Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MAKAMU WA RAIS AFANYA MKUTANO WA HADHARA MBEYA MJINI

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa Mbeya mjini kwenye viwanja vya Ruandanzovwe, Makamu wa Rais yupo mkoani Mbeya kwenye ziara ya kuhamasisha maendeleo.
 Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Mhe. Joseph Mbilinyi (Chadema) wakazi wa Mbeya mjini kwenye viwanja vya Ruandanzovwe, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Sehemu ya Wakazi wa Mbeya mjini waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya Ruandanzovwe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia waliokuwa madiwani wa Chadema ambao wametangaza rasmi kujiunga na CCM  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Ruandanzovwe Mbeya mjini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Mhe. Joseph Mbilinyi (Chadema) mara baada ya kumaliza kuhutubia wakazi wa Mbeya mjini kwenye viwanja vya Ruandanzovwe, Makamu wa Rais yupo mkoani Mbeya kwenye ziara ya kuhamasisha maendeleo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

“SASA TUTAFIKA KONA KWA KONA” WARATIBU ELIMU NJOMBE MJI.

$
0
0

Hyasinta Kissima- Afisa Habari Halmashauri ya Mji Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe imepokea jumla ya pikipiki 13 zenye thamani ya shilingi milioni 39 kwa waratibu elimu Kata 13 lengo ikiwa ni kufanya ufatiliaji na usimamizi wa elimu katika Kata.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Salum Mkuya amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuboresha sekta ya elimu kwa kuhakikisha kuwa wasimamizi wa elimu wanawezeshwa upatikanaji wa vitendea kazi ili kufanya mazingira ya kazi kuwa rafiki.

“Pikipiki hizi zikafanye kazi ya ufuatiliaji kwa kupandisha kiwango cha ufaulu, kuhakikisha wanafunzi wanajua kusoma na kuandika ikiwa ni sambamba na kuthibiti utoro mashuleni.”Alisema Mkuya.Aidha, Mkuya ameiomba Halmashauri kuhakikisha kuwa pikipiki zote zilizokabidhiwa zinapatiwa bima kama serikali ilivyoagiza.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri Edwin Mwanzinga amesema kuwa anaishukuru serikali ya CCM kupitia kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa kutambua umuhimu wa pikipiki hizo kwa waratibu elimu kwani itarahisisha shughuli za usimamizi na ufuatiliaji elimu hususani katika Halmashauri ambazo maeneo mengi jiografia yake ni ngumu kufikika kutokana na ukubwa wa eneo halikadhalika changamoto za miundombinu.

“Najua waratibu mlikua mnafanya kazi katika mazingira magumu niwaombe sasa tukafanye kazi bila visingizio na ni lazima tuwe wa kwanza kimkoa kwa sababu tumepata vitendea kazi. Lakini niwaombe sana mkazitunze pikipiki hizi ili tuweze kwenda nazo kwa muda mrefu. Kwa wale ambao hamjui kuzitumia tusitumie pikipiki hizi kujifunzia. Ni imani yangu mtaenda kujifunza mpate leseni na muweze kuzitumia vizuri na kwa tahadhari” Mwanzinga alisema

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya waratibu elimu Ester Mjuu Mratibu Elimu Kata ya Ramadhani Halmashauri ya Njombe alisema kuwa sasa wataweza kufika kila kona ya Kata zao katika kufuatilia usimamizi wa elimu.“Tunashukuru sana kwa vitendea kazi hivi,miongoni mwa changamoto iliyokuwa inatukabili imepata ufumbuzi tutaenda kufanya kazi kwa kadri mlivyotuelekeza ili kuhakikisha kuwa tunakuwa na Taifa la wasomi kwa kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa karibu kwenye sekta ya elimu.”Alisema
Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Salum Mkuya akikabidhi Pikipiki kwa ajili ya waratibu elimu Kata 13 kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga akitoa mkono wa pongezi kwa Mratibu Elimu Kata ya Ramadhan Ester Mjuu mara baada ya kumkabidhi pikipiki.
Waratibu Elimu Kata kutoka Katika Kata 13 za Halmashauri ya Mji Njombe wakipongeza serikali kwa jitihada za kuwapatia Pikipiki ikiwa kama nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yao.

GOFU LUGALO YAWASILI NA KUANZA VYEMA MUFINDI OPEN

$
0
0
Na Luteni Selemani Semunyu

Wachezaji wa klabu Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo imewasili salama Mufindi Mkoani Iringa kwa ajili ya kushiriki mashindano ya wazi ya mufindi ya utalii karibu Kusini Mufindi gofu challenge yanayotarajiwa kuanza kesho(leo) kwa wachezaji wa ridhaa..

Akizungumza mara baada ya kuwasili Afisa Utawala wa klabu ya Lugalo Kapteni Amanzi Mandengule alisema timu imewasili salama na hakuna majeruhi na siku ya leo wataitumia kwa ajili ya mazoezi ili kuufahamu uwanja.“ Tumefika salama na Timu yetu sote tukiwa salama na Wachezaji wetu wa Kulipwa wameingia uwanjani leo ikiwa ndio siku yao na tunaimani tutafanya vizuri pia kwa kundi hilo” Alisema Kapteni Mandengule.

Kapteni Mandengule aliongeza kuwa licha ya kuwa wamefika salama lakini kuna changamoto ya hali ya hewa kwani Mufindi ni baridi ukilinganisha na Dar es Salaam ambapo hali nin ya Joto lakini watapambana kwa kuwa walilifahamu hilo.Kwa upande wa wachezaji wa kulipwa wachezaji 11 wameingia uwanjani kumenyana katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa iringa kwa kushirikiana na wizara ya maliasili na utalii yakilenga kutangaza fursa na vivutio vya utalii nyanda za juu kusini.

