Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109605 articles
Browse latest View live

Bongo Dansi made in Uswahilini kuwasha moto jukwaa la Alafia Festival katikani ya jiji la Hamburg, Ujerumani Ijumaa

0
0
Bendi maarufu ya Muziki wa dansi barani ulaya The Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni ukipenda waite viumbe wa ajabu Anunnaki au "Watoto wa Mbwa" inayoongozwa na kamanda Ras Makunja inatarajiwa kulitingisha jukwaa la Alafia Festival katikani ya jiji la Hamburg katika viwanja vya hamburg-Altona Ujerumani siku ijumaa tarehe 24-08-2018 kuanzia majira ya saa 2.00 usiku (20.00 hour)
Bendi hiyo maarufu inayodumu kwa miaka 24 sasa katika majukwaa ya kimataifa na mtindo wake wa "Bongo Dansi made in Uswahilini"  inazidi kuwanasa washabiki katika kila pembe barani ulaya,ni juzi kati tu ilitumbuiza katika onyesho kubwa mjini Tuebingen,Ujermani na Mamling Festival nchi Austria,na ijumaa ya tarehe 24 Augosti 2018 watatingisha tena mjini Hamburg-Altona.
Usikose kuungana nao katika tamasha hilo la wazi pia unaweza kujumuika nao mubashara at www.facebook.com/ngomaafricaband 

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanziubar Balozi Seif Ali Iddi akaguwa Majengo mapya ya Skuli za Sekondari

0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanziubar Balozi Seif Ali Iddi alisema wakati Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inazidi  kuimarisha miundombinu ndani ya Sekta ya Elimu, Wanafunzi Nchini wanalazimika kujikita zaidi katika kutafuta Elimu itakayowajengea njia ya Maisha ya furaha wao na Familia zao.
Alisema wanafunzi hao wakiamua kusoma kwa juhudi na maarifa na kufikia kiwango cha Elimu ya juu ya Vyuo Vikuu watakuwa na nafasi pana ya kujihakikishia fursa za ajira zilizozoweya kufanywa na Wataalamu wa Kigeni.
Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akisalimiana na Wananchi wa Mwambe akiendelea na ziara yake ya kukaguwa Majengo mapya ya Skuli za Sekondari zinazojengwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mshirika wa Maendeleo Mfuko wa Kimataifa wa Opec.
Alisema Taifa linahitaji kuwa na Wataalamu wake wenyewe  watakaotokana na Wanafunzi wake ambao watapaswa kuweka malengo ya kusoma kwa bidii kwa lengo la kuwahudumia Wananchi kwa kiwango cha uzalendo zaidi.
Balozi Seif alimuhimiza zaidi Mtoto wa Kike Nchini kusoma kwa ziada ili zile kazi za Kitaalamu zinazofanywa na Wanaume akatolea mfano za huduma za Afya wazifanye wenyewe katika azma ya kulinda na kuheshima mila, sila, Tamaduni na hata imani za Kidini.
Katika kutilia mkazo nafasi ya mtoto wa kike kusoma kwa malengo Balozi Seif  ameagiza Wazazi wowote watakaohusika na kitendo cha kuwaozesha  Watoto wao wa Kike wakati wanasoma Uongozi wa Serikali ya Mkoa usimamie katika kuona Vyombo vya Dola vinawachukulia hatua za Kisheria mara moja Wazazi hao ikiwa ni pamoja na kuwaweka ndani.
“ Jamii inahitaji kuwa na Ewataalamu wa Kike ambao watahusika kushughulikia huduma zinazofanywa na Wanaume Kitaalamu ambazo hazistahiki kutokana na Tamaduni na Imani wa Kidini”. Alisisitiza Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alionya kwamba tabia hii inayoonekana kuendelea kwa baadhi ya Mitaa Nchini inarejesha nyuma maendeleo ya Mtoto wa kike aliyekandamizwa kwa muda mrefu kutokana na mfume Dume uliozoeleka kwa kipindi kirefu kilichopita.
 Balozi Seif akimchum Mtoto Sulhia Ali wa Kijiji cha Mwambe huku Mama yake Mzazi akitabasamu mara baada ya kusalimiana na Wananchi wa Kijiji hicho alipofika kukagua maendeleo ya ujenzi wa Skuli ya Sekondari.
 Mhandisi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Wara Ali Khamis Shaibu akimpatia maelezo Balozi Seif kuhusu ujenzi wa majengo ya Skuli hiyo unaokwenda kwa wakati uliopangwa.
Naibu Katibu Mkuu Wikzara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Maalim Abdulla Mzee Abdulla akiteta na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  kwenye majengo ya Skuli Mpoya ya Sekondari inayojengwa katika Kijiji cha Wara Chake Chake Pemba.
Balozi Seif akikagua baadhi ya Majengo ya Nyumba za Makaazi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar zinazojengwa katika eneo la Pagali Wilaya ya Chake chake Pemba.
Umma wa Wananchi wa Kijiji cha Mwambe waliokuwa wakisikiliza nasaha za Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo pichani alipofika kukagua Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari kwenye eneo hilo.

