Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110089 articles
Browse latest View live

MASHABIKI WA SOKA RUANGWA WAFURIKA KUSHUHUDIA MECHI YA SIMBA SC NA NAMUNGO FC

$
0
0

Mashabiki wa soka, wakiwa kwenye foleni ya kuingia uwanjani kushuhudia mechi ya kirafiki kati ya timu ya Simba SC na Namungo FC kwa ajili ya ufunguzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11.2018 (Picha na Ofisi ya Naziri Mkuu)
Mashabiki wa soka, wakiwa kwenye foleni ya kuingia uwanjani kushuhudia mechi ya kirafiki kati ya timu ya Simba SC na Namungo FC kwa ajili ya ufunguzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11.2018 (Picha na Ofisi ya Naziri Mkuu)

GESI ASILIA KUTUMIKA MAJUMBANI MKOANI MTWARA – KALEMANI

$
0
0

Na Rhoda James- Mtwara

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani jana tarehe 10 Agosti, 2018 amezindua rasmi mradi wa ujenzi wa Mtambo wa kusambaza Gesi Asilia majumbani mkoani Mtwara. Waziri Kalemani, amefanya zoezi hilo leo katika shule ya Ufundi ya Mtwara mara baada ya kuzidua MW4 za umeme katika kituo cha Umeme cha Mtwara.

Waziri Kalemani alisema kuwa, ujenzi wa mtambo huu umegharimu jumla ya billioni 1.5 kwa ajili ya kuwapelekea watumiaji wa awali wasiopungua 150 ambao bada ya miezi mitatu wataanza kutumia gesi hiyo majumbani. Aliongeza kuwa matumizi ya gesi asilia ni madogo sana yaani ni kama hayapo, kwa kuwa wananchi wengi wanatumia kuni na mkaa kwa wengi kuliko gesi.

“Sasa mtugi wa gesi ni takriban shilingi 55,000/- lakini ukitumia gesi asilia kwa matumizi ya nyumbani itakuwa shilingi 25,000/- na utatumia kwa mwezi mzima hivyo ni nafuu kwa mwananchi wa Tanzania,” alisema Wazari Kalemani.

Mwezi mei tulianza matumizi ya gesi manyumbani lakini leo tumeanza matumiz ya gesi asilia katika mkoa wa Mtwara. “hayawi hayawi yamekuwa,” alisema Waziri Kalemani. Aidha, Waziri Kalemani aliendelea kueleza kuwa, Kuna magari zaidi ya 100 wanatumia gesi asilia jijini Dar es Salaam, hivyo kuazia mwezi Machi mwaka kesho (2019) tutaanza usanifu ili magari ya mkoa wa Mtwara nayo yaanze kutumia gesi asilia.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (wa nne kushoto) mara bada ya kuzidua mradi wa ujenzi wa mtambo wa usambazaji wa gesi asilia majumbani mkoani Mtwara. Wengine katika picha ni viongozi mbalimbali kutoka Serikalini wakiwa pamoja na Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia (wa tatu kulia) na wa kwanza kulia Mbunge wa jimbo la Nanyamba, Abdallah Chikota. 
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (wa pili kulia) akifatilia jambo kwenye ramani (haipo pichani) ya jinsi gesi hiyo itakavyo sambazwa majumbani. 
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali serikalini pamoja na wabunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia (mwenye kilemba) na wa nne kushoto ni Mbunge wa jimbo la Nanyamba, Abdallah Chikota. 


MICHUZI TV: UFUNGUZI WA UWANJA WA MICHEZO RUANGWA WAVUKA MASHABIKI LUKUKI

NEWZ ALERT: MTATIRO ABADILI GIA ARIDHINI,AONDOKA CUF,ATANGAZA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS

$
0
0
Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii

JUHUDI za Rais Dk.John Magufuli za kuleta maendeleo zimesababisha Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi(CUF), Julius Mtatiro kuamua kubadili gia aridhini kwa kujivua uanachama wa chama hicho.

Na kwamba amesema kuanzia leo atajikita katika kushiriki katika kufanya siasa za maendeleo na hasa kuunga mkono jitihada za Rais.Wakati anatangaza uamuzi huo ametaja sababu tano zilizomsukuma kufanya uamuzi huo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mtatiro ametaja sababu hizo ambapo ya kwanza ni kutoridhishwa na hali ya ushiriki na mchango wake kwenye siasa za CUF.Amesema sababu ya pili ni mgogoro wa kiuongozi unaoendelea kukikumba chama hicho na sababu ya tatu ni kutoridhidhwa na ushiriki wake kama kijana na kiongozi katika kuchochea maendeleo ya nchi.

Wakati jambo la nne likiwa ni ajenda ya maendeleo ya nchi, huku jambo la mwisho likiwa ni mustakabali wake kuhusu masuala ya siasa.

“Katika tafakari yangu ya kuhama, nilipitia maeneo kama matano ambayo nimefanyia kazi, niliangalia ushiriki na mchango wangu kwenye siasa za CUF, mgogoro unaoendelea kukikumba CUF, eneo la tatu ambalo nimelitafakari kwa upana sana ushiriki wangu kama kijana na kiongozi katika kuchochea maendeleo ya nchi, jambo la nne ajenda ya maendeleo ya nchi, la mwisho ni ustakabali wangu kuhusu masuala ya siasa,” amesema Mtatiro.

Mtatiro amesema ametumia muda wa mwezi mmoja kutafakari uamuzi huo, na kubaini kwamba huu ni muda wake wa kutumia talanta alizo nazo kumuunga mkono Rais John Magufuli kupitia CCM.
Aliekuwa Mwenyeki wa kamati ya uongozi wa chama cha wananchi CUF,Julius Mtatiro chini ya Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar as Salaam kuhusu na tarajio lake la kujiunga na chana cha Mapinduzi (CCM).Waandishi wa habari wakimsikilza aliyekua Mwenyekiti wa kamati ya Uongozi wa chama cha wananchi CUF Julius Mtatiro (Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii).