Katika hatua ya mwanzo ya michuano hiyo Mchezaji George Leverian wa Lugalo ameibuka na ushindi kwa kupiga mpira mrefu na wameingia katika Raundi ya pili itakayoamua mshindi katika vipengele vingine na ushindi wa Jumla.Katika mashindano hayo ya siku tatu mbali na kushiriki katika mashindano hayo lakini watapata fursa ya kutembelea na kujifunza masuala mbalimbali kuhusu sekta ya utali hususani utalii wa nyanda za juu kusini.

Mbali na wachezaji wa kutoka Klabu ya Lugalo pia Wachezaji kutoka Vilabu vya Morogoro Gymkhana, Dar es Salaam Gymkhana, Moshi Club ,TPC, Kili Golf Club ya Arusha na wenyeji klabu ya Mufindi ya Iringa watashiriki katika mashindano hayo.
Baadhi ya wachezaji wa Timu ya Golf ya Lugalo wakiwasili katika uwanja wa Gofu wa Mufindi mkoani Iringa yenye lengo la Kutangaza vivutio vya Utalii vya nyanda za juu kusini hususani Mufindi.
Mchezaji gofu wa kulipwa kutoka Klabu ya Lugalo Geofrey Leverian aliyeibuka mshindi kwa kupiga mpira Mrefu akipiga Mpira wakati wa Mashindano ya wazi ya Mufindi yenye lengo la Kutangaza vivutio vya Utalii vya nyanda za juu kusini hususani Mufindi.

TAGCO NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZAPONGEZWA KWA UTENDAJI

$
0
0
Frank Mvungi- MAELEZO, Tunduru

Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) vimepongezwa kwa kubuni na kuweka utaratibu wa kufuatilia utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini hadi katika ngazi ya Halmashuri.

Akizungumza na Ujumbe wa chama hicho uliofika Ofisini kwake mapema wiki , Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw. Chiza Marando amesema kuwa hili ni jambo la kihistoria ambapo ufuatiliaji wa utendaji wa Maafisa Habari unafanyika katika ngazi zote.

“Tangu nimeanza kazi sijawahi kushuhudia ufuatiliaji wa namna hii na sisi tuko tayari wakati wote kutoa ushirikiano utakaosaidia Afisa Habari katika Halmashauri yetu atekeleze majukumu yake vizuri hasa katika kutangaza miradi ya maendeleo” Alisisitiza Marando.Akifafanua Bw. Marando amesema kuwa Halmashuri yake inatambua umuhimu wa mawasiliano kati ya Serikali na Wananchi hivyo imeweka kipaumbele katika kuwezesha utoaji wa taarifa za maendeleo kwenda kwa wananchi ili waweze kushiriki katika kujiletea maendeleo.

Kwa upande wake Kiongozi wa Msafara wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari – MAELEZO Bi. Gaudensia Simwanza amesema kuwa maafisa habari wanalo jukumu kubwa katika Halmashauri na Mikoa katika kutangaza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao.Aliongeza kuwa kutokana na jukumu hilo wanapaswa kutumia rasilimali zilizopo kutekeleza jukumu hilo kwa weledi.

Ziara ya Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini na Idara ya Habari MAELEZO inafanyika katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kufuatilia na kuona utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini katika ngazi zote ili kutoa msukumo na kuweka mikakati ya pamoja katika kuimarisha Mawasiliano ya Serikali kwa umma ili kuchochea maendeleo na ustawi wa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza kuhusu namna Halmashuri hiyo ilivyojipanga katika kuimarisha mawasiliano ya kikakati hasa kutangaza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza jambo kwa ujumbe wa chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashauri hiyo kukagua na kujionea jinsi maafisa Habari wanavyotekeleza jukumu la kuisemea Serikali katika Mikoa na Halmashuri zao.
Kiongozi wa Ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza jambo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashuri hiyo uliolenga kukagua na kuweka mikakati ya pamoja katika kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma.


Mwakilishi wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Casmir Ndambalilo akisisitiza umuhimu wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kuwajibika katika kuisemea Serikali hasa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mikoa na Halmashuri zao, hiyo ilikuwa katika ziara iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na Idara ya Habari MAELEZO.

DK. HERY MWANDOLELA WA HEAMEDA MEDICAL CLINIC AZUNGUMZIA UMUHIMU WA KUPIMA AFYA

$
0
0

*Afurahishwa na idadi kubwa ya wananchi wanavyojitokeza kupima afya bure
*Ataja kiini cha kuongezeka kwa kasi magonjwa yasiyo ya kuambukiza nchini

Na Said Mwishehe, Glob ya Jamii.
 
DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Heameda Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela amesema uamuzi wa kuweka kambi ya kupima afya za wananchi bure katika Clinic hiyo inalenga kuwahamasisha wananchi kupata fursa ya kutambua afya zao mapema.

Kwa sasa Heameda Medical Clinic ipo katika kampeni hiyo ya kupima afya za wananchi bure iliyoanza Julai 26 na inatarajia kumalizika Julai 27 mwaka huu.

Akizungumza leo na Michuzi Blog wakati wa kamepeni hiyo Dk.Mwandolela amesema Heameda Medical Clinic iliyopo Bunju B jijini Dar es Salaam imeamua kutenga siku tatu ili kutoa huduma hiyo ya wananchi kuwapima afya zao bila gharama yoyote.

"Tumeamua kutenga siku tatu hizi kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na jambo la kubwa na la kujivunia ni namna ambavyo wamejitokeza kwa wingi kupima afya zao.Kwetu sisi kampeni hii ni sehemu ya shukrani kwao.

"Kupima afya ni jambo la msingi katika maisha ya binadamu kwani husaidia kujitambua mapema na kama kuna tatizo inakuwa rahisi kupata ushauri kulingana na madaktari bingwa watakavyoshauri.

"Tunajisikia fahari pale mtanzania anapojenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara.Heameda Medical Clinic tupo kwa ajili ya kuwahudumia na kipindi hiki cha kampeni tumeungana na madaktari bingwa wengine nchini pamoja na madaktari bingwa kutoka India.Lengo ni kuhakikisha afya ya mtanzania inakuwa salama wakati wote,"amefafanua.

