Na Agness Francis,blogu ya Jamii.
Katika kuendeleza Tanzania ya viwanda wafanyabiashara wa kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini wamejitokeza kwa ajili ya kusafiri nchini China kwa lengo kujifunza mbinu za kufanya biashara pamoja kutafuta masoko.
Naibu waziri wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki dkt Damas Ndumbalo amezungumza na wafanyabiashara hao wakati wa mkutano Jijini Dar es Salaam ambapo aliwapongeza kwa kutaka kuleta maendeleo ya nchi kwa kujituma kutafuta masoko nchi za nje pamoja na kujifunza namna ya kuanzisha na kuendesha viwanda kwa ujumla.
"Njia ya kujikwamua kiuchumi hapa nchini ni kuwa na viwanda pamoja na kuwekeza nguvu katika kilimo ambacho malighafi nyingi hupatikana humo,tukasake masoko, teknolojia ya viwanda ambazo zinatumia malighafi zetu za ndani"amesema dkt Ndumbalo.
Aidha mratibu wa safari ya china kushirikiana na BBIC Godwin Msigwa amewapongeza wafanyabiashara na wakulima hao wenye nia ya kutaka kujifunza pamoja na kutafuta masoko nchini humo ambayo ni nchi iliyoendelea kiuchumi hapa duniani.
Naibu waziri wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Damas Ndumbalo akiwa anazungumza na wafanyabiashara na wakulima kutoka sehemu mbali mbali hapa nchini wanaosafiri kuelekea nchini China kujifunza mbinu za kufanya biashara pamoja na kutafuta masoko,Jijini Dar es Salaam ambapo aliwataka kutokukata tamaa na waongeze nguvu katika kuleta naendeleo katika kuelekea Tanzania ya viwanda.
Meneja Mkuu kampuni ya BBIC Zhu Huojian akitoa mafunzo kwa wafanyabiasha na wakulima hao kuhusu mbinu za kufanya biashara na kukuza viwanda,Jijini Dar es Salaam.
Naibu waziri wizara ya mambo ya nje na ushirukiano wa Afrika Mashariki Damas Ndumbalo,akizungumza Jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara wanaosafiri kuelekea nchini China kujifunza namna jinsi uendeshwaji wa biashara unavyokuwa nchini humo pamoja na kutafuta masoko.
Naibu waziri wa wizara ya mambo ya nje na uhusiano wa Afrika Mashariki Damas Ndumbalo akiwa katika picha ya pamoja Jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara wanaosafiri kuelekea nchini China kwa ajili ya mafunzo zaidi ya kibaishara na kutafuta masoko ili kukuza uchumi wa nchi yetu.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA