Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live

TOC FC MABINGWA WAPYA LIGI YA AWESO CUP 2018 PANGANI

$
0
0
TIMU ya TOC FC juzi walitawazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligi ya wilaya ya Pangani maarufu kama Aweso Cup baada ya kuifunga Ushirika FC mabao 4-3 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye viwanja vya Kumba wilayani Pangani.

TOC ambao ni mabingwa walikabidhiwa kombe la Ubingwa,Medali na kitita cha sh.milioni 1 kutoka kwa mdhamini wa mashindano hayo Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo (CCM).

Huku mshindi wa pili timu ya Ushirika FC walikabidhiwa kitita cha laki sita na medali wakati mshindi wa tatu akipata laki nne na medali kwenye tukio ambalo lilihudhuriwa na wageni mbalimbali akiwemo Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama na Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa.

Katika mchezo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkubwa kutokana na timu zote kushindwa kutambiana ndani ya dakika tisini na hivyo kuamuliwa kwa mikwaju ya penati ndipo TOC walipofanikiwa kuibuka videdea.
 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso kulia akimkabidhi kombe la Ubingwa wa Ligi ya wilaya ya Pangani maarufu kama Aweso Cup nahodha wa timu ya  TOC Bato Diasi  kushoto ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama  aliyevaa koti jeupe
 Nahodha wa timu ya  TOC Bato Diasi akiwa amelishikilia kombe lao kulia ni NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso
 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso kushoto akimvalisha medali mchezaji wa timu ya Ushirika FC ambao walishika nafasi ya pili kwenye mashindano ya Kombe la Aweso Cup kushoto ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama
 Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama kushoto akimkabidhi  sh.50000 Twaha Bungala ambaye ni mfungaji bora kwenye mashindano hayo
 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso katikati akimkabidhi kitita cha sh.milioni 1 nahodha wa timu ya TOC Bato Diasi juzi ambao niMabingwa wa Ligi ya wilaya hiyo maarufu kama Aweso Cup  iliyodhaminiwa na Mbunge huyo


TANZANIA YAWEKA MSIMAMO MKALI KWENYE ITIFAKI YA UTALII NA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI YA EAC

$
0
0
Na Hamza Temba-Arusha

Itifaki ya Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) imezua mjadala mzito na mabishano makali katika Mkutano wa Nane wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa jumuiya hiyo uliofanyika Jijini Arusha juzi.

Mvutano huo ulisababishwa na hoja iliyowasilishwa na Tanzania ambayo ilitaka kuboreshwa kwa kifungu cha nne cha itifaki hiyo ambacho kinazitaka nchi wanachama kutangaza eneo lote la jumuiya ya Afrika ya Mashariki kama kituo kimoja cha safari za utalii duniani.Tanzania ikiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, ilipinga vikali na hatimaye ikagoma kusaini itifaki hiyo ambayo imejadiliwa kwa zaidi ya miaka saba mpaka pale mapendekezo yake yalipoingizwa kwenye kifungu hicho.

Kifungu hicho kilikuwa kinasema, "Every Partner State shall market and promote the Community as a single tourist destination", (Kila nchi mwanachama itatangaza jumuiya kama kituo kimoja cha safari za utalii (duniani)).Tanzania ikapendekeza kwenye kifungu hicho uongezwe mstari unaosema, "while maintaining country identites" (huku kila nchi mwanachama ikibaki na utambulisho wake halisi).

Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia), Waziri wa Utalii, Wanyamapori na Mambo ya Kale wa Uganda, Ephraim Kamuntu (katikati) na wawakilishi wa Mawaziri wa Utalii wa Burundi, Kenya na Rwanda wakisaini Itifaki ya Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) katika ukumbi wa EAC Jijini Arusha. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia), Waziri wa Utalii, Wanyamapori na Mambo ya Kale wa Uganda, Ephraim Kamuntu (katikati) na wawakilishi wa Mawaziri wa Utalii wa Burundi, Kenya na Rwanda wakisaini Itifaki ya Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) katika ukumbi wa EAC Jijini Arusha. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwasilisha mapendekezo ya Tanzania kwenye kifungu cha nne cha Itifaki ya Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki katika Mkutano wa Nane wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo uliofanyika jijini Arusha. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki.
Baadhi ya wajumbe wa Tanzania walioshiriki mkutano huo.

MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWAPIGA MSASA ARU KUHUSU WAJIBU WA KUTOA TAARIFA KWA UMMA, PIA MASWALA YA ITIFAKI

$
0
0
MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Profesa Evaristo Liwa akizungumza machache wakati wa ufunguzi wa semina ya viongozi na wafanyakazi wa ARU iliyoendeshwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO pia Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbass (kushoto) na Mwanadilpomasia Lucas Jackson (hayupo pichani) chuoni hapo mwishoni mwa wiki. Katikati ni Naibu Makamu Mkuu wa chuo, Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi. Na Robert Okanda
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO pia Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbass akitoa mada ya kuhusu umuhimu wa taasisi za serikali kutoa taarifa kwa umma na kusisitiza kwa mujibu wa sheria zinapaswa kutoa taarifa wana habari ndani ya siku 21 toka zinapokuwa zimehitajika wakati wa semina hiyo iliyofanyika ARU Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO pia Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbass akitoa mada ya kuhusu umuhimu wa taasisi za serikali kutoa taarifa kwa umma na kusisitiza kwa mujibu wa sheria zinapaswa kutoa taarifa wana habari ndani ya siku 21 toka zinapokuwa zimehitajika wakati wa semina hiyo iliyofanyika ARU Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Profesa Evaristo Liwa (kushoto) na sehemu ya viongozi wa ARU wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO pia Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbass alipokuwa akiwasilisha mada. Kutokea (kushoto) ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Gabriel Kissenga, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi na Mwanadilpomasia kutoka Kituo cha Diplomasia Dar es Salaam, Lucas Jackson (kulia). 

NAIBU WAZIRI MAVUNDE ABARIKI SAFARI YA WAPANDAJI WA MLIMA KILIMANJARO KUTOKA GEITA GOLD MINING (GGM) KWA LENGO LA KUCHANGISHA FEDHA ZA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI.

