Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110002 articles
Browse latest View live

CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu

$
0
0
CHAMA  cha  walimu   Tanzania (CWT)  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa  kimetoa  bati   500  zenye  thamani  ya  zaidi ya  shilingi milioni 8.5 kwa   mwalimu  mstaafu  25  kama  sehemu ya  kuwaaga na  kuwapongeza kwa  utumishi  bora katika  kazi  hiyo ya  ualimu .

Akikabidhi   bati  hizo jana  wakati wa  hafla  fupi ya  kuwaaga  walimu  hao  mgeni  rasmi katika  hafla  hiyo afisa   utumishi  wa  Halmashauri ya  wilaya ya  Kilolo   Josephat  Kayombo   pamoja na  kupongeza   CWT wilaya ya   Kilolo  kwa  kutambua  mchango  wa   walimu   wenzao  ambao  wamestaafu  bado  alitoa  wito  kwa  walimu   waliopo kazini  kuendelea kujituma  kufanya kazi hiyo na  kujiepusha  na  utovu  wa  nidhamu .

Kayombo  alisema   serikali  imeendelea  kuwajali  watumishi  wote  wa umma  wakiwemo  walimu na kuendelea  kulipa  stahiki  zao ambazo  wamekuwa  wakizidai hivyo  ni lazima  kwa  watumishi hao kutimiza  majukumu yao  kwa  ufanisi na  kuepuka   kuonyesha  utovu wa  nidhamu  na  jeuri  pale  mwajili  ambapo amua  kumpangia kituo kipya  cha kazi .

"  Walimu  ni  kielelezo  tosha  kwa  jamii na hakuna yeyote  anayeweza  kujisifu  kwa  mafanikio yake  bila  kutambua  mchango wa  mwalimu   hivyo ni vema  walimu  kwa  umuhumu  wenu  huo kuendelea   kulenda   heshima  yenu kwa   kuonyesha  nidhamu na  kuzingatia  kanuni  na  taratibu za  kazi  na  kujiepusha  kuwa  na  nidhamu  mbovu "  alisema  Kayombo 

 Pia  alisema    kwa  kuwa  serikali  imeendelea  kuwalipa  mafao  yao   wastaafu    ni  vema  walimu    wastaafu  kuwa makini na  wimbi la  matapeli  ambao  wamekuwa  wakizunguka katika vijiji mbali mbali  vya  wilaya ya  Kilolo  na  kuorodhesha majina ya  walimu  wastaafu  kwa  lengo la  kuwatapeli   mafao  yao  ya  ustaafu .

Alisema  kuwa  kiasi cha  fedha  ambacho  wanakipata  baada ya  kustaafu  kinaweza  kuja  kuwa msaada  mkubwa  kwao mbele ya  safari    hivyo  umakini unahitajika  kwa  kuwaepuka  matapeli  hao.
Afisa utumishi  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa Joseptah kayombo (kulia)  akiwa na  viongozi wa chama cha walimu Tanzania (CWT)  wilaya ya  Kilolo wakiwakabidhi bati  walimu  wastaafu 25  kila  mmoja bati 20.
 Viongozi wa CWT  Kilolo (kulia)  wakiwakabidhi walimu wastaafu 25 zawadi ya bati 20 kila  mmoja .

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

OLE NASHA:VETA NI CHOMBO MUHIMU KATIKA UJENZI WA VIWANDA NCHINI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amesema kuwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ni chombo muhimu katika kuzalisha mafundi watakaohudumia viwanda vinavyojengwa nchini.

Ole Nasha ameyasema hayo leo wakati alipotembelea Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ikiwa ni kujua utendaji wa mamlaka hiyo katika uzalishaji wa ujunzi kwa vijana nchini, amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imejipambanua kuwa ni nchi viwanda hivyo licha ya kuwepo kwa wahandisi ni lazima kuwepo kwa mafundi.

Amesema kuwa VETA ni lazima waonyeshe njia katika uzalishaji wa vijana wenye ujuzi ambao watatumika katika viwanda na miradi mbalimbali ya serikali inayojenga wakiwemo mafundi wa reli.

“Wahandisi kazi yao kuweka michoro lakini kazi ya kujenga ni mafundi hivyo ni wajibu wenu VETA wa kuzalisha rasimali hiyo katika ujenzi wa taifa na kazi yenu inaonekana baadhi ya vijana wamemaliza shahada ya kwanza na sasa wanajiunga mafunzo ya ufundi stadi”.amesema Ole Nasha.

