Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

WAFANYAKAZI BENKI YA TIB CORPORATE WAMTEMBELEA MKURUGENZI MSD KUSHEHEREKEA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

$
0
0
WAFANYAKAZI wa benki ya TIB Corporate  wamtembelea Mkurugenzi Mkuu wa bohari ya dawa (MSD) Laurean Rugambwa jijini Dar es Saaam leo.

Uamuzi wa wafanyakazi wa benki hiyo kwenda MSD nimwendelezo wa kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja kwa namna ya kutembelea wateja wao kwaajili ya kutoa shukurani kwa wateja.

Mkurugenzi Mkuu wa bohari ya dawa (MSD) Laurean Rugambwa amewashukuru benki hiyo kwani wamefanya kitu cha tofauti pia amewatia moyo kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na kujituma.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa bohari ya dawa (MSD)  mwenye tisheti ya bluu leo mara baada ya kutembelewa na wafanyakazi hao ofisini kwake.
Mfanyakazi wa benki ya TIB Corporate akiangalia boksi la dawa mara baada ya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa bohari ya dawa (MSD) Laurean Rugambwa kuwaonesha jinsi bohari hiyo ilivyo.
Mkurugenzi Mkuu wa bohari ya dawa (MSD) Laurean Rugambwa  akiwaonesha baadhi ya maboksi ya dawa wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakiwa  kutembelewa na wafanyakazi hao  jijini Dar es Salaam na kuangalia mteja wao anavyofanya kazi.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakitembelea bohari ya dawa (MSD)mara baada ya mazungumzo na mkurugenzi mkuu wa bohari ya dawa jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika Oktoba kila mwaka.

KLABU YA SIMBA WAFANYA KISOMO KUMUOMBA MUNGU MO APATIKANE AKIWA SALAMA

$
0
0

*Hassan Dalali,wanachama watoa ya moyoni, wasema hivi..
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
UONGOZI wa Klabu ya Simba umeamua kufanya dua na kisomo maalumu kwa lengo la kumuomba Mwenyezi Mungu ili Mfadhili wao na mwanachama wa klabu hiyo Mohamed Dewji 'MO' apatikane akiwa salama.

Kisomo hicho kimefanyika leo mchana katika Makao Makuu ya Klabu ya Simba yaliyopo mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ambapo mashabiki wa Simba wameshiriki kisomo hicho. Kabla ya kisomo wameelezwa wazi lengo lao kuu ni kumuomba Mwenyezimungu aweze kuleta wepesi kwenye matatizo yaliyompata Mlezi na Mwekezaji wao Mohamed Dewji 'MO' 

Kaimu Katibu Mkuu wa Klabu ya Simba Hamis Kisiwa amesema kuwa wamekusanyika kufanya dua leo hii wakiamini Mwenyezi Mungu ndio muweza wa kila jambo na hivyo huko aliko Mohammed Dewji apatikane na arudi akiwa salama.

Amesema hayo baada ya kufanyika dua na kisomo maalumu kwa lengo la kumuomba Mungu afanye wepesi kwa kuwezesha Mo kupatikana."Wana Simba tumefanya kisomo ilo Mo aachiweakiwa salama.Kwa mwanachama wa Simba na sio wa Simba wamekusanyika kufanya dua hiyo ili Mohamed aachiwe akiwa salama na ndio msingi wa dua yetu," amesema Kisiwa
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.
Kaimu Katibu mkuu wa Klabu ya Simba Hamis Kisiwa wapili kushoto akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufanya kisomo kumuombea Mlezi wa klabu hiyo Mohamed Dewji ambaye ametekwa jana Oktoba 11 hoteli ya collesium jijini Dar es Salaam.
 Wanachama wa Klabu ya Simba wakimsikiliza kaimu katibu mkuu wa klabu ya Simba Hamisi Kisiwa  jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufanya kisomo kumuombea Mlezi wa klabu hiyo Mohamed Dewji ambaye ametekwa jana Oktoba 11 hoteli ya collesium jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Klabu ya Simba wanawake wakishiriki kwenye kisomo cha kumwombe Mlezi wa klabu hiyo jijini Dar es Salaam leo.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA CRDB JIJINI DAR LEO

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay (kulia) aliyeambatana na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (kushoto) wakati walipofika ofisini kwake Magogoni Ikulu jijini Dar es salaam, Oktoba 12, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia) aliyeambatana na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake, Magogoni Ikulu jijini Dar es salaam, Oktoba 12, 2018 ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha kwake toka aingie rasmi kazini. wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akifuatiwa na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Esther Mwambapa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa alipokuwa akiutambulisha ujumbe alioambatana nao.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, baada ya kukutana leo ofisini kwake, Magogoni Ikulu jijini Dar es salaam, Oktoba 12, 2018 ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha kwake toka aingie rasmi kazini. 