Kuhusu magonjwa ambayo wanapima kwenye kampeni hiyo amesema wanapima magojwa ambayo si ya kuambikiza ambayo kwa kipindi hiki yameshika kasi na kusababisha vifo vya wananchi walio wengi.

Mmoja wa madaktari wa Heameda Medical Clinic iliyopo Bunju B jijini Dar es Salaam wakiendelea kutoa huduma ya upimaji afya bura kwa mmoja wa wakazi wa eneo hilo.
Baadhi wananchi mbalimbali wakiwa wamejitokeza Heameda Medical Clinic kupima afya zao.
madaktari wa Heameda Medicla Clinic iliyopo Bunju B jijini Dar es Salaam wakiendelea kutoa huduma ya upimaji afya bura kwa wananchi.

DK.SHEIN AAGANA NA BALOZI WA MALAWI NCHINI.

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na mgeni wake Balozi wa Jamhuri ya Malawi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bibi.Hawa Olga Ndilowe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya kumuaga Rais, akimaliza muda wake wa kazi Nchini
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na mgeni wake Balozi wa Jamhuri ya Malawi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bibi.Hawa Olga Ndilowe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya kumuaga Rais, kwa kumaliza muda wake wa kazi Nchini

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na mgeni wake Balozi wa Jamhuri ya Malawi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bibi.Hawa Olga Ndilowe baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya kumuaga Rais,kwa kumaliza muda wake wa kazi Nchini,[Picha na Ikulu.] 27/07/2018.

PROF MBARAWA AKAGUA MRADI WA MAJI WA MTO RUFIJI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa ametembelea mradi mkubwa maji wa bwawa katika Mto Rufiji utakaoweza kusaidia matumizi ya maji kwenye kambi ya ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge)

Mradi huo unaotekelezwa Wizara ya Maji na Umwagiliaji kupitia  Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (DAWASA) na umeweza kugharimu kiasi cha Milioni 604.9 ukiwa ni muendelezo wa mradi mkubwa wa maji unaoendelea Kisarawe.

Akizungumza baada ya kutembelea maporomoko ya Mto Rufiji Prof Mbarawa amesema kuwa mradi huo wa maji utakuwa na uwezo wa kuzalisha maji lita 209,000( laki mbili na elfu tisa) kwa ajili ya matumizi ya kambi ya ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).

Amesema, mradi huo wa maji utawasaidia wakandarasi kusa na miundo mbinu wezeshi itakayowapatia maji muda wote wa matumizi yao ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanusi mkubwa.

"Miundo mbinu wezeshi itawapa fursa wakandarasi wafabye kazi kwa ufanisi mkubwa sana kwa  sababu maji yatakuwa yanapatikana muda wote na kila siku na hili litasaidia katika kuhakikisha mradi wetu wa ujenzi wa bwawa la umeme kumalizika kwa muda ulipangwa,"amesema Prof Mbarawa.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akifunga bomba la kisasa la kusafirishia maji  kwenye eneo la kambi lenye jumla ya Km 1463,kipenyo cha nchi 1.5 na nchi 3 kwenye eneo la ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akifunikia bomba la kusafirishia majighafi kwenye eneo la kambi lenye jumla ya Km 1463,kipenyo cha nchi 1.5 na nchi 3 kwenye eneo la ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dr Suphian Masasi wakiwa wanakagua  bwawa la kusafishia maji yanayotoka katika Mto Rufiji kwa ajili ya matumizi ya wakandarasi waujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makamd Mbarawa akirusha maji katika moja ya bwawa la kusafishia maji yanayotoka katika Mto Rufiji kwa ajili ya matumizi ya wakandarasi waujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akiwa anakagua mradi mkubwa wa maji katika Bwawa la Mto Rufiji utakaoweza kuwasaidia wakandarasi kupata maji ya uhakika kwenye ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge) akiambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka (DAWASA) Dr Suphian Masasi.

SERIKALI YAONDOA RIBA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

$
0
0
 Na WAMJW CHATO - GEITA
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza rasmi kuwa hakutakuwa na riba katika mikopo itakayotolewa kwa wanawake, vijana na walemavu katika ngazi ya Halmashauri.

Kauli hiyo imetolewa wilayani Chato na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Jikomboe.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuwasaidia Wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi hivyo imeona ni bora mikopo itolewe bila riba ili kuwapa fursa wanawake, vijana na walemavu kwa ajili ya kuanzisha miradi ya wingi ya kujikwamua kiuchumi.

Ameongeza kuwa suala la riba limekuwa kikwazo kwa makundi mengi kuweza kukopa na kurejesha mikopo kwa wakati.

"Niseme tu tumeliangalia suala hili kwa karibu ili tuwawezeshe wananchi hasa wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi" alisisitiza Dkt. Ndugulile.
 Mbunge wa Chato (CCM) na Waziri wa Madini Dkt. Medard Kalemani akimshukuru Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile kwa ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya siku mbili mkoani humo.
 Mwekahazina wa kikundi cha Jikomboe kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita akiwasilisha risala yao kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wkati wa kuhitimishwa kwa  ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya siku mbili mkoani humo.
 Baadhi ya wananawake wajasiriamali wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akihitimisha ziara  yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbili ya Naibu Waziri huyo mkoani humo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia malighafi inayotumika kutengeneza batiki wakati alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha  Jikomboe kilichopo Wilaya ya Chato wakati akihitimishaziara  yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbiliua  Naibu Waziri huyo  mkoani humo.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


BREAKING NYUZZZZZ......: MBUNGE WA CHADEMA UKONGA ATANGAZA KUJIUNGA CCM LEO

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MBUNGE wa Jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam Mwita Waitara kupitia Chadema ametangaza rasmi kujiunga na Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Ametangaza uamuzi huo leo katika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam ambapo kabla ya Waitara kuzungunza Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole alitangaza kuwa wanapokea mtu muhimu.

