Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110158 articles
Browse latest View live

SERIKALI YAAGIZA WAMACHINGA WATENGEWE MAENEO YA KUFANYIA BIASHARA

$
0
0
Na Angela Msimbira,

Wakuu wa Wilaya wameagizwa kuzisimamia halmashauri nchini kuhakikisha kuwa zinatenga maeneo maalum ya kufanyia biashara ndogondogo (machinga) ili  waweze kuendesha shughuli zao bila kuvunja sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na serikali. 

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemeni Jafo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania – SHIUMA uliofanyika leo katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Dodoma, Jijini Dodoma.

Alisema Wakuu wa Wilaya wana wajibu wa kuratibu na kuhakikisha kuwa maeneo ya kufanyia bishara kwa wamachinga yanatengwa na Halmashauri ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa utaratibu bila kuvunja sheria za nchi. 

Aliongeza kuwa wamachinga ni watu muhimu katika kukuza uchumi wa Tanzania kwa kuwa wafanyabiashara wadogo ndio wanaoleta muunganiko wa watu katika kada mbalimbali wakiwemo wasomi wenye shahada, astashaada, kidato cha sita, kidato cha nne, darasa la saba na wasiosoma kabisa wote huunganika na kufanyabiashara kama wamachinga.

Alisema kati ya watanzania milioni 50, walioajiriwa serikalini na sekta ya umma ni 520,000, hivyo kundi kubwa ni la watu ambao ama wamejiajiri au wameajiriwa katika sekta binafsi. 

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo akiongea na wamachinga wakati  wa kufungua  Mkutano Mkuu wa Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania- SHIUMA leo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Dodoma, Jijini Dodoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo akiongea na wamachinga wakati  wa kufungua  Mkutano Mkuu wa Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania- SHIUMA leo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Dodoma, Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo  akiongea na baadhi ya viongozi wa shirika la umoja wa wamachinga Tanzania – SHIUMA leo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Dodoma, Jijini Dodoma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MISS TEEN HERITAGE INTERNATIONAL 2016 AWAKABIDHI BASATA CHETI CHA SHUKRANI

$
0
0
Na Angess Francis, Globu ya jamii

BARAZA la Sanaa Tanzania (BASATA)limesema kuendele kutoa ushirikiano kwa wasanii wa nyanja mbali mbali hapa nchini ili wafikie mafanikio yao.

Ambapo leo BASATA jijini Dar es Salaam limepokea zawadi ya shukurani kutoka kwa Miss Teen Heritage international 2016 Cesilya Godfrey ambaye ameambatana na uwongozi wake wa kampuni ya See The African Link.

Mrembo huyo amekabidhi Cheti cha kuonyesha fadhila kwa kile alichosaidiwa.Mashindano hayo yalifanyika nchini Sri Lanka na kuwashirikisha washirki 15 wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 18 kutoka nchi mbalimbali duniani.Akizungumza leo akiwa BASATA ,Mrembo huyo amesema alishika nafasi ya pili huku nafasi ya kwanza ikienda kwa raia kutoka Zimbabwe.

Amesema kuwa BASATA ndio waliofanikishia yeye kushiriki kwa kumpa vibali vya kutafuta Wadhamini wa kumpeleka katika mashindano hayo."Niliona matangazo kwenye mitandao kuwa wanatafutwa washiriki wa kushindania Taji hilo,nikavutiwa ndio nikaandika maombi nikakubaliwa,baada ya hapo nikaanza mchakato wa kutafuta wadhamini huku nikisaidiwa na BASATA"amesema.

Mkurugenzi wa BASATA Godfrey Mngereza amesema walikuwa wako bega kwa bega na mrimbwende huyo tangu mwanzo kwa kuanza na kumtambulisha kwa wadhamini ili kufanikisha ndoto zake."Hii ni kuonesha pia Baraza lipo karibu sana na wasanii wa sanaa mbalimbali pamoja na wadau katika kuunga mkono na kutia sapoti kazi zao ili kufanikisha ndoto zao".Amesema Mngereza.

