Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110150 articles
Browse latest View live

Kamishna Mboje atembelea banda la Magereza nane nane Simiyu

$
0
0
 Kamishna wa Huduma za Parole,Viwanda, Huduma za jamii na Programu za Urekebishaji Af. Augustine Mboje  Sangalali(suruali nyeupe) akisalimiana na Mkuu wa Kilimo,Mifugo na Utunzaji wa Mazingira, Kamishna Msaidizi  Mwandamizi wa Magereza Mlasani Deodath Kimaro, alipotembelea Banda la Magereza katika maonesho ya Nane nane yanayofanyika Kitaifa Nyakabindi,Wilayani Bariadi mkoa wa Simiyu.
 Sajini Caroline Mtolera wa Jeshi la Magereza akimuelezea Af. Kamishna Mboje namna ya kutunza mazingira kwa kutengeneza mkaa kwa kutumia mabaki ya taka ngumu.

 Kamishna Mboje akipata maelezo ya shamba darasa toka kwa Mrakibu Msaidizi wa Magereza Nimwindaeli Mzirai alipotembelea banda la Magereza kwenye Nane nane inayofanyika Nyakabindi,Bariadi Mkoani Simiyu.
 Sajini Mateso Alex Linze wa Magereza akimuelezea Kamishna Mboje jinsi ya utunzaji Samaki kwa njia ya kisasa huku banda la kuku likiwa juu ya bwawa la samaki hao.

 Sajini Mahimbo Dafa akimuelezea Kamishna Mboje njia bora na sahihi ya Uhamilishaji wa mbegu za ng’ombe ili kupata mifugo ya kisasa na yenye afya.
Wada Mwinyi  Onanda wa Magereza akimunesha na kumuelezea  Kamishna Af. Mboje mazao mbalimbali yanayolimwa na Magereza mbalimbali kama njia ya urekebishaji wa wafungwa. Picha na Jeshi la Magereza

VODACOM YAWARAHISHIA WATANZANIA KUFANYA MALIPO KATIKA TAASISI ZA SERIKALI KUPITIA M-PESA APP QR

$
0
0
  Mkuu wa Kitengo cha Mwendelezo wa Biashara ya M-Pesa, Vodacom Tanzania Plc,Polycarp Ndekana (Kulia ) akiongea kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzuzi wa huduma mpya na ya kwanza nchini inayomwezesha mwananchi kufanya miamala ya malipo kwa mfumo wa serikali wa Kielektroniki  kwa kupitia Huduma ya M-Pesa APP QR  zaidi ya taasisi za serikali 150 zimesha anza kupokea malipo kwa njia ya huduma  hiyo kwa kupiga *150*00#  wanaoshuhudia kutoka kushoni  Mhasibu wa Fedha  wa RITA, Audiface Cresence  na Afisa Mwandamizi wa Tehama  Wizara ya Fedha , Benard Mabagala.
 Mkuu wa Kitengo cha Mwendelezo wa Biashara ya M-Pesa, Vodacom Tanzania Plc,Polycarp Ndekana (Kulia ) akiwaonyesha  waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,(hawapo pichani) jinsi ya kujiunga na huduma ya malipo kwa njia ya mtandao wakati wa uzinduzuzi wa huduma mpya na ya kwanza nchini inayomwezesha mwananchi kufanya miamala ya malipo kwa mfumo wa serikali wa Kielektroniki  kwa kupitia Huduma ya M-Pesa APP QR  zaidi ya taasisi za serikali 150 zimesha anza kupokea malipo kwa njia ya huduma  hiyo kwa kupiga *150*00#  wanaoshuhudia kutoka kushoni  Mhasibu wa Fedha  wa RITA, Audiface Cresence  na Afisa Mwandamizi wa Tehama  Wizara ya Fedha , Benard Mabagala. 
Mkuu wa Kitengo cha Mwendelezo wa Biashara ya M-Pesa, Vodacom Tanzania Plc,Polycarp Ndekana (kushoto) akimsikiliza Mhasibu wa Fedha  wa RITA, Audiface Cresence (kulia)  wakati akiongea kwa waandishi wa haabari, wakati wa uzinduzuzi wa huduma mpya na ya kwanza nchini inayomwezesha mwananchi kufanya miamala ya malipo kwa mfumo wa serikali wa Kielektroniki  kwa kupitia Huduma ya M-Pesa APP QR  zaidi ya taasisi za serikali 150 zimesha anza kupokea malipo kwa njia ya huduma  hiyo kwa kupiga *150*00#.
 Mkuu wa Kitengo cha Mwendelezo wa Biashara ya M-Pesa, Vodacom Tanzania Plc,Polycarp Ndekana (katikati ) Mhasibu wa Fedha  wa RITA, Audiface Cresence (Kushoto) na Afisa Mwandamizi wa Tehama  Wizara ya Fedha , Benard Mabagala wakiwaonyesha waandishi wa habari jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) vipeperushi vinavyoonyesha   jinsi ya kujiunga na huduma ya malipo kwa njia ya mtandao wakati wa uzinduzuzi wa huduma mpya na ya kwanza nchini inayomwezesha mwananchi kufanya miamala ya malipo kwa mfumo wa serikali wa Kielektroniki  kwa kupitia Huduma ya M-Pesa APP QR  zaidi ya taasisi za serikali 150 zimesha anza kupokea malipo kwa njia ya huduma  hiyo kwa kupiga *150*00#

