Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110150 articles
Browse latest View live

TRA EDUCATES SWEDISH INVESTORS

$
0
0
Veronica Kazimoto,Dar es Salaam 

The Tanzania Revenue Authority (TRA) has provided tax education and explanations on tax matters in relation to investments environment in various sectors in the country.

Speaking to the Swedish Business delegation during a seminar held in Dar es Salaam, TRA’s Director for Taxpayer Services and Education Mr. Richard Kayombo said that, Tanzania tax laws grant various tax incentives in order to make it possible for investors to be encouraged to invest in specific sectors but also give them relief to bring in capital goods and Technology for the benefit of industrialization agenda that is key for the 5th phase government.

The reliefs are embedded in the various tax laws that include the East African Customs Management Act, VAT Act 2014 and the Income Tax.

“Among the incentives granted include Common External Tariffs which applies to all imported goods into the region with three rates of 0%, 10% and 25% depending on the type of goods, harmonized East African Community tariffs of zero rate for imports of raw materials, capital goods, replacement parts, inputs for agriculture, animal husbandry, fishing, livestock and pharmaceuticals medicaments,” Mr Kayombo said.

He added that, “Other incentives under corporate tax include a reduced rate from normal 30% to 25% charged for three years to newly listed companies with the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE), 20% for a new entity dealing in manufacturing of pharmaceuticals and leather products and 10% rate for corporations investing in a plant for assembling Motor Vehicles, tractors and fishing auto boats”.

Under the Value Added Tax (VAT), Mr Kayombo pointed some incentives including zero rate for all exports, exemptions of various items as provided in the respective tax laws that include exemption of imported machinery by local manufacturers and processors of vegetable oil, Textiles, pharmaceuticals, hides and skins and leather manufactured in Tanzania Mainland. On the other hand, he assured the Swedish Business delegates that, as a way fighting corruption, the Authority has a fully-fledged department responsible for staff ethics and integrity so that taxpayers may be treated fairly and with respect.


The Tanzania Revenue Authority’s Director for Taxpayer Services and Education Mr Richard Kayombo explaining tax issues in relation to investments environment in various sectors in Tanzania during the Swedish Business delegation seminar held in Dar es Salaam. 
The Tanzania Revenue Authority’s Director for Taxpayer Services and Education Mr Richard Kayombo explaining tax issues in relation to investments environment in various sectors in Tanzania during the Swedish Business delegation seminar held in Dar es Salaam. 

The Tanzania Revenue Authority’s Director for Taxpayer Services and Education Mr Richard Kayombo explaining tax issues in relation to investments environment in various sectors in Tanzania during the Swedish Business delegation seminar held in Dar es Salaam. Centre is a Senior Investment Manager at Swedfund Ms Audrey Obara and right is a Director and co-founder MTI Investment Dr. Neema Mori. 
Some Swedish Business delegation listening to the Tanzania Revenue Authority’s Director for Taxpayer Services and Education Mr Richard Kayombo (not in picture) during a seminar held in Dar es salaam. 


FOR MORE NEWS CLICK HERE


RC MAKONDA atoa tamko tukio la kutekwa kwa MO DEWJI.

IGP APOKEA KAMERA MAALUM KUSAIDIA MAPAMBANO YA UHALIFU

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akipokea kamera maalum (Drons) kutoka kwa Mwakilishi wa kampuni ya Kifaru Ifigenia Anselmi walipokutana Makao Makuu ya Polisi ambapo kampuni hiyo imetoa kamera tatu kwa ajili ya kusaidia mapambano ya uhalifu hapa nchini .Picha na Jeshi la Polisi

BENKI YA TIB CORPORATE WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUWATEMBELEA TRC, NIC

$
0
0
BENKI ya TIB Corporate washeherekea wiki ya huduma kwa wateja kwa kutembelea wateja wake.

Leo Oktoba 11 benki hiyo wamewatembelea Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Bima la Taifa (NIC) ikiwa ni kwaajili ya kuwashukuru pamoja na kujitadhimini jinsi ya utoaji wa huduma kwa wateja wao.

Akizungumza na wafanyakazi wa benki hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amewashukuru wafanyakazi wa benki hiyo kwa kuwaona wamhimu katika kuendeleza gurudumu serikali ya viwanda hapa nchini kwa utunzaji wa fedha.

Nae Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga amewashukuru kwa kuona nchango wa shirika hilo pia pia amewaasa kujitangaza zaidi ili kuondoa mkanganyiko uliopo katika jina la benki hiyo.


Mkurugenzi mkuu wa benki ya TIB Corporate Frank Nyabundege akizungumza na wafanyakazi wa beki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo Oktoba.
Meneja kitengo cha sheria wa benki ya TIB Corporate Berina Rugaiyamu
 akimkabidhi ua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa baada ya kutembelewa ofisini kwake na wafanyakazi wa TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru wateja wa benki hiyo katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa  akifurahia jambo mara baada ya kutembelewa na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo.
meneja wa rasilimali watu  wa benki ya TIB Corporate Irene Ungani Kyara  akiwamkabidhi Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga mara baada ya kumtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kwaajili ya kushaherekea pamoja na kujitathimini katika wiki ya huduma kwa wateja ambapo benki hiyo imeadhimisha mwaka huu kwa kuwatembelea wateja wake mahali walipo.
Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga mwenye miwaniakizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo  ikiwa ni adhima ya benki hiyo kuwatembelea wateja wake.