Ole Nasha amesema kuwa vyuo vyote vinatakiwa kuangaliwa mitaala na VETA na visivyo na vigezo wavifungie

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya VETA , Peter Maduki amesema kuwa wanajenzi wa vyuo vya VETA kata Mikoa Mitatu na Wilaya moja moja ambavyo vitagharimu sh. bilioni 38.

Amesema Mikoa vitavyojengwa vyuo vya ufundi Geita , Simiyu , Rukwa pamoja wilaya ya Chato ikiwa kuhakikisha kila mkoa unakuwa na chuo cha ufundi stadi.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dk.Pancras Bujulu amesema kuwa changamoto yake ni kutafuta fedha kwa ajili ya kuismamamisha Vete.
Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akizungumza na Menjejimenti ya VETA pamoja na Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wafanyakazi na Menejimenti katika Mkutano na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha.

WANANCHI WALIOPISHA MRADI UMEME WA KV400 KUTOKA SINGIDA HADI NAMANGA WAANZA KULIPWA FIDIA

$
0
0
Na Zuena Msuya,  Singida
SERIKALI imeanza kulipa fidia kwa wananchi 4000 waliopisha mradi wa kusafirisha umeme wa msongo mkubwa wa kilovolti 400  kutoka Singida hadi Namanga ambapo zoezi la ulipaji fidia litakamilika hivi karibuni.
Mradi huo wa kusafirisha umeme wa kV400 kutoka Singida hadi Namanga utaunganisha nchi za Tanzania na Kenya na unafahamika kama  (Kenya – Tanzania Power Interconnector Project), (KTPIP).

Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu alisema hayo alipotembelea eneo la kuhifadhia vifaa vya mradi huo (yard)  katika kijiji cha Nangwa wilayani Hanang mkoani Manyara, mwishoni mwa wiki, ili kukagua vifaa hivyo vitakavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya umeme.

Mgalu alisema kuwa, kazi za awali za utekelezaji wa mradi huo zilikwishaanza na kinachosubiriwa sasa ni kukamisha zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi waliopisha mradi husika ili wakandarasi waanze rasmi kazi ya ujenzi.

Mgalu aliweka wazi kuwa, katika utekelezaji wa mradi huo, vijiji 14 vilivyopitiwa na mradi vitapata umeme ambapo vijiji 7 ni vya  Mkoa wa Singida, 2 kutoka Mkoa wa Manyara na 5 ni vya Mkoa wa Arusha.
 Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu, akikagua yadi ya kuhifadhia miundombinu ya kujenga mradi mkubwa wa kusafirisha umeme wa 400kv kutoka Singida hadi Namanga.
 Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu( kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja Msimamizi wa mradi wa kusafirisha umeme wa msongo mkubwa  wa 400kV, Mhandisi Oscar Kanyama,( kulia) wakati wa ziara ya Naibu Waziri huyo alipotembelea yadi hiyo kukagua vifaa na miundombinu ya kutekeleza mradi huo. 
Baadhi ya vifaa vilivyohifadhiwa katika yadi ya kuhifadhia vifaa na miundombinu ya kujenga mradi wa kusafirisha umeme wa msongo mkubwa wa 400kV kutoka Singida hadi Namanga.

Chaneli ya Utalii Kuzinduliwa Disemba Mwaka Huu

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO
SERIKALI imeazimia kuzindua Chaneli ya Utalii inayotegemewa kurushwa kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) mnamo mwezi Disemba mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Susan Mlawi wakati wa Kikao cha Kamati inayofuatilia uanzishwaji wa chaneli hiyo.

Bi. Susan amesema kuwa vikao vya wadau na wataalam mbalimbali vitakavyowezesha uanzishwaji wa chaneli hiyo vinaendelea ambapo katika kikao hicho imetolewa taarifa ya hatua zilizofikiwa ambazo zimeonekana kuleta mafanikio makubwa.

"Tumekusudia kuifanya chaneli hii ambayo tunatarajia uzinduzi wake utafanyika mwezi Disemba mwaka huu kuwa na vipindi bora vyenye kugusa utalii wa kila aina. Aidha, tunategemea kuweka lugha mbalimbali ambazo zitasaidia watu wengi kutoka mataifa mbalimbali kuweza kuitazama."

