Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110164 articles
Browse latest View live

UONGOZI MPYA WA CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE WAMTEMBELEA JAJI MKUU

$
0
0

Na Magreth Kinabo, Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma amekitaka Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kufanya tafiti katika baadhi ya Sheria ambazo zinahitaji marekebisho ili kuweza kuongeza uzito wa mabadiliko hayo.

Mhe. Jaji Mkuu aliyasema hayo mapema Agosti 17, alipotembelewa na wajumbe wapya wa Baraza la Uongozi wa TAWLA, ambao waliongozwa na Mwenyekiti wao, Bi. Athanasia Soka na Mkurugenzi wa TAWLA, Bi. Tike Mwambipile, waliofika kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.

Akizungumzia kuhusu mabadiliko hayo ya Sheria, Jaji Mkuu alisema yanawezekana kufanyika endapo utatifi wa kina utafanyika ili kuongeza uzito wa mabadiliko hayo, “ni vizuri unapotaka kufanya mabadiliko kisheria kufanya utafiti ,tunaweza kufanya kwa kushirikiana,” alisema Jaji Mkuu.

Awali akizungumzia kuhusu mabadiliko ya Sheria yanayohitajika, Mkurugenzi huyo wa TAWLA, Bi. Tike Mwambipile, aliitaja Sheria ya ndoa.

“Katika sheria hii mathalani kumekuwa na mgawanyo wa mali usio sawa hususani pale ambapo mwanaume inapothibitishwa ndiye anamiliki mali hupata asilimia nyingi na mwanamke hupata asilimia chache wakati ikithibitika mwanamke ndiye anamiliki mali hugawanywa asilimia 50 kwa asilimia 50,” alisema Bi. Mwambipile. 

Mhe. Jaji Mkuu akipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa TAWLA, Bi. Athanasia Soka. 
Mhe. Jaji Mkuu akikabidhi zawadi mbalimbali kwa Mwenyekiti wa TAWLA, Mhe. Jaji Mkuu pia amewapatia nakala za Mpango Mkakati wa Mahakama. 
Mhe. Jaji Mkuu akikabidhi zawadi mbalimbali kwa Mwenyekiti wa TAWLA, Mhe. Jaji Mkuu pia amewapatia nakala za Mpango Mkakati wa Mahakama. 


SPIKA AONGOZA KIKAO CHA MAFUNZO KAMATI YA UONGOZI ZANZIBAR

$
0
0


Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha mafunzo kwa Kamati ya Uongozi, Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge. Kikao hicho kinaendelea kwa siku ya pili katika Ofisi ya Ndogo ya Bunge Zanzibar.anayefuata ni Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Pandu Kificho, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu, Mhe. Jenister Mhagama, Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai, Naibu Spika, Mhe. Dkt. Tulia Ackson na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha mafunzo kwa Kamati ya Uongozi, Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge kinachoendelea kwa siku ya pili katika Ofisi ya Ndogo ya Bunge Zanzibar.
Wajumbe wa Kamati ya Uongozi, Makamu Wenyeviti na Wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge wakimsikiliza mtoa mada kutoka Idara ya Usalama, Ndugu Mluli Mahendeka katika semina ya kuwajengea uwezo inayofanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge, Zanzibar. Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha mafunzo cha mafunzo hayo.

RC MAKONDA AFURAHISHWA NA MKAKATI WA TCRA KUWEKA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI,POSTIKODI DAR ES SALAAM.

$
0
0


 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo amefungua semina ya kimkakati inayolenga kulifanya jiji la Dar es salaam kuwa katika mpangilio wa kisasa na kuhakikisha mitaa yote inawekwa katika mfumo wa anwani za makazi na Postikodi Kama ilivyo kwa majiji makubwa ulimwenguni.

RC Makonda amesema Mfumo huo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi kwakuwa utarahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo kuwezesha kila mwananchi kuwa na anwani, kuwasaidia wageni kujua maeneo, kudhibiti wezi na matapeli, ulinzi na usalama, kusaidia kampeni ya usafi pamoja na kusaidia Jeshi la zimamoto na uokoaji kufika haraka kwenye eneo lenye dharura Kama ajali ya Moto au nyinginezo na kuokoa maisha.

