Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110137 articles
Browse latest View live

MICHUZI TV: POLISI KUIMARISHA MAFUNZO YA VITENDO KWA ASKARI WAKE.


MICHUZI TV: HARUSI YA LULU NA MAJIZO YANUKIA, RC MAKONDA AFUNGUKA KILA KITU

KERO ZA ARDHI TABORA ZITATATULIWA NA WAZIRI WA ARDHI - MAJALIWA

$
0
0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atakwenda katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ili kutatua kero kubwa za ardhi. Ameyasema hayo jana jioni (Jumamosi, Agosti 18 ,2018) wakati akizungumza na wananchi wa Manispaa hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chipukizi.

Waziri Mkuu aliyasema hayo baada ya wabunge na wananchi kueleza changamoto kubwa zinazowakabili ikiwe ya migogoro ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye kiwanja cha Chipukizi katika Manispaa ya Tabora, Agosti 18, 2018.

“Waziri wa Ardhi atakuja hapa na ramani zake, atakutana na watendaji na kumaliza matatizo yote makubwa ya ardhi na yale madogo madogo yatashughulikiwa na Mkuu wa Wilaya,”.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu alisema wilaya zote zinatakiwa zihakikishe zinakuwa na shule moja ya kidato cha tano na sita kwenye kila tarafa nchini na Serikali itapeleka walimu. Alisema uwepo wa shule hizo utaamsha ari ya wanafunzi kusoma kwa bidii, jambo litakaloongeza idadi ya wanaoendelea na masomo ya kidato cha tano na sita.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Emmanuel Nley jumla ya shilingi 1,500,000/= kwa ajili ya ujenzi wa dawati la Jinsia katika Mji wa Tabora na ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa polisi katika wilaya ya Igunga. Makabidhiano ya fedha hizo zilizotolewa na Mbunge wa Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto) yalifanyika baada ya Waziri Mkuu kuhutubiua mkutano wa hadhara katika kiwanja cha Chipukizi kwenye Manispaa ya Tabora, Agosti 18, 2018. Wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri na wapili kushotoi ni Mbunge wa Viti Maalum, Munde Tambwe. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Kadhalika Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji wote kuanzia ngazi ya halmashauri hadi vijiji wawasimamie wanafunzi wa kike na wahakikishe wanamaliza masomo bila ya kukatishwa.

“Huu ni mkakati wa Taifa tunataka watoto wa kike wote walindwe ili waweze kumaliza shule na marufuku kukatisha elimu yao, iwe kwa kuwapa ujauzito au kuwaoa, adhabu yake ni kali,”.


Waziri Mkuu jana jioni alimaliza ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tabora baada ya kuwa amefanya ziara katika wilaya za Igunga, Nzega na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.
Wananchi wa Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Waziri Mkuuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia mkutano wa hadhara kwenye kiwanja cha Chipukizi, Agosti 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Tabora, Hassan Kasubi katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kwenye kiwanja cha Chipukizi katika Manispaa ya Tabora, Agosti 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora, Munde Tambwe katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kwenye kiwanja cha chipukizi katika Manispaa ya Tabora, Agosti 18, 2018.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa zamani wa Tabora Mjini, Aden Rage baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika kiwanja cha Chipukizi kwenye Manispaa ya Tabora, Agosti 18, 2018. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri.

WAZIRI LUGOLA AONYA POLISI KUTUMIWA NA MAFISADI KUPORA ARDHI ZA WANANCHI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Ragati, Jimbo la Mwibara, Wilayani ya Bunda, mkoani Mara, jana. Katika hotuba yake, Lugola aliwaonya Polisi nchini ambao wanatumiwa na mafisadi kuwanyanyasa wananchi maskini kwa kupora ardhi zao na kukimbilia kufungua kesi vituoni wakilazimisha ardhi hiyo kuwa ni mali yao.

Na Felix Mwagara, MOHA

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaonya Polisi nchini ambao wanatumiwa na mafisadi kuwanyanyasa wananchi maskini kwa kupora ardhi zao na kukimbilia kufungua kesi vituoni wakilazimisha ardhi hiyo iwe mali yao.

Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Ragati, Kata ya Kasuguti, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, Lugola alisema amepata malalamiko mengi kutoka sehemu mbalimbali nchini, kuwa mafisadi uonea wananchi maskini kwa kupora kwa nguvu ardhi wakidai wanamiliki wao na wanatumia badhi ya polisi wasiokua waaminifu ili kuwakandamiza wananchi hao.