FUKWE KUIMARISHWA NA KUWA KIVUTIO CHA UTALII-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaweka mikakati madhubuti kwa lengo la kuimarisha matumizi ya fukwe kama sehemu ya kivutio cha utalii ili kongeza idadi ya watalii wanaokuja nchini na kutengeneza ajira kwa wananchi sambamaba na kukuza uchumi wa Taifa.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Oktoba 12, 2018) wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye ufunguzi wa onesho la Kimataifa la Utalii la Swahili International Tourism Expo, katika  Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar ES Salaam.

Onesho hilo linalofanyika kwa siku tatu nchini linahudhuriwa na wafanyabishara wakubwa wa utalii takriban 170  kutoka nchi mbalimbali duniani pamoja na wauzaji wa bidhaa za utalii takriban 300 kutoka ndani na nje ya nchi.

Waziri Mkuu amesema sekta ya utalii nchini inachangia zaidi ya asilimia 25 ya mauzo yote ya nje na takriban ajira 1,500,000, ambapo kati ya ajira zote za moja kwa moja na zile ambazo si za moja kwa moja.

Amesema kutokana na juhudi za utangazaji wa vivutio vya utalii nchini unaoratibiwa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), wageni wengi maarufu duniani wanakuja kuona vivutio hivyo wakijua kwamba Tanzania ni nchi ya amani, yenye utulivu na Watanzania ni watu wakarimu. 

Amsema kati ya wageni hao waliokuja hapa nchini kwa mwaka huu ni pamoja Rais Mstaafu wa Marekani, Bw. Barack Obama aliyekaa siku nane; Rais wa Uswisi Bw. Alain Berset aliyekaa siku 10 pamoja na mchezaji wa golf mstaafu kutoka Marekani, Bw. Jack Nicklaus.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia wadau wa utalii, kwenye ufunguzi wa maonesho ya Swahili International Tourism Expo, yaliyofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere Dar es salaam, Oktoba 12, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania Jaji Thomas Mihayo, wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Julius Nyerere Dar es salaam, kufungua maonesho ya Swahili International Tourism Expo Oktoba 12, 2018, katikati ni Naibu Waziri wa maliasili na Utalii Josephat Hasunga , kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema. 
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifafanuliwa jambo na Mkurugenzi Mkuu wa shirika la ndege Tanzania (ATCL) Ladiclaus Matindi, alipotembelea mabanda, kwenye ufunguzi wa maonesho ya Swahili International Tourism Expo, yaliyofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere Dar es salaam, Oktoba 12, 2018, kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema, Naibu Waziri wa maliasili na Utalii Josephat Hasunga, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania Jaji Thomas Mihayo. 
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia bidhaa za Tanzania zinazotolewa ndani ya ndege ya ATCL, kwenye ufunguzi wa maonesho ya Swahili International Tourism Expo, yaliyofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere Dar es salaam, Oktoba 12, 2018, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa shirika la ndege Tanzania (ATCL) Ladiclaus Matindi na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania Jaji Thomas Mihayo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

PROF. MDOE: WANAFUNZI 124,000 KUNUFAIKA NA MKOPO WA ELIMU YA JUU

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MAOFISA wanaosimamia madawati ya mikopo vyuoni wametakiwa kutokuwa chanzo cha migogoro ili kuhakikisha wanafunzi wanapata huduma bora isiyokuwa na urasimu na badala yake wahakikishe wanaimarisha madawati hayo ili kuhakikisha wanafunzi wenye sifa na uhitaji wanufaika na mikopo kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa James Mdoe wakati akizungumza katika kikao kazi cha siku mbili cha maafisa hao kilichoanza mjini Bagamoyo.

Amesema dhamira ya Serikali ya awamu ya Tano ni kuhakikisha wanafunzi wengi wanapata Elimu ya juu bila kikwazo.

Profesa Mdoe amesema kwa mwaka wa fedha 2018/19 serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 427. 5 ambapo jumla ya wanafunzi 124 watanufaika na mkopo huo, na kuwa ugawaji wa mikopo hiyo uzingatie haki, vigezo, kanuni na sheria.

