Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA SHEREHE ZA KUSIMIKWA KWA ASKOFU MKUU MSAIDIZI WA KANISA LA PENTEKOSTE MOTOMOTO MJINI KIGOMA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inatambua mchango wa madhehebu ya dini katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Makamu wa Rais ameyasema haya leo wakati wa sherehe za kusimikwa wakfu wa Askofu Mkuu Msaidizi pamoja na Maaskofu wane wa majimbo wa Kanisa la Pentekoste Motomoto, Mwanga mkoani Kigoma.

“Serikali imeweka mazingira rafiki kwa madhehebu ya dini nchini kuweza kutoa huduma za kijamii hususan elimu na afya” alisema Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa kanisa kujiepusha na migogoro ya kiutawala ndani ya Kanisa na pia liepuke kuchanganya dini na siasa,

“Kazi kubwa ya Kanisa iwe kuhubiri Amani kwa waumini wake na wananchi kwa jumla” alisema Makamu wa Rais huku akinukuu neno la Mungu katika Waebrania 12:14, ambalo linasema “tafuteni kwa bidii kuwa na Amani na watu wote”.

Aidha, Eneo jingine ambalo Serikali inalitegemea Kanisa ni katika kujenga maadaili mema ya jamii, hivyo Makamu wa Rais alilitaka Kanisa kusaidiana na Serikali katika kupiga vita tamaduni mbaya za nje ili kujenga Taifa lenye maadili ya Kitanzania, pia Serikali inalitegemea Kanisa katika kupiga vita rushwa na ufisadi ambavyo ni adui wa maendeleo ya nchi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Kanisa la Pentekoste Motomoto Jimbo la Tanganyika tayari kwa sherehe ya kusimikwa kwa Askofu Mkuu Msaidizi pamoja na Maaskofu wa Majimbo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa sherehe ya kusimikwa kwa Askofu Mkuu Msaidizi pamoja na Maaskofu wa Majimbo wa Kanisa la Pentekoste Motomoto ,Mwanga mkoani Kigoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Askofu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Motomoto Baba Askofu Ezra Enock Mtamya (kushoto), Askofu Mkuu Msaidizi Bwani J. Mathias na Maaskofu wengine wa Majimbo mara baada ya sherehe ya kusimikwa kwa Askofu Mkuu Msaidizi na Maaskofu wa Majimbo kumalizika katika Kanisa la Pentekoste Motomoto Jimbo Kuu la Tanganyika Mwanga mkoani Kigoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mmoja wa waumini wa Kanisa la Pentekoste Motomoto Jimbo la Tanganyika mara baada ya kumalizika sherehe ya kusimikwa kwa Askofu Mkuu Msaidizi pamoja na Maaskofu wa Majimbo.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS MAGUFULI AHUTUBIA WANANCHI WA MEATU MKOANI SIMIYU

$
0
0
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa  Meatu mjini mkoani Simiyu mara baada ya kuwasili wakati akitokea Bariadi.
 Sehemu ya Wananchi wa Meatu wakifatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipokuwa akizungumza  katika viwanja vya Meatu mjini.
 Ngoma ya kichungaji ya Budimi ya Meatu ikitoa burudani mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwasili Meatu mjini mkoani Simiyu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Meatu mjini kwa ajili ya kuhutubia katika mkutano wa hadhara. PICHA NA IKULU

AZAM TV HIGHLIGHTS: SIMBA FC 4-2 AFC LEOPARDS (FRIENDLY MATCH - 08/09/2018)

Maestro Dekula Guitar Lesson/ Song Makumbele

INTRODUCING "MPAKA NAOGOPA" by Z ANTO

Destination KENYA - A Travel, Education & Conservative Story by Zuriel Oduwole

$
0
0
Following the release of her first series of a new project, telling Africa's stories about great destinations on the continent aimed at the US & European youth and family market, young film maker Zuriel Oduwole, has completed her second episode on Nairobi, after the Pilot edition on Johannesburg. She believes there are 'cool', simpler, and more kid friendly ways to talk about difficult yet pressing issues, in a childlike manner that adults would still enjoy, while taking in the scenery of the great African continent.

