Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live

BBC DIRA YA DUNIA JUMANNE 11.09.2018


Waziri Mkuu Majaliwa Afungua Mkutano wa Tano wa Wadau wa Lishe, atahadharisha ULAJI USIOFAA UNAONGEZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA-MAJALIWA

0
0
WAZIRI MKUUKassim Majaliwa amesemalishe duni pamoja na ulaji usiofaa na mitindo ya maisha vinachangia kwa kiasi kikubwa katika ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza hususan kwa vijana na watu wazima, ambao ndiyo nguvu kazi kwa Taifa. 
“Ni jambo lisilopingika kuwa hatua za kukabiliana na magonjwa ya kusendeka (mfano matatizo ya moyo, saratani, kisukari na shinikizo kubwa la damu) zinachangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza kasi ya maendeleo yetu kwani gharama za matibabu yake ni kubwa mno; si kwa kaya zinazoathirika tu bali kwa Taifa zima.” 
Waziri Mkuu  ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Septemba 11, 2018),  wakati akifungua mkutano wa tano wa wadau wa masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kambarage, Hazina jijini Dodoma.  
Waziri Mkuu amesema lishe iliyozidi inadhihirishwa na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukizwa yanayotokana na mabadiliko ya mitindo ya maisha na ulaji usiofaa kama vile uzito uliozidi, viriba tumbo, shinikizo la damu pamoja na kisukari. 
Amesema kasi ya ongezeko la magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza inapaswa kudhibitiwa kwa kuzingatia ulaji unaofaa na mtindo bora wa maisha. “Huu ni wakati wa kuangalia kwa pamoja kama jitihada zetu zinaleta matunda tunayotarajia.” 
Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya Taifa letu hivyo, uwepo wao katika mkutano huo unaonesha umuhimu wa kuimarisha ushiriki wa kila sekta, kila mdau ikiwemo sekta binafsi kwa nafasi yake katika kupambana na aina zote za utapiamlo.  
Amesema ushiriki wa kila sekta ni wa muhimu kwa sababu hakuna sekta moja pekee inayoweza kuondoa tatizo la utapiamlo, pia ni vema kwa wadau hao wakajitathmini mmoja mmoja katika sekta zao kuona kama wanaelekea katika muelekeo sawa na mipango ya Serikali. 
“Kwa kuzingatia hilo, ofisi yangu imeweka utaratibu maalum wa kuratibu utekelezaji wa kazi za lishe nchini, ambapo kamati ya Kitaifa ya Usimamizi na Ushauri kuhusu masula ya lishe nchini yaani High Level Steering Committee on Nutrition imeundwa ili kusimamia utekelezaji wa azma hiyo.”  
Waziri Mkuu amesema kwamba watu wote wanatambua jitihada kubwa zilizowekwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau katika kupambana na matatizo ya lishe nchini, ambapo taarifa za wataalamu zinasema kuwa kwa sasa nchi inakabiliwa na aina mbili za utapiamlo yaani lishe duni na lishe iliyozidi au iliyokithiri.  
Amesema walengwa wakubwa wa lishe duni ni pamoja na watoto chini ya miaka mitano, wanawake walio katika umri wa kuzaa hususani wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na vijana balehe (hususan wa kike). “Hii ni kwa sababu mahitaji ya virutubishi kwa ajili ya miili yao ni makubwa, ukilinganisha na ule unaohitajika na makundi mengine.” 
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akizungumza wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  akizungumza wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Benilith Mahenge  akizungumza wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".

  Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC), Dkt. Vicent Asey akizungumza wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".

 Mwakilishi wa kundi la vijana Rika Balehe ambaye pia ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Notre Dame ya jijini Arusha, Bi. Najma Mohamed akiwasilisha maoni yao kuhusu masuala ya lishe mbele wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".

 Mtaalamu wa Lishe kutoka UNICEF, Mauro Brero akichangia mada wakati wa hafla ya kufungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe wa kujadili na kutathmini utekelezaji wa afu za lishe leo jijini Dodoma. Mkutano huo unakauli mbiu ya "Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Lishe Bora ni msingi wa maendeleo yetu".Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

WAZIRI DKT KIGWANGALLA ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

0
0
Jopo la Madaktari Bingwa wa MOI linalomhudumia Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla limemruhusu kutoka wodini baada ya kujiridhisha kwamba afya yake imetengamaa na anaweza kurejea nyumbani na atakuwa anakwenda hospitalini hapo  kama mgonjwa wa nje kwa ajili ya muendelezo wa matibabu yaliyosalia.
Jopo hilo la madaktari bingwa watano  wa kada za Mifupa, Usingizi na magonjwa ya ndani limefikia maamuzi hayo baada ya kumhudumia Dkt. Kigwangalla toka tarehe 12/08/2018 alipohamishiwa katika taasisi hiyo kwa ajili ya matibabu ya kibingwa ya mkono wake wa kushoto baada ya kupata matibabu mengine katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt.Respicious Boniface amemtakia kila kheri Dkt Kigwangalla katika kutekeleza majukumu yake ya kitaifa kwani ni muda muafaka wa kwenda kuwatumikia wananchi.
“Kwa niaba ya jumuiya ya Taasisi ya Mifupa MOI, tunakutakia kila la kheri katika kutekeleza majukumu yako ya ujenzi wa Taifa. Ilikuwa ni  heshima kubwa kuwa nawe hapa kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja... Tunaamini umeridhishwa na huduma zetu na kama kuna mahali umeona mapungufu ni vyema ukatujulisha ili turekebishe” alisema Dkt Boniface. 