INTRODUCING "MOYO" BY COCO

TAMKO LA THINK TANKERS KUHUSU TAARIFA YA UBALOZI WA MAREKANI KUHUSU UCHAGUZI WA MARUDIO NCHINI

The Ministry of Foreign Affairs and East Africa Cooperation Delegation will be in Seattle, WA

0
0
DICOTA is proud to announce that during the 2018 DICOTA Convention, Mr. Moremi Marwa- CEO of the Dar Es Salaam Stock Exchange will officially launch Azania Capital Partners, LLC a newly established US Based Tanzania Diaspora private equity firm. Mr Marwa will also speak on the current state of capital and equity markets in Tanzania including regulatory environment and taxation policy. Do not miss this unique opportunity. Register now and book your room www.dicotaus.org/Convention
We warmly welcome back to the US and to DICOTA the Ministry of Foreign Affairs and East Africa Cooperation delegation.   The delegation includes Deputy Permanent Secretary Amb. Ramadhan Muombwa Mwinyi, who is no stranger to many in the Tanzania US Diaspora, Ambassador Mwinyi  was formerly Deputy Permanent Representative of Tanzania to the United Nations and very active in the New York Tanzania Community (NYTC).  Amb. Anissa Mbega, Diaspora Department Director continues to lead and champion many diaspora initiatives. We warmly welcome both.

See you in Seattle! 

TanzaSeattle Community Presents Fundraising Weekend.

NAIBU WAZIRI ULEGA AKUTANA NA WATENDAJI WA MRADI SWIOFISH

0
0
Naibu Waziri  wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Abdalla Ulega akiongozana na Dkt. Rashid Tamatama Katibu Mkuu Uvuvi wamezungumza na watumishi wa upande wa Mradi wa SWIOFish katika ukumbi wa Mvuvi House - Dar es Salaam.

 Mh. Naibu Waziri baada ya kupata maelezo kuhusu Mradi huo  ametoa changamoto kwa watendaji kwa kuwaeleza kuwa elimu inayotolewa kwa jamii za wavuvi iweze kuleta matokeo chanya hata pale mradi utakapo maliza muda wake na kuwepo na matokeo ambayo yataweza kupimika hata kwa macho. 
Hii itasaidia sana jamii zetu ambazo Mara nyingi miradi ikiishà na wao hali zao zinaendelea kuwa duni badala ya kuwa zimeboreshwa.Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo leo jijini Dar as Salaam.


CCM KARATU YAONYA WANAOHUJUMU MIRADI YA MAENDELEO

0
0
Na Woinde Shizza, Arusha

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Karatu  kimeonya baadhi ya watendaji wanaohujumu miradi ya maendeleo ikiwemo miradi ya maji ,barabara ambayo inalenga kutatua changamoto za wananchi. 

Mwenyekiti wa CCM wilayani hapo Lucian  Akonaay ametoa onyo hilo jana ambapo amesema  wanaohujumu miradi watachukuliwa hatua.

Amesema kuwa wananchi bado wana imani na chama hicho katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma muhimu za kijamii ikiwemo maji na miundombinu ya barabara pamoja na huduma za afya.