Ameongeza kusema kuwa hadi kufikia muda huu tayari fedha za mitambo itakayoweza kuanzisha chaneli hiyo zimeshapatikana na ametoa rai kwa TBC kutoa kipaumbele katika maandalizi ya chaneli hiyo na kuandaa utaratibu maalum wa kusimamia matangazo yake.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa ni muhimu chaneli hiyo ionekane sehemu mbalimbali duniani ili kupata wadau wengi watakaoweza kuweka matangazo yao na kuiwezesha chaneli hiyo kujiendesha.

Amefafanua kuwa matangazo kupitia chaneli hiyo itakayotangaza utalii wa Tanzania yataingiza fedha nyingi ambazo zitasaidia kujiendesha badala ya nchi kutumia fedha nyingi kuutangaza utalii nje ya nchi.

"Kupitia chaneli hii, tunataka utalii uchukue sura mpya katika kuvutia uwekezaji kwani itawezesha Tanzania kujitangaza kiutalii katika nchi mbalimbali duniani na kuongeza Pato la Taifa," alisema Prof. adolf Mkenda.

Naye Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo amesema, nchi ikiwa na chaneli yenye maudhui ya utalii itasaidia Watanzania kufahamu kwa urahisi vivutio vilivyopo nchini pia itawafanya wadau mbalimbali kufahamu sio tu utalii bali pia masuala ya kiutamaduni.

Vile vile chaneli hii itawawezesha wadau kufahamu maeneo mahususi ya upigaji picha za mnato na jongefu ambazo zitaifanya nchi kujulikana zaidi nje ya nchi kupitia picha.

Uanzishwaji wa chaneli ya utalii kupitia TBC ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alilolitoa wakati alipotembelea shirika hilo mnamo mwaka 2017.

TCCIA, KAIMU BALOZI WA LIBYA NCHINI WAJADILI FURSA ZA KIBIASHARA,UWEKEZAJI

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

CHAMA cha Wafanyabishara wenye Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA) kimefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania Saleh Kusa Arze ambapo kwa sehemu kubwa mazungumzo yao yamejikita kuangalia fursa za kibishara na uwekezaji baina ya nchi hizo mbili. Katika mazungumzo hayo nchi ya Libya imeonesha nia ya kuwekeza hasa katika sekte ya nishati ya umeme na kilimo na kuna kampuni ya Libya inataka kuwekeza kwenye mradi wa umeme wa megawati 400. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam mbele ya Balozi Arze , Kaimu wa Rais wa TCCIA Octavian Mshiu amesema ujio wa balozi huyo kwenye chemba yao umekuwa wa mafanikio makubwa kwani wamezungumza mambo mengi yanayoonesha nia njema katika eneo la biashara kati ya nchi hizo mbili. "Tunashukuru kwa ujio wa Kaimu Balozi wa Libya nchini kwetu.

Kikubwa ambacho tumezungumza pamoja na mambo mengine kuna moja ya kampuni ya nchi hiyo inataka kuja nchini kuwekeza katika mradi wa umeme wa megawati 400.Tararibu bado zinaendelea na pale tutakapokuwa tayari tutatoa taarifa. 

Mshiu pia ametoa rai kwa wafanyabishara nchini kuitumia TCCIA hasa kwa kuzingatia uwepo wao unalenga kuangalia fursa ambazo wafanyabishara wanaweza kuzitumia vema katika kujenga uchumi wa nchi yetu kwa maslahi ya Watanzania wote. "Mwaka huu tunatarajia kusheherekea miaka 30 ya uwepo wa TCCIA. Tumetoa mchango mkubwa na dhamira yetu ni kuendelea kupanua wigo wa fursa za biashara na uwekezaji nchini.
Kaimu Rais wa Chama cha wenyeviwanda na Kilimo (TCCIA) Octavian Mshiu aliyekaa kushoto akisalimiana na Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania Saleh Kusa Arze leo jijini Dar es Salaam baada ya kufika katika ofisi za TCCIA kwa lengo la kujadili masuala ya biashara na uwekezaji.
 Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania Saleh Kusa Arze(kulia) akifafanua jambo kuhusu fursa za uwekezaji baada ya kukutana na Kaimu Rais wa TCCIA Octavian Mshiu leo jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Rais wa TCCIA Octavian Mshiu (wa kwanza kulia)akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi wa Libya nchini Tanzania Saleh Kusa Arze(wa pili kulia). Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa TCCIA Fatma Hamis na wa kwanza kushoto ni Msaidizi wa Kaimu Balozi.


