Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

MICHUZI TV: WAZIRI MKUU AMESEMA SERIKALI IMEJENGA VITUO VYA AFYA 108


MABARAZA YA WATOTO YAHIMIZWA KUFICHUA VITENDO VYA UKATILI

$
0
0
Na WAMJW- Mwanza
Mabaraza ya Watoto nchini yamehimizwa kutumia elimu wanayoipata kuibua vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ili kuondokana na vitendo hivyo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile wakati akizungumza na wajumbe wa Baraza la Watoto la Mkoa wa Mwanza alipowatembelea na kuona shughuli wanazofanya wajumbe wa Baraza hilo.

Dkt.Ndugulile amesema kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2017 takribani wanawake na watoto 41,000 walifanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kati yao  13,000 wakiwa ni watoto pekee.

Ameongeza kuwa vitendo vya ukatili vimeongezeka ukilinganisha na matukio ya vitendo vya ujambazi nchini ambapo suala hilo halitakiwi kufumbiwa macho na wananchi na wadau.

Aidha Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa wananchi hasa wazazi na watoto kutomalizana nyumbani endapo vitatokea vitendo vya ukatili katika familia zao bali kuviripoti katika mamlaka husika.
  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akihojiwa na wanahabari watoto wa mkoa wa Mwanza wakati alipowatembelea Baraza la Watoto la Mkoa wa Mwanza na kuona shughuli wanazofanya wajumbe wa Baraza hilo.
 Mwenyekiti wa Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Joel Festo akiishukuru Serikali na wadau kawa kuendelea kuwajali watoto kuanzia katika utoaji wa huduma za afya na kutekeleza upatikanaji wa haki zao za msingi ikiwemo haki ya kuishi, kulindwa, kuendelezwa, kushirikishwa na kutobaguliwa.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akimkabidhi Mtunza Hazina wa Baraza la watoto la Mkoa wa Mwnzxa kiasi cha Shillingi 250,000/= ikiwa ni mchango wake kwa ajili ya ununuzi wa printa kwa ajili ya shughuli za ofisi za Baraza hilo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kitaifa wa Baraza la Watoto na Viongozi na wajumbe wa Baraza la Watoto la Mkoa wa Mwanza, viongozi wa mkoa na wadau wa watoto mkoani humo mara baada ya kulitembelea Baraza la Watoto la Mkoa wa Mwanza na kuona shughuli wanazofanya wajumbe wa Baraza hilo. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TOURISTS FLOCK TO TARANGIRE NATIONAL PARK

$
0
0
The Tarangire National Park is the sixth largest national park in Tanzania, it is located in Manyara Region. The name of the park originates from the Tarangire River that crosses the park, which is the primary source of fresh water for wild animals in the Tarangire Ecosystem during the annual dry season. 

The Tarangire Ecosystem is defined by the long-distance migration of wildebeest and zebras. During the dry season thousands of animals concentrate in Tarangire National Park from the surrounding wet-season dispersal and calving areas. It covers an area of approximately 2,850 square kilometers (1,100 square miles.)

The landscape is composed of granitic ridges, river valley, and swamps. Vegetation is a mix of Acacia woodland, Commiphora-Combretum woodland, seasonally flooded grassland, and Baobab trees. The park is famous for its high density of elephants and baobab trees. Visitors to the park in the June to November dry season can expect to see large herds of thousands of zebra, wildebeest and cape buffalo. Other common resident animals include waterbuck, giraffe, dik dik, impala, eland, Grant's gazelle, vervet monkey, banded mongoose, and olive baboon.

Predators in Tarangire include African lion, leopard, cheetah, caracal, honey badger, and African wild dog. The oldest known elephant to give birth to twins is found in Tarangire. A recent birth of elephant twins in the Tarangire National Park of Tanzania is a great example of how the birth of these two healthy and thriving twins can beat the odds.