Aidha RC Makonda amewapongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa kuzifikia Kata 45 Kati ya 102 za mkoa huo na kueleza kuwa atawapatia ushirikiano wa kutosha kuhakikisha Mfumo wa anwani za makazi na Postikodi unafikia jiji Zima.Pamoja na hayo RC Makonda amewaomba TCRA kupeleka elimu hiyo kwa Madiwani na wenyeviti wa mitaa ili kuwajengea uelewa.

Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi unalenga kuhakikika kila Eneo, Kata na Mtaa vinapewa majina na kila nyumba inakuwa na namba ya utambuzi.
CHO2

KATIBU MKUU CCM AAMUA KUWAJIBU UBALOZI WA MAREKANI NCHINI TANZANIA

$
0
0

*Awataka Marekani kuheshimu uhuru kamili wa Taifa letu
*Asema chaguzi hizo zimefanyika kwa misingi ya kisheria

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Dk.Bashiru Ally ameamua kutoa msimamo wa Chama hicho kuhusu taarifa iiliyotolewa na Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kuhusu uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu pamoja na kata 71 uliofanyika hivi karibuni.

Baada ya kufanyika kwa uchaguzi huo ambao CCM imepata ushindi mkubwa , Ubalozi wa Marekani waliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya habari wakionesha kutoridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo.

Hivyo Dk.Bashiru Ally leo amezungumzia taarifa hiyo ya Ubalozi wa Marekani ambapo amesema ameisoma na kuilewa na wao kama Chama wanazingatia zaidi uhuru wa kitaifa na wanayo dhama ya kuulinda.

“Kauli ambayo wameitoa inagusa maeneo mengi na matarajio yangu taasisi zote zinazohusika zitazingatia madukuduku yao.

“Ninachojua mimi chaguzi hizi zimefanyika kwa misingi ya kisheria na mataifa mengine likiwamo la Marekani wanapaswa kuheshimu chaguzi zetu,”amesema Dk.Bashiru Ally.Mbali ya kauli hiyo ya Dk.Bashiru pia wachambuzi waliobobea kwenye medani za siasa nchini akiwamo Dk.Benson Banna wameonesha kusikitishwa na taarifa hiyo ya ubalozi wa Marekani nchini.

ELIM MSINGI KUENDELEA KWA MIAKA7

$
0
0
JOSEPH MPANGALA -MTWARA.

Serikali imesema Imefuta Mpango wa Kufanya Elimu ya Msingi Kuishia darasa la Sita Kutokana na Kuonekana Mfumo wa Kuishia Darasa la Saba Hauna matatizo Yoyote na Umeendelea Kufanya Vizuri kwa Wanaomaliza.

Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha mara baada ya Kumaliza kutembelea Chuo cha Ualimu Kitangali Kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara.Ole Nasha Amesema Mpango wa Elim ya Msingi Kuishia darasa la Sita Ulikuwepo lakini baada ya Kupokea mawazo Wameamua Kuacha kama Ilivyo.

“Kulikuwa na Mpango wa kujaribu kufanya sasa Elimu ya msingi iishie darasa la Sita iwe miaka sita lakini kwa sasa hakuna huo Mpango tumerudi kwenye mfumo wetu wa kawaida kwa sababu moja tu hakuna kitu kilicho haribika, kila mtu aliyesoma Nchi hii amesoma kwa mfumo ule hatujaona kama unamapungufu yoyote kwa hiyo tutaendelea na utaratibu wetu wa Miaka Saba”amesema Ole Nasha

Aidha Naibu waziri amewataka Makandarasi wanaojenga Katika Mradi wa Chuo Cha Kitangali Kuhakikisha wanamalizia Ujenzi Pindi watakapo pata Pesa Kutoka serikalini.

“Mimi ninaloondoka nalo hapa ni kwenda kuhakikisha kwamba Fedha Yaani Certificate hizo ambazo zimetoka karibuni kwamba zinalipwa mapema, Rai yangu kwenu Jamani Mradi huu umechukua muda mrefu,karibia miaka miwili kwa hiyo fedha zikilipwa kila mmoja ajitahidi huu Mradi sasa uishe na ukabidhiwe ili lengoletu lile na chuo kuweza kudahili Wanafunzi wengi zaidi Liweze Kufikia”Amesema Ole Nasha..