Picha za pamoja za wafanyakazi  wa benki ya TIB Corporate.

TASAF YAKUTANA NA WADAU WA MAENDELEO KUJADILI MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI.

$
0
0
Na Estom Sanga -TASAF

Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF imekutana na Wadau wa Maendeleo kujadili masuala mbalimbali ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaohudumia takribani kaya Milioni Moja na Laki Moja nchini kote.

Akitoa taarifa katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bwana Ladislaus Mwamanga amesema hatua kubwa imepigwa katika utekelezaji wa Mpango huo huku akiishukuru Serikali na Wadau wa Maendeleo kwa kuendelea kutoa msaada muhimu katika kufikia mafanikio hayo.

Aidha Bwana Mwamanga amesema msaada wa Serikali na Wadau wa Maendeleo unaoendelea kutolewa umeusaidia kwa kiwango kikubwa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF kuandaa kwa ufanisi Awamu ya Pili ya Mpango huo inayotarajiwa kuanza hapo mwakani.

Amesema maandalizi hayo yanazingatia kwa kiwango kikubwa maelekezo ya Serikali yanayosisitiza umuhimu wa walengwa kufanya kazi za uzalishaji mali ili hatimaye waweze kuondokana na umaskini na kuboresha maisha yao.

Bwana Mwamanga amesema TASAF imekuwa ikitiwa moyo na namna Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wanavyoendelea kutumia fursa hiyo muhimu ya kujumuishwa kwenye Mpango kwa kuzingatia masharti ya Mpango huo.

Vikao vya pamoja kati ya menejimenti ya TASAF na Wadau wa Maendeleo hufanyika kwa lengo la kuona namna shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini zinavyotekelezwa ili kukidhi matakwa na maagizo ya serikali ya kuhakikisha kuwa kero ya umaskini miongoni mwa walengwa inatokomezwa. 
 Wajumbe wa kikao cha menejimenti ya TASAF na Wadau wa maendeleo wakifuatilia mjadala kwenye kikao chao cha kila mwezi kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa TASAF.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga (mbele) akiongoza kikao cha wadau wa maendeleo na menejimenti ya TASAF.

MO UPDATES: TAARIFA KAMILI YA KUTEKWA NYARA KWA MO DEWJI

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU MZUMBE WAASWA KUJINOA NA MITIHANI YA BODI YA NBAA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam katika kozi ya uhasibu wameaswa kujinoa vizuri katika mitihani ya Bodi ya Uhasibu Nchini (NBAA) ili waweze kufanya vizuri katika mitihani hiyo ambayo itaanza hivi karibuni.

Akizungumza na wanafunzi wa wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam Afisa Mitihani wa Bodi ya Uhasibu (NBAA) Humphre Sympholian amesema kuwa mitihani ya bodi sio migumu kinachotakiwa kwa wanafunzi kujiandaa vizuri ambapo wanaweza kufanya vizuri.

Amesema kuwa kwa wale wanaofanya kazi katika kipindi kilichobaki waweze kuomba ruhusa ya kwa ajili ya kujiandaa na mitihani hiyo na kuweza kupata cheti mahususi kwa ajili ya uhasibu (CPA).Sympholian amesema kuwa mitihani hiyo wamekuwa mtihani wa bodi hiyo hauna upendeleo hivyo kila mtu atapata alichokipanda katika kujiandaa kwake na huo mtihani.

“Hatuna upendeleo kwani wanaosimamia sio ndio wanaosahihisha na kusahihisha huko hakuna majina ya wanafunzi kilichopo ni namba tu ambapo hawezi kupenya mwanafunzi wa kwa upendeleo”amesema Sympholian. Mhasibu na Mwalimu wa Chuo Kikuu Mzumbe Victirius Kamuntu amesema kuwa wanafunzi wake wamejiandaa na kuwa na imani kuwa mitihani ya bodi watatafanya vizuri.

Amesema kuwa Chuo Kikuu Mzumbe katika mitihani ya bodi hiyo kwa wanafunzi chuo hicho wamekuwa wakifanya vizuri hivyo kukutana na watu wa bodi kunawafanya kuongeza juhudi ya kufikia malengo 
Mwisho 
Afisa Mitihani wa Bodi ya Uhasibu (NBAA) Humphre Sympholian akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe kuhusiana na mitihani ya Bodi itayofanyika hivi karibuni alipokutana na wanafunzi hao katika Chuo hicho jijini Dar es Salaam.
Afisa Mitihani wa NBAA, Rebecca Siame akieleza sheria zinazotumika na Bodi ya NBAA katika usimamizi wa Mitihani na mwanafunzi atakayebainika kufanya udanganyifu matokeo yake kufutwa wakati alipokutana na wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wanaojiandaa na Mitihani ya Bodi ya Uhasibu Nchini(NBAA).

