Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MICHUZI TV: SUMATRA WATOA MAFUNZO YA USAFIRISHAJI WA MIZIGO KWA WAMILIKI VYOMBO VYA USAFIRI NYANDA ZA JUU KUSINI

$
0
0

Na mwandishi wetu wa Mbeya Emmanuel Madafa


Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkuu wa Chuo na wenyeviti watatu

DAWASA yatekeleza miradi ya kuondoa kero za maji kwa wananchi

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii.

Mamlaka ya maji safi na maji taka (Dawasa) inatekeleza mradi Mkubwa wa upanuzi wa chanzo cha maji Chalinze ili kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa maji kwa wakazi wa mkoa wa pwani.

Mradi huo ambao kwa sasa uko katika hatua ya tatu  utahakikisha pia upatikanaji wa maji katika viwanda unakuwa wa uhakika.

Akiongea katika ziara  ya kukagua.. Maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maji na upanuzi wa chanzo cha mtandao wa maji Chakinze, waziri wa maji na umwagiliaji, Profess Makame Mbarawa.amewahakikishia wawekezaji nchini kuwa jitahada kubwa zinafanywa kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa maji katika viwanda vyote kikiwemo cha Sayona.

Amesema, Dawasa kama sekta ya maji, watahakikisha wanatekeleza  azma ya kumaliza tatizo kubwa la maji hadi kwenye viwanda, kwani hakuna kiwanda kitakachoendelea bila ya kuwa na maji ya kutosha.

Naomba niwahakikishie watanzania wenzangu ambao wanania thabiti ya kujenga viwanda kwa ajili ya kukuza uchumi wetu, sisi kama sekta ya maji tutahakikisha kwamba tunawapa nguvu zetu zote na kuwawekea miundombinu ya kisasa ili huduma ya maji iweze kuwafikia na waweze kufanya kazi zao za uzalishaji ili nchi yetu iweze kukua kufikia uchumi wa wakati 2025" amesema Mbarawa.

Aidha ameongeza, katika kutekeleza hilo tayari kuna mradi wa kupeleka maji kwenye kiwanda kikubwa cha Sayona ambao utahusisha kuuweka bomba la maji kutoka kwenye vyanzo vya maji mpaka kufikia kwenye kiwanda hicho, umbali wa kilometa 70 ujenzi ambao  utagarimu shilingi milioni 12

Wakati huohuo waziri Mbarawa amemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi wa Chalinze kuhakikisha unakamilika mwishoni mwa mwezi November mwaka huu. 

Amesema serikali haitasita kuwachukulia hatua wakandarasi wanaochelewesha miradi kwani lengo la serikali ni kupeleka Huduma  bora ya maji kwa wananchi.

Mradi huo wa Chalinze utahusisha upanuzi wa mtambo wa kusafisha maji wa Chalinze ambao chanzo chake ni mto Wami, lengo kubwa likiwa ni kuongeza uzalishaji kufikia Mita za ujazo 900 kwa saa kutoka mita za ujazo 500.

Mradi huo ambao mpaka utakapokamilika utagarimu USD 41,362023.43 ambazo ni mkopo wa masharti nafuu kutoka serikali ya India kupitia Exim benki utahusisha pia ujenzi wa matanki 19,ulazaji wa mabomba ya ukubwa mbali mbali ya umbali wa kilometa 1022, ujenzi wa vizimba 351  vya kuchota maji katika vijiji na vitongoji vya Bagamoyo na Chalinze huku vizimba vingine vinatarajiwa kujengwa katika baadhi ya maeneo ya halmashauri za Handeni, Tanga na Ngerere mkoani Morogoro.

"Mradi huu ukikamilika wakazi wa pwani na Dar es Salaam watafadika na kusahau kabisa kero ya maji.