Mradi wa Ujenzi wa Chuo cha Ualimu kitangali Unagharimu Shilingi billioni 8 lakini mpaka sasa Wakandarasi wamekwisha Pewa Shilingi Billion 3.2 jambo ambalo limepelekea Mradi huo Kuchukua Miaka 2 Kushindwa Kumalizika.
Kulia Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akiwa na Mkuu wa Chuo Cha mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Mtwara Samweli Kibehele wakati wa ziara ya kutembelea Chuo hicho kwa lengo la kutazama mazingira yanayotumika kufundishia Wanafunzi wa VETA. 
Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akipewa maelezo ya Mradi wa Ujenzi wa Chuo Cha Ualimu Kitangali na Mshauri wa Ujenzi Nicodemus Mgaya katika ziara yake ya kutazama Maendeleo ya Ujenzi Huo.
Naibu waziri wa Elim Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha Akiongea na wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchii FDC ambacho kimeanzishwa mwaka 1975 ambacho kinafundisha masomo ya Umeme,Ufundi wa Magari pamoja na Ushonaji.

BRIGEDIA JENERALI MWANGELA AKAGUA MIRADI,AWAASA WATUMISHI WILAYANI SONGWE KUCHAPA KAZI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemas E Mwangela jana jioni amehitimisha ziara yake ya siku mbili Wilayani Songwe, ambapo amekagua miradi kumi ya maendeleo na kisha kuzungumza na watumishi na watendaji wa taasisi mbalimbali zilizomo wilayani humo.

Brigedia Jenerali Mwangela akiwa ameambatana na baadhi ya maafisa wa Mkoa wa Songwe akiwemo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe wametoa maelekezo yaliyohusu kuboresha utendaji kazi kwa watumishi wa Wilaya ya Songwe.

Amesema “nimegundua kila ambacho alinieleza Mkuu wa Mkoa aliyestaafu kuhusu wilaya ya Songwe ni sahihi, upungufu alio uona nami pia nimeuona, napenda kusema mlikuwa mnamuona ni yeye Mkali ila mimi nasema alikuwa Mvumilivu”.

Brigedia Jenerali Mwangela amesema hatosita kumsema na kumchukulia hatua mtendaji anayeenda kinyume na sheria na taratibu za utumishi wa umma hivyo basi watumishi hao wabadilike na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano, watembelee na kukagua miradi inayotekelezwa wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemas E Mwangela akikagua ujenzi wa Kituo cha Afya Mbuyuni Wilayani Songwe, kituo hicho kilipokea shilingi milioni 400 kutoka serikali kuu na kinatarjiwa kukamilika mwezi ujao.
Wananchi wa Kata ya Mbuyuni Wilayani Songwe wakijitolea shughuli mbalimbali za ujenzi katika Kituo cha Afya Mbuyuni ambapo serikali kuu ilitoa shilingi milioni 400 na kituo hicho kinatarajiwa kukamilika mwezi ujao.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemas E Mwangela akikagua mradi wa maji Mbuyuni ambao ulikamilika mwaka 2014 lakina bado wananchi hawapati maji kutokana na maji katika chanzo hicho kuwa na rangi mbaya, Brigedia Jenerali Mwangela amemuagiza mhandisi wa maji wilayani humo kufaya utafiti wa chanzo kingine haraka.

JAJI MZUNA NA MAJAJI WENZAKE WAKABIDHIWA RASMI OFISI YA MAHAKAMA KANDA YA ARUSHA

$
0
0
Na Catherine Francis –Mahakama Kuu Arusha

Jaji Mfawidhi mpya wa Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Mhe. Mosses Mzuna amekabidhiwa rasmi Kanda hiyo ya Mahakama na aliyekuwa Kaimu Jaji Mfawidhi, Mhe Jaji Sekela Moshi.

Makabidhiano hayo yamefanyika mapema Agosti 16 katika kikao cha utambulisho wa wahe.Majaji wapya pamoja na Jaji Mfawidhi ambayo pia yalihudhuriwa na baadhi ya Watumishi wa Mahakama.

Katika kikao hicho Mhe Jaji Moshi aliwasisitiza watumishi wa Mahakama Arusha kuendeleza ushirikiano, uwajibikaji na kufanya kazi kwa malengo kwani hiyo ndiyo sababu inayoifanya Arusha kuwa kanda ya mfano kwa mafanikio.Jaji Sekele aliendelea kuwahimiza watumishi waache kufanya kazi kwa mazoea bali wajitume kwa bidii ili kuweza kuondoa kabisa mlundikano wa kesi Mahakamani.