Kutokana na hatua hiyo, Lugola amepiga marufuku kwa mwananchi yeyote ambaye anakurupuka kukimbilia kituo cha polisi kufungua kesi za ardhi ambazo hazina uthibitisho wa jinai yoyote, badala yake kesi au malalamiko yake kwanza ayapeleke katika mabaraza ya ardhi katika eneo husika ili ziweze kutatuliwa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akiliangalia panga alilopewa na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ikiwa ni kiashiria cha kupewa ushujaa katika jamii ya Kabila la Wagita, mara baada ya Waziri huyo kumaliza kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibara, Mkoani Mara, jana. Katika hotuba yake, Lugola aliwaonya Polisi nchini ambao wanatumiwa na mafisadi kuwanyanyasa wananchi maskini kwa kupora ardhi zao na kukimbilia kufungua kesi vituoni wakilazimisha ardhi hiyo kuwa ni mali yao.

Lugola ameongeza kuwa, mafisadi hao ambao wanafedha baada ya kuona mmiliki halali wa ardhi hiyo anagoma kuondoka katika sehemu husika, basi utumia fedha zake kwa kukimbilia polisi kufungua kesi bila ya kuwa na uthitisho wowote huku baadhi ya polisi wasiokua waaminifu wakitumiwa katika kufanikisha ardhi hiyo ananyang’anywa mwananchi huyo.

“Kuanzia leo mwananchi yeyote atakaeenda kufungua kesi kituo cha polisi inayohusu masuala ya ardhi na endapo kiwanja hicho kimepimwa lazima awe na hati inayoonyesha yeye ni mmiliki halali, ili iwasaidie polisi wajue wewe ndio mmiliki halali, na kwa upande wa ardhi ambayo haijapimwa lazima mwananchi huyo aende polisi akiwa na uthibitisho kutoka kijijini au katika mtaa unaosema kwamba eneo hilo ni la kwako na polisi wathibitishe hilo,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, na endapo kesi ya mlalamikaji yeyote ipo mahakamani anapaswa kuheshimu makahama na si kuendeleza kufanya usumbufu katika jamii pamoja na kwenda polisi na kuanza kutafuta njia ya kumsumbua mwananchi ambaye ni maskini katika eneo hilo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kushoto), akimkabidhi zawadi ya shilingi 250,000, mshindi wa kwanza wa Bonanza la Kangi la mpira wa miguu lililofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Ragati, Jimbo la Mwibara, Wilayani ya Bunda, mkoani Mara. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Katika hilo, Lugola alifafanua kuwa, endapo mwananchi ana hukumu ya mahakamani inayoonyesha ameshinda kesi hiyo, mwananchi huyo anapaswa kwenda polisi na nakala ya hukumu yake ili polisi waweze kushuhudia kwamba pande zote mbili ziliwahi kugombana kuhusu ardhi na kufikishana mahakamani lakini mmojawapo alishinda.

“Rais Magufuli alianzisha Mahakama ya mafisadi hapa nchini, kwa taarifa niliokua nayo, mahakama hii ina uhaba wa mafisadi, sasa mimi nitaitafutia wateja kwa kuhakikisha wale mafisadi ambao uonea wananchi, utesa wananchi, uiba fedha za serikali au taasisi yoyote nitawafikisha katika mahakama hiyo, hatutakubaliana na manyanyaso ya aina yoyote katika Serikali hii ya awamu ya tano” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kua, hataki kusikia mwananchi anaonewa, na pia aliapa hatacheka na mafisadi, atapambana nao sehemu yoyote nchini na pia yupo tayari kwalolote na ameanza kupambana na mafisadi ndani ya wizara yake na tayari wameanza kurudisha fedha za Serikali. Aidha, Lugola katika hotuba yake alipiga marufuku kwa waendesha bodaboda wenye tabia ya kubeba abiria zaidi ya mmoja kuiacha tabia hiyo ili kuepusha ajali, lakini aliwataka polisi kutorudi nyuma, wahakikishe wanawakamata waendesha bodaboda wasiofuata sheria za usalama barabarani.

Waziri Lugola yupo katika ziara jimboni kwake kwa kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuwaunganisha wananchi kupitia Bonanza lake la michezo ya mpira wa miguu ambalo linashirikisha kila kata wakitoa washindi mbalimbali ambao anawapa zawadi pamoja na kuingia moja kwa moja katika mashindano ya kugombea Kombe la Kangi.

Maugo amchapa Mmalawi, Class amnyamazisha Mazola kwa TKO

$
0
0
Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo wa Tanzania amemchapa kwa pointi, mpinzani wake, Charles Misanjo wa Malawi katika pambano la kimataifa la uzito wa Super Middleweight kwenye ukumbi wa PTA jijini. Wakati Maugo anashinda kwa pointi, bondia nyota nchini,Ibrahim Class alidhihirisha ubora wake baada ya kushinda kwa Technical knockout (TKO) raundi ya tano katika uzito wa Super Feather.

Pambano hayo yaliandaliwa kwa lengo la kutafuta mataulo ya kike kwa wanafunzi wa mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwa kushirikiana na taasisi ya She Can Foundation. Katika pambano hilo lililoandaliwa na promota wa kwanza wa kike nchini, Sophia Mwakagenda wa kampuni ya Lady In Red Promotion, Maugo alipata pointi 77-75 kutoka kwa jaji, Mwinyi Milla,  78-74 (Modesti Rashid) na 76-76 kutoka kwa jaji, Chaurembo Palasa.
Bondia Mada Maugo (kulia) akirusha konde kwa Charles Misanjo wa Malawi katika pambano la kimataifa la uzito wa Super Middle lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA juzi. Maugo alishinda kwa pointi.

