MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya nchini (NHIF)umekabidhi mifuko 245 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Muheza inayojengwa eneo la Lusanga ambayo itaondoa changamoto ambazo walikuwa wakikumbana nazo wananchi.
Makabidhiano hayo yalifanyika juzi wilayani Muheza na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga Ally Mwakababu kwa Mkuu wa wilaya hiyo Mhandisi Mwanasha Tumbo ambapo mifuko hiyo itasaidia ujenzi huo
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo wa saruji,Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha aliushukuru mfuko huo kwa kuona umuhimu kusaidia juhudi walizoanzishwa za ujenzi wa hospitali hiyo ili kuwapunguzia adha wananchi ikiwemo kuunga mkono jitihada za harambee iliyoendshwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu.
Alisema msaada huo umefika wakati muafaka wakiwa kwenye harakati za kuendelea na ujenzi wa hospitali hiyo ambao ni muhimu kwa ustawi wa wakazi wa wilaya hiyo katika kuhakikisha wanakuwa nayo ili iweze
kuwahudumia.
Mkuu huyo wa wilaya alisema ujenzi wa hospitali hiyo ambao utagharimu bilioni 11 mpaka itakapo kamilika lakini hatua iliyopo kwa harambee walioifanya Jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu waliweze kupata bilioni 1.7.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 245 Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Muheza ambayo ilitolewa na mfuko huu kuunga mkono juhudi hizo kushoto ni Mhasibu wa NHIF Tanga Hellena Manyanda na katikati aliyevaa kilemba ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo mkoani Tanga Sophia Kaku
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 245 Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza Julius Mgeni kushoto wanaoshuhudia ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu katikati kushoto ni Mhasibu wa NHIF Tanga Hellena Manyanga na kulia ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Sophia Kaku.
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia akiteta jambo na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tanga Ally Mwakababu katikati .