano Serikalini wa Wizara na Taasisi za Serikali kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu baina ya Tanzania na China katika sekta ya mawasiliano.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 23,2018

TANZANIA YASHRIKI KONGAMANO LA KIMATAIFA LA UWEKEZAJI ,GENEVA USWISI.

$
0
0
*Tanzania ni kati ya nchi 160 zinazoshiriki Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji.

Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji (World Investment Forum) limefunguliwa tarehe 22 Oktoba 2018 Geneva, Uswisi na Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) Dkt. Mukisa Khitui na litaendelea mpaka Oktoba 26,2018. 

Kauli mbiu ya kongamnao ni ‘uwekezaji kwa maendeleo endelevu’ (investing for sustainable development) ambapo majadiliano yatajikita kwenye changamoto za uwekezaji katika mazingira mapya ya utandawazi na mapinduzi ya viwanda (Globalization and Industrialization). 

Kongamano hili la aina yake huandaliwa kila baada ya miaka miwili na UNCTAD kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya Uwekezaji. Takribani washiriki zaidi ya 5,000 wanashiriki kutoka nchi 160 duniani ikiwemo Tanzania na ujumbe wake unaongozwa na Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva, Dkt. James Alex Msekela. 

Washiriki wa kongamnao hilo ni kutoka katika nyanja mbalimbali za umma na sekta binafsi ikiwamo Wakuu wa nchi, Mawaziri Wakuu, Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi za Uwekezaji. Wengine ni Watendaji wa Makampuni ya Kimataifa na Ushirikiano wa Hisa, Wasimamizi wa Mifuko ya Fedha, Wakurugenzi Wakuu wa Mashirika ya Sekta Binafsi, Wataalam wa eneo la Uwekezaji wa Kimataifa,Wabunge,Wawakilishi wa Vyama vya Kiraia, Wasomi Maarufu, na vyombo vya Habari vya Kimataifa. 

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kama mdau wa masuala ya uwekezaji nchini kinashiriki katika kongamano hili ambapo Mkurugenzi Mtendaji Bw. Geoffrey Mwambe atashiriki katika vipindi/midahalo na majadiliano mbalimbali kwa lengo la kuinadi Tanzania kuwa ni nchi bora ya kuwekeza Afrika kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo amani, uchumi imara unaokua kwa kasi, uwepo wa rasilimali, uwepo wa miundo mbinu na uongozi bora. 
Mhe Balozi Dkt. James Msekela (wa tatu kutoka kulia) na Mkuregenzi wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe (wa ili kutoka kulia) wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa uwekezaji Geneva,Uswisi.
Rais wa Namibia Mhe.Dkt Hage Geingob akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe katika Banda la Tanzania kwenye kongamano la kimataifa la Uwekezaji.
Ufunguzi wa kongamano la Kimataifa la Uwekezaji.

MJUMBE WA KAMATI KUU CCM TAIFA, MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MKUTANO WA KAMPENI JIMBO LA JANG`OMBE

$
0
0

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana alikuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kampeni jimbo la Jang`ombe ambapo Chama Cha Mapinduzi kimemsimamisha Bw. Ramadhan Hamza Chande kugombea nafasi ya Uwakilishi katika jimbo hilo.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, Makamu wa Rais amewataka wakazi wa Jang`ombe kufuata nyayo walizoachiwa na Wazazi wao.Mheshimiwa Samia amewambia wakazi wa jimbo hilo kuwa atatoa ushirikiano wa kutosha kwa kufanya kazi pamoja na Viongozi wa Jimbo hilo katika kuboresha huduma za afya na elimu.

Pamoja na Viongozi wengine Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Mbunge mteule wa jimbo la Liwale kutoka mkoani Lindi Bw. Zuberi Kachauka ambaye aliwaambia wakazi wa Jimbo la Jang`ombe kuwa upinzani umekufa kwa kukosa sera na viongozi bora.

Kampeni za Uwakilishi jimbo la Jang`ombe zilianza tarehe 14 Oktoba na zinatazamiwa kukamilika tarehe 25 Oktoba 2018 na tarehe 27 Oktoba wananchi watapiga kura kumchagua Mwakilishi wa jimbo hilo.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi pamoja na Katiba ya Chama mgombea wa CCM nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Jang`ombe Bw. Ramadhan Hamza Chande wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
Wahamasishaji wakiwa wamebeba picha ya mgombea wa nafasi ya uwakilishi kupitia CCM jimbo la Jang`ombe Bw. Ramadhan Hamza Chande wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Baja ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Dkt. Abdulla Juma Sadala wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo wakati wa mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja kushoto ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zuberi Ali Maulid.
Bendi ya Muziki wa Taarab ya Big Star ya CCM Zanzibar ikitumbuiza wakati wa mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea wa CCM wa jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja.

China na Tanzania Kushirikiana Katika Mafunzo kwa Wanahabari

$
0
0

Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, CHINA


Kansela wa Idara ya Habari, Wizara ya Mambo ya Nje katika Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Gong Anmin amemuahidi Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi kushughulikia suala la mafunzo kwa Wanahabari wa Tanzania kwa lengo la kuwajengea uwezo katika sekta ya mawasiliano.

Bw.Gong ameyasema hayo wakati wa mkutano maalumu baina yake na ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Dkt. Abbasi uliolenga kujifunza na kubadilishana uzoefu katika sekta ya habari na mawasiliano na wataalamu wa Serikali ya China. Bw. Gong aliongeza kuwa: "suala la kuongeza uwezo kwa wanahabari ni muhimu kwani itasaidia kuongeza taaluma waliyonayo hivyo nitajitahidi kufanikisha mafunzo kwa wanahabari wa Tanzania ambayo ni nchi rafiki na China kwa miaka mingi"

Mbali na hayo Dkt. Abbasi pia amekutana na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje anayeshughulikia Idara ya Masuala ya Afrika Bw. WAN Li. Katika Mazungumzo yao Bw. Wan amesema kuwa urafiki wa Tanzania na China ni wa muda mrefu na ulianzishwa na waasisi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Mwenyekiti Mao Zedong hivyo kuahidi kutunza na kudumisha urafiki huo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>

DIRA YA KITAA : Fumanizi Bongo vs Nigeria

Viewing all 110114 articles
Browse latest View live




Latest Images