Pamoja na ushindi huo ulilalamikiwa na Misanjo na baadhi ya mashabiki wa ngumi za kulipwa, Maugo alisema kuwa Mmalawi alikuwa anapiga makofi baadala ya ngumi ndiyo maana ameonekana kushambulia sana.

“Mimi nimekuwa nikipigana kwa kutafuta pointi kwa kupiga ngumi, yeye alikuwa anapiga makofi muda wote na kusukuma, hao mashabiki na bondia inaonekana hawajui ngumi, sijapendelewa kwa sababu ya Utanzania, hapana,” alisema Maugo.

Misanjo alisema kuwa haikuwa ngumi za kawaidi bali ni vita. “Matokeo sikubaliani nayo, yanaua mchezo wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania, itatufanya tusiwe tunakuja kupigana kutokana na maamuzi kama haya,” alisema Misanjo. Pambano kati ya Ibrahim Class na Baina Mazola ndilo lilikuwa na msisimko mkubwa ambapo mabondia hao walionyesha uwezo mkubwa. Class alianza pambano kwa kasi na kutawala raundi mbili za mwanzoni huku Mazola alikitawala raundi ya tatu.
Bondia Ibrahim Class (kushoto) akimchapa ngumi mpinzani wake, Baina Mazola katika pambano la uzito wa Super Feather kwenye ukumbi wa PTA juzi.Class alishinda kwa technical knockout (TKO) raundi ya tano.

Mabondia hao walipigana kwa visasi na kuleta burudani ya aina yake. Class alionekana kutumia uzoefu zaidi na kufanikiwa kumchana jicho Mazola katika dakika ya 1.47 ya raundi ya tano na kuibuka mshindi.

“Nimepoteza kwa kuumia, hata hivyo nitamtafuta tena Class ili kuonyesha kuwa mimi ni bora zaidi yake,” alisema Mazola. Class alisema kuwa mpinzani wake ni mzuri na ushindi ni jambo la kawaida sana kwake.

“Mimi ni bondia bora, hilo halina ubishi,Mazola bado sana kwangu, afanyekazi ya zaida kunifikia na kunishinda,” alitamba Class.

Bondia Flora Machela alifanikiwa kushinda kwa TKO raundi ya tano dhidi ya Sarafina Julius katika pambano la uzito wa bantam wakati Asha Ngedere na Happy Daudi wakitoka sare kwa katika pambano la  uzito wa Super Light.

Akizungumza baada ya pambano hilo, promota Mwakagenda aliwapongeza wadau na makampuni yaliyochangia kufanikisha tukio hilo japo lengo la kukusanya mataulo 40,000 halijafanikiwa.

“Huu ni mwanzo na jambo hili ni geni kwangu, ndiyo kwanza nimeandaa ngumi za kulipwa na nimeona changamoto zake, nimejifunza na nitaendelea kuandaa kwa malengo maalum,” alisema Mwakagenda.
Mabondia wa kike, Asha Ngedere (kushoto) na Happy Daudi wakipambana uliongoni. Mabondia hao walitoka sare.

MAKAMU WA RAIS AONDOKA NAMIBIA KUREJEA TANZANIA

$
0
0


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Waziri wa Elimu ya Juu , Mafunzo na Ubunifu wa Namibia Mhe. Dkt. Itah Kandjii-Murangi muda mfupi kabla ya kupanda ndege katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akielekea kupanda ndege katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiaga Viongozi waliomsindikiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

VIONGOZI NA WATUMISHI NCHINI WAKUMBUSHWA KUTEKELZA MAJUKUMU YAO KWA KUTANGULIZA MBELE MOYO WA UZALENDO NA MASILAHI YA TAIFA

$
0
0

Viongozi na Watumishi nchini wamekumbushwa kutanguliza mbele moyo wa uzalendo na masilahi mapana ya taifa wanapotekeleza majukumu yao ili kupeleka maendeleo ya taifa mbele na kuimarisha usalama wa taifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati akifunga kozi fupi ya tano kwa viongozi iliyofanyika Chuo cha cha Taifa cha Ulinzi – Tanzania (NDC) jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mkuchika amesema, ni matumaini kuwa washiriki waliohudhuria kozi hiyo, utendaji wao wa kazi utabadilika kwa kuwa na tija kwani sasa mbinu zote zinazohusu namna ya kufikiri kimkakati, kufanya tathmini katika mambo mbalimbali ili kufikia maamuzi wamezipata.