Akonaay amesema kuwa Chama hicho kimeandaa utaratibu wa kutembelea miradi ya maendeleo  na kujihakikishia kuwa iwapo inatekelezwa kwa viwango stahiki na kwa wakati uliopangwa

 Kwa upande wake Katibu wa CCM Karatu  Solomon Itunda amesema kuwa viongozi wa chama hicho wamekua wakikagua maendeleo ya miradi pamoja na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora ikiwa ni pamoja na kutoa mapendekezo kwa viongozi wa Serikali.

Diwani Mteule wa Kata ya Baray kupitia  Chama hicho Elitumaini Rweyemamu amesema kuwa wamejiandaa kusimamia utekelezaji na kutatu kero za wananchi ili kuboresha huduma za kijamii.
 Wakati huo huo Mkazi wa Karatu ameipongeza Serikali kwa kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa kuchimba visima na kuiomba iongeze visima na mabomba hususan kwenye maeneo yenye watu wengi.

RC MANYARA AZINDUA LIGI YA CHEMCHEM INAYOSHIRIKISHA TIMU 20,LENGO NI KUKOMESHA UJANGIRI

0
0
Na Woinde Shizza, Manyara

MKUU wa Mkoa wa Manyara, Elexander Mnyeti amezindua ligi ya Chemchem inayoshirikisha timu 20, yenye lengo la kupiga vita ujangili ambayo itagharimu zaidi ya sh 35 milioni.

Akizungumza juzi katika uzinduzi huo katika viwanja vya mdori, wilayani Babati, Mnyeti ambaye aliwakilishwa na Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara, Augustine Senga amezitaka timu zitakazoshiriki kucheza kwa nidhamu ili kufikia malengo ya ligi hiyo.

Mnyeti amesema ligi hiyo pia inapaswa kutumika katika kuibua vipaji kwa wachezaji chipukizi ili kuweza kusajiliwa katika timu za ligi kuu."Najua hapa kuna vipaji hivyo michezo hii ni fursa ya kujulikana zaidi na hivyo kuwa sehemu ya kutoa ajira kwa vijana na kujenga afya"amesema

Katibu wa mashindano hayo John Bura amesema jumla ya timu 20 za soka zinatarajia kushiriki michuano hiyo na kutakuwa na zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa nne."Pia kutakuwa na ligi ya wanawake ambayo itashirikisha timu tatu na washindi watapewa zawadi,"amesema

Amesema katika michuano hiyo mchezaji bora,mfungaji bora na timu yenye nidhamu, watapata zawadi na hivyo, akawataka kucheza soka la kuvutia.Awali Meneja wa Chemchem ambao ni wadhamini wa ligi hiyo, Kanali mstaafu Leonard Werema amesema taasisi hiyo inayofanya shughuli za utalii katika eneo hilo la hifadhi ya jamii ya Wanyamapori(WMA) ya Burunge.

Na kwamba inataka ligi hiyo, kusaidia kutoa elimu ya kupiga vita ujangili na uhifadhi.Werema amesema Chemchem imegharamia zaidi ya Sh.milioni 35 katika michuano hiyo, ikiwepo kuandaa uwanja na majengo kuandaa zawadi, imetoa vifaa vya michezo kwa timu zote 23 na gharama nyingi za waamuzi na waratibu wa michuano hiyo chama cha soka wilaya ya Babati.

Katika mchezo wa ufunguzi, mabingwa watetezi, Mdori FC walipata ushindi wa magori 3-2 dhidi ya timu ya City Boys katika mchezo mkali uliochezwa kiwanja cha mdori.
 MKUU wa Mkoa wa Manyara, Elexander Mnyeti pichani juu na chini akisalimiana na baadhi ya wachezaji wakati akizindua  ligi ya Chemchem inayoshirikisha timu 20, yenye lengo la kupiga vita ujangili ambayo itagharimu zaidi ya sh 35 milioni.Akizungumza juzi katika uzinduzi huo katika viwanja vya mdori, wilayani Babati, Mnyeti ambaye aliwakilishwa na Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara, Augustine Senga amezitaka timu zitakazoshiriki kucheza kwa nidhamu ili kufikia malengo ya ligi hiyo.