ALICHOZUNGUMZA DC WA NAMTUMBO MARA TU BAADA YA KUAPISHWA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo

Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Kaguta Museveni kuwasili kesho kwa ziara ya siku moja nchini

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni atafanya ziara ya kikazi ya siku moja hapa nchini tarehe 09 Agosti 2018.

Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano na ujirani mwema uliopo kati ya Tanzania na Uganda.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Rais Museveni atapokelewa na mwenyeji wake Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akiwa nchini, Mheshimiwa Rais Museveni atakutana kwa mazungumzo ya faragha na Mheshimiwa Rais Magufuli yatakayofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yatafuatiwa na Chakula cha Mchana kilichoandaliwa na Mheshimiwa Rais Magufuli kwa heshima ya Mheshimiwa Rais Museveni.

Mheshimiwa Rais Museveni na Ujumbe wake wataondoka nchini siku hiyo hiyo kurejea Uganda.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
07 Agosti 2018

MWENYEKITI WA CCM TARIME ACHANGIA VIFAA VYA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 2.4.

$
0
0
Na Frankius Cleophace Tarime.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tarime Marwa Daud Ngicho amechagia Vifaa mbalimbali katika shule ya Msingi Mturu iliyopo Kata ya Turwa Mjini Tarime Mkoani Mara kwa ajili ya kuanzisha Stationery ya shuke hiyo kwa lengo la kuondokana na adha ambayo wamekuwa wakipata katika kipindi cha Mtihani.

Mwenyekiti huyo ametoa Vifaa mbalimbali ikiwemo Mashine ya kutolea kopi Mitiani huku wazazi na walezi pamoja na wadau wa Elimu wakiunga Mkono harambee hiyo kwa kuchangia zaidi ya shilingi 70,000.Ngicho amesema kuwa ameamua kutoa vifaa hivyo kwa lengo la kuunga jitiada za serikali ya awamu ya tano katika kutoa elimu bure ili kila mtoto wakiwemo watoto wa maskini wanaenda shule.

“Nilipokea barua yenu ya mahitaji hayo yote sasa nimenunua vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi Millioni mbili na Laki Nne wajibu wenu ni kuvitunza ili kizazi na kizazi kiweze kunufaika” alisema Ngicho.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mturu Jumanne Obogo amesema kuwa gharama za kuandaa mitiani kipindi cha Mwaka mzima zilikuwa kubwa ambapo shule hiyo utumia kiasi cha shilingi Mill3.5 jambo ambalo ni changamoto kubwa , hivyo upatikanaji wa vifaa hivyo vitasaida changamoto hiyo hukua wakitoa shukrani zao. 

