Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live

Copa Coca Cola 2013 yafana

0
0
 Mshambuliaji wa timu ya  Mbeya,Yusuf Honroli (kushoto) akiwania mpira na mabeki wa Kilimanjaro,Abidal Ramadhani (kulia) na Simon Soka  katika mashindano ya Copa Cocacola kwenye Uwanja wa Karume 
 Timu ya Copa Coca-Cola ikiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere muda mfupi kabla ya kukwea pipa kuelekea Afrika Kusini kwenye kambi ya mafunzo ya soka yakishirikisha timu za vijana kutoka barani Afrika. Anayehojiwa ni Afisa Habari wa Coca Cola Tanzania Gerald Ndalahwa. Kwa habari kamili na picha zaidi BOFYA HAPA

LAUNCH OF UDSM ALUMNI DAR CHAPTER

0
0
Dear UDSM Alumni,
The University of Dar es Salaam is very pleased to invite you as alumni to the launch of UDSM alumni Dar es Salaam Chapter on 20th September, 2013 from 5pm to 7pm. The event will take place at British Council downtown and will be casual networking. Please arrive promptly.
Launch event program:
            Arrival & registration
            Opening remarks by university leadership and launch of the UDSM Alumni, Dar Chapter
            Short presentations on other alumni chapter experiences
            Drinks + networking
Registration for the event
If you would like to attend, please reply to danielstephen688@gmail.com or call or text 0754 623 3950715 392 370022 2 410 615 as soon as possible, as places are limited. Please state your name, contact address, the name of your study programme at the UDSM, and your graduation year.
  
Daniel M Stephen
CONVOCATION LIAISON OFFICER
UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM

askofu Mkuu wa KKKT IRINGA AMTEMBELEA MKURUGENZI WA HABARI

0
0
 Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri (KKT) Iringa  Mhadhamu  Owdenburg Mdegela (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi wa Habari Assah Mwambene (kushoto) leo alipomtembelea  ofisini kwake jijini Dar es Salaam
 Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri (KKT) Mkoa wa Iringa Mhadhamu Owdenburg Mdegela (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Habari (MAELEZO) Assah Mwambene ofisini kwake alipotembelewa jijini Dar es Salaam. Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

Operesheni Kimbunga yawakamata zaidi ya elfu moja kwa siku moja

0
0
Ile operesheni ya kuwatimua wahamiaji haramu nchini Tanzania imeanza kutekelezwa ambapo juzi na jana, watu 1851 walikamatwa katika mikoa ya kandoni mwa maziwa Nyanza na Tanganyika ndani ya siku moja.

  • Operesheni hiyo  pamoja na mengine inalenga kufukuza majambazi, majangili, pamoja kukamata silaha zinazosadikiwa kutumika katika matendo ya kihalifu nchini.  Baadhi ya watu walisalimisha silaha zao huku wengine wakiziacha kwa wenyeji.

Mkuu wa Operesheni hiyo kubwa kuliko zote zilizowahi kufanyika nchini Tanzania, iliyopewa jina la,

“Operesheni Kimbunga”, Naibu Kamishina wa Polisi, Simon Sirro amewaasa wananchi kuwa makini na ‘kurithishwa’ silaha hizo kwani  ni kinyume na sheria na inawezekana silaha hizo zikawa zimehusika katika vitendo vya kihalifu na hivyo kumsababishia ‘mrithi’ kushitakiwa kwa mujibu wa sheria.

Kuhusu malalamikao ya kutengwa kwa familia za baadhi ya wenyeji na wahamiaji waliooana, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe amesema wengi wa walioondoka kwa hofu hawakuwa na ufahamu kuhusu sheria na hivyo amewataka kuwafike kwenye ofisi za Uhamiaji ili wapatiwe hati za utambulisho na kuishi nchini zitakazotumika kwa muda wa miaka 2 wakisubiri taratibu za kuwapatia uraia.

Mwezi Julai tarehe 29, Rais Kikwete alitoa wito kwa wahamiaji wote haramu waondoke nchini ndani ya siku 14 ambapo ilitarajiwa wangeondoka zaidi ya 50,000 lakini hadi sasa wameondoka 11,600 tu.