“Nataka twende vizuri tukahakikishe huduma bora inatolewa katika mwaka huu mpya wa masomo ikiwa ni pamoja kutoa huduma bora,kusimamamia kumbukumbuku na kuhakikisha mawasiliano ya mara kwa mara yanakuwepo kati ya maafisa mikopo na bodi ya mikopo na kwa haipendezi maafisa mikopo kuwa chanzo cha migogoro,”amesisitiza Profesa Mdoe.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.
Mkurugenzi Mtendaji wa bodi ya mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB )Abdul- Razq Badru akitoa taarifa ya bodi hiyo katika mkutano wo katika bodi na maafisa wa mikopo katika vyuo vikuu nchini katika mkutano uliofanyika mjini Bagamoyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe akizungumza wakati akifungua mkutano wa kikao kazi cha Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa maafisa wa mikopo katika vyuo vikuu uliofanyika mjini Bagamoyo, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa bodi ya mikopo Abdul- Razq Badru.
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adam Mwakalobo akizungumza kuhusiana na ofisi yake inavyoratibu masuala ya elimu ya juu nchini kwa kushirikiana na vyuo vikuu,katika mkutano wa maafisa wa mikopo vyuo vikuu ulifanyika mjini Bagamoyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa mikopo wa vyuo vikuu.

WATU 300 DAR WAFANYIWA UCHUNGUZI WA MACHO

$
0
0
*Ni baada ya Hospitali ya macho ya Dk Agarwal kuamua kufanya uchunguzi bila malipo
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WATU zaidi ya 300 wamefanyiwa uchunguzi wa macho yao na matatizo mbalimbali yamegunduliwa ambayo husababisha uoni hafifu au upofu huku pia ukitolewa ushauri wa namna ya kutunza macho.

Hivyo kati ya hayo yaliyogundulika, yamejumuisha magonjwa ya mtoto wa jicho, mzio wa macho, matatizo ya kisukari yalioathiri macho, presha ya macho na mengine. Uchunguzi huo umefanywa na Hospitali ya macho ya Dk Agarwal ambayo imeamua kutoa huduma ya upasuaji kwa wagonjwa waliobainika kuwa na matatizo ya macho, hasa kwa wale wagonjwa wenye mtoto wa jicho bila tozo yoyote.
Uamuzi huo ni kama mchango wake katika jamii katika harakati za kupunguza na kuondoa mzigo wa upofu hapa nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla. 


Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Daktari Bingwa na Mshauri wa magonjwa ya macho na upasuaji wa Retina katika hospitali hiyo Dk. Emeritus Chibuga. Amefafanua kuwa Hospitali ya macho ya Dakta Agarwal, kama mdau wa kutoa huduma ya macho hapa Tanzania, imetoa huduma za uchunguzi wa macho kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam katika Hospitali ya Mwananyamala

Amesema kuwa mbali ya kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa wote wenye mahitaji makubwa na wasio na uwezo pia Hospitali ya Macho ya Dk Agarwal imetoa ushauri unaohusu afya ya macho kwa watu waliojitokeza kupimwa macho yao na kuwafahamisha 
dalili za hatari zinazoweza kuashiria shida za macho.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.
 Dk. Emeritus Chibuga na Dr. Huzeifa kutoka hospital ya macho ya Dkt. Agarwal wakizungumza na mmoja wa watu walioenda kupata huduma ya kupima macho katika hospital ya Mwananyamala jana katika kuadhimisha siku ya macho duniani.
 Daktari mtaalam wa masuala ya macho kutoka hospital ya Dr. Agarwal iliyopo jijini Dar es Salaam akimpatia maelekezo kijana aliyefika kupatiwa huduma ya kupima macho.
Daktari akimpima mmoja wa wagonjwa wa macho aliyefika katika hospital ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Hospital ya Dr. Agarwal imetoa huduma ya upimaji na ushauri bure kwa watu mbalimbali wanaosumbuliwa na matatizo ya macho.

DKT MPANGO: MAREKEBISHO YA SHERIA YA TAKWIMU HAYAZUII KUFANYA TAFITI

$
0
0

Na. WFM Mjini Bali Indonesia

Marekebisho ya Sheria ya Takwimu ya Mwaka 2018, hayawazuii wadau wa takwimu kutoa takwimu kwa ajili ya matumizi yao bali marekebisho hayo yanaweka misingi ya kuzingatiwa wakati wa utoaji wa takwimu hizo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, alipofanya mkutano na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha (IMF) anayewakilisha Tanzania na nchi nyingine (Africa Group 1 Constituency), Bw. Maxwell Mkwezalamba, katika Mikutano ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) mjini Bali Indoneshia.

Dkt. Mpango amesema kuwa lengo la marekebisho ya sheria hiyo ni kurahisisha ufanyaji wa tafiti na utoaji wa matokeo ya tafiti na sio kuwabana wadau katika ukusanyaji wa taarifa za kitakwimu au kuzuia mijadala ya uchambuzi wa kisera wa matokeo ya takwimu rasmi.