$
0
0
ZAIDI ya Sh Bilioni 20 zimekusanywa kutoka kwa mashirika 40 yasiyo ya kiserikali pamoja na taasisi mbalimbali za serikali kwa ajili ya kusaidia katika kampeni za kupambana dhidi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi ambapo tayari Mamilioni ya watanzania wamekwisha nufaika nazo.

Fedha hizo zimekusanywa kampuni ya Kuchimba dhahabu ya Geita (GGM) kupitia changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro, ijulikanayo kama “Kili Challenge” tangu mwaka 2001 ilipoanzishwa ,mwaka huu ukiwa mwaka wa 17 ikishirikisha washiriki 70 watakao shiriki kupanda Mlima huku wengine wakizunguka mlima huo kwa kutumia Baiskeli .

Akizungumza wakati wa Hafla ya kuwaaga washiriki wa Programu ya Kili Challenge 20018 iliyofanyika katika lango la kupanda Mlima Kilimanjaro la Machame ,Makamu wa Rais wa GGM, Simon Shayo amesema Progaramu hiyo imepanua wigo wa kusaidia Taasisi zinazojikita kuhudumia wachimbaji wadogo wadogo pamoja na maeneo ya wavuvi ambako tafiti zinaonyesha wako kwenye mazingira hatarishi ya kuambukizwa VVU.

“Kila siku na kila mwaka ,tukio hili la hisani linaendelea kuwa na matokeo makubwa kwa jamii inayotuzunguka ,ninayo furaha leo kutagaza kwamba kupitia Kili Challenge tumeweza kuchangisha zaidi ya Bilioni 20 .”alisema Shayo.

Alisema fedha hizo zimekusanywa kutoka katika Mashirika 40 yasiyo ya kiserikali (N.G.O,S) pamoja na taasisi mbalimbali za serikali kupitia Tume ya taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo watanzania zaidi ya Milioni moja wamenufaika nayo.
 Mgeni Rasmi katika tukio hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavunde akikabidhi Bendera kwa washiriki wa changamoto hiyo kwa njia ya kuzunguka mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavundeakijaribu kuendesha Baiskeli kuashiria uzinduzi wa Changamoto ya kuzunguka Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baikeli.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavundeakishirikia zoezi la Kupanda Mlima Kilimanjaro kuashiria mwanzo wa safari ya wapandaji 40 wanashiriki zoezi hilo. 
 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamis Issah ni miongoni mwa washiriki walioanzisha safari hiyo. 

MWALIM COMMERCIAL BANK Plc YATANUA WIGO KWA KUZINDUA HUDUMA YA MWALIMU BANK WAKALA

$
0
0
BENKI ya Mwalimu Commercial Bank Plc (MCB) imetanua wigo wake kwa kuzindua huduma ya Mwalimu Bank Wakala itakayowawezesha Watanzania na wateja wa benki hiyo kupata huduma za benki hiyo kuwa karibu katika maeneo yao wanayoishi au kufanyia kazi.

Akizungumza katika uzinduzi wa Mwalimu Bank Wakala mkoani Tanga juzi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Mwalimu Mwalimu Commercial Bank Plc, Ronald Manongi amesema benki yake imeingia kwenye makubaliano ya kimkakati na Maxcom Africa Plc kupitia mawakala wa Maxmalipo.

Amefafanua lengo ni kuwawezesha wateja wa benki hiyo kuweza kunufaika na benki yao kwa kupata huduma kwa urahisi, haraka na unafuu."Benki yetu ina nia ya dhati ya kuhakikisha kuwa tunasogeza huduma zetu karibu zaidi na wananchi popote pale walipo. "Nia ni kuhakikisha kuwa mtanzania popote alipo aweze kupata huduma za kibenki ili kwa pamoja tuweze kukuza uchumi wa nchi yetu, "alisema.

Manongi amesema kuwa benki yao imehakikisha kuwa inaendelea kuwa bega kwa bega na wateja wake kupitia zaidi ya mawakala 10,000 wa Maxmalipo walioenea katika maeneo mbalimbali nchini. Ameongeza wateja wa Mwalimu benki watapata huduma mbalimbali kama kuweka fedha kwenye akaunti zao, kutoa fedha ikiwa ni pamoja na mishahara kwenye akaunti zao, kuangalia salio na taarifa fupi, malipo ya luku, maji na muda wa maongezi.

“Tumejipanga katika kutoa huduma bora kwa wateja wetu,hivyo kwenye kila huduma tunayoitoa, kwanza tunaangalia mteja wetu anataka nini, ndipo kupitia timu yetu tunabuni njia sahihi yenye ufanisi katika kukidhi mahitaji ya wateja wetu,amesema. Aidha ameongeza wana shauku ya kuona wateja wao wanafanikiwa na wanaamini wateja wakifanikiwa na benki pia itafanikiwa. “Tutaendeleakuja na ubunifu mbalimbali wa kiteknolojia ili kuzidi kurahisisha huduma kwa wateja wetu,"amesisitiza.