Pia Mngereza amempongeza Cecilya kwa kufanikiwa kupeperusha bendera ya nchi kimataifa kwa kufanya vizuri na kunyakua nafasi ya pili.Wakati huo huo Meneja wake Zuberi Mohamed 'Niva' ambaye ni msanii wa Bongo Muvi amesema imekuwa ni faraja kwa nchi kwa mrembo huyo kutangaza utaifa wetu katika nchi zingine mbalimbali.
Mkurungenzi mkuu Baraza la Sanaa Taifa Godfrey Mngereza akipokea Zawadi ya cheti cha shukurani leo ofisini kwake (BASATA) Jijini Dar es Salaam kutoka kwa uongozi mzima wa Kampuni ya See The African Link,ambao ndio kwa sasa unamsimamia kazi za Miss Teen Heritage International 2016 Cecilya Godfrey.

Picha ya Pamoja Mkurugenzi mkuu Baraza la Sanaa Taifa Godfrey Mngereza wa pili kushoto,Meneja wa Miss Teen Heritage international 2016 Zuberi Mohamed (NOVA) kushoto,Miss Tee Heritage International Cecilya Godfrey wa pili kutoka kilia, Meneja wa see the African Link Irene Mitema wa kulia.

DAILY NEWS DIGITAL: Mipaka ya Jeshi na Vijiji vya Kauzeni na Luhungo kuangaliwa

MABINGWA WA NGUMI ZA RIDHAA WAMTEMBELEA MEYA WAO UBUNGO

$
0
0
Na Emmanuel Masaka ,Globu ya jamii

MEYA wa  Ubungo Boniface Jacob ametembelewa na Mabingwa ngumi za ridhaa ambao wameshinda mataji mbalimbali ya ubingwa pamoja na Medali sita katika Shindano la Mchezo wa Ngumi kwa Mkoa wa Dar es Salaam
yaliyofanyika Uwanja wa Taifa .


Mabondia walioshinda Medali hizo ni Shomari Pendeza kilo 49,Khamisi Maya kilo 69,Mustafa Khalidi kilo 52,Prospa John kilo 60,Frank Lucian kilo 56 na Alex Mshamba kilo 56.

Hivyo imeelezwa leo na Meya Jacob kuwa mabondia wameiletea Manispaa ya Ubungo medali za Dhahabu 1,Shaba 2 na Fedha 3 na hiyo ni  heshima kubwa  kwa niaba ya vijana wote katika Manispaa ya Ubungo.

Katika neno la Shukrani Meya Jacob amejitolea kuwa Mlezi wa kambi yao ya Shirikisho la Ngumi kwa Wilaya ya Ubungo zilizopo Kimara.

Pia ameahidi kuwatafutia udhamini wa mchezo huo wa ngumi ambapo pia  amewaeleza kuwapatia pair za Gloves,boxing pad,Punching Bags,Clip bandage,Head protectors,na Boxing gears zingine.
Meya wa ubungo Boniface Jacob akiangalia medali za Dhahabu alizoshinda mabondia Mabingwa wa ngumi za ridhaa, ambapo amejitolea kuwa mlezi wa kambi ya Shirikisho la ngumi wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es Salaam. 
Meya wa ubungo,Boniface Jacob (wapili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mabondia wa ngumi za ridhaa.

SERIKALI KUPITIA WIZARA YA UJENZI,UCHUKUZI NA MAWASILIANO YAOMBWA KUJENGA BARABARA YA BAGAMOYO,MAKURUNGE HADI SAADAN

$
0
0
Afisa Utalii Hifadhi ya Taifa ya Saadan Athuman Mbae akizungumza na waandishi wa habari AFISA Utalii Hifadhi ya Taifa ya Saadan Athuman Mbae ameiomba Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano kuijenga barabara ya Bagamoyo,Makurunge hadi kuingia Hifadhini ili kuondoa kero kwa watalii hasa nyakati za mvua.

Hayo ameyazungumza kwenye maonyesho ya sita ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga na kusema ubovu wa barabara hiyo umekuwa kikwazo kwa wageni wengi.