Mhe. Patrick Willemot amkabidhi zawadi Balozi Kamala

0
0
Mhe. Patrick Willemot Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zinga Metal akimkabidhi zawadi Dr. Diodorus Buberwa Kamala balozi wa Tanzania Ubelgiji baada ya kutembelea Kampuni hiyo. Balozi Kamala yuko kwenye ziara ya kutangaza fursa za uwekezaji Tanzania kwa Makampuni ya Kibelgiji.

NAFASI ZA AJIRA KWA MADAKTARI, MADAKTARI WA MENO, TABIBU, TABIBU WASAIDIZI NA WATAALAMU WA MAABARA

MBUNGE KABATI ATOA MSAADA WA MADAWATI 100 YENYE THAMANI YA SH.MILIONI SITA

0
0
 Afisa Mwandamizi wa manunuzi Bodi ya michezo ya kubahatisha, Sadick Kasuhya kulia akimkabidhi mmoja ya madawati 100 yaliyotolewa kwa ufadhili wa Bodi ya michezo ya kubahatisha kwa Mbunge wa Viti maaluma kupitia chama cha mapinduzi mkoa wa Iringa Lita Kabati tukio lililofanyika katika shule ya msingi Sabasaba mkoani Iringa.
======  =====  ======
Na Denis Mlowe,Iringa   .
  
MBUNGE  wa Viti Maalum  Mkoa wa Iringa(CCM) Lita Kabati  ametoa msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 6.3  kwa shule za msingi  zilizoko mkoani hapa.

Kabati akizungumza wakati akikabidhiwa madawati hayo kwa ufadhili wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania mwishoni mwa wiki, alisema shule nyingi mkoani hapa zina upungufu mkubwa wa madawati hivyo ni jukumu la kiongozi kuweza kusaidia kuondokana na hali hii na kuwashukuru bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania
.
“Nimefanya ziara katika shule za msingi nyingi za mkoani kwangu kuna matatizo mengi kama ukosefu wa madawati na vitabu ndipo nikawaomba wenzetu wa bodi ya michezo kubahatisha wanisaidie madawati kwa shule hizi hakika ninawashukuru sana hakika haitamaliza tatizo lakini itasaidia kupunguza japo kwa uchache” alisema Kabati

Alisema kuwa elimu bora kwa wanafunzi wa shule za msingi unaendana na vifaa wanavyotumia katika kupata elimu ya msingi ikiwemo kakaa katika madawati bora kunachangia maendeleo ya taifa letu katika kukuza elimu.

Kabati aliwataka viongozi wengine kuondokana na tabia ya kufikiria kuwa katika kuleta maendeleo ya mkoa ni mojawapo ya kampeni bali ni kuungana na kuweza kupambana katika kuwaletea maendeleo wananchi wanaowawakilisha.

Akizungumza kabla ya kukabidhi madawati hayo kwa niaba ya mkurugenzi wa bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania, Afisa Mwandamizi wa manunuzi Bodi ya michezo ya kubahatisha, Sadick Kasuhya alisema moja ya majukumu ya bodi kuweza kusaidia jamii katika sekta ya elimu na wataendelea kusaidia shule mbalimbali nchini. 

Alisema kuwa kwa msaada huu wa madawati  100 yenye thamani ya shilingi milioni 6, 3 kutasaidia kupunguza tatizo la madawati kwa baadhi ya shule zitakazokabidhiwa msaada huo.

LAUNCH OF UDSM ALUMNI DAR CHAPTER

0
0
The University of Dar es Salaam is very pleased to invite you as alumni to the launch of UDSM alumni Dar es Salaam Chapter on 20thSeptember, 2013 from 5pm to 7pm. The event will take place at British Council downtown and will be casual networking. Please arrive promptly.

Launch event program:
            Arrival & registration
            Opening remarks by university leadership and launch of the UDSM Alumni, Dar Chapter
            Short presentations on other alumni chapter experiences
            Drinks + networking

Registration for the event
If you would like to attend, please reply to danielstephen688@gmail.comor call or text 0754 623 395; 0715 392 370; 022 2 410 615 as soon as possible, as places are limited. Please state your name, contact address, the name of your study programme at the UDSM, and your graduation year.
 
