Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110027 articles
Browse latest View live

DKT. SHEIN AFUNGUA JENGO LA "CHAWL" JUMBA LA TRENI ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Bw.Khatib Abdulrahman Khatib Babu mara alipowasili katika ufunguzi wa Jumba la "Chawi" maarufu Jumba la Treni liliopo Dajani Mjini ambalo limefanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China, wakati wa sherehe iliyofanyika jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto)akifungua pazia kama ishara ya kulifungua Jumba la "Chawi" maarufu Jumba la Treni liliopo Dajani Mjini Zanzibar lililofanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China, wakati wa sherehe rasmi iliyofanyika leo (kulia) Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Khalid Mohamed Salum.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF Bibi.Sabra Issa Machano (mbele) wakati alipotembelea sehemu mbali mbali za Jengo la "Chawi" maarufu Jumba la Treni lililofanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China liliopo Dajani Mjini Zanzibar baada ya kulifungua rasmi katika sherehe zilizofanyika jana.


Sayari 4 ziko katika mstari angani na Mwezi unazikaribia kati ya 14 hadi 23 Agosti 2018

$
0
0
Zuhura (Venus), Mshtarii (Jupiter), Zohali (Saturn) na Mirihi (Mars) zinaonekana angani zikiwa katika mstari mnyoofu kutoka magharibi kwenda mashariki na Mwezi unazikaribia kati ya tarehe 14 hadi 23 Agosti, 2018.

Muda wa kuziona sayari zote hizi ni kuanzia saa moja. Zuhura itatua magharibi na kupotea baada ya saa tatu.

Sayari huonekana kama nyota angani kwa hiyo namna ya kutofauitsha ni kwa mn'gao wake. Sayari ya Zuhura (Venus) inawaka kabisa kwa unjano upande wa magharibi wakati Mirihi (Mars) inamulika kwa rangi nyekundu upande wa mashariki.

Mshtarii (Jupiter) inan'gaa sana utosini.

Mn'gao wa Zohali (Saturn) ni mkali lakini ni sawa na nyota zingine. Kwa hiyo namna ya kutofautisha ni kwamba mwanga wa sayari zote haumeremeti kama nyota za kawaida.

Kwa hiyo ukiangalia nyota kwa makini na kama haimeremeti basi ni sayari. Imeandaliwa na Dkt. Noorali T. Jiwaji 

PREMIER BET YAZINDUA RASMI FOOTBALL JACKPOT

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Kampuni ya Michezo ya Kubashiri ya Premier Bet imezindua mchezo mpya wa Football Jackpot utakaowapa fursa wateja wa kampuni hiyo kujinyakulia kitita kikubwa cha fedha cha Shillingi Milioni 15.5 za Kitanzania.

Jackpot hiyo iliyozinduliwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Premier Bet, Samir Matar utakuwa mchezo wa kwanza wa Jackpot wenye kima kidogo katika michezo ya kubashiri nchini. Akizungumza na waandishi wa habari, Matar amesema kuwa Jackpot hiyo itakayohusisha mechi 12 za ligi mbalimbali droo yake itakuwa inachezwa kila siku ya Jumatano saa 3.55 usiku na Jumamosi saa 10.55 jioni. 

Ameeleza kuwa, wateja watatakiwa kubashiri mechi 12 zitakazokuwa zimeorodheshwa kwa mawakala wote nchini na atafanikiwa kushinda kitita hicho cha Milioni 15.5 na ikitokea mteja akabashiri mechi 10 au 11 atapatiwa fedha kulingana na ubashiri wake. 

Meneja Rasilimali watu na Utawala Amanda Kombe amesema kuwa lengo la kuanzisha Jackpot hii ni kwa ajili ya kukuza burudani ya soka kwa wateja wa Premier Football Betting ili kuwapa fursa ya kushinda kitita kikubwa cha fedha kwa kutoa hela kidogo. Amanda amesema, kama ikitokea katika siku ambayo Jackpot imechezeshwa mshinda wa Milioni 15 hajapatikana hivyo inapelekea kuongezeka kwa kiwango cha fedha.

Kwa sasa Premier Bet ina jumla ya mawakala 2000 nchini kote na ratiba za mechi zitakazokuwa zinashindanishwa zitakuwa zinapatikana kwa mawakala hao na mteja anaweza kucheza kadri ya uwezo wake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Premier Bet, Samir Matar (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Football Jackpot   utakaowapa fursa wateja wa kampuni hiyo kujinyakulia kitita kikubwa cha fedha cha Shillingi Milioni 15.5 za Kitanzania.


Meneja Rasilimali watu na Utawala Amanda Kombe akiwaonyesha waandishi wa Habari aina ya tiketi ya michezo ya kubashiri ya Premier Bet wakati wa uzinduzi wa Jackpot ya Premier Bet Jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Premier Bet wakionyesha namna ya kutoa risiti katika mashine kwa Mkurugenzi Mtendaji Samir Matar ( picha ya juu)  pia wakitoa tiketi kwa waandishi wa habari waliofika katika uzinduzi huo.