NAIBU WAZIRI NDITIYE AITAKA TCRA KUWACHUKULIA HATUA KAMPUNI ZA VING’AMUZI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano-Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Nchini (TCRA) kuwachukulia hatua kampuni za ving’amuzi kutokana na kuacha kurusha matangazo ambayo yako kwa mujibu wa leseni zao.

Nditiye ametoa agizo hilo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliyotembelea Mamlaka hiyo , amesema watoa huduma za ving’amuzi wanatakiwa kutoa matangazo bure hata kama mtu hajalipia.

Amesema kuwa TCRA ifuatilie na kama kampuni za ving’amuzi zitaendelea kutoonyesha matagazo bure katika vituo vitano vya luninga wawafungie kutokana na ukiukaji wa leseni walizoombea.

Vituo ambavyo vinatakiwa kurusha matangazo bure bila kulipia ni ITV, Chanel Ten, Star TV,EATV pamoja na Clouds.

Nditiye amesema kuwa maoni kamati watayafanyia kazi katika kupata ufumbuzi ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema kuwa sekta ya mwawasiliano ni ya pili katika uchangiaji wa pato la Taifa ambapo mawasiliano inachangia asilimia 13.1.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Suleimani Kakoso amesema kuwa TCRA lazima ijipange katika teknolojia kutokana na kubadilika kila siku.

Amesema kuwa kadri ya mabadiliko ya Teknolojia yanavyoendelea kukua baadhi ya watu wanajifunza namna ya kufanya wizi kwa kutumia teknolojia.
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano-Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliyotembelea Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Malaba akizungumza kuhusiana na utendaji wa TCRA katika utoaji wa huduma za mawasiliano nchini.

VETA YAJIPANGA KUTOA UJUZI KATIKA SEKTA YA VIWANDA

$
0
0
Na Chalila Kibuda Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Elimu  na Mafunzo ya Ufundi Stadi(VETA) imesema kuwa wamejipanga katika utoaji wa elimu ufundi katika uchumi wa viwanda.

Akizungumza mara baada ya kupokoea kikombe cha ushindi Mwenyekiti wa bodi ya VETA, Peter Maduki amesema kuwa dhamira ya VETA ni kuhakikisha viwanda vinapata ujuzi unaotoka VETA.

Amesema kuwa kumekuwa na mafanikio katika utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi ikiwa nipamoja vijana kuingia katika soko la ajira za moja kwa moja na wengine wakijiajiri .

Maduki amesema katika uchumi wa viwanda VETA ina nafasi kubwa hivyo  ni wajibu wao kuzalisha vijana wengi wa kutumika katika uchumi huo na taifa kusonga mbele .

Aidha ametoa wito wa vijana kujiunga na vyuo vya VETA katika kupata ujuzi na kuwa watu kuzalisha pamoja na kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao.

“Hatutarudi nyuma kwa kuliacha jambo la viwanda wakati ni sehemu ya wadau muhimu wa katika utoaji wa ujuzi wa viwanda”

Wafanyakazi wa VETA wakiwa katika furaha ya ushindi wa kikombe katika maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.
.Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano Watanzania, Kassim Majaliwa akikabidhi kikombe cha ushindi kwa Mwenyekiti wa Bodi wa VETA, Peter Maduki katika ufunguzi wa maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mwanafunzi wa VETA kipawa akitoa maelezo ya ubunifu wa uzio wa ulinzi kwa mwananchi aliyepotembelea banda katika maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.

TBA YAJIPANGA KUOKOA MABILIONI KATIKA MIRADI YA UJENZI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jmaii
WAKALA wa Majengo Tanzania(TBA), limesema imejipanga kuokoa mabilioni ya fedha za miradi hapa nchini ambapo itatekeleza miradi 180 ambayo itagharimu Sh billion 350.

Akizungumza katika maonesho 42 ya Biashara ya kimataifa yanayofanyika katika Viwanja Vya mwalimu Nyerere Afisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga amesema gharama hizo ni nafuu ambapo ingetekelezwa na waty wengine ingekuwa kubwa zaidi.