WAGONJWA WA MACHO 300 NCHINI WAFANYIWA UPASUAJI NDANI YA SIKU TANO

$
0
0
Na WAJMW-DODOMA
Watu wenye matatizo ya macho takribani 700 wamefanyiwa uchunguzi na kati ya hao wagonjwa 300 waliobainika kuwa na matatizo ya macho wamefanyiwa upasuaji na kurejeshewa hali ya kuona vizuri.
Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Mpango wa Huduma za Macho kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Bernadetha Shilio wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya siku ya afya ya macho duniani kilichofanyika mapema leo katika viwanja vya Nyerere jijini Dodoma.
“Siku ya afya ya macho duniani ina lengo kuu la kuhamasisha utekelezaji wa dira ya kimataifa ya kutokomeza upofu unaozuilika ifikapo mwaka 2020, na kutathmini haki ya kuona kwa wote ambapo mwaka 2003 serikali ya Tanzania iliungana na mataifa mengine duniani katika kutekeleza azimio hilo”. Alisema Dkt. Shilio
Dkt. Shilio amesema Serikali ya Tanzania inashirikiana na mataifa mengine duniani kuadhimisha siku ya afya ya macho ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa jamii, kutoa huduma za uchunguzi wa macho pamoja na kufanya upasuaji kwa wagonjwa ambao watabainika kuwa na matatizo.
Pia Dkt. Shilio ameiasa jamii ya kitanzania kuzingatia kanuni sahihi za utunzaji wa macho ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza na kusababisha uono hafifu na kupelekea upofu. 
“Matumizi ya rangi na kope bandia kwenye ukingo wa macho, kuvaa miwani bila kupima, kutumia dawa za mgonjwa mwingine wa macho bila ushauri wa daktari, kutokula vyakula bora vyenye virutubisho na kutokua na tabia ya kupima macho angalau mara moja kwa mwaka vimetajwa kuwa visababishi vikubwa vya kuathiri afya ya macho” alisema Dkt. Shilio.
 Mtaalam kutoka Taasisi inayojishugulisha na afya ya macho ONA  Bi. Haika Urasa kulia akitoa miwani ya kusomea kwa mmoja wa wakazi wa Dodoma aliyefika kupata huduma ya afya ya macho katika viwanja vya Nyerere Square wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Afya ya Macho yaliyofanyika mkoani humo leo.
 Mtaalamu wa magonjya yasiyoyakuambukiza Dkt. Nleminyanda Hezron katikati akitoa huduma za kupima sukari kwa baadhi ya wakazi wa Dodoma kupata huduma hizo katika viwanja vya Nyerere Square wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Afya ya Macho yaliyofanyika mkoani humo leo.
 Moja ya Wataalam  wa Afya ya macho akitoa elimu juu ya afya ya macho kwa baadhi ya wakazi wa Dodoma waliofika  katika viwanja vya Nyerere Square wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Afya ya Macho yaliyofanyika mkoani humo leo.

Baadhi ya wakazi wa Dodoma waliofika  katika viwanja vya Nyerere Square  wakisubiri kupata huduma ya afya ya macho na magonjwa yasiyoyakuambukiza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Afya ya Macho yaliyofanyika mkoani humo leo. PICHA NA WIZARA YA AFYA

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Acacia Yachafuka kwa Tuhuma za Rushwa

$
0
0
Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia, kupitia kampuni yake ya North Mara Gold Mine iliyopo mkoani Mara, imeingia katika kashfa baada ya Maafisa Waandamizi wa kampuni hiyo wawili kushtakiwa kwa tuhuma za rushwa ili kupata upendeleo dhidi ya maslahi ya wanavijiji na Serikali ya mkoa huo.

Washtakiwa wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Tarime siku ya Jumatato Oktoba 10, 2018 na kusomewa mashtaka ya rushwa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007.

Kwa nyakati tofauti, watuhumiwa Marteen Van Der, Johannes Jensen, Joseph Kleruu, Bomboga Chikachake, Tanzania O’mtima na Abel Kinyimari wameshtakiwa kwa utoaji na upokeaji wa rushwa wa namna mbalimbali kwa Maafisa wa Serikali na wanasiasa wa mkoani Mara.

Mei 17, 2013 watuhumiwa Marteen Van Der na Johannes Jensen walitoa rushwa ya jumla ya shilingi 93,896,000 kwa Mthamini Mkuu wa Ardhi wa Serikali Adam Yusuph pamoja na kumpa Peter Mrema 30,000,000 ili kupata upendeleo wakati wa upimaji wa ardhi kwa ajili ya kupanua eneo la mgodi huo.

Vile vile mnamo Machi 7, 2012, Mthamini Mkuu wa Ardhi wa Serikali, Joseph Thomas Kleruu alipewa tenda ya kufanya tathmini ya shamba Na. 190 lililopo mkoani humo kinyume cha sheria ili kuwasaidia kupata eneo la kupanua mgodi huo.

