Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110160 articles
Browse latest View live

MAJALIWA ATEMBELEA SHAMBA LA FAMILLIA YA RIWA MKOANI KIGOMA

$
0
0
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua shamba la  kahawa bora iliyopandwa na Familia ya Bibi Victoria Riwa (watano kulia) katika kijiji cha Nyarubanda mkoani Kigoma Julai 30, 2018. Wapili kulia ni Mtoto wa familia hiyo, Gerlad Riwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Bibi Victoria Riwa ( kulia) wa kijiji cha Nyarubanda  mkoani Kigoma wakati alipotembelea shamba  la familia hiyo  linalopandwa miche ya kahawa bora na kufurahishwa na mipango mizuri ya kilimo inayofanywa na familia hiyo.   Kushoto ni Lilian Riwa na wapili kushoto ni  Gerlad Riwa, wote wakiwa ni watoto wa familia hiyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WATATU HOSPITALI YA KASULU MJI KWA TUHUMA ZA KUIBA DAWA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

WAZIRI mkuu Kasimu Majaliwa amewasimamisha kazi watumishi watatu wa Hospitali ya Wilaya ya Kasulu mji ambao wanatuhumiwa kuiba dawa na kwenda kuuza katika maduka ya mjini.

Aidha, Waziri Mkuu ameahidi kuyafunga maduka yote yanayo nunua dawa kwa Watumishi ambao wanaiba dawa katika hospitali za Wananchi na kwenda kuuza kwa ajili ya kujinufaisha wao.

Waziri Mkuu alifikia uamuzi huo leo wakati alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Kasulu na kubaini tatizo la upotevu wa dawa na vifaa tiba katika hospitali hiyo na kumuagiza mganga Mkuu kuwasimamisha kazi watumishi hao wapishe uchunguzi na watakapo bainika wanahusika na tuhuma hizo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

" watumishi wazembe , wezi na wala rushwa na wasio waadilifu hawatufai katika serikali yetu na kamwe hatutawavumilia hivyo tutawaondoa.Aliwataja watumishi wanao husika ni wanaohusika na tuhuma hiyo ni Michael Nindi ambae ni mfamasia wa Wilaya , Tilasi Mbombwe ambae ni mtu wa maabara na Venancea Batega muuguzi.
PMO 0608 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Bibi Pendo Lilola kwa kujifungua salama mtoto wa kiume katika wodi ya wazazi kwenye Hospitali ya wilaya ya Kasulu Julai 29, 2018. Mheshimiwa Majaliwa aliitembelea Hospitali hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Kigoma Julai 30, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

MADIWANI CHADEMA.CUF WAFIKISHWA MAHAKAMA WILAYA YA ILALA KWA TUHUMA ZA KUSHAWISHI RUSHWA

$
0
0
Madiwani wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na mmoja wa Chama cha Wananchi CUF, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, wakikabiliwa na mashtaka mawali likiwamo la kushawishi rushwa ya Sh Milioni 25.

Washtakiwa hao ni Diwani kata ya Segerea, Edwin Kenan Mwakatobe (33) na Diwani wa kata Mchikichini Joseph John Ngowa (45) wote kutoka Chadena na Diwani wa kata ya Mnyamani kupitia CUF, Shukuru Abdallar Dege (42).Wakili wa Takukuru, Devotha Mihayo kutoka Takukuru amewasomea washtakiwa mashtaka yao leo Julai 30.2018 mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Mujaya.

Katika shtaka la kwanza mshtakiwa Mwakatobe anadaiwa tarehe isiyojulikana, Julai 2018 katika Wilaya ya Ilala akiwa Diwani wa kata ya Segerea na mjumbe wa kamati ya Fedha na Utawala katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala alishawishi rushwa ya Sh milioni 25 kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya M/S M+M Architects Co. Ltd, Burhan Mvungi kama kichocheo cha kupendelewa katika tenda na LG/015/2017/2018/HQ/CS/07 Lot 03 ambayo nilikuwa chini ya muajiri wao.