“Tumekubaliana kutumia fursa ya kuboresha Kanuni za Takwimu kwa ajili ya kuweka mazingira ya utekelezaji mzuri wa vipengele vya sheria vilivyorekebishwa kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kuelewa lengo la marekebisho hayo”, alieleza Dkt. Mpango. Marekebisho hayo ya kanuni za takwimu yatawezesha utekelezaji mzuri wa vifungu vya sheria vilivyorekebishwa ambapo ametoa wito kwa wadau kushiriki katika mchakato wa marekebisho hayo.

Aidha, Waziri alieleza kuwa mwezi Novemba mwaka huu Serikali itakutana na wadau wa maendeleo, ili kutoa fursa kwa wadau hao kuelewa kwa kina dhumuni la Serikali kufanya marekebisho yaliyofanyika na kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Septemba 2018.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akielezea maboresho ya sheria ya takwimu inayowafanya watafiti waweze kufanya tafiti zao kwa urahisi kwa maendeleo ya taifa, wakati wa Mkutano kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeziwakilisha nchi za Afrika Bw. Andrew Bvumbe (hayupo pichani), wakati wa mikutano ya mwaka ya Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF na Benki ya Dunia (WB) mjini Bali Indonesia, kushoto ni Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA Bw. Charles Kichere. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeziwakilisha nchi za Afrika Bw. Andrew Bvumbe (wa pili kushoto) akifurahia jambo kwenye mkutano na wajumbe wa Tanzania walioshiriki mikutano Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF na Benki ya Dunia (WB) mjini Bali Indonesia. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikali Wizara ya Fedha na Mipango- Bali Indonesia) .
Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed (kulia), akieleza kuhusu mpango wa kuboresha Sekta ya uvuvi ili kureta tija wakati wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anayewakilisha nchi za Afrika Bw. Maxwell Mkwezalamba (hayupo pichani), wakati wa mikutano ya mwaka ya IMF na Benki ya Dunia (WB) mjini Bali Indonesia. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anayewakilisha nchi za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba, akiipongeza Tanzania kwa hatua iliyochukua ya kukuza uchumi, wakati wa Mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) uliofanyika Mjini Bali Indonesia. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeziwakilisha nchi za Afrika, Bw. Andrew Bvumbe (kulia), akieleza jambo wakati wa Mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kushoto), wakati wa mikutano ya mwaka ya Shirika la Fedha la Kimataifa- IMF na Benki ya Dunia (WB) mjini Bali Indonesia, wa tatu kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed na kushoto ni Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Bw. Charles Kichere. 


SHUBASH PATEL ATOA MABATI 1,000 KUIMARISHA SEKTA YA ELIMU PWANI

$
0
0

NA MWAMVUA MWINYI,PWANI 

SEKTA ya elimu mkoani Pwani, inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa 3,678 katika shule za msingi pamoja na nyumba za walimu 5,188.


Kufuatia changamoto hiyo ,kampuni ya Sayona fruits ,iliyopo Mboga huko Chalinze imetoa mabati 1,000 yenye thamani ya sh.mil 24 ,kwa ajili ya umaliziaji wa majengo mbalimbali ya shule za msingi mkoani humo .

Akipokea mabati hayo ,kutoka kwa mkuu wa kitengo cha mahusiano cha kampuni hiyo ,Abubakar Mlawa , mkuu wa mkoa wa mkoa huo mhandisi Evarist Ndikilo alisema ,wanakabiliana na changamoto hizo kwa kushirikiana na halmashauri,jamii na wadau wa elimu . “Miundombinu ya shule za sekondari na hasa shule za msingi bado kuna upungufu ,ambapo mkoa una jumla ya shule za msingi 613 huku za serikali zikiwa ni 562 na 51 ni za watu binafsi “

“Shule za msingi pekee mahitaji ya vyumba vya madarasa ni 700,671, yaliyopo 3,993 na upungufu ni vyumba vya madarasa 3,678 ” alifafanua Ndikilo. Ndikilo alitaja pia tatizo la nyumba za walimu ili waweze kuishi vizuri hivyo kuna mahitaji ya nyumba hizo 6,779 . Alisema ,nyumba zilizopo ni 1,591 na upungufu ni nyumba za walimu 5,188.

Akipokea msaada wa mabati , mkuu wa mkoa wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto )kutoka kwa mkuu wa kitengo cha mahusiano cha kampuni ya Sayona fruits iliyopo Mboga Chalinze ,Abubakar Mlawa (kulia) ,msaada ambayo umeelekezwa kuimarisha sekta ya elimu .( picha na Mwamvua Mwinyi ).


