Na Bashir Yakub.
( A ).NAMBA YA KESI.
Kesi ya Jinai Na. 22/1998, Mahakama kuu Mwanza , Mbele ya Jaji Mlay.
( B ) WASHITAKIWA.
1. Kapteni Jumanne Rume Mweiru. Huyu ndiye alikuwa Kapteni siku ya tukio, akiendesha toka Bukoba VIA kemondo Bay hadi Mwanza.
2. Gilbert Mokiwa. Huyu alikuwa mkaguzi wa meli, na ndiye alikuwa na wajibu wa kuikagua MV Bukoba.
3. Alphonce Sambo. Huyu alikuwa afisa bandari Bukoba, na wakati meli inaanza safari yeye na wenzake waliratibu safari.
4. Prosper Rugumila.Huyu alikuwa afisa bandari kemondo ambapo MV Bukoba ilipitia ikitokea bandari ya Bukoba na kuongeza abiria na mizigo.
( C ) KOSA WALILOSHITAKIWA NALO.
Kuua bila kukusudia kinyume na kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 ya Sheria za Tanzania.
( D ) MAELEZO YA KOSA.
Kuwa, tarehe 21 / 5 / 1996 majira ya saa 7 :30 asubuhi, eneo la ziwa Victoria Mwanza washitakiwa kwa uzembe walisababisha meli ya MV BUKOBA iliyokuwa ikitokea Bukoba kuelekea Mwanza kupinduka na kuzama ,na hivyo kusababisha vifo vya watu 159.
( E ) MASHAHIDI UPANDE WA MASHTAKA.
Upande wa mashitaka ulileta mashahidi 32 wakiwemo ;
1. Kapteni Cleophas Magoge . Huyu saa 8 : 15 asubuhi,aliitoa MV VICTORIA bandarini Mwanza ilipokuwa inaendelea na matengenezo na kulazimika kuiendesha kuelekea kwenye eneo la ajali baada ya kuambiwa kuwa MV BUKOBA imezama.
Anasema alipofika eneo la tukio aliiona MV Bukoba ikiwa kichwa chini miguu juu, huku mizigo hasa ndizi,watu, na miili mingi ikielea majini. Na aliposogea karibu alimuona Kapteni wa MV Bukoba mshitakiwa wa kwanza akiwa ananing’inia juu ya meli iliyozama.
KUSOMA ZAIDI sheriayakub.blogspot.com