Kwa upande wake, Mhe Jaji Mzuna alimshukuru Mhe Jaji Moshi kwa mapokezi mazuri aliyoyaandaa yeye pamoja na viongozi wake, pia aliwaomba watumishi ushirikiano ili aweze kutekeleza majukumu yake ya kila siku.Kwa kusisitiza hilo alinukuu usemi wa mwandishi John C Maxwell usemao “VALUE TEAM LEADERSHIP ABOVE INDIVIDUAL LEADERSHIP” akiwa na maana ya kuwa uongozi mzuri ni ule wa ushirikiano na siyo wa mtu binafsi.
Aliyesimama ni Jaji Mfawidhi Mhe Jaji Mzuna akiwa anazungumza na watumishi
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Mhe Jaji Mosses Mzuna (katikati), kushoto ni aliyekuwa Kaimu Jaji Mfawidhi Mhe Jaji Sekela Moshi na Mhe. Jaji Thadeo Mwenempazi walipokuwa wakizungumza na Watumishi wa Mahakama, Kanda ya Arusha (hawapo pichani).
Mhe Jaji Thadeo Mwenempazi akizungumza jambo na Watumishi.

Madaktari Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Afrika wa nchini Marekani washirikiana kutibu wagonjwa 22 kambi maalum magonjwa ya moyo

$
0
0
Na Genofeva Matemu na Salome Majaliwa 

17/08/2018 Jumla ya wagonjwa 22 wenye matatizo ya moyo yatokanayo na mfumo wa umeme wa moyo usiofanya kazi sawasawa wamefanyiwa upasuaji mdogo na kuwekewa vifaa maalum vitakavyousaidia moyo kufanya kazi vizuri.

Matibabu hayo yamefanyika katika kambi maalum ya siku saba iliyofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mgonjwa kufanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Magonjwa ya moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Moyo Peter Kisenge alisema kambi hiyo inafanywa na madaktari wa Taasisi ya Moyo kwa kushirikiana na wenzao wa nchini Marekani kutoka Shirika la Madaktari Afrika.

Dkt. Kisenge alisema kambi hiyo ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo ambao mapigo yao yako chini kwa asilimia hamsini kwa dakika kwa kuwawekea kifaa maalum akinachosaidia mapigo ya moyo kuongezeka (Pacemaker).

“Kazi ya kifaa hiki maalum cha mfumo wa umeme wa moyo ni kuwasaidia wagonjwa wasipoteze maisha ghafla, kwani mara nyingi wagonjwa wenye matatizo ya mapigo ya moyo ambayo yako chini hufa vifo vya ghafla”, alisema Dkt. Kisenge.


Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo wa mgonjwa unavyofanya kazi kabla ya kumwekea kifaa maalum cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator – ICD) katika kambi ya matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo. 
Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiandaa vifaa vitakavyotumika katika upasuaji mdogo wa kumuwekea mgonjwa kifaa maalum cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Implantable cardioverter defibrillator – ICD) katika kambi ya matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo. 


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>


WASANII WA FILAMU WAASWA KUJUA THAMANI YA KAZI ZAO

$
0
0
Wanatasnia wa filamu na michezo ya kuigiza nchini wameaswa kujua thamani yao na kazi zao katika kulinda maadili na utamaduni wa kitanzania ili kujijengea heshima mbele ya jamii na wapenzi wa kazi zao.

Rai hiyo imetolewa leo na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Bibi. Joyce Fissoo alipokuwa akizungumza na viongozi wa Kamati ya Matukio, Maadili na Mikataba wa Chama cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni (Tanzania Drama Film Actors Association – Kinondoni) walipotembelea na kufanya kikao katika Ofisi za Bodi ya Filamu Mtaa wa Samora Jijini Dar es salaam.

Bibi. Fissoo alisema baadhi ya wanatasnia ya filamu wanaonyesha mwenendo unaokinzana na maisha na maadili ya kitanzania huku miongoni mwao wakifanya vitendo vinavyodhalilisha utu na heshima hivyo kuitia doa tasnia nzima ya filamu na michezo ya kuigiza.