Dkt. Boniface amemueleza Dkt. Kigwangalla kwamba kwa kuwa yeye ni daktari itakua rahisi kubaini mabadiliko yoyote ambayo sio ya kawaida na hivyo kushauriana na madaktari wa MOI ili kupata ufumbuzi.
Kwa upande wake Dkt. Kigwangalla ameushukuru uongozi wa Taasisi ya MOI, madaktari na wauguzi ambao wamekuwa wakimhudumia katika kipindi chote alipokuwa wodini.
“Nichukue fursa hii ya kipekee kuwashukuru watoa huduma wote kuanzia pale nilipopata tatizo na hadi kufika MOI, watanzania wote ambao mmekua mkiniombea na kunitembelea hapa hospitali baada ya kupata ajali, namshukuru Mungu afya yangu inaendelea vizuri sasa na nimeruhusiwa kwenda nyumbani” alisema Dkt Kigwangalla.

Dkt. Kigwangalla alipata ajali ya gari tarehe  4/08/2018 na kupata matibabu ya awali mkoni Manyara kabla ya kuhamishiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili na baadae katika Taasisi ya Mifupa MOI.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa MOI Dkt.Respicious Boniface (kushoto) akizungumza jambo na  Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa MOI Dkt.Respicious Boniface (kushoto) wakifurahia jambo na  Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla mara alipokuwa amekwenda kumuaga. Kulia ni Mkuu wa Wod hiyo, Happyness Mligo 
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla akiondoka hospitalini kwa furaha kubwa baada ya kuruhusiwa na madaktari.
 (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) 


MARAIS WASTAAFU WA TANZANIA WAMPONGEZA ALIYEKUWA BALOZI WA MAREKANI NCHINI, CHARLES STITH

RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AMETIMIZA AHADI ALIYOITOA JWTZ KWA AJILI YA UFUGAJI WA SAMAKI MKOANI MARA

0
0
 Katibu wa Rais Ndg. Ngusa Samike akikabidhi fedha kiasi cha shilingi Milioni 40 kwa Mkuu wa kikosi cha 27KJ Luteni Kanali Js Mshashi kilichopo Makoko mkoani Mara. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kutoa fedha hizo Septemba 6,2018 alipokuwa ziara Mkoani humo kw aajili ya kuongeza Vizimba 10 vya kufugia Samaki.Makabidhiano hayo yamefanyika Jijini Dodoma mbele ya Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo Septemba 11,2018.

 Katibu wa Rais Ndg. Ngusa Samike akikabidhi fedha kiasi cha shilingi Milioni 40 kwa Mkuu wa kikosi cha 27KJ Luteni Kanali Js Mshashi kilichopo Makoko mkoani Mara. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kutoa fedha hizo Septemba 6,2018 alipokuwa ziara Mkoani humo kwaajili ya kuongeza Vizimba 10 vya kufugia Samaki.Makabidhiano hayo yamefanyika Jijini Dodoma mbele ya Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo Septemba 11,2018.

Katibu wa Rais Ngusa Samike akiagana na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo mara baada ya kukabidhi fedha kiasi cha shilingi Milioni 40 kwa Mkuu wa kikosi cha 27KJ Luteni Kanali Js Mshashi kilichopo Makoko mkoani Mara. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kutoa fedha hizo Septemba 6,2018 alipokuwa ziara Mkoani humo kwaajili ya kuongeza Vizimba 10 vya kufugia Samaki.Makabidhiano hayo yamefanyika Jijini Dodoma mbele ya Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo Septemba 11,2018.
PICHA NA IKULU.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU TAKWIMU ZA DENI LA SERIKALI KWA BENKI KUU YA TANZANIA

0
0

Benki kuu ya Tanzania (BoT) inakanusha taarifa potofu zinazozosambazwa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii zikidai kuwa Benki Kuu imechapisha noti zenye thamani ya shilingi trilioni 1.5 kwa ajili ya matumizi ya serikali.


Benki Kuu inauarifu Umma kuwa, taarifa hiyo sio sahihi na inalenga kuathiri imani ya Wananchi na wadau wa kimataifa kuhusu uthabiti wa fedha ya Tanzania. Aidha, Benki Kuu inawaasa Wananchi kuwa utoaji wa taarifa potofu kuhusu sekta ya fedha unaweza kuleta athari kubwa kwa mwenendo wa uchumi. Hivyo ni vyema Wananchi wajue yafuatayo kuhusu utoaji wa fedha kwa matumizi ya Serikali:


  • Mapato ya serikali hayawiani moja kwa moja na matumizi yake mwezi-hadi-mwezi. Kuna wakati mapato yanakuwa makubwa mfano miezi ya mwisho wa robo mwaka na wakati mwingine yanakuwa madogo. Kwa sababu ya kupishana kwa mapato na matumizi ya serikali, sheria imeruhusu serikali kuchukua mkopo wa muda mfupi kutoka Benki Kuu ili kuziba pengo pale linapotokea na kurejesha baadaye. Utaratibu huu unatumika duniani pote na hapa Tanzania sheria inairuhusu Serikali kukopa kutoka Benki Kuu kwa vipindi vifupi hadi ukomo wa asilimia 12.5 ya mapato ya ndani ya serikali ya mwaka uliotangulia.


