Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110115 articles
Browse latest View live

SIMBA DAY 2018: MBWEMBWE ZATAWALA UTAMBULISHO WA WACHEZAJI, BENCHI LA UFUNDI LA SIMBA SC...


MTENDAJI MKUU, MAHAKAMA YA TANZANIA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI MBALIMBALI YA UJENZI WA MAHAKAMA NCHINI

$
0
0
Na Festo Sanga, Mahakama ya Mkoa- Kigoma

Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Bw. Husssein Kattanga amefanya ziara mkoani Kigoma na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Mahakama Kuu lililoanza kujengwa rasmi tarehe Oktoba 28, 2017 chini ya mkandarasi Masasi Construction Co Ltd. 

Ujenzi huo wa Jengo la Mahakama Kuu utasogeza huduma za Kimahakama karibu na wananchi wa Mkoa huo kwani wamekuwa wakisafiri kutoka Kigoma kwenda Tabora kufuata huduma za Mahakama Kuu.

Katika ziara hiyo Mtendaji Mkuu wa Mahakama alipata fursa ya kutembelea mahakama ya Wilaya Kasulu na kukagua ujenzi wa Mahakama ya Wilaya Kasulu inayotegemewa kumalizika mwezi April 2019 chini ya Mkandarasi M/S Molad Tanzania LTD.

Ujenzi wa Mahakama mbalimbali nchini unalenga katika kusogeza huduma ya haki karibu zaidi na wananchi na vilevile ni utekelezaji dhahiri wa nguzo ya pili ya mpango mkakati wa Mahakama (2015/2016-2019/2020) ya upatikanaji wa haki kwa wakati.

Aidha ujenzi wa jingo hilo la Mahakama na unaotarajiwa kukamilika mwezi Juni 2019 utawezesha uhifadhi wa kumbukumbu na nyaraka mbalimbali na kuimarisha matumizi ya vifaa vya TEHAMA katika huduma ya utoaji haki.
Hali ya jengo la Mahakama kuu kanda ya Kigoma lilipofikia
Mtendaji Wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma Bw. Moses Mashaka akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi mbele ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga na Mtendaji wa Mahakama Kuu, Bw. Leonard Magacha.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Bw Hussein Kattanga (wa kwanza kulia) akikagua kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Mahakama ya Wilaya Buhigwe ikiwa ni muendelezo wa kusogeza huduma kwa wananchi mkoani Kigoma.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama Bw. Hussein Kattanga akitoa maelekezo alipotembelea ujenzi wa Mahakama ya Wilaya Kasulu mkoani Kigoma katika ziara yake aliyofanya Wilayani humo Agosti, 08, 2018.
Picha ya pamoja ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama , viongozi wa Mahakama Mkoa wa Kigoma na wakandarasi wa Masasi Construction wakiwa mbele ya jingo la Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma linaloendelea kujengwa. (Picha na Festo Sanga, Kigoma

WAZIRI LUGOLA ATOA ONYO KALI KWA ASKARI WA USALAMA BARABARANI...

WAZIRI MWAKYEMBE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA YA MZEE MAJUTO ALIYEFARIKI JANA

$
0
0

. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) akizungumza na aliyekuwa nguli wa filamu nchini Bw. Amri Athumani maarufu kama King Majuto Enzi za uhai wake.

TANTRADE WAIBUKA WASHINDI WA TATU MAONESHO YA KILIMO KITAIFA (NANE NANE) MKOANI SIMIYU

$
0
0
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa akimkabidhi Cheti  Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Bw. Edwin Rutageruka baada ya Banda la TanTrade "Business Clinic" kuibuka Mshindi wa Tatu kwenye Maonesho ya Kilimo Kitaifa (Nane Nane 2018) yaliyofanyika Mjini Bariadi Mkoani Simiyu. Banda hilo lilizijumuisha Taasisi za Udhibiti za Serikali kwa lengo la kutatua changamoto za Wakulima, Wavuvi, Wafugaji na Wafanyabiashara waliotembelea Maonesho hayo yaliyovutia Wananchi wengi.

Dk.Shein akutana na Ujumbe wa UAE Ikulu Zanzibar.