 
 
Daniel M Stephen
CONVOCATION LIAISON OFFICER
UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM


//michuzi2.rssing.com/chan-7007653/article5089-live.html

Wavunjifu wa amani wachukuliwe hatua

0
0
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa Mhe.Hamza Hassan Juma akiongea na Maofisa wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo kutembelea Makao makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai DCI Robert Manumba.
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Paul Chagonja akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kati ya Maofisa wa Makao Makuu na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa wakati wa ziara yao Makao Makuu ya Polisi jana.Kushoto ni Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe Hamza Hassan Juma.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa Mhe.Hamza Hassan Juma akipokelewa na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi Thobias Andengenye Makao Makuu ya Jeshi la Polisi wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo kutembelea Makao makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi).


Frank Geofray-Jeshi la Polisi

Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa imelipongeza Jeshi la Polisi kwa jinsi linavyotekeleza majukumu yake kwa kuwachukulia hatua wachochezi wanaotumia mgongo wa siasa au dini hapa nchini. 

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mh. Hamza Hassan Juma aliyasema hayo jana wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipotembelea makao makuu ya Jeshi la Polisi kwa lengo la kujifunza na kuweka mikakati ya pamoja katika kukabiliana na uhalifu pamoja na kuboresha maisha ya askari Polisi.

Alisema, Jeshi la Polisi linapaswa kutomuonea muhali mtu yeyote ama taasisi itakayotumia mwamvuli wa siasa au dini kupandikiza na kueneza chuki ndani ya jamii kitendo ambacho hupelekea uvunjifu wa amani.

Aidha, Mwenyekiti wa kamati hiyo, alishauri kuwa viwanja vyote vinavyomilikiwa na Jeshi la Polisi vipatiwe hati miliki ili kupunguza uvamizi katika maeneo na viwanja vya Polisi na endapo kuna wavamizi wowote wachuliwe hatua za haraka.

Kwa upande wake Kamishina wa operesheni na mafunzo wa Jeshi la Polisi (CP) Paul Chagonja alibainisha matishio yanayoikabili nchi kwa sasa ambayo ni misimamo mikali ya kisiasa, migogoro ya wafugaji na wakulima, biashara ya dawa za kulenya, mauaji yanayosababishwa na imani za kishirikina na watu kuwania mali pamoja na ajali za barabarani zinazosababisha vifo kutokana na waendesha pikipiki na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi limejipanga na linaendelea na mikakati mbalimbali ya kiusalama katika kukabiliana na matishio hayo ikiwemo kupeleka askari katika tarafa ili kuimarisha ulinzi ngazi ya tarafa hadi familia.

Aidha, aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wahalifu waliopo kwenye jamii kabla hawajatekeleza adhima yao ya kutenda uhalifu.

Aliongeza kuwa hivi sasa Jeshi hilo linaendelea kutekeleza program ya maboresho ili kuboresha vitendea kazi pamoja na maslahi ya askari ambapo kila askari hivi sasa pamoja na mambo mengine anapata matibabu kwa kutumia bima ya afya na zaidi ya shilingi bilioni 42 zimekopeshwa kwa askari kupitia chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi ( Ura Saccos) kwa lengo la kuboresha maisha ya askari binafsi.

Shamo Towers & Shopping Centre

0
0
Shamo Towers & Shopping Centre sasa unaweza kupata  huduma mbalimbali  Kama;

- huduma  za ki Benki
- Huduma za afya na pharmacy  Aga Khan Medical centre.
- Boutique ya kisasa 
- Baby shop & Gift Shops
- Electronics shop
- Coffee Shop & fast food restaurant.
- stationaries Shop.
- Furniture centre.
- village Supermarket, Voda Shop & Bureau de change. Kufunguliwa karibuni.

Mbezi towers ipo Mbezi Beach, karibu na tangi bovu. 

DUKA LA GALINA - FUN ZONE GIFT SHOP

COFFEE SHOP- BOOGIE WOOGIE 

DUKA LA KIAFRICA -WAQWETU.

