Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109935 articles
Browse latest View live

Letshego Bank express commitment in improving services aiming at reaching SMEs

$
0
0
Dar-es-Salaam, Tanzania – Wednesday, 10 October 2018:

Letshego Bank Tanzania has expressed its commitment to serve Tanzanians especially, financially underserved micro and small entrepreneurs with simple and accessible financial solutions.

The Bank’s newly appointed Chief Executive Officer Mr Thabit Ndilahomba said in Dar es Salaam yesterday that extending Letshego’s reach and enhancing the bank’s value proposition for customers, staff and other stakeholders is one of his priorities. “In line with Letshego Group’s regional strategy, Letshego Tanzania offers simple and accessible financial solutions that focus on the needs of individuals, as well as micro and small entrepreneurs,” he said.

Thabit Ndilahomba, CEO Letshego Bank Tanzania added, “I am excited about the opportunities that my new role presents in delivering a strategy that not only enhances Letshego’s brand and reputation in Tanzania, but also stands to bring further value and benefits to one of our most important stakeholders, our customers,”

“By increasing access to appropriate financial solutions and encouraging our customers to use their funds for productive purposes, Letshego aims to support the growth of economically active members in the local economy,” Formerly, the Chief Financial Officer FINCA, Mr Thabit plans to bring to his new role a valuable understanding and appreciation for the financial dynamics and performance of the business as a whole.

On his part, Letshego’s Group CEO, Smit Crouse said Mr Thabit’s local experience gained from multiple growth sectors in Tanzania, as well as his financial skills and background position him well in delivering Letshego’s strategic ambition for Tanzania. “Letshego remains committed to Tanzania while progressing in its ambition towards providing solutions that create opportunity and flexibility for both individuals and small businesses, across Tanzania,” he said.


Letshego Bank Tanzania CEO Thabit Ndilahomba gestures as he makes presentation during launch of TIMIZA AKIBA (Past event). The recently appointed CEO is committed to extending Letshego’s reach and enhancing their value proposition for customers, staff and other valued stakeholders in Tanzania which is in line with Letshego Group’s regional strategy. (Photo by our Correspondent).

FOR MORE NEWS CLICK HERE

MKURUGENZI MKUU NIDA ANZA KWA KUKAGUA SHUGHULI ZA USAJILI KWENYE OFISI ZA WILAYA; NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) Dkt. Anold Mathias Kihaule, ameenza kazi kwa kukagua utendaji wa ofisi za Usajili za Mkoa wa Dar-es-salaam ambapo pamoja na mambo mengine amezungumza na wananchi na kutembelea ofisi ya Serikali ya Mtaa ambako huduma ya utoaji wa fomu na ugawaji wa Vitambulisho zinaendelea.

Katika ziara hiyo Dkt. Kihaule aliyekuwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa Mamlaka hiyo; amepongeza kazi nzuri inayofanywa na wafanyakazi wa NIDA na kusisitiza watumishi kuzingatia utoaji wa huduma unaozingatia viwango ili kuweza kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima kwa wananchi.

Aidha amewashukuru viongozi na Watendaji katika Serikali za Mitaa kwa kazi nzuri ya kuwahudumia wananchi kuhakikisha wanapata Vitambulisho vya Taifa na kuahidi kuendelea kuwapa ushirikiano katika kuhakikisha malengo ya Serikali yanafikiwa.

Dkt. Anold Mathias Kihaule aliteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndg. Andrew W. Massawe aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Ajira na Walemavu.