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake uliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni  mwa mwaka huu,[Picha na Ikulu.] 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy (katikati) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake uliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni  mwa mwaka huu,[Picha na Ikulu.] 09/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na  Waziri wa Nchi Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali ya Nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bibi Reem Ibrahim Alhashimy baada ya mazungumzo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake waliofika nchini kufuatia ziara ya Rais.aliyoifanya mwanzoni  mwa mwaka katika Nchi hizo,[Picha na Ikulu.] 09/08/2018.

NAIBU WAZIRI WA MADINI ATOA HEKO KWA NFRA KWA ELIMU WANAYOITOA KUHUSU UHIFADHI WA MAHINDI BAADA YA KUVUNA

$
0
0
Na Mathias Canal, NFRA-Simiyu

Naibu Waziri wa Madini Mhe Stanslaus Nyongo amepongeza Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwa elimu wanayoitoa kuhusu njia bora za kuhifadhi nafaka ya mahindi mara baada ya kuvuna.

Nyongo ametoa pongezi hizo jana 8 Agosti 2018 wakati akizungumza na uongozi wa NFRA mara baada ya kutembelea banda la NFRA kwenye maadhimisho ya maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu ambapo Rais mstaafu wa srikali ya awamu ya tatu Mhe Benjamini Willium Mkapa ndiye alikuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho hayo.

Pamoja na mambo mengine Mhe Naibu Waziri Nyongo amepongeza elimu inayotolewa kuhusu utunzaji huo wa mahindi mara baada ya kuvuna kwa kufuata taratibu zote za kuvuna wakati muafaka, ikiwa ni pamoja na Kukausha vizuri mahindi baada ya kuvuna.Mhe Nyongo pia amepongeza elimu inayotolewa na NFRA kuhusu utambuzi wa mahindi kama yamekauka kwa kutumia njia za kienyeji ambazo ni rafiki kwa wakulima wa chini pamoja na njia za kisasa.

Pia alijionea na elimu kuhusu matumizi bora ya mifuko ya kuhifadhia mahindi ikiwa ni pamoja na mifuko ya PICS, Vihenge vya chuma sambamba na maghala ya tofali.Alisema kuwa njia hizo zitaleta ufanisi iwapo mahindi yameandaliwa vizuri kabla ya kuhifadhi huku akiisihi NFRA kuongeza nguvu katika utoaji elimu ili wakulima waweze kunufaika kwani mkulima akielimika ipasavyo ni sehemu ya mafanikio ya mtu mmoja mmoja sambamba na ukuzaji wa uchumi wa Taifa.
Naibu Waziri wa Madini Mhe Stanslaus Nyongo akisikiliza maelezo kuhusu uhifadhi wa nafaka ya mahindi mara baada ya kutembelea banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwenye maadhimisho ya maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 8 Agosti 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal-NFRA)
Naibu Waziri wa Madini Mhe Stanslaus Nyongo akisikiliza maelezo kuhusu uhifadhi wa nafaka ya mahindi mara baada ya kutembelea banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwenye maadhimisho ya maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 8 Agosti 2018.
Baadhi ya wananchi wakipata elimu kuhusu njia bora za kuhifadhi mahindi baada ya kuvuna mara baada ya kutembelea banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwenye maadhimisho ya maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 8 Agosti 2018.
Baadhi ya wananchi wakipata elimu kuhusu njia bora za kuhifadhi mahindi baada ya kuvuna mara baada ya kutembelea banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwenye maadhimisho ya maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 8 Agosti 2018.

SPIKA NDUGAI AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA YA KONGWA

$
0
0
 Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kongwa avalishwa rasmi vazi la jadi la uchifu na kupewa mbuzi na wazee wa jadi kama ishara ya heshima na kukubalika katika Kijiji cha Nghumbi kiliopo wilaya ya Kongwa.
 Wananchi mbalimbali wa Kijiji cha Gomaye wakimsikiliza kwa makini Mheshimiwa Spika Job Ndugai ambaye alifanya ziara katika Kijiji hicho mapema leo.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kongwa akilisikiliza kwa makini kikundi cha ngoma ambacho kilitoa buruduni katika Kjiji cha Njoge wilaya ya Kongwa. Spika anatarajia kutembelea vijiji kumi na mbili katika ziara yake wilayani humo.