Alisema mpaka sasa wanajivunia kutekeleza miradi saba ambayo ni pamoja na mradi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam ambao umegharimu Sh.billioni 10 ambapo wameweza kuokoa billioni 80 endapo mradi huo ungetekelezwa na wakandarasi wengine.

Amesema kwa mradi wa ujenzi hospitali ya Geita  wameweza kuokoa billioni 75  na wamejenga kwa billioni 17.

Pia mradi wa hospitali ya Wilaya ya Chato wameokoa Sh.Billioni 60 na wamejenga kwa billioni 13

Katika ujenzi wa Nyumba za magomeni Jijini Dar es salaam wameokoa sh billioni 86 na ujenzi utagalimilu billioni 20.

Mwakalinga alisema TBA inajivunia kuwa na rasilimali watu iliyo bora ambapo mpaka sasa inawataalamu 83 wahandisi 73 pamoja na wabunifu majengo 10.

"Tunajivunia rasilimali watu tulizonazo...ambao ni wazalendo na ndio maana tunajivunia ujenzi ulio bora " alisema Mwakalinga.

Amesema katika mwaka 2017 /2018 uliomalizika mwezi Juni TBA imetoa asilimia 15,ya mapato taluopatikana katika miradi yao ambao ni billioni 2 na kuzipeleka hazina.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch.Elius Mwakalinga akizungumza  na waandishi wa habari kuhusiana uokoaji nwa fedha  miradi mbalimbali wakati  alipotembelea banda TBA katika maonesho 42 ya Biashara ya kimataifa yanayofanyika katika Viwanja Vya mwalimu Nyerere.
  Afisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch.Elius Mwakalinga akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa wakala huo TBA katika maonesho 42 ya Biashara ya kimataifa yanayofanyika katika Viwanja Vya mwalimu Nyerere.
Mteja akipata maelezo ya katika banda la TBA alipotembelea banda TBA katika maonesho 42 ya Biashara ya kimataifa yanayofanyika katika Viwanja Vya mwalimu Nyerere

MANISPAA YA TEMEKE YAHUDUMIA WANANCHI MSIMU WA SABASABA

$
0
0
Na Zainab Nyamka,Glogu ya jamii
HALMASHAURI ya Manispaa ya Temeke imepiga kambi katika viwanja vya sabasaba ikiwa na lengo maalumu la kuwahudumia wananchi katika msimu wa sabasaba na kuwataka wakazi wa Temeke wajitokeze kwa wingi ukizingatia maonesho hayo yanafanyika katika Manispaa yao.

Akizungumza na blogu ya jamii Afisa biashara wa Manispaa ya Temeke bi. Telphina Mbegu ameeleza kuwa katika msimu huu wa sabasaba wanatoa huduma mbalimbali ikiwa pamoja na leseni za biashara kwa wateja wapya na kwa wateja ambao leseni zao zimeisha muda wake wa matumizi.

Aidha ameeleza kuwa wanatoa leseni mbalimbali kama na ushauri kama  taratibu za ujenzi makazi, vileo na huduma mbalimbali za kibiashara.

Pia ameeleza kuwa kama Manispaa wanasikiliza kero na maoni ya wananchi na kuyafanyia kazi na kutatua kero hizo zinazowakabili wananchi wa Manispaa hiyo.

Kuhusiana na kero walizopokea Mbegu ameeleza kuwa wananchi wengi wametoa kero kuhusiana na miundombinu hasa ya barabara, mifereji na takataka katika maeneo mbalimbali katika maeneo wanayoishi.

Pia ameeleza kuwa wanatoa elimu kwa wafanyabiashara wanaotaka kuanza biashara kwa kutoa elimu kuhusiana na upataji wa leseni kwa ajili ya biashara hizo.