  • Ili kupata picha halisi ya utekelezaji wa bajeti ya serikali na hali ya deni la Taifa, ni vyema kuangalia mwenendo mzima katika kipindi cha miezi kumi na mbili ya mwaka wa fedha husika, badala ya kuangalia mwezi mmoja mmoja, ambapo kuna mabadiliko ya kimsimu. Mtazamo wa mwaka mzima hutoa uhalisia wa mapato na matumizi, na ongezeko la deni lililohitajika kuwezesha utekelezaji wa bajeti ya serikali katika kipindi hicho. Taarifa ya kila mwezi ya uchumi ya Benki Kuu toleo la mwezi Julai inaonesha kwamba mkopo wa muda mfupi (overdraft) wa Benki Kuu kwa serikali uliongezeka kutoka shilingi bilioni 610.0 mwezi Mei 2018 hadi shilingi bilioni 1,937.4 mwezi Juni 2018, sawa na ongezeko la shilingi bilioni 1,327.4. Ongezeko hili halipaswi kuangaliwa kama tukio la mwezi Juni 2018 pekee kwani taarifa hiyohiyo inaonesha kuwa kati ya mwezi Juni 2017 na mwezi Mei 2018 overdraft ya Benki Kuu ya Tanzania kwa serikali ilipungua kwa shilingi bilioni 936.6, kutoka shilingi bilioni 1,546.6 hadi shilingi bilioni 610.0.  Kupungua huku kulichangiwa na mapato ya kawaida ya serikali pamoja na mikopo kutoka nje ya nchi.


  • Aidha, Benki Kuu haijachapisha noti mpya katika kipindi hiki, hata hivyo noti mpya, hazichapishwi kiholela ili kutoa pesa kwa serikali, bali huchapishwa kulingana na taratibu za kisheria. Kwa kawaida utengenezaji wa noti na sarafu huanza baada ya kukamilika kwa mchakato wa usanifu wa michoro, aina ya karatasi itakayotumika, alama za utambulisho wa nchi pamoja na alama za usalama. Na mara baada ya kukamilika kwa mchakato huo, Benki Kuu huandaa kiasi gani kitakachoweza kutosheleza mahitaji ya nchi kwa kipindi maalum kwa kuzingatia ukuaji wa pato la Taifa, Mfumuko wa bei na pia kufidia fedha zilizochakaa ambazo hazipaswi kurudi katika mzunguko na kiasi kilichobaki (buffer stock) ili kutosheleza kipindi chote cha mchakato wa uchapishaji.
Benki kuu inawaasa Wananchi kutotoa taarifa zisizo za kweli zenye lengo la kuupotosha Umma na kusababisha hofu na kupoteza imani juu ya uthabiti wa fedha ya Tanzania na badala yake wawe wanaomba kupewa taarifa kutoka Taasisi husika.


BENKI KUU YA TANZANIA


Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki

11 Septemba, 2018

ARUSHA UNITED YAPANIA KUPANGA LIGI KUU MSIMU UJAO

0
0
 Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MKIRUGENZI Mtendaji wa timu ya Arusha United Saad Kawemba amesema kuwa kwa sasa kikosi chao kipo tayari kwa ajili ya kuanza ligi daraja la kwanza baada ya kucheza michezo kadhaa ya kirafiki.

Akizungumzia maandalizi ya kikosi chao lkilichorejea jana kutokea mkoa wa Lindi, Kawemba amesema walikuwa wamepanga kuweka maandalizi ya kikosi chao katika mikoa 2 ambayo ni Dar es Salaam na Tanga na kucheza mechi za kirafiki ila wakabahatika na kuongeza mkoa mwingine ambao ni Lindi.

Kawemba amesema kuwa, wameweza kucheza mechi sita za kirafiki na katika michezo hiyo walifanikiwa kushinda michezo miwili na kutoa sare moja na mitatu wakipoteza.

Amesema kuwa, walianza mechi ya kwanza ya kirafiki na Simba ambapo walipoteza mchezo huo, walicheza pia na Coastal Union ya Tanga na mechi zingine wakicheza Lindi na Dar es Salaam na mchezo mwingine watacheza alhamisi dhidi ya Namungo ya Arusha.

Kawemba amewataka wana Arusha kuwa na imani na timu kwani wana uhakika wa kuoanda ligi kuu msimu ujao kutokana na kikosi kuwa kizuri na ushindani, akielezea kuwa kupoteza mechi yoyote katika mchezo wa kirafiki sio kama wana timu isiyo ya ushindani bali mwalimu anakuwa anaangalia makosa yaliyopo ili aweze kuyafanyia kazi kabla ya kuanza kwa ligi.

"Tumecheza michezo sita ya kirafiki na Alhamisi tutacheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya Namungo na mechi hizo zimekuwa na mchango mkubwa sana katika kikosi chetu kwani zimeweza kumsaidia Mwalimu kuona makosa yaliyopo kabla ya kuanza kwa ligi na kupoteza mechi ya kirafiki haimaanishi kuwa kikosi ni kibaya ila tuna imani na timu yetu mwakani itashiriki ligi kuu Tanzania bara,"amesema Kawemba.