Tanzanian Hassan Mwakinyo destroys Briton Sam Eggington in 2nd round TKO

$
0
0
In a shocking upset, little known 23-year-old Tanzanian Hassan Mwakinyo (12-2, 8 KOs) destroyed Sam Eggington (23-5, 15 KOs) in a 2nd round knockout on Saturday night in a scheduled 10 round fight on the undercard of Amir Khan vs. Samuel Vargas on Sky Sports and DAZN at the Arena Birmingham in Birmingham, England. 
 Mwakinyo hurt the 24-year-old Eggington in round two, and then flurried on him with nonstop punches to the head until the referee Kevin Parker was forced to step in and stop the contest. The official time of the stoppage was at 1:02 of round two. 
 Mwakinyo was brought in as a replacement opponent on a couple of weeks’ notice or the 5’11” Eggington to fight. This was supposed to have an easy fight for Eggington, but he was hurt at the end of the 1st round and he never really recovered from the shot. 
Mwakinyo continued to tee off on the defenseless Eggington in the 2nd round. He was hitting Eggington at will with punches, and he wasn’t even trying to block the shots. Eggington was just taking the punches with his chin and he looked like he was hoping Mwakinyo would get tired from hitting him. 
That didn’t turn out to be the case unfortunately. If promoter Eddie Hearn of Matchroom Boxing needs an opponent for Kell Brook, then Mwakinyo would be a good option if he can’t make the Amir Khan vs. Brook fight for December. For Eggington, it might be time for him to consider retiring from boxing. 

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 10, 2018


MKUU WA WILAYA YA TEMEKE AUNGANA NA BENKI YA KCB KUFANYA USAFI MBAGALA ZAKHIEM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
 MKUU wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva akishirikiana na wafanyakazi wa Benki wa KCB pamoja na   wafanyabiashara wa eneo la Mbagala Zakhiem wamefanya  usafi kwa pamoja katika eneo hilo ikiwa ni kuweka mazingira safi na salama.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaniva ameiomba Benki ya KCB  kutoa huduma nzuri na bora kwa wakazi wa Mbagala, na ikiwezekana kuwapa punguzo la riba na masharti nafuu katika mikopo ili kuweza kupata wateja wengi zaidi.


Ameyasema hayo mapema wakati akifungua zoezi la usafi katika wilaya hiyo lililofanywa na benki ya KCB maeneo ya Mbagala Zakhiem, na kuwaomba watoe mikopo ya riba nafuu katika eneo hilo kwa kuwa lina wafanyabiashara wengi na wadogo wakiwa wanahitaji kupewa nguvu ili waweze kufikia malengo yao.



Lyaniva ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, aliipongeza Benki ya KCB kwa juhudi na kufanikisha kuwaleta wadau mbali mbali pamoja na wananchi wa Mbagala kushiriki katika kufanya usafi. “Mlichokifanikisha leo si kidogo na ninawapongeza lakini pia iwe chachu ya kutaka kufanya zaidi katika jamii yenu, ni mfano mzuri wa kuigwa hata na makampui mengine.” aliongeza DC Lyaniva.

Aliendelea kusema kuwa anafurahia kuona wawekezaji wengi wanaendelea kuwekeza katika wilaya ya Temeke kwani anategemea ubora wa huduma kwa wananchi wake, lakini pia watamsaidia katika shughuli nyingi za kijamii ikiwemo kujenga Madarasa, Zahanati na hata huduma za usafi katika maeneo hayo kwani ndio malengo ya serikali ya awamu ya tano.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva  akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya KCB Zuhura Muro(kulia)  wakifanya usafi na pamoja kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama Mbagala Zakhiem Jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa  Benki ya KCB, wafanyabiashara wadogo wadogo, kampuni ya Green Waste wakiendelea na usafi Mbagala Zakhiem kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama.
Picha ya Pamoja

HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI YAOKOA TZS 3.96 BILIONI NDANI YA MIEZI 10