Home to more than 550 bird species, the park is a haven for bird enthusiasts. The park is also famous for the termite mounds that dot the landscape. Those that have been abandoned are often home to dwarf mongoose.

In 2015, a giraffe that is white due to leucism was spotted in the park.Current wildlife research projects in the park include the Tarangire Elephant Project, Tarangire Lion Project, and Masai Giraffe Conservation Demography Project.
 A velvet monkey tries to solicit some cookies from some tourists taking a breather at the gates of the Tarangire National Park, however it is strictly forbidden to feed animals in national parks mainly for fear of spreading deceases to the wild animals.
A motorcade of tourists  is surrounded by a large herd of elephants in the Tarangire National Park. The park is famous for the highest concentration of elephants per square kilometer in the world. Photos by Issa Michuzi

VIONGOZI WA KISIASA TUHAMASISHE WANANCHI KUENZI UTAMADUNI WAO - WAZIRI MKUU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa wakiwemo mawaziri na wabunge wawahamishe Watanzania kuendeleza utamaduni wao.

Ametoa wito huo leo (Jumatano, Julai 18, 2018) wakati akizungumza na wazee na wananchi wa Makunduchi mara baada ya kushuhudia maadhimisho ya sikukuu ya Mwaka-Kogwa yaliyofanyika Makunduchi, wilaya ya Kusini, mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

“Mawaziri wote, tuna dhamana ya kuwahamasisha Watanzania waendeleze utamaduni ili uwe ni jambo hai. Wabunge na wawakilishi tukiwa kwenye majukwaa, tusisitize Watanzania waendeleze utamaduni,” amesema.

Amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) zinasimamia uwepo wa utamaduni na zenyewe zinaongozwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imelenga kuihamasisha  jamii kuuenzi,  kuulinda  na  kuudumisha utamaduni wa Mzanzibari na kushiriki katika uandaaji wa matamasha 50 ya utamaduni.

“Lazima utamaduni uendelezwe ndani na nje ya nchi na ni lazima tufanye jitihada tuwarithishe watoto utamaduni wetu. Kwa mfano, hapa Zanzibar mnalo tamasha la ZIFF, lile ni la kimataifa, vyombo vya muziki ni vya kisasa. Ni vema sasa, tukaangalia uwezekano wa kuwa na tamasha la huku chini ambalo litatumia ala za muziki za asili,” alisema.

Akizungumzia sherehe za Mwaka Kogwa, Waziri Mkuu alisema hii ni mara yake ya kwanza tangu azaliwe kuona watu wakichapana viboko si kwa ugomvi wala chuki, bali wakiwa na furaha.

“Mwaka Kogwa ni utamaduni wetu, pande zote za visiwani na zimekuwa zikifanyika kila mwaka lakini hivi sasa ni Makunduchi peke yake ambao mmeweza kuendeleza utamaduni huu, wengine wameacha kuadhimisha sherehe hizi,” amesema.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuhitimisha  Sherehe za Mwakakogwa, eneo la Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Sherehe za Mwakakongwa  zilizofanyika Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,  Hassan Khatib Hassan. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria katika Sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika  Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika sala ya kumwombea Rais wa Awamu ya Nne wa Zanzibar, Idris Abdul Wakil kwenye kaburi la Rais huyo enero la Makunduchi, Zanzibar Julai 18, 2018.  Wengine pichani kutoka kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Sira Ubwa  Mwamboya, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja , Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,  Hassan Khatib Hassan.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mohammed Abdulwakil ambaye ni Kaka wa Rais  wa Awamu ya Nne wa Zanzibar, Idris Abdul Wakil  Wakati  alipozulu kaburi la Rais huyo, eneo la Makunduchi, Zanzibar Julai 18, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akivalishwa kofia na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Mwakakogwa, Mwalimu Makungu Mwita katika sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa ametembelea mradi wa uchimbaji wa visima virefu vya Kimbijii na Mpera wenye thamani ya Bilioni 19.6  vitakavyosaidia kupatikana kwa lita za maji Milioni 260 kwa siku.

