Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110104 articles
Browse latest View live

DKT SHEIN AZINDUA MFUMO WA KUIMARISHA USALAMA KATIKA MJI WA ZANZIBAR WAFANYIKA

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein akibonyeza kitufe kuashiria Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein akitoa hatuba ya Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. 
Makamanda pamoja na Wananchi mbalimbali waliohudhuria katika Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ Haji Omar Kheir akitoa hotuba ya makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein katikati akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali katika Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein kushoto akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt,Abdalla Juma Sadalla(MABODI)Mara baada ya kuasili katika Uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa kuimarisha usalama katika mji wa Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa Idrisa Abdull Wakil Kikwajuni mjini Zanzibar. PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

WAWILI WATIWA NGUVUNI WAKICHIMBA MCHANGA NDANI YA ENEO LA MRADI WA SGR NA KUMKWAMISHA MKANDARASI.

TCRA YAKUTANA NA VIONGOZI SHINYANGA..YAWATAKA WAMILIKI WA VING'AMUZI NA VISIMBUZI KUHESHIMU SHERIA

$
0
0

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesisitiza juu ya umuhimu wamiliki wa ving'amuzi na visimbuzi vinavyorusha matangazo yake hapa nchini kuheshimu sheria na kuhakikisha wana leseni zinazowaruhusu kuonesha chaneli za ndani bure badala ya kuwatoza wananchi fedha yoyote.

Hali hiyo imebainishwa leo Oktoba 3,2018 mjini Shinyanga kwenye semina ya siku moja iliyoendeshwa na Mamlaka hiyo kwa viongozi mbalimbali wa serikali, mashirika ya umma na asasi za kiraia mkoani Shinyanga.

Semina hiyo ililenga kuwapa uelewa viongozi hao juu ya sababu za TCRA kufungia baadhi ya ving’amuzi kurusha chaneli za ndani baada ya kubaini vimekiuka masharti ya leseni zao ambapo hata hivyo lengo ni kumwokoa mtumiaji wa ving’amuzi na visimbuzi kutotozwa gharama kubwa.

Mtoa mada katika semina hiyo, Mhandisi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Francis Mihayo alisema lengo la mamlaka hiyo ni zuri ambalo limezingatia sheria za mawasiliano nchini.Mihayo alisema maamuzi yaliyochukuliwa na TCRA kuagiza kuondolewa kwa chaneli za ndani kwenye baadhi ya ving’amuzi na visimbuzi vya makampuni ya DSTV, AZAM TV na Zuku TV ambavyo havikuwa na leseni ya kurusha chaneli za ndani umelenga kusimamia sheria zilizopo.

Alisema ving’amuzi vilivyozuiliwa vinapaswa kuheshimu sheria za nchi na kwamba vituo vilivyoshinda tenda ya kuonesha chaneli za ndani zipatazo nane ndizo zinazopaswa kuonesha chaneli hizo na si vituo vingine.Alifafanua kuwa baada ya kuhama kutoka kwenye analojia kuja digitali, serikali iliweka sheria na taratibu ambazo zinatakiwa kufuatwa ili jamii iendelee kunufaika na uhabarishwaji pasipo kurudishwa nyuma na gharama kubwa.

"Kuna kitu kinaitwa FTA (hii ni ya kurusha Maudhui Bila kulipia) na vipindi vya kutolipia ni Vipindi vya Kijamii ikiwemo taarifa ya Habari, vinapaswa kuwa Bure.Na kuna mfumo wa (Subscription by payment) pay TV yaani watumiaji wanapata vipindi vya TV kwa kulipia, na hivi vipindi ni vile ambavyo si vipindi vya kijamii.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mheshimiwa Zainab Telack akifungua semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa viongozi mbalimbali wa serikali, mashirika ya umma na asasi za kiraia mkoani Shinyanga kwa ajili ya kuwapa uelewa viongozi hao juu ya sababu za TCRA kufungia baadhi ya ving’amuzi kurusha chaneli za ndani baada ya kubaini vimekiuka masharti ya leseni zao.Picha zote na Suleiman Abeid -Malunde1 blog.

Mhandisi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Francis Mihayo TCRA Makao Makuu jijini Dar es Salaam akitoa mada wakati wa semina ya siku moja iliyoendeshwa na Mamlaka hiyo kwa viongozi mbalimbali wa serikali, mashirika ya umma na asasi za kiraia mkoani Shinyanga kwa ajili ya kuwapa uelewa viongozi hao juu ya sababu za TCRA kufungia baadhi ya ving’amuzi kurusha chaneli za ndani baada ya kubaini vimekiuka masharti ya leseni zao.

Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mheshimiwa Zainab Telack wakisikiliza mada ukumbini.
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mada ukumbini.

MICHUZI TV: ALICHOKIZUNGUMZA RAIS DKT MAGUFULI ALIPOKUTANA NA WATAALAMU MBALIMBALI W...