SIMBA WAFANYA KISOMO KWA AJILI YA MO DEWJI, WAZEE WATOA UJUMBE...

CHUO CHA UANDISHI WA HABARI DSJ WAPATA RAIS MPYA, AAPISHWA RASMI

$
0
0
Na Khadija Seif,globu ya jamii

RAIS mpya wa Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam(DSJ) Esther Amandus ameapishwa rasmi huku akitumia nafasi hiyo kutoa shukrani kwa wote walioshiriki uchaguzi huo.

Sherehe za kuapishwa kwa Rais huyo pamoja na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali umefanyika leo chuoni hapo.Pia wanafunzi wengine waliopo na wale waliowasoma chuoni hapo walishiriki tukio hilo.

Akizungumza chuoni hapo Amandus ametoa shukrani kwa kila mmoja aliyeshiriki kwenye uchaguzi kwani wote walifanya uchaguzi wa haki na demokrasia .Amesema anatarajia kufanya kazi na wanafunzi wote wa DSJ katika kuzisikiliza shida ,kero na mahitaji yao ili kutetea maslahi ya chuoni hicho.Pia ameshukuru uongozi chuoni hapo na kuwaomba kushirikiana nao bega kwa bega katika kukiletea maendeleo chuo .

Amesisitiza chuo cha DSJ kimetoa waandishi mahiri ambao wako kwenye tasnia ya habari nchini akiwemo Salum kikeke,Charles Hillary na wengine wengi ambao wameleta mapinduzi kwenye habari na kuwa mifano ya kuigwa kwa mazuri ambayo wanafanya kama kutangaza na kuripoti taarifa kwenye lafudhi zinazoeleweka.

Hata hivyo licha ya kuwepo kwa mafanikio mengi chuoni hapo pia changamoto hazikosekani basi kwa pamoja wakishirikiana na wanafunzi ambao wapo kwa muda mrefu chuoni hapo wataweza kuleta mabadiliko makubwa.
Ametoa rai kwa wanachuo waimarishe umoja na mshikamano ili kukuza demokrasia na utawala bora 
chuoni hapo.

Aidha Rais huyo mpya ameahidi kuyafanyia kazi mapendekezo aliyoyatoa Mkuu wa chuo Joachim Rupepo, kupitiwa upya na kurekebishwa kwa Katiba ya Serikali ya Wanafunzi (DASJOSO).

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Serikali ya mpito Darbina Amani amewashukuru wanafunzi wote chuoni hapo kwa ushirikiano walioonesha kipindi chote walichokua madarakani na kuomba radhi kwa wote ambao waliwakwazwa .

Amani amewataka wanafunzi kuonesha matatzo uadilifu,hekima n heshima juu ya uongo huo mpya ili Kule mabadiliko mengi .

Rais mpya wa Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) Esther Zalamulla akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 12, 2018 jijini baada ya kuapishwa rasmi 

Rais mpya wa Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam(DSJ) Esther Zalamulla (kulia) wakipongezana na Waziri wa Michezo mstaafu Makame Mohamed leo Oktoba 12, 2018 jijini baada ya kuapishwa rasmi 

Picha ya pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chuo hicho wakiwa na Mkuu wa Chuo Joachim Rupepo(wa pili kushoto aliyekaa)

BALOZI WA UGANDA AMUAGA- DK.SHEIN

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Uganda Mhe.Dk.Aziz Ponary Mlima ayefika kumuaga Rais Ikulu Mjini Zanzibar leo,Balozi aliteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli
DSC_2420
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na  Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Uganda Mhe.Dk.Aziz Ponary Mlima  alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kumuaga Rais,Balozi aliteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli
Picha na Ikulu

KILICHOSEMWA NA MSD KUHUSU MAJINA YA DAWA

TAARIFA YA KUANZA KWA VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE

KIHAMIA:UCHAGUZI SIYO VITA , NI UTARATIBU WA NCHI WA KUPATA VIONGOZI

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Liwale,-Lindi

Maandalizi ya uchaguzi mdogo Jimbo Liwale Mkoani Lindi na kata nne Tanzania Bara yamekamikika kwa asilimia 100

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi Taifa (NEC) Dkt. Athumani Kihamia kwamba vifaa vimefika wakati hivyo amewataka wananchi wa Liwale watambue kuwa uchaguzi siyo vita bali ni sera ya nchi ya kupata viongozi kwa kuchaguliwa,

"Vifaa vya uchaguzi vimefika kwa wakati, watendaji wa uchaguzi wamepatiwa mafunzo ya kutosha pia ulinzi na usalama umeimarishwa hivyo wananchi msiogope kuja kupiga kura hapo kesho".'' Kwa upande wa kampeni zipo salama hakuna mtu aliyejeruhiwa wala kurupushani, hakuna malumbano yeyote makubwa ambayo yanaashiria ubunjifu wowote wa Amani''Amesema Kihamia.