“Sasa mnatambua dhana ya usalama wa Taifa vema na kwa mapana zaidi, si kulinda mipaka na mali za wanajamii tu, bali pia inahusisha kutunza mazingira, kuwa na chakula cha kutosha, kupiga vita rushwa na madawa ya kulevya na mengine mengi ambayo ninyi mnayafahamu zaidi,” Mhe. Mkuchika amesema na kuongeza kuwa usalama wa watu ni muhimu kuliko jambo jingine lolote, hivyo masuala ya usalama yawe ni sehemu ya kuzingatia katika utendaji wa kila siku na hasa pale maamuzi yanayogusa masilahi ya nchi na jamii yanapotolewa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akipokea zawadi ya tai, kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Luteni Jenerali, Paul Massao, baada ya kufungua kozi fupi ya tano ya Viongozi, iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akimtunuku cheti Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James baada ya kuhitimu kozi fupi ya tano ya Viongozi iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na washiriki wa kozi fupi ya tano ya Viongozi, iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi, jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira akitoa neno la shukrani baada ya kuhitimu kozi fupi ya tano ya Viongozi katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi, jijini Dar es Salaam.


RAIS DKT. MAGUFULI AHANI MSIBA WA BI. PATRICIA MAZIGO, CHATO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akizungumza na wanakijiji wa Rubambagwe plot (Chato) wakati alipokwenda kutoa pole kwenye msiba wa Patricia Tibengana Mazigo (75) aliyefariki juzi tarehe 16-8-2018 Chato mkoani Geita. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwafariji wafiwa wakati alipokwenda kutoa pole kwenye msiba wa Patricia Tibengana Mazigo (75) aliyefariki juzi tarehe 16-8-2018 Chato mkoani Geita.


Naibu Spika Baraza la Wawakilishi Aongoza Ujumbe wa Zanzibar Mkutano wa 49 Mabunge Wanachama Nchi za Jumuiya ya Madola, Botswana

$
0
0
Makamu wa Rais wa Botswana Mhe Slumber Tsogwane akipata picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati Tendaji na viongozi mashuhuri huko Gaborone Botswana.  
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar akibadilishana mawazo na Mhe Maria Ndilla Kangoye ambae ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Kanda ya Afrika na pia Mbunge wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. 
Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Mabunge wanachama wa nchi za Jumuiya ya Madola tawi la Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said pamoja na Katibu wa tawi hilo ambae pia ni katibu wa Baraza la Wawakilishi Raya Msellem wakisikiliza mada zinazojadiliwa. 
Mwenyekiti wa kamati tendaji ya nchi wanachama wa mabunge ya nchi za Jumuiya ya Madola Mhe Simai Mohammed Said akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Baraza kutoka Rodrigues Regional Assembly Mauritius Mhe Marie Pricie Anjela Speville, katikati ni Makamu wake Mhe Ramdally Jean Rex. 

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

CCM YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA DADA WA RAIS DKT JOHN MAGUFULI

NEWZ ALERT:DADA WA RAIS DKT MAGUFULI AFARIKI DUNIA

$
0
0
Bi.Monica Joseph Magufuli enzi za uhai wake

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM PEMBA LEO

$
0
0
NA IS-HAKA, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema CCM inaendelea kuimarika na hakuna Chama chochote cha kisiasa nchini kinachoweza kushindana nacho katika uringo wa siasa za ushindani wa sera za maendeleo kwa wananchi wa makundi yote.

Kauli hiyo aliitoa mara baada ya kuwasili kisiwani Pemba katika mwendelezo wa ziara yake ya kujitambulisha ambapo amezungumza na wanachama mbalimbali katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari ya Fidel Castro Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kutokana na uimara huo hakuna chama kingine mbadala wa Chama Cha Mapinduzi kinachoweza kushuka kwa wananchi nyumba kwa nyumba na kuratibu kero zao kisha kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

Dk.Bashiru aliwahakikishia wanachama na viuongozi hao kuwa CCM bado ipo imara na itapata ushindi wa kihistoria mwaka 2020 kwa nchini nzima kuliko ushindi unaopatikana kwa sasa katika uchaguzi mdogo unaoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.
 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally Akizungumza na wanachama na viongozi wa CCM wa Mikoa miwili ya Pemba katika ukumbi wa skuli ya Fidel Castro.
 Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndugu Mberwa Hamad Mberwa akimpa tia Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru zawadi ya ndizi ya mkono wa Tembo.
  KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akitembea kuelekea ofisi ndogo ya CCM Chake chake mjini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM Tanzania akisalimiana na mwanachama mpya kutoka chama cha CUF aliyejiunga na CCM Amina Juma Nassoro

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

SERIKALI YA ZANZIBAR YAKABIDHI FEDHA ZA FIDIA KWA WANANCHI.

$
0
0
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekabidhi Fedha za fidia kwa Wananchi waliopisha Ujenzi wa Karantini ya Mifugo katika eneo la Nziwengi katika Jimbo la Gando liliomo ndani ya Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Fedha hizo zilizotolewa na Serikali na Kukabidhiwa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi zimelengwa kwa Wakulima 40 waliokuwa wakiendesha shughuli zao za Kilimo na Mifugo katika eneohilo linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa Hekta 60.9.

Akikabidhi fedha hizo kwa Wakulima hao, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema subra iliyofanywa na Wakulima hao wa Jimbo la Gando hatimae imeleta neema itakayowaenea Wananchi wa jimbo hilo hasa wakati huu wa kuelekea kwenye Siku Kuu ya Iddi El – Hajj.

Balozi Seif aliwaasa na kuwakumbusha Wakulima na Wananchi hao wa Gando wawe makini katika matumizi ya fedha walizokabidhiwa kuzilenga kwenye uanzishaji wa shughuli za Kilimo walizokuwa wakizifanya katika maeneo mengine.

“ Nimefarajika kushuhudia kitendo hichi cha ulipaji wa fidia kwa wakulima wa Gando nikiwa kama Mwakilishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Kazi hii”. Alisema Balozi Seif.Alieleza kwamba Serikali Kuu katika kushajiisha Kilimo Nchini imeanza kutoa Miche ya Minazi bure kuwapa Wakulima katika maeneo mbali mbali kama inavyofanywa kwa Miche ya Mikarafuu.

Akitoa Taarifa fupi ya ujenzi wa Karantini ya Mifugo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Nd. Ahmad Kassim Haji alisema eneo la Gando lilikuwa likikumbwa na miripuko ya Maradhi mengi yanayotokana na uingizwaji wa Mifugo kiholela.

Mkurugenzi Mkuu wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar Nd. Makame Haji Kushoto akimuonyesha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ramani ya Ujenzi wa Nyumba za Wahanga wa Mvua za Masika zilizopita zinazotaka kujengwa katika Kijiji cha Tumbe Mkoa wa Kaskazini Pemba,
Balozi Seif akimkabidhi Mkulima Bibi Safia Hamad Khamis wa Kijiji cha Gando Hundi ya Fedha kwa ajili ya Fidia ya mazao yao ili kupisha Ujenzi wa Karantini ya Midugo kwenye eneo la Nziwengi.Kulia ya Balozi Seif ni Mkuu wa Mkoa Kaskazini Pemba Mh. Omar Khamis Othman na kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Kilimo Mh. Rashid Ali Juma na Naibu Wake Dr. Makame Ali Ussi.
Balozi Seif akimkabidhi Hundi Bwana Ali Khamis Ali kwa ajili ya ulipwaji wa fidia ya mazao yao ili kupisha Ujenzi wa Karantini ya Midugo kwenye eneo la Nziwengi.Picha na – OMPR – ZNZ.


DC JERRY MURO AAHIDI KUSIMAMIA UBORA WA ELIMU ARUMERU, AMSHUKURU RAIS KWA KUTOA PIKIPIKI KWA WARATIBU WA ELIMU

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya Arumeru mkoani Arusha Jerry Muro amemshukuru Rais Dk.John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kutoa vitendea kazi kwa lengo la kuboresha sekta hiyo huku akiahidi kusimamia ubora wa elimu.

Muro amesema hayo wakati anakabidhi Pikipiki mpya 18 kwa waratibu wa elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambazo zimetolewa na Rais kupitia Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, ikiwa sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Tano Chini ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ya kufuatilia Ubora wa Elimu Nchini.

"Tunashukuru kwa vitendea kazi hivi ambavyo tumepewa na Rais kupitia Waziri wa Elimu.Tunaamini vitendea kazi hivi vitatumika kwa lengo ambalo limekusudiwa.

" Tutahakikisha tunainua kiwango cha ufaulu katika Halmashauri yetu ya Arumeru pamoja na kuinua kiwango cha elimu.Lengo ni kuhakikisha mtoto wa maskini anapata elimu iliyo bora,"amesema.

Amefafanua kuwa kupatikana kwa pikipiki hizo na kisha kuzigawa kwa waratibu wa elimu wilayani huo kunatoa nafasi ya wao kutimizamajukumu yao ya kufuatilia ubora wa elimu katika shule za Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh.Jerry Muro akiwa na baadhi ya piki piki alizowakabidhi Waratibu wa elimu katika halmashauri ya wilaya ya Meru

WATUMISHI WA SERIKALI WAHIMIZWA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII

$
0
0
 
NA LUSUNGU HELELA-DODOMA .

Mkurugenzi wa Utawala na Raslimali Watu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Lusius Mwenda ametoa wito kwa watumishi wa Serikali kuwa mstari wa mbele kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa ajili ya kujifunza mambo mapya ikiwa pamoja na kupumzisha akili. 

Pia amewataka watumishi hao kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio hivyo ili waweze kuona na kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi ambazo wanaweza kuanza kuzifanya kwa ajili ya kujiingizia kipato ikiwa ni njia mojawapo ya kuanza kujiandaa kwa ajili ya kustaafu. 