Mbae alisema Hifadhi hiyo imekuwa ikipokea wageni wengi kutokea Jijini Dar es salaam na nje ya nchi kupitia barabara hiyo huku miundombinu hiyo ikiwa haiwezi kupitika kwa nyakati zote."Wageni wetu wamekuwa wakitumia barabara hiyo kufika katika hifadhi yetu na tuna idadi kubwa ya wageni hofu yetu ubovu wa barabara unaweza kukwamisha wageni na labda kupungua"Alisema Mbae.

Aidha alisema uwepo wa miundombinu mizuri utarahisisha kwa wananchi toka Mikoa ya Tanga,Dar na Pwani kutembelea katika hifadhi hiyo na kujionea vivutio vilivyopo kwa siku moja.Alisema ipo haja kwa Serikali kuelekeza nguvu kwenye ujenzi wa barabara hiyo ili kuirahisishia hifadhi hiyo kupokea wageni wengi kwa nyakati zote na kuongeza pato la Taifa.

Hata hivyo alisema Hifadhi hiyo imeweka mfumo wa matumizi ya master card visa card katika maswala ya ulipaji wa gharama za ulipaji ili kudhibiti mapato yaingiayo kama aerikali inavyoagiza."Tunamfumo wa kieletronics kwenye maswala yetu ya malipo na hii itatusaidia kupunguza vitendo vya kihalifu kwa wageni wetu kutokana kutokutembea na fedha nyingi"Alisema Mbae (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

DC HAPI AENDELEA NA ZIARA YAKE WILAYA YA KINONDONI

RAS SHINYANGA AFUNGUA MAFUNZO KWA KAMATI YA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela amefungua mafunzo kwa wajumbe wa kamati ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoa wa Shinyanga yanayolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kupiga vita ukatili katika jamii.

Mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza leo Jumatano Mei 30,2018 yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga yamekutanisha wadau mbalimbali wanaohusika katika kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la Investing in Children and their Societies (ICS – Africa). 

Awali akizungumza,Afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Glory Mbia alisema lengo la mafunzo hayo ni kupata maoni na mapendekezo mbalimbali katika kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. “Lengo la mafunzo haya ni kupata uelewa wa pamoja na kutengeneza mkakati namna gani tunafanya katika kutokomeza vitendo vya kikatili katika mkoa”,alisema Mbia. 

Akifungua mafunzo hayo, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo alisema mkoa wa Shinyanga bado una tatizo kubwa la ukatili dhidi ya watoto na wanawake hivyo zinahitajika nguvu za pamoja 

“Tunamshukuru mwenyezi Mungu mauaji dhidi ya albino yamebaki historia katika mkoa wetu,lakini katika jamii kumekuwa na unyanyasaji hasa wa watoto,kupitia kamati hii naamini kwa pamoja kama tutaamua kwenda pamoja hatua kwa hatua tutaweza kutokomeza vitendo vya ukatili katika mkoa huu”,alieleza Msovela. “Akina mama na watoto wengi wameathirika kisaikolojia,kimwili,wapo watoto wamekosa elimu kutokana na unyanyasaji wanaopitia kwa pamoja naamini sheria ambazo zipo na umoja huu tutaweza kukabiliana na ukatili wanaofanyiwa wanawake na watoto”,alisema. 
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akifungua mafunzo ya kujengea uwezo kwa wajumbe wa kamati ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoa wa Shinyanga leo Mei 30,2018 - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akifungua mafunzo na kuwataka wajumbe wa kamati hiyo kushirikiana katika kupiga vita vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Shinyanga.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Glory Mbia akielezea malengo ya mafunzo hayo ambapo alisema lengoni kupata maoni na mapendekezo mbalimbali kuhusu namna ya kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Shinyanga. 

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 30/05/2018


KIJANA ALIYEMWOKOA MTOTO APATA DILI MALI, AONEKANA JESHI LA ZIMA MOTO UFARANSA AKIPATA MAFUNZO

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

RAIS  wa Mali Ibrahim Boubacar Keita amempongeza kijana Mamoudou Gassama (22) aliyemwokoa mtoto aliyenusurika kuanguka kutoka ghorofani na kumtaka arejee nchini Mali kwani ameandaliwa kazi ya jeshi.