Uzinduzi wa Mwalimu Bank Wakala ulifanyika pamoja na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo.
   Mkuu wa Kitengo cha Mauzo wa kampuni ya Maxcom Afrika Plc,  Gasper Mrosso (kulia), akimuelekeza mmoja ya wanahisa wa Benki ya Mwalimu Commercial Bank Plc (MCB), ambaye pia ni Katibu wa Chama cha Walimu Handeni (CWT), Hamisi Ngomero  jinsi ya kutumia mashine maalum za POS ili kuweza kupata huduma mbalimbali za kibenki kupitia huduma ya MCB Wakala wakati wa uzinduzi wa rasmi wa MCB Wakala uliofanyika pamoja Mkutano Mkuu wa pili wa Wanahisa wa benki hiyo mjini Tanga mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia wa pili kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commecial Bank,   Ronald Manongi na Mkurugenzi Mtendaji wa Maxcom Afrika Charles Natai.
  Ofisa Mtendaji Mkuu wa  Mwalimu Commecial Bank Plc,  Ronald Manongi, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya MCB Wakala uliofanyika pamoja na Mkutano Mkuu wa pili was Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Tanga mwishoni mwa wiki. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mwalimu Commecial Benki  Ronald Manongi (kushoto) akishuhudia mteja wa benki hiyo ambae pia ni Katibu wa Chama cha Walimu Handeni (CWT), Hamisi Ngomero (wa pili kushoto), akipata hutuma kupitia MCB Wakala huduma iliyozinduliwa wakati wa Mkutano Mkuu wa pili wa Wanahisa wa benki hiyo mjini Tanga hivi karibuni. Wa tatu kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mauzo wa kampuni ya Maxcom Afrika Gasper Mrosso,  Mkurugenzi Mtendaji wa Maxcom Afrika Plc, Charles Natai na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Ubunifu wa Maxcom, Deogratius Lazari.  
  Baadhi ya wanahisa wa benki hiyo wakihudhuria Mkutano wao Mkuu wa pili wa Mwaka mjini Tanga hivi karibuni.

WANAMUZIKI WA INJILI WAWASHA MOTO IBADANI JIJINI DODOMA

$
0
0
Na Dotto Mwaibale, Dodoma.

WAIMBAJI wa Nyimbo za injili ambao ni wanachama wa Umoja wa Muziki Tanzania (TAMUFO), leo wameshiriki ibada ya Jumapili katika Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Anglikana Jijini Dodoma ambapo pia walipata fursa ya kutoa burudani ya nyimbo mbalimbali ikiwa ni njia ya kuhubiri na kulifanya kanisa hilo kuwaka moto wa furaha kutokana na burudani safi kutoka kwa watumishi hao wa mungu.

Wanamziki hao ambao wapo jijini Dodoma wamepokelewa na Kanisa hilo na kesho watatembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia umoja wao TAMUFO.Mbali ya kesho kwenda Bungeni leo jioni watashiriki katika tamasha kubwa la nyimbo za injili ambalo litaenda sanjari na uzinduzi wa Albam ya nyimbo ya injili ya Kwaya ya Safina ambayo ipo katika hilo Kuu la Anglikana Dodoma ambapo kwaya mbalimbali zitatoa burudani ya nyimbo za kuabudu.

Akizungumzia kuhusu wanamuziki hao Rais wa Umoja wa Muziki Tanzania (TAMUFO), Dk.Donald Kisanga, alisema wanayofuraha ya kufika Dodoma salama na kuwa leo hii watashiriki katika tamasha hilo na kesho asubuhi watakwenda kutembelea Bunge.Katibu wa TAMUFO, Stellah Joel, amesema makundi mbalimbali ya wanamuziki wanaounda umoja huo yatakuwepo kama vile, waimbaji wa nyimbo za injili, Dansi, Bongo Fleva, Muziki wa Asili na Taarabu.

"Wanamuzi wote kutoka katika makundi hayo tayari wamefika Dodoma na kuwa maandalizi yote yamekamilika.Amewataja baadhi ya wanamuziki hao kuwa ni Hamza Kalala, Mzee Makasy, Witness Mweupe, Emanuel Mbasha, Madamu Ruth Mwamfupe , Happyness Sanga kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na wengine.
Muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Jijini Dar es Salaam, Madamu Ruth Mwamfupe akiimba katika ibada hiyo huku akisindikizwa na waumini wa kanisa hilo. 
Waumini wakiwa ibadani.
Mwanamuziki Mzee Makasy ambaye hivi sasa ni mwimbaji wa nyimbo za injili baada ya kuokoka akitoa burudani.
Mwimbaji wa nyimbo za injili Emmanuel Mbasha kutoka Dar es Salaam, akiimba.
Viongozi wa dini wa kanisa hilo wakisalimiana na Emmanuel Mbasha ambaye ni muimbaji wa nyimbo za injili.



NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI ATAKA WANAO HUJUMU SHIRIKA LA RELI WACHUKULIWE HATUA

$
0
0
Na EmanuelMadafa,Mbeya

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye amewaagiza askari polisi kitengo cha reli kuwakamata watu wanaotuhumiwa kupiga mawe treni pindi zinapopita kwenye maeneo yao na kuhasababisha uharibifu ambao huigharimu serikali pesa nyingi katika matengenezo vingine watawajibishwa wao

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, alipotembelea Karakana ya Tazara iliyopo Jijini Mbeya.Amesema wapo baadhi ya watanzania wamekuwa wakiendelea na vitendo vya kuhujumu treni hivyo lazima wachukuliwe hatua kali ili kukomesha vitendo hivyo kwa kuhakikisha zinatolewa adhabu kali kwa watako bainika kufanya vitendo hivyo.

Waziri Nditiye amewataka madereva wa treni kusimamisha treni endapo itatokea kuna baadhiya watu wamefanya tukio la kupiga mawe treni mara iwapo safarini ili wahusika wakamatwe na kuhojiwa ili watoe sababu za kufanya kitendo hicho sanjali na kuchukuliwa hatua mara moja.

Wakati huo Naibu Waziri , amewahakikishia wafanyabiashara na wachuuzi kuwa hatua ya uimarishaji wa usafiri na usafirishaji kupitia Reli nchini,uko pazuri na tayari muda wa kuondoa mizigo mizito inayotumia malori umefika.Amesema katika kuimarisha usafiri huo, zaidi ya shilingi bilioni 10 zimetolewa na serikali kuboresha vichwa vya magari moshi na karakana mbalimbali nchini.

Amesema serikali haitegemei kuona malori ya kiendelea kusafirisha mizigo mizito ambapo wakati mwingine yamekuwa chanzo cha kuharibu miundombinu ya barabara pamoja na kuua soko la Tazara.“Barabara hizi zimejengwa kwa gharama kubwa sana, tunategemea mizigo hiyo kuanza kusafirishwa kwa kutumia njia ya reli na kwamba ni jukumu la wafanyakazi kuanza kuwashawishi wateja wao wa zamani na wapya ili wafanye kazi na Tazara,”amesema.