Akizungumza wakati anatangaza huo amesema ameamua kurudi CCM kwasababu lengo lake ni kusaidia wananchi wa Ukonga jijini Dar es Salaam na kufafanua kuna mambo anashindwa kufanya kutokana na kukwamishwa na viongozi wa ngazi za juu wa Chadema.

Amefafanua kila anapotaka kuzungumza na viongozi wa Serikali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa Ukonga viongozi wa Chadema wanamzuia asizungumze na mawaziri kisa wapo CCM. Amesema kwa mazingira hayo ameona ni bora akahamia upande wa pili ambao ni wa CCM na kufafanua kuwa anajua Watanzania watashituka lakini anaomba wamuelewe kwani nia yake ni njema.

Amesema amesema Chadema inajinasibu kuwa ni chama cha demokrasia lakini ukweli ni kwamba hakuna semokrasia na hivyo kuanzia sasa si mbunge wa Chadema.Pia ametangaza kujivua nafasi zote ikiwamo ya Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Pwani na kuongeza pia si Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam. Amesema amesema anataka kuwa huru kwani amechoka kukaa maisha ya kutokuwa huru na kuongeza kwa sasa anaangalia namna bora ya kuendelea kuwatumikia wananci.

",Haya ni maamuzi yangu binafsi,nimetafakari vya kutosha.Nimekaa katika chama cha maigizo na pale Chadema ni sanaa tu.

" Nimepata baraka za wazee wangu wa kabila la Wakurya,hivyo niko salama na kwamba wananchi wanaohitaji maendeleo lazima waunge mkono juhudi za serikali,"asema Waitara.
Amefafanua kuingia kwake CCM haina maana amenunuliwa bali ni uamuzi wake na kueleza Rais Dk.John Magufuli anafanya kazo nzuri ambayo inastahili kuungwa mkono na Watanzania wote. Amesema kuwa Rais Magufuli amefanikisha kuziba mianya ya rushwa na ameimarisha ukusanyaji wa kodi.

Hivyo amesema kuna mambo mengi ambayo yamemuondoa chadema na hayupo tayari kibaki Chadema kwani hataki kufa kwa ugonjwa wa moyo. Ametumia nafasi hiyo kueleza ugomvi wake na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe umetokana na uchaguzi ndani ya chama hicho.

Amesema baada ya kuhoji kumuuliza Mbowe amekaa muda mrefu hapo ndipo tatizo lilipoanzia na amedai kutishiwa maisha hovyo ameona ni bora akaa kando. Ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa suala la uenyekiti Chadema si la Waitara peke yake bali kuna wabunge wengi wa Chadema wanataka mabadiliko.

Amesema kuna wabunge wengi wanataka Mbowe aondoke na wamejipanga kumng'oa maana wanachotaka ni mabadiliko na kusisitiza Mbowe ameshamtikia kauli za vitisho. Amesema anakumbuka Chacha Wangwe alipotaka kugombea uenyekiti wa Chadema alishughulikiwa na leo hayupo,hivyo naye anaogopa yasimkute ya Wangwe.

WANACHUO KUTOKA SOKOINE NA MUHIMBILI WATEMBELEA MAMLAKA YA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI

$
0
0
 Mtumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali,  Bw. Boniface Majinyali (kulia) akiwaonyesha kwa vitendo namna uchunguzi wa sumu unavyofanyika kwenye maabara baada ya wanachuo hao kutembelea maabara hiyo.

 Baadhi ya viongozi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, wahadhiri na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)mara baada ya kumaliza kutembelea maabara.
Mtumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Bw. Alois Ngonyani (kulia) akiwafahamisha wanachuo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (Morogoro) na Muhimbili (Dar es Salaam) kuhusu uchunguzi unaofanywa kwenye maabara ya mazingira mara baada ya kutembelea maabara hiyo. 

Muleba kuunganishwa umeme gridi ya Taifa

$
0
0
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), lipo mbioni kuiunganisha Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera na umeme wa gridi ya Taifa ili kuvutia wawekezaji hasa wa sekta ya viwanda nchini.

Akizungumza leo wakati wa kazi ya kuunganishaji wa laini ya umeme wa grid ya Taifa inayofanyika katika vijiji ya Kitete Wilayani Chato Mkoani Geita, Meneja wa Tanesco Wilaya ya Muleba, Julius Bagasheki, amesema kazi ya uunganishaji wa umeme wa gridi ni utekezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya chama tawala CCM kwa kuhakikisha wanatekeleza sera ya Tanzania ya Viwanda.

Amesema umeme huo wa gridi kwa Wilaya ya Muleba tayari wameanza na mradi wa uunganishaji 33KV ambao sasa unakwenda kuifanya Muleba kuwa na umeme wa uhakika. “Umeme wetu tunachukulia kutoka Uganda ila ila kwa mradi huu sasa unakwenda kuifanya Wilaya ya Muleba kuwa na umeme wa uhakika wa gridi wa Taifa ambao haukatiki ovyo.

“Sisi Tanesco Muleba na Mkoa wa Kagera kwa ujumla tumejipanga vema kuitekeleza kwa vitendo sera ya Tanzania ya viwanda. Hivyo tunawaalika wawekezaji mbalimbali hasa wa sekta ya viwanda sasa waje Muleba kujenga viwanda kwani muda si mrefu tunakwenda kuwa na umeme wa uhakika wa gridi ya Taifa ambao ni mkombozi wa uhakika,” amesema Bagasheki

Baadhi ya wananchi ambao wameshafikiwa wa umeme wa REA III, katika Kijiji cha Kitete, wamesema kuwa hatua ya kupata huduma hiyo sasa wanakwenda kupata maendeleo ya kasi ya kuweza kujiletea maendeleo kwa kuwa na uhakika wa umeme.
 Meneja wa Tanesco, Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera, Julius Bagasheki, akieleza kuhusu kazi ya uungwanishaji wa umeme wa gridi ya Taifa ambayo itasaidia kupata umeme wa uhakika ili kuruhusu uwekezaji wa viwanda vya uhaka wilayani hapa
 Meneja wa Tanesco, Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera, Julius Bagasheki (mwenye fulana ya mistari) akiwaongoza mafundi wa Tanesco, kusimika nguzo mpya ili kuruhusu uunganishahi wa umeme wa gridi ya Taifa
 Mafundi wakiendelea na kazi ya kuunganisha nyaya ili kuweza kuinganisha Wilaya ya Muleba kwenye umeme wa uhakika wa gridi ya Taifa.