RC HAPI AKUTANA NA WAZEE WA MKOA WA IRINGA, ASIMIKWA RASMI KUWA CHIFU WA WAHEHE

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Ally Salum Hapi leo amefanya mkutano na wazee wa Mkoa wa Iringa ambapo wamemsimika rasmi kuwa Chifu wa wahehe, kama ishara ya kumpokea na kumpa nguvu ya kutawala mkoa wa IRINGA.

Katika mkutano huo uliofanyika ukumbi wa siasa ni Kilimo, wazee wa Iringa wamejitokeza kwa wingi kiasi cha wengine kukosa nafasi ya kukaa na hivyo kusimama na wengine mamia kuketi nje ya ukumbi huo.

RC Hapi alianza kwa kuwapa salamu za Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli na baadae kutoa hotuba ya dira ya uongozi wake mkoani Iringa, vipaumbele vyake na kuwaomba ushirikiano wananchi wa Iringa.

"Mhe Rais amenituma niwape salamu zake. Lakini pia amenipa kazi ya kuhakikisha tunawatumikia na kutatua kero zenu ili wana Iringa mjivunie kuwa hamkukosea kumchagua Rais Magufuli na mjisikie fahari na nchi yenu. Siku zote nitasimama upande wenu wananchi na hasa wanyonge..."
Alisema Hapi

Katika hatua nyingine RC Hapi alitoa fursa wazee hao kueleza matarajio yao na changamoto zao ambazo wangependa serikali ya mkoa izifanyie kazi. Wazee wamemueleza RC Hapi changamoto za huduma zisizoridhisha hospitali ya Mkoa, majibu mabaya ya watoa huduma, migogoro ya ardhi, Maji na mikopo ya kina mama na ucheleweshwaji wa pembejeo kwa wakulima.



Aidha, wazee hao wakiongozwa na Kaimu Chifu wa Wahehe Mzee Gerald Malangalila wameeleza mkutano huo kuwa ni wa kihistoria kuwahi kutokea mkoani Iringa na wazee kujaa ukumbini hadi kukosa mahali pa kuketi.

"Mhe Mkuu wa Mkoa na ndugu wazee, sasa naweza kusema kuwa ile ziara ya Mhe. Rais alipokuja Iringa, mawazo yetu tuliyompa ameyafanyia kazi. Haijawahi kutokea kwa miongo mingi kiongozi akapokelewa kwa umati mkubwa wa wazee kama Huu hapa kwetu. Hii ni dalili kuwa kama ilivyo kwa Rais, nawe umeletwa na Mungu. Sasa tumekutawaza kuwa Chifu wetu, tutakutii, tutakupa ushirikiano na tutakulinda..."
Alisema Chifu Malangalila 

Akitoa neno la shukrani Mzee Agustino Mkini ambaye ni Mwenyekiti wa baraza la wazee wa IRINGA alimshukuru Mkuu wa Mkoa na kumuahidi ushirikiano katika kujenga Iringa Mpya.

"Tunamshukuru sana Mhe Rais kwa kukuleta Iringa. Tunataka yale uliyokua unayafanya Kinondoni tukikuona, uyafanye Iringa..."
RC Hapi alimaliza kwa kula chakula pamoja na wazee wa Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Ally Salum Hapi akisisitiza jambo wakati akizungumza na wazee wa Mkoa wa Iringa, mapema leo mchana.
 Sehemu ya wazee wa Mkoa wa Iringa, wakimsikiliza Mkuu wao wa Mkoa, Ally Hapi.

MKURUGENZI MTENDAJI CRDB BANK, DK. KIMEI ATEMBELEA OFISI ZA MKOA ZA SIDO JIJINI DAR ES SALAAM, AZUNGUMZA NA WAJASIRIAMALI

$
0
0
.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, akizungumza na wajasiriamali wa Sido, wakati wa semina yao, iliyofanyika Sido Mkoani, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga, Ofisa Mtendaja Mkuu wa Kampuni ya Mlako Purified Ice Cubes, Joseph Mlay (kushoto) na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka.
Baadhi ya wanasemina wajasiriamali, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, wakati alipowatembelea na kuzungumza nao katika mafunzo yao ya wiki moja, Sido Mkoani Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
Mwenyekiti wa semina ya wajasiraimali wa Sido, akitoa shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei. 
Meneja wa Kampuni ya kutengeneza manukato na vipodozi ya efa, Obed Musiba (kulia), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia), kuhusu chupa za vipodozi na manukato zinazotengenezwa na moja ya mashine zao kwenye kiwanda chao. Kushoto ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Sido Incubator Programme Star Natural Products, George Buchafwe (kulia), amkimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (katikati), kuhusu vipuri vya mashine za kutengenezea sabuni vinavyotengenezwa na kampuni yake katika Ofisi za Sido Mkoa wa Dar es Salaam, jijini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka. 

MAANDALIZI YA UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA BUYUNGU YAKAMILIKA, WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WAPIGWA MSASA