Pia Mwalimu huyo amesema kuwa licha ya shule hiyo kupatiwa vifaa hivyo bado inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa Matundu ya vyoo na kuomba Mgeni rasmi kuwasaidia kutatua changamoto hiyo ambapo baadhi ya wadau na wazazi katika harambee hiyo wameweza kutoa Mifuko ya Saruji pamoja na ahadi mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa Vyoo hivyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tarime Daud Marwa Ngicho akikabidhi moja ya kifaa kati ya Vifaa vilivyotolewa katika Shule ya Msingi Mturu kwa ajili ya kuanzisha Stationery Vyenye thamini ya Mill2.4 ikiwemo Mashine ya Kutolea Kopi Mitihani.
Wazazi na walezi wakiwa katika harambee ya kuchagia Vifaa vya Stationery katika Shule ya Msingi Mturu ambapo wazazi hao pamoja na walimu na wadau wa elimu wamechangia zaidi ya 70,000.
Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mturu Jumanne Obogo akibainisha changamoto mbele ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime Daud Marwa Ngicho.
Baadhi ya Vifaa vilivyotolewa na Mgeni rasmi Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime Daud Marwa Ngicho vyenye thamani ya shilingi Mill 2.4.

WAZIRI MPINA ATOA SIKU SABA KWA MAKATIBU WAKUU WA KILIMO NA MIFUGO

$
0
0
Na John Mapepele
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ametoa siku saba kwa makatibu wakuu wa Kilimo na Mifugo kuwasilisha wizarani kwake taarifa ya kwanini bei ya mbegu za mahindi na mtama pamoja na gharama za uhimilishaji mifugo nchini ni kubwa licha ya uwepo wa usimamizi wa Serikali,pia kuendelea kuagiza mbegu za matunda na mbogamboga nje ya nchi ambazo zinaweza kuzalishwa hapa nchini.

Mbali na hilo, Waziri Mpina pia amezitaka Taasisi za TPRI,TFDA,TBS na Kurugenzi ya Huduma za Mifugo katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujitathmini upya utendaji kazi wao kama wanastahili kuwepo baada ya kushamiri kwa dawa na viuatilifu vya kilimo na mifugo feki na vilivyokwisha muda wa matumizi na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima,wafugaji na Taifa kwa ujumla.

Akifungua maonesho ya Kilimo Nane Nane, Kanda ya Kaskazini yanayofanyika katika viwanja vya Themi jijini Arusha, Waziri Mpina alisema ni jambo la aibu kwa viongozi kuendelea kuwakutanisha wakulima na wafugaji katika maonesho hayo kila mwaka huku changamoto zao za msingi ikiwemo kuuziwa mbegu kwa bei kubwa, dawa na viuatilifu visizoua wadudu kwenye mazao na mifugo yao zikiwa hazijapatiwa ufumbuzi.

Alisema baadhi ya wazalishaji wa mbegu za kilimo nchini wamekuwa wakiuza kwa bei kubwa kiasi cha kuwakatisha tamaa wakulima kutumia mbegu bora ambapo baadhi ya kampuni zimekuwa zikiuza kilo moja ya mbegu ya mahindi kwa sh. 6,000 wakati bei wanayonunua kwa wakulima wa kilimo cha mkataba cha uzalishaji mbegu kwa kilo ni sh 1,200 na bei ya mahindi ya kawaida kwa kilo ni sh. 600 tu.

Pia gharama za uhamilishaji mifugo nchini dozi moja huuzwa wastani wa sh 3,000 kutoka katika vituo vya Taifa vya uhamilishaji mifugo lakini kampuni binafsi za uhamilishaji huwatoza wafugaji wastani wa sh 20,000 hadi sh 40,000 kwa dozi, gharama ambazo wafugaji wengi hawawezi kuzimudu.

Pia Waziri Mpina aliagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinakuwa na shamba darasa la bwawa la ufugaji wa samaki ili kuongeza upatikanaji wa chakula na biashara ya mazao ya uvuvi, ajira na mapato ya Serikali.