Akizungumzia udhamini wa timu yao, Kawemba amewataka wadau mbalimbali wanaopendelea soka na wasio wajitokeze kuidhamini timu hiyo kwani kwa sasa kwani itakapopanda ligi kuu msimu ujao thamani yao itapanda zaidi.

Arusha United iliyo chini ya kocha Fred Felix Minziro akiwa na historia ya kuzipandisha timu za ligi daraja la kwanza katika kipindi mitatu uongozi wa timu hiyo umekuwa na imani kuwa msimu ujao kuwa timu yao itaingia Ligi Kuu.Minziro amefanikisjha timu ya Singida United, KMC kupanda ligi kuu katika misimu miwili tofauti.


MkuruenziMtendaji wa timu ya Arusha United Saad Kawemba.

FARU WA SERENGETI KULINDWA KWA VIFAA MAALUMU

0
0

Na Woinde Shizza Globu ya jamii Arusha.

Vita dhidi ya ujangili wa Faru, imeendelea kushika kasi na sasa Faru wa serengeti,wataanza kulindwa na vifaa maalum vya kielekroniki katika mradi ambao utagharimu zaidi ya 2.5 bilioni

Mradi huo,unafadiliwa na shirika la uhifadhi za Friedkin conservation Fund(FCF) kwa kushirikiana na shirika la Frunkfurt zoological society na kusimamiwa na shirika la hifadhi za taifa nchini(TANAPA) na taasisi ya utafiti wa wanyamapori(TAWIRI).Mratibu wa Mradi wa uhifadhi wa Faru katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Philbert Ngoti alisema, vifaa hivyo ambavyo vitawezesha Faru wa Serengeti kuwa salama zaidi.

Alisema Faru wa Serengeti wanafungwa vifaa vya aina mbili,vya kielekroniki VHF transmitter ambacho kinawezesha kuwafatilia walipo kila siku na pia wanafungwa katika mguu wa kulia kifaa cha kisasa cha LoRa collar ambacho pia kinafatilia na kuonesha mienendo yao kila siku.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Japhet Hasunga, alisema zoezi la ufungwaji wa vifaa ya utambuzi na usalama kwa Faru ni muhimu sa katika kuimarisha vita dhidi ya ujangili.

Alisema zoezi hilo pia litasaidia kuongeza ufatiliaji wa faru,wanyama ambao wapo hatarini kutoweka duniani na sasa kila siku watajulikana wapo wapi, wanakula nini, wanaumwa ama wanamatatizo na hivyo kuchukuliwa hatua.
Meneja miradi wa shirika la Frunkfurt Tanzania, Rian Habuschagne, alisema katika mradi huo ambao ni mara ya kwanza kufanyika nchini, pia kumejengwa minara ya mawiliano katika maeneo yote ya mapito ya Faru.

Alisema zoezi la kufungwa vifaa hivyo linasimamiwa na watafiti na wahifadhi maarufu wa Faru barani Afrika, wakiongozwa na Pete Morkel na wanatarajia Faru wote wa serengeti kufungwa vifaa hivyo."hili zoezi linagharama kubwa tunawashukuru Friedkin Conservation Fund kwa msaada mkubwa wa fedha na helkopta, pia Frunkfurt ,TANAPA na taasisi ya utafiti wa wanyamapori(TAWIRI)"alisema.HIfadhi ya Taifa ya Serengeti ni moja ya maeneo yenye Faru wengi kwa sasa hapa nchini kutokana na kuimarishwa ulinzi

Picha naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Japhet Hasunga akiwa anashikiri zoezi la kuwafunga Faru wa serengeti vifaa vya ulinzi na mawasikiano
 
  Faru wa serengeti wakianza kulindwa na vifaa maalum vya kielekroniki katika mradi ambao utagharimu zaidi ya 2.5 bilioni 

WAMBURA AWAONYA WAAMUZI, LIGI KUENDELEA WIKIENDI HII

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

LIGI kuu Tanzania Bara inatarajia kuendelea tena mapema wikiendi hii kwa timu zote 20 kuanza kukamilisha  mzunguko wa nne  wa ligi huku timu za Simba, Yanga na Azam ratiba zao za zikitafutiwa ratiba nyingine.

Akizungumzia ratiba ya ligi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi  Boniface Wambura amesema mzunguko wa nne wa ligi utaanza wikiendi hii baada ya kumalizika kwa ratiba ya michezo ya kimataifa ya kirafiki ya FIFA iliyochezwa tarehe 3 hadi 11 Septembe.

Amesema kutokana na kalenda ya FIFA, kuna baadhi ya mechi za Simba, Yanga na Azam zuki zilizoondolewa kwa ajili ya kupisha ratiba hiyo na wao kuwa na mechi pungufu baada ya  wachezaji wao kwenda katika timu za taifa na kupelekea kuhairisha mechi zao.

Wambura amesema kuwa, kwa timu zilizokuwa hazijakilimisha mzunguko wa pili na wa tatu watapangiwa tarehe ya kucheza mechi zao kwani kwa sasa kutakuwa na ligi ndefu ,mechi nyingi 380 na hiyo ni  kutokana na timu kuwa nyingi."timu ambazo hazijafanikiwa kufikisha idadi ya mzunguko wa mechi zao na watapangiwa ratiba ili kucheza mechi hizo, ila kwa sasa ligi itakuwa ndefu na itahitaji umakini mkubwa kutokana na timu kuwa nyigi,"amesema Wambura.

