Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110029 articles
Browse latest View live

NI AIBU VIWANJA VYA NDEGE KUKOSA HATI - NAIBU WAZIRI NDITIYE


HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA KUTOKA NEW YORK, MAREKANI

VOA SWAHILI: Duniani leo August 30, 2018

KUMBILAMOTO AENDELEA NA MIKUTANO YA KAMPENI KATIKA KATA YA VINGUNGUTI

$
0
0
 Mgombea Udiwani wa Kata ya Vingunguti Kupitia Chama cha Mapinduzi , Omary Kumbilamoto akizungumza  na Wakazi wa Mtaa wa Butiama Vinguti wakati wa Mkutano wake wa Kampeni ya kuomba ridhaa kwa Wananchi wamchague kuwa Diwani wa kata hiyo.
 Mgombea Udiwani wa Kata ya Vingunguti Kupitia Chama cha Mapinduzi , Omary Kumbilamoto  akiwa amebebwa juu juu na Mkada wa Chama Chake wakati akiwa anawasili kwenye uwanja wa Butiama Vingunguti .


 Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam akimwaga sera na jinsi Ilani ya CCM inavyotekelezwa katika Serikali hii ya awamu ya tano
 Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakichea kwa pamoja mtindo wa Mduara wakati wa mkutano wa Kampeni za Udiwani kata ya Vingunguti
Wakazi wa Mtaa wa Butiama waliohudhuria Mkutanowa wa kampeni za udiwani za Omary Kumbilamoto

DK SHEIN ATEMBELEA KITUO CHA UTAFITI MIFUGO LANGONI

$
0
0

Na Faki Mjaka, Maelezo Zanzibar 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amesema azma ya serikali anayoiongoza ni kuhakikisha kuwa tafiti za Mifugo na Afya zinafanyika Zanzibar badala ya kufanyika nje ya Zanzibar.
Amesema kuundwa kwa Taasisi za kitafiti na kujengewa uwezo Taasisi hizo ni hatua muhimu itakayo chochea kasi ya maendeleo na kupunguza gharama.
Rais Shein ameyasema hayo alipofanya ziara katika eneo la Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Dole Wilaya ya Magharibi A na eneo la Binguni ambapo Hospital ya Rufaa itakayojumuisha Taasisi ya Utafiti ya Afya inajengwa.
Akiwa katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Dkt Shein ameridhishwa na maendeleo ya Taasisi hiyo ikiwemo ukarabati wa majengo mbalimbali na shughuli za kitafiti zinazoendelea katika Taasisi hiyo.
Dkt Shein alijionea Tafiti zinazoendelea katika Taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na ufugaji wa kuku wa Kienyeji na chakula cha Samaki.
Aidha ameahidi kuendeleza mashirikiano yake kwa Taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kusaidia kuiwezesha kifedha ili kukidhi bajeti ya Taasisi hiyo.
Akiwa Binguni Dkt. Shein aliweza kukagua mipaka ya eneo ambalo Hospital ya kisasa ya Rufaa inatarajiwa kujengwa.
Amezitaka Taasisi zinazohusika na eneo hilo kuhakikisha wanafanya marekebisho ya upimaji wa eneo hilo ili kurahisisha ujenzi wa Hosptiali hiyo.
Ujenzi huo ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambapo Dkt Shein aliahidi kuijenga Hosptal hiyo katika mikutano ya kujinadi kuchaguliwa.
Akielezea kwa undani Dktk Shein amesema Tayari Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeshaomba Fedha za Mkopo na kwamba kila kitu kimeenda sawa hivyo ujenzi unaweza kuanza mara tu fedha zitakapopatikana.
Dkt Shein amewataka Wananchi kujitolea kwa hali na mali ili kufanikisha ujenzi huo pale utakapo anza.
Katika Ujenzi huo kutakuwa na Hospital ya Rufaa na Taasisi ya Utafiti wa Afya na nyumba za Wafanyakazi.
Awali akitoa Salamu za Kichama Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dkt Abdallah Sadala amempongeza Dkt Shein kwa kuendelea kuitekeleza vyema Ilani ya CCM kama alivyoahidi kwa wananchi na hivyo kuomba wananchi waendelee kumuunga Mkono.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiangalia mwani katika eneo la Taasisi ya  Utafiti wa Mifugo Zanzibar, Dole Wilaya ya Maghribi "A" Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo wakati alipotembelea akiwa katika ziara maalum
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya angalia mwani katika eneo la Taasisi ya  Utafiti wa Mifugo  Dkt.Kassim Gharib (wa pili kulia)  wakati alipotembelea katika eneo la Taasisi hiyo iliyopo   Dole Wilaya ya Maghribi "A" Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo wakati alipotembelea akiwa katika ziara maalum
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akimuuliza suala Mtafiti wa Magonjwa na Uzalishaji Mifugo Dkt.Waridi Abdulla Mussa (kulis) alipokuwa akipata maelezo kutoka kwa Mtafiti huyo alifikas kuasngaslias kuku wa asili (kienyeji) akiwa katika ziara ya kutembelea  katika eneo la Taasisi ya  Utafiti wa Mifugo  Dole Wilaya ya Maghribi "A" Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akiuliza suala kwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi Ahmed Abrahmani Rashid (kulia) alipofika kutembelea Eneo la ujenzi wa Hospitali kubwa ya Rufaa inayotarajiwa kujengwa Binguni  Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja  leo akiwa katika ziara maalum,(katikati) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Hassan Khatibu Hassan
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Hassan Khatibu Hassan(kushoto) alipotembelea Eneo la ujenzi wa Hospitali kubwa ya Rufaa  inayotarajiwa kujengwa Binguni Katika  Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo (kulia) Mhe.Haji Omar Kheir Kaimu Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idare malum za SMZ Mhe.Haji Omar Kheri. 
Picha na IKULU. 