Amefafanua kuwa kila mtumishi wa Serikali anatakiwa kuanza kujiandaa kwa ajili ya kustaafu kuanzia ile siku ya kwanza aliyoajiriwa. Amesema watumishi walio wengi mara baada ya kustaafu hali zao za kiuchumi huteteleka kwa vile katika kipindi cha utumishi wao walikuwa hawatembelei maeneo tofauti na yale waliyoyazoea kwa ajili ya kujifunza na kukutana na watu tofauti. 

Ametoa Rai hiyo jana katika kituo cha utalii Kolo kilichopo wilayani Kondoa mkoani Dodoma alipokuwa ameongozana na Watumishi zaidi ya 50 kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii , Ikiwa ni moja ya jitihada za Wizara hiyo kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watumishi wa Serikali kwa kuanza na Watumishi wa Wizara yenye dhamana. Kivutio cha Utalii, Kolo kipo ni kivutio mashuhuri sana kwa michoro yake ya miambani kwa vile inafanana na michoro ya Afrika Kusini na kimebeba tamaduni za waafrika. 

” Tunataka Watumishi muwe mabalozi wazuri kuanzia kwenye ngazi ya familia hadi ngazi ya taifa kwa kuhamasisha jamii kuona umuhimu wa kutembelea vivutio vya utalii ikiwemo maeneo ya kihistoria ambavyo yamesheheni chimbuko la tamaduni zetu pamoja na harakati za binadamu katika kupambana na mazingira yake.” alisema .

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Lusius Mwenda (kushoto) akiwa ameongoza na Watumishi zaidi ya 50 wa Wizara hiyo wakipanda kilima kwenda kuangalia michoro ya miambani katika kituo cha Utalii cha Kolo kilichopo wilayani Kondoa mkoani Dodoma jana ikiwa lengo la ziara hiyo ni kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watumishi wa Serikali. Wa pili ni Mkuu wa Kituo cha Kolo, Zuberi Mabie. 
Mkuu wa Kituo cha Utalii, Kolo chenye michoro ya miambani, Zuberi Mabie akiwa na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii akiwaonesha michoro ya miambani katika kituo cha Utalii cha Kolo kilichopo wilayani Kondoa mkoani Dodoma jana ikiwa lengo la ziara hiyo ni kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watumishi wa Serikali.

Mkuu wa Kituo cha Utalii, Kolo chenye michoro ya miambani, Zuberi Mabie akizungumza na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakati walipotembelea kituo cha michoro ya miambani, Kolo kilichopo wilayani Kondoa wakati walipotembelea katika kituo hicho ikiwa la lengo la ziara hiyo ni kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watumishi wa Serikali. 


MCHENGA BBALL STARS AANZA KUTETEA UBINGWA WA SPRITE BBALL KINGS

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mabingwa watetezi wa michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings, Mchenga Bball Stars wamefanikiwa kuondoka na ushindi wa kwanza katika hatua ya fainali, baada ya kushinda game 1 kwenye 'Best of five' dhidi ya wapinzani wao Flying Dribblers.

Mchezo huo uliochezwa mwishoni mwa wiki huu kwenye uwanja wa taifa wa ndani uliweza kuwa wa ushindani mkubwa sana huku mabingwa watetezi wakitawala zaidi katika quarter zote nne na kufanikiwa kushindwa kwa pointi 103 dhidi ya 73 vya Flying Dribblers.

Mchenga walianza mchezo huo kwa kasi wakishinda quarter ya kwanza kwa pointi 27 dhidi ya 10 za Flying Dribblers kabla ya kuendelea kuongoza kwa pointi 62 kwa 25 hivyo kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa tofauti ya pointi 37. Katika quarter hizo mbili mchezaji Baraka Sadick alifunga pointi 32. 

Baada ya mapumziko Mchenga walirejea kwa kasi tena na kuongoza kwa pointi 62 dhidi ya 44 za Flying Dribblers. Mabingwa hao watetezi waliendelea na moto wao katika quarter ya 4 na kufanikiwa kufikisha pointi 100 ambapo hadi mwisho wa mchezo wakaongoza kwa pointi 103 kwa 73.

Katika mchezo huo mchezaji Baraka Sadick wa Mchenga Bball Stars ameibuka kinara wa jumla kwa kufunga pointi 48, Assist 6 na kuchukua rebound 4. Amefuatiwa na mchezaji Baraka Mopele wa Flying Dribblers ambaye amefunga pointi 29 na rebound 4.

Game 2 ya michuano hiyo inayodhaminiwa na kinywaji cha Sprite, itachezwa Jumatano Agosti 22, 2018 kwenye viwanja vya Don Bosco Oysterbay. Mechi hizi zinaweza kwenda hadi game 5 endapo Flying Dribblers watarejea na kusawazisha katika game 2 na zinazofuata.