Akizungumzia kuhusu waamuzi wa ligi kuu kutokuwa makini katika maamuzi yao uwanjani, Wambura amesema kuwa waamuzi waliofanya makosa katia mzunguko wa kwanz ana wa pili tayari wameshawachukulia hatua na kuwataka waamuzi wengine kuchezesha mpira wa kutumia kanuni 17 za mpira.Wambura amesema, waamuzi wanatakiwa waangalie mechi zao zilizopita pamoja na kufanya mazoezi kwa sana na hii inatokana na idadi ya mechi na msimu huu watakuwa wamepata mechi nyingi za kuchezesha.

Amesisitiza kwa sasa wana waamuzi makini wakiwa wanasimamiwa vizuri na kamati ya waamuzi na hawatasita kwuachukulia hatua wale ambao watashindwa kuchezesha kwa sheria 17 za soka.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi  Boniface 

QUEEN MLOZI AWAOMBA WAPIGA KURA KUCHAGUA VIONGOZI WATAKAOWALETEA MAENDELEO

0
0
Pichani kulia Katibu Mkuu UWT ,Queen Mlozi akimuombea  kura Mgombea wa Udiwani kwa tiketi ya ccm katika kata ya kizota mkoani Dodoma ndugu Jamal Paul. Katika Kampeni hizo Ndugu Mlozi amewaomba wakazi wa kata hiyo kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi wakati wa kupiga kura na kumchagua kiongozi  atakae wafaa na kuwaletea maendeleo ya kweli na si maneno matupu.
katibu Mkuu Uwt Queen Mlozi akiagana na Mbunge wa Dodoma Mjini Mh Antony Mavunde mara baada ya Mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani kwa tiketi ya  chama cha Mapinduzi (CCM) katika kata ya kizota,uliofanyika jana.

Dk Mengi ataka watanzania kujiamini ujasiriamali

0
0
Na Mwandishi Wetu
Wajasiriamali nchini wametakiwa kujiamini kuwa wanaweza kuletea maendeleo kwa kugundua na kutumia ipasavyo fursa za uwekezaji zilizopo nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi kwenye mazungumzo na wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, waliomwalika awasimulie uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga.
Amesema Watanzania hawana budi wajiamini kuwa kwa jitihada zao wanaweza kujikwamua kiuchumi kwa kuwekeza kwenye fursa anuwai  zilizopo nchini, wakati huu ambapo Rais John Magufuli anahamasisha uwekezaji, hususan  wa viwanda, baada ya kuboresha mazingira ya uwekezaji.
Alisema hilo linawezekana kwa kujifunza kusema kwamba nitaweza na lazima na kisha kutekeleza uthubutu huo kivitendo.
Alisema kwamba yeye akiwa anatoka katika familia maskini aliweza kufanikisha kuwa mfanyabiashara mkubwa kutokana na dhamira yake ya kusema nitaweza na kutekeleza msemo huo kwa vitendo.
Aidha alisema aliandika kitabu hicho kama alivyoshauriwa na mtoto wake Rodney ili kuwashawishi watanzania wengi zaidi kuwa na uthubutu na ushauri katika kujikita kwenye ujasiriamali na kutumia fursa.
Aidha aliwataka watanzania kujifunza na kuwa wabunifu na watunga sera kuona kama elimu yetu ya sasa inakidhi mahitaji halisi au inatakiwa kuboreshwa ili kusaidia katika harakati za kuipeleka nchi yetu kwenye uchumi wa kati.
Alisema hayo wakati akijibu maswali katika mdahalo huo kuhusu elimu na kama elimu yetu inafaa kwa sasa.
 Alisema kitabu alichotunga kinaelezea uzoefu wake katika ujasiriamali kutokana na ukweli kuwa hata wakati wa kuanzisha IPP ni kuwezesha ubunifu na teknolojia miongoni mwa watanzania.
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi akizungumza na wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, waliomwalika awasimulie uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral Beach, Masaki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Mafunzo wa Asasi ya EO tawi la Tanzania, Bi. Miranda Naiman.
 Mmoja wa wajasiriamali hao ambao ni wamiliki wa makampuni  mbalimbali nchini akiuliza swali kwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo na wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, waliomwalika awasimulie uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral Beach, Masaki jijini Dar es Salaam.
 Wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, wakimsikiliza Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi (hayupo pichani) alipokuwa akiwasimulia uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral Beach, Masaki jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi akitia saini nakala za kitabu chake ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’ zilizonunuliwa na wajasiriamali hao ambao ni wamiliki wa makampuni  mbalimbali nchini mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika hoteli ya Coral Beach-Masaki, jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi katika picha ya pamoja na wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania huku wakiwa wameshika nakala za kitabu chake ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’ mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika hoteli ya Coral Beach-Masaki, jijini Dar es Salaam.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DC GODFREY CHONGOLO ASEMA KIPAUMBELE CHAKE NAMBA MOJA WILAYANI KINONDONI NI MAPATO

0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
MKUU  wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam Godfrey Chongolo amesema kipaumbele chake namba moja,mbili na tatu ni mapato.

Amesema ili halmashauri  ifanye mambo yake vizuri ni lazima iwe na mapato ambayo yatasaidia katika kufanikisha mambo mbalimbali yakiwamo ya kutatua changamoto zilizopo wilayani Kinondoni.