Pichani ni mmoja wa wakazi wa Kinondoni akimuelezea Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulish vya Taifa(NIDA), Dkt. Anold Mathias Khaule (wa pili kushoto) namna alivyopatiwa huduma katika ofisi ya Usajili Wilaya ya Kinondoni
Mkurugenzi Mkuu wa NIDA akikagua fomu ya mmoja wa wananchi waliojitokeza kusajiliwa. Kutoka kulia ni Bw Dickson Mbanga Afisa Usajili wilaya ya Kinondoni na katikati ni Bw. Alphonce Malibiche, Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho vya Taifa.
Mkurugenzi Mkuu NIDA akikagua sehemu ya kutunzia Vitambulisho vya Taifa katika ofisi ya Usajili wilaya ya Kinondoni. Kuli ni Afisa Usajili wilaya ya Kinondoni na wa kwanza kushoto ni Bw. Melkiory Ndofi Mkurugenzi wa Idara ya Fedha na Utawala.
Mkazi wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Gift Emmanuel Nkya (aliyevaa nguo nyeusi) mwanafunzi wa mwaka wa kwanza chuo cha Biashara CBE, akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA alipotembelea kituo cha Usajili Kawe jijini Dar-es-salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Dkt. Anold Mathias Kihaule akiweka saini katika kitabu cha wageni ofisi ya Usajili wilaya ya Kinondoni wakati alipofanya ziara kukagua namna shughuli za Usajili zinavyofanyika kituoni hapo
Mkurugenzi Mkuu wa NIDA (aliyevaa koti) akiingia kwenye ofisi ya Serikali Mtaa wa Mzimuni wakati wa ziara yake kukagua uendeshaji shughuli za Usajili Wilaya ya Kinondoni. Hapa alishuhudia utaratibu wa ugawaji fomu za Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi na utaratibu wa kugawa Vitambulisho vya Taifa kupitia ofisi za Watendaji.


HABARI - AZAM TV 09/10/2018

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

VOA SWAHILI: Duniani Leo October 9, 2018

ITV: TAARIFA YA HABARI YA SAA TANO USIKU.. 09 OKTOBA 2018

NEWS ALERT: RAIA WA SYRIA,SUDAN KUSINI WAKAMATWA JNIA WAKISAFIRISHA MAMILIONI YA FEDHA

$
0
0
ABIRIA wawili Raia wa Sudan Kusini na Syria leo wamekamatwa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wakisafirisha fedha taslim dola elfu 70 za Kimarekani sawa na shilingi milioni 156 za Kitanzania na paundi 3410 za Sudan bila kufuata taratibu.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria la JNIA, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi, Barnabas Mwakalukwa alimtaja Raia wa Sudan Kusini Bi. Nada Zaelnoon Ahamed (38) mwenye hati ya kusafiria namba P01563534 amekamatwa saa 10:00 jioni akiwa eneo la ukaguzi wakati akiingia ndani tayari kusafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ 485) akielekea Nairobi.

Hata hivyo, Afande Mwakalukwa amesema abiria huyo mbali na fedha hizo za Kimarekani pia amekamatwa na paundi za Sudan 3410, ambazo zote kwa pamoja alishindwa kutoa taarifa ya fedha alizokutwa nazo kwa mujibu wa sheria ya utakatishaji fedha ya mwaka 2006 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.

Pia alimtaja Bw. Mohamed Belal (31), Raia wa Syria mwenye hati ya kusafiria namba 003-16L096876 aliyekuwa akisafiri kwa ndege ya Shirika la ndege la Ethiopia (ET 864) kuelekea Syria kupitia Addis Ababa amekamatwa na dola za kimarekani 10,000 sawa na Tsh. milioni 20 za Kitanzania, ambazo naye alishindwa kuzitolea taarifa. “Watuhumiwa wote wawili wamezuiwa na hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya uchunguzi zaidi na hatua za kisheria zilizopo,” amesema Afande Mwakalukwa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela amewapongeza maafisa usalama wa JNIA kwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha wasafiri, wadau na maeneo yote ya viwanja vya ndege yanabaki salama na vitendo vya kiuhalifu havina nafasi katika viwanja hivyo. Bw. Mayongela amesema pamoja na watumishi hao kufanya kazi katika wakati mgumu kutokana na baadhi ya abiria kuwa watata kila wanapotaka kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kanuni.