Hata hivyo amesema ,serikali haiwezi kuendelea kuwalipia mishahara lazima itafika pahala ambapo itasitisha na kuiacha Tazara iendelee na majuku yake kwa kujiendesha yenyewe, hivyo wanapaswa kujipanga kwa kuwa wabunifu.
Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kulia akisikiliza maelezo kutoka kwa Boniface Phiri ambaye ni Mhandisi uzalishaji kiwanda cha kuzalisha mataaluma ya Reli kwa kutumia zege kinachomilika na Tazara kilichopo katika Kijiji cha Mswiswi Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya. 
Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kulia akipokea ufafanuzi kutoka kwa Boniface Phili Mhandisi uzalishaji kiwanda cha kuzalisha mataaluma ya Reli kwa kutumia zege kinachomilikiwa na Reli ya Tazara kilichopo katika Kijiji cha Mswiswi Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya
Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kulia akisikiliza maelezo namna ya utengenezaji wa mataaluma ya reli kwa kutumia zege kutoka Mhandisi Boniface Phili Mhandisi uzalishaji kiwanda cha kuzalisha mataaluma ya Reli kwa kutumia zege kinachomilikiwa na Tazara kilichopo katika Kijiji cha Mswiswi Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya
Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye pili kushoto akisikiliza maelezo kutoka kwa mafundi ya karakana ya Reli ya Tazara iliyopo katika kituo cha Iyunga Jijini Mbeya

PANAMA YACHEZEA KICHAPO CHA MABAO 6-1 KUTOKA KWA ENGLAND, SENEGAL NA JAPANA ZATOKA SARE 2-2

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MICHUANO ya Kombe la Dunia imeendelea tena leo nchini Urusi huku Timu ya Taifa England ikiishushia kichapo Timu ya Taifa ya Panama mabao 6-1 huku Senegela na Japan wakitoka sare ya 2-2.

Kwa upande wa ushindi ambao England wameupata tayari wamejihakikishia kuingia hatua ya pili wakati Panama sasa kwa matokeo hayo wanalazimika kuondoka kwenye michuano hiyo.

Mechi kati ya England na Panama kwa sehemu kubwa ilitawaliwa na akili nyingi za kisoka na hasa kwa wachezaji wa England walionesha kuutawala mchezo huo.Pasi maridadi na zenye uhakika ambazo zilikuwa zinapigwa na wachezaji wa England zilisababisha Panama kupoteza muelekeo na mvua ya magoli ikaanza.

Mabao matatu ya England yamefungwa na mshambuliaji Harry Kane aliyekuwa nyota wa mchezo huo.Wafungaji wengine ni John Stones ambaye yeye alipachika mabao mawili na mshambuliaji Jesse Lingard akitupia goli moja.Hata hivyo Panama ambao licha ya kufungwa mabao hayo mashabiki wake walionekana wenye furaha na wanaoshangilia bila kuchoka na ilipofika dakika ya 78 ya mchezo timu yao ikapata bao moja lililofungwa na Felipe Baloy.

Hadi dakika 90 za mchezo zinamalizika England wameibuka na ushindi huo mnono.Kwa matokeo hayo England wanashika nafasi ya kwanza kwa kuwa na alama sita na Ubelgiji inashika nafasi ya pili kwa alama sita na tofauti iliyopo ni idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.


SENEGAL , JAPAN WATOA SARE YA 2-2

Mchezo mwingine kwenye michuano hiyo ni kati ya Senegal na Japan ambapo hadi dakika 90 zinamalizika timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2.
Mechi kati ya Senegal na Japan zilikuwa zinasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soko hasa wa Bara la Afrika kutokana na kuipa nafasi Senegal kutokana na ushindi walioupata kwenye mchezo wao wa kwanza.

Ushindi wa Senegal katika mchezo wa kwanza uliibua shangwe kwa mashabiki wa soko wa Afrika wakiamini huenda ikafika mbali.Katika mchezo wa leo Senegal ilikuwa ya kwanza kupata bao kwani katika dakika ya 11 mshambuliaji wake Sadio Mane aliandika bao la kuongoza.

Hata hivyo mpira huo ulikuwa na kasi na ushindani wa hali ya juu kutokana na kila timu kuonesha umahiri hasa katika kusakata kabumbu ambapo nguvu, akili, mbinu za mchezo na pasi zilisababisha mechi kuwa na mvuto wa aina yake.Dakika ya 34 ya mchezo Japan wakasawazisha kupitia kwa mchezaji wake Takashi Inui.Kasi ya mpira iliendelea na ilipofika dakika ya 71 Mshambuliaji wa Senegal Moussa Wague akaipatia timu yake bao la pili.

Bao la pili la Senegal lilidumu kwa dakika nane tu kwani ilipofika dakika ya 78 Japan wakapata bao la kusawazisha baada ya mchezaji wake Keisuke Honda kupata bao.Hivyo hadi mpira unamalizika mabao yalikuwa 2-2.

Dawa za kulevya kilo 38 zaangamizwa

$
0
0
Na Miza Kona, Maelezo-Zanzibar 

Kamati ya Kuangamiza Dawa za kulevya Zanzibar, imeangamiza kilo 38 za mihadarati aina heroini na vidonge vya valium ambazo zilikamatwa kuanzia mwaka 2010.

Zoezi la kuangamiza dawa hizo limefanyika leo katika jaa la Kibele, Wilayaya Kati.Kabla ya hatua ya kuzingamiza, dawa hizo zilikuwa zikitumika kama vielelezo vya ushahidi katika mahakama na vituo vya polisi kisiwani Unguja, ambapo sasa kesi zake zimemalizika na kutolewa hukumu.

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kuangamiza dawa za kulevya ambae pia ni Mfamasia Mkuu wa Serikali Habibu Ali Sharif, amesema zoezi hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa na hakuna athari yoyote iliyotokea wakati lilipotekelezwa.Aidha amesema, kamati yake inaendelea kuangalia uwezekano wa kuangamiza dawa kama hizo hapo baadae katika sehemu zilikopatikana badala ya kuzipeleka kwenye jaa la Kibele.