Kuhusu sekta ya mifugo Waziri Mpina alisema licha ya mikoa hiyo ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara kuwa na takribani asilimia 15 ya mifugo yote nchini lakini hakuna kiwanda hata kimoja cha kuchakata mazao ya mifugo hali ambayo inasababisha mifugo mingi kutoroshwa nchi jirani ya Kenya ajili ya kutafuta masoko.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akizungumza

WATANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA MCHICHA NAFAKA

$
0
0
WATANZANIA hususani watoto na akina mama wajawazito wametakiwa kutumia zaidi mchicha nafaka kama chakula kitakachowaongezea viini lishe muhimu kwa afya ya miili yao. 

Wito huo umetolewa mjini Arusha wakati wa Kongamano la linalojadili Afya na na Lishe bora liliwakutanisha wataalamu wa masuala ya lishe kutoka ndani na nje ya nchi wakiwamo wanajamii. 

Kongamano hilo lililoanza Agosti 6 na kukamilika Agosti 9, Mwaka huu linafanyika hapa ambapo wataalamu wanabadilishana uzoefu kuhusu masuala ya afya na lishe bora limeandaliwa na Shirika la World Vission Tanzania (WVT), wakishirikiana na Taasisi ya Amaranth ya Marekani na ECHO. 

Akizungumza kwenye kongamano hilo Mkurugenzi wa Uendeshaji Miradi ya Shirika la World Vission Tanzania, Dk. Yosh Kaslima alisema kupitia shughuli wanazofanya kwenye mikoa 13 na wilaya 36 wamebaini kuwapo tatizo la lishe bora kwa watoto na mama wajawazito. 

“Wananchi hawajui wawalishe nini watoto na akina mama wajawazito, kwa hiyo tunatarajia kupitia kongamano hili washiriki watatoa na kupokea elimu mimea gani ina virutubisho vitakavyowawezesha kuboresha afya za watoto wakiwa wadogo,” alisema Kaslima. 

Kwa upande wake mgeni rasmi katika Kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema, ujumbe wa kongamano hilo unaohamasisha lishe ni muhimu kwani umekuja kwa wakati sahihi. “Hii inakwenda sambamba na Sera ya Taifa ya Chakula na Lishe ya mwaka (2007) inayohamasisha uhusiano wa chakula na lishe katika sekta mbalimbali na utokomezaji wa utapiamlo hasa kwa watoto na kina mama,”

“Kumuelimisha kila mwananchi, aelewe kuwa ana wajibika moja kwa moja kutunza afya yake na ile ya familia yake. Kujenga ushirikiano kati ya sekta ya umma, sekta binafsi, mashirika ya dini, asasi za kijamii na jamii katika kutoa huduma za lishe na afya,” alisema Gmbo kupitia kwa Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega.
 Wataalamu wa masuala ya afya na lishe kwa mama na mtoto wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kongamano la Kimataifa kuhusu Lishe katika maeneo kame nchii lililofanyika mjini Arusha 
Wataalamu wa masuala ya afya na lishe kwa mama na mtoto wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kongamano la Kimataifa kuhusu Lishe katika maeneo kame nchii lililofanyika mjini Arusha katika picha ya pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega

Introducing "Sikutegemea" Official audio by Sampamba


Introducing "FINE GIRL" by Kingsure Ft. Mee Brown & Mapachi

Introducing "TOGOLA" by Nitho

DC ARUMERU AWAFARIJI WANANCHI WA KATA YA MBUGUNI ILIYOKUMBWA NA MAFURIKO

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh Jerry Muro amefanya ziara kata ya Mbuguni,iliyokumbwa na changamoto ya mafuriko Aprili Mwaka huu, ambapo amewatembelea wananchi waliokumbwa na mafuriko hayo na kuwafariji kwa kutoka misaada mbalimbali ikiwemo magodoro,mablanketi, vifaa vya kuhifadhia maji dawa za kutibu maji na vyandarua pamoja na vifaa vya chakula kwa kila Kaya 60 zilizoathirika.

DC Muro pia ametoa msaada wa vifaa vya usafi kwa wanafunzi wa Shule ya mbuguni,ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Mh.Rais John pombe Magufuli katika kuhakikisha mtoto wa kike anapata Elimu bora huku akiwa katika mazingira bora ya kusoma.

Wananchi wamemshukuru Mh Rais kwa kumteua Jerry Muro kuwa Mkuu wa Wilaya ambaye tayari ameanza kuwahudumia kwa kuwaletea misaada. 