INTRODUCING "Washa" by TID & CASSIM MGANGA

Introducing: Sampamba - Vyeo (Official Music Video)

BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA 31.08.2018


VOA SWAHILI: Aretha Franklin, malkia wa Soul, azikwa mijini Detroit hii leo

VOA SWAHILI: Duniani Leo August 31, 2018

HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA KUTOKA NEW YORK, MAREKANI, LEO

Vitabu Nilivyonunua Nairobi

$
0
0
Na Profesa Joseph Mbele

Nilisafiri tarehe 15 Julai mwaka huu kutoka Marekani kwenda Tanzania. Nilishukia Nairobi, kwa shughuli binafsi, ikiwemo kununua vitabu vya ki-Swahili. Kitabu nilichotamani zaidi ni Sauti ya Dhiki cha Abdilatif Abdalla ambacho nilitaka kukisoma kwa makini kuliko nilivyowahi kufanya kabla. Ninawazia pia kutafsiri kwa ki-Ingereza baadhi ya mashairi.

Nilivyoingia tu katika duka la vitabu la Textbbook Center, Kijabe Street, nilikitafuta kitabu cha Sauti ya Dhiki. Nilikiona, kikiwa na jalada tofauti na lile la mwaka 1973. Nilinunua pia Kichwamaji, Kaptula la Marx, na Dhifa, vya Euphrace Kezilahabi; Mashetani, tamthilia ya Ebrahim Hussein, na Haini, cha Adam Shafi.
Tangu zamani, nimekuwa na baadhi ya vitabu vya Kezilahabi, Ebrahim Hussein, na Adam Shafi. Ninafurahi kujipatia vile ambavyo sikuwa navyo. Hata hivi, nimegundua kuwa sasa nina nakala mbili za Mashetani na mbili za Kichwamaji. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala atembelea maonesho ya jeshi la zimamoto na uokoaji jijini Dodoma

$
0
0
Maadhimisho ya Juma la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Maonesho ya wadau wa jeshi hilo yamefungwa leo Dodoma, ambapo msisitizo ulikuwa ni kwa watanzania kushiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa kufunga ving'amuamoto viwandani.
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akisindikizwa na Maafisa mbalimbali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwenda kutembelea mabanda ya wadau wakati wa maazimisho ya Juma la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji yalifanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, akioneshwa kifaa mahsusi kiitwacho "king'amua moto" kitumikacho kugundua moto ukiwa hatua za awali na kuwezesha kukabiliwa kwa urahisi  wakati akitembelea mabanda ya wadau wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwenye maonesho yaliyoandaliwa sambamba na maazimisho ya Juma la Jeshi hilo yalifanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akipata maelezo ya namna ya utoaji wa huduma mbalimbali  za kiuhamiaji mbalimbali toka kwa Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji, Alice Mhoja wakati akitembelea mabanda ya wadau wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwenye maonesho yaliyoandaliwa sambamba na maazimisho ya Juma la Jeshi hilo yalifanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
 Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakionesha namna ya kuokoa mtu aliyenaswa katika jengo refu.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akipata maelezo ya namna ya kutumia zana mbalimbali  zinazotumika kuzima mioto ya aina tofauti toka kwa Luteni Kalalawina wakati akitembelea mabanda ya wadau wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwenye maonesho yaliyoandaliwa sambamba na maazimisho ya Juma la Jeshi hilo yalifanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

SOMA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 1,2018

MAKAMU WA RAIS AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI JIJINI DODOMA LEO TAREHE 31 AGOSTI 2018

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri , kushoto ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa TAMISEMI, Mkapa House leo jijini Dodoma.
Kikao kikiendelea
Kikao kikiendelea
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Mwaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma.