 

TUPAMBANENI NA UDANGANYIFU WA HUDUMA- MKURUGENZI MKUU

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga akielezea mwelekeo wa utoaji huduma kwa wanachama wa Mfuko wakati alipokutana na Watoa huduma wa Mkoa wa Kinondoni leo.
 Baadhi ya Watoa Huduma wa Mkoa wa Kinondoni katika kikao cha pamoja na Uongozi wa NHIF ambao ulijadili namna bora ya utoaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wake.
 Watoa Huduma wakifuatilia kwa makini majadiliano juu ya uimarishaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wa NHIF.

Na Grace Michael
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Bernard Konga amewataka Watoa Huduma wote nchini kushirkiana na Mfuko katika kupambana na udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wanachama katika kujipatia huduma za matibabu.

Aliyasema hayo leo wakati akizungumza na Watoa Huduma wa Mkoa wa Kinondoni, Dar es Salaam juu ya uimarishaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wake hasa katika kipindi hiki ambapo wananchi wengi zaidi wanajiunga na Mfuko huo.

“Niwahimize kwamba kwa pamoja tuunganishe nguvu zetu katika kuulinda huu Mfuko kwa kupambana na udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa kushirikiana na baadhi ya wanachama. Uhai wa Mfuko huu unatakiwa kulindwa kwa gharama zozote ili uendelee kuwahudumia Watanzania na uwepo hata kwa vizazi vinavyokuja,” alisema Bw. Konga.

Amewapongeza watoa huduma ambao wamekuwa wakitoa taarifa za udanganyifu walizozibaini katika vituo vyao na kuwaomba waendelee na utaratibu huo ili kuulinda Mfuko. Alisema hatua hiyo inaonesha uzalendo wa Watoa huduma hao katika kuhakikisha Mfuko huo unaendelea na uhai wake kwa manufaa ya wanachama na wananchi kwa ujumla.

“Tumeamua sisi kama NHIF kukutana na watoa huduma wetu wote, tukae na tujadili kwa pamoja ili changamoto zinazotuhusu sisi na nyie watoa huduma tuzimalize ili wanachama wetu wanapofika huko wapate huduma stahiki,” alisema Bw. Konga.

SERIKALI YATOA SIKU 30 KWA MADIWANI WA KIGOMA UJIJI

$
0
0
Yasema wasipojirekebisha italivunja baraza lao

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku 30 kwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kujirekebisha na kumaliza tofauti zao ndani ya siku 30 na iwapo wataendelea na vurugu Serikali haitosita kuvunja baraza la Madiwani.

Amesema hatua hiyo inatokana na Madiwani hao kutumia muda mwingi wakigombana badala ya kuwahudumia wananchi, Serikali inataka kuona wananchi wakihudumiwa kwa kuboreshewa maendeleo katika maeneo yao na si kushuhudia viongozi wakigombana kwa maslahi binafsi. 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Julai 28, 2018) wakati akizungumza na wananchi wa mkoa wa Kigoma katika mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Kigoma Ujiji kwenye uwanja wa Kawawa, akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Kigoma.

“Serikali hairidhishwi na utendaji wenu na nimewapa muda wa mwezi mmoja kumaliza tofauti zenu. Nataka muendelee kufanya kazi za kuwatumikia wananchi wa Manispaa hii ambao wamewachagua ili muwatatulie kero zao na si kuendeleza migogoro,” amesisiza.

Amesema Madiwani hao wanatakiwa kufuatilia changamoto zinazowakabili wananchi wao ikiwemo ya upatikanaji wa dawa katika hospitali, zahanati na vituo vya afya, ambapo licha ya Serikali kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ununuzi wa dawa lakini bado wananchi wanaendelea kukosa huduma hiyo.

Waziri Mkuu amesema matatizo ya madiwani wa Manispaa hiyo anayafahamu na iwapo watashindwa kujirekebisha Serikali haitosita kulivunja baraza hilo kwa sababu Madiwani wake wanatumia muda mwingi kugombana badala ya kuwahudumia wananchi.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa mkoa wa Kigoma kwamba Serikali itaboresha miundombinu ya mkoa huo ikiwemo ya reli, barabara, ujenzi wa bandari na uwanja wa ndege utakaokuwa na uwezo wa kutua ndege kubwa.

Amesema lengo la maboresho hayo ni kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha biashara utakaounganisha nchi za Rwanda, Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na Burundi kwa kuimarisha vivutio vya uwekezaji.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, JULAI 28, 2018.
Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa akizungumza wakati alipoongoza Mkutano wa Wadau wa Michikichi kwenye ukumbi wa NSSF mjini Kigoma Julai 28, 2018. Kulia ni mkewe Mary na wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu, Emmanuel Maganga. 
Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa akizungumza wakati alipoongoza Mkutano wa Wadau wa Michikichi kwenye ukumbi wa NSSF mjini Kigoma Julai 28, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba.
Washiriki wa Mkutano wa Wadau wa Michikichi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipoongoza mkutano huo kwenye ukumbi wa NSSF mjini Kigoma Julai 28, 2018.

CCM WAZINDUA KAMPENI ZA UDIWANI ARUSHA

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha

Chama cha mapinduzi kimesema kuwa kipo kwa ajili ya kuwatumikia na kusikiliza shida za wananchi na wamejipanga kuhakikisha wanaisimamia serikali ipasavyo ili ilani ya chama hicho inatekelezwa kwa asilimia zote na serikali inayoongozwa na chama hicho.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni ya ccm katika kata ya Kaloleni jijini Arusha Naibu Katibu mkuu wa ccm Bara Rodrick Mpogoro amesema kuwa wakazi wa jiji la Arusha wanategemea sekta ya utalii na jiji hilo ni kitovu cha utalii ndio maana ccm chini ya serikali inayoongozwa na chama hicho ikaona hilo na kuamua kufufua shirika la ndege ili watalii waje moja kwa moja na kusaidia mkoa huo kukua kiuchumi.