Athari zinazoweza kukukumba kwa kusitisha huduma ya malazi hotelini

$
0
0
Na Jumia Travel Tanzania

Ushawahi kukumbana na kadhia ya kunyimwa huduma ya malazi? Au kulipishwa kwa kutozingatia masharti ya hoteli kuhusu huduma zao?

Wasafiri wengi siku hizi hufanya maandalizi ya mapema pindi wanapotaka kusafiri. Lengo la kufanya hivi linaweza kuwa kupata bei nzuri zaidi au kuepuka usumbufu wa maandalizi ya dakika za mwisho. Lakini kwa baadhi yetu, kufanya maandalizi ya namna hiyo huona kama ni kujisumbua tu kwa sababu kuna uwezekano wa kuahirisha safari yenyewe.

Unaweza kuona kuwa ni jambo la kawaida wewe kama mteja kuamua kuahirisha safari yako na kuwaambia hoteli wasitishe huduma ya malazi uliyoweka. Lakini kuna masuala muhimu ya kuzingatia kuhusu sera zinazowekwa na hoteli hususani katika kusitisha huduma ya chumba ambayo Jumia Travel ingependa kukupatia ufahamu. 




Kuna umuhimu kwa wasafiri kuzifahamu sera za hoteli husika ukizingatia kumekuwa na mitandao mingi iliyoibuka kwa kasi katika utoaji wa huduma za malazi. Ushauri wa kwanza, msafiri anashauriwa pindi anapofikiria kusitisha huduma ya chumba hotelini aliyoifanya ni kujaribu kusoma kwa makini sera za hoteli ili kufahamu kwamba hatohitajika kulipia gharama zaidi pale atakapoamua kusitisha huduma.


Mambo muhimu ya kuzingatia

Endapo utakuwa umefanya huduma ya malazi ya chumba hotelini moja kwa moja utakuwa na faida mbili:

Kwanza, kama umeenda hotelini moja kwa moja na kufanya huduma kwa utaratibu uliozoeleka unaweza kuwa na faida ya kusitisha huduma yako hata masaa 24 kabla ya kuripoti. Utaratibu huu unaweza kukupa faida ya kurudishiwa takribani pesa zako zote kama ulishalipa au hautokatwa chochote kama hautokuwa umelipa. Mara nyingi njia hii ni rahisi na huwa haina matatizo.

Pili, kama utakuwa umefanya huduma ya malazi ya kabla basi ujue suala la kusitisha huduma kwako litakuwa ni changamoto kwako. Hii ni kutokana na sababu ya kwamba kwa mtazamo wa hoteli, utakuwa umepewa ofa ya bei nzuri tofauti na wengine na hawatokuwa tayari kukuachia uende kirahisi. Ukiachana na kufanya huduma ya malazi moja kwa moja hotelini, siku hizi kuna njia za kufanya huduma kupitia mitandao mbalimbali.

Mfumo wa kufanya huduma za malazi kwa njia ya mtandao unakupatia fursa ya kuperuzi na kulinganisha huduma za hoteli mbalimbali kwa urahisi na wakati mmoja. Faida ya kutumia mitandao kama hii ni kwamba mingi miongoni mwao huonyesha sera za hoteli katika kusitisha huduma ya malazi uliyoifanya.

KUSOMA ZAIDI  BOFYA HAPA>>>>>>>

KENYA YAZUIA UINGIZAJI WA VIGAE, HALI INAYOSABABISHA HASARA KWA WAWEKEZAJI KUTOKA TANZANIA

$
0
0

NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA

KIWANDA cha Goodwill Tanzania Ceramic co.ltd kilichopo Mkiu ,Mkuranga Mkoani Pwani, kinachozalisha vigae kinakabiliwa na tatizo la ukosefu wa soko baada ya nchi ya Kenya kuzuia uingizwaji wa bidhaa hiyo. Hatua hiyo iliyochukua nchi hiyo inasababisha shehena kubwa ya vigae kurundikana kwenye magodauni na kupata hasara.

Meneja uajiri katika kiwanda hicho ,Msafiri Figa aliyasema hayo wakati kamati ya siasa mkoa, ilipokwenda kutembelea kuona shughuli za uzalishaji kiwandani hapo. Alisema ,walikuwa wakitegemea soko la Kenya zaidi kutokana na kupata oda nyingi kutoka kwa wafanyabiashara wa nchi hiyo . Figa alisema ,kipindi kiwanda kinaanza lengo lao ilikuwa kuzalishaji mita za mraba 80,000 sawa na vigae 800,000 kwa siku lakini kwa sasa tangu waanze kuzalisha wanazalisha vigae 600,000 kwa siku.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (wa nne kulia) akiangalia kigae wakati kamati ya siasa mkoani Pwani ilipokwenda kutembelea kiwanda cha Goodwill ceramic co.ltd Mkuranga na kukuta shehena ya vigae iliyorundikana katika kiwanda katika kiwanda hicho kwa kukosa soko.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) akiongea jambo na MNEC Kibaha ,Hajji Jumaa , wakati kamati ya siasa mkoani Pwani ilipokwenda kutembelea kiwanda cha Goodwill ceramic co.ltd ,Mkuranga na kukuta shehena ya vigae iliyorundikana katika kiwanda katika kiwanda hicho kwa kukosa soko.