Chongolo amezengumza hayo leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu ateuliwe na Rais Dk.John Magufuli kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Awali Wilaya hiyo alikuwa Ali Hapi ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa.Chongolo kabla ya kuhamishiwa Kinondoni alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido.

"Kwangu mimi kipaumbele changu namba moja ni mapato,kipaumbele changu namba mbili ni mapato na kipaumbele changu namba tatu ni mapato.

" Kwanini? Ni kwasababu ukiwa na mapato unaweza kufanya mambo mengi yakiwamo ya kutatua changamoto zilizopo.

"Kwa mfano kuna malalamiko ya kuwepo kwa makelele mengi kutoka kwenye mabaa lakini ukiwa na fedha itakuwa rahisi wanaohusika na mazingira wakaenda kukagua na kuchukua hatua," amesema Chongolo.

Ametoa maelezo hayo leo wakati anajibu swali aliloulizwa na mtangazaji Baby Kabaye wa Clouds Tv ambaye alitaka kujua mikakati ya Chongolo katika eneo la mapato.

Hivyo amesema unahitaji msuli wa kimapato ili kutatua changamoto,ukiwa na kipato ni rahisi kuwajengea uwezo watumishi kufika kwenye maeneo yenye changoto na kuzitatua kwa wakati.

Amesema inafahamika Wilaya ya Kinondoni huko nyuma ilikuwa inasifika kimapato na anao uhakika mapato yataongezeka kutokana na mikakati ambayo wameiweka.

Amefafanua wao wanaangalia mapato kama sehemu ya kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi na kusisitiza miongoni mwa huduma hizo ni pamoja na kuimarisha ulinzi wa wananchi na mali zao.

Akifafanua kuhusu ulinzia anasema amepata nafasi ya kuzungumza na Kamanda wa Polisi Kinondoni na moja ya mipango iliyopo ni kuhakikisha inatengenezwa mifumo ya kuimarisha ulinzi.

Amesema kuwa anatambua changamoto ya uhalifu katika Wilaya hiyo ambapo alielezea huko nyuma namna ambavyo kulikuwa na uhalifu ukiwamo wa wizi wa vifaa vya magari.

"Katika eneo la ulinzi hatutakuwa na msamaha kwa atakayebainika kujihusisha na uhalifu.

"Atachukuliwa hatua na kwa mamlaka niliyonayo mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama.

"Hivyo tumejipanga kuhakikisha kunakuwa na usalama wa kutosha kwa wananchi," amesema Chongolo.

Kwa kukumbusha tu Rais Magufuli katika moja eneo ambalo alipata nafasi ya kuzungumzia ni kuhusu mapato na hiyo ni baada ya Wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika mapato.

Mastercard partner with Vodacom to take Tanzania cashless

0
0
Anyone who has been able to buy something without getting out of their chair can attest to the convenience and simplicity of shopping online. Unfortunately, that has been a distant dream for most Tanzanians – until now. Mastercard has partnered with market leader Vodacom and BancABC to introduce the first online card in Tanzania – the M-Pesa virtual card.

“Vodacom’s M-Pesa is already an industry trailblazer with over 8.2 million subscribers and over 100,000 agents countrywide that enable citizens to transact safely and easily, but customers are limited when it comes to making online payments on international websites. The introduction of this functionality through the M-Pesa virtual card will revolutionize how people transact by removing the barrier of having bank accounts and risk of putting bank details online,” says Hisham Hendi, Vodacom Tanzania PLC’s Acting Managing Director.

Africa's mobile internet connections are expected to grow rapidly due to affordable smartphones and high-speed networks being rolled out by Mobile Network Operators like Vodacom.  This surge in internet connections will create a demand for digital content, social media, m-commerce and even online education and a need to make payments easily and securely.

The virtual card will allow M-Pesa mobile wallet holders to make payments on any local or international website or app so long as Mastercard is accepted for payment without the need for a bank account or credit card.  Customers can request the virtual card from the M-Pesa USSD menu or soon on the M-Pesa app and top the card up via the wallet. Once the card is topped up with funds, the virtual card is ready for use.  

“The continued roll out of innovative technology solutions in the e-commerce space represents an opportunity for greater financial inclusion and means that more people will be able to make payments, without the inconvenience of cash. With 60 percent of these transactions happening on mobile platforms, the future of financial inclusion undoubtedly lies in the mobile device that most of us carry around with us,” says Raghav Prasad, Division President Sub Saharan Africa, Mastercard.

Simple and secure online payments have been proven to improve access to financial services, widely allowing more people to become part of the financial mainstream. Tanzania has made great strides in financially including its citizens in the past decade: the percentage of Tanzanians forming part of the economy sat at only 15.8 percent in 2009 but that number jumped to 65.3 percent in 2017, driven largely by the introduction of easily accessible mobile wallet solutions like M-Pesa.

Collaboration between industry leaders in payments, technology and financial services means life-changing solutions can be developed and rolled out rapidly to make a tangible difference in the lives of Tanzanians by allowing them to buy and pay for goods and services more easily than ever before.

ULAJI USIOFAA UNAONGEZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA-MAJALIWA

0
0
 WAZIRI MKUUKassim Majaliwa amesemalishe duni pamoja na ulaji usiofaa na mitindo ya maisha vinachangia kwa kiasi kikubwa katika ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza hususan kwa vijana na watu wazima, ambao ndiyo nguvu kazi kwa Taifa.