Kamishna Msaidizi na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa akinyanyua juu moja ya bunda la Dola za Kimarekani zilizokamatwa leo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), zikisafirisha isivyo halali na raia wa Sudan Kusini Bi. Nada Zaelnoon Ahamed na Bw. Mohamed Belal, raia wa Syria. 
Jumla ya Dola za Kimarekani 70,000 sawa na Tsh. milioni 156 za Kitanzania zikiwa zimekamatwa leo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), zikisafirishwa na Raia wawili wa Syria Bw. Mohamed Belal na Bi. Nada Zaelnoo Ahamed raia wa Sudan Kusini kwa kutofuata taratibu. 
Bi.Nada Zaelnoon Ahamed (38) Raia wa Sudan Kusini (katikati mwenye ushungi) akiwa mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), baada ya kukamatwa na dola 60,000 za Kimarekani na Paundi 3410 za Sudan. 

Raia wa Syria, Bw. Mohamed Belal (31) mwenye fulana nyeupe akiwa mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), baada ya kukamatwa na dola 10,000 za Kimarekani, ambazo hakuzitolea taarifa kwa Maafisa wa Forodha wa kiwanjani hapo. 
Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha (kushoto) akimsikiliza Kamishna Msaidizi wa Polisi, Barnabas Mwakalukwa (aliyesimama) alipokuwa akitoa maelezo kwa waandishi wa habari leo ya kukamatwa kwa Raia wawili wa Sudan Kusini na Syria waliokuwa wakisafirikisha fedha taslim milioni 156 bila kufuata sharia. 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wa pili kulia) akisisitiza jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jengo la Pili la abiria la Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wakati walipokamatwa Raia wawili wa Syria na Sudan Kusini wakisafirisha mamilioni ya fedha bila kufuata taratibu.

Kusoma zaidi BOFYA HAPA

MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA KAHAWA CHA AMIMZA MJINI BUKOBA

$
0
0


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu usindikaji wa kahawa yenye viwango vya juu kutoka kwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha kahawa cha AMIMZA kilichopo Bukoba, Bw. Amiri Hamza (wapili kushoto) wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 9, 2018. Watatu kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage na wapili kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha kisasa cha kusindika kahawa cha AMIMZA cha mjini Bukoba Oktoba 9, 2018. Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa kiwanda, Amiri Hamza na kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage. Wapili kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa . Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa nchi zote 16 za SADC

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu wamesaini mkataba wa makubaliano ya MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). 

Hatua hii inafuatia uteuzi wa serikali ya Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) ulifanywa wakati wa mkutano wa SADC wa mawaziri wa Afya wa nchi wanachama, uliofanyika mwezi Novemba, 2017 nchini Afrika Kusini. 
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bw. Laurean Bwanakunu amesema tangu wakati huo hadi sasa wamekuwa wakishirikiana na na Sekretarieti ya (SADC) kuandaa rasimu ya mpango wa utekelezaji wa manunuzi ya pamoja yaani SADC Pooled Procurement Services (SPPS). 

 Amesema kulingana na mpango huo, uratibu wa manunuzi unaanza rasmi tarehe leo, tarehe 9/10/2018, kupitia mkataba wa makubaliano yaani Memorandum of Understanding (MoU) kati ya MSD na Sekretarieti ya SADC. 
 Bwanakunu ameongeza kuwa MSD itakuwa na majukumu ya kupokea mahitaji ya manunuzi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kutoka kwa nchi hizo 16 za Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kununua dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara, kusimamia takwimu na taarifa za dawa pamoja na kusimamia Kanzidata (Database) ya dawa za nchi hizo. 

 Ameongeza kuwa MSD itasimamia bei elekezi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara, kusimamia mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao kwa nchi zote wanachama, kutoa huduma za kitaalam na kupanga bei elekezi. MSD pia itaanzisha kitengo maalumu ndani ya kurugenzi ya manunuzi kwa ajili ya kazi hii ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba ba vitendanishi vya maabara kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya SADC tu. 

 Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax ameeleza kuwa Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa nchi za Ukanda wa SADC ni heshima kubwa kwa Taifa, kuaminiwa kwa huduma bora, uwezo na kukidhi vigezo vya kitaalamu katika mnyororo wa ugavi. 