Katika shtaka la pili inadaiwa kuwa madiwani hao, Mwakatobe, Ngowa na Dege Julai 24, 2018 katika baa ya Kwetu Pazuri iliyopo Tabata Wilaya ya Ilala, wote wakiwa wajumbe wa kamati ya fedha na utawala ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala walipokea rushwa ya Sh milioni 3 kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya M/S M+M Architects Co. Ltd, Burhan Mvungi kama kichocheo cha kupendelewa katika tenda na LG/015/2017/2018/HQ/CS/07 Lot 03 ambayo ilikuwa chini ya muajiri wao.

Hata hivyo, washtakiwa hao wamekana kutenda makosa hayo wako nje kwa dhamana.Kesi imeahirishwa hadi Agosti 13 , mwaka huu wa ajili ya kutajwa.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi katika kesi hiyo umeishakamilika, katika tarehe hiyo washtakiwa hao watasomewa Maelezo ya awali.


MAKAMU WA RAIS AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI MBEYA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa Chunya kwenye uwanja wa Sabasaba ikiwa ni siku ya kuhitimisha ziara yake mkoani Mbeya.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Kilimo Dkt. Mary Mwanjwelwa mara baada ya kumalizika kwa kikao cha majumuisho ya ziara yake katika Ukumbi wa Mkapa mkoani Mbeya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Mbarali Mhe. Haroon Pirmohamed katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe muda Mfupi kabla Makamu wa Rais ajarejea Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiteta jambo na Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki wakati wa mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Sabasaba wilaya ya Chunya ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara ya Makamu wa Rais mkoani Mbeya. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

ATCL YADAIWA KUKIUKA TARATIBU ZA SHERIA YA MANUNUZI-NAIBU GAVANA BANK KUU.

$
0
0
NAIBU Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BOT), Yamungu Kagandabila (47), ameieleza mahakamani ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ilisaini mkataba wa kukodisha ndege kabla haijapata kibali cha dhamana ya serikali.

Pia imeelezwa, kamati ya wataalam ya Uchunguzi ya Deni la Taifa (TDMC), ilibaini ATCL iliwasilisha maombi ya dhamana kwa Waziri wa Fedha (kwa sasa Wizara ya Fedha na Mipango) kwa kukiuka taratibu za sheria za manunuzi.

Kagandabila ambaye ni shahidi wa upande wa jamuhuri katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya bilioni 71, inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL David Mattaka na wenzake wawili amedai hayo leo Julai 30.2018 wakati akitoa ushahidi wake dhidi ya washtakiwa hao.

Kabla ya kuanza usikilizwaji wa kesi hiyo, Mattaka na washtakiwa wenzie, vigogo kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Ofisa Mtendaji Mkuu mstaafu, Dk. Ramadhan Mlinga na Mwanasheria Bertha Soka. Walisomewa Maelezo ya awali.

Akiongozwa na wakili wa Serikali, Vitalis Peter kutoka Takukuru mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwinzile shahidi huyo alidai ATCL iliwasilisha ombi la kutaka kupata dhamana ikiwa imeisha kiuka sheria yenyewe ya mikopo, dhamana na misaada.Amedai Januari 2008 akiwa Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera na deni la Taifa, ATCL iliwasilisha maombi ya dhamana Wizara ya Fedha kupitia Wizara ya Miundombinu.

Alidai kuwa Januari 11, 2008 walikaa kikao cha TDMC na kubaini kwamba ATCL ilishasaini mkataba wa kukodi ndege bila dhamana ya serikali na kukiuka sheria mbali mbali ikiwemo hawakufuata sheria ya manunuzi ya umma.Pia amedai, maombi ya TTCL hayakuwa yameambatanishwa na maamuzi ya bodi ya ATCL na pia hayakuwa yameambatanishwa na business planing kuweza kusapoti ombi lao hilo.