Amesema vituo vya kupiga kura vitafunguliwa kesho saa moja asubuhi na vitafungwa majira ya saa kumi jioni 13oktoba 2018, hivyo wananchi wamejitokeze kwa wingi kutimiza haki yao ya msingi ya Kikatiba ya kupiga kura.Aidha wananchi wametakiwa wakishapiga kura warudi manyumbani mwao na kuendelea na shughuli zao za kihalali zinazotekelezwa kila siku.

'' Hakuna haja ya kusema kuwa kuna mwananchi anayelinda kura maana tayari wana mawakala wao kayika mchakato mzima wa upigaji kura hadi kuhesabu hadi kumtangaza mshindi'',Mkurugenzi wa huduma za kisheria kutoka NEC Emmanuel Kawishe amesema hakuna changamoto ila baadhi vyama ambao hawakupata taarifa sahihi kuhusiana na maswala ya mawakala, hadi kufikia kusema tume imekataa wakati ilishakubaliana na vyama hivyo.

Ikumbukwe kuwa uchaguzi huo mdogo unafanyika katika jimbo la Liwale kutoka na aliyekuwa mbunge Zuberi Kuchauka wa awali kuhama kutoka chama cha CUF na kuhamia CCM.
Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi Taifa (NEC) Dkt. Athumani Kihamia akiwa  Liwale leo na kuzungumzia maandalizi ya Uchaguzi ndani ya jimbo hili. Picha na Vero Ignatus. 
Mkurugenzi wa huduma za Kisheria Tume ya Taifa ya Uchaguzi Emmanuel Kawishe. Picha na Vero Ignatus.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA


WANANCHI KISIWANI UNGUJA WAISHUKURU SERIKALI KUPITIA TASAF.

$
0
0
Na Estom Sanga-Zanzibar

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF- Ksiwani Unguja Bw. Ayoub Mohamed Mahmoud amepongeza jitihada zinazofanywa na Mfuko huo katika kutekeleza maelekezo ya serikali ya kusaidia jitihada za kuwandolea kero ya umaskini wananchi. 

Bwana Mahmoud ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi amesema TASAF imekuwa kielelezo sahihi na cha kujivunia katika kutekeleza wa sera za kupambana na umaskini kwa kushajihisha wananchi kujiletea maendeleo kwa kutumia nguvu na raslimali zilizoko kwenye maeneo yao. 

Kiongozi huyo ameyasema hayo wakati alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kianga unatekelezwa na Wananchi kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF kupitia utaratibu wa Mfuko huo wa kuendeleza miundombinu ya Afya,Elimu na Maji kwenye maeneo ya Walengwa. 

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mjini Magharibi amesema miradi iliyoibuliwa na Wananchi kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na TASAF imeleta mageuzi makubwa katika maeneo mengi ya visiwa hivyo kufikia hatua ya baadhi yao kuzalisha bidhaa za kilimo kama vitunguu maji na hivyo kujiongezea kipato na kuukimbia umaskini uliokuwa unawakabili. 

Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw. Ladislaus Mwamanga amesema tangu Mfuko huo ulipoanzishwa na Serikali, umetoa mchango mkubwa katika kusaidia jitihada za kuboresha maisha ya wananchi huku akisisitiza kuwa mafanikio hayo yametokana na sera sahihi za kupambana na umaskini zinazoratibiwa na serikali. 

Bwana Mwamanga amesema TASAF imekuwa ikizingatia kwa kina maelezo ya Serikali yanayotilia mkazo pamoja na mambo mengine umuhimu wa wananchi wakiwemo Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuondokana na adha ya umaskini na kujiongezea kipato chao. 

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amesema licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini, Serikali kupitia Mfuko huo imeamua kubosheresha kuboresha zaidi utekelezaji wa Mpango huo ili uweze kuwafikia wananchi wote wanaokabiliwa na Umaskini nchini huku msisitizo ukiwa ni kuibua shughuli za uzalishaji mali kwa kufanya kazi na kisha kulipwa kulingana na kazi watakayokuwa wameifanya. 