Amesema kuwa mgombea wa chama cha mapinduzi kwenye kata hiyo atasaidia ukuaji wa maendeleo kwa wananchi na kuhakikisha kuwa malengo ya huduma bora yanawafikia wananchi kwa kasi badala ya hapo awali kwani chama hicho kimejipanga kuhakikisha wanashinda chaguzi mbali mbali kama hapo awali.“Najua Teyari wagombea 12 wa ccm wanasubiria kuapishwa kati ya wagombea 20 hivyo hawa 8 ninaimani kuwa nao watapigiwa kura na chama chetu kuendelea kupata ushindi katika uchaguzi huu”alisema Mpogoro

Kwa upande wake Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka alisema anayoimani na chama hicho kushinda uchaguzi kwani teyari dalili zinaonyesha kuwa chama hicho teyari kimeshinda kwa kishindo uchaguzi huo.Amesema kuwa wakati akimndai mgombea urais wa ccm 2015 kwenye uwanja wa sheikh Amri Abeid aliwaambia huyu ndio rais lakini wengi walimshangaa na kuona kinyume kwa mapenzi yao lakini sasa wanaona yale aliyowaeleza na wengi wanakubaliana na kauli hiyo.

“Najua wengi mmesahau wakati ule wa kampeni ya urais leo nakuja tena hawa wanaorudi ccm sio bahati mbaya hata mgombea wa ukawa 2015 alishasema upinzani ukishindwa uchaguzi huo wasubiri miaka 50 sasa wenyewe mnaona hilo linajitokeza kwa sababu alitambua mgombea wa ccm ni mtu muadilifu na anafanyakazi kile anachoamini kwa maslahi ya wanyonge”alisema sendeka

Nae Moja wa wananchi wa Kaloleni na Kada wa chama hicho John Mshana amesema kuwa anaamini wagombea waliotoka chadema wameaacha maslahi mapana na kuamua kuona wananchi waliowachagua ndio wenye maamuzi na wao kurudi ccm kwa maslahi mapana ya wananchi kuwatumikia kwa mapana badala ya huko walikokuwa awali.

Amesema kuwa kulikuwa na mtu mmoja alikuwa mjanja sana akamshika kipepeo na kumuuliza mwenzake mjanja huyu kipepeo amekufa au yu hai basi Yule mwezake alijibu kuwa uhai wa kipepeo upo mikononi mwako ndio hawa wagombea wetu uhai na maendeleo ya wananchi yapo mikononi mwao kwa sasa.

WAZIRI MKUU AZINDUA KAMPENI YA KUFUFUA ZAO LA MICHIKICHI

$
0
0
*Lengo ni kumaliza tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula nchini

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua kampeni ya kufufua zao la michikichi mkoani Kigoma na kuagiza kuanzishwa kwa kituo cha utafiti wa zao hilo katika chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Kihinga kilichopo mkoani Kigoma kwa kuwa ndiko zao la Michikichi linalimwa kwa wingi.

Amesema Serikali imedhamiria kumaliza changamoto ya upatikanaji wa mafuta ya kula nchini kwa kuhamasisha kilimo cha zao la michikichiki kwa sababu kila mwaka Serikali hutumia zaidi ya sh. bilioni 600 kwa ajili ya kuagiza mafuta ya kula kutoka nje ya nchi.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Julai 28, 2018) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa wa Kigoma, wadau wa zao la michikichi na wabunge wa mkoa wa Kigoma baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku nne inayolenga kuhamasisha maendeleo na kilimo cha zao la Michikichi.Amesema Serikali haiwezi ikaendelea kutumia fedha nyingi za kigeni kuagiza mafuta ya kula kutoka nje wakati uwezo wa kulima michikichi na kuzalisha mafuta ya mawese kwa wingi tunao, hivyo amewataka viongozi wa Serikali wabadilike na wawafuate wakulima kwenye maeneo ya vijijini na wakawasimamie na kuwashauri namna bora ya kulima zao hilo.

Aidha, ameagiza Wizara ya Kilimo ianze taratibu za kisheria za kukihamisha chuo cha Kihinga kutoka Wizara ya Elimu Sayansi ya Teknolojia kwenda wizara ya Kilimo ili shughuli za tafiti za zao la michikichi lifanyike kwa ufanisi. Pia, ameiagiza Wizara ya Kilimo kuwahamishia mkoani Kigoma watumishi wa kituo cha utafiti wa michikichi cha Bagamoyo ifikapo mwezi Agosti, 2018 isipokuwa wale wanaohusika na utafiti wa zao la minazi tu.

Kadhalika, amewataka viongozi wa mikoa yote inayolima michikichi waanzishe mashamba ya michikichiki ili waoneshe mfano kwa wananchi. “Serikali inataka kuona mabadiliko kwenye zao hili. Sioni umuhimu wa Taifa kuendelea kuagiza mafuta ya kula kutoka nje ya nchi wakati uwezo wa kuzalisha ndani upo,”.


Muhimbili Yaendelea Kupata Mafanikio, Watoto 24 Wafanyiwa Upasuaji

$
0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) inaendelea kupata mafanikio makubwa kutokana na kuboresha huduma za upasuaji wa watoto, huku ndani ya siku mbili watoto 24 wakiwa wamefanyiwa upasuaji.

Wataalamu wa upasuaji wa watoto wa Muhimbili wamesema idadi ya watoto wanaofikishwa katika hospitali hiyo kutokana na matatizo mbalimbali, inaeendelea kuongezeka kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Watoto waliofanyiwa upasuaji ni wale wenye matatizo mbalimbali wakiwamo waliozaliwa bila kuwa na njia ya haja kubwa na wengine wenye matatizo kwenye mfumo wa chakula na hewa.Upasuaji wa watoto hao 24 umefanywa na wataalamu wa upasuaji wa watoto wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa upasuaji wa watoto kutoka Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri.