Imeelezwa kuwa kati ya Januari 2013 na Disemba 2017, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyakunguru, Abel Mnyakibari alipewa rushwa ya jumla ya shilingi 966,687,343 kutoka katika mgodi huo ili ajiepushe na kukataa kuwalipa fidia baadhi ya wanakijiji vile vile kati ya Januari 2010 na Disemba 2015, Mwenyekiti huyo alipewa rushwa ya jumla ya shilingi 90,251,475 kwa ajili ya kumshawishi asifatilie fidia ya wanakijiji zaidi ya 800 wa Kijii cha Kewanja.

Kati ya Januari 2006 hadi Mei 2018, Diwani wa Kata ya Kemambo na Mkurugenzi Mtendaji, Bogomba Chichake na Tanzania O'mtima walipewa zabuni ya shilingi 7,709,575,914,19 na shilingi 1,102,880,8 ili kutoihamisha shule ya Nyabigena kutoka eneo la Mrambwe kwenda eneo la Mgema kwa ajili ya kuusaidia mgodi huo kujenga shule kwa bei nafuu.

Kampuni ya Acacia inamiliki migodi mitatu ya dhahabu nchini ikiwemo ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi, imeandikishwa katika soko la hisa la London. Mnamo Julai 2017, Kampuni hiyo iliipeleka Tanzania katika Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi kuhusiana na katazo la kusafirisha makinikia.

MAKUMBUSHO YA NYERERE KUFANYIWA DUA BAGAMOYO

$
0
0
FAMILIA ya sheikh Mohammed Ramiya, imeiangukia serikali na wizara ya utalii kuangalia uwezekano wa kuweka sehemu ya kumbukumbu kati ya hayati sheikh Ramiya na Mwl.J.K Nyerere, eneo la Zawiyani kata ya Dunda,Bagamoyo ili kuenzi historia ya ukombozi wa nchi yetu .

Aidha familia hiyo inakumbuka wakati marehemu sheikh Ramiya (78) akiugua kabla ya kufikwa na umauti wake mwaka 1985 ,Mwl. Nyerere alimchukua kumuuguza nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam .

Akizungumzia namna anavyomkumbuka hayati Mwl.Nyerere, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya, aitwae Ramiya Mohammed Ramiya alisema ,watalii wengi wakienda kwenye makumbusho za Bagamoyo wanakuta historia ya sheikh huyo na hayati Mwl. J.K Nyerere .

Alieleza watalii hao, huwa na shauku ya kwenda kujua historia ya picha na nyumba aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi huyo ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961.

Ramiya alisema ,enzi hizo mwalimu Nyerere alikuwa rafiki wa sheikh Ramiya ,na alipelekwa huko na wazee wa Dar es salaam kwa nia ya kuombewa dua kwa ajili ya kupata uhuru bila kumwaga damu .

"Tukiacha marehemu baba kupigania uhuru,kuheshimika lakini pia sheikh Ramiya alikuwa mtu wa dini hivyo tutapendezwa kama serikali itatambua umuhimu wa kuweka makumbusho hiyo hapa basi iwe ya kidini zaidi " 

"Historia itakuwa haipotei ,lakini iwe tofauti kwa kuwa ni sehemu ya dini ,haitowezekana eneo hilo watu wakawa nje ya maadhi ya kiislamu ,isiruhusiwe wadada kwenda vichwa wazi ,ama kuvaa suruali bila kujistili " alibainisha Ramiya .
 Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya ,aitwae Ramiya Mohammed Ramiya akielezea namna anavyomkumbuka hayati Mwl. J. K .Nyerere huko Zawiyani ,Bagamoyo. (Picha na Mwamvua Mwinyi)
 Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya   ,aitwae Ramiya Mohammed Ramiya (wa kulia )akionyesha historia ya  nyumba aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi hayati Mwl.J.K Nyerere ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961, nyumba ambayo kwasasa ina karne mbili  , imekuwa gofu na ilijengwa kwa mawe ,(wa kushoto) ,Mwenyekiti wa CCM Bagamoyo alhaj Abdul Sharif .
 Jumba lenye historia aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi hayati Mwl.J.K Nyerere ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961, nyumba ambayo kwasasa ina karne mbili  , imekuwa gofu na ilijengwa kwa mawe ,ipo eneo la Zawiyani ,Dunda wilayani Bagamoyo.
Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya, aitwae Ramiya Mohammed Ramiya, akionyesha historia ya picha mbalimbali baina ya hayati sheikh Ramiya na Mwl. J.K. Nyerere.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAMPUNI YAZINDUA SMART MAUZO KULETA UAMINIFU KATI YA MMILIKI NA MSIMAMIZI KIBIASHARA

$
0
0
 Khadija Seif,Globu ya jamii
KAMPUNI ya Oval Technical Limited wametambulisha  application mpya ya kibiashara inayojulikana kama SMART MAUZO kwa lengo la kukabiliana na changamoto za kibiashara.

Meneja Mauzo wa kampuni hiyo Hamza Mohamed amesema leo jijini Dar es Salaam amesema  lengo la kuanzishwa kwa mfumo huo kuwa kumekuepo kwa changamoto nyingi nchini zinazowakabili wafanyabiashara.