Mshindi wa mashindano hayo atanyakua kitita cha Shilingi Milioni 10 pamoja na Kikombe, Mshindi wa pili Milioni 3 na mchezaji bora MVP kupata milioni 2.
Mchezaji wa timu ya Flying Dribblers, Steve Mtemihonda (kushoto), akimiliki mpira huku akizongwa na mchezaji wa timu ya Mchenga Stars, Mohamed Yusuph, wakati wa mchezo wa kwanza wa fainali ya mpira wa Kikapu Sprite Bball Kings, uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa wa ndani. Mchenga alishinda pointi 103 dhidi ya 73 za Flying Dribblers.
Mchezai wa timu ya Mchenga Stars, Baraka Sadick (kulia) akimiliki mpira huku akizongwa na wachezaji wa timu ya Flying Dribbers wakati wa mchezo wao wa kwanza wa fainali ya mpira wa kikapu Sprite Bball Kings uliofanyika Uwanja wa ndani wa Taifa Dar es Salaam. Mchenga alishinda pointi 103 dhidi ya 73 za Flying Dribblers.

WFP YAADHIMISHA SIKU YA MISAADA KWA KUELEZEA MAFANIKIO NA MAHITAJI

$
0
0


SHIRIKA la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema kwamba kutoka mwaka 2010 imeingiza katika uchumi wa Tanzania zaidi ya dola za Marekani milioni 278 kutokana na huduma mbalimbali inazotoa kusaidia wakimbizi ambao wapo nchini.

Aidha fedha hizo zimeingia katika mfumo wakati Tanzania inatumika kama kituo cha lojistiki kusaidia maeneo mengine ya ukanda wa Afrika Mashariki wenye matatizo.

Hayo yamesemwa katika maadhimisho ya Siku za msaada duniani, inayokumbukwa kuadhimisha mauaji ya watoa misaada wakati wa mashambulio ya anga ya Baghdad, Irak miaka kadhaa iliyopita.

Aidha siku hiyo inaadhimishwa Agosti 19 kila mwaka kutoa neno kwa jamii ya dunia kuwakumbuka watoa misaada ambao wapo katika hatari ya maisha kutokana na vurugu zinasumbua duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mwakilishi Mkazi wa WFP nchini Tanzania, Michael Dunford alisema kwamba kumekuwepo na uingizaji mkubwa wa fedha katika uchumi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na kuwa na kusaidia chakula kwa wakinbizi waliopo nchini Tanzania kwa kusaidiana na mashirika mengine.

Kwa Tanzania kwa sasa inahifadhi wakimbizi 297,000 kutoka Burundi na Kongio (DRC) katika maeneo ya Nyarugusu, Nduta na Mtendeli mkoani Kigoma .
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Michael. Dunford.

Rotary Dar Marathon yaadhimisha miaka kumi ya kubadilisha maisha

$
0
0

Tukio maarufu la riadha la Rotary Dar Marathon ambalo hufanyika siku ya 14 Oktoba – siku ya Nyerere kila mwaka tangu 2009 litaadhimisha mwaka wa kumi tangu kuanza kwa tukio hilo.

Dhima ya Rotary Dar Marathon inaendelea kuwa "ponya maisha, badilisha jamii” na ni katika mwaka wa tatu tangu RDM imeanza kukusanya fedha kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za hospitali ya (CCBRT) kuwa na mradi wa hsopitali binafsi ili waweze kupunguza gharama ya hudua za ulemavu zinazotolewa na hospitali hiyo kwa wana jamii. 

 Fedha zote zitakazokusanywa mwaka huu kutokana na tukio la RDM zitakabidhiwa kwa CCBRT ili kukamilisha ujenzi wa kliniki hiyo binafsi na manunuzi ya vifaa husika.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya maandalizi, mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Rotary Dar Marathon, Rotarian Catherinerose Barreto, alisema kwamba kamati inayojumuisha wajumbe kutoka klabu nane za Rotary za jijini Dar es Salaam imeshaanza maandalizi kuhakikisha mwaka huu RDM inakuwa tukio ambalo ni la ubora wa hali ya juu. Aliongeza pia mlezi wa RDM Mheshimiwa Rais mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi atakuwepo na kushiriki matembezi ya siku hiyo.