Alisema hatua hiyo inalenga kudhibiti uingizaji na utumiaji, pamoja na kupunguza gharama za usafirishaji.Sharif aliitaka jamii kubadilika na vijana kuacha tabia ya kuiga mambo yasiyokuwa na tija, na badala yake wafuate maadili ya asili ya nchi yao ili waweze kuwa raia wema wa kulijenga taifa.Aidha amewahimiza wazee umuhimu wa kukaa na watoto wao na kuwapa mafunzo kuhusiana na mwenendo sahihi wa kuishi bila kujiingiza kwenye vitendo na biashara haramu za dawa za kulevya.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Abdalla Hassan Mitawi, amesema serikali imekuwa ikichukua hatua za kuwasaka, kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria watu wanaoingiza, kusambaza na kuuza dawa hizo hatari ili kukinusuru kizazi cha sasa na baadae.

Aidha amefahamisha kuwa, baada ya zoezi hilo, serikali itatoa taarifa juu ya utekelezaji wake, ikilenga kubaini kama kuna watendaji wanaofanya udanganyifu katika utendaji ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya Bi. Kheriyangu Mgeni Khamis, amesema zoezi hilo ni la pili kufanyika ambapo mwezi uliopita kamati iliangamiza dawa za kulevya aina ya bangi.

Zoezi la uangamizaji dawa za kulevya linakwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya kupambana na dawa za kulevya duniani inayofikia kilele Juni 26, 2018.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO-ZANZIBAR.

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAZUNGUMZIA MIKAKATI YA SERIKALI KUANDAA MAZINGIRA MAZURI YA UFUGAJI KUKU

$
0
0
Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

NAIBU Waziri wa Mfugo na Uvuvi atembelea shamba la AKM Glitters Company Ltd lililopo Dar es salaam eneo la Mbopo na Mbezi Beach, ambapo lengo la ziara yake ni kuangalia fursa walizonazo Watanzania katika ufugaji.

Akiwa katika ziara yake katika kampuni hiyo Naibu Waziri ulega ameona kazi mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ikiwemo ya shamba la kuku wazazi, sehemu ya kutotoleshea vifaranga na chakula cha kuku wazazi.Ulega amesema ufugaji wa kuku ni fursa kubwa  ambayo ikiitumia vizuri, mhusika anaweza kuongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja, na taifa zima kwa ujumla wake.

" Serikali lengo letu ni kuhakikisha nyama ya kuku isiwe kitoweo kwa watu wa juu tu, bali kiwe kwa hali zote kuanzia ngazi ya watu wa kipato cha chini na kati."Tunataka watu wote wajiingize kwenye ufugaji wa kuku, ili tuweze kujitosheleza wenyewe na tutoe ajira nyingi kwa watu ili kuendeleza tasnia hii ya kuku na kuuza kuku kwa bei ya chini kuliko kutegemea kuku kutoka nje,"amesema.

Amefafanua katika bajeti  ya serikali kwa mwaka huu wamependekeza pendekezo ambalo limeletwa Wizara ya Fedha na Mipango, kwamba riba imeondolewa kwa asilimia 5 kutoka kwa wakina mama na vijana."Sasa haitakuwa ni hiari kwa Halmashauri bali ni sheria kuwa Halmashauri zote kadri ya mapato yao ya ndani yanavyopatikana yatakwenda moja kwa moja kwa vijana na akina mama kwa asilima 5 kila mmoja," ameongeza.Amesema Serikali imeona hivyo, ili kusaidia hasa wakina mama walio wengi na kufuta riba hiyo.

Kwa upande wake Mkurugezi Mtendaji wa kampuni hiyo Elizabeth Swai alizungumzia suala la usafirishaji vifaranga ikiwa ni changamoto kuwafikia wakazi wa vijijini ambapo Naibu Waziri alisema, Serikali imejiweka katika mazingira mazuri katika hili kuhakikisha usafirishwaji unawafikia pia watu waliopo vijijini.
 Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiangalia kuku wa wazazi katika shamba la (AKM) lililopo Mbopo jijini Dar as Salaam.(picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wafanyakazi wa shamba la kuku wazazi,kituo cha kutotolea vifaranga mbopo jijini Dar as Salaam.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa shamba hilo.