Akizungumza leo katika mkutano na waandishi wa habari, Daktari Bingwa wa Watoto katika hospitali hiyo, Dkt. Mwajabu Rashid Mbaga amesema wataalamu wa muhimbili na wa Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri wameshirikiana kufanya upasuaji mgumu (difficult cases) kwa watoto hao.

Dkt. Mbaga amesema upasuaji huo umekuwa ukifanywa mara kwa mara na wataalamu wa Muhimbili kwa muda mrefu na kwamba katika siku mbili wamekuwa na wataalamu wa Chuo Kikuu cha Alexandria kwa ajili ya kubadilisha uzoefu.“Kuanzia Alhamisi hadi Ijumaa wiki hii tumekuwa na jopo la watalaamu wenzetu 10 wa upasuaji kutoka Chuo Kikuu cha Alexandra kilichopo Misri wakiongozwa na Prof. Saber Mohamed Waheeb mshauri mwelekezi katika upasuaji wa watoto na Dkt. Mohamed Abdelmalak Morsi bingwa wa upasuaji wa watoto,” amesema Dkt. Mbaga.
Madaktari na wataalamu wengine wakiendelea na upasuaji kwa mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa chakula (Gastroeso Phageal Reflux disease).
Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Mwajabu Rashid Mbaga akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya wataalamu wa upasuaji wa watoto wa Muhimbili na wale wa Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri kufanya upasuaji kwa watoto 24 wenye matatizo mbalimbali. Watoto hao wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa huduma hiyo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa MNH, Dkt. Julieth Magandi, Dkt. Petronilla Joseph Ngiloi wa MNH, Prof. Saber Mohamed Waheeb kutoka Misri, Dkt. Mohamed Abdelmalak kutoka Misri na Dkt. Ibrahimu Mkoma wa MNH.
Madaktari bingwa wa upasuaji wa watoto kutoka Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri wakifanya upasuaji kwa mmoja wa watoto ambaye ana tatizo kwenye mfumo wa chakula (Gastroeso Phageal Reflux) disease) kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Kulia ni Prof. Saber Mohamed Waheeb kutoka Misri, Dkt. Mwajabu Rashid Mbaga wa Muhimbili na Dkt. Mohamed Abdelmalak kutoka Misri wakifanya upasuaji.
Dkt. Julieth Magandi wa Muhimbili akipokea zawadi kutoka kwa Prof. Saber Mohamed Waheeb wakati wa mkutano wa wataalamu hao na waandishi wa habari leo.

KAMISHNA JENERALI KASIKE AFANYA ZIARA YA KWANZA MKOANI MOROGORO

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike amehitimisha ziara yake fupi mkoani Morogoro kwa kuongea na baadhi ya maafisa, askari na watumishi raia wa Ofisi ya Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Morogoro na Gereza Kihonda.

Jenerali Kasike ametumia ziara hiyo ya kwanza tangu ateuliwe kuwa mkuu wa Jeshi hilo Julai 13 mwaka huu kuwataka watendaji wote ndani ya Jeshi la Magereza kutambua alama za nyakati na kubadilika kabisa kimtazamo, kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kujisikia aibu kwa kuona Jeshi lao linatajwa kwa ubaya wa kushindwa kutimiza majukumu yake sawasawa.

Amewataka maafisa na askari wote kujiandaa kupokea mpango kazi wa kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa ambao hivi sasa unaandaliwa katika ngazi ya makao makuu ya Jeshi hilo.

Jenerali Kasike amewatolea wito viongozi wote ndani ya Jeshi la Magereza kuwa tayari kupokea maoni ya walio chini yao bila kujali vyeo vyao ili kuweza kufikia malengo tarajiwa.Aidha amesisitiza kuwa ni lazima watendaji wote kufuata maadaili kwakuwa suala la maadili ya kazi halihitaji raslimali ni mtu kubadilika tu.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike akikagua shamba la miwa la gereza Mbigiri, Morogoro lililopo chini ya mradi wa ubia kati ya Magereza na mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF. Mradi huo ukikamilika unatarajiwa kuzalisha zaidi ya tani elfu 30 za sukari kwa mwaka.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike (wa kwanza kushoto) akikagua baadhi ya matrekta na mitambo inayotumika katika kuandaa mashamba ya miwa ya gereza Mbigiri kwenye mradi wa ubia kati ya Magereza na mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF wa kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari. Jenerali Kasike ametembelea mradi huo leo Julai 27, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akitoa hotuba wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa zahanati ya gereza la Mahabusu Morogoro iliyofanyika leo tarehe 27 Julai, 2018.Kamishna Kasike alitumia hafla hiyo kuwakubusha na kuwasihi wageni waalikwa kuitikia wito wa serikali wa kupima afya zao mara kwa mara ikiwa ni njia mojawapo ya kupambana na ukimwi.
Mkuu wa Gereza la Mahabusu Morogoro Marakibu wa Magereza Zephania Neligwa akisoma risala kwa mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike katika hafla fupi ya uzinduzi wa zahanati ya gereza la Mahabusu Morogoro iliyofanyika leo tarehe 27 Julai, 2018. Mrakibu Neligwa amesema ujenzi wa zahanati hiyo pamoja na ununuzi wa vifaa vya tiba na dawa hadi inazinduliwa imegharimu zaidi ya shilingi 24.8 milioni.
Baadhi ya maafisa na askari wa Kingolwira Complex inayojumuisha Chuo cha Ufundi KPF, Gereza Mtego wa Simba, Gereza Mkono wa Mara na Gereza Kuu la Wanawake wakifuatilia kwa makini maelekezo ya kiutendaji kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike (hayupo pichani) alipowatembelea kwa mara ya kwanza leo tarehe 27 Julai, 2018 mara baada ya kufanya uzinduzi wa Zahanati ya gereza la Mahabusu, Morogoro.