MBUNGE AZZA HILAL AKABIDHI VIFAA TIBA VYA MILIONI 36.5 KWENYE VITUO VYA AFYA WILAYANI KAHAMA

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad (CCM) amekabidhi msaada wa Vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 36.5 kwa ajili ya vituo vya afya na zahanati sita zilizopo katika halmashauri ya wilaya ya Ushetu,Msalala na Kahama Mji wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Mheshimiwa Azza amekabidhi vifaa tiba hivyo leo Jumanne Oktoba 16,2018 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Anamringi Macha wakati wa Kikao cha Baraza la UWT wilaya ya Kahama uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Kahama.
Vifaa tiba hivyo ni pamoja na shuka 100,mashine za kupima damu,wingi wa damu,sukari,joto,mapigo ya moyo na vifaa vya kusaidia kujifungua kwa akina mama ambavyo kupatikana kwake kumetokana na jitihada za mbunge huyo kuhakikisha vifo vya mama na mtoto vinapungua mkoani Shinyanga.
Awali akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa tiba hivyo,Mheshimiwa Azza Hilal alisema kupitia Kampeni yake ya ‘Afya Yangu Mtaji Wangu’ na kuwajali akina mama aliamua kutafuta wadau kwa ajili ya kusaidia kumaliza changamoto ya uhaba wa vifaa tiba katika vituo vya afya na zahanati.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad (CCM) akizungumza wakati akikabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 36.5 kwa ajili ya zanahati na vituo vya afya wilayani Kahama leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Kahama.Kushoto ni Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kahama,Telephora Saria,kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama Thomas Myonga. 
Vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 36.5 kwa ajili ya zanahati na vituo vya afya wilayani Kahama vilivyotolewa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad (CCM) kwa kushirikiana na wadau wake Bahari Pharmacy Ltd na Brett &Beileys.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad akikabidhi vifaa tiba kwa  Mkuu wa wilaya ya Kahama,Anamringi Macha.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad akikabidhi shuka ikiwa ni sehemu ya shuka 100 alizotoa kwa ajili ya vituo vya afya na zahanati wilayani Kahama.
Wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha akiwa ameshikilia boksi lenye mashine ya kupimia sukari mwilini. Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama Thomas Myonga.Wa kwanza kushoto ni  Mbunge wa Jimbo la Ushetu,Mheshimiwa Elias Kwandikwa ambaye ni Naibu Waziri wa Ujenzi akifuatiwa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Azza Hilal Hamad akiwa ameshikiliwa vifaa tiba.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

DC Uyui Atoa Mkono wa Pole kwa Wananchi Walioathiriwa na Uvamizi wa Tembo

$
0
0
Na Mwandishi wetu- Uyui 

Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora Mhe. Gift Msuya amewatembealea na kuwapa pole wananchi walioathirika na uvamizi wa Tembo katika Kijiji cha SawMill Kata ya Migiri. 

Akizungumza na wananchi hao mara baada ya kuwatembelea na kuwafariji amesema kuwa ameshawaagiza Askari wanyamapori kufika katika kijiji hicho na kuwaondosha tembo hao ili wasiendele kuleta madhara katika eneo hilo ikiwemo kuharibu mali na kudhuru wananchi . 

“Jukumu la Serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa salama na wanaendelea na shughuli zao za uzalishaji kama kawaida ndio maana nimewaagiza askari wanyamapori kufika hapa mara moja na kuwaondosha tembo hawa” ; Alisisitiza Msuya 

Akifafanua amesema kuwa tembo hao ambao idadi yao haikufahamika waliingia katika kijiji hicho na kuanza kuharibu mazao ya chakula yaliyokuwa yamehifadhiwa na wananchi hao katika vihenge. 

Pia aliwataka wananchi katika maeneo hayo kuishi kwa tahadhari kwa kutoa taarifa haraka pale watakapoona wanyama hao wameingia katika makazi yao ili Serikali ichukue hatua stahiki kwa haraka kuepusha maafa. 

Tembo hao ambao idadi yao haikufahamika mara moja walivamia makazi ya watu usiku wa kumakia tarehe 15 Oktoba na kusababisha uharibifu wa wa mazao ya chakula yaliyokuwa yamehifadhiwa na wananchi hao.

Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Gift Msuya akitoa mkono wa pole kwa mmoja wa wananchi walioathirika na uvamizi wa tembo katika kijiji SawMill Kata ya Migiri Wilayani humo. (Picha zote na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Uyui) 

BALOZI SIMON MUMWI AWASILISHA HATI ZAKE ZA UTAMBULISHO KWA RAIS PUTIN WA URUSI

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Urusi Meja Jenerali mstaafu Simon Mumwi akipata picha ya kumbukumbu na Rais Vladimir Putin baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa kiongozi wa nchi hiyo katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow leo 

NEWS ALERT:BASI LA NEW FORCE LATUMBUKIA MLIMA KITOGA,12 WAJERUHIWA

$
0
0
Leo tarehe 16/10/2018 majira ya saa 13:00 mlima Kitonga katika barabara kuu ya Iringa – Morogoro Wilaya ya Kilolo na Mkoa wa Iringa . Gari lenye namba za usajili T 852DHA aina ya ZHONGTONG BUS mali ya NEWFORCE wa Dsm likiendeshwa na IDD s/o BAKARI MALULI , kabila Mhehe, miaka 38 na mkazi wa Dsm akikwepa gari lenye namba za usajili T.623DMG, likiendeshwa na RAMADHAN S/O SALIMIN ambapo basi hilo la kampuni ya New force kwa kuepuka kugongana uso kwa uso liliacha barabara na kupinduka hatimaye kusababisha majeruhi 12 ambao ni .

1.LEONARD s/o POTES, KYUSA, 32 YRS WA MPANDA
2.JAMES s/o NDUNGURU, MNGONI, 49YRS, WA DSM,
3.IDD s/o BAKARI MALULI, MHEHE, 38YRS, DEREVA WA DSM
4.BAKARI s/o ZAYUMBA, MBONDEI, 27YRS WA MBEYA
5.NDEKE S/o MWAIFUSE 53YRS, WA DSM
6.TABIA d/ o FRANCIS, KYUSA, 65YRS, WA MBEYA
7 .GRACE D/o BONIPHACE, MCHAGA 24YRS, WA MOROGORO
8.GRORY D/o BONIPHACE MCHAGA 24YRS, WA MOROGORO
9.ANNA D/o ALEX 22YRS, MUHAYA, WA DSM
10.AZIZA D/o MUHINA, MZIGUA, 43YRS WA DSM
11.SAWA s/o MTINGALA MAKUA, 52YRS, WA DSM
12.IAN D/o EVANCE 2YRS, KYUSA WA MBEYA

Waliolazwa hospitali teule ya Itunda wilaya ya Kilolo. Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa gari namba T623 kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari..Amedhibitisha Kaimu Rpc Kamishna msaidizi wa Polisi. DEUSDEDIT KASINDO.
 Mmoja wa wasamaria wema akimsaidia mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo
 Baadhi ya abiria walionusurika kifo wakitoka kwenye basi hilo mara baada kupata ajali 

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA CRDB AKUTANA NA MSAJILI WA HAZINA

$
0
0
Msajili wa Hazina, Athumani Selemani Mbuttuka (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela (kulia) alipokuwa akimkaribisha ofisini kwake, jijini Dar es salaam alipokwenda kwa lengo la kujitambulisha. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela (wa tatu kushoto) akizungumza wakati akielezea mipango na mikati yake kwa Benki hiyo, kwa Msajili wa Hazina, Athumani Selemani Mbuttuka (kushoto) wakati alipompembelea ofisini kwake jijini Dar es salaam, alipokwenda kwa lengo la kujitambulisha. 

BALOZI WA TANZANIA NCHINI SWEDEN, DKT. WILLIBROD SLAA AMTEMBELE SPIKA WA BUNGE. MHE. JOB NDUGAI

$
0
0


Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Balozi wa Tanzania Nchini Sweden, Dkt. Willibrod Slaa wakati Balozi huyo alipomtembelea nyumbani kwake Jijini Dodoma leo

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongea na Balozi wa Tanzania Nchini Sweden, Dkt. Willibrod Slaa wakati Balozi huyo alipomtembelea nyumbani kwake  Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akifurahi jambo na Balozi wa Tanzania Nchini Sweden, Dkt. Willibrod Slaa wakati Balozi huyo alipomtembelea nyumbani kwake  Jijini Dodoma.