Mradi huo wa visima vya maji uliochini ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) una lengo la kuongeza wingi wa maji katika maeneo mbalimbali ya Jijini Dar es Salaam na kufikia lita Milioni 720 kwa siku kufikia mwaka 2032.

Prof Mbarawa akiwa ameongozana na Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA  Dkt Suphian Masasi ameweza kukagua visima hivyo na kuwataka wakandarasi wa mradi huo kuhakikisha unakamilika kwa wakati.

Akizungumza wakati wa kukagua visina hivyo, Prof Mbarawa amesema kuwa mradi huo utawasaidia wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwa utasaidia upatikanaji wa maji safi na salama na yatakayotosheleza kwa matumizi yao.

" Mradi huu wa Kimbiji na Mpera utakaotoa Lita Milioni 260 kwa siku utasaidia sana wananchi wa Dar es Salaam, ukichukulia Mradi wa Ruvu Juu na Ruvu chini unatoa lita Milioni 502 kwa siku kwa ujumla wake utaleta chachu ksa wananchi kupata maji kwa uhakika,"amesema Prof Mbarawa.
WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa (katikati), akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa miradi ya maji wa kampuni ya EGIS, Dk. Charles Kaaya, kuhusu kupima urefu wa kisima kirefu katika mradi wa maji wa visima virefu vya Kimbiji, wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasi.
 WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa  akinywa maji katika moja ya Kisima ya miradi ya maji ya Kimbiji na Mpera wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasi.
 WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akiwa pamoja Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasikatika mradi wa maji wa visima virefu vya Kimbiji, wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam utakaofanikisha upatikanaji wa lita Milioni 260 kwa siku.


'KUMKAMATA MTUHUMIWA KABLA YA UPEPELEZI KUKAMILIKA KUNASABABISHA KESI KUTOMALIZIKA KWA WAKATI'

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii

IMEELEZWA kuwa kumkamata mtuhumiwa kabla upelelezi haujakamilika ni moja ya sababu inayosababisha kesi kushindwa kumalizika kwa wakati na kusababisha haki kupatikana kwa mhusika kwa haraka.

Hakimu Mkazi, Augustine Rwizile ambaye ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu amesema hayo leo mkoani Morogoro alipokuwa akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari za Mahakama kwa lengo la kuwasaidia kuandika habari za mahakama kwa ufasaha.

Amesema mtuhumiwa anatakiwa kukamatwa baada ya upelelezi kukamilika ndipo kesi ipelekwe mahakamani,  ili mshtakiwa akisomewa tuhuma zake basi  iweze kusikilizwa na kumalizika ndani ya muda ambao umepangwa.

"Kinachotakiwa kabla ya mtuhumiwa kufikishwa mahakamani ni kufanyika kwa upelelezi,  kukusanya ushahidi na kisha mtuhumiwa apelekwe mahakamani hapo kesi itasikilizwa kwa haraka,"amesema Hakimu Rwezile.

Ameongeza kuwa,  " sehemu kubwa hapa kwetu, tunaanza na ukamataji, mtu anakaa mahabusu na baadae ndipo anapelekwa mahakamani, akisahapelekwa huko ndiyo upelelezi unaanza jambo ambalo si sahihi, na limekuwa likilalamikiwa na  watuhumiwa kuwa wamekaa mahabusu muda mrefu bila kuletwa mahakamani, jambo hilo huchangiwa na suala la upelelezi kutokukamilika".

Ameongeza matakwa ya sheria yanataka mtuhuhumiwa akikamatwa anatakiwa kufikishwa mahakamani ndani ya saa 24.