Amedai kuwa baada ya kubaini hayo, waliwaagiza ATCL kurekebisha kasoro na kuwataka kuonyesha idhini ya bodi kama ilikubakubaliana na ukodishwaji wa ndege hiyo na pia ATCL walitakiwa kuwasiliana na PPRA ili waweze kuonyesha njia waliyotumia kupata ndege hiyo.Hata hivyo, pamoja na yote hayo Waziri wa fedha aliidhinisha kutolewa kwa dhamana hiyo kwa ATCL pamoja na kwamba walikiuka utaratibu kwa kuingia mkataba huo.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa mkataba ulisainiwa Oktoba 9, 2007 na Mattaka alisaini kwa niaba ya ATCL na Andrew Wettern kwa niaba ya Wallis Trading Inc na kuisababishia Serikali hasara.

MICHUZI TV: SERIKALI YAONDOA VIKWAZO ADA YA BIDHAA ZA CHAKULA

IGP AKUTANA NA VIONGOZI RSA

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akipokea fulana yenye ujumbe wa kuhamasisha juhudi za usalama barabarani kutoka kwa Mwenyekiti wa Mabalozi wa Usalama barabarani (RSA) Bw. John Seka wakati alipofika kujitambulisha ofisini kwake Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam akiwa na Viongozi wengine wa RSA. (Picha na Jeshi la Polisi )

GAZETI LA MWANAHALISI LATOKEA MAHAKAMANI

$
0
0
Na Humphrey Shao , Globu ya Jamii

Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam imelifungulia gazeti la Mwanahalisi ambalo lilifungiwa na Serikali kutokana na kile kilichodaiwa kuchapisha habari ambazo zipo kinyume na maadili.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaaam leo, Mkurugenzi wa Mwanahalisi Publisher, Saed Kubenea amesema baada ya kufungiwa gazeti la mwanahalisi walikwenda kufungua kesi Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam.

Amesema kuwa baada kufungua kesi hiyo iliyodumu kwa muda wa mwaka mmoja, mahakama kuu imeona gazeti la mwanahalisi lilifungiwa kimakosa.

Kubenea ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo amesema kuwa kwa mujibu wa hukumu ya mahakama imeoshenya Waziri hakuwa na sheria katika kulifungia gazeti hilo.

Katika kesi hiyo Mwanahalisi ilisimamiwa na Wakili wawili ambao niJeremia Mtobesya akiongozwa na Wakili wa kujitegemea Dkt. Regemeleza Nshallah.

Katika hatua nyengine amebainisha kuwa wanatarajia kwenda mahakamani kwa ajili ya kumdai fidia waziri aliyelifungia gazeti la mwanahalisi.

Mwaka wa jana gazeti Mwanahalisi lilifungiwa kwa muda wa miaka miwili kutokana na kile kinachodaiwa kuwa na mfululizo wa matukio ya ukiukwaji wa misingi na sheria za taaluma ya uandishi wa habari, kuandika habari za uchochezi na kuhatarisha usalama wa Taifa.

katika taarifa yake Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abassi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema kuwa serikali imechukua uamuzi wa kulifumgia Gazeti hilo kwa mujibu wa kifungu cha Sheria ya Huduma za Habari namba 12 ya mwaka 2017, ambapo kwa muda mrefu idara hiyo imekuwa ikiwakumbusha wahariri wa gazeti hilo juu ya kufuata misingi ya taaluma bila mafanikio.
Mbunge wa Ubungo na Mmiliki wa Kampuni ya Hali halisi Publisher , Saed Kubenea akizungumza na Waandishi wa habari juu uamuzi uliochokuliwa na Mahakama kwa gazeti la Mwanahalisi.
Waandishi Mbalimbali wa Habari waliohudhuria katika Mkutano huo

WAZIRI MBARAWA APIGA MARUFUKU USAMBAZAJI WA MAJI KWENYE MELI KWA KUTUMIA MAGARI

$
0
0
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akiongea mara baada ya kumaliza kufanya uzinduzi na ukaguzi wa mfumo wa mita za malipo ya kabla (Pre Paid meter).  Pembeni ni Afisa Mtendaji Mkuu Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (Dawasco). 