(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA AMBULANCE MALI YA JWTZ KUPATA AJALI - RPC WANKYO

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa akitolea ufafanuzi tukio la ajali iliyohusisha gari la kubebea wagonjwa(ambulance), Mali ya JWTZ na gari aina ya Toyota canter yenye namba za usajili T.764 ACK ,huko eneo la Kibiki, Bwilingu Chalinze Mkoani Pwani.(picha na Mwamvua Mwinyi).

NA MWAMVUA MWINYI, PWANI

ELINIKUNDA Mushi (50), amefariki dunia baada ya gari la kubebea wagonjwa (ambulance) mali ya jeshi la wananchi wa Tanzania  (JWTZ) , lililokuwa likimuwahisha hospital ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu kupata ajali eneo la Kibiki, kata ya Bwilingu, Chalinze mkoani Pwani. Katika ajali hiyo watu wengine wanne walijeruhiwa baada ya dereva wa ambulance kudaiwa kuligonga gari nyingine kwa nyuma, lililokuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara kwa ajili ya matengenezo .

Akitoa taarifa kuhusu tukio hilo, kamanda wa polisi mkoani Pwani, (ACP) Wankyo Nyigesa ,alisema ajali hiyo imetokea alfajiri agost 31 mwaka huu. Alieleza, gari namba 3489 JW 12 aina ya Ashok Leyland inayomilikiwa na kikosi cha jeshi 911 KJ cha Ihumwa Dodoma, mali ya JWTZ, lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Dar es salaam aliligonga gari lingine lenye namba za usajili T. 764 ACK aina ya Toyota canter na kusababisha kifo cha mtu mmoja .

Nyigesa alisema, aliyepoteza maisha ni Elinikunda ambae alikuwa mgonjwa akipelekwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi. 

"Watu wanne walijeruhiwa ambao ni pamoja na Beatrice Shidodolo (56) muuguzi wa hospital ya  Dodoma, Ufo Swai (48) mkazi wa Ngerengere yeye alikuwa akimhudumia mgonjwa akiwa Dodoma "alisema Nyigesa. 

Nyigesa aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Justine Patrick (28) ambae alikuwa dereva wa gari namba T. 764 ACK iliyokuwa imeegeshwa kwa matengenezo na Rashid Rais (35) alikuwa fundi wa gari hilo wakazi wa Chalinze. 

Uchunguzi wa awali umebaini katika ambulance hiyo ilikuwa imepakia watu wengine wanne ambao hawakuweza kupata majeraha yoyote ambao ni MT. 3480 SGT Elimasa Mushi (40) askari wa JWTZ makao makuu ya Jeshi. 

Nyigesa aliwataja wengine kuwa ni MT 95881 PTE Taulin Kaira (30) askari wa  911 KJ aliyekuwa msindikizaji wa gari hilo la wagonjwa, Eveline Stanley (25) alipewa msaada wa usafiri na mtoto wake wa miezi 11 anaitwa Nicholous Petro na dereva wa gari hilo MT. 67451 SGT Shaban Mpwate. 

Kamanda huyo alifafanua, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya Jeshi ya Lugalo na majeruhi wamepelekwa katika hospital hiyo. Dereva wa ambulance Shaban Mpwate,anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi. 

Nyigesa aliwaasa madereva wa magari ya dharura kama magari ya wagonjwa kuhakikisha wanachukua tahadhari kubwa wanapokuwa wamepewa kipaombele na watumiaji wengine wa barabara ili kuweza kuepuka ajali zembe. 

SERIKALI KUTOTOA KAZI YA UJENZI WA BARABARA KWA MKANDARASI ASIYEKUWA NA UWEZO WA KIFEDHA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Mara, Mhandisi Mlima Ngaile, wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51, Wilayani Bunda, mkoani humo.

Serikali imeeleza kuwa haitatoa kazi za ujenzi wa miundombinu ya barabara hapa nchini kwa kampuni za ujenzi ambazo hazina uwezo wa kifedha wa kufanya kazi hizo. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Kamwelwe, amesema hayo Wilayani Bunda, Mkoani Mara mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 na kubaini kuwa kampuni ya ujenzi ya Nyanza Road Works kuwa na uwezo mdogo wa kifedha na hivyo kuchelewesha mradi huo.