" Ikitokea mtuhumiwa amekamata na amefikishwa mahakamani halafu akatoa malalamiko kuwa baada ya kukamatwa amekaa mahabusu kwa muda mrefu basi hakimu unatakiwa kuliangalia suala hilo kabla hajaendelea na hatua nyingine, "amesema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Habari , Elimu na Mawasiliano, Mahakama Mkuu ya Tanzania, Nurdin Ndimbe amewataka wanahabari kutumia mafunzo hayo ya siku tano kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu za mahakama wakati wa kuripoti taarifa za mahakama.

CHINA YAITUMIA TANZANIA KUZINDUA TEKNOLOJIA MPYA

$
0
0
*Ni ya mwamvuli unaotumia mionzi ya jua kutengeneza umeme, kuanza kutumika Karagwe

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
CHAMA cha Kukuza Uhusiano kati za Tanzania na China umefanikisha kupatika kwa msaada wa miavuli 100 inayotumia nguvu ya jua kuzalisha umeme ambayo imekabidhiwa kwa Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.

Miavuli hiyo ambayo ni teknolojia mpya iliyozinduliwa China inakwenda kuanza kutumika wilayani humo kwenye baadhi ya shule, zahanati na kituo cha afya kwa lengo la kuhakikisha nishati ya umeme inapatikana kwa ustawi wa maendeleo ya nchi yetu.

Msaada huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Taasisi ya Maendeleo ambayo ipo chini ya Chama cha Kikomunisti cha China(CPC).

Hivyo Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa wa CPC Song Tao ndio aliyokabidhi msaada huo ambapo amesema wanatambua urafiki , udugu na ujamaa wa nchi hizo mbili na hivyo wanatambua umuhimu wa kuendelea kuisaidia Tanzania.

Akizungumzia msaada huo Katibu Mkuu wa Chama cha Kukuza Uhusiano wa Tanzania na China Joseph Kahama amesema msaada huo umetokana na jitihadaza chama chao katika kuhakikisha uhusiano wa nchi hizo mbili unaendelea.

Amefafanua kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kuzinduliwa kwa teknolojia hiyo ambayo kwa hapa nchini itakwenda kuanza kutumika wilayani Karagwe.

Amesema miavuli hiyo ya jua itasaidia kuweka mazingira mazuri ya wanafunzi kusoma katika shule ambazo msaada utapelekwa na kufafanua kuwa giza litakapoingia basi wafunzi watapata mwanga kupitia msaada huo.

Pia amesema kwenye vituo vya afya na zahanati  msaada huo unakwenda kusaidia kuboresha mazingira ya utoaji huduma za afya na kueleza miavuli hiyo inaweza kutumika katika vifaa mbalimbali vinavyotumia umeme.

"China imeamua kuitumia Tanzania kuzindua teknolojia hiyo ambayo haiko mahali kokote duniani .Tumepewa miavuli 100 na mingine itaingia nchini Oktoba mwaka huu .

Alipoulizwa kuhusu thamani ya msaada huo amejibu kuwa hawezi kuifahamu ila anachojia teknolojia mpya nayo ina gharama zake.

Awali Mwenyekiti wa Chama cha Kukuza Uhusiano wa Tanzania na China Dk.Salim Ahmed Salim ameipongeza nchi ya China kwa msaada huo na ni uthibitisha unaodhihirisha urafiki wao wa muda mrefu.



KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BENCHI LAMKIMBIZA JUMA LUIZIO SIMBA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mchezaji wa zamani wa simba Juma Luizio amereja katika timu yake ya zamani Mtibwa Sugar ili kukitumia kikosi hicho cha Mabingwa wa Kombe la Azam Sports Federation (FA).

Mabingwa wa kombe la FA  leo wamefanikisha kuinasa saini ya Juma Luizio ambaye alitimka kwenda kucheza soka la kulipwa nchini Zambia katika Klabu ya Zesco kabla ya kuja kwa mkopo kwenye Klabu ya Simba.

Luizio aliyekuzwa na timu ya vijana ya Mtibwa Sugar  amekuwa na msimu mbaya katika klabu ya Simba akiwa hapati nafasi kwenye kikosi cha Mabingwa hao wa Ligi Kuu Ya Vodacom msimu wa 2016/17.