Akizungumza na vyombo vya habari balozi wa Mali nchini Ufaransa ametoa pongezi kwa kijana huyo kutoka kwa Rais wa Mali na kumtaka arejee nchini kuendelea na kazi ya jeshi aliyoandaliwa.

Aidha Mamoudou ameonekana akiwa na maafisa wa jeshi la zima moto la nchini Ufaransa akipata  mafunzo na kufanya baadhi ya shughuli katika kikosi hicho.


Ikumbukwe kuwa mapema jumamosi wiki iliyopita kijana raia wa Mali Mamoudou Gassam (22)  alifanya kitendo cha kishujaa cha kumuokoa mtoto mdogo ambaye alitaka kudondoka kutoka jengo la ghorofa ya nne, na baadaye kukutana na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron na kupatiwa zawadi nono, ikiwemo hati ya uraia wa nchini Ufaransa na nafasi ya kazi katika jeshi la zimamoto.

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AZINDUA WIKI YA MAZIWA NCHINI,AAHIDI KUINUA SEKTA HIYO.

$
0
0


Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(wa pili kulia) akikata utepe kuzindua Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na viongozi wa Baraza la Kilimo nchini na Bodi ya Maziwa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina akitoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro jijini Arusha.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina akiwapa wanafunzi wa Shule ya Msingi Baraa ya jijini Arusha baada ya kuzindua Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo.
Meneja wa kampuni ya Milkcom maafuru Dar Fresh,Tunnu Mssika akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi wakati akikagua mabanda ya waoneshaji bidhaa mbalimbali zinazotokana na mifugo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(katikati) akipewa maelezo na Mjasiriamali wa kampuni ya Mpilika Leather kutoka Dodoma,Anna Malongo ,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo .
Wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kitaifa mkoa wa Arusha wakifatilia kwa makini hotuba za viongozi.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(kushoto) akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Baraza la Wakulima nchini(ACT),Dk Sinare Sinare(kulia)kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,wa pili kulia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Maziwa,Lucas Malunde. Imeandaliwa na www.rweyeamuinfo.blogspot.com

MNYETI AAGIZA MANYARA IKAMILISHE VIWANDA 100

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti ameziagiza Halmashauri za Wilaya za Mkoa huo kuhakikisha zinatekeleza agizo la uanzishwaji wa viwanda 100 na hadi mwezi Septemba mwaka huu viwe vimekamilika. 

Mnyeti akizungumza na watumishi na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati, alisema kila halmashauri ya mkoa huo wenye halmashauri saba, inapaswa iwe na viwanda 15. Mnyeti alisema serikali ilitoa agizo la kila mkoa uanzishe viwanda 100 hivyo na mkoa wa Manyara nao unapaswa kuhakikisha unatekeleza agizo hilo kwa kila halmashauri kuwa na viwanda 15. 

Alisema agizo hilo linatakiwa kutekelezwa kwa kila sekta ikiwemo kilimo na mifugo ambazo ndizo shughuli kuu za kiuchumi kwa wananchi wengi wa mkoa huo. “Watumishi wa umma wanapaswa kutambua kila taaluma waliyoisomea wanapaswa kuwekeza kwenye fikra ya viwanda kwa kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa sekta hiyo,” alisema Mnyeti. 

Aliwapongeza mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Raymond Mushi na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Hamis Malinga kwa kutekeleza agizo hilo la uanzishwaji wa viwanda vipya. “Kwenye miezi mitatu iliyopita Halmashauri ya Babati mlikuwa mmeshafanikisha uanzishwaji wa viwanda nane na hadi kufikia mwezi Septemba mtakuwa mmekamilisha viwanda 15 hongereni sana,” alisema Mnyeti. Mkuu wa wilaya ya Babati, mhandisi Raymond Mushi alisema wananchi wa eneo hilo ni wachapakazi wazuri na hujishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji, uvuvi, ujasiriamali na nyinginezo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati, wakiwemo maofisa tarafa, madiwani, watendaji wa kata, vijiji, walimu na wenyeviti wa vijiji, juu ya kufanya kazi kwa uadilifu na kutumikia jamii, kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo mhandisi Raymond Mushi.
Mkuu wa Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, Mhandisi Raymond Mushi akizungumza na wananchi wa Kata ya Madunga juu ya kufanya kazi na kuwahusia kuwa siku mbili ambazo mtu hawezi kufanya chochote ni jana na kesho hivyo waitumie siku ya leo kwa kutimiza wajibu wao, kulia ni Mkuu wa Mkoa huo Alexander Mnyeti na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Nicodemus Tarmo.
Mkuu wa Wilaya ya Babati Vijijini Mkoani Manyara, Vrajilal Jituson, akizungumza na wananchi wa Kata ya Madunga ambao wanachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo yao ikiwemo suala la elimu.
Mbunge wa viti maalum wa mkoa wa Manyara, Esta Mahawe akizungumza na wananchi wa Kata ya Madunga ambapo alijitoa mashuka 10 kwa ajili ya wagonjwa watakaotumia kwenye zahanati ya kijiji hicho iliyozinduliwa na Mkuu wa mkoa huo Alexander Mnyeti.