 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa amepiga marufuku Mamlaka ya Bandari (TPA) kuacha kununua maji katika magari binafsi ya kusambaza maji kwa ajili ya matumizi ya kwenye meli  na kuwataka wachukue maji kutoka mamlaka inayotambulika kisheria kufanya kazi hiyo.

Profesa Mbarawa ametoa agizo hilo wakati wa uzinduzi wa mita za malipo ya kabla(Pre Paid meter) au mita za Luku katika Hotel ya Sea Cliff, Kiwanda cha Pepsi Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) akiwa ameambatana na Uongozi  wa Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (Dawasco). Akizungumza baada ya kutembelea TPA, Waziri  Mbarawa amewataka mamlaka hiyo kuhakikisha maji yote yanayotumika katika meli zinazotia nanga bandarini yanatoka Dawasco.

Mbarawa amesema kuwa matumizi ya maji yanayotoka kwa wauzaji wa nje hayajulikani yanatoka wapi na usalama wake haujilikani kwahiyo yatakapokuja kuleta madhara kwa watumiaji ndani ya meli lawama zitakuja kwa serikali na sio wauzaji hao wa maji ya maboza.

“Napenda kuwaagiza Mamlaka ya Bandari kuachana na ununuzi wa maji kutoka mamlaka zisizohusika kwahiyo Kwahiyo  masuala ya ujanja ujanja yaishe kuanzia sasa maji  na na nakuagiza mtendaji wa Dawasco ukutane na Mkurugenzi wa bandari kwa ajili ya suala hili,” amesema Mbarawa.

Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa amechukua maagizo hayo kama aliyovyoelekezwa na Waziri.

Dawasco wamemfunga mita hizo na zitatumika kwa wateja wakubwa pamoja na viwanda ambapo mteja atahitajika kulipia maji kabla na kiasi ulicholipia kikisha basi maji yatakatika, mfumo huo utasaidia katika kuongezea mapato Mamlaka husika pia kwa watumiaji sugu waliokuwa wanadaiwa maji kwa muda mrefu watakuwa wanalipa madeni kila watakapokuwa wananunua maji.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa (kulia) wakati akikagua mfumo wa namna mfumo wa mita za malipo ya kabla (Pre Paid meter) kwa wateja wa majumbani.

Mashine zilizofungwa katika kiwanda cha kampuni ya SBC Tanzania Limited (PEPSI), kwa ajili ya wateja wa majumbani.

TANZANIA BADO BORA KWA UKAGUZI WA MAHESABU BARANI AFRIKA

$
0
0


Na Humphrey Shao Globu ya Jamii


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad, amesema Tanzania ni moja ya nchi zinazofanya vizuri katika bara la Afrika na kushika nafasi ya tatu kwa bara zima.

Profesa Assad amesema hayo leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kurejea nchini akitokea nchini Marekani kukabidhi nafasi ya ujumbe wa bodi ya ukaguzi ya Umoja wa Mataifa (UNBoA) kwa nchi ya Chile baada ya Tanzania kumaliza kipindi chake cha miaka sita iliyoanza Julai mosi 2012

Makabidhiano hayo yamefanyika jana kwenye Ukumbi wa Mikutano uliopo kwenye jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Jijini New York nchini Marekani na Tanzania kumaliza kupongezwa kwa kazi nzuri iliyofanya 

Pamoja na kufanya makabidhiano hayo, CAG Prof. Assad pia alihudhuria Kikao cha kawaida cha 72 cha bodi hiyo na kuwasilisha jumla ya ripoti 13 za Ukaguzi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UN)

Ripoti alizowasilisha baada ya kutiwa saini na wajumbe wa bodi ya UN ni pamoja na Ukaguzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa Wakimbizi wa Palestina na Mashariki (UNRWA), Mfuko wa Akiba kwa Watumishi wa UNRWA Wakazi (UNRWA – SPF), Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake (UN – Women) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Mazingira (UNEP). 