KIJIJI CHA CHIMBILA B KUSAMBAZIWA MAJI-MAJALIWA

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga sh. milioni 250 kwa ajili ya usambazaji wa huduma ya maji safi katika kijiji cha Chimbila ‘B’ kichopo kata ya Mnacho.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Agosti 9, 2018) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mnacho wilayani Ruangwa akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi wilayani hapa.Waziri Mkuu amesemaSerikali imedhamiria kumaliza tatizo la maji, ambapo itahakikisha wananchi wanapata huduma hiyo katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Amesema mbali ya maji kusambazwa kwa wananchi, pia yatasambazwa kwenye taasisi zote za umma zikiwemo shule za msingi na sekondari pamoja na vituo vya kutolea huduma za afya.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea shule ya Sekondari ya Mnacho na kuzungumza na wanafunzi, ambapo amesema Serikali inatarajia kujenga mabweni mawili katika shule hiyo ili wanafunzi waweze kuishi shuleni na kupata fursa nzuri ya kujisomea.Waziri Mkuu ameyasema hayo baada ya wanafunzi wa kike shuleni hapo kuiomba Serikali iwajengee mabweni ili waweze kuishi shuleni na kupata muda mwingi wa kujisomea.

Wanafunzi hao wamemueleza Waziri Mkuu kwamba kitendo cha kuishi nyumba kinawakosesha muda wa kujisomea kwa sababu ya hupangiwa kazi nyingi wanapofika nyumbani, hivyo kukosa muda wa kujisomea.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, AGOSTI 9, 2018.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnacho iliyopo katika Kijiji cha Chimbila B, Kata ya Mnacho Wilayani Ruangwa, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku nne, Agosti 9 2018 .
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifurahia jambo na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnacho iliyopo kwenye Kata ya Mnacho Wilayani Ruangwa, Agosti 9 2018. (Picha na Ofisi ya Naziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Kaimu Mkuu wa Shule Muhsin Ibrahim, baada ya kukagua darasa la kompyuta katika Shule ya Sekondari Mnacho iliyopo kwenye Kata ya Mnacho Wilayani Ruangwa Agosti 9 2018. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Chimbila B, kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Mnacho iliyopo kwenye Kata ya Mnacho, Agosti 9 2018. (Picha na Ofisi ya Naziri Mkuu).

WAJAWAZITO CHALINZE WAKEMEWA KUTUMIA DAWA ZA KIENYEJI WAKATI WA KUELEKEA KUJIFUNGUA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,CHALINZE .

HOSPITAL ya wilaya ya Chalinze ,Msoga mkoani Pwani ,inakabiliana na changamoto za uzazi ambapo baadhi ya akinamama wamekuwa wakitumia dawa za mitishamba ili kujifungua haraka hali inayosababisha wakati wa kujifungua kuwa na uchungu mkali ,mtoto kuchoka na kutokwa damu nyingi. 

Mganga mfawidhi katika hospital hiyo Patricia Kihula ,alisema wapo akinamama wajamzito wanaoshikwa uchungu kisha kunywa mizizi ama dawa za kienyeji jambo ambalo ni hatari kwa mama na mtoto. Alisema kwasasa wanaendelea kutoa elimu katika klinik . 

Patricia alisema ,hali hiyo inasababisha mama akiwa tayari kanywa mizizi mchungu unakuwa mkali kabla ya njia kufunguka na mtoto kuchoka toka akiwa tumboni . “Tunatoa elimu kwa jamii wasiwe na tabia hiyo ,”na sisi tumeanza kupambana na tabia hiyo kwa kuwapa chai kabla ya kujifungua kwani tumegundua wanapewa dawa hizo ndani ya chai “. 

” Tumetoa maagizo chai inapaswa kutolewa kituoni hapa hapa ,na chai ikitoka nyumbani tunamwelekeza aliyeleta chai aanze kuionja ili kujiridhisha isiwe na dawa za kienyeji”alifafanua Patricia. Patricia alieleza kuwa , hakuna kesi ya kifo cha mtoto ama mama na badala yake zipo kesi mbili kila mwezi, za mama kuwa na uchungu mkali ,kutokwa damu nyingi au mtoto kutokwa kachoka sana . 