Uzinduzi wa huduma bandari ya Mwanza Kusini hadi Portbell Uganda

CCM YENDESHA MAFUNZO YA KIMKAKATI ZANZIBAR

WASHINDI 10 WA PROMOSHENI YA BIA YA KILIMANJARO WAONDOKA DAR KWENDA URUSI KOMBE LA DUNIA 2018

$
0
0
 Bia rasmi ya Tanzania katika msimu huu wa kombe la dunia ya Kilimanjaro Lager,ya kampuni ya TBL,imefanikisha ndoto za watanzania 10,ambao wamejishindia safari ya kugharamiwa safari ya kwenda nchini Urusi kuona baadhi ya mechi za michuano hiyo mikubwa ya soka ya FIFA Duniani kupitia promosheni yake ya Kombe la Dunia iliyozinduliwa rasmi nchini Mei 12,2018. 
 Washindi hao 10 ambao wameondoka jijini Dar es Salaam kwa ndege ya Shirika la Emirates kuelekea Russia,wamepatikana kwa kushiriki katika promosheni hiyo ambapo zilifanyika droo mbalimbali chini ya usimamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini (Tanzania Gaming Board). 
 Akiongea katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,wakati wa kuwaaga washindi hao,Meneja Masoko na Udhamini wa TBL,George Kavishe,alisema kuwa anayo furaha kuona bia ya Kilimanjaro ya TBL inafanikisha safari ya baadhi ya watanzania kuona mashindano ya Kombe la Dunia mubashara kutoka viwanjani nchini Urusi. 
 Kavishe alisema kuwa washindi hao wataweza kuangalia mechi mbalimbali zitakazochezwa katika kipindi watakachokuwa nchini humo kabla ya kurejea nyumbani mnamo Juni 30,2014 
 “Lengo kubwa la promosheni hii ni kuwazawadia wateja wetu ili waburudike katika msimu huu wa shamrashamra za kombe la dunia la FIFA 2018 na promosheni inaendelea pia kwa wateja kujishindia fedha taslimu shilingi milioni moja kwa wiki kwa wiki kumi,na muda wa maongezi wa simu wa shilingi 2,500/- kila wanaponunua bia ya Kilimanjaro na kushiriki mara (sita) 6 kutuma namba iliyopo chini ya kizibo kwenda 15451 fedha taslimu kiasi cha shilingi 1,000,000/- Kila wiki kwa wiki Kumi. 
 Akiongea kwa niaba ya washindi wenzake,Charles John kutoka mkoani Geita,alisema kuwa wanayo furaha kuona safari yao inatimia ya kwenda kushuhudia mechi za kombe la dunia mubashara viwanjani nchini Urusi na alishukuru bia ya Kilimanjaro kupitia promosheni yake kwa kufanikisha safari hiyo. 
 Alisema kuwa anaamini kupitia safari hiyo mbali na kupata burudani ya soko pia wataitangaza Tanzania bila kusahau kujifunza mambo mengi ambayo walikuwa hawajakutana nayo kabla “Safari hii inaleta furaha na kuleta kumbukumbu ambazo si rahisi kuzisahau maishani”.Alisema John Kwa furaha.
 Meneja wa Masoko na Udhamini wa TBL Group George Kavishe akiongea na waandishi wa habari   wakati wa kusindikiza washindi wanaokwenda Urusi kupitia promosheni ya bia ya Kilimanjaro,katika uwanja wa ndege wa JK.Nyerere.
 Ujumbe wa washindi wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kwenda Urusi.
Ujumbe wa baadhi ya washindi ukiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es salaam tayari kwa safari ya kwenda Urusi kupitia promosheni ya bia ya Kilimanjaro na Kombe la Dunia. Huku wengine waendelea kujishindia mamilioni ya fedha taslimu 


VOA Swahili: Ronaldo Vs Messi, Russia 2018

Utafiti wa miaka 6 wa uwezeshaji kiuchumi kama sehemu ya uzazi wa mpango wakamilika

$
0
0
Na Mwandishi wetu
TAASISI ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shule ya Uchumi ya Norway (NHH) umekamilisha utafiti uliochukua miaka sita uliopelemba kama uwezeshaji wasichana kiuchumi ndio njia ya kuwezesha uzazi wa mpango.
Matokeo ya utafiti huo ‘Girls’ Economic Empowerment: The Best Contraceptive?’ umeelezwa kuja kusaidia kuelewa uzazi kwa wasichana na athari ya hali hiyo katika maamuzi yao ya kiuchumi.
Utafiti huo uliofanywa kuanzia mwaka 2013 hadi 2018, ulifanywa kufuatia programu iliyotengenezwa na Femina Hip, taasisi inayojishughulisha na kubadili tabia za vijana kwa kutumia mawasiliano.
Katika programu hiyo wasichana wa sekondari walipewa mafunzo ya ziada nje ya utaratibu wao yaliyochanganywa na elimu ya afya ya uzazi, uwezeshaji kiuchumi na elimu ya maisha.
Ubalozi wa Norway jijini Dar es salaam ulifadhili sehemu ya programu hiyo.
 Maarifa yaliyopatikana kutokana na utafiti huo yanatarajiwa kuwasaidia watengeneza sera, wanazuoni na  watu wa asasi zisizo za kiserikali kutambua athari za kuwezesha au kutowezesha wasichana kiuchumi katika uzazi.
Lengo kuu la utafiti huo ni kuwa na uelewa mpana utakaowezesha uundaji wa sera stahiki kuhusu uchumi na uzazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF Dk Tausi Kida alisema kwamba amejisikia furaha sana kufanyakazi na  Shule ya Uchumi ya Norway, ubalozi wa Norway na Femina katika kutafuta suluhu kwa matatizo yanayokabili taifa.
Alisema kwamba tabia, maarifa, ujuzi na maamuzi kwa vijana kuhusu afya yao ya uzazi kuna athari kubwa kwa maendeleo na afya kwa ujumla.
Imeelezwa kuwa wakati wa kuanza kwa utafiti huo, kundi la utafiti lilionesha kwamba hali ya kimaskini waliyokuwa wanakabiliana nayo iliwafanya wajihusishe na ngono.
Utafiti ulibaini kwamba kuwasaidia wasichana kabla ya ndoa kunawapa fursa zaidi za kukua kiuchumi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kwa wadau na wageni waalikwa wakati wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi msaidizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Wanawake Jinsia Watoto na Wazee (jinsia), Bi. Mboni Mgaza akisoma hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad akizungumza jambo wakati wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Vyombo vya habari wa Femina Hip, Amabilis Batamula akielezea jinsi Femina Hip kupitia program hiyo ilivyoweza kufikia wasichana wakati wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Profesa kutoka Shule ya Uchumi ya Norway (NHH),  Kjetil Bjorvatn akiwasilisha matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Kutoka kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez,  Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida pamoja na Mkurugenzi msaidizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Wanawake Jinsia Watoto na Wazee (jinsia), Bi. Mboni Mgaza wakimsikiliza Mshehereshaji wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Shemu ya washiriki kutoka taasisi mbalimbali wakishiriki kuchangia maoni wakati wa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida akifurahi jambo katika picha ya kumbukumbu na baadhi ya wageni waalikwa mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti wa uwezeshaji wasichana kiuchumi kama njia ya uzazi wa mpango uliofanyika mwishoni mwa wiki ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MAREHEMU AMINA CHIFUPA MIAKA 11 BAADAYE

$
0
0

"Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na mume wake Mohamed Mpakanjia zinasema kwamba Mhe. Amina  Chifupa- Mpakanjia ambaye alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam amefariki dunia  majira ya saa tatu kasorobo - Juni 26, 2007...."