"Kadri siku zikienda imekuwa tukizalisha mita za mraba 50,000 kutokana na tatizo soko ,tulilenga soko la ndani kwa asilimia 60-70 na soko la nje asilimia 30-40 lakini imebadilika na kuwa soko la ndani 30-40 nje ikawa asilimia 60-40 huku tukizalisha mita za mraba ya vigae 30,000-20,000 kwa siku " .

Figa alielezea, wana wafanyakazi 900 kutoka Tanzania,ajira zisizo za moja kwa moja 2,000-3,000 na wachina 60 ambao ni pamoja na wataalamu mbalimbali.Nae mkuu wa mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo ,alisema hali iliyopo ni hatari kwani inakwenda kuuwa viwanda na kuweka hofu ya kuzima ndoto yetu.

"Mwaka mmoja na nusu uliopita eneo hili lilikuwa pori ambapo sasa kuna kiwanda kikubwa ambacho kinatengeneza ajira na kuliingizia mapato Taifa"Ndikilo alieleza ,tatizo la ukosefu wa soko sio la kubeza ,sio la masihala,hivyo amekiomba chama kisimamie hilo. Alisema ,wapo wafanyabiashara wanaagiza vigae China suala hili linakandamiza wawekezaji wa ndani .
Mfanyakazi katika kiwanda cha Goodwill ceramic co.ltd ,Mkuranga akipakia mabox ya vigae, wakati kamati ya siasa mkoani Pwani ilipokwenda kutembelea na kukuta shehena ya vigae iliyorundikana katika kiwanda katika kiwanda hicho kwa kukosa soko .

"Wapo watendaji serikalini wanaotoa vibali kwa wanyabiashara kuagiza nondo Uturuki na vigae China,Spain na wengine kuchukua chuma nje hivyo kuna kila sababu kuliangalia tatizo hilo" alisisitiza Ndikilo.Alisema, serikali inafanya kazi lakini baadhi ya watendaji wanasababisha tatizo hili kwa maslahi binafsi.

Kwa upande wake ,mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Ramadhani Maneno alisema ,wataishauri serikali kupitia wizara husika kuanza kutazama muundo wa sera ya masoko . Alisema, wataangalia namna ya kukaa na wizara ya viwanda na biashara ,wizara ya fedha kuweka masharti kwa wafanyabiashara ,"Kuwawekea masharti bila kuwaonea haya kuwa ukiwa Tanzania hakuna budi kutumia bidhaa zinazozalishwa viwanda vya ndani.

"Duniani kote ukizalisha lazima utegemee soko hivyo kama ukizalisha bila kuuza ni kazi bure kwani uzalishaji ukipungua kwa kukosa soko ajira zitapungua na kukatisha tamaa wawekezaji" alibainisha Maneno.
Shehena ya vigae iliyorundikana katika kiwanda cha vigae cha Goodwill Ceramic co.ltd ,Mkiu Mkuranga mkoani Pwani kwa kukosa soko .(picha na Mwamvua Mwinyi).

JK amjulia hali Dkt. Kigwangalla kitengo cha mifupa MOI

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya tarehe 14, Agosti 2018 amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya mifupa MOI,  hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Hii inakuwa ni mara ya pili kwa Kikwete kumtembelea Dk Kigwangalla ambapo awali alimtembelea Agosti 8,  alipokuwa amelazwa Wodi ya Mwaisela akipatiwa Matibabu ya awali.

Kikwete amemtakia kila lakheri katika kipindi hiki kwa kuuguza majeraha ya mkono na sehemu za mwili ikiwemo mbavu ambazo kwa sasa hali yake inaendelea kuimarika kwa majibu wa Madaktari wa kitengo hicho cha mifupa MOI.

Awali tokea kufanyiwa operesheni ya mkono ameweza kufanya mazoezi taratibu ikiwemo kutembea mwenyewe katika viunga hivyo vya Muhimbili.

Dkt. Kigwangalla alipata ajali ya gari mnamo Agosti 4, 2018 huko Manyara akiwa katika ziara ya kikazi ambapo katika ajali hiyo iliyokuwa na watu 6, watano walijeruhiwa na mmoja alifariki dunia ambaye alikuwa afisa habari mwandamizi wa Wizara hiyo, Hamza Temba.
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla kitengo cha mifupa MOI anapopatiwa matibabu. Kulia ni Mke wa Waziri Dk Kigwangalla, Dkt. Bayoum Awadhi Kigwangalla.