“Nawapongeza Chama cha Waigizaji kwa kushirikiana na serikali katika kukemea wale wanachama wachache wanao chafua taswira ya tasnia. Ni muhimu kuendelea kuongeza nguvu katika nidhamu, matumizi ya lugha zenye staha, mavazi yanayoonyesha taswira chanya ya taifa letu; hivyo endeleeni kuiunga mkono Serikali katika hatua inazozichukua” alisema Fissoo

Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (katikati) akiongoza kikao na viongozi wa Kamati ya Matukio, Maadili na Mikataba wa  Chama cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni (Tanzania Drama Film Actors Association-Kinondoni) walipotembelea ofisi za Bodi ya Filamu kuwatambulisha viongozi wa chama hicho kwa uongozi wa Bodi ya Filamu hivi karibuni katika Ofisi za Bodi ya Filamu Mtaa wa Samora jijini Dar es salaam. 
Baadhi ya wanachama na viongozi wa Kamati ya Matukio, Maadili na Mikataba wa Chama cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni (Tanzania Drama Film Actors Association-Kinondoni) wakifuatilia taarifa iliyokua ikitolewa wakati wa kikao na Bodi ya Filamu kuwatambulisha viongozi hao hivi karibuni katika Ofisi za Bodi ya Filamu Jijini Dar es Salaam 
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (wanne kulia) katika picha ya pamoja na Wanachama na Wajumbe wa Kamati ya Matukio, Maadili na Mikataba wa Chama cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni (Tanzania Drama Film Actors Association-Kinondoni) baada ya kikao na wajumbe hao walitembelea ofisi za Bodi ya Filamu kuwatambulisha viongozi wa chama hicho kwa uongozi wa Bodi ya Filamu hivi karibuni katika Ofisi za Bodi ya Filamu Jijini Dar es salaam.

WAENDESHA MASHTAKA KUJENGEWA CHUO

$
0
0
Na Mwandishi Maalum, Dodoma 

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, inakusudia kujenga Chuo cha aina yake kwaajili ya waendesha mashtaka nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo na ujuzi wa uendeshaji wa kesi na mashauri ya jinai.

Mkurugezi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, (DPP) Bw. Biswalo Mganga amesema Chuo hicho kitajengwa eneo la Usagara. Jijini Mwanza ambako tayari hekta 25 zimeshapatika kwaajili ya ujenzi huo.

Kwa Mujibu wa DPP ujenzi wa Chuo hicho unatokana na ukweli kwamba, hakuna chuo chochote kinachotoa mafunzo ya uendeshaji na usimamiaji wa kesi za jinai na kwa sababu hiyo Ofisi yake imeona kuna haja na umuhimu wa kuwapo kwa Chuo hicho.

Alikuwa akizungumza wakati hafla ya uzinduzi wa ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, uliofanywa mwanzoni mwa wiki hii, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Jijini Dodoma

“Mhe. Waziri Mkuu, moja ya mikakati na mipango tuliyonayo ni kujenga chuo cha aina yaka katika Afrika ya Mashariki kitakachotoa mafunzo na namna ya kuendesha kesi za jinai. Tumeshapata hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekta 25 eneo la Usagara Mwanza kwaajili ya ujenzi wa chuo hicho”. Amebainisha Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka.





 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Bw. Biswalo Mganga akisalimia na Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  muda mfupi kabla ya  Waziri Mkuu kuzindua Ofisi  ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wakili Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, tukio lilofanyika kati kati ya wiki Jijini Dodoma. Katika taarifa yake DPP Mganga alieleza mpango wa Ofisi yake kujenga Chuo kitakachotoa mafunzo kwa Waendesha Mashtaka nchini. (Picha na  Habari  kwa hisani ya  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Waganga Wakuu wa Mikoa/Halmashauri Wapigwa Msasa Kuhusu Sheria ya Takwimu

$
0
0


Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini leo Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya mkutano huo ni; “Uboreshaji wa Mazingira ya Kutolea Huduma za Afya ni Msingi wa Wananchi Kuelelekea Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa Kati”.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa akizungumza alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu takwimu za afya katika Mkutano Mkuu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya leo Jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), anayeshughulikia Sekta ya Afya, Dkt. Zainabu Chaula, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ambaye ndiye mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mkutano huo, Anthony Mtaka na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya. Kauli mbiu ya mkutano huo ni; “Uboreshaji wa Mazingira ya Kutolea Huduma za Afya ni Msingi wa Wananchi Kuelelekea Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa Kati”.


Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa akizungumza alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu takwimu za afya katika Mkutano Mkuu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini leo Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya mkutano huo ni; “Uboreshaji wa Mazingira ya Kutolea Huduma za Afya ni Msingi wa Wananchi Kuelelekea Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa Kati”.
Baadhi ya washiriki wa mkutano Mkuu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini wakifuatilia mada kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) leo Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya mkutano huo ni; “Uboreshaji wa Mazingira ya Kutolea Huduma za Afya ni Msingi wa Wananchi Kuelelekea Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa Kati”.

MKUCHIKA AWATEMBELEA BAADHI YA VIONGOZI WAKUU WASTAAFU IKIWA NI SEHEMU YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE

$
0
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akiagana na Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Cleopa D. Msuya.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akifafanua jambo kwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Cleopa D. Msuya alipomtembelea nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Cleopa D. Msuya alipomtembelea nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Joseph S. Warioba alipomtembelea nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akifafanua jambo kwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Joseph S. Warioba alipomtembelea nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

JESHI LA POLISI LATAHADHARISHA WANANCHI KUHUSU WAMATAPELI WANAOTANGAZA AJIRA ZA POLISI

WAMILIKI WA VIWANDA VYA SARUJI WAAHIDI KUONGEZA UZALISHAJI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

WAMILIKI wa Viwanda vya Kuzalisha Saruji wamesema kuwa wataongeza uzalishaji wa saruji ili kuondoa hali ya upunguaji wa saruji nchini pamoja na kurudisha bei ya zamani ya saruji na sio ya 14000 pamoja na 15000.

Wamiliki wa viwanda vya Saruji waliyasema hayo wakati walipokutana na serikali kupitia Wizara ya Viwanda , Biashashara na Uwekezaji wakiongozwa na Najibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanaya walisema walikuwa na changamoto ya upatikanaji wa makaa yam awe pamoja na baadhi ya viwanda kuharibika Mitambo.

Akizungumza na wadau hao Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa wamiliki hao wazalishe saruji ya kutosheleza nchi kwanza na zaida ya saruji hiyo wauze nje ya nchi.Amesema kuwa kuuza saruji nje ya nchi ni fursa kiuchumi hivyo lazima viwanda vizalishe kwa kukidhi mahitaji ya ndani na ziada iuzwe nje, kuuza saruji nje na ndani kukawa na uhaba sio sawa.

Amesema kuwa wazalishaji wa makaa ya mawe wazalishe kwa wingi makaa hayo katika kuweza kulisha viwanda vya saruji pamoja na Tarula na Tanroad kujenga miundombinu sehemu yanakotoka makaa ya mawe.
Shirika la Taifa la Madini (Stamico) limesema kuwa litaongeza kasi katika uzalishaji wa makaa ya mawe katika miradi yake ya Kiwira pamoja na Kaburu ili kuhakikisha viwanda vya saruji vinapata makaa ya mawe ya kutosha.

Akizungumza na waandishi habari Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa Stamico , Alex Rutagwelela amesema kuwa kazi yao ni kuhakikisha wanalisha makaa ya mawe ya kutosha kwa wazalishaji wa saruji nchini.

Amesema kuwa changamoto ya viwanda vya saruji ni makaa ya mawe hivyo kasi ya uzalishaji lazima iongezeke katika kutatua tatizo la upungufu wa saruji usiwe kujirudia kwa mara nyingine kutokana na miradi mingi inayotekelezwa inahitaji saruji hiyo.

Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wazalishaji wa Saruji katika mkutano wa kujadili upungufu wa Saruji nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Profesa Joseph Bushweishaija akitoa maelezo kuhusioana na mkutano na huo kwa wadau wa uzalishaji wa viwanda vya saruji.
Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa Stamico, Alex Rutagwelela akizungumza na waandishi habari kuhusiana na stamico iliyojipanga katika uzalishaji wa makaa ya mawe .
Baadhi ya wazalishaji wa viwanda vya Saruji nchini 

MISA TANZANIA,INTERNEWS ZAWANOA WAANDISHI WA HABARI GEITA,SIMIYU NA SHINYANGA

$
0
0
Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Tawi la Tanzania kwa kushirikiana na Internews Tanzania wameendesha mafunzo kwa waandishi wa Habari Kanda ya Kaskazini/Magharibi (Geita, Shinyanga na Simiyu) kuhusu Changamoto za Sheria mpya za habari.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoanza Agosti 17,2018 hadi Agosti 18,2018 yanafanyika katika ukumbi wa Alpha Hotel Mjini Geita.