$
0
0
 Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Buyungu wilayani Kakonko Lusubilo, Kigoma Bw. Joeli Mwakibibi akizungumza na Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Kupigia Kura Jumamosi Agosti 11, 2018 wakati wa mafunzo ya Kusimamia uchaguzi  mdogo wa Ubunge utakaofanyika Agosti 12 mwaka huu.
 Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Buyungu wilayani Kakonko Lusubilo, Kigoma Bw. Joeli Mwakibibi akiwaapisha Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Kupigia Kura Jumamosi Agosti 11, 2018 ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kufuata sheria wakati wa mafunzo ya Kusimamia uchaguzi  mdogo wa Ubunge utakaofanyika Agosti 12 mwaka huu.
 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Athumani Kihamia akizungumza na Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Uchaguzi katika jimbo la Buyungu (hawapo pichani), wilayani Kakonko wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kusimamia Uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo hilo Jumamosi Agosti 11, 2018.
 Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Kiziguzigu Bi. Jesca Masawe akifafanua jambo kwa Wasimamizi wasaidizi wa Vituo vya Kupigia Kura wakati wa mafunzo ya kusimamia uchaguzi mdogo katika jimbo la Buyungu leo.
 Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata ya Kakonko  Bi. Martina Ulungi akitoa ufafanuzi kuhusu namna ya kufunga lakiri (seal) za usalama kwenye maboksi ya kura wakati wa mafunzo kwa Wasimamizi wasaidizi wa Vituo vya Kupigia Kura leo wilayani Kakonko.
 Mafunzo kwa vitendo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi Mdogo jimbo la Buyungu yakiendelea leo katika jimbo la Buyungu.
Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya kupigia Kura wakifanya mazoezi kwa vitendo ya kufunga vituturi vya kupigia Kura vitakavyowekwa kwenye vituo vya kupigia Kura wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kusimamia uchaguzi mdogo leo wilayani Kakonko.
PICHA KWA HISANI YA NEC/BUYUNGU.

MKUU WA MKOA WA RUVUMA CHRISTINA MNDEME AAGIZA TAKUKURU KUICHUNGUZA KAMPUNI YA ARDHI PLAN

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amemwagiza kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Mbinga kuchunguza malipo ya zaidi ya shilingi milioni 525 iliyolipwa kampuni ya ARDHI PLAN na kuzuia madai ya zaidi ya shiingi milioni 500 inayodai kampuni hiyo,kutokana na upimaji wa Ardhi usiozingatia kanuni ya matumizi bora ya Ardhi katika vijiji vya Halmashauri ya Mbinga. Ambapo kampuni hiyo ni ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashuri hiyo Gombo Samandito.

Sherehe za uzinduzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu unaojengwa na halmashauri ya wilaya ya Ruangwa na amezitaka wilaya nyingine kuiga mfano huo.
Uwanja huo unaoitwa Majaliwa umezinduliwa kwa mechi kati ya timu ya wilaya ya Ruangwa ya Namungo FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza na timu ya Simba SC ya Dar es Salaam, ambayo ndio mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara, 2018/2019.
Waziri Mkuu amezindua uwanja huo leo (Jumamosi, Agosti 11, 2018), ambapo ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Ruangwa na wananchi kwa kushiriki kikamilifu katika ujenzi huo.
Uwanja huo unajengwa katika kitongoji cha Mtichi kata ya Nachingwea na ndio utakaokuwa unatumiwa na timu ya Namungo FC kuchezea mechi za nyumbani.Amesema suala la ujenzi wa uwanja ni jambo muhimu na hata Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linahamasisha ujenzi wa uviwanja katika ngazi za mikoa na wilaya ili kutoa fursa kwa wananchi hususani vijana kushiriki katika michezo, hivyo amezitaka halmashauri nyingine ziige mfano wa wilaya ya Ruangwa.
Akizungumzia kuhusu mechi ya kirafiki kati ya timu za Simba na Namungo, Waziri Mkuu amesema “Michezo ni burudani na wananchi wanataka kuburudika, Simba chapeni kazi onesheni uwezo wenu wa mwisho ili Namungo nao waweze kupata ufundi,”.
Pia amesema mbali na kucheza na Simba, timu hiyo ya Namungo inatarajiwa kucheza na timu ya Dodoma FC ya jijini Dodoma keshokutwa (Jumatatu, Agosti 13, 2018). Pia timu hiyo itacheza na timu za Yanga na Azam za jijini Dar es Salaa hivi karibuni.
Waziri Mkuu ametaja faida ya timu kama za Simba, Yanga, Azam na Dodoma FC kucheza na timu ya Namungo FC kuwa ni pamoja na kuwaimarisha wachezaji kwa kuwafanya wajiamini na kuondoa uoga wa kupambana na timu nyingine.
Aidha, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuipongeza timu ya Namungo FC kwa hatua waliyofikia, kwani ilianza kwa kushiriki mashindano ya kugombea kuku, mbuzi na ng’ombe na sasa inashiriki ligi daraja la kwanza Tanzania Bara. “Hakikisheni mnafikia lengo letu la kucheza ligi kuu,”.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi amesema kutokana na jitihahada za kuboresha maendeleo zinazofanywa na Mbunge wa jimbo la Ruangwa ambaye ndiye Waziri Mkuu, uongozi wa mkoa umeamua kuupa uwanja huo jina la Majaliwa ili kumuenzi.
Kwa upande wake, Msemaji wa Timu ya Simba, Bw. Haji Manara amesema timu hiyo ipo Ruangwa na benchi lake lote la ufundi wakiwemo wachezaji 27 na kwamba  ameshangazwa na wingi wa watu waliojaa uwanjani hapo.
“Hakuna uwanja Tanzania unaoweza kujaza watu 20,000 kwa mechi za kawaida nje ya Dar es Salaam na Mwanza. Nimeambiwa kulikuwa na tiketi 20,000 ambazo zimeisha zote,” amesema.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi waliyofika kushudia mechi ya kirafiki kati ya timu ya Simba SC na Namungo FC kwenye uzinduzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Jumamosi 
Agosti 11, 2018. Mchezo ulimalizika kwa mabao 0-0.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na mkewe Mama Mary Majaliwa na viongozi wengine  wakikata utepe kuzindua uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11, 2018
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na viongozi wengine wakikimbia kuashiria kuzinduliwa rasmi kwa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11, 2018
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa Simba, kabla mechi ya kirafiki kati ya timu ya Simba SC na Namungo FC kwenye uzinduzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11, 2018
8
  Wachezaji wa timu ya Simba SC na Namungo FC, wakisakata kabumbu, kwenye mechi ya kirafiki kati ya timu hizo mbili, baada ufunguzi wa uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Agosti 11, 2018.