TCU imefunga dirisha la awamu ya kwanza

$
0
0
Katibu mtendaji Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), Prof Cherles Kihampa akizungumza na waadishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ya kujiunga na masomo katika vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini, alisema Agost 15 mwaka huu itakuwa siku ya mwisho kutuma maombi hayo.
Na Chalila , Kibuda,Globu ya Jamii.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kufunga dirisha la awamu ya kwanza la maombi ya kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu hapa nchini.

Akizungumza na wanahabari makao makuu ya Tume hiyo jijini Dar es salaam, Prof. Charles Kihampa amesema kwamba dirisha hilo linafungwa leo Agost 15, na kufunguliwa kwa awamu ya pili septemba 3 mwaka huu.

Aidha Prof.Kahampa amewasisitiza waombaji wasome mwongozo wa programu zilizoidhinishwa kudahili pamoja na vigezo vya udahili vinavyotakiwa kwa kila programu ya masomo kabla ya kuanza kutuma maombi yoyote ya udahili.

Ikumbukwe kuwa dirisha la maombi ya elimu ya juu lilifunguliwa rasmi kwa awamu ya kwanza Julai 20, 2018.

TUKEMEE MAPEPO YA MCHANA NA USIKU-RC RUVUMA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa RUVUMA Christine Mndeme amemtaka mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mh.Sophia Kizigo kuhakikisha anawashirikisha viongozi wa dini na wazee katika wilaya hiyo ili kuweka mambo sawia katika utendaji wa kazi za serikali.

WAANDISHI WA HABARI RAFIKI WA WANYAMAPORI WAFIKA MTAMBASWALA

$
0
0
 Kikundi cha waandishi wa habari rafiki wa wanyamapori na urithi wa asilia wakiwa katika eneo la Mangaka wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara, wakiwa njiani kuelekea daraja la umoja Mtambaswala kuangalia vivuko vya tembo na swala kutoka mbuga ya wanyama ya Seloue kuelekea Msumbiji.

DStv sasa kurusha Serie A- kifurushi cha Bomba!

$
0
0
Siku chache tu kabla ya kuanza kwa moja ya ligi maarufu Duniani – Ligi kuu ya Italia Serie A, MultiChoice imetangaza neema ya burudani kwa wateja wake kwa kuweka michezo yote 380 ya ligi hiyo katika kifurushi cha chini kabisa cha DStv Bomba ambacho hulipiwa shilling 19,000 tu kwa mwezi.

Kama hiyo haitoshi, DStv pia itaonyesha mechi zote 380 za ligi ya Hispania – La Liga katika kifurushi hicho cha bomba huku mechi 108 za ligi kuu ya uingereza (EPL) nazo zikionyeshwa katika kifurushi hicho cha chini kabisa.

“Kama ilivyo ada, sisi DStv kila uchao tunahakikisha kuwa tunamfikishia mtanzania burudani popote alipo na kwa gharama nafuu. Hii ndiyo sababu tumeamua kuiweka ligi hii maarufu katika kifurushi chetu cha Bomba kinachopatikana kwa shilingi 19,000 tu kwa mwezi” amekaririwa Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Alpha Mria.

“Tunatambua kuwa ligi ya Italia ni moja ya ligi zenye mvuto mkubwa ulimwenguni na kama kawaida kwa kupitia DStv, tunawafanya watanzania kuwa sehemu ya ulimwengu wa burudani hususan soka, hivyo tumeamua kwa makusudi kabisa kuiweka ligi hii ya italia kwenye kifurushi cha bomba” amebainisha Alpha.

Wiki iliyopita DStv ilitangaza kuirejesha ligi hiyo ya Italia na kuweka michezo michache kwenye kifurushi cha Bomba, lakini kutokana na maoni ya wateja wake wengi, imeamua kuishusha ligi hiyo katika kifurushi cha chini kabisa.

Ligi Kuu ya Italia inatarajiwa kuanza Jumamosi hii ambapo washabiki wa soka watamshuhudia mwanasoka nguli Christiano Ronaldo akiiwakilisha timu maarufu ya Juventus kwa mara ya kwanza. Mtanange huo wa ufunguzi utakuwa kati ya Juventus na Chievo na utaonyeshwa mubashara kupitia DStv chanel ya SuperSport 8 (HD).

Mbali na hayo, wateja wa DStv wataendelea kufurahia  msimu huu mpya wa soka na katika kunogesha zaidi michuano ya ligi ya uingereza itatangazwa kwa lugha ya kiswahili.

Ili kuwapa wateja wake uhuru zaidi wa kufurahia soka popote walipo,  DStv inaendelea kutoa huduma ya DStv Now ambapo mteja wa DStv anaweza kutazama matangazo katika vifaa zaidi ya vinne kama vile simu, kompyuta, na televisheni ya kawaida.