Kurejea kwa Luizio kwenye klabu ya Mtibwa yawezekana ameenda kuziba nafasi ya Hassan Dilunga anayewaniwa na klabu ya Simba na kukiwa na uhakika wa tayari ya kumwaga wino kwa wekundu hao wa msimbazi.

VYAMA VYA UKOMBOZI BARANI AFRIKA VYATAKIWA KUINGIA KATIKA AWAMU YA PILI YA UKOMBOZI WA KIUCHUMI

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
VYAMA vilivyoshiriki kupigania ukombozi wa Bara la Afrika sasa vimetakiwa kuingia awamu ya pili ya ukombozi wa kiuchumi kwa ajili ya maendeleo ya Bara la Afrika huku vikitakiwa kukomesha rushwa, ufisadi na ubadhirifu.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd wakati anafunga mkutano wa siku mbili uliohusisha vyama vilivyokuwa mstari wa mbele kupigania ukombozi Kusini mwa Bara la Afrika.

"Awamu ya kwanza ilikuwa ni kupigania uhuru kwa nchi za Afrika na sasa uhuru tunao, hivyo vyama hivyo vinatakiwa kuingia awamu ya pili ya ukombozi wa kiuchumi.

"Kuna kila sababu ya kujifunza kutoka China ambapo wameendesha mapinduzi ya kiuchumi na  kuwakomboa wananchi wake wapatao bilioni  mbili,"amesema.

Amefafanua kama si China mambo yangekuwa mabaya na kama ingekuwa inatolewa Kombe la Dunia kwa nchi ambayo imefanikiwa kujenga uchumi imara basi kombe lingekwenda China.

Balozi Idd amesema China imekuwa ikitoa msaada kwa nchi mbalimbali za Afrika ikiwamo Tanzania ambayo imekuwa ikinufaika na misaada ya nchi hiyo na miradi mbalimbali ambayo imeacha alama isiyofutika akitolea mfano reli ya TAZARA.

Amesema kwa upande wa Zanzibar kuna miradi mingi ya maendeleo imefanyika ikiwamo pia ujenzi wa kiwanda cha sukari , viwanja vya kisasa vya mpira.

Akifafanua zaidi kuhusu mkutano huo, amesema ni vema yale ambayo wamekubaliana yakatekelezwa kwa vitendo na si maneno matupu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiufunga mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China ukiofanyika kwa siku mbili Jijini Dar es Salaam .
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa kutoka Chama cha Kikoministi cha China (CPC)  Xu Lyuping akitoa salamu za Chama cha Kikoministi wakati wa kufungwa  kwa mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama Kinachotawala Nchini Cape Vade Bwana Miguel Petro akitoa salamu za Chama hicho wakati wa kufungwa  kwa mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China leo Jijini Dar es Salaam. Picha na – OMPR – ZNZ.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

LIGI KUU TANZANIA BARA KUANZA AGOSTI 22

$
0
0
*Simba, Mtibwa kupambana Agosti 18 katika mechi ya Ngao ya hisani

Na Khadija Seif,globu ya jamii

PAZIA la michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2018-2019 linatarajia kuanza rasmi Agosti 22 mwaka huu.

Ambapo kabla ya kuanza kwa ligi kutakuwa na mechi ya Ngao ya Hisani itakayowakutanisha Simba na Azam FC katika uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza.Mechi hiyo itachezwa Agosti 18 mwaka huu

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura amesema jumla ya timu 20 zitashiriki katika ligi hiyo huku akisisitiza ligi itaanza Agosti 22 na kumalizika Mei 29 mwakani.

Amesema kuwa  mpangilio wa ratiba umezingatia matakwa ya mdhamini mkuu ambaye ni Azam TV na  kalenda ya michuano ya kimataifa.