Ametaja baadhi ya changamoto kama kutohifadhi taarifa sahihi za mauzo ya bidhaa zao na kupelekea kupata hasara katika biashara zao.

Pia amesema changamoto nyingine ni kutokua na uaminifu baina ya mmiliki na msimamizi kutofahamu idadi ya manunuzi yanayofanyika kila siku,wiki,mwezi Kwenye duka .

Mohammed amesema mfumo  huo utawawezesha wafanyabiashara wengi nchini kutatua changamoto zao na mpaka sasa zaidi ya wanafanyabiashara 200 wamejisajiri na huduma hiyo ya Smart Mauzo.

Aidha amesema , kujiunga na mfumo huo unaingia kwenye uwanja wa kupakua huduma za kimtandao na kuandika www.smartMauzo.com na kisha kulipia huduma hiyo kwa kiasi cha Sh.5000 za kitanzania na kwa mwezi na ukishasajiriwa utaweza kulipia Sh.3000 kwa kila mwezi.

Ametoa rai kwa ambao hawajajisajiri waweze kujisajiri ili kuleta chachu katika sekta ya biashara kwani kuna msemo usemao mali bila daftari huisha bila habari, hivyo basi daftari hilo ni mtandao huo ambao utawezesha kuandika kila taarifa ya manunuzi pamoja na bidhaa zilizodukani.
Meneja masoko kampuni ya oval technique limited Hamza Mohammed akizungumza na wanahabari wakati akitambulisha huduma ya smart Mauzo jijini Dar es salaam.

NAHODHA WA SERENGETI BOYS ATIMKIA DENMARK KUKIPIGA KABUMBU

$
0
0
Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
MCHEZAJI wa kikosi cha Serengeti boys  Maurice Abraham ameanza majaribio katika klabu ya Midtjylland  nchini Denmark, ambao ndio mabingwa wa ligi kuu msimu uliopita 2017-18 nchini humo.

Ambapo Klabu hiyo ya Midtjylland ni matokeo ya  vilabu viwili mahasimu (Ikast na Herning) vilivyomua kuungana mwaka 1999 na kuunda klabu moja  iliyipanda daraja kucheza ligi kuu ya Denmark Danish Superliga  Mwaka 2000.

 Klabu hiyo  katika msimu wa 2014-15 ndio ilishinda taji la Danish Superliga kwa mara ya kwanza kabla ya kushinda tena taji  hilo mara ya pili msimu huo uliopita. 

Maurice a.k.a chuji ambaye ni Nahodha wa timu ya Taifa ya vijana U-17 alipata mualiko kutoka nchini Denmark kufanya majaribio katika klabu ya Midtjylland baada kuonyesha kiwango cha juu mno katika michuano ya kuwania Afcon 2019 kanda ya Cecafa ambapo Serengeti ilimaliza ikiwa imeshikilia nafasi ya tatu. 

Kocha mkuu wa Serengeti boys Oscar Mirambo ambaye pia ni kaimu mkurugenzi wa ufundi wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, amesema kuwa  Chuji aliondoka Oktoba 7  ambapo alipata mualiko wa  kwenda nchini Denmark  kwa ajili ya majaribio. 

"Nyota wengi wa kikosi hicho cha vijana ambao ndio wenyeji wa fainali Za Afcon 2019 watakaondoka kwa utaratibu Kama uliofanywa kwa Maurice"amesema Mirambo. 

Kocha mirambo amesema "mialiko ipo mingi na baadhi ya wachezaji ila siwezi kusema nani anafuata sasa, lakini Maurice ameanza na tunasubiri taratibu  zikamilike kwa wengine ndipo tutaweka wazi"

Wananachi wa Mikoa ya Nyanda za juu kusini watakiwa kushiriki maonyesho ya Mifuko ya Uwezeshaji

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
BARAZA la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limewataka wananchi wa Mikoa Nyanda za Juu Kusini kushiriki maonyesho ya bidhaa za wajasiriamali na huduma za mitaji yatakayo fanyika katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe mjini Mbeya kuanzia tarehe 19 hadi 23, Octoba, 2018 ili kujionea fursa za uwezeshaji kuelekea katika uchumi wa viwanda.

Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi. Beng’i Issa alisema hayo jana jijini Dar es Salaam kuwa maonyesho hayo hayo ni ya bidhaa za wajasiriamali na huduma za mitaji na yatafunguliwa na Waziri Kassim Majaliwa Octoba 20, 2018 na ambayo yanalenga kunadi fursa za uwezeshaji.

“Maonyesho haya yatawezesha upanuaji wa wigo wa masoko ya wajasiriamali wanaotengeneza bidhaa za mikono kwa kutumia mali ghafi za Tanzania,” na hiyo inatoa hamasa kwa wananchi kujikita katika viwanda vidovidogo.