TIMU YA NETIBOLI YA UTUMISHI YATAKIWA KUJINOA ZAIDI

0
0
Wachezaji wa timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakijadili jambo mara baada ya mazoezi katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma imetakiwa kujinoa zaidi ili kujiimarisha na kujiweka katika nafasi nzuri ya kupata ubingwa wa mashindano ya michezo ya SHIMIWI yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni mjini Dodoma.

Hayo yalisemwa jana na Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu alipotembelea timu hiyo ili kuangalia maendeleo ya timu iliyokuwa katika mazoezi makali kwenye viwanja vya Leaders Club vilivyopo jijini Dar es Salaam.

Bw.Mkwizu alisema ili timu hiyo iweze kupata ushindi inatakiwa ijiimarishe na kujiongezea stamina kwa kufanya mechi nyingi za kirafiki na timu kongwe hapa nchini.

“Mnatakiwa mfanye mazoezi ya ziada na mcheze mechi nyingi za kirafiki na timu ambazo zimekuwa zikicheza ligi mbalimbali kama Filbert Bayi,Ikulu,Wizara ya Elimu,Wizara ya Afya na JKT.” Alisema Bw. Mkwizu.

Aliongeza kuwa iwapo timu hiyo itahitaji msaada wowote ili kufanikisha mechi za kirafiki na kufanya mazoezi yatakayoijenga timu ,kocha asisite kuongea na uongozi wa timu .

Naye kocha wa timu hiyo Bw.Mathew Kambona alisema ana mpango wa kuiboresha kiufundi timu hiyo ili iweze kucheza michuano mbalimbali mwakani.

“Nina mkakati wa kuiimarisha timu na kuiandaa ipasavyo ili tuwe na timu ya kudumu itakayoshiriki kwenye ligi mbalimbali “alisema Bw.Kambona.

Aidha,kocha Kambona alisema timu hiyo kwa sasa inakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na kiwanja kizuri cha kufanyia mazoezi ili kujiandaa kikamilifu.

“Tunaomba ofisi itusaidie tupate kiwanja cha mazoezi kwani mashindano yamekaribia na ninahitaji kuiandaa timu itakayotoa upinzani kwa bingwa mtetezi” alifafanua Bw. Kambona.

Kwa upande wa wachezaji wa timu hiyo wameuomba uongozi wa michezo wa Utumishi kuhudhuria katika mazoezi na mechi mbalimbali za majaribio na kushiriki na kocha bega kwa bega ili kubaini mapungufu yaliyopo na kuyaboresha kabla ya mashindano kuanza.

Timu ya mpira wa pete ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma imedhamiria kunyakua kikombe cha ubingwa kwenye michuano ya SHIMIWI ya mwaka huu itakayofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dodoma kuanzia Septemba 20 mwaka huu .

Serikali yahimizwa kurahisisha kilimo cha mkataba

0
0
Na Mwandishi Wetu

Sekta ya pamba nchini ina uwezo wa kuwakwamua wakulima wa pamba katika dimbwi la umaskini endapo serikali kwa kushirikiana na wadau wengine wataweza kusaidia uwepo kilimo cha mkataba nchini.

Akiongea na vyombo vya habari hivi karibu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania, Gabriel Mwalo, alisema kuna faida nyingi katika kilimo cha mkataba lakini kukosekana kwa usimamiaji mzuri pamoja na ukosefu wa uungwaji mkono wa kutosha kutoka Serikalini kunawafanya wawekezaji kutochangia fedha nyingi zinazohitajika katika mfumo.

Sasa wakati umefika kwa Serikali kuyaangalia matatizo yanayokwamisha kilimo cha mkataba na mkazo uwekwe kwenye uzalishaji wa pamba pasiwepo ucheleweshaji wa utekelezaji wa sera ya Serikali,” Bw. Mwalo alisema.