$
0
0
Mkuu wa Idara ya  huduma za tiba radiolojia (Interventional Radiology) Dkt. Frolence Lwakatare (katikati) akiongea na wanahabari wakati akielezea jinsi huduma hiyo ilivyo muhimu kwa jamii ambalo amesema kuwa inapunguza hatari kwa mgonjwa maana upasuaji huwa unahatarisha maisha ya mgonjwa. Kulia ni Joan mmoja ya wagonjwa walipatiwa matibabu na Kushoto ni Daktari Bingwa wa Meno, Kimywa na Uso, Dkt. William Siang'a.
Mkurugenzi wa wa huduma za Tiba Shirikishi Dkt. Praxeda Agweyo (katikati) akiongea na wanahabari kuelezea huduma mpya walioyoianzisha tokea Novemba 2017 inahusisha utalaam wa kutumia vifaa vya radiolojia kama X-Ray, MRI, CT-Scan na Ultra-Sound kutibu moja kwa moja ugonjwa au kuchukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi.  Kulia ni Joan mmoja ya wagonjwa waliopatiwa matibabu na (kushoto) ni Mkuu wa Idara ya  huduma za tiba radiolojia (Interventional Radiology) Dkt. Frolence Lwakatare. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Daktari Bingwa wa Meno, Kimywa na Uso, Dkt. William Siang'a akieleza machache.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
*Wagonjwa 45 wahudumiwa, wagharimu Tshs. 360 Mil. badala ya Tshs. 4.320 Bil kama wangeenda nje ya nchi

*Mmoja agharimu Tshs. 8 Mil. badala ya Tshs. 96 Mil. nje ya nchi

Hospitali ya Taifa Muhimbili imeanzisha kwa mara ya kwanza hapa nchini utoaji wa huduma za tiba radiolojia (Interventional Radiology) ambapo kabla ya uanzishwaji wake wagonjwa waliokuwa wanahitaji huduma hizi walikuwa wakienda nje ya nchi.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam wakati akielezea kuanzishwa wa huduma hiyo, Mkurugenzi wa wa huduma za Tiba Shirikishi Dkt. Praxeda Agweyo amesema kuwa tiba hiyo inahusisha utalaam wa kutumia vifaa vya radiolojia kama X-Ray, MRI, CT-Scan na Ultra-Sound kutibu moja kwa moja ugonjwa au kuchukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi.

Amesema kuwa huduma ambazo zimeanza kutolewa kupitia njia hiyo kwa sasa ni kuondoa uvimbe kwenye sehemu ya kinywa, uso na shingoni (sclerotherapy for haemangioma and lymphangioma), kuweka mirija kwenye figo ambazo mirija ya kutoa mkojo imeziba (nephrostomy tube placement), kuzibua mirija ya nyongo iliyoziba (percutaneous trans hepatic biliary drainage) na kuzibua mirija ya uzazi iliyoziba (fallopian tube recanalization). Tiba nyingine ni kunyonya usaha ndani ya tumbo (abscesses drainage).

Mikocheni veterans ndani ya michezo ujirani mwema Rwanda

$
0
0
Kikosi cha Timu ya Mikocheni Vrterans.
Na Mwandishi Wetu.
TIMU ya Mikocheni veterans itashiriki tamasha maalum ya ujirani mwema lililopangwa kufanyika Kigali, Rwanda kuanzia Septemba 22.

Timu hiyo inatarajia kuandoka nchini Septemba 19, ikiwa na wachezaji na mashabiki 23 kwa ajili ya safari hiyo kwa mujibu wa Seneta wa timu hiyo, Yassin Ally Yassin.

Yassin alisema kuwa mechi ya kwanza itakuwa dhidi ya Karibu Sports Club ya Rwanda Septemba 24 na mechi nyingine zitafuatia.

Aliwataja wachezaji wanaondoka kuwa ni Adam Mohamed Mselem, Fumu Mahamud, Dornad Mtoka, winchande Chambuso, Ally Salim, Adnan Juma, Omary Mkuku, Jumanne Mnkumbu na Hamis Kisukari.

Wengine ni Agapiti Manday, Fikir Muhango, Belanus Komba, Eric Frederic , Ian Balegele, Timothy Kipilimba, Abdul Hamis Said, Suleima Masatu, Nassoro Abdul Mwinchui, Hassan Mbegu Mohamed, Neema Visent Msema na Witness David Mbingi.

Viongozi ambao wataambatana na timu hiyo ni Chriss Chale ambaye ni Mweka Hazina, Adam Mselem (Seneta) na Aidan Mshani ambaye ni kocha. Alisema kuwa wamejiandaa vilivyo na wanatarajia kucheza mechi kadhaa za kirafiki ili kujiandaa na tamasha hilo.