WAZIRI LUGOLA AKUTANA NA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA YAKE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0

 WAJADILI MIKAKATI MBALIMBALI YA UTENDAJI KAZI 

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akizungumza na Watendaji Wakuu wa Wizara na Taasisi zake katika kikao cha kujadili masuala mbalimbali yakiwemo utendaji kazi wenye weledi. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimfafanulia jambo Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, (CGP) Phaustine Kasike (kulia aliyesimama), katika kikao cha kujadili masuala mbalimbali ya utendaji kazi wa Wizara hiyo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu. Kulia meza kuu ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo, Wanja Mtawazo, wakati alipokua anatoa taarifa yake katika kikao cha watendaji wakuu wa Wizara na Taasisi zake kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu. Kulia meza kuu ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima.

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu (kushoto), alipokua anamfafanulia jambo katika kikao cha watendaji wakuu wa wizara na taasisi zake kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

HALOTEL INAKUSUDIA KUWEKEZA DOLA ZA KIMAREKANI 700 KATIKA SEKTA ZA MAWASILIANO

$
0
0
Na Karama Kenyunko Globu ya jamii
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Halotel inakusudia kuwekeza dola za kimarekani (USD) 700 katika sekta Umma na  mawasiliano nchini ikiwa na malengo ya kuwafikia wateja zaidi ya milioni Sita katika kipindi cha miaka mitano toka kuanzishwa kwake.

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Son, amesema hayo leo Oktoba 16,2018 wakati wa maadhimisho ya miaka mitatu ya Halotel yaliyofanyika katika ofisi zao.

Son amesema, pamoja na mipango hiyo ya kuwekeza, kampuni hiyo pia imekusudia kuboresha zaidi Huduma ya utumaji wa pesa kwa njia ya mtandao, 'Halopesa' kwa ajili ya Wateja binafsi, mashirika na serikali kwa ujumla.

 "Mpaka sasa tunatimiza miaka mitatu Halotel inefanya uwekezaji wa dola za kimarekani (USD) 500 ikiwa ndio kampuni inayoongoza kwa kwa kuwekeza miuondombinu ya mawasiliano katika sehemu mbalimbali nchini inayowafikia asilimia 95 ya wananchi wote ikiwa n vituo 4400 vya kupokea mawasiliano" amesema Son.

Kampuni hiyo imepanga kuimarisha mtandao wake wa 4G ili kuwafikia Wateja wengi zaidi hadi wale walioko pembezoni mwa miji na kuwapa gharama nafuu za mawasiliano ambapo mpaka sasa Wateja zaidi ya milioni tatu na wengine zaidi ya milioni moja waliojiunga na Halopesa.

Ameongeza, kuwa kupitia Huduma hio wanaamini watakuwa wameisaidia serikali na taasisi zote za kibiashara kuendeleza Utoaji wa Huduma zao kwa ufanisi ukizingatia Halotel imekuwa ikishiriki katika shughuli mbali mbali za kijamii zinazoliwezesha taiga kufikia malengo yake mbali mbali

Naibu mkurugenzi mkuu wa Halotel Nguyen Van Son akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kusheherekea miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake hapa nchini kulia ni  katibu wa  kampuni hiyo Nguyen Thi Thuy Linh.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Halote, Mhina Semwenda kulia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuadhimisha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake hapa nchini. kushoto ni Naibu mkurugenzi Mkuu wa Halotel, Nguyen Van Son.
 Waandishi wa habari wakimsikiliza Naibu mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Son jijini Dar es Salaam leo Oktoba 16.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya jamii

WAKILI AIAMBIA MAHAKAMA HANS POPPE ALIKUWA NCHINI MAREKANI KWA MATIBABU

$
0
0

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
WAKILI Augustine Shio anayemtetea Mwenyekiti wa Usajili wa klabu ya Simba Sc Zacharia Hans Poppe ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam kuwa mteja wake alikuwa yupo nchini Marekani

Ameyaeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati akimuombea dhamana mteja wake. 
Wakili Shio ameeleza kuwa Hans Poppe alikuwa nchini Marekani kwa matibabu lakini aliamua kukatisha matibabu hayo na kurudi nchini kusikiliza tuhuma zinazomkabili.
Amedai kuwa Hanspope alimuandikia barua na kumjulisha kuwa anarudi nchini Oktoba 15 mwaka 2018 na kumtaka awajulishe Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu ujio wake.
Wakili Shio amedai, aliwafikishia ujumbe Takukuru ndipo usiku wa jana Oktoba 15 2018, ambapo saa 7:25 usiku Hans Poppe aliwasili na alipofika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alikamatwa na TAKUKURU  lakini baadaye waliweza kumruhusu alale nyumbani kwake na asubuhi walimfikisha mahakamani.