Amefafanua kuwa mechi katika ligi hiyo zitakuwa zinachezwa kati ya saa 8 mchana na saa nne usiku na kwamba asilimia 90 ya mechi zitachezwa kuanzia saa 12 jioni hasa katika siku za kazi.

"Tunatangaza rasmi ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2018-2019 ambapo jumla ya timu 20 zitashiriki kwani awali tulikuwa na timu 16 na sasa timu nne zimeongezwa,"amefafanua Wambura.

Kuhusu mtanange wa Ngao ya hisani Wambura amesema kumekuwa na kawaida kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu kunakuwa na mechi inayowakutanisha mabingwa wa Ligi kuu pamoja na bingwa wa Kombe la Shirikisho la Azam.

VIONGOZI YANGA WAWAITA YONDAN,KESSY OFISINI KWA ABASS TARIMBA

$
0
0
Na Agness Francis, Blogu ya jamii

VIONGOZI wa Klabu Yanga wameamua kukutana na wachezaji Hassan Kessy na Kelvin Yondan kwa ajili ya kuhakikisha wanabaki katika klabu hiyo

Hata hivyo bado haijafahamika iwapo wamemalizana na wachezaji hao au laa zaidi ya kuwa wamewaita na kukutana nao katika Ofisi za Abass Tarimba leo jijini Dar es Salaam .

Hatua hiyo imekuwa wakati kukiwa na madai kuwa kuna uwezekano tayari Yondan ameshafanya mazungumzo na Simba FC na kilichobakia ni kuingizwa fedha tu ili asaini.

Hivy wakati kukiwa na madai hayo viongozi wa Yanga nao inaelezwa wamefanya mazungumzo na wachezaji hao ili waweze kubaki kwenye klabu hiyo kwa ajili ya msimu wa ligi kuu unaotarajia kuanza Agosti 22 mwaka huu.

"Wachezaji hao wameitwa na viongozi wa Yanga kwa ajili ya mazungumzo.Hata hivyo bado hatujafahamu nini ambacho kimeendelea aidha wamekubali kubaki au laa,"amesema mmoja wa watoa taarifa.

Wakati hayo yakiendelea wachezaji ao wamegoma kusafiri na timu kutokana na kutolipwa fedha zoa za usajili wa msimu ujao.

Wachezaji hao walitakiwa kuambatana na wenzao kuelekea nchini Kenya kucheza mchezo wa raundi ya tatu kundi D dhidi Gor Mahia katika katika michuano inayoendelea ya Shirikisho barani Afrika.

FLYOVER YA TAZARA JIJINI DAR ES SALAAM YAKARIBIA KUMALIZIKA UJENZI WAKE

$
0
0
 Daraja la juu "Flyover" llinalojengwa na serikali katika eneo la  TAZARA  jijini Dar es salaam likiwa katika hatua za Mwisho za ujenzi wake. 
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SERIKALI KUTOVIVUMILIA VYUO VITAKAVYOTOA MAFUNZO KINYUME NA UTARATIBU

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imesema haitavivumilia  vyuo ambavyo vitabainika vinatoa mafunzo yake kinyume na utaratibu uliowekwa na lengo ni kuhakikisha vijana wanapata elimu bora.

Pia imeiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), kuongeza kasi ya ukaguzi na kuvifungia vyuo hivyo bila kujali ni vya umma au binafsi na kufafanuliwa Serikali hutenga Sh.bilioni 427.5 kwa ajili ya utoaji wa elimu kwa vyuo vya elimu ya juu nchini, hivyo haitarajii kuona madudu yanafanyika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati anafungua maonesho ya 13 ya Vyuo  vya Elimu ya Juu katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Amesema Serikali haitaweza kuvumilia uwepo wa vyuo visivyokuwa na sifa nchini kwani vimekuwa ni chanzo vya kuzalisha uwepo wa wanafunzi wasio na sifa.