Hiyo ndiyo habari kuu iliyotawala vyombo vyote vya habari nchini na kuitikisa Tanzania na Watanzania ambao wengi walishindwa kuamini masikio na macho yao wakati TV, Magazeti, Redio na mitandao vilipokuwa vikitangaza  habari hiyo ya kusikitisha na kustua.

Amina Chifupa, ambaye alikuwa  mtangazaji maarufu sana wa kituo cha Clouds 88.5FM, hasa kwa vipindi vyake vya "Chei Chei Shangazi" na "Aftrika Bambaataa", aliingia bungeni baada ya kushinda nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM. 

Katika kipindi chake cha kifupi cha takriban miaka miwili  Bungeni, Marehemu alijizolea umaarufu mkubwa sana kwa  hoja zake nzito sio tu za  kutetea maslahi ya vijana na kukemea rushwa, bali pia kwa kuamua 'kumshika nyati mapembe'  kwa kupambana na janga la madawa ya kulevya kwa nguvu zake zote. Hadi sasa hajatokea  tena mbunge aliye shupavu kama yeye wa aliyekemea na kusema kwa sauti janga hilo la Taifa.

 Kwa bahati mbaya Amina Chifupa aliaga dunia  siku ya kilele cha Maadhimisho ya Kupambana na Madawa ya Kulevya Duniani, Juni 26. Hivyo ndio kusema kwamba, wakati Tanzania inaadhimisha siku hiyo Jumanne  huko mkoani Iringa, Wananchi pia watakuwa wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 12 ya kifo cha Amina Chifupa wa Mpakanjia. Unaweza ukaiita  AMINA CHIFUPA DAY.

Marehemu Amina alizaliwa Mei 20, 1981 jijini Dar es Salaam, alisoma Shule ya Msingi Ushindi, Mikocheni, Dar (1988-1994) kabla ya kujiunga na masomo ya sekondari ya kidato cha kwanza hadi cha nne katika Shule ya Wasichana ya Kisutu, Dar (1995-1998). Elimu ya Juu ya Sekondari alisoma katika shule ya Makongo (1999-2001) kabla ya kujiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari cha Royal (2001-2003) ambako alifuzu Diploma ya Uandishi wa Habari.
Mwaka 1999 alianza kazi ya utangazaji wa kituo cha redio cha Clouds FM cha jijini Dar na aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Mama Shughuli.  
Katika siasa alikuwa kada wa CCM, Kamanda wa CCM wa Umoja wa Vijana katika tawi la Mikocheni A jijini Dar, Katibu wa Kamati ya Uchumi ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa Dar, Mama Mlezi wa UVCCM na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) matawi ya Bunju na Mbagala.
Mwaka 2005 aliteuliwa kuwa mbunge akiwakilisha kundi la vijana kupitia CCM ambako alidumu na cheo hicho kwa muda mfupi  hadi mauti yalipomkuta Juni 26, 2007.
Amina Chifupa alizikwa Juni 28, 2007 kijijini Lupembe Wilayani Njombe mkoa wa Iringa (sasa ni mkoa a Njombe) karibu kabisa na eneo alilokuwa akiishi bibi yake. Mazishi yake yalihudhuriwa na watu wengi maarufu wakiiongozwa na aliyekuwa Spika wa Bunge wa wakati huo Samwel Sita, ambaye pia ni marehemu.
Miaka mitatu baadaye, aliyekuwa mume wa  marehemu Amina Chifupa, Mohamed 'Medi' Mpakanjia, naye alifariki  dunia. Wawili hao walijaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Abdulrahman anayejulikana zaidi kama Rahman.
Baba mzazi wa marehemu Amina Chifupa, Mzee Hamisi Chifupa aalifariki  dunia usiku wa kuamkia Mei 27, 2017  nyumbani kwa mwanaye wa kike, Upanga, jijini Dar es Salaam.
Amina Chifupa daima atakumbukwa kwa kujitolea kupambana na matajiri wanaofadhili au kujihusisha na uingizaji wa dawa za kulevya nchini. Alikuwa mbunge mdogo zaidi katika historia ya chombo hicho cha  kutunga sheria na kupitisha bajeti ya nchi yetu.
Alisimama kidete na kutamka bayana angewaweka hadharani vigogo wote wanaojihusisha na madawa ya kulevya, pia alienda mbali zaidi kwa kutamka hata kama angekuwa mume wake anahusika naye angemtaja. Alikuwa jasiri kiasi hata  alifikia uamuzi wa kuwasilisha majina ya vigogo waliokuwa wakifanya biashara hiyo ya “unga” makao makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam.
Aliamua kujitoa mhanga kutetea kizazi cha vijana kinachoteketea kwa kutumia madawa ya kulevya ilihali waoingiza wanazidi kuwa matajiri tishio na baadhi yao wana nguvu ya ushawishi katika nyanja mbalimbali serikalini.
Alikuwa ni hazina kwa taifa na mfano kwa vijana wenye umri mdogo kama wake kwamba inawezekana kujitoa pasipo woga kulitetea taifa na kuwaweka wazi wote wanaotumia utajiri wao, vyeo vyao kufanya au kuwezesha uhalifu hususani katika suala zima la madawa ya kulevya. 
Lakini maskini ya Mungu ndoto yake hiyo na nyinginezo zilikatizwa ghafla na mauti saa tatu za usiku wa Juni 26, 2007 siku ya Jumanne katika hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam.
Mola aiweka mahali pema peponi roho ya marehemu Amina Chifupa wa Mpakanjia. WOTE NA TUSEME.... AMINA!