AZAM TV: Maneno ya Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi kwa Rais John Pombe Magufuli

KUMBUKUMBU YA MPENZI WETU MAMA KATHERINE LAWRENCE SAGUTI SEPTEMBA 22, 1936 - OCTOBA 4, 2009

$
0
0
MAMA, Leo hii unatimiza miaka tisa (9) tokea ulipotuacha hapa duniani. Kila siku tunakukumbuka Mama. Umetufundisha kukua katika upendo, ukweli, uaminifu na kumcha Mungu. Tunamuomba Baba  Mungu atuwezeshe tuyaendeleze na kuyaenzi mema yote uliyotufundisha na tuyaendeleze kwa vizazi vyetu vijavyo. MAMA, daima tutaendelea kujivunia zawadi tuliyopewa na Baba Mungu ya maisha yako kwetu sisi kwa maana uliyagusa maisha yetu kwa njia ya pekee.

Unakumbukwa daima na mume wako mpenzi Mzee Lawrence Shelukindo Saguti, watoto, wakwe na wakamwana, wajukuu na vilembwe

...........Tunaendelea kusimama imara na neno toka Ufunuo wa Yohana 12: 11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

..........Na tukimsifu Mungu tukiimba:
Amini Bwana awapenda, Amini,atawabariki, Atawahurumia wote, wamjiao yeye.
Kweli tutaona furaha, Tukifika kwenye Raha kuu, Tukisafishwa mioyo yetu na Yesu Mwokozi.


Endelea kupumzika kwa amani MAMA!


AMEN

SERIKALI YASIMIKA TAA ZA KUONGOZEA MAGARI MANISPAA YA MOROGORO

$
0
0

Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) kikosi cha Umeme, imefanikisha mradi wa kufunga taa za kuongozea magari (Traffic lights) katika Manispaa ya Morogoro. Taa hizo za kisasa ambazo zinatumia nishati ya jua zimesimikwa katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe inayotokea kituo kikubwa cha mabasi cha Msamvu kuingia mjini. 

Akizungumza wakati wa tukio la usimikaji wa taa hizo, Kaimu meneja wa Kikosi cha Umeme kutoka wakala huo Mhandisi Pongeza Semakuwa alisema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni mia moja na sitini na sita na ni wa kwanza kufanywa na wakala katika manispaa hiyo, ‘’taa hizi ni za kisasa zaidi na zinatoa suluhisho la muda kwa watumiaji kwakua zinahesabu sekunde mtumiaji akiwa anaona, tupo kwenye majadiliano na TARURA na kuna uwezekano tukasimika taa katika maeneo mengine hapa,’’ alisema Mhandisi Pongeza.

Aidha Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Manispaa ya Morogoro Mhandisi Mnene James amesema wataendesha mafunzo wakishirikiana na TEMESA kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara hizo kuhusu namna sahihi ya kutumia taa hizo na alama za kivuko cha waenda kwa miguu ili kuepusha ajali ambazo zimekua zikitokea mara kwa mara katika eneo hilo hasa kwa madereva wa bodaboda. 

Kukamilika kwa mradi huo kunaifanya Manispaa ya Morogoro kuwa na makutano ya pili kuwekwa taa za kuongozea magari baada ya makutano ya barabara ya Mazimbu na Iringa eneo la Tumbaku kupitiwa na mradi kama huo hivi karibuni.
 Muonekano wa taa za kuongozea magari (traffic lights) zilizosimikwa na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) katika manispaa ya Morogoro katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe inayotokea kituo kikubwa cha mabasi cha Msamvu kuingia mjini. Taa hizo za kisasa zinatumia umeme wa jua.
 Mafundi kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakifunga taa za kuongozea magari (traffic lights) katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe manispaa ya Morogoro. Kukamilika kwa mradi huo kunaifanya Manispaa ya Morogoro kuwa na makutano ya pili kuwekwa taa za kuongozea magari baada ya makutano ya barabara ya Mazimbu na Iringa eneo la Tumbaku kupitiwa na mradi kama huo hivi karibuni.
 Fundi kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) akiunganisha nyaya katika paneli ya sola itakayotumika katika kuongozea mfumo wa taa za kuongozea magari zilizosimikwa katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe manispaa ya Morogoro.
 Kaimu meneja wa Kikosi cha Umeme kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Pongeza Semakuwa kulia akikadiria na kuseti sekunde katika kidhibiti muda (‘’controller’’) ya kuongozea taa za barabarani ambazo zimesimikwa katika manispaa ya mji wa Morogoro katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe.
Mafundi kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakiweka boksi la kuhifadhia kifaa cha kudhibiti na kukadiria muda wa kuwaka kwa taa za kuongozea magari barabarani (‘’controller’’), taa hizo zimesimikwa katika manispaa ya mji wa Morogoro katika makutano ya barabara ya Mei mosi na Korogwe. PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO 