“Mpaka sasa tumejiandaa vilivyo na maandalizi ya safari yetu yanakwenda vizuri, morali ya wachezaji ipo juu na tunatarajia kupata ushindi huko Rwanda,” alisema Yassin.

Alisema kuwa mbali ya kushiriki tamasha la Rwanda, pia timu yao ina mipango ya kushiriki katika matamasha mengine ya nchi za ukanda wa Afrika Mashariki ili kujifunza mambo mbalimbali na kudumisha ushirikiano na wadau wa soka.

VIGOMA VYA KEKO FURNITURE NA GOMS UNITED KUANZA IJUMAA

$
0
0
VIGOMA VYA KEKO FURNITURE NA GOMS UNITED KUANZA IJUMAA KWENYE KUPIMA UZITO PALE SOKO LA VETENAL LILIOPO TAZARA KUKUTANA KATIKA MASUMBWI SEPTEMBA 15 TAIFA.

Na Mwandishi Wetu 
Haidari Mchanjo Katika ali isiyokuwa ya kawaida kwa mashabiki wa michezo baada ya kucheza mashindano ya mpira wa miguu yajulikanayo kama Ndondo Cup sasa timu za Goms United na Keko Furniture zinakutana katika masumbwi ambapo Goms united inawakilishwa na bondia Haidari Mchanjo na Keko Furniture anatoka Fred Sayuni 
mashabiki wa mabondia hawo wamepanga kuanza shangwe zao siku ya ijumaa wakati wa kupima uzito kwenye soko la vetenal lililopo maeneo ya Tazara Dar es Salaam kuanzia saa nne na watacheza jumamosi katika uwanja wa ndani wa Taifa 'Indoor Stadium'

Mabondia pamoja na kambi zao watapima uzito ijumaa na watacheza siku ya jumamosi ambapo kwa sasa yameshafanyikamaandalizi ya kutosha kwa mabondia wote kilichobaki ni mpambano tu kufanyika

Akizungumzia pambano hilo mratibu wa mapambano ya ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' kutoka kampuni ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion amesema kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali ya ngumi wakati Abdallah Pazi 'Dula Mbabe' atazipiga na Geoger Dimoso na Vicent Mbilinyi atavaana na Saidi Mpoma 'Kidedea' wakati Mohamedi Kashinde atakumbana na Sadiki Momba na Imani Daudi ataoneshana umwamba na Paul Kamata.

Na mpambano mwingine utawakutanisha Faraji Sayuni na Issa Nampepeche Ramadhani Shauri atakumbana na Said Amani wakati Mwinyi Mzengela atakumbana na Kassimu Rajabu 'Boxer Mnyama' Saidi Zungu na Tonny Rashidi Super D aliongeza kwa kusema kuwa mapambano hayo yote yataanza kuanzia saa 12 jioni ili zimalizike kwa wakati

mapambano hayo yameandaliwa na kampuni ya ngumi za kulipwa ya Super D Boxing Promotion inayoendelea kuinuwa vipaji vya mabondia mbalimbali nchini ili kujikuzia kipato na kujiweka nafasi nzuri kwa mabondia kucheza kila wakati

Watuhumiwa wa mauaji ya mwanaharakati wa ujangili wa meno ya Tembo wafikia 17

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii
WATUHUMIWA wa mauaji ya Mwanaharakati wa kupambana na mauaji ya Tembo sasa wamefikia 17 baada ya leo Septemba 10.2018 mshtakiwa mwingine raia wa Burundi kusomewa mashtaka yake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. 

Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Hamisi Ali , mshtakiwa  Habonimana Nyandwi  raia wa Burundi ameunganishwa leo na kusomewa mashtaka mawili ya kula njama ya  kufanya mauaji na mauaji ya Mkurugenzi na Mwanzilis hi-Mwenza wa Shirika lisilo la kiserikali la Palms Foundation, Wayne Lotter (52).