 Makubaliano hayo yameshuhudiwa na Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye amesema kwamba SADC imeipa Tanzania heshima kubwa na kuichagiza MSD kuhakikisha inatekeleza majukumu yake vizuri ili isionekane kuwa SADC ilifanya makosa kuichagua Tanzania.
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu wakisaini mkataba wa makubaliano ya MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) makao makuu ya MSD jijini Dar es salaam Oktoba 9, 2018
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu wakibadilishana nyaraka baada ya kusaini  mkataba wa makubaliano ya MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) makao makuu ya MSD jijini Dar es salaam Oktoba 9, 2018 
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu wakionesha nyaraka za mkataba wa makubaliano ya MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) makao makuu ya MSD jijini Dar es salaam Oktoba 9, 2018
Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akipeana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu baada ya hafla hiyo fupi makao makuu ya MSD jijini Dar es salaam Oktoba 9, 2018

BENKI YA DUNIA YAAHIDI KUTOA FEDHA KUKUZA MATUMIZI YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA TANZANIA

$
0
0
Benki ya Dunia imeahidi kuwekeza zaidi nchini Tanzania katika Sayansi na  Teknolojia ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi  kwa lengo la kuisaidia Tanzania kukuza uchumi wa viwanda na kuondoa umasikini  kwa wananchi wa wake.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, alipofanya mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Bw. Hafez Ghanem, katika mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Mjini Bali Indonesia.                     
Dkt. Mpango amesema kuwa Benki ya Dunia imeamua kuwekeza katika teknolojia kwa kuwa ni eneo sahihi linaloweza kukuza uchumi wa Taifa kwa zaidi ya mara mbili kutokana na tafiti zilizofanywa na Benki ya Dunia.
“Kimsingi Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia amefurahia ajenda za maendeleo za Tanzania kuhusu kujenga uwezo wa rasilimali watu katika kukuza uchumi wa viwanda na ameahidi kuanza kwa kuwekeza zaidi kwa watoto wenye umri mdogo ili mipango ya maendeleo ya nchi iwe endelevu”, alieleza Dkt. Mpango.
Aidha Waziri Mpango alimueleza Makamu wa Rais wa Benki hiyo kuwa Tanzania imeweka  mikakati  mbalimbali ya kujenga uchumi wa viwanda utakaotumia malighafi za ndani ili kuongeza ajira kwa wananchi walio wengi.
Kuhusu umuhimu wa Sekta Binafsi katika maendeleo ya nchi Waziri Mpango alisema Makamu wa Rais Bw. Ghanem, ameahidi kuwekeza zaidi katika miradi ya pamoja kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), kwa kuiwezesha Serikali ya Tanzania na wadau wengine kwenda kupata mafunzo yatakayoongeza ujuzi wa utekelezaji wa miradi hiyo katika nchi zilizofanya vizuri katika eneo hilo ili kuongeza ufanisi wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.
Kwa upande wake Kamishna na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere, amesema kuwa mfumo wa dunia ya sasa unazitaka nchi kujitegemea kimapato hivyo TRA itaendelea kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa  kuwa Benki ya Dunia imeahidi kuboresha miundomibnu ya ukusanyaji mapato kwa nchi ya Tanzania.
Waziri Mpango ameiomba Benki ya Dunia iendelee kuisaidia Tanzania kwa kutoa rasilimali fedha katika kuwezesha miundombinu ya kukuza uchumi ikiwemo ya miradi ya nishati ya umeme, ujenzi wa reli kwa kiwango cha Kimataifa (SGR), na miradi ya maji.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia ameahidi kutembelea Tanzania mwanzoni mwa mwaka ujao ikiwa ni juhudi za kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo kati ya benki hiyo na Tanzania.
Mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), inaendelea mjini Bali Indonesia ambapo imewakutanisha wadau wa masuala ya fedha wakiwemo Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu kutoka nchi mbalimbali Dunia kujadili Sera na misaada inayotolewa na Taasisisi hizo.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango wa  Zanzibar Dkt. Khalid Salum Mohamed, muda mfupi kabla ya Mkutano na Makamu wa Rais wa  Benki ya Dunia (WB) Bw. Hafez Ghanem, katika mkutano wa mwaka wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na WB,  Mjini Bali, Indonesia.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na ujumbe wake  na Makamu wa Rais wa  Benki ya Dunia (WB) Bw. Hafez Ghanem na ujumbe wake katika mkutano wa mwaka wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na WB mjini Bali, Indonesia.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)  (wa pili kushoto) akielezea miradi ya maendeleo ambayo inahitaji fedha ili iweze kuchochea uchumi ikiwemo miradi ya Nishati ya Umeme na ujenzi wa miundombinu ya Reli ya Kisasa kwa kiwango cha Kimataifa – SGR alipofanya Mkutano na Makamu wa Rais wa  Benki ya Dunia (WB) Bw. Hafez Ghanem, katika mkutano wa mwaka wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na WB Mjini Bali Indonesia.
 Makamu wa Rais wa  Benki ya Dunia (WB) Bw. Hafez Ghanem (katikati) akieleza nia ya Benki yake ya kuwekeza kwenye mafunzo ya Miradi ya pamoja kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma Mjini Bali Indonesia alipofanya Mkutano na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)  (hayupo pichani).
Waziri wa Fedha na Mipango wa  Zanzibar Dkt. Khalid Salum Mohamed(kulia) akizelezea miradi ya kukuza utalii  ambayo inahitaji fedha ili kuweza kuchochea maendeleo wakati wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)  na Makamu wa Rais wa  Benki ya Dunia (WB) Bw. Hafez Ghanem, katika mkutano wa mwaka wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na WB, Mjini Bali Indonesia