TTCL YAMUONGEZA MSANII MAN FONGO TAMASHA LA RUDI NYUMBANI KUMENOGA

$
0
0

Mkuu wa Biashara Mkoa wa Dar es Salaam wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Bi. Mary Kinabo (kushoto) akisaini mkataba leo Dar es Salaam na msanii wa muziki aina ya singeli, Man Fongo (kulia) ili msanii huyo kushiriki katika kampeni kubwa ya Rudi Nyumbani Kumenoga inayoendelea mikoa yote ya Tanzania. Anayeshuhudia kulia ni mwanasheriaa wa TTCL, .Wasanii wengine wanaaonogesha kampeni hiyo ni pamoja na Asley Isihaka maarufu kama Dogo Asley na Shilole ‘Shishi Baby’.
Mkuu wa Biashara Mkoa wa Dar es Salaam wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Bi. Mary Kinabo (kushoto) akibadilishana mkataba na msanii wa muziki aina ya singeli, Man Fongo (kulia) mara baada ya kuusaaini ili msanii huyo kushiriki katika kampeni kubwa ya Rudi Nyumbani Kumenoga inayoendelea mikoa yote ya Tanzania. Anayeshuhudia kulia ni mwanasheriaa wa TTCL. Wasanii wengine wanaaonogesha kampeni hiyo ni pamoja na Asley Isihaka maarufu kama Dogo Asley na Shilole ‘Shishi Baby’.
Mkuu wa Biashara Mkoa wa Dar es Salaam wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Bi. Mary Kinabo (kushoto) akimpongeza msanii wa muziki aina ya singeli, Man Fongo (kulia) mara baada ya kuusaini mkataba ili msanii huyo kushiriki katika kampeni kubwa ya Rudi Nyumbani Kumenoga inayoendelea mikoa yote ya Tanzania. Anayeshuhudia kulia ni mwanasheriaa wa TTCL.
Mkuu wa Biashara Mkoa wa Dar es Salaam wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Bi. Mary Kinabo (kushoto) pamoja na msanii wa muziki aina ya singeli, Man Fongo (kulia) wakionesha mkataba mara baada ya msanii huyo kushiriki katika kampeni kubwa ya Rudi Nyumbani Kumenoga inayoendelea mikoa yote ya Tanzania. Anayeshuhudia kulia ni mwanasheriaa wa TTCL.
Sanii wa muziki aina ya singeli, Man Fongo (kulia) akizungumza mara baada ya kusaini ili kushiriki katika kampeni kubwa ya Rudi Nyumbani Kumenoga inayoendelea mikoa yote ya Tanzania.
Mkuu wa Biashara Mkoa wa Dar es Salaam wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Bi. Mary Kinabo na Man Fongo wakizungumza.
Afisa Masoko Mkuu wa Shirika la mawasiliano Tanzania (TTCL), Laibu Leornad (kushoto) akizungumza katika hafla hiyo.

TAASISI YA MAENDELEO YA JAMII TENGERU YADHAMIRIA KUPAMBANA NA UKEKETAJI, NDOA NA MIMBA ZA UTOTONI

$
0
0
Na Mwandishi Wetu- Arusha
Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru imeadhimiria kupambana na vitendo vya ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni kwa kuzalisha wataalamu wa maendeleo ya jamii ambao watasaidia kutoa elimu na kuhamasisha jamii ili kuondokana na ukatili huu wa kijinsia ambao kwa kiasi kikubwa humkosesha haki mtoto wa kike katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa mkoani Arusha na Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt.  Bakari George wakati akifungua mdahalo wa siku moja uliofanyika Chuoni hapo wenye lengo la kujadili changamoto ziwapatazo watoto wa kike na kusababisha kukatiza ndoto zao kuelekea mafaniko ya kimaisha.

Aidha Mkuu huyo wa Chuo aliwataka washiriki wa mdahalo huo kujadiliana kwa uwazi ili kutoa fursa kwa washiriki wa mdahalo huo kupata elimu sahihi ya changamoto zinazowakabili watoto wa kike na kuwa kikwazo kwao kufikia ndoto zao kielimu lakini pia kutoa fursa kwa wanafunzi wa chuo chake kutambua namna bora kukomesha vitendo vya ukatili kwa kuwa itakuwa jukumu la kiutendaji kwa kwakuwa wao ni wataalamu wa maendeleo ya Jamii.

Dkt. Bakari amesema kuwa vijana ni waathirika wakubwa wa mimba na ndoa za utotoni ikiwemo tatizo la ukeketaji hususani katika mikoa ambayo inaongoza kwa mimba na ndoa za utotoni na ukeketaji tatizo ambalo kimsingi linatokana na mila na desturi potofu hapa nchini.
 Kaimu Mkuu wa Taasisi ya  Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt. Bakary George akifungua mdahalo wa kujadili masuala ya Mimba na Ndoa za utotoni pamoja na ukeketaji uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru.
 Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Bw. Christopher Mushi akieleza lengo la mdahalo  kwa wajumbe wa mdahalohuo  uliojadili masuala ya Mimba na Ndoa za utotoni pamoja na ukeketaji uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru.
Wadau na wanafunzi  mbalimbali wakifuatilia kwa makini mdahalo wa kujadili masuala ya Mimba na Ndoa za utotoni pamoja na ukeketaji uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano- WAMJW

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KUKAMILIKA KWA MRADI WA MAJI KISARAWE KUTANUFAISHA SEKTA YA VIWANDA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na MajiTaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyenge amesema kuwa kukamilika kwa mradi wa Kisarawe kutanufausha mji mzima wa kisarawe, eneo la sekta viwanda na vitongoji jirani na mji huo.

Akiwa katika awamu ya kwanza ya ziara ya siku 2 Pia aliongozana na Mwenyekiti wa kamati ya Bodi ya Ufundi Mhandisi Gaudence Aksante sambamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja

Akizungumza  baada ya kumaliza ziara ya siku ya kwanza, Jenerali Mwamunyange amesema kuwa mradi huo ukikamilika shida ya maji ya miaka mingi inakwisha chini ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.