Washtakiwa wengine ambao walishasomewa mashtaka yao ni raia wa Burundi, Nduimana Jonas maarufu Mchungaji (40) mkazi wa Kamenge Burundi, Godfrey Salamba (42) mkazi wa Kinondoni Msisiri A. Inocent Kimaro (23) mkazi wa Temeke Mikoroshini, Chambie Ally (32) mkazi wa Kia/Boma na Ofisa wa NBC, Robert Mwaipyana (31) mkazi wa Temeke Mikoroshini. Meneja wa Benki ya Backlays, Khalid Mwinyi (33) mkazi wa Mikocheni B, Rahma Almas (37) mkazi wa Mbagala B na Mohammed Maganga (61) mchimba makaburi.
 Wengine ni, Allan Mafue, Ismail Mohammed, Leornad Makoye, Amino Sham, Ayoub Selemani, Joseph Lukoa, Gaudence Matemu na Abuu Mkingie,

Washtakiwa wote hao wanakabiliwa na mashtaka mawili ambapo katika shtaka la kwanza wanadaiwa kuwa kati ya Julai Mosi na Agosti 16, 2017 walikula njama ya kufanya mauaji ya Lotter.

Katika shtaka la pili, washtakiwa hao wanadaiwa Agosti 16, 2017 katika makutano ya barabara za Chole na Haile Selasie Kinondoni Dar es Salaam walimuua Lotter.

Washtakiwa wote wako rumande  kwa kuwa kesi ya mauaji inayowakabili haina dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 17.2017 kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wake bado haujakamilika.

GESI BADO INA NAFASI KUBWA KATIKA KUCHANGIA PATO LA TAIFA – NAIBU WAZIRI

$
0
0
         Na Veronica Simba – Dodoma
NAIBU Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, amesema kuwa gesi asilia inayopatikana nchini, ingali na nafasi kubwa ya kuchangia katika Pato la Taifa, tofauti na hofu ya baadhi ya watu kuwa Serikali haiipi tena kipaumbele sekta hiyo.

Alitoa kauli hiyo jana, Septemba 9, 2018 jijini Dodoma, wakati akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, walizoziwasilisha katika semina maalum iliyoandaliwa na Wizara kuhusu masuala ya umeme, mafuta na gesi asilia.

Awali, wakitoa maoni na hoja mbalimbali wakati wa semina hiyo, baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo, walionyesha wasiwasi wao kuwa Serikali hailipi tena kipaumbele suala la gesi asilia kama ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita.

“Serikali haijabadili msimamo na mtazamo wake kuhusu gesi asilia hata kidogo. Ndiyo maana Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limepewa dhamana ya kufanya kazi kibiashara ambapo pamoja na mambo mengine, linashughulika na biashara ya gesi ili kukuza mchango wake katika Pato la Taifa,” alifafanua Naibu Waziri.

Akifafanua zaidi, alisema kwamba, miradi mbalimbali ya gesi asilia inaendelea hivi sasa ambayo ni pamoja na uunganishaji wa gesi katika kiwanda cha saruji cha Dangote, katika viwanda vikubwa vilivyopo Mkuranga pamoja na kuunganisha majumbani.
 Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, akizungumza wakati wa Semina ya Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini (hawapo pichani), kuhusu masuala ya umeme, mafuta pamoja na gesi. Semina hiyo ya siku mbili iliandaliwa na Wizara ya Nishati ambapo ilihitimishwa jana, Septemba 9, 2018 jijini Dodoma.
Meza Kuu – Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. Hamisi Mwinyimvua, Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Dustan Kitandula na Kaimu Katibu wa Kamati Agnes Nkwera, wakiwa katika Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati kwa Wajumbe wa Kamati hiyo (hawapo pichani), kuhusu masuala ya umeme, mafuta pamoja na gesi. Semina hiyo ya siku mbili ilihitimishwa jana, Septemba 9, 2018 jijini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakichangia hoja na kutoa maoni wakati wa Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati kwa Wajumbe wa Kamati hiyo kuhusu masuala ya umeme, mafuta pamoja na gesi. Semina hiyo ya siku mbili ilihitimishwa jana, Septemba 9, 2018 jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wa Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati kuhusu masuala ya umeme, mafuta pamoja na gesi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiwemo Wabunge, Viongozi na Maafisa waandamizi kutoka Serikalini, wakiwa katika Semina hiyo ya siku mbili ambayo ilihitimishwa jana, Septemba 9, 2018 jijini Dodoma.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.                                                                        

Naibu Waziri Ndiye aagiza Mabasi kuanza kusafiri saa 11 katika Kituo cha Ubungo

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Ndiye ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) pamoja na Jeshi la Polisi Nchini kuratibu safari za mikoani kuanzia Dar Salaam kuondoka saa 11.