Ripoti nyingine ni za Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Mazingira ulio chini ya UNDPGEF, Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Mazingira ulio chini ya Shirika UNEP-GEF, Mfuko wa Mikopo Midogo midogo ulio chini ya UNRWA - MD Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi (UN Habitat), Shirika la Umoja wa Mataifa la Ukuzaji Mitaji (UNCDF), Mahakama ya Umoja wa Mataifa inashughulikia Mauaji ya kimbari ya Yugoslavia ya zamani (ICTY), pamoja na ripoti ya Mpango wa Kupunguza Shughuli za Mahakama za Kimataifa zinazoshughulikia Mauaji ya Kimbari (MICT). 

Prof. Assad amesema Tanzania itaendelea kuwa mjumbe mwangalizi ”Observer Member” kwenye Jopo la Wakaguzi wa Nje wa Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo baada ya kung’atuka kwenye nafasi ya Ujumbe wa bodi hiyo.Amesema katika kipindi cha miaka sita mbali ya kuwa mjumbe wa bodi ya UNBOA,pia Tanzania ilipata fursa ya kuongoza bodi ya Ukaguzi wa umoja wa Mataifa kwa kipindi cha miaka miwili,

Nimekuwa mwenyekiti wa UNBoA kwa miaka miwili mfululizo kuanzia Januari Mosi, 2015 hadi 31 Desemba, 2016, ambapo nimekuwa na jukumu la kuwasilisha taarifa za UNBoA katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa”alisema

Tanzania inaingia katika historia ya dunia kuwa nchi ya kwanza katika Ukanda wa Afrika Mashariki na ya tatu (3) Barani Afrika kuteuliwa mjumbe wa Bodi ya Ukaguzi wa Umoja wa Mataifa (UNBoA) tangu kuanzishwa kwa Bodi hiyo mwaka 1946. Nchi nyingine za Afrika ambazo zimewahi kuwa wajumbe wa Bodi ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa ni Ghana na Afrika ya Kusini tu. 
Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa esabu za Serikali .Profesa Mussa Assad akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kurejea kutoka kwenye Mkutano wa Baraza la ukaguzi la Umoja wa Mataifa
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali .Profesa Mussa Assad mara baada ya kurejea kutoka kwenye Mkutano wa Baraz la ukaguzi la Umoja wa Mataifa

RAIS DKT. MAGUFULI AKABIDHI HATI ZA VIWANJA VYA DODOMA KWA MABALOZI WA NCHI MBALIMBALI NA WAWAKILISHI WA MASHIRIKA YA KIMATAIFA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Mabalozi wa nchi mbalimbali na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa baada ya kuwakabidhi bila malipo hati za viwanja vya kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018.
Balozi wa Rwanda nchini na Kiongozi wa Mabalozi  Mhe. Eugene Segore Kayihura akimshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa niaba ya mabalozi na wawkilishi wa mashirika ya kimataifa kwa kupatiwa bila malipo hati za viwanja vya kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018
 Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuongea na mabalozi na wawkilishi wa mashirika ya kimataifa baada ya kuwapatia  bila malipo hati za viwanja vya kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Balozi wa Afrika ya Kusini nchini Tanzania Mhe. Thamsangqa Dennis Mseleku hati hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018
Rais  wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke  hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018.

BALOZI MPYA WA KENYA NCHINI MHE. DAN KAZUNGU AKABIDHI HATI ZA UTAMBULISHO WA RAIS MAGUFULI, NAYE AKABIDHIWA HATI YA KIWANJA CHA DODOMA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 30, 2018

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu  mara baada ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 30, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya Picha kutoka kwa Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu. Zawadi hiyo ya picha imetoka kwa Mama mzazi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Mama Ngina Kenyatta na katika picha hiyo anaonekana Rais Dkt. Magufuli akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Mama Ngina Kenya walipokuwa Nairobi nchini Kenya.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Balozi wa  Kenya nchini Mhe. Dan Kazungu  hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018
 Balozi wa  Kenya nchini Mhe. Dan Kazungu  akielekea kuketi baada ya kupatiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018. Hii ilikuwa kazi ya kwanza kwa balozi huyu ambaye alijiunga na wenzie baada ya kukabidhi hati za utambulisho kwa Rais muda mfupi uliopita.