 Jenerali Mwamunyange amesema kuwa, DAWASA ina dhamira ya  kufikisha maji Kisarwe na kuondokana na uhaba wa upatikanaji wa maji kama agizo la Rais alivyoagiza wakati wa uzinduzi wa mtambo wa Ruvu Juu uliopo Mlandizi  mkoani Pwani.

Katika ziara hiyo, Jenerali amejionea hatua miradi ya maji ilipofikia  na lengo zaidi ni kuongeza maji katika Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani na wananchi wawe na matumaini kwani mradi huo utakamilika ndani ya muda mfupi  na utapeleka maji lita 4,080,000 kwa siku.

Jenerali amesema, kulikuwa na changamoto ya kuendelezwa kwa miradi na mingine ikikaa mda mrefu zaidi ila DAWASA wameweza kukaa chini na wakandarasi na wamewahimiza kuhakikisha wanamaliza miradi hiyo kwa wakati na zaidi matatizo yao yametatuliwa.

Amesema, "nafahamu Jiji la Dar es Salaam linakua kila siku na kwa kila mwaka asilimia 5.7 ongezeko la wakazi na linakuwa na maji yanahitajika kwa wingi,"

Amemalizia kwa kuwekea msisitizo, kuwa DAWASA kupitia kwa menejimenti yake na Bodi wana mikakati ua kutafuta vyanzo vipya vya maji ili  kuongeza maji katika maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Dar es Salaam, kuboresha miundo mbinu iliyochakaa na ile inayovuja.

Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa mradi huo wa matanki yaliyojengwa sehemu tofauti yatasaidia ongezeko la wateja Milioni 1 wapya.

Amesema kuwa, mradi wa Salasala umeshatandikwa Km40 kwa ajili ya kuanza kuunganisba maji katika maeneo ya Madale, Changanyikeni, Mivumogi na Goba na zaidi changamoto kubwa ilikuwa ni mtandao kuwa mdogo na maji kuwa mengi.

DAWASA kwa siku inazalisha maji Lita Milioni 502 kwa siku.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na MajiTaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyenge akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kutembelea miradi mbalimbali ya maji inayosimamiwa na Mamlaka hiyo.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya MajiSafi na MajiTaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akimuelezea jambo Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na MajiTaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyenge pamoja naMwenyekiti wa kamati ya Bodi ya Ufundi Mhandisi Gaudence Aksante sambamba wakati wa ziara ya kutembelea miradi mbalimbali. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na MajiTaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyenge (katikati( akishuka ngazi katika moja ya Tanki lilijojengwa kwa ajili ya kuhifadhi maji.

BENKI YA TPB YASAIDIA KUTATUA CHANGAMOTO YA UHABA WA MADARASA,OFISI ZA WALIMU KATIKA SHULE YA MSINGI MISRAY

$
0
0

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii.

UONGOZI wa Shule ya Msingi Misray iliyopo wilayani Kondoa wameishukurua benki ya TPB kwa kuwasaidia kuwajengea vyumba viwili vya madarasa,ofisi za walimu pamoja na samani zake.

Umesema msaada huo sasa utaondoa changamoto kubwa ambayo walimu na wanafunzi wa shuleni hapo walikuwa wanaupata ikiwemo ya kukatisha masomo pindi mvua inaponyesha.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Misray Veronica Gabriel ametoa shukrani hizo mbele ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya TPB Dk.Edmund Mndolwa.

Ambapo makabidhiano ya msaada huo yalifanyika shuleni hapo na mgeni rasmi alikuwa Dk.Kijaji ambaye ndiye aliyekabidhi kwa uongozi wa shule hiyo.Mwalimu Gabriel amesema kuwa wanatoa shukrani kwa uongozi wa benki hiyo na kuahidi msaada huo wa majengo watautunza pamoja na samani zote ambazo zimetolewa."Napenda kuwahakikishia uongozi wa Benki ya TPB kuwa huu msaada umesaidia kutatua tatizo la uhaba wa majengo duni yaliyooezekwa kwa nyasi na ilitulazimu kukatisha masomo pindi mvua inaponyesha.

" Kwa kweli ilikuwa changamoto kubwa sana .Tunatoa rai kwa taasisi nyingine kutoa misaada kama hii kwa ajili ya kuondoa changamoto zilizopo,"amesema.Kwa uoande wake Dk.Mndolwa amesema wao kama taasisi ya fedha inayohudumia jamii wameguswa na matatizo hayo na ndio maana walipopokea naombi kutoka kwa uongozi wa shule hiyo wakaona ni vema wakasaidia.

"Tumetoa msaada huu baada ya kushuhudia mazingira magumu ambayo watoto hawa walikuwa wanakabiliana nayo kutokana na kukosa majengo ya madara." Hawa watoto wetu sote na ni jukumu letu kama wazazi kuona umuhimu wa jambo hili la kuwasaidia kwani hawa watakuwa viongozi wetu wa baadae.Ujenzi umegharimu Sh.Milioni 63 ,"amesema Dk.Mndolwa.