Akifungua Mafunzo hayo,Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Tawi la Tanzania, Sengiyumva Gasirigwa alisema kupitia mafunzo hayo waandishi wa habari watajengewa uelewa kiuhusu sheria mbalimbali zinazohusu vyombo vya habari na waandishi wa habari na namna waandishi wa habari wanavyoweza kuishi na sheria hizo. 

"Lengo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari na kuangalia changamoto zinazotolewa na sheria hizi sambasamba na kukumbushana miiko ya uandishi wa habari lakini pia kufahamu nafasi ya mwandishi wa habari kama mtetezi wa haki za binadamu",alisema.

Naye Afisa Mradi wa Boresha Habari kupitia Shirika la Internews linalofadhiliwa na USAID Victoria Rowan aliwasihi waandishi wa habari waliopata fursa ya kushiriki mafunzo hayo kutumia vyema elimu wanayopewa. 
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Tawi la Tanzania, Sengiyumva Gasirigwa akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari mikoa ya Geita Shinyanga na Simiyu kuhusu Sheria za vyombo vya habari katika ukumbi wa Alpha Hotel Mjini Geita - Picha zote na Kadama Malunde & Joel Maduka 
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Tawi la Tanzania, Sengiyumva Gasirigwa akielezea malengo ya semina hiyo 
Afisa Mradi wa Boresha Habari kupitia Shirika la Internews Victoria Rowan akielezea jambo ukumbini.


Waziri Dk. Kigwangalla kuruhusiwa muda wowote MOI, Kikwete amtembelea tena

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya mifupa MOI, hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa mara nyingine tena.

Hii inakuwa ni mara ya tatu kwa Kikwete kumtembelea Dk Kigwangalla ambapo awali alimtembelea Agosti 8,2018 alipokuwa amelazwa Wodi ya Mwaisela akipatiwa Matibabu ya awali na juzi Agosti 15,2018 katika wodi ya Taasisi ya Mifupa MOI.

Akiwa hospitaini hapo mapema jana, Kikwete ameweza kumjulia hali na kubadilishana nae mawazo mbalimbali huku akimtakia unafuu aendelee na majukumu yake ya kila siku na akimpongeza kwa shughuli zake anazozifanya katika kuinua sekta ya Utalii pamoja na kulinda rasilimali za Maliasili.

“Nikutakie kheri. Nashukuru kwa kukuta unaendelea vizuri sasa na nilikuja ukiwa upo unaongea ukiwa umelala kitandani na kwa sasa nimekuja tena umeweza kuimarika na hata kutembea na kukaa kama hivi hongera sana” alieleza Kikwete wakati akimjulia hali Waziri Kigwangalla wodini hapo.

Tayari jopo la Madaktari bingwa wa MOI wamebainisha kuwa Dkt. Kigwangalla kwa sasa anaendelea vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani ambapo kwa sasa sehemu zilizobakia ni mkono wake wa kushoto ambao kila siku unaendelea kuimarika.

Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla kitengo cha mifupa MOI anapopatiwa matibabu alipomtembelea kwa mara nyingine jana. 
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla kitengo cha mifupa MOI anapopatiwa matibabu alipomtembelea kwa mara nyingine jana. Picha zote na Andrew Chale.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA APOKEA MIFUKO 50 YA SARUJI KWA AJILI YA JIMBO LA BUKENE

$
0
0

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akimkabidhi mbunge wa Bukene, Selemani Zedi (kushoto) mifuko 50 ya saruji iliyotolewa na Mbunge wa Viti  Maalum mkoa wa Tabora kupitia  CCM, Munde Tambwe  (wapili kushoto ) baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Taifa wa Bukene wilayani Nzega  Agosti 17, 2018 saruji hiyo imetolewa kwa jimbo la Bukene ili isaidie katika ujenzi wa miundombinu ya  huduma za  jamii jimboni humo. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya wananchi baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Taifa wa Bukene wilayani Nzega, Agosti 17, 2018. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI UFUNGUZI RASMI MKUTANO WA KILELE WA 38 WA SADC