Pia wananchi wamempongeza Rais Magufuli kwa kuendelea kutafuta wadau mbalimbali wa Maendeleo ambao wameanza kuunga mkono jitihada za serikali hususani katika upande wa kukabiliana na majanga kupitia kazi nzuri inayofanywa na Shirika la msalaba mwekundu Tanzania ( Tanzania RedCross )
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh Jerry Muro akigawa msaada wa vifaa mbalimbali ikiwemo mablanketi kwa mmoja wa waathiriwa na mafuriko kutoka kijiji cha Mbuguni,ambao walikumbwa na adha ya mafuriko Aprili mwaka huu.
 DC Muro akikabidhi msaada wa vifaa vya usafi kwa  mmoja wa Wanafunzi wa Shule ya mbuguni
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh Jerry Muro akizungumza na Wakazi wa Mbuguni mara baada ya kutoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa waathiriwa wa mafuriko waishio katika kijiji hicho
Baadhi ya vifaa mbalimbali vilivyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh Jerry Muro,ikiwa ni sehemu ya msaada wa vifaa mbalimbali kama vile mablanketi,vifaa vya kufanyia usafi kwa wanafunzi wa shule,Magodoro na vinginevyo kwa waathiriwa na mafuriko kutoka kijiji cha Mbuguni  waliokumbwa na adha hiyo Aprili mwaka huu.

MTIBWA, KMC KUITAMBULISHA REHA FC.

$
0
0
Matokeo mazuri ya kila jambo yanahitaji maandalizi timamu na ndivyo tunavyofanya kuelekea msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.

Wakati maandalizi yakiwa yamenoga jana tumetangaza tarehe rasmi ya utambulisho wa timu kwa wakazi wa Temeke na mkoa wa Dar es salaam kwa ujumla.w

Mtendaji mkuu wa klabu Abubakar Jafo amewaambia wanahabari kwamba kuanzia leo ni wiki ya REHA FC ambapo kilele chake itakua siku ya jumapili kwenye uwanja wa Bandari Tandika. 

"Wiki ya Reha itahusisha shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufungua matawi yetu na kuhitimishwa kwa michezo maalum itakayohusisha timu nne ambazo ni Mtibwa, KMC na Transit Camp  na wenyeji Reha fc" amesema Jafo.

Jafo amesema michezo hiyo itaanza jumamosi kwa mchezo wa mapema saa 8 mchana kati ya Reha dhidi ya Transit Camp na saa 10 jioni Mtibwa itacheza na KMC kisha washindi watacheza fainal siku ya jumapili jioni huku waliofungwa wakicheza mchana. "Siku hiyo tutaitumia kuwatambulisha wachezaji wetu pamoja na benchi la ufundi".
Mtendaji Mkuu wa timu ya Reha Fc Abubakar Jafo 

NEC YAIJIBU CHADEMA UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA BUYUNGU

WAZIRI KALEMANI AWASIMAMISHA KAZI WATENDAJI TANESCO KWA KUSHINDWA KUWASHA UMEME VIJIJINI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii

WAZIRI wa Nishati Dkt.Medard Kalemani amefanya ziara katika Wilaya ya Mkuranga katika kukagua utekelezaji wa utoaji wa huduma ya umeme kwa wananchi na hakuridhishwa na utendaji wa baadhi ya wahusika katika idara hizo na kuamua kuwaweka kando ili wenye kasi watekeleze jukumu hilo.

Katika Ziara hiyo Kalemani  amemuagiza meneja Tanesco  mkoa wa Pwani kumsimamisha kazi  Mhandisi wa Mkoa na  pia amemuagiza meneja wa wilaya ya Mkuranga Mhandisi, Regina Mvungi kumsimamisha mhandisi mwenye dhamana hiyo katika wilaya ya Mkuranga kwa kushindwa kufanya kazi ya kuwasha umeme kwenye vijiji vilivyo kwenye mradi kata ya Vikundi.