INTRODUCING "UNAJISHAUWA" BY G VAN

KATIBU TAWALA CHEMBA AKAGUA UJENZI ZAHANATI INAYOJENGWA NA WANAKIJIJI,ACHANGIA VIFAA VYA UJENZI

0
0
KATIBU tawala wa wilaya ya Chemba mkoani Dodoma Mhe. Zahara Michuzi ametembelea katika kijiji cha Hamai na kukagua ujenzi wa zahanati ya Hamai inayojengwa na wananchi wa kijiji hicho,pia amepata fursa ya kusikiliza changamoto zao,ambapo  pia ametoa vifaa vya ujenzi na kushiriki kufanya baadhi ya kazi za ujenzi wa zahanati hiyo.

Akizungumza na Mafundi ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Hamai, Zahara  amesema kuwa zahanati hiyo inatakiwa imalizike kwa haraka na kwa ufanisi mzuri ili kusaidia wananchi kupunguza  umbali wa kutembea kwa ajili ya kufuata huduma muhimu ya kijamii ya afya.

Pia wakati wa ziara ya kutembelea ujenzi wa zahanati hiyo ya kijiji, Zahara ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo Mbao, misumari chokaa pamoja na vigae kuhakikisha ujenzi wa Zahanati hiyo unaisha kwa muda uliopangwa.

Wakati huo huo Zahara pia amewashukuru Wananchi waliojitokeza na kujitolea kujenga kituo hicho cha Afya, kwani maendeleo yanahitaji ushirikiano wa pamoja,Hivyo amewaomba waendelee na moyo huo huo wa kushirikiana ikiwemo pamoja na Serikali.

Katibu tawala wilaya ya Chemba mkoani Dodoma  Mh. Zahara Michuzi  akionesha baadhi ya vifaa mbalimbali vya ujenzi alivyochangia katika ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Hamai kilichopo wilaya ya Chemba mkoani Dodoma .
 Katibu tawala wa wilaya ya Chemba, Mh. Zahara Michuzi akitembelea  ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Hamai kilichopo wilaya ya Chema mkoani Dododma.
 Katibu tawala wa wilaya ya Chemba, Mh. Zahara Michuzi akisaidia kupaka rangi kwenye jengo la zahanati ya kijiji cha Hamai kilichopo wilaya ya Chemba mkoani Dododma, alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Katibu tawala wa wilaya ya Chemba, Mh. Zahara Michuzi akizungumza na wajenzi wa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Hamai kilichopo wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, mara baada ya kuchangia vifaa ya ujenzi pamoja na kuwaongezea wahandisi wa ujenzi kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo hilo la zahanati.

Migogoro ya wazazi katika familia, imetajwa kuwa ni moja ya sababu kubwa inayoathiri elimu

0
0
Na Emauel Madafa , Michuzi Blog , MBEYA.

MIGOGORO ya wazazi katika familia, imetajwa kuwa ni moja ya sababu kubwa inayoathiri elimu na malezi bora ya watoto.

Kauli hiyo imetolewa jijini Mbeya na Afisa Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani kwenye mahafali ya wanafunzi 63 wa darasa la saba.

Amefafanua kuwa uongozi wa shule hiyo umekuwa ukipokea kesi nyingi za namna hiyo, hivyo kuwaomba wazazi wakiume kutambua wajibu wao kwa watoto ikiwa na kuwatendea haki kwa kutimiza haki zao za msingi ikiwemo elimu.Aidha, amewataka wazazi kujenga mshikamano, umoja, amani na upendo kwenye familia ili watoto waweze kuiga mambo yaliyomema na kukua katika maadili.

Amesema kuna watoto wengi wameacha masomo na wengine kuhamishwa shule kutokana na jukumu la kusomesha mtoto kuachiwa mama pekee jambo hali ambayo imekuwa ikimnyima haki mtoto. Kwa upande wake Meneja wa bima Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Consolatha Gabone amesema moja ya changamoto zinazo poteza ndoto za watoto ni mifarakano ndani ya familia hasa pale wazazi wanapo tengana au kufariki.