“Endapo inatokea mama kutokwa damu nyingi tunawapelekea hospital ya rufaa ya Tumbi kwa ajili ya upasuaji ili kuokoa maisha ya mama na mtoto na akitokwa damu nyingi pia huwa tukimchunguza kujua chanzo na hupatiwa matibabu” Patricia aliiomba akinamama wajawazito waache kutumia vitu,ama madawa ya majani,mitishamba ,dawa za kienyeji kwa kuweka kwenye njia ya uke ama kunywa bali wakisikia uchungu wakimbilie hospital kupata matibabu ya uhakika. 


Nae mganga mkuu wa halmashauri ya Chalinze, Rahim Hangai ,alisema wamepokea kesi za aina hiyo ambapo wameanza kutoa elimu ili kupunguza tatizo hilo . Alielezea ,wakitumia dawa hizo husababisha kupata uchungu wa kasi na kupasua kizazi ama mtoto akafa kabla ya kuzaliwa . Dk.Hangai alisema, dawa za kienyeji haziongezi uchungu ,waepuke madhara ambayo yataleta athari kwao. Mamamjamzito Hamisa Kheri alisema wengi wao wanajidanganya kutumia dawa hizo ili kuzaa haraka bila ya kuwa na uchungu kwa muda mrefu.

Mganga Mfawidhi hospital ya wilaya ya Chalinze Msoga,Patricia Kihula akitoa ufafanuzi wa jambo ,wakati mbunge wa Chalinze Ridhiwani alipokwenda kutembelea hospital hiyo .(picha na Mwamvua Mwinyi) 

Halmashauri Zatakiwa Kutenga Maeneo ya Kilimo kwa Vijana

$
0
0
Na. Georgina Misama - MAELEZO

Halmashauri zote nchini zimetakiwa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya Vijana kuyatumia katika shughuli za kilimo.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dodoma na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Antony Mavunde wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu maadhisho ya siku ya Vijana Duniani.

Mavunde alisema hadi hivi sasa Serikali imetenga takribani hekta laki mbili katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwapa vijana fursa ya kuyatumia katika shughuli za kilimo."Nazitaka Halmashauri zote nchini ambazo bado hazijatenga maeneo hayo, kufanya hivyo ili kuendana na kauli mbiu ya mwaka 2018 inayosema 'Mazingira salama kwa Vijana' ambapo serikali ina wajibu wa kuandaa mazingira hayo kwa vijana." alisema Mavunde.

Akiongelea kuhusu mwitikio wa vijana kwenye shughuli za kilimo, Mavunde alisema kuwa vijana wengi wameanza kujishughulisha katika kilimo na ipo mifano mingi hai ya vijana walioamua kujiajiri kwenye kilimo biashara kama SUGEKO na wanafanya vizuri.

Wakati huo huo Mhe. Mavunde amesema kuwa, Agosti 11 litafanyika kongamano kubwa la Vijana na Wadau wa Maendeleo ya Vijana katika Ukumbi Wa Mikutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mgeni rasmi katika kongamano hilo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo.KUSOMA ZAIDI  BOFYA HAPA>>>>>>

PASS VINARA KATIKA MAONESHO YA NANE NANE KWA TAASISI ZISIZO ZA KISERIKALI

$
0
0
Mgeni rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya Nane nane na Rais Mstaaafu wa awamu ya tatu,Benjamini Mkapa akikabidhi cheti kwa Mkurugenzi wa Biashara wa Taasisi ya kusaidia sekta binafsi ya Kilimo nchini (PASS) Killo Lusewa baada ya taasisi hiyo kuibuka kinara wa maonesho hayo kwa taasisi zisizo za Kiserikali,maonesho yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu.
  Mkurugenzi wa Biashara wa taasisi ya kusaidia Sekta Binafsi katika Kilimo (PASS) akionesha cheti cha ushindi baada ya taasisi hiyo kushika nafasi ya kwanza kwa taasisi zisizo za kiserikali na kukabidhiwa na Rais Mstaafu,Benjamini Mkapa.
Wafanyakazi wa Taasisi ya kusaidia sekta Binafsi katika Kilimo(PASS) wakifurahia mara baada ya kutangazwa washindi wa kwanza  kwa taasisi zisizo za Kiserikali katika maonesho ua nane nane ambayo yamefanyika kitaifa mkoani Simiyu.