 

NEWS ALERT: Ving’amuzi vya AZAM , ZUKU na MULTICHOICE vyatakiwa kuendelea kutoa huduma zao bila mashati yeyote

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
 WAZIRI wa UJenzi, Uchukuzi na Mawasiliano , Mhandisi Isaac Kamwelwe amewataka watoa huduma wa ving’amuzi vya Azam, ZUKU pamoja na Multichoice kuendelea kutoa huduma zao za maudhui katika vituo vya televisheni bure kwa channel ambazo ziko katika leseni zao bila ya kuweka masharti. 
 Kamwelwe ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam kuhusiana na kadhia iliyojitokeza kwa watoa huduma hao. 
Amesema kuwa sheria na kanuni za nchi lazima zifuatwe kwa watoa huduma hao kutokana na masharti ya leseni walizopewa. 
 Amesema kuwa ving’amuzi vya Azam, ZUKU pamoja na Multichoice havijazuiliwa bali vitaendelea kutumika kwa mujibu wa masharti ya leseni zao walizopewa na mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) Waziri wa Kamwelwe amesema utaratibu wa huduma za utangazaji kwa mfumo wa dijitali ulifikiwa baada ya maridhiano ya muda mrefu na wadau mbalimbali kwa waraka wa mashauriano na wadau hivyo lazima utaratibu uliowekwa uzingatiwe. 
 Amesema baada ya agizo hilo la serikali tayari Azam wametekeleza hivyo wadau wengine ambao walikuwa hawatoi huduma hiyo waendelee kutoa huduma bure kwa wananchi ili kupata habari katika vituo vya Luninga ambavyo vinatakiwa kurushwa bila malipo.
Waziri wa UJenzi, Uchukuzi na Mawasiliano , Mhandisi Isaac Kamwelwe akizungumza na waandishi habari kuhusiana na sintofahamu za ving’amuzi vya AZAM,ZUKU pamoja na Multichoice kususia utoaji wa matangazo ya Channel ambazo zinatolewa bure Jumamosi Agosti 11, 2018 jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) Mhandisi James Kilaba akifafanua jambo kuhusiana na hatua mbalimbali za TCRA itazozichukua kwa ving’amuzi hivyo ikiwa ni pamoja na ukiukaji wa leseni.

RAIS DKT MAGUFULI ATEKELEZA AHADI YAKE KWA KUKABIDHI MATREKTA 10 KWA CHUO KIKUU CHA KILIMO CHA SOKOINE (SUA) CHA MOROGORO

$
0
0
Na Sultani Kipingo, Kibaha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametekeleza ahadi yake ya kutoa matrekta 10 kwa Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ili kuimarisha utoaji wa mafunzo ya kilimo na kuzalisha wataalamu bora wa kilimo nchini.
Matrekta hayo 10 aina ya Ursus yamekabidhiwa Jumamosi Agosti 11, 2018 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James huko Kibaha Mkoani Pwani na kueleza kuwa SUA imepatiwa matrekta hayo ikiwa ni juhudi za Serikali za kuendeleza kilimo ambacho kinatoa ajira kwa watanzania wengi.
Matrekta hayo yana thamani ya Shilingi Milioni 587.5
Bw. Doto James amekitaka Chuo Kikuu cha SUA kuyatumia matrekta hayo vizuri na kwamba Serikali itafuatilia kupitia kitengo cha Wizara ya Fedha na Mipango cha kufuatilia fedha za miradi ya maendeleo katika taasisi ambayo inapokea fedha za Serikali.
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha SUA Prof. Yonika Ngaga amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi hiyo pamoja na kutekeleza ahadi ya kujenga mabweni ya chuo, ambapo SUA imepokea shilingi Bilioni mbili na kuahidi kuwa chuo kitajiimarisha zaidi katika utoaji taaluma bora ya kilimo inayoendana na wakati wa sasa.
Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya Mandeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Japhet Justine amesema benki hiyo imejipanga kumuondoa mkulima katika kilimo cha jembe la mkono na kumpeleka katika kilimo cha kisasa na kinachotumia zana za kisasa, hivyo ametoa wito kwa wakulima kutumia benki hiyo kupata mikopo itakayowasaidia kulima kisasa
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Prof. Damiani Gabagambi amesema Tanzania ina mahitaji ya matrekta milioni 6 ikilinganishwa na matreka takribani 30,000 yaliyopo na hivyo ametoa wito kwa wakulima na wadau wa kilimo kujitokeza kununua matrekta mengi zaidi ili yatumike kulima katika eneo kubwa linalofaa kwa kilimo hapa nchini.
Akiwa ziarani mkoani Morogoro Mhe. Rais Magufuli alitembelea Chuo Kikuu cha SUA na kujulishwa kuwa chuo hicho kinakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba na ubovu mkubwa wa matrekta na ukosefu wa mabweni ya wanafunzi hali iliyokuwa ikiathiri utoaji wa taaluma ya kilimo na hivyo akaahidi kununua matrekta hayo pamoja na kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni, ahadi ambazo amezitekeleza.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Profesa Raphael Chibunda wapili kutoka (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa NDC Profesa Damian Gabagambi wakwanza (kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo wapili kutoka (kulia), akikata utepe kuzindua Matrekta 10 ambayo ameyakabidhi kwa Chuo hicho cha SUA kutekeleza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akipunga mkono pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuzindua na kuyakabidhi Matrekta hayo 10 kwa Chuo cha SUA katika hafla fupi iliyofanyika katika kiwanda cha kuunganisha Matrekta hayo cha URSUS- TAMCO Kibaha mkoani Pwani.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akiangalia ubora wa  moja ya matrekta hayo 10 aliyoyakabidhi kwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine SUA.

 Sehemu ya Matrekta 10 yaliyokabidhiwa leo kwa Chuo cha SUA ikiwa ni  utekelezwaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.
 Sehemu ya Matrekta 10 yaliyokabidhiwa leo kwa Chuo cha SUA ikiwa ni  utekelezwaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.