Amewaomba wakazi wa Temeke na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo ili waweze kujifunza na kuelimika zaidi kupitia shughuli zinazofanywa na Manispaa hiyo.
 Afisa biashara wa Manispaa ya Temeke Telphina Mbegu akielezea huduma wanazozitoa katika banda liliopo ndani ya Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.
 Afisa biashara wa Manispaa ya Temeke  Telphina Mbegu akimuelezea Jambo mwananchi aliyetembelea banda lao ndani ya Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.

WATANZANIA WATAKIWA KUNUNUA VIFAA VYA UMEME VYENYE UBORA KUEPUKA MAAFA

$
0
0
Na Agness Francis, Globu ya Jamii.
WATANZANIA wametakiwa kutumia vifaa vya umeme vyenye ubora ili kuepukana na kuunguza vitu vyao kutokana na kutokuwa na ubora unaotakiwa kwa matumizi ya nyumbani au viwandani.

Hayo yamesemwa na Meneja Masoko wa Tropical Power Tanzania Rigobert Manega wakati wa maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam na kusema kuwa kwa mwaka huu wamewaletea watanzania transfoma zenye ubora wa hali ya juu kwa matumizi ya majumbani, viwandani na sehemu zingine mbalimbali.

Manega amesema kuwa muitikio wa wananchi kwa mwaka huu umekuwa ni mzuri sana na wengi wakionekana kuanza kuamini vitu vinavyotengenezwa nyumbani.

Amesema wamekuwa wanatoa ushauri kwa watu binafsi, makampuni hata taasisi za kiserikali pindi wanapohitaji vifaa vya umeme ili kuendana na mahitaji yake.

Ameeleza kuwa kwa sasa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) wamekuwa wateja wao wazuri kutokana na ubora wa vifaa vya umeme wanavyovitengeneza hapa hapa nchini vikiwa na ubora wa hali ya juu.

Manega amesema kuwa, kwa sasa vifaa vyao vinauzwa ndani na nje ya nchi na mteja kabla ya kununia kifaa mtaalamu wao anaenda katika jengo, hotel au kiwanda kwa ajili ya kuangalia ni aina gani ya Transfoma inahitajika ili iweze kufanya kazi kwa ustadi unaotakiwa.

Baadhi ya bidhaa zingine wanazoziuza ni pamoja na waya za umeme mkubwa HTna LV, cables za umeme, waya za wiring za majumbani, PVC na vifaa vingine vya umeme.
Meneja Masoko wa Tropical Power Tanzania Rigobert Magena akizungumza na Globu ya Jamii na kuelezea umuhimu wa watanzania kutumia vifaa vyenye ubora na vinavyozalishwa ndani ya Tanzania kwenye Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar.
Meneja Masoko wa Tropical Power Tanzania Rigobert Magena akionyesha moja ya Transfoma wanayotengenza katika Kiwanda chao na zinatumika kwa matumizi mbalimbali nchini na nje ya Tanzania kwenye Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar.

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA ATOA MATAMKO

BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA 06.07.2018

GRACE PRODUCTS ATAJA SABABU ZA KUTWAA TUZO YA THE INTERNATIONAL QUALITY SUMMIT AWARDS

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MSHINDI wa tuzo ya The International Quality Summit Award amewataka watanzania kupenda vitu vya nyumbani kwa sababu ni bidhaa zinazotengenezwa kwa malighafi asili na kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ya Tanzania kwenda uchumi wa Viwanda.

Mwishoni mwa Mwezi wa June,Dr Elizabeth Kilili aliweza kunyakua tuzo ya International Quality Summit Awards iliyofanyika nchini Marekani akiwapiku nchi 116 kutoka duniani kote.

Akizungumza na Globu ya Jamii katika maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Sabasaba, Mkurugenzi Mtendaji Dr Elizabeth amesema kuwa ameweza kufanikiwa kupata tuzo hiyo kwa sababu alibuni na kuthubutu kutengeneza vipodozi akiwa hajanakili au kukopi kutoka kwa mtu yoyote na zaidi amekuwa anatumia vitu vya kiasili kuvitengengeza.