SERIKALI YAZINDUA MFUMO WA UBORESHAJI UPATIKANAJI DAWA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SERIKALI imezindua mfumo wa kitaifa wa uboreshaji upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kupitia mshitiri(Mzabuni binafsi).

Mfumo huo maarufu kwa jina la Jazia unalenga kuongeza ufanisi wa upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vinavyokosekena Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ili kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya katika vituo vya tiba.

Mfumo huo umezinduliwa rasmi leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Ofisi ya Rais(TAMISEMI) Suleiman Jaffo ambapo amesema unakwenda kusaidia kuondoa changamoto ya kukosekana kwa dawa na vifaa tiba katika vituo vya tiba.

"Mfumo huu wa uboreshaji upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kupitia mshitiri kutaongeza kasi ya upatikanaji dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ili kupunguza muda wa kusubiri huduma na kupatikana kwa bidhaa za afya wakati wote,"amesema Jaffo.

Ameongeza mfumo huo ambao umezinduliwa rasmi leo utakuwa ni wa nchi nzima na kutoa maagizo kwa mikoa yote nchini kujiunga na mfumo huo na ifikapo Oktoba 30 mwaka huu na tayari unatumika nchini kote.Amesema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi madhubuti wa Rais Dk.John Magufuli moja ya vipaumbele vyake ni kuboresha sekta ya afya nchini kwa kuondoa changamoto zilizipo.

"Hivyo mfumo huu unakwenda kumaliza tatizo la kukosekana kwa dawa katika vituo vya tiba,"amesisitiza.Amesema anatambua na kuthamini kazi nzuri ya MSD katika kusambaza dawa na vifaa tiba lakini mfumo huo utasaidia pale ambapo MSD wameshindwa kufikisha dawa au vitaa tiba hivyo.Ametoa maagizo kwa halmashauri zote nchini kuanzia sasa baada ya mfumo huo kuzinduliwa rasmi upatikanaji wa dawa katika vituo vya tiba uwe asilimia 98 na kuwataka wakurugenzi wa halmashauri kushiriki kikamilifu.

Amesisitiza ni matumaini yake mfumo huo umekuja kumaliza tatizo la kukosekana kwa dawa na kama tatizo basi limepata tiba yake.Kikubwa ni kuhakikisha mfumo unasimamiwa vema kwa maslahi ya Watanzania wote.Ametumia nafasi hiyo kuzungumzia mikakati ya Serikali ya Awamu ya tano katika kuboresha sekta ya afya ikiwemo ya ujenzi wa hospitali za Wilaya na ujenzi wa vituo vya afya na lengo ni kuu ni kuboresha sekta ya afya nchini.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI),Selemani Jafo akizungumza  na wadau mbalimbali wa afya katika  hafla ya uzinduzi wa mfumo wa mshitiri Kitaifa leo jiji Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI),Selemani Jafo akizindua mfumo wa kitaifa wa uboreshaji upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kupitia mshitiri (Mzabuni binafsi) jana jijini Dar es Salaam.(kushoto) Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda.(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii).
 Sehemu ya wadau wa afya wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa Mshitiri Kitaifa jana jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja.