Prof.Joyce amesema hivi karibuni Serikali  ilifanya ukaguzi kwa baadhi ya vyuo na kubaini kuwepo kwa programu nyingi zilizokuwa zikiendeshwa kinyume cha taratibu.

“Sasa TCU ongezeni kasi ya ukaguzi kwa vyuo vyote nchini na endapo mkibaini viko  baadhi  vinaendesha mafunzo  kinyume cha taratibu zilizoweka aidha kiwe cha Umma au binafsi  fungia mara moja.
 Waziri wa Elimu wa Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza katika Maonesho ya Vyuo vikuu nchini pamoja na vya nje vinavyoshiriki maonesho hayo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar Salaam.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia akipata maelezo katika Chuo Kikuu Mzumbe  pamoja kuangalia jnisi wanafunzi wanapoomba udahili kwa njia ya kieletroniki (hawapo pichani)katika maonesho ya vyuo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo kutoka kwa Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Venaranda Malima kuhusiana Bodi hiyo katika maonesho ya vyuo Vikuu.
 Wanafuzi wakipata maelezo kutoka kwa  Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano wa Umma wa Taasisi ya Uhasibu Nchini (TIA) Lilian Rugaitika. Kuhusiana na kozi wanazozitoa katika maonesho ya vyuo vikuu jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI SHEREHE ZA MWAKAKOGWA ZANZIBAR

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama ngoma ya asili wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Zanzibar kuwa mgeni rasmi katika Sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika Makunduchi, Julai 18, 2018.  Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Ayoub Mohammed Mahmoud.
.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuhitimisha  Sherehe za Mwakakogwa, eneo la Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiingia kwenye eneo la Shereza za Mwakakogwa zilizofanyika Makunduchi, Zanzibar Julai 18, 2018. 
 Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria katika Sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika  Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika sala ya kumwombea Rais wa Awamu ya Nne wa Zanzibar, Idris Abdul Wakil kwenye kaburi la Rais huyo enero la Makunduchi, Zanzibar Julai 18, 2018.  Wengine pichani kutoka kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Sira Ubwa  Mwamboya, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja , Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,  Hassan Khatib Hassan. 


BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO JULAI 18, 2018


MWANAFUNZI KUFANYIWA USAJILI PAPO HAPO BANDA LA TAASISI YA USTAWI WA JAMII KATIKA MAONESHO YA 13 YA VYUO VIKUU MNAZI MMOJA

$
0
0
Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii anawakaribisha wahitimu wote wa kidato cha sita na kidato cha Nne pamoja na wazazi wa wahitimu kwenye banda la Taasisi hiyo katika maonyesho ya 13 ya vyuo vikuu kwenye viwanja vya Mnazi mmoja, kukutana na wahadhiri wa taasisi na kupata maelezo ya kina kuhusu programu za masomo zitolewazo na Taasisi hiyo pia kupata maelezo ya jinsi ya kujiunga na Taasisi kwa mwaka huu wa maosmo 2018/2019 ambapo mwanafunzi atafanyiwa usajili papo hapo katika banda la Taasisi ya Ustawi wa jamii.

Ili kusajiliwa mwanafunzi afike na Vivuli vya vyeti vya kitaaluma na cheti cha kuzaliwa pamoja na ada a Usajili ambayo ni Tsh. elfu 10,000/ tu. 
Mhadhiri msaidizi wa idara ya Rasilimali watu Bi. Christina fille akitoa maelezo na kujibu maswali kwa wanafunzi mbali mbali waliofika kwenye Banda la Taasisi ya Ustawi wa Jamii. 
Wanafunzi na Wananchi mbali mbali wakipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Taasisi ya Ustawi wa jamii kwenye maonyesho ya 13 ya Vyuo vikuu katika viwanja vya Mnazi mmoja Dar es salaam.

BENKI YA STANBIC YAZINDUA KAMPENI YA ‘ZAIDI YA BENKI’

$
0
0

 Chachu ya ukuaji wa uchumi jumuishi Tanzania. 