Kwa Upande wao wananchi wa shehia ya Kianga wameishukuru Serikali kwa kuuwezesha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kutekeleza miradi kadhaa ya maendeleo kwenye shehia yao ukiwemo mradi huo mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Afya kitakachowapunguzia adha ya kufuata huduma hiyo mbali na eneo lao.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,bw. Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akihutubia wananchi wa Shehia ya Kianga,wilaya ya Magharibi A mkoa wa Mjini Magharibi kisiwani Zanzibar (hawapo pichani) baada ya kukagua ujenzi wa kituo cha Afya unaotekelezwa na TASAF kwa kushirikiana na Wananchi wa eneo hilo.


 Mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi ,Unguja Bw. Ayoub Mohamed  Mahmoud (aliyesisima nyuma ya meza) akiwahutubia wananchi wa Shehia ya Kainga baada ya kukagua ujenzi wa jengo la kituo cha Afya cha shehia hiyo unaojengwa na TASAF kwa kushirikiana na wananchi.

 Mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi Bw. Mahmoud akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw.Mwamanga na maafisa wa serikali baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Kituo cha Afya-Kianga (nyuma yao)

 Baadhi ya wananchi wa Shehia ya Kianga kisiwani Unguja wakisikiliza hotuba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Ladislaus Mwamanga( hayupo pichani) baada ya kukagua jengo la kituo cha Afya kinachojengwa na TASAF kwa kushirikiana na Wananchi.

 Sehemu ya jengo la Kituo cha Afya Kianga katika mkoa wa Mjini Magharibi kinachoendelea kujengwa TASAF na Wananchi wa eneo hilo ambacho kitapunguza tatizo la kufuata huduma za Matibabu mbali na eneo lao.

19 YEARS MEMORIAL OF THE LATE MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

ULEGA AFUNGUA RASMI MAONESHO YA NNE YA NDEGE WAFUGWAO NCHINI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii

NAIBU Waziri wa kilimo na uvuvi na Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega amezindua rasmi maonesho ya nne ya ndege wafugwao katika viwanja vya maonesho (sabasaba) jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo Ulega ameeleza kuwa maonesho ya mwaka huu yamehusisha makampuni mengi ya ndani na nje ya nchi kama Kenya, Poland na China na amewakaribisha kuwekeza nchini kutokana na kuwepo kwa fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali.

Aidha ametoa pongezi kwa vyama vyote vya wadau wa ndege wafugwao chini ya chama mama cha Tanzania Poultry show (TPS) kwa kutoa kipaumbele katika suala la ufugaji wa kuku.Pia amewataka kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja  na wao kama serikali wapo pamoja kama walezi wao, katika kuhakikisha wanasonga mbele zaidi na amewapongeza kwa ushirikiano wao kupitia vyama vyao.

Ulega amesema kuwa Rais Magufuli ameendelea kusimamia maendeleo ambapo hadi sasa tozo zilizokuwa kero kwa wafugaji, wakulima na wavuvi zimeondolewa ili kuweza kuendeleza shughuli za hizo.Kuhusiana na changamoto zilizotolewa na wafugaji hao hasa katika mashudu na soya ambazo huagizwa kutoka nje Ulega amesema kuwa maandalizi yameanza katika nyanda za juu kusini ambako soya zimelimwa na wanavutia uwekezaji katika usindikaji ili kuweza kuvutia uwekezaji wa kuchakata soya na kupunguza gharama za kuagiza bidhaa hizo kutoka nje.

Kuhusiana na machinjio zinazochinja kuku Ulega amesema kuwa sehemu hizo zimekuwa na ubora wa chini sana na amewataka wahakikishe wanaboresha machinjio hayo yanayosimamiwa na halmashauri na manispaa hasa kwa kuzingatia wanaweka  sehemu ya machinjio ya kuku ili kuleta thamani.Mwenyekiti wa chama cha ndege wafugwao Harko Bhaghat amemshukuru Naibu waziri na wizara kwa ujumla kwa kutoa kipaumbele kwa wafugaji na kusema kuwa hadi sasa wamepata mafanikio makubwa na kubwa zaidi ni baada ya serikali kuondoa tozo katika bidhaa za mifugo.

Bhaghati amewataka wafugaji kujisajili ili waweze kupata fursa mbalimbali za kuendeleza soko la ndege wafugwao hasa kuku.
Naibu Waziri wa  Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wafugaji wa ndege wafugwao, katika ufunguzi wa maonesho ya nne ya ndege wafugwao nchini jana jijini Dar es Salaam . (Picha na Emmanuel Massaka wa Globu  ya Jamii)
 Mwenyekiti wa chama cha wafugaji wa ndege Harko Bhaghati akisoma risala mbele ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Abdallah Ulega.
 Mtaalamu na mshauri wa mifugo kutoka kampuni ya Animal Care Dkt. Bakari Mwanga akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega  kuhusu uzalishaji na utunzaji wa mifugo unaofanywa na kampuni yao.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akitembelea mabanda mbalimbali katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam
Sehemu ya wafugaji waliojitokeza ili kupata semina na mafunzo kuhusiana na ufugaji wa kuku.