Taarifa ya kusikitisha iliyotufikia hivi punde,Kafariki dunia kwa sababu hizi hapa

RELI YA KISASA ITASAIDIA SHUGHULI ZA KIJESHI - CDF MABEYO

WAFANYABIASHARA MKOANI SONGWE WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPATIWA HUDUMA YA NAMBA YA UTAMBULISHO YA MLIPAKODI INAYOAMBATANA NA ELIMU YA KODI

$
0
0

Na. Benedict Liwenga-TRA. 

WAFANYABIASHARA Mkoani Songwe wametakiwa kujitokeza kwa katika Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). 

Kauli hiyo imetolewa leo na Afisa Kiongozi wa Kituo cha Huduma cha TRA mjini Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Walipakodi mkoani hapo ambapo amewataka Wafanyabiashara kujitokeza kwa wingi kuweza kupatiwa huduma hiyo pasipo gharama yoyote. 

Bwana Mwita ameeleza kuwa, mwitikio wa wafanyabiashara katika kampeni hiyo ni mkubwa, ambapo wengi wa Wafanyabiashara ambao walikuwa hawana Namba ya Utambulisho ya Mlipakodi (TIN) wameshasajiliwa na kupatiwa TIN hizo. 

“Zoezi hili ni zuri na mwitikio wa watu ni mkubwa, niwaombe Wafanyabiashara waendelee kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupatiwa TIN na elimu kuhusu masuala ya kodi”, alisema Mwita. 

Kwa upande wake Kiongozi wa msafara kutoka TRA Makao Makuu ambaye pia ni Afisa Mkuu Mwandamizi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Bi. Rose Mahendeka amesema kwamba, zoezi la usajili na utoaji elimu kwa mlipakodi litadumu mkoani Songwe kwa muda siku sita, ambapo wafanyabiashara wanahimizwa kuchangamkia fursa hiyo ili waweze kutatua kero mbalimbali zinazowakabili. 

“Kampeni hii katika Mkoa huu wa Songwe litadumu kwa muda wa siku sita na tayari tumeshaanza na maeneo mbalimbali kama vile Vwawa, Mlowo, Tunduma na baadaye tunaendelea na maeneo ya Mkwajuni, Ileje pamoja na Saza lengo ni kuwahamasisha wananchi hususan wafanyabiashara kuitikia wito wa kampeni hii”, alisea Mahendeka. 
 Afisa Mkuu Mwandamizi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bi. Rose Mahendeka (kushoto) akiwaeleimisha baadhi ya Wafanyabiashara wa Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendelea Mkoani Songwe. 
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) (kushoto) wakiwasajili na kuwapatia elimu ya kodi Wafanyabiashara wa Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendelea Mkoani Songwe.(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-TRA).

WAZIRI ASITISHA ZIARA AKISUBIRI KISIMA KITOE MAJI

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Arusha

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof.Makame Mbarawa amelazimika kusitisha ziara kwa masaa mawili na nusu akisubiri kisima katika kijiji cha Levolosi Kata ya Kimnyaki Wilayani Arumeru kinachochimbwa kitoe maji kabla ya kwenda kusaini mkataba.

Aidha Prof. Makame Mbarawa amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kumrudisha Wizarani mara moja Mhandisi wa Miamba Amir Msangi kwa uzembe wa kutoonekana kwenye eneo la mradi.

Waziri alitoa agizo hilo jana wakati alipotembelea Kijiji cha Levolosi, Kata ya Kimnyaki kujionea zoezi la uchimbaji wa visima vitatu na baada ya hapo alitia saini ya mkataba wa ujenzi wa mtandao mpya wa maji,mitambo ya kutibu maji safi ujenzi wa ofisi kuu ya AUWSA na ujenzi wa ofisi kuu ya AUWSA Kanda ya Kati wenye thamani ya Sh.bilioni 520.