Benki ya Stanbic Tanzania imezindua kampeni maalumu kwa ajili ya chata yake, yenye kauli mbiu isemayo “Zaidi ya Benki”, ikijitofautisha na taasisi nyinginezo kwa kuwa benki yenye kugusa wateja wake kwa kutoa huduma na bidhaa zenye kuwezesha wateja hao pamoja na watanzania kwa ujumla kufikia malengo yao ya kimaisha.

"Nia na madhumuni ya kampeni hii ya 'Zaidi ya Benki' ni kudhihirisha mchango wetu katika kuboresha maisha ya watu na ya jamii kwa ujumla; mara nyingi watu wanapofikiria benki, huwa wanawaza miamala ya kifedha tu, huku wakisahau kinachojiri baada ya mteja kuondoka na fedha zake," alisema Bi. Desideria Mwegelo, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Stanbic Tanzania.

"Sisi hapa Stanbic, tuna desturi ya kufikiria yanayotokea kabla na baada ya miamala kufanyika. Tunaamini kwamba kila tunachofanya hata kiwe kidogo vipi, kina athari katika maisha ya mteja wetu kwa namna moja au nyingine, na ndio sababu huwa tunamfikira mteja katika kila tunachokifanya na kuhakikisha tunaongeza matokeo chanya,” aliendelea kusema.

Kwa mfano, tunaposhiriki katika miradi ya kuleta umeme katika jamii, kwa namna nyingine tunakuwa tumewezesha ukuaji wa viwanda, elimu na fursa nyinginezo zitokanazo na kuwepo kwa umeme.Hali kadhalika kupitia mikopo ya nyumba, watu wanawezeshwa kumiliki nyumba ambazo familia zao hazitokaa zisahau.

Tanzania imesheheni jamii ya vijana wenye jitihada, akili na nguvu, na wenye kutafuta fursa za kujikwamua na kujiendeleza kimaisha kwa kila hali, benki ya Stanbic inataka kuwa sehemu ya jitihada hizo katika kufanikisha ndoto zao na za familia na jamii kwa ujumla.

'Kama wanachama wa Standard Bank Group yenye historia ndefu ya zaidi ya miaka 155 na kuwepo katika nchi 20 barani Afrika, tunaelewa changamoto, tamaduni na watu wa bara hili. Sisi ni zaidi ya benki,’ alisema Bi. Mwegelo. 'Stanbic inahamasishwa na vijana wa kitanzania wenye shauku ya kutumia fursa lukuki zilizopo nchini kwa kutumia ubunifu na mawazo mbadala. Tunataka kufanikisha ndoto zao za kufikia mafanikio ya kifedha. '

Dira ya Maendeleo ya Taifa la Tanzania inatazamia kiwango kikubwa cha maendeleo ya rasilimali watu na inategemea nchi kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Malengo ya Stanbic yanaendana na yale ya taifa huku ikijitahidi kutumia fursa zitokanazo na huduma za kifedha kuboresha maisha ya Watanzania. 


 Hivi karibuni, Benki ilipokea tuzo kwenye tuzo za “Banker Africa Awards” kwa kuwa ‘Benki bora kwa biashara ndogo ndogo na za kati’ nchini Tanzania. Huu ni mfano hai mwingine wenye kudhihirisha nia ya Stanbic katika kuleta maendeleo ya kweli kwenye biashara na ukuaji wa uchumi jumuishi nchini Tanzania.

ALICHOKISEMA BALOZI SEIF ALI IDD KUHUSU VYAMA VYA SIASA BARANI AFRIKA

TANZANIA PRISONS YAANZA KUJIFUA KWA AJILI YA MSIMU MPYA WA LIGI KUU 2018/19

AMANI NATURE RESERVE YATAJWA KUWA MAHALA SAHIHI KWA FUNGATE

Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images