Dr Elizabeth amesema kupitia kampuni yake ya Grace Natural Products ametengenza vipodozi bora na vimewasaidia watu wengi sana hususani wale waliotumia bidhaa za kemikali (sumu) na watakapoanza kutumia bidhaa zake huwasaidia kwa asilimia kubwa.

Amesema, moja ya sababu iliyoweza kumpatia tuzo hiyo ni namna alivyoweza kutengeneza vipodozi vya kiasili kwa ajili ya walemavu wa ngozi (albinism) na vimekuwa msaada mkubwa sana kwa matumizi yao ya ngozi kwakuwa na vimekuwa vikiuzwa kwa bei nafuu zaidi huku zikipata mjini na vijijini.



Dr Elizabeth ameeleza kuwa vipodozi vyake anatengeneza kwa kutumia mazao ya nyuki, matunda na mafuta ya asili ambayo hayana madhara kwa ngozi ya mtu yoyote bali itamfanya mtumiaji kuwa na ngozi nzuri na kuvutia.

Akizungumzia muitikio wa wananchi kwenye maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba kwa mwaka huu yamekuwa sio mkubwa sana tofauti na miaka mingine ila ameweza kupokea pongezi mbalimbali kutoka kwa watanzania waliofika kwenye banda lake.

Grace Product iliyoanza kazi miaka 10 iliyopita imeweza kuleta ushindani mkubwa katika soko la vipodozi na kufanikiwa kuwavutia watu wengi katika matumizi akiwa anatengeneza mafuta ya watoto, mafuta ya nywele, sabuni za kuogea, dawa za kusafishia choo pamoja na Shampoo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Grace Natural Products Dr Elizabeth Kalili akionesha tuzo yake ya The International Quality Summit Awards katika banda lake kwenye maonyelakeya 42 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba.

Mkurugenzi Mtendaji wa Grace Natural Products Dr Elizabeth Kalili akiwaonyesha bidhaa kwa wateja waliojitokeza katika banda lake lililopo ndani ya Jengo la Sabasaba Hall kwenye maonyelakeya 42 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba.

JAFO AWAAGIZA WATAALAM BAGAMOYO KUTUNZA VIFAA TIBA

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo amewaagiza wataalam wa sekta ya afya wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kutunza vifaa tiba vilivyotolewa kwa msaada kutoka Taasisi ya Dhi Nurein Foundation.

Taasisi hiyo imesaidia ujenzi wa jengo la dharula, wodi ya wazazi, pamoja na vifaa mbalimbali vya afya ambapo Mradi huo umegharimu zaidi ya Sh.Milioni 900. Hatua hiyo ya taasisi hiyo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya ya Bagamoyo na maeneo mengine hapa nchini. 

Akizungumza katika uzinduzi wa Mradi huo kwa niaba ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Jafo amesema taasisi hiyo inaungana na taasisi zingine hapa nchini zinazosaidia miradi mbalimbali na kuagiza vifaa hivyo kulindwa na kutunzwa bila kupoteza. 

Jafo amesema kuna baadhi ya watu wachache hapa nchini wasio waadilifu wamekuwa na tabia ya kuchukua vifaa vizuri vya hospitali na kuvihamishia katika hospitali zao binafsi. Wakati huo huo, Waziri Jafo amewapongeza sana Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, pamoja na Mbunge wa Bagamoyo Shukuru Kawambwa kwa kufanikisha upatikanaji wa mradi huo.