Prof.Mbarawa alisema serikali imeamua kuleta wataalam wake toka Wizarani ili wasimamie na kujifunza Teknolojia mpya ya uchimbaji visima vikubwa kwa ajili ya kuweza kufundiaha wenzao utaalam huo hapo baadaye.

"Lakini cha kushangaza nimepata taarifa huyu Amir Msangi haonekani eneo la kazi na hivyo namwagiza mtaalam mwenzake Fatuma Mambo kumtaarifu Katibu Mkuu ili arudishwe Wizarani huyu na hapa aletwe mwingine atakayepata ujuzi huu,"alisema.Amesisitiza kuwa lengo kubwa la serikali ni kuwaleta wataalam hao ili kuhakikisha miradi ya maji inayotekelezwa inakuwa na ubora uliokusudiwa.

Alisema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia wananchi kupata maji kwa asilimia 95 ifikapo mwaka 2020.Aidha alisema miradi hiyo inatekelezwa na AUWSA kwa ufadhili wa serikali kupitia mkopo wa masharti nafuu toka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Mhe Mbarawa akiongozwa na wataalamu wa kampuni ya Sinohydro Corporation Ltd kuangalia mwamba unaotoa maji ardhini kwa kutumia camera maalumu. Picha na Vero Ignatus. 
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Mbarawa akikagua urefu wa kisima katika kijiji cha Levolosi kata ya Kimnyaki akiwa ameambatana na wahandisi toka wizara ya maji na mamlaka ya maji safi na usafishaji jijinla Arusha AUWSA. Picha na Vero Ignatus


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

TAARIFA YA HABARI ZA SAA KUTOKA ITV

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 10,2018

MAJALIWA ATEMBELEA KITUO CHA UTAFITI WA MAZO CHA MARUKU MKOANI KAGERA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Dkt. Nyabisi Malyatabu ambaye ni Meneja wa Kanda wa Taasisi ya Utafitiwa Kahawa Tanzania (TACRI), Maruku mkoani Kagera  kuhusu kilimo bora cha kahawa wakati  alipotembelea  Taasisi hiyo, Oktoba 9, 2018. Watatu kushoto ni Naibu Waziri wa kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mhogo aina ya tegemeo unaostawi vizuri katika maeneo ya Kanda ya Ziwa  wakati alipotembelea Kituo cha Utafiti cha Maruku mkoani Kagera, Oktoba 9, 2018. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt, Mary Mwanjelwa na kushoto ni Mkuu wa Kituo, Innocent Ngyetabwa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama vyakula mbalimbali vilivyotengenezwa kwa kutumia unga wa mhogo, ndizi na nafanka nyingine wakati alipotembelea kituo cha Utafiti  cha Maruku mkoani Kagera, Oktoba 9, 2018. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt, Mary Mwanjelwa na kulia kwa Waziri Mkuu ni Mkuu wa Chuo cha  Kilimo - MATI- Maruku, Laurent Luhembe. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama uzalishaji wa miche ya Kahawa bora kwa kutumia majani ya kahawa wakati alipotembelea Kituo cha Utafiti wa Kahawa Tanzania (TACRI)  cha Maruku mkoani Kagera, Oktoba 9, 2018.  Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa na kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera,  Brigedia Jenerali, Marco Elisha Gaguti na wapili kushoto ni Afisa Ugani wa TACRI, Aretas Urassa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RC NDIKILO AKABIDHIWA MIFUKO YA SARUJI 960 KWA AJILI YA KUKARABATI UWANJA WA CCM PICHANDEGE

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
MKUU wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo amekabidhiwa mifuko ya saruji 960 kutoka kwa wadau wa maendeleo, kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa Chama Cha Mapinduzi (Sabasaba), Picha Ndege Kibaha ,ambao haujawahi kutumika tangu mwaka 1989.

Uwanja huo unatarajiwa kutumika kwenye maonyesho ya bidhaa mbalimbali  zinazozalishwa katika viwanda mkoani hapo kuanzia octoba 29-Novemba 4 mwaka huu.