Hans Poppe kwa sasa yupo nje kwa dhamana, huku wenzake wawili ambao ni Rais wa Klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange wanaendelea kusota mahabusu kwa kuwa mashtaka yao hayana dhamana.


Mtuhumiwa Haspope akitoka nje ya mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kusomewa mashtaka yanayomkabiri na baadaye kuachiliwa kwa dhamana.

TWANGA PEPETA KUSHEREHEKEA MIAKA 20 TANGU KUANZISHWA KWAKE Oktoba 27, 2018 ukumbi wa Life Park Mwenge, Dar es salaam

$
0
0


Na Khadija Seif, Globu ya jamii
Ni furaha kwa kwenda mbele! Ndivyo unavyoweza kuielezea Bendi ya African Stars Twanga Pepeta ambayo mwaka huu imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake. Sherehe za kusheherekea miaka ya uwepo wa bendi hiyo iliyosheheni wanamuziki maarufu na wenye vipaji katika muziki was dansi inatarajia kufanyika Oktoba 27 mwaka huu katika ukumbi wa Life Park zamani New World Cinema eneo la Mwenge  Jiji la Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kampuni ya African Stars Entertainment (ASET) Twanga Pepeta  Iron Lady Asha Baraka ameeleaza leo   jijini Dar es Salaam namna ambavyo wamejipang kusheherekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa bendi hiyo.

"Katika sherehe hiyo  ya miaka 20 ya bendi yetu  itapambwa  na vipaji vipya kutoka kwa vijana wadogo kama Tarick  na Fetty Kalumba," amesema.

Amefafanua kuwa usiku wa sherehe hiyo kutakua na muda wa kuwaenzi waanzilishi pamoja na wasanii ambao wametangulia mbele ya haki kama Hamisi Amigoras, Abuu Semhando "Baba Diana", Banza Stone, MCD na wengine ambao wamefanya jitihada mpaka hapo bendi ilipofikia.

Asha Baraka ameongeza kwa siku ya kesho kazi zao zitaanza kusambazwa katika vituo vya habari ili kuhamasisha wapenda muziki. wadau pamoja na viongozi mbalimbali kwa lengo la kuwahamasisha kufika katika sherehe hiyo ya miaka 20 na vibao kama Povu, Rekebisha na vingine vitatumbuizwa kwa mara ya kwanza.
Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa bendi hiyo ambae pia  ni muimbaji wa siku nyingi Luiza Mbutu amewaahidi mashabiki na wadau mbalimbali wa muziki wa dansi kujitokeza kuwaunga mkono kwa hali na mali ili kufanikisha sherehe hizo.
Pia amesema sanjari na hilo  watatembelea kituo cha watoto ya yatima kilichopo  Kinondoni Moscow kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali kama kurudisha fadhila kwa jamii pamoja na kuwatembelea  wagonjwa katika Hospitali ya  Mwananyamala iliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Pia amesema waendesha bodaboda watapewa reflecta kwa ajili ya kumuenzi Mwanamuziki Abuu Semhando ambae alipata ajali ya pikipiki.

Wakati huo huo Hassan Mussa 'Super Nyamwela' ambaye ni  Kiongozi wa wanenguaji amessema wamejipanga kuhakikisha wanatoa burudani ya aina yake ambayo itakonga nyoyo za mashabiki, wapenzi na wadau wa bendi hiyo na muziki maarufu nchini. Amesema umahiri na uhodari wake katika kunengua na kumiliki jukwaa uko palepale au zaidi na kwamba jukwaa la wanenguaji zaidi ya 18 watakuwa jukwaani siku ya sherehe hizo.

Amesema katika idara ya ushereheshaji  kuna baadhi ya wanenguaji ambao wamekuwa bado wanaigaiga baadhi ya miondoko hivyo wanakaribishwa kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa bendi ya  Twangapepeta  kwani ndio kisima cha burudani.
Msanii mpya ambaye ametambulishwa rasmi kwenye bendi hiyo Fetty Kalumba  ambaye amesema amejipanga vizuri kwenye kusherehesha usiku huo na kuhimiza wapenzi wa Twanga kufika na kujumuika pamoja.
 Kiongozi na Muimbaji wa bendi ya Twanga Pepeta Luiza Mbutu akitambulisha baadhi ya vipaji vipya vitakavo tumbuiza usiku wa miaka 20 ya bendi hiyo itakayofanyika katika ukumbi wa Life Park. wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa bendi ya African Stars Asha Baraka.
Mnenguaji Mkuu wa bendi ya Twanga Pepeta Hassan Mussa 'Super Nyamwela'  akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya miaka 20 ya kuanzishwa kwa bendi hiyo itakayofanyika ukumbi wa Life Park Jijini Dar es Salaam.