 Sehemu ya Matrekta 10 yaliyokabidhiwa leo kwa Chuo cha SUA ikiwa ni  utekelezwaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipotembelea chuo hicho mkoani Morogoro tarehe 7 Mei 2018.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James akizungumza katika hafla hiyo fupi ya kukabidhi ya matrekta 10 aliyoyakabidhi kwa Chuo cha Kilimo cha Sokoine SUA katika kiwanda cha kuunganisha Matrekta cha URSUS- TAMCO Kibaha mkoani Pwani.
PICHA NA MPIGA PICHA WETU

CCM YAFUNGA KAMPENI ZA UDIWANI MTWARA

$
0
0

Joseph Mpangala -Mtwara.

Mbunge wa nanyumbu William Dua amelazimika kupiga magoti kumuombea Kura Mgombea wa Udiwani Kupitia Chama Cha mapinduzi CCM kata ya Nalingu iliyopo Mtwara Vijijini Shaibu Mtavanga katika Siku ya Mwisho ya Kufunga kwa kampeni za Uchaguzi wa Udiwani Zitakazofanyika Jumapili ya Wiki hii.

Katika Mkutano wa Hadhara Uliohudhuliwa na mamia ya wananchii wa Kijiji cha Nalingu Mbunge wa nanyumbu Seleman Dau alisema Kitendo cha Kupiga magoti kwa utamaduni wa kabila lake ni heshima kubwa hivyo Kuwaomba wakazi wa kijiji hicho Kumpigia Kura ya Ndio Diwani anayegombea kwa Tiketi ya Chama cha mapinduzi.

Awali Mbunge wa Mtwara Vijijini Hawa Ghasia{CCM}amesema tayari anavisima 30 ambavyo vipo kwenye Mpango wa Kujengwa ili kumaliza changamoto ya maji iliyopo katika Nalingu hivyo Kuwaomba wananchii kujitokeza Kupiga Kura ili aweze kushirikiana na Diwani atakayewaletea maendeo.

“Tunauwezo wa kujenga Barabara kwa maendelao ya hapa Nalingu,Tayari ninavisima 30 Nahitaji Kujenga ili kuweza Kuondokana na Changanoto ya Maji na hili nawaambia Ukweli Nawaahidi Kuleta Zahanati itakayoweza kutatua Changamoto za Afya hasa kwa akina mama wajawazito”Amesema Hawa Ghasia.

Akimnadi Mgombea wa Udiwani Shaibu Mtavanga Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Mtwara Mohamed Saidi Sinani Amewaahakikishia wananchii wa nalingu Kuwa iwapo watamchagua Mgombea wa CCM watahakikisha matatizo ya kata hiyo yanatatuliwa kwa haraka ziadi.
 Mbunge wa Nanyumbu William Dua akipiga Magoti Kuomba Kura Kwa Wananchii ili waweze kumpigia Kura ya Ndio Mgombea Udiwani Kata ya Naingu iliyopo Mtwara Vijijini Shaibu Mtavanga.
 Mbunge wa Mtwara Vijijini Hawa Ghasia akihutumia wakazi wa nalingu katika Mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi wa udiwani Unaotarajia Kufanyika Jumapili ya wiki Hii.
 Mwenyekiti wa Wilaya ya Mtwara Vijijini Nashir Mfaume Mohamedi akiongea na wananchii wa Nalingu katika Mkutano wa hadhara katika kampeni za Uchaguzi wa Udiwani kata ya nalingu.
  Katibu wa CCM Mkoa wa Mtwara Zakaria Mwansasu akiomba Kura ya Ndio kwa Mgombea wa Udiwani kata ya nalingu Shaibu Mtavanga katika Uchaguzi Unaotarajia Kufanyika Jumapili ya Wiki Hii.
Mwenyekiti Mstaa wa CCM Mkoa wa Mtwara Mohamed Said Sinani akimnadi Mgombea wa Udiwani Kata ya Nalingu Mtwara Vijijini Shaibu Mtavanga katika Kuhitimisha Kampeni za Uchaguzi wa udiwani Mkoani Mtwara.

WEZI WA MAJI YA DAWASCO WAKAMATWA TEMBONI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (DAWASCO) leo limeendesha operesheni ya kuwakamata wale wote waliojiunganishia maji na mkufanya biashara ya maji bila ya kuwa na kibali. Akizungumza Kaimu Meneja wa DAWASCO mkoa wa Kimara, Frank Sulley amesema wameamua kuendelea na operesheni yao maana watu hao wamekuwa wakihujumu shirika hilo kwa kuiba maji huku wakiharibu miundo mbinu. 

"Leo tupo eneo la Kimara Temboni na tumewamata mama (jina kapuni) ambaye alikuw akifanya biashara ya maji na kuharibu miundo mbinu, kwa kukata bomba na kujaza tanki lake na kufanya biashara ya kuuza maji ambapo amekuwa akiuza tsh 6,000 kwa tanki la lita 1,000,' amesema Sulley. 

Amesema kuwa kumekuwa na mchezo wa kujiunganishia maji kwa njia ya kinyemela kwa kukata bomba nyuma ya mita na kutumia huku mita ikiwa haisomi jambo linalohujumu uchumi wa shirika hilo. Aliongeza kuwa amewataka wateja kujitokeza kujisalimisha wale wote waliojiunganishia kinyemela kabla ya muda haujaisha. Wafanyakazi wa DAWASCO wakifukua shimo kuweza kupaini jinsi uunganishani wa maji kinyemela ulivyofanywa na mkazi wa Kimata Temboni jijini Dar es Salaam wakati wa oparesheni ya kuwabaisni wanaofanya biashara ya maji kinyemela iliyofanyika mapema leo. Kaimu Meneja wa DAWASCO mkoa wa Kimara, Frank Sulley akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi stali mpya ya wizi wa maji unavyofanyika jijini Dar es Salaam.
Moja ya Tanki la maji lilipo ardhini linalotumika katika wizi wa maji na kuwauzia watu wa magari makubwa (maboza).
Moja ya muunganiko wa maji mabomba ya maji unaopeleka maji kwenye tanki. 
Gari hili lilikutwa eneo la tukio likijiandaa kupandisha maji na kuenda kusambaza kwa wateja, ambapo wao wamekuwa wakinunua maji kwa tsh 6,000 kwa tanki la lita 1,000 na kwenda kuliuza mtaani kwa tsh 12,00-15,000/- 