MKURABITA Yakabidhi Hati Miliki 661 za Ardhi Wilayani Ikungi

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), NBalozi Daniel Ole Njolay akikabidhi a Hati za Hakimiliki za Kimila wakati wa hafla ya kukabidhi Hati 661 za Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa vijiji vya Kimbwi na Nkununkhana kata ya Puma wilayani Ikungi jana. Hati hizo zimetolewa ikiwa ni muendelezo wa zoezi la urasimishaji wa mashamba katika maeneo hayo lililoanza mwaka 2011 na kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa hati 405. Kutoka kushoto ni Mratibu wa MKURABITA, Bibi. Seraphia Mgembe na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu.Mtendaji Mkuu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Bibi. Seraphia Mgembe akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi Hati 661 za Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa vijiji vya Kimbwi na Nkununkhana kata ya Puma wilayani Ikungi jana. Hati hizo zimetolewa ikiwa ni muendelezo wa zoezi la urasimishaji wa mashamba katika maeneo hayo lililoanza mwaka 2011 na kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa hati 405. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Kapteni Mstaafu John Chiligati, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA, Balozi Daniel Ole Njolay na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu.Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi aliyemaliza muda wake Kapteni Mstaafu John Chiligati akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Hati 661 za Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa vijiji vya Kimbwi na Nkununkhana kata ya Puma wilayani Ikungi jana. Hati hizo zimetolewa ikiwa ni muendelezo wa zoezi la urasimishaji wa mashamba katika maeneo hayo lililoanza mwaka 2011 na kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa hati 405.
Baadhi ya wananchi waliopatiwa Hati za Hakimiliki ya Kimila wakisoma hati zao wakati wa hafla ya kukabidhi Hati 661 za Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa vijiji vya Kimbwi na Nkununkhana kata ya Puma wilayani Ikungi jana. Hati hizo zimetolewa ikiwa ni muendelezo wa zoezi la urasimishaji wa mashamba katika maeneo hayo lililoanza mwaka 2011 na kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa hati 405.Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njolay (aliyejifunika shuka) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi waliokabidhiwa Hati za Hakimiliki za Kimila wakati wa hafla ya kukabidhi Hati 661 za Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa vijiji vya Kimbwi na Nkununkhana kata ya Puma wilayani Ikungi jana. Hati hizo zimetolewa ikiwa ni muendelezo wa zoezi la urasimishaji wa mashamba katika maeneo hayo lililoanza mwaka 2011 na kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilitolewa hati 405. (Picha zote na: Frank Shija, MAELEZO, Ikungi, Singida)

RC MNYETI AWAPA ONYO WANAOFUNGIA VIWANDA OVYO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amesema hatakubali kuona maamuzi mabovu yanatolewa kwenye mkoa wake ikiwemo kufungia kiwanda bila sababu ya msingi.

Mnyeti ameyasema hayo mjini Babati kwenye kiwanda cha pombe cha Mati Super Brands Ltd ambacho kilifungiwa hivi karibuni na mkemia wa serikali na yeye akaagiza kifunguliwe.Alisema viongozi wa serikali wanapaswa kuwa wasaidizi kwa kuwaelewesha kitaalamu wawekezaji ili warekebishe mapungufu pindi yakiwepo na siyo kufungia viwanda.

Alisema hivi sasa serikali ipo kwenye mchakato wa ujenzi wa viwanda vipya hivyo wataalamu wanatakiwa kutumia elimu yao kuwaelimisha wawekezaji na siyo kuwakandamiza.“Hizo mbwembwe kafanyie sehemu nyingine siyo Manyara, haiwezekani mtu eti anajiita mtaalamu wa serikali anafungia kiwanda sababu ya ukosefu wa komeo la mlango au kuwa na eneo dogo la kuhifadhi bidhaa,” alisema Mnyeti.

Alisema kabla ya kukifungulia kiwanda hicho kilichofungiwa na mkemia alifuatilia na kupeleleza ili kujiridhisha sababu ya kukifungulia akabaini hazina mantiki.Mkurugenzi wa kiwanda cha Mati Super Brands Ltd, David Mlokozi alisema ili kuunga mkono kauli ya Tanzania ya viwanda wapo mbioni kuanzisha viwanda vingine mkoani Manyara.

Mlokozi alisema hivi karibuni watamuomba mkuu huyo wa mkoa afungue kiwanda kingine cha vinjwaji vikali ili kukuza uchumi wa nchi na kutoa ajira kwa wananchi wa eneo hilo.Alisema kwenye kiwanda hicho wakati huu wa uzalishaji hulipa sh60 milioni kama kodi ya mapato serikalini kupitia mamlaka ya mapato nchini (TRA).
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akikagua kinywaji kinachotengenezwa na kampuni ya Mati Super Brands Ltd ya Mjini Babati, kushoto ni katibu muktasi wa kampuni hiyo Melania Daniel na katikati ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Babati mjini Elizabeth Marley.
Mkurugenzi wa kiwanda cha Mati Super Brands Ltd cha mjini Babati David Mlokozi akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti, kushoto na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Babati mhandisi Raymond Mushi.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha kampuni ya Mati Super Brands Ltd cha mjini Babati.

MAKAMU WA RAIS AKAGUA MELI KATIKA BANDARI YA KIWIRA NA ITUNGI KYELA MBEYA

$
0
0


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa mkoa wa Mbeya pamoja na Wafanyakazi na Wataalam kutoka kampuni ya Songoro Marine wanaoshiriki katika kuunda meli ya MV. Mbeya II itakayobeba abiria 200 pamoja na tani 200 za mizigo katika bandari ya Itungi wilayani Kyela mkoani Mbeya. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua maendeleo ya ujenzi wa meli ya MV. Mbeya II itakayobeba abiria 200 pamoja na tani 200 za mizigo katika bandari ya Itungi wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua meli mbili mpya za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 kila moja ambazo ni Mv. Njombe na Mv. Ruvuma katika bandari ya Kiwira wilayani Kyela mkoani Mbeya. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images