WAZIRI PROFESA NDALICHAKO AAGIZA VYUO VINAVYOTOA ELIMU YA 'UBABASHAJI' VIFUTWE

$
0
0
 Na Said Mwishehe, Globu ya jamii 

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ametoa maagizo kwa Baraza la Elimu ya Ufundi(Nacte)kutosita kuchukua hatua ikiwamo ya kuvifuta vyuo ambavyo vitabainika kutoa elimu kwa ubabaishaji.

Pia amelishauri Baraza hilo kuhakikisha linasimamia na kutoa muongozo kuhusu program mbalimbali za utoaji elimu ya ufundi ambayo ametaka iwe inaendana na soko la ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wanapata fursa ya kuajiriwa kwa ajili ya kufanya kazi katika miradi mikubwa inayoendelea nchini.

Profesa Ndalichako ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua rasmi Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi nchini ambalo Mwenyekiti wake ni Profesa John Kandoro.

Kuhusu vyuo ambavyo vinashindwa kutoa elimu bora, Profesa Ndalichako amesema baraza hilo lisisite kuchukua hatua ikiwamo ya kuvifutia usajili vyuo ambavyo vitabainika kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.

Amefafanua haiwezekani vijana wawe wanalipa fedha kwenye vyuo ambavyo elimu wanayotoa ni ya ubabaishaji na kwamba hilo halikubaliki na lazima hatua zichukuliwe.

“Kuna vyuo ambavyo vipo kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za Serikali za kutoa elimu bora lakini pia kuna vyuo ambavyo vimeanzishwa kwa ajili ya biashara na hivyo ndivyo vyenye matatizo.“Kama kuna mtu aliamua kuwekeza kwenye kunzisha chuo kwa ajili ya kufanyabiashara basi atambue ni bora atafute kazi nyingine ya kufanya na sio hiyo tena,”amesema Profesa Ndalichako.
 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungunza leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua rasmi Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
 Baadhi ya washiriki kwenye uzinduzi wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi wakimsikiliza mgeni rasmi Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako(hayupo pichani).
 Mkurugenzi wa Nacte akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi.
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi Profesa John Kandoro akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Baraza hilo.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

MFUMUKO WA BEI WA TAIFA UMEPUNGUA KUFIKIA ASILIMIA 3.3

$
0
0

Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.

Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Julai, 2018 umepungua hadi kufikia asilimia 3.3 ikilinganishwa na asilimia 3.4 mwezi Juni, 2018.

Hayo yameelezwa leo na Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa sensa na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ephraim Kwesigabo alipokuwa akitoa taarifa ya mfumuko wa bei kwa mwezi Julai mwaka huu.Kwesigabo amesema, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 imepungua ikilinganishwa na kasi ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 kumechangiwa hasa na kupungua kwa mfumuko wa bei wa baadhi ya bidhaa za vyakula, ambapo bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei kati ya Julai, 2017 na Julai 2018 ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 9.5, mtama kwa asilimia 17.8, unga wa mihogo kwa asilimia 14.1, matunda jamii ya machungwa kwa asilimia 22.2, maharagwe kwa asilimia 5.8 na mihogo mibichi kwa asilimia 12.5,” amefafanua Kwesigabo.

Ameendelea kusema kuwa ni zaidi ya miaka 15 tangu itokee tarakimu kama hiyo ya mfumuko wa bei ambayo iko vizuri kwa uchumi wa nchi.

Aidha ametaja hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya nchi za Afrika Mashariki kama ifuatavyo; Uganda mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 3.1 kutoka asilimia 2.2 kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018. Kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 4.35 kutoka asilimia kutoka asilimia 4.28 kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

Mfumuko wa bei wa Taifa unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Jamii Bw. Ephraim Kwesigabo akitoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei kwa mwezi Julai 2018 leo Jijini Dodoma ambapo mfumuko huo umeshuka kwa asilimia 3.3 kwa mwezi Julai 2018 ikilinganishwa na asilimia 3.4 kwa mwezi June 2018.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Said Ameir akisisitiza jambo wakati wa hafla ya kutoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei kwa mwezi Julai 2018 Jijini Dodoma.

Meneja wa Takwimu za mazingira na uchambuzi Bibi Ruth Minja akisisitiza kuhusu umuhimu wa takwimu katika kuchochea maendeleo .