Amesema kutokana hali hiyo wameamua kuanzisha huduma ya bima ya maisha ambayo inatoa fursa kwa wategemezi kutimiza ndoto zao bila kuathiri mfumo wa maisha licha ya kuondokewa na wazazi.Gabone amesema kuwa imekuwa ni jambo la kawaida kwa wazazi kuwa na bima za magari na mali nyingine na kusahau bima za maisha ikiwemo elimu ambayo ni njia ya kumwezesha mwanafunzi kufikia ndoto zake kabla ya kuanza kujitegemea.

Amesema ili kuweza kuonyesha upendo kwa watoto ni vema wakafungua bima ya elimu ili kuweza kutimiza malengo ya watoto. Wengi wamesau kwa habari ya maisha yao wenyewe unajua mzazi anapo kuwa amekata bima ya maisha ni kuonyesha upendo kwa familia lakini kuna wakati unaweza kupata madhara hivyo ukashindwa kusomesha lakini ukakata bima hasa ya elimu watoto wataendelea na masomo hivyo niwashuri wazazi kukata bima ili kuwezesha kutimza malengo ya watoto wao’alisema Gabone.
Afisa Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani akizungumza kwenye mahafali ya wanafunzi 63 wa darasa la saba.
Wahitimu wa elimu ya msingi darasa la Saba katika shule ya St.Merys Mbeya wakiwa makini kumsikiliza Afisa Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani katika shehere za mahafali ya 63 ya shule hiyo.
Rose Lwakatare (Mtoto wa Mchungaji Mama Lwakatare ) akizungumza katika sherehe hizo zilizofanyika shuleni hapo .
Meneja wa bima (TIRA)Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Consolatha Gabone akizungumza katika mahafali hayo 
Wanafunzi wakitoa burudani katika sherehe hizo.
Wazazi na Walezi ambao walipata fursa ya kuhudhuria sherehe hizo 

POLISI KILIMANJARO YANASA RAIA WA ETHIOPIA 25 WALIONGIA NCHINI BILA KUFUATA SHERIA.

0
0
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini

Jeshi la Polisi linawashikilia raia 25 wa Ethiopia miongoni mwao tisa ni watoto wenye umri chini ya miaka 18 wakiwa katika kichaka eneo la Himo wakisubiri gari kwa ajili ya kuwavusha kuendelea na safari yao ya Afrika Kusini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Maidizi wa Polisi,Hamis Issah amesema raia hao wa Ethiopia walikamatwa na askari Polisi wakati wa doria wakiwa na kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Baraka itema (25) aliyejitambulisha kama fundi ujenzi .

Raia hao 25 wa Ethiopia wanaendelea kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kwa kusaidiana na jshi la Polisi na kwamba mara baada ya taratibu kukamilika watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili za kuingia nchini bila ya kibali.


Raia 25 wa Ethiopia waliokamatwa wakati wakijaribu kupita nchini bila ya kufuata Sheria wakishuka kwenye gari walipofikishwa kituo kikuu cha Polisi mjini Moshi.
Baadhi ya raia hao wa Ethiopia wakiwemo watoto tisa wenye umri chini ya miaka 18 wakiwa kituo kikuu cha Polisi mjini Moshi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamis Issah akitoa taarifa juu y akukamatwa kwa raia 25 wa Ethiopia waliongia nchini bila ya kufuata Sheria.