Kutokana na msaada huo shule hiyo imefanikiwa kutatua changamoto ya tatizo la madarasa,ofisi ya walimu na samani zake baada ya benki hiyo kusaidia.


Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji akipiga makofi wakati wa uzinduzi wa jengo la darasa katika Shule ya Msingi Misray wilayani Kondoa.Majengo hayo yamejengwa na Benki ya TPB
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB Dk.Edmund Mndolwa wa kwanza kulia pamoja na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji anayefuata wakiwa pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali na walimu wakati wa kukabidhiwa kwa majengo mawili ya madarasa, ofisi na samani kwa shule ya msingi Misray.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji akiwa pamoja na viongozi wa benki ya TPB na wanafunzi wa Shule ya Msingi Misray wilayani Kondoa baada ya kukabidhiwa msaada wa majengo mawili ya madarasa,ofisi za walimu na samani zake

VODACOM YAWAKUMBUKA WATEJA WAKE WA SIKU YA KWANZA INAANZISHWA

$
0
0

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi akikata keki maalum ya kuwashukuru wateja kwa kuiamini kampuni hiyo ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Harieth Lwakatale akishuhudia.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi (kulia) akimuhudumia mmoja wa wateja aliyefika kupata huduma kituo cha Makao Makuu ya Ofisi za Vodacom Tanzania jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Harieth Lwakatale (kulia) akiwakabidhi zawadi baadhi ya wateja wa mtandao huo walio jiunga siku ya kwanza na yapili mtandao huo ulipoanzishwa nchini Tanzania. Wateja hao wa kwanza walipata fursa ya kutembelea na kujifunza shughuli za Vodacom Tanzania ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja. 
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Harieth Lwakatale (kulia) akimkabidhi zawadi mmoja wa wateja wa mtandao huo walio siku ya kwanza na yapili mtandao huo ulipoanzishwa nchini Tanzania. Wateja hao wa kwanza walipata fursa ya kutembelea na kujifunza shughuli za Vodacom Tanzania ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja. 

WALIMU TABORA WATAKIWA KUZINGATIA WARAKA WA ELIMU NAMBA 24 WA 2002 WAKATI WA KUTOA ADHABU YA VIBOKO

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tabora Msalika Makungu amewataka walimu katika shule mbalimabli mkoani humo kuzingatia Waraka wa Elimu namba 24  wa mwaka 2002 wakati utoaji adhabu za viboko kwa wanafunzi ili kuepuka kuingia katika matatizo na kushitakiwa kwa makosa mbalimbali.

Alisema lengo ni kuhakikisha wanapotoa adhabu za viboko kwa wanafunzi watukutuku wanazingatia matakwa ya Waraka huo na kuepuka kuingia tuhuma za kushitakiwa kwa makosa ya jinai kama yaliyotokea hivi karibuni mkoani Kagera.

Makungu ametoa kauli hiyo jana wakati wa kikao kazi cha siku moja na Maafisa Elimu Kata, Walimu wa wakuu wa shule za Msingi na Sekondari kutoka Wilaya ya Tabora, Wilaya ya Uyui na Sikonge ili kuwapitisha katika  mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi wao.

Alisema kuna baadhi ya walimu wanasifika kwa utoaji wa adhabu ya viboko jambo ambalo ni hatari kwao na kwa ajira zao na familia zao.

 “Hivi walimu wenye tabia ya kupenda kuchapa viboko vingi kinyume cha maagizo ya waraka huu…wanafanya hivyo hivyo na kwa watoto wao au ni sawa na usemi usemao mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu”aliuliza.

Makungua alisema walimu wanadhamana kubwa ya kuwafundisha na kuwalea watoto kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Nchi ili hatimaye waje kuwa viongozi na watumishi wema wa nchi hii.

Alisema Waraka huo unaeleza vizuri namna ya utoaji wa adhabu ya viboko izingatie ukubwa wa kosa, umri, jinsi, afya ya mtoto na visizidi vinne kwa wakati mmoja na kutaka mtoto wa kike adhibiwe na Mwalimu wa Kike labda kama hakuna.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Msalika Makungu(katikati) akitoa ufafanuzi juu ya walimu kuzingatia  Waraka wa Elimu namba 24 wa mwaka 2002 kuhusu adhabu ya viboko. Ametoa ufafanuzi huo jana wakati wa kikao kazi cha siku moja cha Maafisa Elimu Kata na Walimu wa Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari kwa Wilaya za Tabora , Uyui na Sikonge. Wengine kwenye picha ni Katibu Tawala Msaidizi(ELIMU) Susan Nussu(kulia) na Afisa wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora Shukuru Kazembe(kushoto)
Baadhi ya Maafisa Elimu Kata na  Walimu wa Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari kutoka Wilaya za Tabora , Uyui na Sikonge wakiwa katika kikao kazi cha siku mjini Tabora jana kilichowaelimisha mambo mbalimbali ikiwemo uzingatiaji wa araka wa Elimu namba 24 wa mwaka 2002 kuhusu adhabu ya viboko.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MKUU WA MKOA WA IRINGA ATEMBELEA ATEMBELEA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MAKAO MAKUU – DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, akiweka sahihi kwenye kitabu cha wageni alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam, mapema leo tarehe 04/10/2018.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (wa pili kushoto) akitoa maelezo ya utendaji kazi wa Jeshi hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, akifuatilia kwa karibu maelezo aliyokuwa akiyatoa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CGF Thobias Andengenye, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, alipotembelea  Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo.
 Kamishna wa Operesheni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CF) Billy Mwakatage akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo.
 Picha ya Pamoja, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (wa kwanza kushoto) akiwa na. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, pamoja na Kamishna wa Operesheni (CF) Billy Mwakatage (wa kwanza Kulia), mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo, Jijini Dar es Salaam mapema leo. 
(Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)