Pia Jafo amewaomba wananchi wajiunge katika mifuko mbalimbali ya bima ya afya ikiwemu CHF iliyo boreshwa ili waweze kupata huduma bora ya matibabu wao na familia zao.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akiongea na wananchi wa Bagamoyo
Dkt. Saleh kutoka nchini Saudia kutoka taasisi iliyofadhili mradi huo akitoa maelezo ya mradi kwa Waziri wa Tamisemi Mhe. Selemani Jafo.
Wananchi wa Bagamoyo wakiwa katika mkutano wa uzinduzi wa Mradi wa afya ya mama na mtoto katika hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja mjini Bagamoyo.

IGP AFUNGA MAFUNZO YA POLISI WANAMAJI

$
0
0


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na wanafunzi waliohitimu mafunzo katika Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza baada ya kuangalia Onesho lao la utayari katika ukanda wa Ziwa Viktoria Mwanza. (Picha na Jeshi la Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bi. Mary Tesha wakati wa ufungaji wa mafunzo ya Polisi Wanamaji yaliyokuwa yakiendeshwa katika Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza (Picha na Jeshi la Polisi) 

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akifuatilia kwa kutumia darubini mazoezi kwa vitendo katika Ziwa Viktoria Mwanza yaliyokuwa yakioneshwa na askari waliohitimu mafunzo katika Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza.Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bi. Mary Tesha. 

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akifanya mazoezi mafupi na askari wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Mwanza baada ya Askari hao kuonyesha zoezi lao la utayari wakati wa Ziara ya IGP mkoani humo (Picha na Jeshi la Polisi).
Askari Polisi wakionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kupitia kwa vitendo katika Ziwa Viktoria Mwanza wakati wa kufunga mafunzo yao katika Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza.

JITIHADA ZA UFUFUAJI NA UENDELEZAJI VIWANDA ZA ZAA MATUNDA MBEYA, WAKULIMA, WAWEKEZAJI WAPONGEZA

Rais Magufuli amteua Jenerali Mstaafu Mwamunyange kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA


Tanzania yasisitiza ushirikiano kutekeleza SDGs

$
0
0
SERIKALI ya Tanzania imeomba wadau wa maendeleo na taasisi mbalimbali zikiwemo za Umoja wa Mataifa kuendelea kufanyakazi nayo kuhakikisha kwamba ajenda ya kimataifa ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030 inaendelea kutekelezwa nchini.
Hayo yalisemwa katika kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa malengo hayo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dk Augustine Mahiga.
Aidha alisema serikali imetengeneza mikakati kadhaa ya kuwezesha kutekelezwa kwa malengo hayo ya dunia.
Alisema wakati Tanzania imekaza nia ya kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda suala linalosisitizwa katika SDG 9 ni muhimu na kwamba serikali ya Tanzania inataka kuendeleza ushirikiano huo ili malengo ya dunia yafikiwe pia nchini Tanzania.
Alisema Tanzania chini ya uongozi wa Rais John Magufuli inaendelea kutekeleza mpango wa maendeleo endelevu wa Umoja wa Mataifa (SDGs) wenye lengo la kufikia ustawi kwa kila mkazi wa dunia hii.
Ili kutekeleza malengo hayo, mpango wa maendeleo wa miaka mitano umeingiza malengo ya SDGs.
“Kama nchi tangu tumeanza kutekeleza SDG kwenye  mwaka 2016, tumechambua na kuingiza vipengele vya SDGs kwenye mipango mbalimbali ya kitaifa ikiwamo mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano 2016/17-2020/21 (FYDP II) na mpango wa tatu wa kukuza uchumi wa Zanzibar na kupunguza umaskini (MKUZA III)” alisema.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dk. Augustine Mahiga akitoa neno la ufunguzi wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango akizungumza kwenye kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Adolf Mkenda akitoa neno la ukaribisho wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa maelezo mafupi kuhusu mkutano wa mashauriano baina ya Serikali ya Tanzania na mashirika ya Umoja wa Mataifa wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Adolf Mkenda
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad akitoa maoni wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Hawa Ndilowe akizungumza wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akibadilishana mawazo na mmoja wa wadau wa maendeleo wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam
 Baadhi ya wadau wa maendeleo, viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na Waheshimiwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini walioshiriki kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam
Picha ya pamoja ya viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo kutoka mashirika mbalimbali na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MMILIKI WA KIWANDA ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI KWA TUHUMA ZA KUHUSIKA NA UCHOMAJI WA KIWANDA HICHO