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI UJENZI WA VIBANDA ENEO LAO LA STENDI MPYA MUGUMU MJINI

$
0
0
WANANCHI wilayani Serengeti mkoani Mara wametakiwa kijitokeza kwa wingi katika ujenzi wa  vibanda eneo la ujenzi wa Stendi mpya inayojengwa eneo la Stendi Kuu Mjini Mugumu baada ya stendi iliyokuwaikitumika kuwa finyu na miundombinu kuwa mibovu.

Ambapo hali hiyo  kusababisha mabasi makubwa kupaki nje ya stendi hiyo kinyume cha sheria.Hayo yamesemwa leo  na Mwenyekiti wa Halamshauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Juma Porini  katika baraza la madiwani la mwaka.Amesema  kuwa mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa vibanda hivyo umekuwa mdogo baada ya kutangaziwa mpaka sasa.

Hivyo Mwenyekiti ametumia fursa hiyo kuwatangazia tena wananchi kujitokeza kwa wingi kwani muda ambao ulitolewa kwa ajili ya kukamiliasha maombi umeisha.Lakini amesema  wameamua kuongeza muda kwa lengo la wananchi kijitokeza kwa wingi.“Mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa vibanda hivi umekuwa mdogo licha ya kuwatangazia na bei ni nafuu kuchukua fomu ni Sh.50,000 tu, na akishajenga kibanda hicho atakitumia kwa muda wa miaka mitano.

"Katika kipindi hicho  akatakuwa anakitumia kwa kulipa 20,000 tu na baada ya miaka mitano kibanda kitarudishwa na ataanza kukitumia kwa kupangisha kulingana na mikataba itakavyosema” amesema Mwenyekiti.Aidha Mbunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara Samson Ryoba(Chadema) anasema kuwa wanaendelea kujenga Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti bila kujali itikadi za vyama kwa lengo la kuletea wananchi Maendeleo.

Huku Katibu wa Madiwani Chadema Samson Wambura akitoa mapendekezo ya Chama hicho likiwemo suala la uboreshaji wa masoko katika Mjini Mugumu.Aidha Mkurugenzi wa Halmashaurti Juma Hamsini amesema kuwa tayari Halmashauri hiyo imeishaagiza taa za kufunga katika baadhi ya masoko ya jioni ili kuongeza ulinzi wa mali za wananchi.Pia ameahidi  kuendelea kutafuta wadau kwa lengo la kufunga taa za barabarani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Porini akisisitiza suala la wananchi kujitokeza kwa lengo la ujenzi wa vinanda eneo la Stendi Kuu ambapo kunajengwa stendi mpya ya Magari.
Madwani WilayaniSerengeti Mkoani Mara wakiwa katika baraza la Mwaka.
Mbunge wa Jimbo la Serengeti CHADEMA Samson Ryoba akisisitiza suala la Ushirikiano baina ya Madiwani wote bila kujali itikadi za vyka kwa lengo la kuletea wananchi Maendeleo.
Katibu wa Madiwani wanaoyokana na CHADEMA Wilaya ya Serengeti Samson Wambura akisoma hoja pendekezi za kamati ya chama hicho likiwemo suala la kuboresha Masoko katika Mji wa Mugumu.
Mkurugenzi wa Halamashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Hamsini akifafanua jambo kwa madiwani hao na kueleza jitiada za Halamashauri hiyo likiwemo suala la ununuzi wa taa za barabarani pamoja na Masoko ya jioni. 

BRANCH YAADHIMISHA MWAKA MMOJA NCHINI, AGUSIA MALENGO YA KUANZISHWA KWAKE

$
0
0

Na Khadija Seif , globu ya jamii.

KAMPUNI ya kidigital ya huduma za kifedha (Branch) imeadhimisha mwaka mmoja tangu kuanza kwake.

Ambapo imejikita katika sekta ya teknolojia-fedha kwa kutangaza kujiunga na mfumo wa huduma mpya na Airtel jijini Dar es salam.

Mwanzilishi wa Kampuni hiyo Branch, Ofisa Mtendaji Mkuu Matthew Flannery ameeleza dhumuni la kuanzishwa kwa Kampuni hiyo ni kutokana na uhitaji mkubwa wa kifedha ili kuendeshea biashara mbalimbali kwa wateja ambao wanakosa mikopo ya kufanikisha mahitaji yao, hivyo basi huduma hiyo itawapa fursa za kupata fedha haraka zaidi.

Flannery amesema zaidi ya asilimia 75 ya wateja wanatumia mikopo ya Branch kuwasaidia kuanzisha na kukuza biashara zao au kutimiza mahitaji mengine ya kifedha. 

Akizungumzaa na wanahabari Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Afrika Masharki Dan Karuga amefafanua kuwa Branch ni kampuni ya kipekee inayotoa huduma vyenye viwango vya hali ya juu katika huduma za kifedha,kupitia mpango wao wa kutoa mikopo hususani kwa makundi ya watu wasiofikiwa kiurahisi.