Makamu Mwenyekiti NEC atembelea Kata ya Mlowa Bwawani kukagua maandalizi Uchaguzi Mdogo

$
0
0
Hussein Makame, NEC aliyekuwa Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mbarouk Salim Mbarouk ametembelea kata ya Mlowa Bwawani katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma kuangalia maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa diwani wa kata hiyo.

Akizungumza na Wasimamizi wa Uchaguzi wa kata hiyo na Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Mtera Elizabenth Gumbo kwa niaba ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mtera, Jaji Mbarouk ameridhishwa na maandalizi ya Uchaguzi wa kata hiyo.

Jaji Mbarouk amewasisitiza wasimamizi wa Uchaguzi wa kata hiyo kutumia vipaza sauti kufikisha ujumbe kwa wananchi kwani njia hiyo itarahisisha kufikisha ujumbe wa uchaguzi kwa wananchi wengi zaidi wakiwemo wasiojua  kusoma na kuandika badala ya kutegemea zaidi taarifa za mabango.

Akitoa taarifa ya maandalizi ya Uchaguzi wa kata hiyo kwa niaba ya, Afisa Uchaguzi wa Jimbo hilo Elizabenth Gumbo alisema maandalizi ya Uchaguzi huo yanakwenda vizuri.Alisema wameshapokea vifaa vya awali vya Uchaguzi ikiwemo mfano wa karatasi ya kupigia, mabango ya Uchaguzi, fomu za Uchaguzi, bahasha za karatasi za kura na fedha za bajeti ya Uchaguzi wa kata hiyo.

Gumbo alisema ameshavitaarifu vyama vya siasa kuwasilisha orodha ya majina ya mawakala wa vyama vyao na kwamba wamewaomba wawsilishe na picha za mawakala hao na ratiba ya kuwaapisha inasubiri muda ambao watakapowasilisha orodha hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC Jaji Mbarouk Salim Mbarouk (kulia) akimueleza jambo  Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Mtera mkoani Dodoma, Elizabenth Gumbo (kushoto) wakati alipotembelea kata ya Mlowa Bwawani. Kulia ni Mwanasheria wa NEC, Hamidu Mwanga.
2 (7)
Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Mtera, Elizabenth Gumbo (kushoto) akieleza maandalizi ya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani kata ya Mlowa Bwawani kwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mbarouk Salim Mbarouk (katikati).Kulia ni Mwanasheria wa NEC Hamidu Mwanga.
5 (2)
Mwanasheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Hamidu Mwanga (katikati) akizungumza jambo na Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Mtera mkoani Dodoma, Elizabenth Gumbo nje ya jengo la Halmashauri ya Manispaa ya Chamwino mkaoni Dodoma.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Jaji Mbarouk Salim Mbarouk.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>


MGALU AMUAGIZA DC SUMBAWANGA KUTUMIA MAMLAKA YAKE KUWATUPA NDANI SAA 48 WASIMAMIZI WA UTEKELEZAJI WA MRADI WA REA

$
0
0

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule kutumia mamlaka yake kuwatupa ndani saa 48 wasimamizi wa utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini (REA) awamu ya tatu wa Kampuni ya Nakuroi Investment iwapo watasuasua katika ujenzi wa miundombinu ya umeme wilayani humo.

Naibu Waziri huyo, ametoa agizo hilo leo akiwa katika kijiji cha Kilyamatundu kilichopo mpakani mwa mikoa ya Mbeya na Songwe tarafa ya Kipeta wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi inayolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu mkoani humo.

Kabla ya kutoa agizo hilo, Naibu Waziri huyo alionyeshwa miundombinu inayowezesha upatikanaji wa umeme katika kijiji jirani cha Kamsamba iliyopo umbali wa mita 100 na kuonyesha kushangazwa kwanini Kijiji cha Kilyamatundu kinashindwa kunufaika na huduma ya umeme kwa kuwa miundombinu ipo jirani kiasi hicho.