SERIKALI IPO TAYARI KUSAIDIA WAWEKEZAJI WA MADINI-NYONGO

$
0
0
Na Greyson Mwase, Sumbawanga

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini ipo tayari kuwasaidia wawekezaji kwenye shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini ili uchimbaji wao ulete manufaa kwa nchi.

Aliyasema hayo leo tarehe 12 Oktoba, 2018 mara baada ya kumaliza ziara yake katika mgodi wa makaa ya mawe wa Edenville International (T) Limited uliopo katika kijiji cha Nkomolo II Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku moja katika mkoa huo yenye lengo la kukagua shughuli za uchimbaji wa madini, kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wa madini.

Katika ziara yake Nyongo aliambatana na Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Giliard Luyoka, Katibu Tawala Msaidizi – Sehemu ya Miundombinu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Happiness Shayo, Wataalam wa Madini, Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na waandishi wa habari.

Alisema kuwa katika kuhakikisha watafiti na wachimbaji wa madini wanafanya kazi katika mazingira mazuri, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imeanza kusogeza huduma zake kwa kuhakikisha kuwa inaanzisha ofisi za maafisa madini wakazi katika mikoa yote ambapo mkoa wa Rukwa unatarajiwa kupata ofisi kwa mara ya kwanza.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Nyongo aliushauri uongozi wa mgodi huo kujikita kwenye uzalishaji wa makaa ya mawe ambayo ni bora na kuuza katika nchi za jirani kwa kuwa mahitaji ya makaa ya mawe ni makubwa.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ( wa kwanza mbele) akiendelea na ziara katika mgodi wa makaa ya mawe wa Edenville International (T) Limited uliopo katika kijiji cha Nkomolo II Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa. 
Meneja wa mgodi wa makaa ya mawe wa Edenville International (T) Limited, Jamhuri Mbamba (kushoto) akimwonesha Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) moja ya makaa ya mawe kwenye mgodi huo. 
Meneja wa mgodi wa makaa ya mawe wa Edenville International (T) Limited, Jamhuri Mbamba (katikati) akielezea hali ya uzalishaji wa makaa ya mawe katika mgodi huo kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) katika ziara hiyo.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

“TUSICHANGANYE SIASA KWENYE MAENDELEO” – GAVANA SHILATU

$
0
0

Na Mwandishi Wetu, Mihambwe 

Mara nyingi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. John Pombe Magufuli amekuwa akisisitiza maendeleo hayana chama akiwa na maana kwenye suala la maendeleo tuweke pembeni itikadi za kisiasa na tuungane kuleta maendeleo. 

Kauli inayofanana na hiyo imesemwa na Afisa Tarafa wa Mihambwe, Gavana Emmanuel Shilatu wakati alipotembelea mradi wa maji wa kijiji cha Mihambwe uliopo kata ya Mihambwe ambapo ameshangazwa na mradi mzuri wa maji kutokufanya kazi kutokana na misuguano ya kisiasa. 

“Hii tabia ya kupangua pangua maamuzi halali ya vikao, tabia ya mivutano ya kisiasa isiyo na tija ni sehemu ya tatizo ya kusimama kwa mradi huu. Ulivyo simama mmepata faida gani? Wewe uliyesababisha hauathiriki na tatizo la ukosefu wa maji? Acheni hizi tabia, tushirikiane kwa pamoja tuhakikishe mradi huu wa maji ufanye kazi tena kama awali” alisema Gavana Shilatu wakati alipotembelea eneo lilipo mradi huo wa maji. 

Wakizungumza mara baada ya ziara hiyo, Mjumbe wa Serikali ya Kijiji alimwomba Gavana Shilatu azidi kuwaunganisha zaidi wawe kitu kimoja. 

“Leo hili kwetu ni tukio la kipekee la sote kwa pamoja kukutana na kujadili mambo ya kimaendeleo. Ninamwomba Afisa azidi kuitisha vikao vya kutuunganisha na kutuweka kwenye mstari mmoja. Kiukweli nimependa sana anavyotuleta pamoja kwenye masuala ya kimaendeleo.” alisema Mjumbe wa Serikali ya Kijiji ya Mihambwe. 

Ziara hiyo ya kutembelea mradi wa Maji, Gavana Shilatu aliambatana na Mtendaji Kata, Afisa Maendeleo kata ya Mihambwe, Serikali ya Kijiji cha Mihambwe pamoja na Wajumbe wa kamati ya mradi wa maji.
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images