Tukio la Rotary Dar Marathon (RDM) licha ya kulenga lengo msingi la kuchangisha fedha kusaidia shughuli mbalimbali ili kuboresha ubora wa maisha kwa jamii zetu pia linahakikisha kutoa tukio lenye ubora wa kimataifa na la kufurahiwa na wanaoshiriki katika mbio au matembezi.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Rotary Dar Marathon, Catherinerose Barretto (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kutangaza maandalizi ya mbio na matembezi ya hisani ya Rotary Dar iliyofanyika wikiendi hii jijini Dar es salaam. Mashindano hayo yanatarajia kutimua vumbi, Oktoba 14 mwaka huu ambapo pia Rotary Dar Marathon itasheherekea kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake 2008.
Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya Rotary Dar Marathon, Hawa Mkwela akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza maandalizi ya mbio na matembezi ya hisani ya Rotary Dar iliyofanyika wikiendi hii jijini Dar es salaam. Mashindano hayo yanatarajia kutimua vumbi, Oktoba 14 mwaka huu ambapo pia Rotary Dar Marathon itasheherekea kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake 2008.
Mwenyekiti wa bodi ya Rotary Dar Marathon, Sharmila Bhatt akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza maandalizi ya mbio na matembezi ya hisani ya Rotary Dar iliyofanyika wikiendi hii jijini Dar es salaam. Mashindano hayo yanatarajia kutimua vumbi, Oktoba 14 mwaka huu. Rotary Dar Marathon inatarajia kuwavutia washiriki 16,000 kwa mwaka huu.
Wajumbe wa kamati ya maandalizi ya Rotary Dar Marathon wakifurahia jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika wikiendi hii jijini Dar es Salaam ambapo walitangaza rasmi maandalizi ya matembezi hayo kwa mwaka huu yanayotarajiwa kufanyika tarehe Oktoba 14, mwaka huu. Mbio za Rotary Dar zitaanza na kuishia katika viwanja vya ‘The Green’, Oysterbay.

 

MICHUZI MEDIA GROUP YATOA SALAMU ZA POLE KWA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI KWA KUFIWA NA DADA YAKE

$
0
0
MICHUZI MEDIA GROUP INATOA SALAM ZA POLE KWA FAMILIA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KUFUATIA KIFO CHA DADA YAKE MPENDWA BI.MONICA JOSEPH MAGUFULI KILICHOTOKEA TAREHE 19/08/2018 WAKATI AKIPATIWA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA BUGANDO JIJINI MWANZA

MICHUZI MEDIA GROUP INAUNGANA NA FAMILIA YA RAIS DKT. MAGUFULI KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU CHA KUONDOKEWA NA DADA YAO MPENDWA. INAWAOMBEA WAWE NA MOYO WA SUBIRA NA KUMTANGULIZA MUNGU KATIKA KILA JAMBO.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA. 
JINA LA BWANA NA LIHIMIDIWE - AMINA

TAARIFA KWA UMMA

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
 
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ndugu January Makamba (Mb), leo anaanza ziara ya mikoa 19 nchini, ambayo itafanyika kwa awamu tatu. Ziara hiyo inamadhumuni yafuatayo:- 

1. Kukagua, kutathmini na kuzungumza na viongozi, wataalam, watendaji na wananchi wa mikoa husika kuhusu maeneo yanayopendekezwa kuhifadhiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira. 

Kama inavyofahamika, Sheria ya Mazingira, hasa vifungu vya 47, 51, 54, 56, na 58 (3), inatoa mamlaka kwa Waziri mwenye dhamana ya mazingira kutangaza, kutamka au kuamuru, kupita kwenye Gazeti la Serikali, baadhi ya maeneo nchini kuwa ni Maeneo Lindwa Kimazingira (Environmental Protected Area) au Maeneo Nyeti Kimazingira (Environmental Sensitive Area). 


Nyenzo hizi zimewekwa ili kuyalinda maeneo muhimu kwa mifumo ya kiikolojia (ikiwemo vyanzo vya maji, mito, maziwa, mabwawa, milima na vilima, chemichemi, ardhi oevu, mazalia ya samaki, misitu, nk.) ambayo hayana ulinzi wa Sheria nyingine. Sheria imeweka vigezo kwa maeneo hayo.

 Ofisi ya Makamu wa Rais, kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), iliomba na kupokea kutoka katika Halmashauri mbalimbali nchini mapendekezo ya maeneo hayo. Jumla ya maeneo 77 yalipendekezwa, ikiwemo vyanzo muhimu vya maji, mazalia ya samaki na wanyama adimu, maeneo ya ardhi oevu, mabwawa, mito na chemichemi nyeti. Mikoa iliorodhesha maeneo hayo kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na Sheria. Katika awamu ya kwanza, maeneo takriban 20 yanatarajiwa kuhifadhiwa kwa kutumia Sheria ya Mazingira. 

Katika ziara yake, Ndugu Makamba anatarajia kuyaona maeneo hayo, kutathmini hoja na haja ya kuyahifadhi na kuzungumza na viongozi wa mikoa, halmashauri na wananchi katika maeneo hayo ilikubaini utayari na uwezo wao katika kusimamia uhifadhi mara maeneo hayo yatakapotangazwa. Vilevile, katika ziara hiyo, Ndugu Makamba atapokea mapendekezo ya maeneo mapya hasa pale ambapo mapendekezo yaliyotolewa awali hayakutokana na ushirikishwaji mpana. Orodha ya maeneo yanayopendekezwa itatolewa kadri ziara inavyoendelea katika kila mkoa. 


Viewing all 110137 articles
Browse latest View live




Latest Images