"Mkandarasi nataka nguzo na vifaa vingine vifike hapa Alhamisi ijayo kama ulivyoahadi na ujenzi wa miundombinu ya umeme ianze mara moja,mkuu wa wilaya hakikisha inatumia mamlaka yako kuwatupa ndani saa 48 hawa jamaa kama watasuasua kutekeleza mradi huu, sisi lengo letu umeme upatikane hapa kijijini haraka iwezekanavyo" alisema
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akihutubia wananchi wa kata ya Mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, leo akiwa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu. (0163 -205, 207)
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwahoji maswali wasimamizi kutoka kampuni ya kampuni ya Nakuroi Investment inayosuasua katika utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa REA awamu ya tatu katika vijiji vya mkoa wa Rukwa, leo mbele ya wananchi wa kata Mtowisa, Sumbawanga mkoani Rukwa. (0179 - 80)
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akitoa ufafanuzi wa jambo kwa msimamizi wa kampuni ya Nakuroi Investment kuhusu ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa umeme katika kijiji cha Kilyamatundu wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ambapo yupo katika ziara ya kikazi mkoani humo. (417)
Baadhi ya watumishi wa Shirika la umeme nchini, Tanesco mkoawa Rukwa wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Subira Mgalu wakati aliwahutubia wananchi wa kata ya Mtowisa mkoani Rukwa leo, ambapo yupo katika ziara ya kikazi ya kukaguautekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu.(0150).


MEYA MWITA ATEMBELEA HOSPITAL YA AGA KHAN JIJINI HAPA LEO

$
0
0

MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo amefanya ziara katika hospitali ya Aga Khan ya jijini hapa na kuwaona wagaonjwa sambamba na kupata nafasi ya kuona maendeleo ya mradi wa upanuzi wa hospitali hiyo ulio mbioni kukamilika .

Katika ziara hiyo , Meya Mwita amekutana na uongozi wa juu wa Hospitali hiyo ikiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Utoaji Huduma za Afya Aga Khan Kanda ya Afrika Mashariki, Sulaiman Shahabuddin ambapo walipata nafasi ya kuzungzumza mambo mbalimbali.

Meya Mwita ameipongeza Taasisi ya Huduma za Afya Aga Khan Tanzania kwa kuamua kuwekeza katika Mkoa wa Dar es Salaam hususani sekta ya Afya ambapo bado changamoto ni nyingi jijini hapa pamoja na nchi nzima.

Aidha Meya Mwita amefarijika kuona hosipitali hiyo imewekeza katika vifaa tiba vya kisasa zaidi kuwemo nchini pamoja na uwepo wa Watanzania wengi katika eneo la utoaji huduma za viwango vya juu kabisa Tanzania.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi za Huduma za Afya Aga Khan Kanda ya Afrika Mashariki Sulaiman Shahabuddin amemshukuru Meya Mwita kwa kutenga muda wake na kutembelea hospitali hiyo.

Amefafanua kuwa "ni faraja kwetu sana kukuona mahali hapa Mstahiki Meya ,Hospitali hii ni kwa ajili ya Wana Dar es Salaam na Watanzania wote, Ninacho mshukuru Mungu ni kuona hospitali hii sasa ikianza kuhudumia hata mataifa ya jirani kama Comoro, Zambia, Malawi, Msumbiji " amesema.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Halmashauri Zatakiwa Kutenga Maeneo ya Kilimo kwa Vijana

SPIKA NDUGAI KUTEMBELEA VIJIJI 12 NDANI YA JIMBO LAKE

$
0
0
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kongwa akilisikiliza kwa makini kikundi cha ngoma ambacho kilitoa buruduni katika Kjiji cha Njoge wilaya ya Kongwa. Spika anatarajia kutembelea vijiji kumi na mbili katika ziara yake wilayani humo.
Wananchi mbalimbali wa Kijiji cha Gomaye wakimsikiliza kwa makini Mheshimiwa Spika Job Ndugai ambaye alifanya ziara katika Kijiji hicho mapema leo.
Wananchi mbalimbali wa Kijiji cha Gomaye wakimsikiliza kwa makini Mheshimiwa Spika Job Ndugai ambaye alifanya ziara katika Kijiji hicho mapema leo.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kutoka kwenye chumba cha mkutano wa Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam. 

 Rais wa Uganda Yoweri Museveni akizungumza na wanahabari hawapo pichani mara baada ya kikao chake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari hawapo pichani mara baada ya kikao chake na Rais wa Uganda Yoweri Museveni Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
Viewing all 110115 articles
Browse latest View live




Latest Images