Ndikilo alikabidhiwa saruji hiyo kutoka kampuni ya Mwanza Huduma Ltd ambao wametoa mifuko 660 na kampuni ya saruji Kisarawe Lucky Cement Company mifuko 300.

Aidha Ndikilo alielezea ,wameamua kuandaa maonyesho hayo ili kuvitangaza viwanda hivyo na bidhaa wanazozalisha ambapo mkoa unakadiriwa kuwa na viwanda 400.

"Misaada hii kwani itasaidia kufanikisha ukarabati wa uwanja wa maonyesho hayo yatakayoanza mwishoni mwa mwezi huu," alisema Ndikilo.

Alisema ,maonyesho hayo pia yatahamasisha uwekezaji wa viwanda kwenye mkoa na kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano.

"Tunaunga mkono jitihada za Rais Dk John Magufuli za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda vitakavyopelekea kuwa nchi yenye uchumi wa kati," alisema Ndikilo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Kisarawe Lucky Cement Company Samir Jaffar alisema , wamejitolea Saruji hiyo yenye thamani ya sh.milioni nne kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za mkoa katika suala la uwekezaji wa viwanda.

Jaffar alisema , wao kama wenye viwanda wanampongeza Rais kwa kuweka nguvu kwenye suala la viwanda kwani ndiyo njia pekee ya kuinua uchumi na kufungua milango ya ajira.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo akipokea mifuko ya saruji 960 kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Kisarawe Lucky Cement Company Samir Jaffar  kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa Chama Cha Mapinduzi (Sabasaba), Picha Ndege Kibaha ,ambao haujawahi kutumika tangu mwaka 1989.

TESEA KUNUFAISHA WANAFUNZI, WALIMU NCHINI ILI KULETA CHACHU YA ELIMU BORA

$
0
0
Na Khadija Seif Globu ya Jamii

MTANDAO wenye vifaa saidizi vya elimu umezinduliwa rasmi jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wadau wa elimu ,walimu na waandishi wa habari nchini.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mwanzilishi wa Taasi isiyo ya kiserikali yenye mtandao wa kielimu nchini  (TESEA )Abdul Mambokileo amefafanua lengo la kuanzishwa kwa mtandao huo  unawataka wadau pamoja na walimu kuutumia kikamilifu kupata kuelewa baadhi ya mambo yanayohusu elimu ikiwemo maswali yatakua waongoza kuwafundisha wanafunzi na kufaulu .

Hata hivyo amesema  kumekuwepo na changamoto nyingi katika sekta ya elimu ukiachilia mbali suala la majengo,madawati pamoja na chakula zipo changamoto  ambazo kusababisha wanafunzi pamoja na walimu kukosa nyenzo za kujifunzia.

Mambokileo amefafanua aliiona fursa hiyo  na kuanzisha huduma ili kuipa kipaumbele elimu kwani msingi wa maisha mazuri ni pamoja kuwa na elimu ambayo itakuwezesha kupanga na kuendesha biashara,maisha huku ukiwa na ujuzi ambao unasaidiwa na elimu hata kama ni ya shule ya msingi .

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Taifa wa Shule binafsi Charle Ela  amepongeza juhudi hizo zinazofanywa na TESEA ambazo ipo kwa ajili ya kufanya mapinduzi ya kielimu na kusaidia Serikali kupunguza fedha kwenye kuwekeza katika sekta ya elimu.

Aidha,Totela amewapa ushauri walimu kuangalia upya swala la mafunzo ya vitendo ili kuboresha elimu bora kwani wanafunzi wengi wamekua wakijifunza zaidi kwa nadharia na kupeleka kudumaza akili zao.

Hivyo basi mtandao huo utawawezesha kujifunza zaidi kwani kuna silabasi ambazo zimewekwa pamoja na maswali mbalimbali na kuwataka wadau wengine kuleta mabadiliko na mapinduzi katika kuboresha elimu bora nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasi hiyo ya  elimu isiyo ya kiserikali (TESEA) amepongeza wadau,walimu kufanikisha kuzinduliwa kwa mtandao huo na kuomba waingie na kupakua kwa kuandika WWW.TESEA.COM .
Viewing all 109935 articles
Browse latest View live




Latest Images