Kamati ya Bajeti Yaipongeza NBS kwa Ufanisi wa Kazi Zake

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa akifafanua jambo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika semina iliyoandaliwa na NBS jana Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Mhe. Hawa Ghasia akisisitiza jambo wakati wa semina ya ya wajumbe wa Kamati hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS),jijijini Dodoma jana. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa.
Meneja wa Takwimu za Mazingira, Bibi. Ruth Minja akiwasilisha mada mbele ya wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika semina iliyoandaliwa na NBS jana Jijini Dodoma. Mtakwimu Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Bw. Steven Maganda akiwasilisha mada kuhusu utafiti wa kaya mbele ya wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika semina iliyoandaliwa na NBS jana Jijini Dodoma. Mbunge wa Jimbo la Mvomero, mkoani Morogoro Jeetson Patel akichangia mada wakati wa semina ya wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jana Jijini Dodoma.[ Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakifuatilia mada wakati wa semina kwa wajumbe hao iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jana Jijini Dodoma.(Picha na Idara ya Habari - MAELEZO)

TPDC KUKIONGEZEA UZALISHAJI KIWANDA CHA DANGOTE-TANZANIA

0
0
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Katika kuunga mkono juhudi za serikali katika kampeni ya Tanzania ya Viwanda, Shirika la Taifa la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limesaini mkataba na Kampuni ya Saruji ya Dangote-Tanzania, utakaosaidia kiwanda hicho kuachana na matumizi ya mafuta ya dizeli katika uzalishaji wa umeme. 

Akizungumza jijini Dar es Salaaam wakati wa hafla fupi ya kusaini makubaliano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba amesema mkataba huo na Dangote utadumu kwa miaka 20 tofauti na mikataba mingine ambao huingia na makampuni.

 "Tunajua Serikali iko kwenye hatua za kujenga uchumi wa viwanda, kwa hiyo sisi (TPDC) kwa nafasi yetu tutahakikisha viwanda vinazalisha bidhaa kwa gharama nafuu kupitia matumizi ya gesi, wataanza kutumia futi za ujazo milioni nane na baada ya miaka miwili ijayo wataanza kutumia futi za ujazo milioni 20,” amesema Mhandisi Musomba. Amesema kuwa tokea Septemba mwaka jana wao walikuwa tayari wameshafikisha huduma hiyo mlangoni mwa kiwanda cha Dangote, walichokuwa wanasubiri ni ukamilishwaji wa mitambo ili kuingiza gesi waanze matumizi. 

 Kwa mujibu wa TPDC, kiwanda hicho ni sehemu ya viwanda saba vilivyopo kwenye mpango wa shirika katika mwaka wa fedha 2018/19, hivyo bado kuna vingine sita vitaunganishwa hapo baadaye. Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda hicho cha Saruji, Jagat Rathee ameishukuru serikali kwa kuweza kuwawekeza nishati ya gesi ambao pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji lakini wataweza kutunza mazingira.

 "Kiwanda kilikuwa kinatumia wastani wa lita 106,000 za Dizeli ambazo zilizalisha wastani wa megawatt 20 (18MW -22MW) za gesi asilia kwa siku katika uzalishaji wa tani 2000 tu hivyo kutumia nishati ya gesi tutafikia wastani wa tani 6000 kwa siku huku gharama za uendeshaji zikishuka kwa asilimia 60. Kiwanda hicho kinaongeza idadi ya viwanda vinavyotumia gesi asilia kwa ajili ya uzalishaji wa umeme kufikia 42 nchini, ambavyo vinatumia futi za ujazo milioni 15 tu kutoka akiba ya futi za ujazo trilioni 57, zinazoweza kutumika miaka 40 ijayo nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba (kutoka kulia waliokaa) akisani mkataba wa makubaliano na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha Saruji cha Dangote-Tanzania (wa kwanza) katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba (kutoka kulia) akibadilishana mkataba wa makubaliano na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha Saruji cha Dangote-Tanzania, Jagat Rathee (wa kwanza) katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba (katikati) akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam katika hafla fupi ya kusaini makubaliano na Kampuni ya Saruji ya Dangote-Tanzania ya kuwasambazia nishati ya gesi katika uzalishaji na kuachana na matumizi ya Dizeli katika uzalishaji wa umeme. Pembeni kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha Saruji cha Dangote-Tanzania na kushoni ni mmoja ya wafanyakazi wa TPDC.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha Saruji cha Dangote-Tanzania akizungumza na wanahabari katika hafla fupi ya kusaini makubaliano na Kampuni ya Saruji ya Dangote-Tanzania ya kuwasambazia nishati ya gesi katika uzalishaji na kuachana na matumizi ya Dizeli katika uzalishaji wa umeme. 