Mhandisi Kamwelwe ameeleza changamoto nyingine iliyochelewesha mradi ni kutokana na kampuni ya Inter Consult iliyofanya usanifu wa barabara kukosea michoro ya mradi huo na hivyo kumsababishia mkandarasi kushindwa kufanya kazi yake kikamilifu.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, (kulia) akifafanua jambo kwa Meneja wa mradi Mhandisi Antener Mehari, wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51, Wilayani Bunda, Mkoani Mara.

"Aliyesanifu mradi huu hakufanya vizuri na hivyo kumsababishia mkandarasi kuongezewa muda wa kazi miezi 35 mingine kutokana na kuongezeka kwa makalvati katika barabara hiyo na ukubwa wa tuta la barabara", alifafanua Waziri Mhandisi Kamwelwe.

Waziri huyo amemtaka Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya DOCH na Mkandarasi kuongeza vifaa na wataalam wengine ili kuhakikisha kasi ya mradi huo inaenda kwa haraka. Aidha, Mhandisi Kamwelwe, ameiagiza Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Mara kumsimamia mkandarasi huyo ili akamilishe mradi huo ifikapo mwezi Juni mwakani badala ya mwezi Desemba 2019.

Kwa upande wake Meneja wa TANROADS, mkoa wa Mara Mhandisi Mlima Ngaile, amemuahidi Waziri Kamwelwe kuwa atamsimamia mkandarasi huyo kikamilifu na kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa viwango.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, (kushoto) akizungumza na Mhandisi Andrew Nantori, kutoka kampuni ya M/S Mbutu JV anayejenga barabara ya Makutano-Sanzate yenye urefu wa KM 50 baada ya kukagua barabara hiyo na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wake, mkoani Mara.

Katika hatua nyingine Waziri Mhandisi Kamwelwe amekagua ujenzi wa barabara ya Makutano - Sanzate yenye urefu wa KM 50 na kuridhishwa na kasi ya makandarasi 10 wazawa walioungana kupitia kampuni ya M/S Mbutu JV na kuwaahidi kuwaongeza sehemu ya barabara kutoka Sanzate hadi Nata na ile ya Mugumu hadi Serengeti pindi watakapokamilisha mradi huo.

Waziri Kamwelwe ameongeza kuwa pamoja na mradi wa barabara hiyo kuwa na maeneo korofi na mawe hadi sasa mradi umefikia asilimia 69 na KM 10 tayari zimeshawekwa lami.

Naye Mkandarasi wa Kampuni hiyo Mhandisi Andrew Nantori ameishukuru Serikali kwa kuwaamini makandarasi wazawa na amemuahidi Waziri Kamwelwe kuwa hatowaangusha.

Mradi wa ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 na barabara ya Makutano-Sanzate yenye urefu wa KM 50 inafadhiliwa na Serikali kwa asilimia 100.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 inayojengwa kwa kiwango cha lami, wilayani Bunda, mkoani Mara.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Makutano-Sanzate yenye urefu wa KM 50 inayojengwa kwa kiwango cha lami ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 69. Barabara hiyo inajengwa na makandarasi wazawa M/S Mbutu JV.

WADAU WA ELIMU WATAKIWA KUCHANGIA ILI UBORESHA VYUMBA VYA MADARASA RORYA

$
0
0
Diwani wa kata ya Baraki Mh Mwita Laurian akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Erengo ambapo mahafari hayo yameambatana na harambee kwa lengo la kuboresha vyumba vya madarasa hayo.

Na Frankius Cleophace, Rorya.

Wadau wa elimu Wilayan Rorya Mkoni mara wametakiwa kuendelea kuchangia fedha kwa lengo la kuboresha Vyumba vya madarasa katika shule za msingi wilayani Rorya Mkoani Mara ili kuweza kuweka mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia ikiwemo shule ya Msingi Erengo ambayo inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa majengo pamoja na upungufu wa Madarasa.

Wananchi kwa kuliona hilo katika mahafari ya darasa la saba Shule ya Msingi Erengo  wanachangi fedha kupitia harambee ambapo wamechangia zaidi ya Millioni moja pamoja na vifaa vyenye thamani ya shilingi Millioni moja huku wakiomba serikali kuwaunga mkono ili kuendeleza jitihada hizo , Makutano Gijagida ni Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Erengo na Charles Maganya ni mratibu Elimu kata ya Baraki wanazungumzia changamoto za shule hiyo huku wakipingeza nguvu za wananchi haowaliojitoa kuchagia katika harambee iliyoandaliwa.
Wanafunzi wa darasa la saba awakitoa burudani ya nyimbo katika mahafari hayo.