Aidha Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ametoa siku 14 Wilayani Mkuranga katika  kuhakikisha umeme unawaka katika vijiji vyote vilivyokatika mpango huo.Waziri hiyo aliyasema hayo Leo hii wakati wa ziara ya kutembelea wilayani Mkuranga ili kuona namna ya upatikanaji wa huduma ya Nishati ya Umeme katika Kata ya Kisiju,Vikindu na Tambani.

Kalemani amesema kuwa mradi wa umeme vijijini (REA) awamu ya pili haikufanya vizuri katika Tarafa ya Kisiju hivyo natoa siku 14 kuanzia kesho kuhakikisha umeme unawaka, aidha Kalemani ametoa  maagizo  kwa viongozi wa Tanesco katika ngazi ya Mkoa na Wilaya kuhakikisha umeme huo unawaka kwa wakati.

Naye Mbunge wa Mkuranga na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh Abdallah Ulega amesema  wananchi katika vijiji ambavyo vilitakiwa kupata umeme walikata minazi na miembe yao ili kupisha miundo mbinu ya umeme lakini ni zaidi ya miaka mitano tangu miundombinu ya umeme iwekwe na hakuna umeme.

Aidha Ulega amemshukuru Waziri Kalemani kwa ziara yake jimboni hapo kwani anaamini italeta mabadiliko na amewataka watendaji waliopewa maagizo na Waziri wayafanyie kazi mara moja.
 Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani(katikati)kwa kushiriki na viogizo mbalimbali akikata utepe kuashiria uzinduzi wa umeme katika kijiji cha Mkokozi Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (alienyosha mkono) akizungumza na wanachi wa kata ya Kisiju wilaya ya Mkuranga  ambapo amewaagiza  watendaji wa Tanesco siku  14  wahakikishe umeme umewaka (Picha Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi na Mbunge wa jimbo la mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa  kijiji cha Kisiju ambapo amemshukuru Waziri Kalemani kwa ziara yake jimboni.
 Wananchi wa Wilaya ya Mkuranga  wakimsikiliza Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

WAZIRI UMMY AKABIDHI MADAWATI 40 SHULE YA SEKONDARI CHUMBAGENI JIJINI TANGA

$
0
0
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto na Wazee Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) leo amekabidhia madawati 40 na viti katika shule ya sekondari ya Chumbageni Jijini Tanga ikiwa ni mpango wake wa kuhakikisha changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu zinapatiwa ufumbuzi. 

Halfa hiyo ya makabidhiano ilifanyika leo shuleni hapo na kuhudhuriwa na walimu, wanafunzi na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ,Diwani wa Kata ya Chumbageni Saida Gadafi wakiwemo viongozi wengine. Hatua ya kukabidhiwa madawati hayo shule ya Sekondari ya Chumnageni ilitokana na ombi la Diwani wa Kata ya Chumbageni Saida Gadafi ambaye alimueleza waziri Ummy uwepo wa uhaba wa madawati kwenye shule hiyo. 

Akizungumza namna alivyoweza kuipatia ufumbuzi changamoto hiyo, Waziri Ummy alisema baada ya ombi hilo aliwapata wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambao walilikubali na kumpatia kiasi cha sh, milioni 5.4 ambazo wameweza kununua madawati 40 na viti “Mh Saida umetenda wajibu wako ipasavyo maana taarifa ya mkuu wa shule inasema kuna uhaba wa viti 163ubawa wa meza 100 hivyo kupatina kwa hivyo vilivyokabidhiwa leo kumepunguza nusu lakini nitaendelea kushirikiana nanyi “Alisema 