Baraza limeshirikiana na Mifuko ya Uwezeshaji, Vikundi vya kifedha na program za serikali za uwezeshaji kuandaa maonyesho hayo na yatafungwa na Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji, Bw. Charales Mwijage, aliongeza kusema,Bi. Issa. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Bengi Issa wa pili kushoto akisisitiza jambo wakati walipokuwa akizungumza kuhusu maonyesho ya Mifuko ya Uwezeshaji, Taasisi za Vikundi vya Kifedha na program za uwezeshaji yatakayo fanyika Viwanja vya Ruanda Nzovwe Mbeya kuanzia tarehe 19 hadi 23 octoba 2018, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Kusaidia Sekta Binafsi ya Kilimo (PASS), Bw. Nicomed Bohay, kushoto mwakilishi wa IR-VICOBA, Bi. Augustina Mosha na wa pili kusho ni Mwenyekiti wa VICOBA FETA,Bw. Filbert Sambali. (Picha na Mpiga Picha wetu, Dar es Salaam).

ATUMIA MSAFARA WA MAGARI YA WAOMBOLEZAJI KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limemkamata kijana mmoja jina linahifadhiwa mkazi wa Daraja Mbili halmashauri ya jiji la Arusha akiwa na kilogramu 207 za dawa ya kulevya aina ya Mirungi.

Akitoa taarifa hiyo mapema leo ofisini kwake, Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi alisema kwamba, mtuhumiwa huyo alikamatwa jana saa 6:00 Mchana akiwa anatokea mpakani mwa mkoa wa Kilimanjaro kuingia mkoa wa Arusha aliamua kutumia mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa hazo kwa kujipachika katikati ya msafara wa magari yaliyokuwa yanakwenda msibani.

Kamanda Ng’anzi alisema kwamba Jeshi hilo lilipata taarifa juu ya uwepo wa mtu huyo aliyekuwa anasafirisha Mirungi kwa kutumia gari ndipo walipowapeleka askari haraka katika eneo la Kikatiti wilayani Arumeru na kuweka mtego.

“Wakiwa katika eneo hilo baada ya muda askari hao waliona gari aina ya Suzuki Escudo rangi ya Kijivu lenye namba za usajili T 505 CNC likiwa katikati ya msafara wa magari yaliyokuwa yanaelekea msibani lakini kwa umahiri mkubwa walilibaini ndipo wakalizuia”. Alifafanua Kamanda Ng’anzi.

Kamanda Ng’anzi alisema kwamba baada ya kufanya upekuzi waligundua kuwepo kwa dawa hazo yaliyohifadhiwa nyuma ya “boot” yakiwa yamehifadhiwa kwenye viroba tofauti tofauti vyote vikiwa na uzito wa kilogramu 207.
  Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) ramadhani Ng'anzi akiwaonyesha waandishi wa habari viroba mbalimbali vya dawa za kulevya aina ya Mirungi vilivyokuwa vinasafirishwa kwa kutumia gari aina ya Suzuki Escudo lenye namba za usajili T 505 CNC. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
Gari aina ya Suzuki Escudo rangi ya kijivu lenye namba za usajuili T. 505 CNC ambalo lilikamatwa eneo la Kikatiti wilayani Arumeru likiwa na viroba vya dawa za kulevya aina ya Mirungi yenye uzito wa Kilogramu 207.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi akionyesha baadhi ya pikipiki zilizokamatwa kutokana na msako ambazo zilikuwa zinatumiwa na wahalifu waliokuwa wanapora pochi kwa watembea kwa miguu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU MZUMBE WAASWA KUJINOA NA MTIHANI YA BODI YA NBAA

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam katika kozi ya uhasibu wameaswa kujinoa vizuri katika mitihani ya Bodi ya Uhasibu Nchini (NBAA) ili waweze kufanya vizuri katika mitihani hiyo ambayo itaanza hivi karibuni.

Akizungumza na wanafunzi wa wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam Afisa Mitihani wa Bodi ya Uhasibu (NBAA) Humphre Sympholian amesema kuwa mitihani ya bodi sio migumu kinachotakiwa kwa wanafunzi kujiandaa vizuri ambapo wanaweza kufanya vizuri.

Amesema kuwa kwa wale wanaofanya kazi katika kipindi kilichobaki waweze kuomba ruhusa ya kwa ajili ya kujiandaa na mitihani hiyo na kuweza kupata cheti mahususi kwa ajili ya uhasibu (CPA).
Sympholian amesema kuwa mitihani hiyo wamekuwa mtihani wa bodi hiyo hauna upendeleo hivyo kila mtu atapata alichokipanda katika kujiandaa kwake na huo mtihani.

“Hatuna upendeleo kwani wanaosimamia sio ndio wanaosahihisha na kusahihisha huko hakuna majina ya wanafunzi kilichopo ni namba tu ambapo hawezi kupenya mwanafunzi wa kwa upendeleo”amesema Sympholian. 