GHARAMA UKARABATI WA BARABARA NDANI YA JIMBO KUONGEZEKA ZAIDI-TAASISI YA MAENDELEO JIMBO LA VUNJO (VDF)

0
0
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

TAASISI ya Maendeleo ya jimbo la Vunjo(VDF) imesema gharama zilizotengwa awali kwa ajili ya ukarabati wa Km 272.8 za barabara katika vijiji vyote vya jimbo hilo huenda zikaongezeka kutokana na kuwepo kwa miamba katika maeneo ambayo yanahitaji upanuzi.

Katibu wa taasisi hiyo,James Mbatia amesema ikiwa imengia wiki ya tatu tangu kuanza kwa ukarabati kwa baadhi ya maeneo katika barabara hizo tayari wamekutana na changamoto ya uwepo wa miamba ambayo imelazimika kuvunjwa kwanza .

“Tulipanga hii kazi kutumia miezi sita kuimaliza lakini sasa inaweza kuchukua hadi mwaka mmoja kutokana na changamoto ambazo zimeanza kujitokeza hizi za kukutana na miamba na wakati mwingine hali ya hewa”alisema Mbatia.

Mbatia ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Vunjo alisema awali walipanga kutumia kiasi cha Sh Bil 7.29 kukamilisha kazi hizo lakini kwa namna shughuli inavyoendelea huenda gharama ikazidi huku akiendelea kutoa wito kwa wadau kuendelea kuchangia

“Hadi sasa tunashukuru kazi inaendelea vizuri tukishirikiana nawenzetu wa TARURA,TANESCO na tasisi nyingine ,lakini kipekee niombe serikali ione umuhimu wa kusaidia katika kutatua changamoto hii ya barabara kwa wakazi hawa wa jimbo la Vunjo”alisema Mbatia.

Kutokana na kuendelea kwa shughuli ya ukarabati wa barabara hizo tayari wananchi katika vijiji vya Shira na Mshiri vilivyopo katika jimbo la Vunjo wameanza kunufaika na mradi huo unaotekelezwa na Taasisi ya Maendeleo ya jimbo la Vunjo (VDF).Shughuli ya upanuzi wa barabara katika kijiji cha Mshiri,Marangu ikiendelea kwa uondoaji wa miti iliyo kando ya barabara ya awali sambamba na uondohaji wa Miundo mbinu ya umeme ili kupisha shughuli za upanuzi.

Michuzi Blog imefika katika maeneo mbalimbali ya vijiji vilivyoko katika jimbo la Vunjo na kujionea mitambo ikiendelea na shughuli za upanuzi wa barabara pamoja na uondoaji wa miti na mawe makubwa yaliyokuwa katika maeneo ya barabara hizo.
Katibu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jimbo la Vunjo,James Mbatia akitoa salamu kwa baadhi ya wananchi walioshiriki katika ukarabati wa miundo mbinu ya barabara unaoendelea katika jimbo hilo kwa kuchangia nguvu kazi.
Mafundi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakiondosha Nyaya ili kupisha upanuzi wa barabara hizo.
Upanuzi wa barabara mbalimbali ukiendelea katika jimbo la Vunjo. 
Moja ya eneo ambalo kazi ya upasuaji wamiamba ililazimika kufanyika ili kupanua barabara .
Muonekano wa barabara katika maeneo mbalimbali wakati ukaraba huo ukiendelea .