NEWS ALERT: ZACHARIA HANS POPPE APANDISHWA KIZIMBANI LEO, AACHIWA KWA DHAMANA

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya  Usajili ya Klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka mawili kabla ya kuachiwa kwa dhamana.

Hans Poppe leo Oktoba 16, 2018 ameunganishwa katika kesi ya kughushi nyaraka za klabu na utakatishaji wa fedha inayomkabili Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu,
Baada ya kuunganishwa katika kesi hiyo, wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro amewasomea washtakiwa wote  mashtaka 10 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.  Katika mashitaka hayo 10, Hanspope anakabiriwa na mashtaka 2,  shtaka moja ni la kuwasilisha nyaraka za uongo na shtaka lingine ni la kughushi.
Katika mashtaka hayo 10, yamo ya kula njama, kutoa nyaraka za uongo, matumizi mabaya ya madaraka, kughushi, utakatishaji fedha, kuwasilisha nyaraka za kughushi na kuendesha biashara bila kufuata sheria. Katika shitaka la utakatishaji Aveva na Kaburu wanahusishwa na shtaka la kutakatisha kiasi cha dola 300,000 (zaidi ya sh. Milioni 650).


Katika shitaka la kughushi linalowakabili washtakiwa wote, imedaiwa Machi 15, 2016 washtakiwa kwa pamoja walighushi hati ya malipo ya kibiashara ya Mei 28, 2016 wakionyesha kwamba nyasi bandia zilizonunuliwa na Simba zinathamani ya dola 40,577, zaidi ya Sh. Milioni 90 huku wakijua kwamba sio kweli.
Pia katika shtaka jingine inadaiwa Aveva, Nyange na Hans Poppe kati ya March 10 na Septemba 30, 2016 waliwasilisha nyaraka za uongo kuonyesha Simba imenunua nyasi bandia zenye thamani ya Dola za Kimarekani 40,577.

Hata hivyo, shtaka la mwisho halikusomwa kwa sababu linamuhusu mshtakiwa 4  Franklin  Lauwo ambaye bado hajafikishwa mahakamani.

Baada ya kusomewa mashtaka yao Mahakama ilitoa masharti ya dhamana kwa Hans Poppe yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh.milioni 15 kila mmoja, 
Mshtakiwa alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana na kuachiwa huku Aveva na Kaburu wakirudishwa rumande kwa kuwa mashtaka dhidi yao hayana dhamana.  Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 19, mwaka huu.

Mwenyekiti wa Kamati ya  Usajili ya Klabu ya Simba, Zacharia Hanspope akiwa na  Makamu Rais wa Simba SC Godfrey Nyange "Kaburu"  katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam leo Oktoba 16, 2018
Mwenyekiti wa Kamati ya  Usajili ya Klabu ya Simba, Zacharia Hanspope (kushoto) akiwa na Rais wa klabu ya Simba  Evans Aveva (kulia) na Makamu wake, Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu wakiwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

TFDA:ELIMU YA MADHARA YATOKANAYO NA VIPODOZI

TAIFA STARS YAICHAPA CAPE VERDE 2-0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Mchezo wa kufuzu Mataifa Afrika (AFCON) 2019 nchini Cameroon baina  ya Tmu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' na Cape Verde  umemalizika katika  Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kwa wenyeji kutoka kidedea kwa mabao 2-0.

Taifa Stars wameshinda magoli mawili yaliyofungwa na mshambuliaji wa Difaa El Jadida ya Morocco Saimon Msuva katika dakika ya 29 akipokea pasi ya Mshambuliaji wa GRC Genk Mbwana Samatta. Mpaka Mapumziko Taifa Stars wanatoka kifua mbele kwa goli 1-0.

Katika kipindi cha Pili, Samatta aliipatia Taifa Stars goli la pili akimalizia pasi ya Mudathiri Yahya, akifuta lawama baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza.
Taifa Stars walifanya mabadiliko ya kumtoa Abdi Banda na kuingia John Bocco, Mudathir nafasi yake ikichukuliwa na Feisal Toto














Rais Magufuli ateua Makamishna wa Tume ya Kurekebisha Sheria na NARCO

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Viewing all 110002 articles
Browse latest View live




Latest Images