techno brain limited invite daily news staff for familiarization tour

0
0
Techno Brain this week invited staff of the country's leading  English daily, Daily News, to its offices for a familiarization tour and for Techno Brain to interact with the media in tandem with the company's  focus on expansion and growth on the African Continent and world. Techno Brain is a Homegrown IT solution firm with 18 offices in the world. 
 Daily News staff were impressed with the growth the company has  in Africa and the world as a whole. Attendees from TBL were Eng August Kowero – ICT advisor Techno Brain,  Dipesh Panjoli – country manager Techno Brain,  James Mbandi – Marketing Techno Brain,  Darius Elias- Sales and  Elizabeth Riziki - HR 
From the the  Daily News  were Amina Lumuli – HR, John Mcharo - Mechanical Eng, Nelly Mtema – Journalist, Gasper Sango – System Admin,  Nicodemus Ikonko – Chief sub Editor,  Robert Okanda photo journalist, Katuma Nasamba Journalist, Ichikaeli Maro – Research / Innovation writer, Joctan Matogo – Financial manager,  Tuma Abdullah – Editor and Felix Mushi – Advertising manager.
 Eng. August Kowere ICT Adviser for Techno Brain giving the welcome speech

 Darius Elias - Sales, explaining the Corporate presentation to the Daily News team

 Dipesh Pancholi – Country Manager- emphasizing a point on the Techno Brain Presentation

 James Mbandi Marketing Manager- explaining to Daily News Team how the Access control system works during the tour

 Eng. Kowero Presenting a gift to Tuma Abdallah – Daily News Editor

Dipesh Thakar Techno Brain Director of planning and legal affairs meeting the Daily News Team.

WAREMBO REDD'S MISS TANZANIA WATEMBELEA KIWANDA CHA TBL ARUSHA

0
0
Mtaam wa Upishi wa Pombe kutoka Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Tawi la Arusha, Jacob Mgowe akiwatembeza baadhi ya washjiriki wa shindano la Redd’s Miss Tanzania 2013 wakati wartembo hao walipotembelea kiwanda hicho kujionea uzalishaji wa pombe zake.

Camera aina ya Kodak 10 megapixels inauzwa

0
0
 Camera aina ya Kodak 10 megapixels inauzwa,kwa mtu anayehitaji anaweza kuwasiliana kwa simu 0768808819 ama email misasophie@yahoo.com

MH. LUHANJO AKABIDHIWA GARI NA NAIBU WAZIRI WA MAJI

0
0
Mwenyekiti wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Wanging’ombe Philimon Luhanjo akikagua gari alilokabidhiwa. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Christopher Sayi. Nyuma ya Luhanjo ni Meneja wa Mamlaka ya Wanging’ombe, Mhandisi Najib Wasumbwile.
Mwenyekiti wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Wanging’ombe Philimon Luhanjo akisaini kitabu cha wageni ofisi kwa Naibu Waziri wa Maji, Wakwanza Kulia ni Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Dk. Binilith Mahenge, katikati ni K.G Bwire mfanyakazi wa Wizara ya Maji.
Kutoka kushoto; Naibu Waziri wa Maji, Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanging’ombe, Katibu Mkuu Wizara ya maji na Mbwire wakielekea kwenye gari, tayari kwa ajili ya kukabidhiwa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Wanging’ombe.
Mwenyekiti wa Mamlka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Wanging’ombe, Philimon Luhanjo akimshukuru Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Dk. Binilith Mahenge kwa kumkabidhi gari. Wakwanza kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Chritopher sayi.

Ardhi haiwezi kuwa chanzo cha upotevu wa amani - Waziri Mkuu Pinda

0
0
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali itahakikisha kuwa ardhi ambayo Watanzania wamepewa na Mungu haibadiliki na kuwa chanzo cha upotevu wa amani nchini.
 
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Septemba 10, 2013) wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa siku tatu unaojadili haki na amani katika masuala ya ardhi Tanzania ulianza jana jijini Dar es Salaam.
 
“Tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa ardhi yetu haileti laana bali inabakia kuwa baraka ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia. Ninawasihi wale wote wenye mamlaka na utoaji wa ardhi wahakikishe kuwa wanatimiza wajibu wao wanaposimamia masuala ya ardhi ili haki isipotee na hatimaye kuepusha migogoro ya ardhi,” alisema.
 