“Ni jambo lisilopingika kuwa hatua za kukabiliana na magonjwa ya kusendeka (mfano matatizo ya moyo, saratani, kisukari na shinikizo kubwa la damu) zinachangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza kasi ya maendeleo yetu kwani gharama za matibabu yake ni kubwa mno; si kwa kaya zinazoathirika tu bali kwa Taifa zima.”

Waziri Mkuu  ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Septemba 11, 2018),  wakati akifungua mkutano wa tano wa wadau wa masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kambarage, Hazina jijini Dodoma. 

Waziri Mkuu amesema lishe iliyozidi inadhihirishwa na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukizwa yanayotokana na mabadiliko ya mitindo ya maisha na ulaji usiofaa kama vile uzito uliozidi, viriba tumbo, shinikizo la damu pamoja na kisukari.

Amesema kasi ya ongezeko la magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza inapaswa kudhibitiwa kwa kuzingatia ulaji unaofaa na mtindo bora wa maisha. “Huu ni wakati wa kuangalia kwa pamoja kama jitihada zetu zinaleta matunda tunayotarajia.”

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya Taifa letu hivyo, uwepo wao katika mkutano huo unaonesha umuhimu wa kuimarisha ushiriki wa kila sekta, kila mdau ikiwemo sekta binafsi kwa nafasi yake katika kupambana na aina zote za utapiamlo. 

Amesema ushiriki wa kila sekta ni wa muhimu kwa sababu hakuna sekta moja pekee inayoweza kuondoa tatizo la utapiamlo, pia ni vema kwa wadau hao wakajitathmini mmoja mmoja katika sekta zao kuona kama wanaelekea katika muelekeo sawa na mipango ya Serikali.

“Kwa kuzingatia hilo, ofisi yangu imeweka utaratibu maalum wa kuratibu utekelezaji wa kazi za lishe nchini, ambapo kamati ya Kitaifa ya Usimamizi na Ushauri kuhusu masula ya lishe nchini yaani High Level Steering Committee on Nutrition imeundwa ili kusimamia utekelezaji wa azma hiyo.” 

Waziri Mkuu amesema kwamba watu wote wanatambua jitihada kubwa zilizowekwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau katika kupambana na matatizo ya lishe nchini, ambapo taarifa za wataalamu zinasema kuwa kwa sasa nchi inakabiliwa na aina mbili za utapiamlo yaani lishe duni na lishe iliyozidi au iliyokithiri. 

Amesema walengwa wakubwa wa lishe duni ni pamoja na watoto chini ya miaka mitano, wanawake walio katika umri wa kuzaa hususani wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na vijana balehe (hususan wa kike). “Hii ni kwa sababu mahitaji ya virutubishi kwa ajili ya miili yao ni makubwa, ukilinganisha na ule unaohitajika na makundi mengine.” 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, SEPTEMBA 11, 2018.

VIDEO: INTRODUCING RAWBEENA_KIDOGO (KENYA)


MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 12, 2018

OFISA MTENDAJI MKUU DAWASA MHANDISI LUHEMEJA AANZA KAZI KWA KISHINDO

0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
OFISA Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja ametembelea mradi wa maji wa Chalinze ili kujionea maendeleo ya mradi na kupanga utaratibu wa kuongeza kasi ya ujenzi.
Ametembelea mradi huo ikiwa ni siku yake ya nne tangu kutangazwa rasmi  Septemba  8 mwaka,  amefanya maamuzi ya kuongeza nguvu katika usimamizi na kutaka mkandarasi wa  Kampuni ya OIA ya India kutekeleza kazi usiku na mchana ili kuleta matokeo yanayotarajiwa.
Akizungumzia mradi huo Mhandisi  Luhemeja amesema mradi utazinduliwa Desemba mwaka 2018. 

Leo pia anaendelea na ziara katika miradi ya usambazaji maji.

TAWA yawakamata,wapokonya baiskeli 60, Nyaya 100 za majangiri

0
0
NA RIPOTA WETU,KILOMBERO
MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika kipindi cha mwaka 2017/18 imekamata baiskeli 60 za watuhumiwa wa ujangiri zikiwamo Nyaya zaidi ya 100 ndani ya Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi- Msolwa.

Mkuu wa Kanda hiyo, Augustine Ngimilanga alisema pamoja na kukamata nyenzo hizo askari wa doria pia walikamata watuhumiwa wa ujangiri waliofunguliwa kesi 92 zinazoendelea Mahakama ya wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.

“Watuhumiwa 18 wameshasomewa kesi zao na kuhukumiwa baadhi wamefungwa miaka mitatu na wengine miaka tisa jela,” alisema Ngimilanga na kuongeza:

“Tumeweka mkakati wa kuhakikisha maeneo yote yanakuwa na ulinzi wa doria muda wote, hii ni pamoja na kukabiliana nao kabla hawajaingia na kufanya uharibifu,” alisema.

 Mofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi -Msolwa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi na Kijiji cha Msolwa Station Kilombero mkoani Morogoro mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Ukombozi kujionea mchango wa uhifadhi kutoka kampuni za uwindaji wa kitalii. 
 Afisa Habari na Mawasiliano wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA),Twaha Twaibu kushoto akiwa na Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Magharibi-Msolwa Pori la Akiba Selous Augustine Ngimilanga wakiangalia baiskeli zilizotumiwa na majangiri kubebea wanyamapori.
 Mofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), katika Pori la Akiba Selous Kanda ya Kaskazini Magharibi -Msolwa wakiwa katika picha ya  na viongozi na Kijiji cha Msolwa Station Kilombero mkoani Morogoro baada ya kutembelea jengo la Ofisi ya Kijiji cha Msolwa Station linalojengwa kwa fedha kutoka kampuni za uwindaji wa kitalii. 



Serikali Haijavunja Mkataba wa Wanufaika wa Mikopo ya Elimu ya Juu - Prof. Ndalichako.

0
0
Na Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Serikali imesema haijavunja mkataba wowote na wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu bali makato ya asilimia 15 kutoka kwenye mshahara ghafi wa mnufaika wa mkopo huo ni ya kisheria.

Hayo yameelezwa leo Bungeni, Jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Mhe. Paschal Yohana Haonga juu ya kinachodaiwa kuwa Serikali imevunja mkataba kinyume na makubaliano kwa kuwa wakopaji walisaini mkataba wa asilimia 8 na siyo 15.

"Kilichofanyika mwaka 2016 katika marekebisho ya Sheria ya Bodi ya Mikopo (SURA 178) ni kuiboresha sheria hii kwa kutaja kiwango mahsusi cha asilimia 15 kinachopaswa kukatwa kutoka mshahara ghafi wa mnufaika. Awali, kabla ya marekebisho hayo, kifungu cha 7(1) (h), kiliipa Serikali mamlaka ya kupanga kiwango cha makato na kubadilisha kiwango pale itakapoona inafaa," alifafanua Prof. Ndalichako.

Ameendelea kusema kuwa, Serikali inafahamu umuhimu wa kuwashirikisha wadau katika marekebisho ya sheria yoyote. Hivyo basi, katika mchakato wa marekebisho ya Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (SURA 178) ya mwaka 2016, wadau mbalimbali walishirikishwa.

Amewataja wadau walioshirikishwa kuwa ni pamoja na wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi (TUGHE na TUCTA), Chama cha Mawakili nchini (TLS) pamoja na wanafunzi kutoka Taasisi za Elimu ya Juu kama vile Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Elimu ya Biashara - Dodoma (CBE) na Chuo cha Mipango (IDRP).

Aidha amesema, makato hayo ya asilimia 15 yana lengo la kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali zinarejeshwa kwa wakati iliziweze kuwasomesha Watanzania wengine wahitaji. Hivyo, kwa sasa Serikali haina mpango wa kusitisha makato hayo.

Prof. Ndalichako ametoa wito kwa wanufaika wote wa mikopo ya Elimu ya Juu kuhakikisha kuwa wanarejesha kwa wakati mikopo waliyokopeshwa na Bodi hiyo ili iweze kusaidia watoto wengine wenye uhitaji.
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof Joyce Ndalichako akijibu maswali mbalimbali ya wabunge leo Bungeni Jijini Dodoma.

AZAM WATUA KANDA YA ZIWA, KUCHEZA MECHI TATU UGENINI

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

KIKOSI cha Azam FC,kimefika salama  mkoani Shinyanga tayari kabisa kwa mchezo wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) dhidi ya Mwadui utakaofanyika Uwanja wa Mwadui Complex keshokutwa Ijumaa saa 8.00 mchana.


Azam FC imewasili ikiwa na kikosi chake kamili isipokuwa kiungo mshambuliaji, Tafadzwa Kutinyu, atayeungana na timu muda wowote kaunzia sasa akitokea kwenye majukumu ya timu ya timu yake ya Taifa Zimbabwe.

Wachezaji wengine wa Azam FC ambao hawajaungana na timu ni mshambuliaji Wazir Junior pamoja na beki Yakubu Mohammed na Donald Ngoma, ambao wanaendelea na programu ya kujiweka fiti kabla ya kuanza kucheza mechi za ushindani wakitoka kwenye majeraha huku Joseph Kimwaga, akiwa majeruhi.


"Wachezaji wote wameshaungana na timu isipokuwa Tafadzwa Kutinyu ambaye ataungana na wenzake muda wowote atakuja na ndege hadi Dar es Salaam halafu ataunganisha mpaka Mwanza na baadae kuja kuungana na wenzie hapa Shinyanga,"amesema Iddy.

Iddy amesema kuwa, baada ya mchezo huo bado wana mechi zingine mbili katika kanda ya Ziwa wakicheza na Biashara ya Mara na kuja kumalizia na Alliance kabla ya kurejea Dar es Salaam.


Mara baada ya kuwasili, kikosi hicho kinatarajia kufanya mazoezi leo Jumatano jioni kwenye Uwanja wa Kambarage mjini hapa kabla ya kesho Alhamisi kujifua tena katika Uwanja wa Mwadui itakaochezea mchezo huo, unaotarajia kuwa mkali na wa aina yake.


Azam FC  inashika nafasi ya pili kwenye ligi ikiwa na pointi sita ikishinda mechi mbili za awali ilizocheza, ikizidiwa pointi moja na Mbao inayoongoza kileleni ikiwa na pointi saba lakini ikicheza mechi moja zaidi.
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live




Latest Images