Mhasibu na Mwalimu wa Chuo Kikuu Mzumbe Victirius Kamuntu amesema kuwa wanafunzi wake wamejiandaa na kuwa na imani kuwa mitihani ya bodi watatafanya vizuri.
Amesema kuwa Chuo Kikuu Mzumbe katika mitihani ya bodi hiyo kwa wanafunzi chuo hicho wamekuwa wakifanya vizuri hivyo kukutana na watu wa bodi kunawafanya kuongeza juhudi ya kufikia malengo.
 Afisa Mitihani wa Bodi ya Uhasibu (NBAA) Humphre Sympholian akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe kuhusiana na mitihani ya Bodi itayofanyika hivi karibuni alipokutana na wanafunzi hao katika Chuo hicho jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mitihani wa NBAA, Rebecca Siame akieleza sheria zinazotumika na Bodi ya NBAA katika usimamizi wa Mitihani na mwanafunzi atakayebainika kufanya udanganyifu matokeo yake kufutwa wakati alipokutana na wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam.

Baadhi ya wanafunzi wanaojiandaa na Mitihani ya Bodi ya Uhasibu Nchini(NBAA)

TPB YATOA MSAADA WA FIMBO NYEUPE KWA CHAMA CHA WASIOONA DAR

$
0
0
BENKI ya TPB, imetoa msaada wa fimbo nyeupe 20 kwa chama cha wasioona tawi la Dar es Salaam, zenye thamani ya sh milioni 1. Msaada huo ulitolewa jana na Meneja wa Mawasiano wa Benki ya TPB, Bi. Chichi Banda na kukabidhiwa Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Seif Jega. 

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bi Chichi Banda alisema benki hiyo ilitoa msaada huo kama sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake katika jamii. ‘’Katika uendeshaji wa benki yetu, huwa tuna utaratibu wa kutenga kiasi cha faida kila mwaka kwa ajili ya kusaidia jamii katika maeneo makuu matatu ambayo ni afya, elimu na ustawi wa jamii’’. Hivyo basi tunawaomba wananchi muendelee kutuunga mkono kwa kutumia huduma zetu za kibenki kwani tunachokipata kama faida, mara zote tumekuwa tukirudisha kwenu kupitia misaada tunayotoa’’, alisema Chichi. ‘’Tunaamini msaada huu, utaenda kupunguza changamoto kwa wale wasioona ambao walikosa kifaa hiki muhimu katika maisha yao’’, aliongeza Chichi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Seif Jega, aliushukuru uongozi wa benki ya TPB kwa msaada huo ambao utawasaidia katika maadhimisho ya SIKU YA FIMBO CHEUPE dunia utakaofanyika kitaifa mkoani Mwanza siku ya tarehe 25 Oktoba 2018. Katika maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajia kuwa Makamu wa Raisi, Mhe. Mama Samia Suluhu. ‘’Kwa kweli tumefarijika sana, kupokea huu msaada kutoka benki ya TPB, na tunaahidi tutaufikisha kwa wanachama wale ambao walikuwa hawajapata bado fimbo hizi’’, alisema Jega. 
Cheo: Meneja Mawasiliano
Jina: Chichi Banda
Namba: 0682 136414
Meneja Uhusiano wa Benki ya TPB, Bi. Chichi Banda (kulia) akikabidhi fimbo cheupe 20 zenye thamani ya sh milioni 1 kwa chama wa wasioona mkoa wa dar es salaam. Akipokea msaada huo ni Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Seif Jega (katikati) aliyeambatana na Mjumbe wa kamati ya utendaji wa chama hicho Bi Lucy Bupamba (kushoto). Fimbo hizo zitatumika katika maadhimisho ya siku ya fimbo nyeupe duniani, ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Mwanza oktoba 25. 
Meneja Uhusiano wa Benki ya TPB, Bi. Chichi Banda (kulia) akikabidhi vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh milioni 3.9 kwa Jeshi la Magereza Tanzania. Akipokea msaada huo ni Mrakibu Msadizi wa Magereza (Afisa Michezo Jeshi la Magereza) ASP Bakari Sudi (katikati), akishuhudia tukio hilo ni SGT Edwin Masinga ambaye ni kocha mkuu wa timu ya mpira wa volleyball Magereza. Vifaa hivyo vitatumika siku ya Michezo ya Wanajeshi Tanzania (BAMMATA) itakayofanyika mwanzoni mwa mwezi Novemba. 

NBS: Utafiti wa Huduma za Uzazi wa Mpango na Huduma za Uzazi Kufanyika hivi Karibuni

$
0
0
UTAFITI wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango pamoja na dawa zinazohusiana na huduma za uzazi nchini utanarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba waka huu.

Akifungua mafunzo ya siku kumi na moja kwa wadadisi wa utafiti huo, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dk. Albina Chuwa amesema taarifa zitakazokusanywa kwenye utafiti huo ni pamoja na upatikanaji wa njia za uzazi wa mpango katika ngazi mbalimbali za vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu huyo, utafiti huo utakusanya taarifa zinazohusu mfumo wa ugavi wa dawa au vifaa vinavyohusiana na njia za uzazi wa mpango pamoja na huduma za uzazi na uwepo wa watumishi waliosomea utoaji wa huduma hizo.