“Kazi nzuri inafanywa kwenye shule ya sekondari Chumbageni na nimeambiwa kiwango cha ufaulu kinaongezeka mwaka hadi mwaka asilimia 51 hadi asilimia 77 lakini pia nitoe pongeze kwa Halmashauri ya Jiji la Tanga kutatua changamoto ya elimu sio watu kusubiri mpaka serikali kuu kwani wamekuwa wakijiongeza na diwani Saida kutatua changamoto ya elimu kwenye kata yake “Alisema. 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto na Wazee Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kulia akimkabidhi madawati 40 Diwani wa Kata ya Chumbageni (CC) Saida Gadafi kwa ajili ya shule ya Sekondari Chumbageni ili kuweza kukabiliana na upungufu uliopo kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Chumbageni Gabriel Habash 
AWAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto na Wazee Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kulia akiwa amekaa kwenye mmoja ya madawati 40 aliyoyakabidhi leo kwa shule ya Sekondari Chumbageni kushoto ni Diwani wa Kata ya Chumbageni (CC) Saida Gadafi ambaye alimuomba Waziri huyo madawati hayoi kwa ajili ya shule ya Sekondari Chumbageni ili kuweza kukabiliana na upungufu uliopo 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto na Wazee Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kushoto akifurahia jambo na wanafunzi wa shule ya Sekondari Chumbageni mara baada ya kuwakabidhi madawati hayo 
 Sehemu ya madawati na viti ambayo yamekabidhiwa leo na Waziri Ummy kwa shule ya Sekondari Chumbageni.


Bodi ya nyama Tanzania na Abachem Engineering

KIPINDI MAALUM CHA RAIS DKT.JOHN MAGUFULI ALIPOKUTANA NA VIONGOZI WA CCT NA TEC.IKULU DSM

BENKI YA POSTA YATOA MSAADA WA MAGODORO NA MASHUKA SHULE YA SEKONDARI MLALE MKOANI SONGWE

$
0
0
 Meneja Mahusiano wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Bi. Noves Moses  akimkabidhi msaada wa magodoro na mashuka Mbunge wa Jimbo la Ileje Mkoani Songwe Janeth Mbene (wapili kushoto) wenye thamani ya shilingi milioni 3.3 kwa  ajili ya Shule ya Sekondari Mlale kama sehemu ya kupunguza changamoto zinazoikabili shule hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo Bi. Furaha Mhagama.
Meneja Mahusiano wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Bi. Noves Moses  akimkabidhi msaada wa magodoro na mashuka Mbunge wa Jimbo la Ileje Mkoani Songwe Janeth Mbene (wapili kushoto) wenye thamani ya shilingi milioni 3.3 kwa  ajili ya Shule ya Sekondari Mlale kama sehemu ya kupunguza changamoto zinazoikabili shule hiyo. Kushoto ni mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo aliyeshuhudia mmsaada huo kwao.
 Mbunge wa Jimbo la Ileje Mkoani Songwe Janeth Mbene akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) na wanafunzi  ya Sekondari ya Mlale mara baada ya kupokea msaada wa magodoro na mashuka yenye thamani ya Milioni 3.3 kutoka benki ya TPB.

SHIBUDA AWAGEUZIA KIBAO VYAMA VYA SIASA KUHUSU LUGHA WANAZOTUMIA KUMSHAURI RAIS

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

*Awaambia zama zimebadilika …hii ni Awamu ya Tano

MWENYEKITI wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini John Shibuda amewashauri viongozi wa vyama vya siasa kuwa makini na matumizi ya lugha wanayotumia pindi wanapotaka kumshauri Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk.John Magufuli.

Wakati huo huo amewahakikishia kuwa Rais Magufuli hawezi kuufuta mfumo wa vyama vingi bali kilichopo anaviimarisha na kwamba ipo siku atazungumzia hilo kwa kina.Shibuda ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati viongozi wa vyama vya siasa nchini vilipokutana kwa lengo la kujadili mabadiliko ya kikatiba na kisheria kuhusu uchaguzi kabla ya Uchaguzi kuu wa mwaka 2020.

Katika mkutano huo ambao umeandaliwa na Jukwa la Katiba Tanzania (Jukata),Shibuda amesema ni vema wanasiasa wakawa makini katika matumizi ya lugha hasa kwa kuzingatia zama zimebadilika.Amesema lugha ambazo walikuwa wanazitumia katika awamu zilizopita lazima wanasiasa wajue zama hizi hazina nafasi na hivyo kushauri wachague lugha ya kusema wanapotaka kushauri au kuzingumza jambo kwa Rais.

“Kikubwa lazima tutambue kila kabila na utamaduni wake.Lugha ambazo unaweza kuzitumia kumwambia Mzaramo au Mkwere anaweza kucheka lakini lugha hiyo hiyo ukiitumia kwa Mkurya atakukata panga.“Lugha ambazo unataka kumwambia Rais wa Serikali ya Awamu Tano lazima ziwe na staha kwani kinyume na hapo anaweza kukupa jibu ambalo litakukwaza.Tukubali kuwa mila na desturi zinatofautina sana,”amesema Shibuda.