SITAMVUMILIA ANAYEIHUJUMU NHIF- RC MBEYA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Mbeya
SERIKALI mkoani Mbeya imesema itachukua hatua kali kwa mtu yeyote atakayejihusisha na udanganyifu wa huduma zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Onyo hilo  limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Albert Chalamila wakati akifungua mkutano wa wadau wa NHIF mkoani humo. “Kufanya udanganyifu kwa huduma za Mfuko ni kuhujumu jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali za kumairisha upatikanaji wa huduma za matibabu kwa wananchi, hivyo ndani ya Mkoa huu sitavumilia kuona hili.
 “Tunasikia kuna baadhi ya wadau wa Mfuko wasio waaminifu wamekuwa wakihujumu Mfuko huu, kwa upande wa Mkoa wa Mbeya niliweke tu wazi kuwa atakayejihusisha na udanganyifu wowote nitakula naye sahani moja, ni lazima huu Mfuko tuulinde ili uweze kuhudumia wananchi na hata vizazi vijavyo,” alisema Bw. Chalamila.
Ili kuhakikisha huduma za Mfuko zinalindwa, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wadau wote mkoani humo kuhakikisha kila mmoja anakuwa mlinzi wa huduma za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Akisisitiza juu ya wananchi kujiunga na huduma za Mfuko, ameweka wazi kuwa ili taifa liweze kufikia malengo yake na kutimiza ndoto ya Rais Dkt. John Magufuli ya Tanzania kuwa ni nchi ya Uchumi wa Kati kupitia uwekezaji wa Viwanda ni lazima huduma za matibabu ziwe za uhakika kwa wananchi wote.
“Ni azma ya Serikali hii kuwafikia watanzania wote na huduma bora za matibabu kupitia Bima ya Afya, kukamilika kwa azma hii kutaruhusu watu wengi zaidi kutumia huduma za matibabu ambazo awali walishindwa hivyo niwaombe tu watoa huduma mjipange kuweka mazingira mazuri ya kuwahudumia watu hawa,” alisema Mkuu wa Mkoa.
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Albert Chalamila akifungua mkutano wa Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani humo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHIF, Mama Anne Makinda akihutubia wadau wa mkutano huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bw. Beranrd Konga akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Mfuko kwa Wadau wa Mkoa wa Mbeya.

 Sehemu ya Wajumbe wa Bodi ya NHIF wakifuatilia taarifa ya utekelezaji.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MKUU ATEMBELEA ENEO UTAKAPOJENGWA MRADI WA KUZALISHA UMEME WA STIEGLERS GORGE

$
0
0

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama eneo lililoandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa Mradi wa  Kuzalisha Umeme katika  Maporomoko ya Mto Rufiji- Stieglers Gorge wakati alipotembelea eneo hilo Oktoba 4, 2018. Kushoto kwake ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   akizungumza baada ya kutembelea eneo  la ujenzi wa Mradi wa  Umeme wa Moporomoko ya  Mto Rufiji – Stieglers Gorge, Oktoba 4, 2018. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kanda ya Tanzania wa TAZARA,  Fuad Abdallah wakati alipotembelea Stesheni ya TAZARA ya Fuga kukagua ujenzi wa tawi la reli hiyo  litalounganisha steheni hiyo na eneo utakapojengwa Mradi wa Umeme wa Maporomoko ya mto Rufiji – Stieglers Gorge, Oktoba 4, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo wakati alipowasili kwenye  eneo utakapojengwa  Mradi wa  Umeme katika Maporomoko ya Mto Rufiji  - Stieglers Gorge, Oktoba 4, 2018. Kulia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na wapili kulia ni  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Stephen Kebwe. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka wa Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) kuhusu ujenzi wa tawi la reli litakalounganisha Stesheni ya Fuga katika  reli ya TAZARA na eneo utakapojengwa  Mradi wa Umeme wa Maporomoko  ya Mto Rufiji – Stieglers Gorge  wakati alipotembelea eno hilo Oktoba 4, 2018.  Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji  wa Kanda ya Tanzania wa TAZARA, Fuad Abdallah. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua ujenzi wa tawi la reli litakalounganisha Stesheni ya Fuga katika reli ya TAZARA na  eneo utakapojengwa Mradi wa Umeme wa Moporomoko ya Mto Rufiji – Stieglers Gorge wakati alipotembelea Stesheni hiyo, Oktoba 4, 2018. Kushoto ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kanda ya Tanzania wa TAZARA, Fuad Abdallah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Eneo litakapojengwa tuta la kukinga maji  katika  Mradi wa Kuzalisha Umeme kwenye  Maporomoko ya Mto Rufiji- Stieglers Gorge  ambalo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alilitembelea, Oktoba 4, 2018.