Utafiti huo ambao ni mara ya tatu kufanyika nchini kuanzia mwaka 2015 utaangalia pia uwepo wa miongozo mbalimbali kutoka wizara za afya inayoongoza huduma hizo na pia utakusanya maoni ya wateja waliofika kwenye kituo husika kwa ajili ya huduma za uzazi wa mpango.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya akizungumza leo mkoani Morogoro kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dkt. Albina Chuwa wakati wa ufunguzi wa Semina ya mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango.
Baadhi ya wadadisi wa utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango ambao ni wauguzi na madaktari kutoka katika Hospitali na Zahanati mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea mkoani Morogoro.
Baadhi ya wadadisi wa utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango ambao ni wauguzi na madaktari kutoka katika Hospitali na Zahanati mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea mkoani Morogoro. 


IGP SIRRO AKUTANA NA MKURUGENZI TAKUKURU

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Diwani Athuman wakizungumza na Maofisa Wakuu wa Polisi waliopo Makao Makuu ya Polisi wakati wa kikao cha kuweka mikakati ya kuzuia na kupambana na rushwa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Diwani Athuman (kushoto) wakati Mkurugenzi huyo na ujumbe wake walipotembelea Makao Makao Makuu ya Polisi na kufanya kikao na Maofisa Wakuu wa Polisi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuzuia na kupambana na rushwa. Wengine ni Naibu Mkurugenzi Mkuu Brigedia Jenerali John Mbungo na Kamishna wa Utawala na Raslimali watu Albert Nyamhanga. (Picha na Jeshi la Polisi).
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Diwani Athuman wakiwa katika picha ya pamoja na Maofisa na Viongozi wengine baada ya kumaliza kikao kwa lengo la kuongeza kasi katika kuzuia na kupambana na rushwa. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Diwani Athuman baada ya kumaliza kikao na Maofisa Wakuu wa Polisi Makao Makuu ya Polisi kwa lengo la kuongeza kasi katika kuzuia na kupambana na rushwa. (Picha na Jeshi la Polisi)

AFREXIMBANK KUIPATIA TANZANIA ZAIDI YA SH. TRILIONI MOJA KUGHARAMIA UJENZI WA RELI NA VITUO VYA BIASHARA

$
0
0
Na: WFM,  Mjini Bali Indonesia
African Export Import Bank (Afreximbank) ya Misri, imeonyesha nia ya kuipatia Tanzania mkopo wa zaidi ya Shilingi trilioni moja (dola za Marekani zaidi ya milioni 500) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kipaumbele hasa ya miundombinu ya reli na kujenga vituo vya biashara (SEZ and Industrial parks).
Hayo yalibainishwa mjini Bali Indonesia, na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango baada ya Mkutano na Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel,  uliofanyika  wakati wa mikutano ya mwaka  ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ikiendelea.
Waziri Mpango, alisema kuwa Afreximbank imethibitisha kuwa ipo tayari kutoa mkopo wa  dola za Marekani milioni 125  (takribani Shilingi bilioni 285.9) kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Kimataifa  (SGR),  kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Dodoma.
“Afreximbank wanania pia ya kutoa  dola milioni 400 (takribani Sh. Bilioni 914.9) ambazo wanaweza kutukopesha kwa ajili ya kugharamia miradi ya miundombinu itakayorahisisha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani na Bara la Afrika kwa ujumla,  ili kuchochea kasi ya ukuaji wa biashara katika nchi hizo kwa lengo la kuondoa umasikini”, aliongeza Dkt. Mpango.
Alisema kuwa kwa kuwa tayari Tanzania ilikuwa na mkakati wa kufungua vituo vya biashara katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara na mikoa mingine, suala la mkopo huo ni fursa kubwa kwa  maendeleo ya nchi, hivyo jambo hilo litafanyiwa kazi kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji  na Sekta Binafsi, ili Taifa liweze kunufaika na fedha ambazo benki hiyo ipo tayari kuzitoa.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto), akizungumzia miradi ya miundombinu ikiwemo ya Reli ya Kisasa kwa kiwango cha kimataifa, katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi, wakati wa Mkutano na Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel, uliofanyika Bali Indonesia, kulia ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. John Rubuga.
Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. John Rubuga, na Afisa Mwandamizi wa Wizara hiyo Bw. Elias Shosi, wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel, alipokuwa akizungumzia maamuzi ya benki yake kuikopesha Tanzania zaidi ya Shilingi trilioni moja wakati wa mkutano uliofanyika Bali, Indonesia.
Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. John Rubuga, na Afisa Mwandamizi wa Wizara hiyo Bw. Elias Shosi, wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel, alipokuwa akizungumzia maamuzi ya benki yake kuikopesha Tanzania zaidi ya Shilingi trilioni moja wakati wa mkutano uliofanyika Bali, Indonesia.
Meneja wa Afreximbank Kanda ya Afrika Mashariki Bw. Kudakwashe Matereke, akieleza jambo wakati wa Mkutano kati ya Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hawapo pichani), mjini Bali Indonesia wakati wa mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa – IMF.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) na Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel, wakipeana mkono baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao uliofanyika mjini Bali Indonesia wakati wa mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa – IMF.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)

TAZAMA LIVE KUHAMA KWA NYUMBU

Viewing all 110150 articles
Browse latest View live




Latest Images