$
0
0
 Na Linda  Shebby, Pwani


JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia mmiliki wa kiwanda cha kuchapisha nyaraka  mbalimbali kinachofahamika kwa jina la Yukos Enterprises  kilichopo katika eneo la Tondoroni Kata ya Kisarawe Mkoa wa Pwani  aliyetajwa kwa jina la Magora Magira Masegese kwa tuhuma za kukihujumu kiwanda hicho kwa kukichoma moto katika  majengo makubwa mawili  yenye mitambo  mbalimbali  yaliyopo katika kiwandani hapo.

Akizungumza leo katika mkutano na waandishi wa  habari  Kaimu Kamanda  wa Polisi  Mkoa wa Pwani SSP   Blasius Chatanda  amesema kuwa Jeshi la Polisi pia  linamshikilia  Meneja  wa Kiwanda hicho  Elia Elson  pamoja na  walinzi wawili  ambao ni Sai Kwilasa na Razi Kadilio kwa mahojiano zaidi na kuwa thamani ya mali  iliyoungua bado haijafahamika hadi hivi sasa.

"Baada  ya taarifa kutufikia tuliwasiliana na wenzetu  wa zimamoto  na kuweza  kufanikiwa  kufika  kwa wakati  na kuuzima moto  huo kabla  haujaenea  kwenye majengo mengine yaliyopo kwenye kiwanda hicho" alisema Kaimu Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Pwani SSP Chatanda.

Aidha Kalimu Kamand alisema kuwa  baada ya jeshi hilo kufanya ukaguzi  katika moja ya jengo  ambalo moto uliwahi kuzimwa , walikuta majaba matano  yaliyokuwa kwenye  kona  ya jengo hilo ndani  yake  kukiwa na  mafuta  aina ya petroli pamoja na karatasi  rola  lililokuwa limetandikwa  kwenye korido za jengo hilo  ambalo ndani  yake kulikuwa  na nyaraka  mbalimbali ambazo  zilikuwa  zimemwagiwa  mafuta  ya petroli lakini hazikuweza  kuungua.

Aidha  Mrakibu  Msaidizi   huyo wa Jeshi  la Zimamoto Mkoa wa Pwani Happines Shirima amesema  changamoto waliyokumbana nayo walipofika ni kutoka kwa mmiliki wa kiwanda hicho aliposhindwa kuwafungulia lango kuu kwa madai kuwa mtoto wake ndiye anayejua zilipofunguo gali iliyochangia wafikie uamuzi wa kuvunja mlango ili kuweza kuwaokoa  baadhi ya wafanyakazi ambao walikuwemo ndani ya kiwanda gicho wakati kikiwaka moto.

WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haina mpango wa kununua madeni yaliyosababishwa na mikopo ya kibenki kwenye vyama vikuu vya ushirika nchini.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.

“Serikali ya awamu ya tano hatuna biashara ya kununua madeni ya vyama vikuu, kulikuwa na tabia ya watu wa ushirika kukopa na hali ikiwa mbaya wanakimbilia Serikalini. Serikali hii hatuna biashara hiyo,” amesema.

Waziri Mkuu amesema anazo taarifa kwamba Chama Kikuu cha mkoa wa Kagera (KCU) kimekopa fedha Benki ili kiweze kulipa deni la mwaka 2014. “Nimeambiwa KCU wamekopa fedha benki ili kulipa deni la mwaka 2014, hii inaingia akilini kweli? Mnakopa fedha kulipa deni la zamani, ni kwa nini msiwatafute waliosababisha deni na kuwachukulia hatua?,” alihoji.