Na kufanikisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wateja mbalimbali nchini kote. Karuga ameeleza lengo la huduma hiyo ni kutoa fursa kwa wananchi kupata mikopo haraka kupitia simu za mikononi ,na watumiaji wanaweza kutumia smartphone zenye uwezo wa Internet kujipatia mkopo kuanzia Sh. 50,000 hadi Sh.100,000.

" Inachukua sekunde chache kutoka kutuma maombi hadi kukubaliwa kwa ombi la mkopo,pia haihitaji kuonana ana kwa ana na mtoa huduma kwa njia ya vikao."Utaratibu mrefu wenye sura simu,dhamana ya kujaza fomu za karatasi. Pia tangu ianze huduma zake Tanzania,Branch imekwishatoa mikopo ya zaidi ya Sh.billioni 12 na mikopo zaidi ya 400,000,"amesema Karuga

Amesema kuwa Branch international, inatarajia kutoa mikopo ya Sh. Billioni 570 na kutoa mikopo mipya zaidi ya laki tano amesema Karuga.

Nae mmoja wa watumiaji wa hudumu ya Branch, Mtangazaji mahiri wa Radio ya EFM Dina Marios alikiri wazi urahisi wa kuitumia huduma hiyo popote na kwa wakati wowote ule kujipatia mkopo ambao unaweza ukatumia kuanzisha biashara yako.

Hivyo amewahimiza Watanzania kujitokeza kutumia huduma hiyo ili kujiongezea kipato kwa namna moja ama nyingine na hatimae kujikwamua kiuchumi.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Branch Afrika Masharki, Dan Karuga akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani),mapema leo jijini Dar kuhusu kampuni hiyo kuadhimisha mwaka mmoja na mikakati yake mbalimbali ikiwemo na kujitanua kibiashara zaidi nchini Tanzania
Pichani kushoto ni Mwanzilishi wa Kampuni Branch, Ofisa Mtendaji Mkuu Matthew Flannery akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani),mapema leo jijini Dar kuhusu kampuni hiyo kuadhmisha mwaka mmoja ,dhumuni la kuanzishwa kwa Kampuni hiyo hasa kwa nchini Tanzania pamoja na mikakati mingine ya kujitanua zaidi kibiashara
Mmoja wa watumiaji wa hudumu ya Branch, Mtangazaji mahiri wa Radio ya EFM Dina Marios akitoa ushuhuda mbele ya Waandishi wa Habari,namna kampuni hiyo inavyoweza kuwanufaisha Watanzania,kupitia mikopo inayotelewa iliyo na masharti nafuu kabisa.
Baadhi ya Wanahabari wakifutilia yaliyokuwa yakijir ukumbini humo

MAKAMU WA RAIS KUMUWAKILISHA RAIS KATIKA MKUTANO WA SADC NCHINI NAMIBIA

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anaondoka nchini leo kuelekea Windhoek, Namibia kushiriki kwenye Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (38th Ordinary Summit of SADC Heads of State and Government) unaotarajiwa kufanyika tarehe 17 na 18 Agosti, mwaka huu akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. 


Mkutano huo utakaofanyika chini ya Uenyekiti wa Namibia, utatanguliwa na Mikutano mingine mitatu ambayo ni Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Organ Troika, Mkutano wa Baraza la Mawaziri na Mkutano wa Makatibu Wakuu. Aidha, Mkutano huo utapokea na kujadili agenda mbalimbali ikiwemo Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa SADC, Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama, taarifa ya Mwenyekiti anayeondoka wa SADC Organ, taarifa ya Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, hali ya kiuchumi katika kanda ya SADC na taarifa kuhusu utekelezaji wa Kaulimbiu ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa mwaka 2017.

Vilevile, Mkutano utapokea Kaulimbiu ya Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali na kupokea taarifa ya hali ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa SADC. Katika Mkutano huo, Tanzania inategemea kuteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa SADC kwa kipindi cha Agosti 2018 hadi Agosti 2019.

Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam
15/8/2018

IGP SIRRO AFANYA MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI WA MWANZA NA PWANI

IGP APONGEZA UTULIVU CHAGUZI NDOGO.

$
0
0
Na Jeshi la Polisi.

Jeshi la Polisi nchini limewahakikishia wananchi kuendelea kuwepo kwa hali ya usalama na Amani hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwepo kwa hali ya utulivu na usalama katika chaguzi ndogo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro wakati akiwa katika ziara katika Shule ya Polisi Moshi (CCP) ambapo aliweza kuzungumza na Wakufunzi na Askari waliopo mafunzoni Chuoni hapo ikiwa na lengo la kukagua mwenendo wa mafunzo yanayoendelea katika Vyuo vya Polisi nchini.

IGP Sirro amesema katika maeneo yaliyofanya uchaguzi mdogo hali ilikuwa shwari licha ya kuwepo kwa matukio madogo ambayo yanaendelea kushungulikiwa na upelelezi utakapokamilika majalada yao yatapelekwa kwa Waendesha mashtaka kwa hatua zaidi.