Maganya amesema kuwa shule yake inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa vyumba vya madarasa hivyi amezidi kuomba wadau wa elimu na wazazi kuzidi kujitoa kwa wingi kwa lengo la kutatu changamoto hiyo.

“Mazuingira ya shule yakiwa mazuri wanafunzi watapenda kusoma pia walimu watkaa shuleni hivyo sasa wazazi na wadau wa elimu kwa mkoa wa Mara na nje ya mkoa tuendelee kujitoa” alisema Mwalimu mkuu.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

TAA yachangia vyoo salama kwa mtoto wa kike

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wakwanza kulia) akiwaongoza Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha (watatu kulia) na Afisa Uhusiano, Bi. Bahati Mollel (wapili kulia) kukabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 5 (5,000,000/=) kwa mgeni rasmi kwenye hafla ya bunge kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo salama vya shule nchi nzima kwa mtoto wa Kike, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda (wapili kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya hafla hiyo, Mbunge wa Muleba Kusini, Prof. Anna Tibaijuka. Hafla hiyo ilifanyika jana usiku kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi kwenye hafla ya Bunge ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo salama vya shule nchi nzima kwa ajili ya mtoto wa Kike, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda (wapili kushoto), akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wakwanza kulia) wakati akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni tano (5,000,000), kama mchango wa TAA kusaidia juhudi za Bunge kuchangisha fedha za ujenzi huo. Hafla hiyo ilifanyika jana usiku kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya hafla hiyo, Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka, na wapili kulia ni Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha.

MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), imeunga mkono juhudi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Umoja wa Wabunge Wanawake wa Bunge hilo (TWPG) kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga vyoo salama vya shule nchi nzima kwa ajili ya mtoto wa Kike kwa kutoa mchango wa kiasi cha Shilingi Milioni Tano (5,000,000), katika hafla ya kuchangisha fedha kwa dhumuni hilo, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela, alikabidhi msaada huo wa fedha kwa mgeni rasmi, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda.

Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyoudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Wabunge, Wakuu wa Taasisi za Umma na Binafsi, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, aliwapongeza Wabunge hao kwa hatua hiyo ya kuhakikisha kunakuwepo kwa mazingira bora shuleni ili kutoa haki sawa ya kupata elimu kwa wanafunzi wa jinsia zote. “Wazo hili litasaidia sana serikali katika kuhakikisha mazingira ya shule yanaboreshwa ili kutoa nafasi sawa kwa wanafunzi wote wa kike na kiume,” alibainisha Spika Ndugai.

Alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, amefurahishwa na kitendo hicho na kwamba ameshindwa kuhudhuria hafla hiyo kwa vile bado yupo kwenye msiba wa dada yake huko Chato mkoani Geita.

Kwa upande wake, mgeni rasmi Mhe. Anne Makinda aliwapongeza Wabunge hao wanawake kwa hatua hiyo ya kuunga mkono juhudi za serikali na kuwataka Wabunge wanaume kuwaunga mkono wenzao katika kufanikisha kampeni hiyo inayolenga kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 3.5 zitakazowezesha kujenga vyoo salama vya shule kwenye majimbo yote 264 nchi nzima.

Taasisi Mbalimbali zilichangia kwenye harambee hiyo, ambapo pia vitu mbalimbali vilinadiwa na fedha zitakazopatikana zitakwenda kufanya kazi ya ujenzi huu.

MAKONTENA YA RC MAKONDA YAANZA KUPIGWA MNADA BANDARINI DAR

$
0
0
Na Ripota Wetu, Globu ya jamii

MAKONTENA ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ambayo yamebeba samani za walimu yameanza kupigwa mnada.

Hatua ya kupiga mnada makontena hayo inakuja baada ya Rais Dk.John Magufuli kutoa maagizo ya kuhakikisha yanalipiwa kodi na ikishindikana yapigwe mnada.

 Rais Dk.Magufuli alitoa kauli hiyo juzi akiwa mkoani Chato na sababu za kutoa ufafanuzi na maelekezo hayo baada ya kuona Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam analazimisha makontena hayo yatolewe bila kulipiwa kodi.

Hivyo leo makontena hayo yameanza kupigwa mnada kuanzia saa tatu ya asubuhi na unafanyika bandari ya Dar es Salaam upande wa Malawi Cargo.

Mnada huo tangu ulipoanza asubuhi unaendelea kufanyika hadi sasa.

Katika mnada huo wananchi, taasisi,mashirika na  baadhi ya viongozi wa Serikali wamejitokeza kwa lengo la nununua samani zilizopo kwenye makontena hayo.
Viewing all 110029 articles
Browse latest View live




Latest Images