“Ninyi mlikuwa watu sita ambao mlikubaliana kama viongozi, mlienda kukopa kuzidi uwezo mlionao. Leo hii ni kwa nini serikali ije kulipa wakati mmetumia ninyi?,” aliuliza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya tatno inasisitiza masuala ya ushirika kwa sababu imeamua kuwahudumia wananchi kuanzia ngazi ya chini kuanzia pembejeo, dawa hadi masoko.

“Tunataka tuondoe utaratibu wa chama kikuu kukopa fedha benki ili kikanunue mazao. Vyama vingi vimetengeneza hasara, leo hii vyama vikuu vina madeni. Hii ni kwa sababu mlikopa fedha benki wakati hata hamjui mna kilo ngapi ambazo zimevunwa.
 Waziri Mkuu, Kassim  Majalawa akizungumza katika Maadhimisho ya siku ya ushirika dunianiyaliyofanyika kitaifa  kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
 Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba akizungumza wakati alipomkaribisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa  Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Ushirika nchini, Bibi Renata Mwageni (kushoto) Tuzo ya  Rais John Pombe Magufuli iliyotolewa na Wanaushirika nchini  ili kutambua mchango wa Rais  katika kuendeleza sekta ya ushirika na kuinua uchumi wa wananchi wa Tanzani ya 2018 . Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye  Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye  uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Juni 7, 2018.  Wapili kushotoi ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab  Telack.
 Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya  Siku ya Ushirika duniani  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mizani ya Kielektroniki ya kupima uzito wa pamba wakati alipotembelea banda la Chama Kikuu  cha Ushirika cha Nyanza katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa  Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na watatu kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwaanjelwa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitazama pamba iliyostawi vizuri wakati alipotembelea banda la Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza  baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.  Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama samaki waliokaushwa  wakati alipotembelea banda la Vyma vya Ushirika katika Soko la Kimataifa la Kirumba – Mwaloni wilayani Ilemela baada ya kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula ambaye pia ni Mbunge wa Ilemela .
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa TANESCO wakati alipotembelea banda lao katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa furahisha jijini Mwanza  Julai 7, 2018.  Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

IGP AFANYA ZIARA KATIKA VISIWA VYA ZIWA VIKTORIA

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na Wakazi wa kata za Kagongo, Nyasungu na Kiriba zilizopo Visiwani Ziwa Victoria Mkoani Mara wakati wa Ziara yake ya kuhakikisha wahalifu wanaovamia wavuvi na vitendo vya wizi wa mifugo vinakomeshwa katika maeneo hayo. (Picha na Jeshi la Polisi)
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na Diwani wa Kata ya Kiriba Msendo Nyamsora wakati wa ziara ya kikazi ya IGP katika Visiwa vilivyopo Mkoani Mara kwa lengo kuhakikisha wahalifu wanaovamia wavuvi na vitendo vya wizi wa mifugo vinakomeshwa katika maeneo hayo. 
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akiagana na Wakazi wa kata za Kagongo, Nyasungu na Kiriba zilizopo Visiwani Ziwa Victoria Mkoani Mara baad ya kuzungumza  nao wakati wa Ziara yake ya kuhakikisha wahalifu wanaovamia wavuvi na vitendo vya wizi wa mifugo vinakomeshwa katika maeneo hayo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akisalimiana na Wakazi wa kata za Kagongo, Nyasungu na Kiriba zilizopo Visiwani Ziwa Victoria Mkoani Mara baad ya kuzungumza  nao wakati wa Ziara yake ya kuhakikisha wahalifu wanaovamia wavuvi na vitendo vya wizi wa mifugo vinakomeshwa katika maeneo hayo. (Picha na Jeshi la Polisi)

MKUU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI AFANYA MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA WA MIKOA NA WAKUU WA VITENGO WA JESHI HILO

Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images