Katibu Mkuu wizara ya Fedha Doto James awataka watanzania kuchangamkia fursa ya kununua matrekta (TEMCO) Kibaha

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KATIBU Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Doto James amewataka watanzania kuchangamkia fursa ya kununua matrekta yaliyopo katika kiwanda cha kuunganisha matrekta ambacho kinamilikiwa na Serikali kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Amesema kuwa matrekta hayo yanaubora wa hali ya juu na kuwahakikishia wananchi watakaoyanunua matrekta hayo kutokuwa na hofu kwani uingizwaji wake Serikali inahusika moja kwa moja.Katibu James aliyasema hayo Kibaha mkoani Pwani wakati akikabidhi matrekta kumi kwa Chuo cha kilimo Sokoine (SUA) ikiwa ni utekelezaji wa ahadi I littles na Rais Dkt.John Magufuli baada ya kufanya ziara chuoni hapo .

Alifafanua rais alipofanya ziara chuoni hapo alihaidi mambo mawili la kutoa shilingi bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi ahadi ambayo tayari imetekelezwa na jana amekamilisha ahadi ya kukabidhi matrekta hayo." Ninawataka kwenda kutumia vizuri matrekta haya na kuyafanyia matengenezo iwapo yatahitaji matengenezo kwani sisi watanzania hatuna utaratibu wakutuza vitu hata kama tukiona vimeharibika."alisema James.

Nakuongeza kuwa" Sisi kama serikali tunachombo maalum cha kufatilia fedha na ahadi zote ambazo zinatekelezwa ,hivyo hata matrekta haya tutafatilia kuona yanatumikaje na iwapo mkitumia vizuri na hata kama.mkiomba zingine tutawapa"alisema James.Akizungumzia taasisi hizo za fedha hususani Mfuko wa Pembejeo wa Serikali pamoja na Benki kuwaeleza wananchi kuwa wanafedha kwa ajili ya kilimo ili waweze kuchangamkia fursa hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Doto James akikata utepe pamoja na viongozi wengine wakati wa kukabidhi matrekta kwa Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) cha Mkoani Morogoro kwenye kiwanda cha TEMCO Kibaha mkoani Pwani leo. Matrekta hayo yametolewa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa chuo hicho.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Doto James akikata wakishangilia mara baada ya kukata utepe pamoja na viongozi wengine wakati wa kukabidhi matrekta kwa Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenye kiwanda cha TEMCO Kibaha mkoani Pwani leo. Matrekta hayo yametolewa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa chuo hicho.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Doto James akijaribu kuwasha moja ya Matrekta yaliyokabidhiwa kwa Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenye kiwanda cha TEMCO Kibaha mkoani Pwani leo. Matrekta hayo yametolewa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa chuo hicho.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Doto James akizungumza wakati wa kukabidhi matrekta kwa Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenye kiwanda cha TEMCO Kibaha mkoani Pwani leo.
Dk. Leonard Akwilapo Katibu Mkuu Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia akizungumza katika hafla hiyo kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Doto James . KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>

DKT. KIJAJI AWATAKA WAFANYABISHARA KIGOMA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIBIASHARA NA NCHI JIRANI ZA BURUNDI NA RWANDA

$
0
0
Benny Mwaipaja, Kakonko, Kigoma

NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, amewashauri wakazi wa Wilaya ya Kakongo na mkoa wa Kigoma kwa ujumla kuchangamkia fursa za biashara kati ya mkoa huo na nchi jirani za Rwanda na Burundi kwa kuuza mazao ya kilimo yaliyochakatwa likiwemo zao la muhogo ili waweze kunufaika na biashara hiyo ya mipakani.

Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo mjini Kakonko baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa wilaya hiyo, mkutano uliolenga kujadili fursa na changamoto za ufanyaji biashara katika eneo hilo yakiwemo masuala ya kikodi.

"Nakuomba Mkuu wa Wialaya ya Kakonko uwakutanishe na kuwaunganisha wafanyabiashara hawa ambao nafurahi wengi wao ni vijana ili waandae andiko la namna ya kununua mashine za kuongeza thamani ya mazao ili wauze nje yakiwa yamechakatwa badala ya mfumo wa sasa ambao wanauza mazao ghafi nje ya nchi na hivyo kupata hasara" alisisitiza Dkt. Kijaji

Awali, wafanyabiashara wa Kakonko walimweleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu kijaji, aliyeambatana na Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. Elijah Mwandumbya, kwamba, bei ya zao la muhogo imeshuka kutoka shilingi 600 kwa kilo katika msimu uliopita hadi kufikia shilingi 150, hali iliyowasababishia wakulima maumivu makubwa.

"Wafanyabiashara wanaonunua mazao yetu kutoka Burundi ni watu wa kati kwa maana ya madalali ambao wananunua mazao yetu kwa bei nafuu na kuyapeleka n hini kwao ambako huyachakata na kuyauza kwa bei kubwa nchini mwao na nchi za Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo, hivyo tunaiomba Serikali itupatie mikopo kupitia Benki ys Kilimo ili tusnzishe viwanda vya kuchakata mazao yetu" alieleza mfanya biashara Dkt. Brighton Gwamagobe

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (katikati), akiwaasa wafanyabiashara wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma (hawapo pichani) kutumia fursa zilizopo katika nchi jirani ikiwemo Burundi kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani ili kukuza uchumi wa Wilaya hiyo, alipofanya mkutano na Wafanyabiashara hao Wilayani hapo, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala, na kulia ni Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Kakonko Bw. Kadudusi Bunabuna.

Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA anaye husika na kodi za, ndani Bw. Elijah Mwandumbya, akifafanua masuala mbalimbali ya kikodi kwa wafanyabiashara wa wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma, wakati Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji alipokutana na wafanyabiashara hao kujadili fursa na changamoto wanazopata.


Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala, akizungumza na wafanyabiashara wa Wilaya hiyo wakati wa Mkutano kati ya Wafanyabiashara hao na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (hayupo pichani).

Mfanyabiashara wa Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma Bw. Musa Ndiliwe, akieleza kuhusu kuimarishwa kwa mazingira bora ya kibiashara katika Soko la Ujirani mwema kati ya yao na wenzao wa Nchini Burundi kwa lengo la kukuza biashara, wakati wa mkutano kati ya wafanyabiashara hao na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) Wilayani hapo.

Maafisa wa Wizara ya Fedha na Mipango walioko kwenye msafara wa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, wakifuatilia mkutano kati ya Serikali na wafanyabiashara wa wilaa ya Kakonko mkoani Kigoma.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>

WAZIRI LUGOLA AENDA KUHANI MSIBA NYUMBANI KWA MWANAHABARI MAREHEMU SAGATI, MWIBARA WILAYANI BUNDA

$
0
0


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akiweka shada la maua kwenye kaburi la Mwanahabari marehemu Shadrack Sagati, katika Kijiji cha Mwiruruma, Kata ya Iramba, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Waziri Lugola alifika msibani ili kutoa pole kwa wafiwa kijijini hapo, leo Jumamosi Agosti 11, 2018. Wapili kutoka kulia ni Mfungo Sagati, baba wa marehemu, na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Isaka Mahera. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kushoto) akimpa mkono wa pole Mfungo Sagati, baba wa Mwanahabari marehemu Shadrack Sagati, mara baada ya Waziri huyo kufika cha Kijiji cha Mwiruruma, Kata ya Iramba, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani wa Mara kwa ajili ya kutoa pole kwa familia.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (katikati) akizungumza na Dora Mwishangi (kushoto), mama mdogo wa Mwanahabari marehemu Shadrack Sagati, katika Kijiji cha Mwiruruma, Kata ya Iramba, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara kwa ajili ya kutoa pole kwa familia, leo Jumamosi Agosti 11, 2018. Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Isaka Mahera. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (katikati) akisaini kitabu cha maombolezo, alipofika nyumbani kwa Mwanahabari marehemu Shadrack Sagati, aliyefariki kwa ajali ya gari mkoani Geita Julai 31, 2018. Kushoto ni Mfungo Sagati, baba mzazi wa marehemu, na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Isaka Mahera. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

ASASI ZA KIRAIA ZAOMBWA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI KUTATUA CHANGAMOTO MBALIMBALI

$
0
0

Asasi za kiraia zimeombwa kushirikiana na wananchi katika kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa upatikanaji wa huduma ya maji. 

Diwani wa Kata ya Kwembe wilayani Ubungo, Dweza Kolimba amesema asasi za kiraia zina nafasi kubwa ya kuleta maendeleo katika jamii kwa kushirikiana na wananchi na watendaji wa serikali. 

Akizungumza katika semina iliyoandaliwa na asasi ya Pakacha kwa ajili ya kujadili utatuzi wa changamoto ya maji, kuanzia ufuatiliaji wa rasilimali fedha na utekelezaji wake, Kolimba amesema upatikanaji wa maji katika kata yake umekuwa wa shida, hivyo kupitia asasi kama ya Pakacha, wananchi wanaweza kuelimishwa kushirikiana na viongozi ili kutatua kero hizo. 

Amesema upatikanaji wa maji umekuwa wa shida katika kata yake, huku akisema kuwa wananchi wengi watapata maji baada ya mradi mkubwa wa Luguruni kukamilika. “Tayari mabomba yamesambazwa, hivyo tunaomba mradi huu uishe mapema ili watu wapate maji,” amesema Kolimba. Everyline Francis, mjumbe wa kamati ya maji ya Kata ya Kwembe amesema jamii ipewe elimu ya kutunza vyanzo vya maji na kuzuia uharibifu wa mazingira. 

Upatikanaji wa maji umekuwa na changamoto katika kata za Kwembe, Msigani na Kibamba, hivyo asasi ya Pakacha, kwa ufadhili wa The Foundation For Civil Society kulazimika kutoa elimu kwa wananchi juu ya ufuatiliaji na utunzaji wa vyanzo vya maji. 

Akizungumza kwa niaba ya Mhandisi wa maji wa Manispaa ya Ubungo, Hamad Sendekwa amesema ameomba wananchi washirikiane na watendaji ili kutatua kero za maji na jitihada zinaendelea kuhakikisha huduma hiyo muhimu inapatikana wakati wote. Alisema ushirikiano huo utasaidia kuibua changamoto zinazokwamishwa na rasilimali fedha au kutowajibika kwa baadhi ya watendaji. 

Alisema asasi zinaweza kuleta mabadiliko kwa kufuatilia miradi ya maji, ambayo inakwamishwa kwa sababu mbalimbali na kuwaelimisha wananchi jinsi ya kulinda miundo mbinu ya maji na ufuatiliaji wake. Katibu wa Pakacha, Haroun Jongo amesema lengo la semina hiyo ni kutoa msukumo kwa utelekezaji wa miradi ya maji kwa kuibua hoja kwa wananchi, kwa lengo moja tu, kuleta maendeleo. 

Amesema lengo la semina hiyo ni kuleta jukwaa la majadiliano kati ya viongozi, wananchi na watendaji wa serikali za mitaa ili kutatua kero za maji kwa wananchi kupitia mfumo wa Pets. Pets ni mfumo unaowezesha ufuatiliaji matumizi ya rasilimali za umma zinazotoka Serikali Kuu au halmashauri kwa maendeleo ya wananchi kuanzia ngazi za mitaa hadi kata na kuendelea. 