Kusoma yote tuliyoandika kumhusu Amina Chifupa

Senior Government Officials from Six African Countries to participate in the Negotiation Skills Training in Zanzibar

$
0
0

25 June, 2018
Zanzibar – The Chief Secretary of the Revolutionary Government of Zanzibar, Dr. Abdulhamid Yahya Mzee will officiate a six-day regional negotiation skills training for 35 senior Government officials from Tanzania, Uganda, Ghana, Namibia, Rwanda and Nigeria today.
The training, which will run from the 25th– 30th June, 2018, is organised by UONGOZI Institute in collaboration with the International Senior Lawyers Project (ISLP), a US based NGO specialising on legal issues. According to a statement released by UONGOZI Institute, the training aims to enhance negotiation capacities and competencies of African senior government officials in oil and natural gas commercial contracts.
“This particular training targets senior officials from Ministries responsible for Finance, Environment, Energy and Minerals; and the Attorney General’s offices,” said Prof. Joseph Semboja, Chief Executive Officer of UONGOZI Institute.
He added, “We believe that if key personnel involved in the negotiation of oil and natural gas contracts are equipped with the necessary skills and techniques, they will be able to secure lucrative deals for the benefit of their countries.”
Participants will gain an in-depth overview of oil and natural gas regimes including; key issues to consider while negotiating oil and natural gas commercial contracts, joint ventures of oil and natural gas and agreements that govern them, and unique challenges faced by African nations in negotiating high-stake investment deals. The training is part of a series of workshops organised by UONGOZI Institute with the aim of enhancing capacity of senior government officials in negotiating natural resource commercial contracts and other high-stake investment deals.  
About UONGOZI Institute: UONGOZI Institute is an independent government agency that provides services to senior leaders who have a demonstrable impact upon their society’s development as well as individuals who have been recognised as emerging leaders with the potential to make a positive impact in their societies.
UONGOZI Institute                            
62 Msasani Road, Oyster Bay,
P.O. Box 105753,                              
 Dar es Salaam, Tanzania          

TBL kuiona Liverpool live EPL baada ya kutwaa kombe la Standard Chartered 2018

$
0
0
Na Mwandishi wetu
Timu ya soka ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imetwaa kombe la benki ya Standard Chartered baada ya kuitandika kwa mikwaju ya penalti  2-1 timu ya Mwananchi Communications Limited .
Kwa ushindi huo, timu ya TBL sasa itakuwa na ziara ya siku 3 nchini Uingereza na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa ya Standard Chartered yaliyopangwa kufanyika kwenye uwanja wa Anfield, Septemba mwaka huu.
Aidha timu hiyo ya TBL wakifika Anfield wataona mechi ya msimu mpya wa EPL mubashara na kuzungumza na magwiji na kupata nafasi ya kunolewa nao.
Katika michuano hiyo Mchezaji wa Mwananchi, Saidi Seif alifunga mabao manane na kuwa mfungaji bora.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na gwiji la timu ya Liverpool, Sami Hyypia walishuhudia mechi hiyo na kutoa zawadi kwa washindi.
Akizungumza mara baada ya mashindano hayo kumalizika, Dk Mwakyembe aliipongeza timu ya TBL kwa kutwaa ubingwa na kuishukuru benki ya Standard Chartered kwa kutoa mchango wake kukuza sekta ya michezo.
“Naipongeza benki ya Standard Chartered kwa kuendesha mashindano haya na kuleta hamasa katika soka, nimefarijika sana na nimeshuhudia vipaji vingi, soka ina wigo mpana na ninaamini tunaweza kufanya vyema katika mashindano mbalimbali kwa kutumia vipaji vyetu,” alisema Dk Mwakyembe.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani alisema kuwa benki yao ni wadau wakubwa wa maendeleo ya michezo nchini na katika sekta nyingine na kuahidi kuendelea kufanya hivyo kwa maendeleo ya taifa.
 Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani kwa pamoja wakikabidhi kombe kwa kapteni wa kampuni ya TBL mara baada ya kutwaa ubingwa wakombe la benki ya Standard Chartered baada ya kuitandika kwa mikwaju ya penalti  2-1 timu ya Mwananchi Communications Limited katika mashindano yaliyofanyika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Mabingwa wa mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered kampuni ya Bia ya TBL wakishangilia mara baada ya kukabidhiwa kombe hilo wakati mashindano hayo yalipofikia tamati mwishoni wa wiki katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (kulia) akimpongeza Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia (wa pili kushoto) kwa kuja nchini kushuhudia mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi (kushoto).
 Kapteni wa timu ya kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Majuto Omary (katikati) akimtambulisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (kushoto) kwa kikosi cha timu hiyo wakati wa fainali kati ya TBL na MCL katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Kapteni wa timu ya kampuni ya TBL akimtambulisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe kwa kikosi hicho baada ya kutinga fainali za mashindano ya kombe la Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani akisalimiana na kikosi cha timu ya TBL kabla ya kukipiga kwenye fainali za mashindano ya kombe la Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia akisalimiana na kikosi cha timu ya kampuni ya TBL kabla ya kuanza mchezo wa fainali na timu ya Mwananchi Communications Limited wakati wa mashindano ya kombe la Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia, Mkurugenzi wa Ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi pamoja na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani katika picha ya pamoja na timu zilizotinga fainali mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Wachezaji wa timu ya TBL (kijani) na Mwananchi Communications Limites (nyeupe) wakimenyana katika fainali za mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Wadau kutoka makampuni mbalimbali wakitazama mechi ya timu zilizoingia fainali kwenye mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 25, 2018

TASWIRA MBALIMBALI ZA WASHABIKI KATIKA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA NCHINI URUSI

$
0
0
 Mwanalibeneke wa Globu ya Jamii na Mtaa kwa Mtaa, Othmna Michuzi akiwa pamoja na baadhi ya mashabiki wa timu ya Mexico na Urusi, wakati wakiwa kwenye treni kuelekea kwenye uwanja wa Spartak, uliopo nje kidogo ya mji wa Moscow, nchini Urusi kunakofanyika michuano ya Kombe la Dunia. 
 Mshabiki wa timu ya Taifa ya Tunisia akiwa nje ya uwanja huo wakati alipofika kuishangilia timu yake ilipokuwa ikikipiga na timu ya Taifa ya Ubelgiji. japo walichezea kichapo cha bao 5-2 lakini shangwe zake zilikuwa hazielezeki.
 Furaha ya ushindi kwa mashabiki wa timu ya Ubelgiji.
 Uwanja huu siku hiyo ulichukua idadi ya washabiki kama inavyosomeka kwenye ule ubao.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI.
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live




Latest Images