Marais Wastaafu na viongozi mbalimbali wa serikali wawasili Chato kushiriki mazishi ya dada yake Rais Dkt Magufuli

0
0
 Marais Wastaafu Mzee Al-Hassan Mwinyi,Mh William Mkapa na Mh Jakaya Mrisho Kikwetee wakiwa na wake zao pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh John Mongella (pichani kushoto) wakiwa wamewasili uwanja wa ndege jijini Mwanza tayari kuelekea Chato mkoani Geita kushiriki mazishi ya Dada yake Rais Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki hivi karibuni hospitali ya Bugando alikokuwa akipatiwa matibabu
 Rais Mstaafu awamu ya tatu,Mh.William Benjamin Mkapa akiwasili uwanja wa ndege jijini Mwanza mapema leo tayari kuelekea kwenye msiba wa dada yake Rais Dkt John Magufuli,wilayani Chato mkoani Geita.
  Rais Mstaafu awamu ya tatu,Mh.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameambatana na mkewe Salma Kikwete sambamba na viongozi wengine wakiwasili uwanja wa ndege jijini Mwanza mapema leo tayari kuelekea kwenye mazishi ya dada yake Rais Dkt John Magufuli,wilayani Chato mkoani Geita.

Mambo 5 ya kuyafahamu kuhusu Eid Al-Adha au ‘Sikukuu ya Kuchinja’

0
0

Na Jumia Tanzania

Katika ya dini ya Kiislamu, Eid Al-Adha au ‘Sikukuu ya kuchinja’ ni sikukuu kubwa inayofanyika baada ya kuisha kwa Hija. Sikukuu hii huashiria kuisha kwa ibada ya Hija eneo la Mina, nchini Saudi Arabia, lakini huadhimishwa na Waislamu duniani kote kama ishara ya kumbukumbu ya imani aliyoionyesha Ibrahimu.
Eid Al-Adha huanza siku ya kumi ya Dhu’l-Hijja, mwezi wa mwisho kwenye kalenda ya Kiislamu, na hudumu kwa muda wa siku nne. Huanza baada ya siku ambayo Waislamu kumali Hija wakishuka kutoka Mlima Arafat.

Sikukuu hii husherehekewa na Waislamu duniani kote, kama zilivyo tamaduni za imani ya dini nyingine. Lakini Eid Al-Adha ni nini? Yafuatayo ni mambo matano ambayo Jumia ingependa uyafahamu kuhusiana na sikukuu hii.

Historia ya Eid. Eid Al-Adha, ni sikukuu ya Kiislamu inayoadhimishwa kukumbuka tukio la Nabii Ibrahimu kuwa tayari kumtoa sadaka mwanaye wa pekee kwa kuchinja kama alivyoagizwa na Mungu. Ingawa alikuwa ni mtu mwema na aliyempenda mwanawe; imani yake na kujitoa kwa Mungu vilikuwa na nguvu zaidi kiasi ambacho angeweza kufanya chochote alichoagizwa. Kitendo cha utayari wa Ibrahimu kumtoa sadaka mwanaye wa pekee kwa Mungu kilipelekea Mungu kutoruhusu kuchinjwa kwa mtoto yule na badala yake akampatia mwanakondoo kuwa mbadala.

Kitendo cha kuchinja mnyama. Kwa wengi walio nje ya imani ya Kiislamu wamekuwa wakilitafsiri hili tukio tofauti. Kinyume chake, Waislamu huwachinja wanyama wao kwa kutanguliza sala kwanza na kuwachinja kwa jina la Mungu, ambaye amewapa mamlaka juu ya wanyama hao na haki ya kuwala. Hata hivyo, Wailsamu wanapolitaja jina la Mwenyezi Mungu wakati wa kuchinja, ni kutukumbusha kwamba uhai ni kitu kitakatifu. Kwa hiyo kiuhalisia, hukifanya kitendo hiko kwa kumbariki mnyama na kumshukuru Mungu, pamoja na kutambua utakatifu wa maisha ya mnyama.

Nyama hugawiwa kwa familia, jamaa na maskini. Eid Al-Adha pia hujulikana kama ‘Sikukuu ya Kuchinja.’ Kondoo, ng’ombe, mbuzi, au ngamia ni sadaka kwa jina la Mwenyezi Mungu. Nyama itokanayo na sadaka hugawanywa katika mafungu matatu: theluthi moja kwa ajili ya familia, theluthi nyingine kwa marafiki na majirani, na theluthi inayobakia hugawiwa kwa maskini. 

DC MJEMA AELEZA ALICHOBAINI KWENYE ZIARA YAKE

Viewing all 109605 articles
Browse latest View live




Latest Images