VOA SWAHILI: Duniani Leo Julai 30, 2018

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 30.07.2018

INTRODUCING "CHAGUO" BY JOZEE FT BEKA FLAVOUR OFFICIAL VIDEO


Introducing new music from PAUL SOLO, "ZIMA"

INTRODUCING "NIOE" BY KEISHA

Dk. Kalemani azindua umeme usiku vijijini

$
0
0
WAZIRI wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, ameendelea na ziara yake vijijini y kukagua miradi ya umeme REA III inayoendelea huku akilazimika kuzindua umeme usiku.

Amesema amelazimika kufanya uzinduzi huo usiku ili kutoa maana halisi ya uwepo wa mwanga wa umeme kwa wananchi ili nao waone hali halisi kuliko ya jinsi raha ya umeme ilivyo.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ihanga Wilayani Chato, alisema kuwa Serikali pamoja na watalaamu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa kushirikiana na REA wamekuwa wakifanyakazi usiku na mchana ili kuhakikisha kazi ya uunganishaji umeme inafanyika kwa maslahi ya wananchi na kuvutia wawekezaji hasa wa viwanda.

“Ninawashukuru sana wananchi kwani watu wengi wana shauku ya umeme na kila unapokwenda ukiwaambia leo ninakuja kuwaunganishia umeme wako tayar kusubiri mpaka usiku, niwapongeze wananchi kwa kweli walikuwa na shauku kubwa na leo wamepata furaha.

“Na mimi kama mbunge wao bahati nzuri ni Waziri wa Nishati ilikuwa ni lazima kuwatembelea hata kama ingekuwa usiku. Lakini pia huu ni mwanga ili udhibitishe kama ni mwanga ni vizuri ukawasha usiku ikaonekana kuwa kweli hii ni taa. Nadhani walitaka wajiridhishe na wameshuhudia kwa sababu tumewasha usiku na kwangu nitatembea usiku na mchana kuwatumikia Watanzania ili mradi nitahakikisha wanapata maendeleo,” alisea Dk. Kalemani 

Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ihanga Wilayani Chato usiku wa jana baada ya kuzindua umeme
Wananchi wa Kijiji cha Ihanga Wilayani Chato, wakimsikiliza kwa Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani
Diwani wa Viti Maalumu, Grace Kubilima (CCM), ambaye pia ni mkazi wa Kijiji cha Ihanga, akimshukuru Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, baada ya kuzindua umeme jana usiku katika kijiji hicho.

MIPANGO YA MATUMZI YA ARDHI KUNUSURU MISITU NCHINI

$
0
0
Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) inatarajia kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi katika vijiji 120 vinavyozunguka misitu ya Hifadhi ya Serikali Kuu.

Akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya NLUPC and TFS kilichofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NLUPC Dkt. Stephen Nindi ameahidi kuwa taasisi yake itatoa ushirikiano wa kitaalamu kwa ajili ya kunusuru rasilimali za nchi wakati wowote kwa faida ya nchi na watanzania wote.

Naye Mtendaji Mkuu wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo amesema kuwa mipango hiyo ya matumizi ya ardhi inalenga kumaliza changamoto zote ya kuhifadhi misitu nchini kwenye vijiji vinavyozunguka hifadhi hizo pamoja na kuwasaidia wanavijiji kuwa na matumizi rafiki ya ardhi yatakayosaidia kutunza misitu hiyo.“Mpaka sasa zaidi 60% ya misitu iliyopo nchini haijahifadhiwa na lengo letu ni kuhakikisha misitu hiyo inahifadhiwa. Hivyo nawataka wataalamu wa Tume pamoja na Wakala kuhakikisha lengo hili linafikiwa kwa kuweka mikakati ya kitaaaluma kwa kuzingatia wakati uliopo,” alisema Professa Silayo.