Mwezeshaji, Enock Daniel Kijo akitoa mafunzo kwa washiriki wa semina ya maji iliyoandaliwa na asasi ya Pakacha Group kwa ufadhili wa The Foundation For Civil Society kwa kata za Kwembe, Msigani na Kibamba za Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. 

MBUNGE WA ZAMANI WA UKONGA MWITA WAITARA AMWAGA CHECHE

AL MUNTAZIR SEMINARI YAWAKUTANISHA WANAFUNZI BARANI AFRIKA NCHINI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

SHULE ya sekondari ya Seminari ya Kiislamu Al Muntazir kwa mara nyingine tena wamewakutanisha wanafunzi wa shule za Sekondari nchini na nje ya nchi kwa lengo la kufanya mashindano ya kujadili mada mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Mjadala huo umepewa jina la "Mwalimu Nyerere Schools Invitational Debate Championships" ili kuwajenga na kuwaandaa wanafunzi hao kuwa wataalamu na wajuzi kwa miaka ijayo.Akizungumza na vyombo vya habari Mkuu wa shule ya Al Muntazir Reuben Kimani ameeleza kuwa mashindano hayo kwa shule za Sekondari na hiyo ni mara ya tatu yamefanyika yakihusisha washiriki zaidi ya 200.

Na hiyo ni kwa lengo la kuwafanya wawe na fikra pana kwa elimu ya chuo watakayoendelea nayo, ambapo ameeleza kuna shule kutoka Zimbabwe na Kenya na wenyeji Tanzania wakiwakilishwa na shule za Tusiime, Shaaban Robert, shule ya wavulana na wasichana Feza, Aghakan na wenyeji Al Muntazir.

Aidha ameeleza kuwa mashindano hayo yatachukua siku 3 wale watakaofanya vizuri watatunukiwa vyeti na watashiriki mdahalo mkubwa utakaofanyika Desemba mwaka huu nchini Botswana. Kuhusiana na maandalizi kwa wanafunzi wao Kimani ameeleza kuwa wametoa mafunzo kwa wiki mbili yakihusisha utafiti hivyo hawana shida kwa shindano hilo na amewataka wanafunzi kuja kujishiriki kwa kutazama na kupata uzoefu kutoka kwa wanafunzi kutoka barani Afrika.

Mwalimu na mlezi wa klabu ya Lugha ya kiingereza kutoka Al Muntazir Seminari Bi. Getrude Mtenga akieleza namna shule yao ilivyojipanga katika kukabiliana na mashindano hayo.
Mkuu wa shule ya Sekondari ya Seminari ya Al Muntazir, Reuben Kimani akitoa neno kwa washiriki kabla ya kuanza kwa mashindano hayo.
Baadhi ya wanafunzi walioshiriki mdahalo huo kutoka shule za sekondari nchini.
Wanafunzi kutoka Zimbabwe (wenye suti za bluu) wakisikiliza mjadala uliokuwa unaendelea.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>

NAONA MBOWE NAYE AMEAMUA KUWAFUATA WAITARA, MTATIRO !

$
0
0
Na Said Mwishehe

SITAKI kuamini hiki...yaani hata Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe naye ameamua kuhamia CCM.

Ni nini kimetokea kwa Mbowe?Hivi kweli ameamua kwa ridhaa yake kujiunga CCM? Amenunuliwa?Ujue unaposikia Mbowe naye ameamua kujiunga CCM lazima kuna maswali ya msingi ambayo utajiuliza tu.

Au Mbowe ameamua kuondoka Chadema kutokana na kulalamikiwa na baadhi ya wabunge wa chama hicho kuwa anaendesha chama kwa maamuzi yake.Hili sidhani.Haiwezi kuwasababu ya kumfanya Mbowe kujiunga na CCM.

Au ameamua kuondoka Chadema na kuachana na nafasi zake zote alizonazo kwasababu tu ya kuchoshwa na tuhuma ambazo zinaelekezwa kwake kila kukicha na wale wanaohama kuwa hataki kuachia Uenyekiti kwa wengine.Hata hivyo kwa kuwa Mbowe yupo nitaelewa tu sababu zilizomfanya naye aondoke Chadema na kwenda kujiunga na CCM.

Hata hivyo wakati hayo yakiendelea nikawa natafakari hivi ni kweli Mbowe hizi habari za kwamba ameondoka Chadema na kujiunga na CCM.Binafsi sawa nilishangaa kusikia Mbowe kaondoka Chadema lakini kwa hali ya kisiasa nchini inavyoendelea nikaona huenda anaweza kuwa na uamuzi huo na ni haki yake kimsingi.

Wakati bado naendelea kutafakari sababu za Mbowe kuondoka Chadema ...napigiwa simu na marafiki zangu wengine wakiniambia Mbowe ameitisha mkutano anazungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake.Habari za Mbowe kuamua kuitisha mkutano zikaanza kunipa picha na kuanza kuamini huenda ikawa kweli.

Nikaona isiwe tabu acha niende nikamsikilize angalau niwe na cha kuwaambia watanzania kupitia chombo changu cha habari ninachofanyia kazi.Nikauliza muda wa mkutano nikaambiwa. Sikutaka kupoteza muda nikachukua 'not book' yangu na kalamu na kwa kuhakikisha napata tukio vizuri nikabeba na kamera kwa ajili ya picha.

Nikaingia kwenye daladala huyo hadi nyumbani kwa Mbowe.Nilipofika nikakutuna na waandishi wengine wengi tena wengi kweli kuliko hata wale waliojitokeza wakati ule anazungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu mwaka 2015.Muda ulipowadia Mbowe akaingia eneo la mkutano.Wakati anaingia kwenye eneo la mkutano hakuwa na kiongozi yoyote maana aliingia peke yake tu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>
Viewing all 110089 articles
Browse latest View live




Latest Images