“ Hali iliuwa shwari na ni wazi kuwa wananchi sasa wameelewa umuhimu wa kutii sheria bila ya kushurutishwa na natoa rai waendelee kudumisha hali hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za Wahalifu na uhalifu katika maeneo yao” Alisema Sirro.

Katika hatua nyingine akiwa Shule ya Polisi Moshi zamani CCP IGP Sirro alitoa pongezi zake kwa Walimu na Uongozi kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuwapika Askari hususani katika mafunzo yao ya awali ambapo ametaka kila Askari kutambua wajibu wake

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Polisi Moshi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Mungi amesema Chuo hicho kinaendelea kutoa mafunzo kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kuwa kila Askari anayetoka anakuwa na ukakamavu wa kutosha na nidhamu ya kuwahudumia Wananchi licha ya kuwepo kwa Changamoto za madeni ya maji na umeme.

Alisema wanaendelea kuboresha miundombinu ya Chuo hicho kwa kutumia miradi iliyopo ili kukiweka katika hali ya usalama zaidi ikiwemo kujenga uzio imara kuzunguka maeneo hayo.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro 

JESHI LA POLISI LAFANYA MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI MIKOA YA MWANZA NA PWANI

Balozi Dkt. Abdallah Possi atoa wito kwa wawekezaji kuja Tanzania

$
0
0
Ilikuwa katika viwanja vya maonyesho ya International Afrika Festival Tübingen nchini ujerumani ambapo katika maonyesho hayo mwaka huu 2018 nchi lengwa ilikuwa ni Tanzania na mgeni wa heshima rasmi alikuwa balozi wa Tanzania nchini ujerumani mheshimiwa dkt. Abdallah Possi ambaye alihutubia ummati wa kadamnasi ya waudhuriaji wakiwemo wawekezaji kuwa Tanzania kuna fursa kubwa za uwekezaji na pia nchi salama.

onyesho hilo kubwa lilinogeshwa na bendi za muziki kama Ngoma Africa band maarufu FFU-Ughaibuni inayoongozwa na kamanda Ras Makunja,bendi ya Mvula-Mandondo Band inayoongozwa na msanii Saidi Kanda yenye maskani kule Uingereza nayo ilifanya vizuri,wasanii wa kizazi kipya kama Nashi MC kutoka Tanzania naye alitingisha jukwaa msanii wa picha za kuchora Chilonga Haji naye alikuwa moja ya waonyeshaji wa bidhaa toka Tanzania.onyesho lilifana sana sana na kuitanga za Tanzania kimataifa.
Balozi wa Tanzania nchini Ujermani Mhe. Dk. Abdallah Possi akiwa na wawekezaji wakiangalia naadhi ya bidhaa katika maonyesho mjini Tubingen,Ujerumani.
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dk. Abbdalaah Possi akiwa katika maonyesho ya Gaiexpo mjini Tubingen,mwaka huu nchi lengwa ilikuwa Tanzania.
Ngoma Africa Band wakiwa jukwaani katika onyesho la Tubingen.

Tanzeela Qambrani: Mwanamke mwenye asili ya Tanzania ateuliwa mbunge Pakistan na kuweka historia

$
0
0
Mwanamke mwenye asili ya Tanzania amekuwa wa kwanza wa asili ya Afrika kuteuliwa kuwa mbunge nchini Pakistan, na kutoa matumaini kwa watu wa jamii ndogo na maskini nchini humo yenye asili yake Afrika.

Tanzeela Qambrani, 39, aliteuliwa na chama cha Pakistan People's Party (PPP), cha waziri wa zamani Benazir Bhutto kuhudumu katika kiti kilichotengewa wanawake kwenye bunge la mkoa wa Sindh kusini mwa India.

Ana matumaini kuwa uteuzi wake baada ya uchaguzi wa mwezi uliopita utasaidia kuondoa unyanyapaa ambao umekuwepo dhidi ya jamii ya Sidi, jina wanaloitwa watu wa asili ya Afrika wanaoishi maeneo ya pwani ya Makran na Sindh nchini Pakistan.

"Kama jamii ndogo iliyopotelea kwenye jamii kubwa za wenyeji, tumekuwa na wakati mgumu kudumisha mizizi yetu ya Afrika na tamaduni, lakini ningependa kuona kuwa jina Sidi linakuwa lenye heshima," Bi Qambrani ambaye mababu zake walitokea Tanzania aliiambia BBC.

Mwanamke huyo aliapishwa Jumatatu wiki hii na amenukiliwa na mtandao wa The News International akisema kwamba alijihisi kama Nelson Mandela.
Alivalia mavazi ya kitamaduni ya Kiafrika wakati wa kuapishwa kwake.

BADO TUNAHITAJI WAWEKEZAJI KWENYE SUKARI-MAJALIWA

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania bado inawahitaji wawekezaji zaidi katika sekta ya uzalishaji wa sukari ili iweze kukidhi mahitaji. 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Mauritius nchini Tanzaniamwenye makazi yake Maputo nchini Msumbiji, Mheshimiwa Jean Pierre Jhumun, ofisini kwake jijini Dodoma. 