Professa Silayo anasema hatua hiyo ni utekelezaji wa maagizo ya Serikali yanayoelekeza kutatua migogoro ya mipaka kati ya wananchi na maeneo ya jirani na hifadhi kwa kushirikisha wadau katika kuhakiki mipaka ya maeneo ya hifadhi kwa kuweka alama za kudumu; kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi; na kuzingatia utawala wa Sheria katika kusimamia rasilimali za maliasili.Mtendaji huyo anaongeza kuwa uharibifu wa misitu nchini ni mkubwa katika maeneo ambayo vijiji vimeanzishwa ndani ya misitu bila kufuata sheria na TFS imeendelea kuzuia upanuzi zaidi wa vijiji hivyo, na hadi sasa kuna vijiji 228 vinavyofahamika na miji kadhaa.

NLUPC na TFS wameunda kikosi kazi kitakachoandaa mikakati ya namna bora ya kufanya kazi hiyo ambapo wameanza kwa kupitia orodha ya misitu ya hifadhi yenye migogoro kwa kanda zote saba za TFS. Kanda hizo ni za Mashariki, Kaskazini, Kati, Kusini, Nyanda za juu Kusini, Ziwa na Magharibi. 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo (aliyesimama) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Dkt. Stephen Nindi wakiongoza kikao cha pamoja kati ya NLUPC na TFS juu ya maandalizi ya upangaji wa mipango ya matumizi ya ardhi katika vijiji vinavyozunguka hifadhi za Misitu inayosimamamiwa na Serikali Kuu. 
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu, Sera na Mawasiliano (DLCCP) wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Bibi Albina Burra (kulia) pamoja na Watalamu wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wakifuatilia kwa maokini mazungumzo kati ya taasisi zao.

RC MNYETI KUZINDUA MICHUANO YA CHEMCHEM CUP AGOST 19 MDORII BABATI

$
0
0
Na Ripota wetu, Manyara

Jumla ya timu 20, zinatarajiwa kushiriki ligi ya Chem Chem CUP, wilayani Babati mkoa wa Manyara ambapo zawadi zenye thamani ya sh 4.5 milioni zitatolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mratibu wa ligi hiyo, ambayo hufanyika kila mwaka,katika uwanja wa Mdori, Charles Godluck alisema, lengo lake ni kupiga vita ujangili na kuhamamisha jamii uhifadhi za mazingira.Godluck alisema, ligi ya chem chem CUP,mwaka huu inatarajwa kufunguliwa na Mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti, Agosti 19 na itatanguliwa na mkutano wa kutolewa jezi wa timu zote agosti 10 mwaka huu.

"hivi sasa tumezitaka timu zote ifikapo Agosti 4 ziwe zimethibitisha lakini pia kujitokeza kwenye kikao cha kupanga ratiba Agosti 10"alisema.Alisema mwaka huu bingwa wa soka, atapewa zawadi ya fedha taslimu 1.7 milioni na kombe,mshindi wa pili fedha 1.1 milioni, wa tatu 600.000 na wa nne 300,000.
"pia kutakuwa na zawadi wa kocha, bora, timu bora na mchezaji bora"alisema.
Alisema katika michuano hiyo, pia kutakuwa na michezo kwa wasichana ambapo, bingwa atazawadiwa 400,000 na pia kutakuwa na ngoma za kitamaduni na michezo mingine.Meneja wa taasisi ya Chemchem Foundation, Recardo Tossi, ambao wamewekeza ujenzi wa hoteli katika eneo la Mdori, alisema ligi hiyo, imekuwa ikishirikisha zaidi ya wanamichezi 400 na kuwa na ufanisi mkubwa.

"tunataka jamii ambayo inazunguka kijiji cha Mdori na tarafa nzima ya Mbugwe na wilaya ya babati, kuwa wahifadhi wazuri na kupiga vita ujangili"alisema.Na hapa chini ni baadhi ya matukio katika picha ya michuano iliyofanyika mwaka jana ambapo timu ya mdori fc ilijinyakulia kombe la michuano hiyo.
Viewing all 110160 articles
Browse latest View live




Latest Images