“Ninawasihi Watanzania iwe ni wanasiasa, viongozi wa dini, asasi za kiraia, wasomi na umma wote kwa ujumla. Ninaomba tuitunze amani tuliyonayo na tutambue kwamba Tanzania ndiyo nchi pekee tuliyojaliwa kuwa nayo. Madhara ya ukosefu wa amani ni makubwa. Tuangalie nchi za wenzetu zenye migogoro  na tuone jinsi machafuko hayo yatatuathiri sisi wenyewe, watoto wetu na wajukuu wetu,” alisisitiza.
 

EAC ELECTION OBSERVER MISSION TO THE 16th -18th SEPTEMBER PARLIAMENTARY ELECTIONS IN THE REPUBLIC OF RWANDA

0
0
The East African Community is pleased to announce the arrival of its Observer Mission for the Parliamentary Elections in the Republic of Rwanda scheduled to take place on 16th – 18th September 2013.

The Mission is in the country at the invitation of the Government of Rwanda and the National Electoral Commission. It is led by Hon. Musa Sirma, Former Minister for EAC Affair’s, Republic of Kenya and comprises 40 members drawn from the East African Legislative Assembly, Electoral Management Bodies (EMBs)’ Civil Society Organisations (CSOs), and National Human Commissions from 4 EAC countries namely Burundi, Uganda, Tanzania and Kenya.

The overall objective of the Mission is to promote democracy and governance in the respective EAC Partner States, which includes Rwanda. Specific objectives include:

- Assess whether the conditions exist for the conduct of parliamentary elections that allow the people of Rwanda to freely express their will;

- Assess and determine whether the elections are conducted in accordance with the constitutional and legal framework governing elections in Rwanda;

- Determine whether the outcome of the electoral process as a whole reflect the will of the people of Rwanda; and - Assess whether the elections meet the benchmarks set out in the 2002 Durban Declaration on the Principles

Governing Democratic Elections in Africa by the African Union, the EAC Principles of Election Monitoring and Observation

The Mission’s advance team arrived on 5th September 2013 followed by the rest of the Observers on 9th September 2013. The Missions will remain in the country until 20th September 2013.

The Members of the Mission are attending a pre-deployment training and holding consultative sessions with stakeholders from 10th – 13th September 2013. On 14th September 2013, teams will be deployed to all provinces and districts of Rwanda where they will continue interacting with stakeholders and observe the concluding stages of the election campaign. On polling days, Monday 16th to Wednesday 18th September 2013, the EAC observer teams will observe the voting and counting processes at the polling stations. On Thursday 19th 2013, all EAC teams will reconvene in Kigali for debriefing session, after which the Mission will issue an interim statement on its preliminary findings on the electoral process.

The EAC Election Observer Mission is committed to working closely with all the relevant stakeholders in Rwanda and other election observer groups. They will act in an impartial, objective and transparent manner at all stages of the electoral process.
Kenya’s Former Minister of EAC, Hon Musa Sirma makes arrival statement of the EOM as EAC Deputy Secretary General in charge of Political Federation Hon Charles Njoroge and Hon Abubakar Zein Abubakar EALA team leader looks on.
Group photo opportunity, members of EAC Election Observer.

President Kikwete has sent a congratulatory message to H.E. Manmoon Hussain, President of the Islamic Republic of Pakistan

0
0
H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Manmoon Hussain, President of the Islamic Republic of Pakistan following his election as the President of Pakistan.
The Message reads as follows:
His Excellency Manmoon Hussain,
President Elect,
Islamabad,
PAKISTAN.

Your Excellency

I have received with great joy the news of your election as the President of the Islamic Republic of Pakistan.

On behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and, indeed, on my own behalf, I wish to extend to you and through you to the Pakistan Muslim League-N Party, our profound congratulations on your momentous victory.  Your election to lead your great country and its people is a clear testimony of confidence and trust that the people of Pakistan have to your Pakistan Muslim League-N Party.

As you prepare to assume office in your new mandate, I wish to assure, you of my personal commitment as well as that of the Government of the United Republic of Tanzania, to continue to work closely with you and your Government to further strengthen the excellent bilateral relations that so happily exist between our two countries.

While wishing you a very successful term and continued personal good health, please accept, Mr President, the assurances of my highest consideration and esteem”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation, Dar es Salaam

9th September, 2013
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live




Latest Images