“Mwaka jana nilikiwa nchini Mauritius nilihudhuria Jukwaa la Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Tanzania na Mauritius, ambapo nilipata fursa ya kuwashawishi wawekezaji wa Mauritius waje kuwekeza kwenye viwanda vya sukari nchini,”. 

Ameongeza kuwa Tanzania ina fursa kubwa ya maeneo ya uzalishaji wa sukari ambayo bado hayajaendelezwa, hivyo kama kuna wawekezaji walio tayari na wamekidhi vigezo waendelee na hatua za uzalishaji. 

Waziri Mkuu ameongeza kuwa mbali na kuhitaji wawekezaji kwenye sekta ya sukari, pia amewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Mauritius kuja kuwekeza kwenye sekta ya uvuvi. “Mnaweza kuja kuwekeza kwenye viwanda vya usindikaji wa samaki kwani tuna bahari, mito na maziwa yenye samaki wa aina mbalimbali,” 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Mauritus nchini mwenye makazi yake, Maputo nchini Msumbiji, Jean Pierre Jhumun, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dodoma, Agiosti 15, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Mauritius nchini mwenye makazi yake Maputo nchini Msumbiji, Jean Pierre Jhumun (wapili kushoto) Balozi wa Heshima wa Mauritius nchini, Kazim Rizvi (kulia), Mwenyekiti wa Mfuko wa Uwekezaji Sukari nchini Mauritius, Gansam Boodram (wapili kulia) na kushoto ni Mwenyeji wa ujumbe huo katika jiji la Dodoma, Kapteni Mstaafu John Chiligati. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Mauritius nchini mwenye makazi yake Maputo nchini Msumbiji, Jean Pierre Jhumun (wapili kulia) na ujumbe wake, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dodoma Agosti 15, 2018. Wengine kutoka kushoto ni Balozi wa Heshima wa Mauritius nchini, Kazim Rizvi, Mwenyekiti wa Mfuko wa Uwekezaji Sukari nchini Mauritius, Gansam Boodram na watatu kushoto ni Mwenyeji wa ujumbe huo katika jiji la Dodoma, Kapteni Mstaafu John Chiligati. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

WATAALAM KUCHUNGUNZA UCHIMBAJI MADINI HIFADHI YA AMANI, TANGA

$
0
0

Na Zuena Msuya, Mheza ,Tanga 

Serikali imesema itawaleta wataalam kutoka kituo cha Utafiti wa Miamba(GST), Wizara ya Maliasili na Mazingira kwenye eneo walilokuwa wakitumia wachimbaji wadogo kwa shughuli za madini, ambalo pia linadaiwa kuwa liko katika chanzo cha maji, kufanya utafiti na kujiridhisha kama eneo hilo liruhusiwe kuendeleza na shughuli za uchimbaji madini ama laa. 

Hayo yalisemwa na Naibu waziri wa Madini Dotto Biteko alipotembelea katika kijiji cha Sakale katika Kata ya Mbomole Tarafa ya Amani wilayani Mheza mkoani Tanga, wakati akizungumza na wananchi waliomuelezea kero yao ya kuzuiwa na serikali kutokuchimba madini eneo hilo licha ya kuwatokuwepo na viashiria vya uharibifu wa mazingira na misitu kama serikali inavyosema. 

Naibu Waziri Biteko, alisema kuwa kiu ya serikali ni kuwapatia maeneo ya uchimbaji wachimbaji wadogowadogo ili waweze kubadilisha maisha yao kupitia uchumi wa madini, hii ni kutokana Rais kubadilisha sheria za nchi kwa upande wa madini kutoka kuwanufaisha wageni na sasa kuwanufaisha watanzania. 

“Serikali yenu ni sikivu,Mheshimiwa Rais amebadilisha sheria ya madini ili kuwanufaisha watanzania badala ya wageni ,hapa leo tumekuja kuangalia kwa macho ili tufanye uamuzi sahihi …siwezi kumiambia mchimbe sasa hivi ila tutaleta wataalamu wetu wa GST,maliasili na mazingira kwa pamoja ili waje kuona uwezekano wa kupewa eneo la kuchimba ikiwa hapa au kwengine”alisema. 
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko,( mwenye Tshit nyekundu) na Mbunge wa Mheza Balozi Rajab Adad (mbele) wakielekea eneo lililokuwa likitumiwa na wachimbaji wadogo kuchimba madini pia likidaiwa kuwa chanzo cha maji katika hifadhi ya misitu wa asili wa amani, mheza Tanga.
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko,( katikati) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Sakale, Mheza mkoani Tanga, waliokuwa wakiomba kuruhusiwa kufanya shughuli za uchimbaji madini katika eneo linalodaiwa kuwa ni chanzo cha maji yanayotumika Mkoa wa Tanga.

Viewing all 110027 articles
Browse latest View live




Latest Images