Akifafanua katika hilo Shibuda ametoa mifano kuwa hata unapotaka kwenda kuoa ukienda kutoa posa Bukoba watakwambia nenda na mkungu wa ndizi, ukienda Tanga watakwambia nenda na kuku wa kitoweo na ukienda Usukumani utaambiwa uswage Ng’ombe.“Vivyo hivyo hata unapotaka kumshauri Rais lazima uzingatie mila na desturi.Nimeona hili niwaambie kwani kuna changamoto ya matumizi ya lugha miongoni mwetu,”amesema Shibuda.
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini John Shibuda akizungumza katika mkutano wa ulioandaliwa na Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) kwa lengo la kujadili mabadiliko ya kikatiba na kisheria kuhusu uchaguzi kabla ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ,mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es salaam 
Mjumbe wa Kamati kuu ya CHADEMA Profesa Mwesiga Baregu akitoa mchango wake katika mkutano uliolenga kujadili mabadiliko ya kikatiba na kisheria kuhusu uchaguzi kabla ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Katibu Mkuu wa Jukwaa la Katiba Tanzania Bw. Deus Kibamba akifafanua jambo katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha CCK Bw. Renatus Mhabi akichangia hoja katika majadiliano hayo.
John Mnyika Naibu Katibu Mkuu Bara chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA akichangia hoja katika mkutano huo.

'WANAUME KUOGOPA KUPIMA TEZI DUME KISA AIBU NI UJINGA' HAYA YABAINIKA UZINDUZI WA KLINIKI ZA JIONI BUGANDO

$
0
0

NA. GSENGOtV

Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku, Kushindwa kuzuia mkojo, yaani ukichelewa kidogo unaweza kukutoka bila breki, Maumivu wakati wa kukojoa, Kuishiwa nguvu za kiume, Kupungua kwa uwingi wa mbegu (low sperm count), Maumivu wakati unafika kileleni, Damu kutokea kwenye mkojo au kwenye mbegu za kiume, Maumivu nyuma ya mgongo au hata nyonga nk basi uonapo dalili hizo unaweza kuanza kuhisi una saratani ya tezi dume.

Kupitia dalili hizo ni wazi kwamba afya ya mgonjwa itakuwa matatani kwenye mataabiko.Wahenga walironga mficha maradhi kifo humuumbua. Kila kiungo cha mwanadamu kikipata tatizo ni jukumu la matabibu kufanya uchunguzi na kutoa huduma kwa eneo lililodhurika, Haiingii akilini kwamba uendelee kuteseka ile hali tiba ipo. Nao wataalamu wanasema uchunguzi wa kutumia kidole hauhitaji gharama kubwa kama ilivyo njia nyingine za kutumia vifaa maalum vya uchunguzi.

Ni tamaduni tu za watu wenye mawazo machafu ndizo zinazo wafanya wengi kudhani kipimo cha kidole ni udhalilishaji, lakini madaktari waliosomea fani hiyo wanasema kuwa ni njia ya kawaida sana.Kwa kuliona hilo Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza imezindua hudumu za kliniki za muda wa jioni kwa siku za wikiendi na sikukuu, lengo likiwa ni kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za Afya kwa wananchi wote ambao watahitaji huduma za kibingwa muda wote.

Hasa wale ambao hawawezi kufika hospitali kutokana na kubanwa na kazi. Fuatilia kile kilichojiri katika uzinduzi ikiwa ni pamoja na mashuhuda wanaume wa Tezi dume.
Huduma za uchukuaji vipimo zikiendelea katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza 
Licha ya kuwa na idadi kubwa ya wahitaji wa kupima afya, idadi ya madaktari wahudumu wa afya iliendana na kasi. 
Meza na meza vitengo kwa vitengo katika Uzinduzi wa Huduma za Kliniki za Jioni za Bure Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>>
Viewing all 110150 articles
Browse latest View live




Latest Images