Ndiye ameyasema hayo  leo wakati alipofanya ziara katika kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo majira ya saa 10 kuangalia hali ya Usafiri pamoja na changamoto za abiria wanaotumia usafiri wa Mabasi ya Mikoani.

Amesema kuwa Sumatra na Polisi kuratibu kuanza safari saa 11.
Aidha amesema kuwa safari za Dar es Salaam kwenda Dodoma na Dodoma Kwenda Dar es Salaam kwenda masaa 24.

Amesema maagizo hayo yatekelezwe ndani ya wiki mbili ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bora ya usafiri kwa Mabasi ya Mikoani.

Amesema kuanza kufanya safari saa 24 Dodoma ni kutaka wananchi kufanya kazi pamoja kuongeza uzalishaji.

Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra Gilliard Ngewe amesema maagizo ya Naibu Waziri ni utekelezaji tu  hakuna maelezo juu ya maagizo hayo.
Amesema usafiri wamejipanga kudhibiti usafiri kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Ndiye akizungumza katika kituo cha Mabasi Ubungo wakati alipofanya ziara majira ya Saa 11alfajili
Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra , Gilliard Ngewe akizungumza akizungumza kuhusiana na Udhibiti wa Usafiri wa Mabasi ya Mikoani
Pics mbalimbali za matukio katika kituo cha Ubungo

THTU yakutana kujadili masilahi ya wanachama

$
0
0


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
BARAZA la Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu Juu (THTU) limesema kuwa litaendelea kuwa na busara katika kufatilia madai yao kwa kufuata taratibu za Kiutumishi.

Baraza hilo lilikutana kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya stahiki zao katika vyuo vya umma nchini.

 Mwenyekiti wa  Taifa wa chama cha wafanyakazi Taasisi ya elimu ya juu (THTU) Dkt. Paul Loisulie akizungumza katika baraza hilo amesema kuwa serikali kuna vitu imefanya vizuri lakini vingine bado vinavyohusiana na madai hivyo busara lazima itumike.

Amesema kuwa kuna Mamlaka za serikali ambazo zipo kwa ajili yao ambazo zinatakiwa kuzifikia katika kupata ufumbuzi.

Dkt. Loisulie amesema kikao cha baraza ni cha dharula kwa wanachama kuwa na dukuduku kuhusiana  madai yao katika utumishi wa umma.
Aidha liosure ameeleza kwakina dhumuni la kikao hicho ni kutoa muelekeo juu ya maslahi ya wafanyakazi kwani wengi wao wamekua wakilalamikia masilahi ya malimbikizo ya mishahara ikiwa baadhi yao walishalipwa katika awamu zilizopita.

Dkt. Loisulie amesema madai hayo yalishapelekwa kwa sehemu husika na swala hilo litapelekwa pamoja na wataandaa walaka wa matatizo ya watumishi ili waweze kushughulikiwa. 

Mwenyekiti huyo amefafanua kuhusu sheria zilizojadiliwa ni pamoja na sheria ya bodi ya mikopo na wameona ipo haja ya  kupendekeza sheria na kanuni hizo kwa serikali ili kuboresha kanuni na sheria hizo kwa lengo la kuleta nafuu kwa watumishi.
 Mwenyekiti wa chama cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu (THTU) Dkt.John Loisulie  akizungumza katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Chama hicho kuhusiana na madai mbalimbali ya masilahi ya Wafanyakazi wa taasisi ya Elimu ya Juu.

Viongozi wa THTU wakiwasikiliza wajumbe wa baraza hawapo pichani
Picha mbalimbali wajumbe wa baraza hilo.

WAZIRI MKUU AREJEA DODOMA

$
0
0


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma akitoka Dar es salaam Septemba 10, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge (kulia) na Mkuu wa wilaya ya Dodoma Patrabas Kitambi wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma akitoka Dar es salaam, Septemba 10, 2018. 
(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

JUMAA ATOA MISAADA KATIKA SEKTA YA ELIMU MAGINDU NA MUUNGANO

$
0
0
 Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa (kushoto )akimkabidhi mabati Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Magindu, Kasule Ambogo (mwenye kofia )
 Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa (kushoto )akimkabidhi mabati Diwani wa kata ya Kilangalanga Mwajuma Denge.
Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa (kulia)akimkabidhi jezi za michezo ,Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Mlandizi Kati ,Ally Nyambwilo. (Picha na Mwamvua Mwinyi)

NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA VIJIJINI
MBUNGE wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Mkoani Pwani ,Hamoud Jumaa ametoa mabati 60 kwa ajili ya kuezeka darasa moja chakavu katika shule ya msingi Magindu .