MKUU WA MKOA WA IRINGA ATEMBELEA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MAKAO MAKUU – DAR ES SALAAM

$
0
0

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, akiweka sahihi kwenye kitabu cha wageni alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam, mapema leo tarehe 04/10/2018.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (wa pili kushoto) akitoa maelezo ya utendaji kazi wa Jeshi hilo kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 04/10/2018.
Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, akifuatilia kwa karibu maelezo aliyokuwa akiyatoa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CGF Thobias Andengenye, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam, mapema leo tarehe 04/10/2018.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye akisalimiana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 04/10/2018.
Kamishna wa Operesheni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CF) Billy Mwakatage akisalimiana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 04/10/2018.
Picha ya Pamoja, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (wa kwanza kushoto) akiwa na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi, pamoja na Kamishna wa Operesheni (CF) Billy Mwakatage (wa kwanza Kulia), mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo, Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 04/10/2018. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)

WALIODANGANYA MATOKEO SHULE ZA MSINGI WANAIHUJUMU SERIKALI-MTANDAO WA ELIMU TANZANIA

$
0
0
MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET) umetoa kauli na kulaani vitendo vya udanganyifu kwenye Shule za Msingi nchini, vilivyofanywa na baadhi ya watendaji wa elimu hadi kusababisha Baraza la Mitihani Tanzania kufuta matokeo ya Darasa la Saba kwa baadhi ya shule.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania, Bi. Cathleen Sekwao alisema kitendo kilichofanywa na watendaji hao waliopewa dhamana ya kusimamia elimu ni sawa na kuhujumu juhudi kubwa za Serikali na wadau wengine wa elimu zinazofanyika kuinua kiwango cha elimu nchini.

Alisema kitendo cha wanafunzi hao kufutiwa matokeo ya mitihani kimewaathiri wanafunzi kisaikolojia na hisia na kuwapotezea uwezo wao wa kujiamini katika kufanya mitihani mingine, licha ya kwamba walioshirikishwa hawakuwa na uwezo wa kupinga wanachoelekezwa na walimu au viongozi katika jambo hilo.

“Ikumbukwe kuwa mtoto wa Darasa la Saba hana uwezo wa kupinga anachoelekezwa na viongozi au walimu wake hivyo huamini kila anachoambiwa afanye ni chema bila kujua madhara yake ya baadae. Ni dhahiri kuwa kitendo cha kufutiwa matokeo ya mitihani kimewaathiri watoto hao kisaikolojia na kihisia na hivyo kuwapotezea uwezo wao wa kujiamini katika kufanya mitihani mingine na safari yao ndefu ya kutimiza ndoto zao,” alisema Bi. Sekwao.

Alipongeza uamuzi uliofanywa na Serikali kupitia Baraza la Mitihani kuwafanya warudie mitihani ni jambo jema, inaonesha dhahiri kwamba kuna nia ya kuwapa fursa watoto hao. Pamoja na hayo alishauri muda uliotolewa wa kurudia mitihani hiyo ni mdogo kuwawezesha watoto hao kujiandaa na kujijenga kisaikolojia ili kuwa tayari kufanya mtihani mwingine.

“…Tunapendekeza kuwa angalau wapewe mwezi mmoja wa kujiandaa na kujengwa kisaikolojia…Mtandao unaipongeza Serikali kwa kuweza kubaini kitendo hiki cha hujuma na kuchukua hatua za awali. Ni matarajio yetu kuwa uchunguzi utakapokamilika wale wote waliohusika watachukuliwa hatua stahiki za kisheria na kinidhamu ili iwe fundisho kwa umma,” alisisitiza Bi. Sekwao.

Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Cathleen Sekwao (kushoto) akitoa kauli ya mtandao huo kupongeza Serikali kupitia Baraza la Mitihani kufuta matokeo ya darasa la saba kwa baadhi ya shule kwa ile kuonekana uwepo wa mchezo mchafu kuchezea mitihani hiyo. Kulia ni Meneja Programu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met), Bw.Nicodemus Shauri Eatlawe. 

Meneja Programu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met), Bw.Nicodemus  Shauri Eatlawe (kulia) akitoa ufafanuzi kwa wanahabari kuhusiana na kauli ya mtandao huo juu ya kufutwa kwa matokeo ya mitiani darasa la saba. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa REPSSI nchini Tanzania, Edwick Mapalala na Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Cathleen Sekwao wakifuaatilia.

Mkurugenzi wa REPSSI nchini Tanzania, Edwick Mapalala (kushoto) akizungumza kwenye mkutano huo wa TEN/MET na waandishi wa habari. Kulia ni Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Cathleen Sekwao akifuatilia. 

Afisa Programu wa TenMet, Bi. Alistidia Kamugisha (kushoto) akichangia hoja katika mkutano huo na wanahabari. Kulia ni Bi. Edwick Mapalala. 

MWENYEKITI WA BODI DAWASA AKAGUA MRADI WA MAJI CHALINZE

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mwenyekiti wa Bodi ya ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA)  Mkuu wa Majeshi mstaafu  Jenerali Davis Mwamunyange  amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa upanuzi wa mtambo na mfumo wa CHALIWASA awamu ya tatu ambao chanzo chake ni mto Wami. 

Katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi anatarajiwa kutembelea kazi mbalimbali za mradi ikiwemo shughuli za upanuzi wa chanzo, ujenzi wa matenki na kazi za ulazaji mabomba. 

Mradi huu unaojengwa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji  kupitia na DAWASA unahusisha ujenzi wa Matenki 19, ulazaji wa mabomba ya ukubwa mbalimbali kwa kilometa 1, 203, ujenzi wa vizimba vya kuchota maji pamoja na upanuzi wa mtambo wa kusafisha maji wa CHALINZE. Lengo ni kuongeza uzalishaji kufikia mita za ujazo 900 kwa siku kutoka mita za ujazo 500.

Kazi hii itakapokamilika, wakazi waliopo maeneo ya Manga hadi Tengwe katika Mkoa wa Tanga, mji na vitongoji  vya Wilaya ya Chalinze na baadhi ya maeneo ya Bagamoyo na Kibaha katika mkoa wa Pwani watafaidika.

 Mradi pia utanufaisha baadhi ya maeneo ha Mkoa wa Morogoro ikiwa ni pamoja na  maeneo ya Kizuka A na B, Ngerengere, Kinoko A and B, Tukamisasa, Lulenge, Visakazi hadi Bwawani  pamoja na Sangasanga A na B,Hadi utakapokamilika, mradi utagharimu dola za Marakani 41,362,023.43 ambazo ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya EXIM ya India.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na MajiTaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyange akizungumza na wanahabari baada ya kutembelea mradi wa Chalinze ulio chini ya kampuni ya Jain Irrigation System akiwa sambamba na Mbunge wa Jimbo Chalinze Ridhiwani Kikwete.

Meneja Mradi kutoka kampuni ya Jain Irrigation System inayojenga mradi wa Chalinze  P. G. Rajan Wapcos akimuelezea Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyange mradi mzima pamoja na matenki 19 ya kuhifadhia maji.

TIC YASEMA KUKAMILIKA KWA UWANJA WA NDEGE JENGO LA TATU KUTAVUTIA WAWEKEZAJI WENGI ZAIDI

$
0
0
Na Grace Semfuko-MAELEZO.

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kinatambua kuwa miezi michache ijayo Serikali kwa kukamilisha ujenzi wa majengo na ufungaji wa mitambo ya kisasa kukidhi mahitaji ya teknolojia ya kimataifa, jengo la tatu (terminal 3) Uwanja wa Kimataifa Julius Nyerere( JNIA) ni ukurasa mpya wa fursa za kuongeza kasi ya uwekezaji hapa nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Geoffrey Mwambe alitembelea eneo la Ujenzi na kupokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania ( TAA), Richard Mayongela kwa ziara ya kutambua zaidi mapya ya jengo la tatu ili kumpa nafasi ya kujenga vishawishi kwa wawekezaji kuhusu manufaa ya chombo hicho kinachokamilika wakati tayari tatizo la foleni ya magari toka uwanjani huo kuingia jijini umeisha baada ya barabara la juu kukamilika katika maungo ya barabara za Mandela toka Bandarini na Nyerere itokayo JNIA. 

TIC ni taasisi ya Serikali, imekuwa ikifanya juhudi za kufafanua kwa wawekezaji fursa zilizopo Tanzania kwa lengo la kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje nchi , na hivyo kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo na kuwa chombo chenye kila hitaji la abiria wa anga katika dunia ya sasa, utaongeza idadi ya wawekezaji kwa sababu ya huduma mpya hizo. “Huduma yetu usafiri wa anga inabadilika kabisa” amesema Mkurugenzi Mkuu TAA, Mayongela.

Mayongela amesema kukamilika kwa uwanja huo mpya jengo la tatu kutaondoa kabisa msongamano wa abiria uliopo uwanja wa pili (Terminal 2) uliojengwa miaka 34 iliyopita, ambao kwa wakati huo ulilenga kuhudumia abiria Milioni 1.5 na sasa umezidiwa kwa kuhudumia abiria hadi milioni 2.5 kwa mwaka, kutokana na ongezeko la abiria nahatimaye kusababisha kuzidiwa kwa uwanja huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Bw.Richard Mayongela akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Geoffrey Mwambe walipotembelea uwanja wa ndege wa tatu wa Mwalimu Julius Nyerere kukagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo ambao unajengwa na Serikali kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 560 za kitanzania, ujenzi huo ulianza Mwezi Juni 2013 unatarajia kukamilika mwezi mei 2019 (Picha na Grace Semfuko)
Jengo jipya la tatu la Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere linavyoonekana kwa mbele likiwa limelamilika kwa asilimia 82 ya ujenzi wake, jengo hilo linagharimu zaidi ya shilingi bilioni 56 za kitanzania na linatarajia kukamilika ujenzi wake Mei 31 mwaka 2019
Jengo jipya la tatu la uwanja wa mwalimu Julius Nyerere likiwa katika hatua mbalimbali za umaliziaji wa ujenzi wake, Jengo hilo la tatu linatumia zaidi ya shilingi Bilioni 560 za kitanzania na lilianza kujengwa Mwezi juni 2013 na kutarajiwa kumalizika mwezi Mei 2019


Viewing all 110104 articles
Browse latest View live




Latest Images