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa meza kuu na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa meza kuu na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga akiwa na ujumbe wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa meza kuu na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na viongozi wenzake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kilele wa kawaida wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa hoteli ya Safari mjini Windhoek nchini Namibia leo Ijumaa Agosti 17, 2018

RAIS DKT MAGUFULI AAGA MWILI WA MAREHEMU MEJA JENERALI MSTAAFU JOSEPH ANAEL LESULIE. ADA ESTATE JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0


Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli akitia saini katika kitabu cha Maombelezo cha Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Joseph Anael Lesulile, Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa marehemu,aliyefariki dunia agosti 14,2018 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam,Agosti 17,2018
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli akiwapa pole familiya ya Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Joseph Anael Lesulile, Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa kufiwa na baba yao aliyefariki dunia agosti 14,2018 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam,Agosti 17,2018
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Joseph Anael Lesulile, Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa marehemu,aliyefariki dunia agosti 14,2018 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam,Agosti 17,2018

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Joseph Anael Lesulile, Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa marehemu,aliyefariki dunia agosti 14,2018 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam,Agosti 17,2018
Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Joseph Anael Lesulile, Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa marehemu,aliyefariki dunia agosti 14,2018 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam,Agosti 17,2018. Picha na Ikulu.

HATUTAONGEZA MUDA WA UJENZI, NAIBU WAZIRI KWANDIKWA

$
0
0

Ujenzi wa daraja la Kikamba wilayani Songwe linalounganisha Mkoa wa Songwe na Katavi ukiendelea daraja hilo linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias John Kwandikwa akisisitiza jambo kwa Mbunge wa Songwe Mhe. Philipo Mulugo alipokagua ujenzi wa daraja la Kikamba wilayani Songwe, daraja hilo linaunganisha Mkoa wa Songwe na Katavi.
 Muonekano wa barabara ya Chunya –Makongolosi KM 39 ambayo ujenzi wake unaendelea, barabara hiyo ni sehemu ya barabara ya Mbeya-Rungwa yenye urefu wa KM 293 inayounganisha kwa njia fupi mkoa wa Mbeya na mikoa ya Singida na Tabora.

SERIKALI imesema haitamwongezea mkataba mkandarasi China Railway 15 Bureau Group Corporation anayejenga barabara ya Chunya –Makongolosi kwa kiwango cha lami muda wake utakapomalizika.


Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Elias John Kwandikwa amesema muda wa miezi 27 aliyopewa kujenga barabara hiyo yenye urefu wa  KM 39 unatosha na hivyo ni jukumu lake kuhakikisha kuwa anakuwa na vifaa na wafanyakazi wa kutosha wakati wote.


“Mkishindwa kukamilisha barabara hii kwa wakati hamtapata tena kazi hapa nchini kwani mtakuwa mmeshindwa kazi kwa kukiuka mkataba na kuiongezea Serikali gharama”, amesema Mhe. Kwandikwa.


Naye Kaimu meneja wa wakala wa barabara (TANROADS) mkoa wa Mbeya Mhandisi Selemani Lawena amesema barabara ya Chunya –Makongolosi ni sehemu ya barabara ya Mbeya-Rungwa yenye urefu wa KM 293 ambayo inaunganisha kwa njia fupi mkoa wa Mbeya na mikoa ya Singida na Tabora.

“Barabara hii ikikamilika itafungua uchumi wa mikoa ya Mbeya na Songwe na kuhuisha shughuli za kilimo,mifugo, uchimbaji madini na ufugaji nyuki na hivyo kuongeza fursa za maendeleo kwa jamii na serikali kwa ujumla”, amesema mhandisi Lawena.


Mhandisi lawena amesema sehemu ya Mbeya- Chunya KM 72 imekamilika na ujenzi wa Chunya –Makongolosi KM 39 unatarajiwa kukamilika Januari 2020.


Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kwandikwa amekagua ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Iwambi-Mbalizi KM 6.5 jijini Mbeya  ambayo itatumiwa na magari madogo ili kupunguza msongamano na ajali katika mlima Mbalizi na kusisitiza umuhimu wa wadau wote wa usafiri kushirikiana ili kupunguza ajali na hivyo kulinda maisha na mali.


IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO


Viewing all 110164 articles
Browse latest View live




Latest Images