Aidha amekabidhi sh. mil.mbili ambayo imenunuliwa bati 56 zitakazotumika kuezeka darasa jingine moja kati ya madarasa manne chakavu kimiundombinu yaliyopo shuleni hapo .

Pamoja na hayo ,Jumaa amechangia matofali 1,000 na mifuko ya saruji 100 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati katika kata ya Boko ,kijiji cha Mpiji .

Akikabidhi mabati hayo ,kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Magindu ,Kasule Ambogo ,mbunge huyo alisema ,anatekeleza ahadi alizozitoa na kushirikiana na serikali ya awamu ya tano katika kuboresha na kutatua changamoto za sekta ya elimu .

Hata hivyo ,alikabidhi mabati mengine 25 yanayokwenda kutumika kuezeka ofisi ya walimu shule ya msingi Muungano kata ya Kilangalanga .

"Pia tumefanya harambee kwa ajili ya ujenzi wa zahanati katika kata ya Boko ,kijiji cha Mpiji ,ambapo tumepata sh.milioni 7 ,tofali 5,274 ,kokoto gari tatu, mchanga gari moja na mawe gari saba" alifafanua Jumaa.

Jumaa alisema kuwa ,ataendelea kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo hasa kwa kutatua changamoto na kero za jumla ili kuinua maendeleo ya jimbo hilo .

Kwa mujibu wake ,kufuatia harakati hizo amewahi kutoa kontena la vitabu mbalimbali vya kujifunzia 40,000 ambavyo viligawanywa katika shule za msingi na sekondari za jimbo zima .

Akipokea mabati ,Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Magindu ,Ambogo alishukuru na kumuomba Jumaa kutochoka kusaidia changamoto zinazowakabili .

Ambogo alisema ,kwasasa wanategemea shida waliyokuwa wakiipata wanafunzi inaenda kuwa historia .

Nae diwani wa kata ya Kilangalanga ,Mwajuma Denge alisema haijawahi kutokea Mbunge wa kuwashika mkono kwa namna hiyo .

Alishukuru msaada wa mabati 25 yatakayotumika katika ofisi ya walimu shule ya msingi Muungano kata ya Kilangalanga na sh .mil moja kwa ajili ya kumalizia ofisi hiyo.

WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUTUMIA MAWAKALA WALIOTHIBITISHWA NA TRA KUPATA KARATASI ZA RISITI

$
0
0
SERIKALI imetatua tatizo la kuwepo kwa karatasi za risiti  zinazofutika maandishi zinazotolewa na Mashine za Kielektroniki za kutolea Risiti (EFDs)  kwa kuwataka wafanyabiashara wote kununua karatasi hizo kwa mawakala waliothibitishwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Tanga Mjini Mhe. Mussa Bakari Mbarouk, aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu risiti zinazotolewa na Mashine za EFDs kufutika maandishi kwa muda mfupi na muda ambao utatolewa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kurekebisha hali hiyo.
Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali inatambua kuwa kuna karatasi feki, lakini tatizo la kufutika kwa risiti halihitaji kutoa muda kwa TRA wa kufanya marekebisho kwa kuwa Serikali ililifanyia kazi, hivyo ni jukumu la wafanyabiashara kufuata maelekezo ya ununuzi wa karatasi hizo kwa wakala waliothibitishwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Naibu Waziri Kijaji, akijibu maswali ya  Msingi ya Mbunge huyo aliyetaka kujua bei halisi za Mashine ya EFDs na kwa nini Serikali isitoe Mashine hizo bure kwa wafanyabiashara, alisema kuwa kuna aina tano za Mashine ambazo mfanyabiashara anaweza kununua kulingana na mahitaji yake.
“Mashine za EFDs ni kama Rejista za kielektroniki za kodi (ETR) ambayo bei yake ni Sh. 590,000 na hutumiwa na wafanyabiashara wasiotumia mifumo ya Kompyuta na kihasibu na Mashine za kielektroniki zinazoweka alama/saini(Electronic Signature Devices) ambazo hutumiwa na walipa kodi wanaotumia mifumo ya kompyuta na kihasibu, bei yake ikiwa ni kati ya Sh. 1,000,000 hadi 1,200,000”, alieleza Dkt. Kijaji.
Alisema kuwa Mashine nyingine ni Printa za kielektroniki za kodi (Electronic fiscal printers) ambazo hutumia mfumo maalum wa kompyuta, bei yake ikiwa ni kati ya Sh. 1,500,000 hadi Sh. 1,700,000, pia zipo mashine ya Printa za Pampu za Mafuta ya Petroli au Dizel (EFPP) ambazo hutumiwa na wafanyabiashara wa mafuta, bei yake ikiwa ni Sh. 6,000,000 ikijumuisha gharama za ufungaji na uunganishwaji kwenye pampu za mafuta.
Aidha kuna Mashine ya Printa za Maduka ya kubadilisha Fedha za Kigeni, bei ya mashine hizo ni Sh. 2,150,000 ikiwa ni pamoja na program ya mfumo wa software.
“Ubora wa Mashine hizo ni lazima uthibitishwe na Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA kabla mashine hizo hazijaingizwa sokoni na kuanza kutumika”, alifafanua Dkt. Kijaji.
Dkt. Kijaji alisema kuwa wafanyabiashara wasiosajiliwa kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) wanaponunua mashine za EFDs hulipa gharama za ununuzi wa mashine hizo na baadae Serikali hurejesha gharama kwa kumruhusu mlipakodi kujirejeshea fedha zake kwa utaratibu wa Input- Output tax kwenye mauzo ya mwezi husika.
Vilevile kwa wafanyabiashara wasiosajiliwa kwenye VAT na wanaoandaa hesabu za mizania, hujirejeshea gharama za ununuzi wa mashine kwa kuingiza gharama husika kama gharama za kuendesha biashara kwa mujibu wa sheria ya Kodi ya Mapato.
Naibu Waziri huyo amebainisha kuwa, kwa wafanyabiashara wasioandaa hesabu za mizania wanajirejeshea gharama za mashine kwenye kiasi cha kodi walichokadiriwa kwa mwaka husika na iwapo hawatakuwa wamejirejeshea kwa asilimia miamoja, kiasi kilichobakia kitasogezwa mwaka unaofuata.
Imetolewa na ;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb).

Serikali Imetoa Kibali cha Ajira 15,000 Kuziba Pengo la Walioghushi Vyeti

$
0
0
NaLilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.
SERIKALI imetoa kibali cha kuajiri watumishi wapya 15,000 ili kuziba pengo lililosababishwa na kuondolewa kwenye orodha ya malipo ya mishahara watumishi wa Umma waliobainika kughushi vyeti.

Hayo yameelezwa leo Bunge, Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Capt. (Msataafu) George Mkuchika alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Aida Khenani kuhusu mkakati wa Serikali wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokumbwa na sakata la vyeti feki.

"Vibali vya kuajiri watumishi hao vimetolewa katika ngazi ya Wizara, Idara zinazojitegemea, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waajiri wote wameendelea kujaza nafasi hizo, " alisema Mhe. Mkuchika.

Vilevile, amesema Serikali imetoa vibali vya ajira kwa Mamlaka zote za Serikali za Mitaa Kumb. Na. CFC.26/205/01/PF/91 cha tarehe 22 Agosti, 2017 na kibali Kumb. Na CFC.26/205/01/GG/95 cha tarehe 12 Machi, 2018 kuziba nafasi zote za Watendaji wa Vijiji na Mtaa zilizoachwa wazi kutokana na zoezi la kuhakikiwa vyeti kwa kuajiriwa watumishi wapya.

Aidha, amesema katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa kutambua umuhimu kwa kuajiri watumishi wa kada mbalimbali Serikali imetoa vibali vya kuajiri watumishi 22, 150 wakiwemo watumishi wa kada za Ualimu 6,840, Fundi Sanifu wa Maabara za shule 160, kada za Afya 8,000, Wahadhiri wa Vyuo Vikuu 624 na watumishi 6,526 wa kada nyingine.
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live


Latest Images