SPIKA NDUGAI AWAFARIJI WAFIWA NA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO MSIBA WA MAREHEMU KASUKU BILAGO.

$
0
0
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki waliofika nyumbani kwa marehemu kasuku Bilago Wilayani kakonko Mkoani Kigoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akitoa heshima za mwisho nyumbani kwa marehemu Kasuku Bilago Wilayani kakonko Mkoani Kigoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akiwasabai watoto wa marahemu, Kasuku Bilago Wilayani kakonko Mkoani Kigoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto)akimfariji Mke wa marehemu Ndg. Pietha Bisangwa Bilago leo Wilayani kakonko Mkoani Kigoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiteta jambo na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe (kulia) katika msiba wa marehemu, Kasuku Bilago Wilayani kakonko Mkoani Kigoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE

INTRODUCING "SIELEWI" BY JOSSIAN WAWENCY

MICHUZI TV: TWENZETU RUSSIA 2018 - UCHAMBUZI WA KUNDI A & B

TAARIFA KWA UMMA: uteuzi wa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita kutoka shule zote za Tanzania Bara mwaka 2018 kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa Sheria.

$
0
0


  Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limefanya uteuzi wa wanafunzi waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kutoka shule zote za Tanzania Bara kwa mwaka 2018, kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa Sheria.
Sanjari na uteuzi huo, JKT limewapangia Makambi ya JKT watakayokwenda kupatiwa mafunzo kwa muda wa miezi mitatu na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 01-10 June 2018. 
Wahitimu hao, wamepangiwa katika Kambi za JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu – Pwani, JKT Makutupora – Dodoma, JKT Mafinga – Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba – Tanga, JKT Makuyuni – Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa, Nachingwea- Lindi na JKT Mtabila – Kigoma.
 Aidha, wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (physical disabilities) wanatakiwa kuripoti kambi ya Ruvu JKT iliyopo mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia wa jamii hiyo. 
Vijana watakaochaguliwa watatakiwa kujigharamia nauli za kwenda na kurudi kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa wakiwa na vifaa vifuatavyo:
 Bukta ya rangi ya Dark blue yenye mpira kiunoni (lastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini isiyo na zipu. Aidha bukta za wanawake zinatakiwa kuwa na lastic magotini.
  1. Raba za michezo zenye rangi ya kijani.
  2. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari.
  3. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
  4. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangwa kwenye mikoa yenye baridi.
  5. Track Suit ya rangi ya kijana au bluu 
Mkuu wa JKT anawakaribisha vijana wote walioteuliwa ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujifunza Uzalendo, Umoja wa Kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na Utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa letu. 
Orodha kamili ya majina ya vijana na makambi ya JKT waliyopangiwa vinapatikana kwenye tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.go.tz

MWANZA YAJIUNGA NA LIGI YA MIJI INAYOPATA HUDUMA YA USAFIRI KIDIJITALI

$
0
0

Mwanza, ‘The Rock City’ kama inavyofahamika kwa wengi nchini Tanzania, leo imeingia kwenye ligi ya miji ya kisasa duniani baada ya kuingia rasmi kwa huduma ya usafiri kidijitali jijini humo. 

Mwanza, Taxify, ambayo ni miongoni mwa Kampuni kubwa zinazotoa huduma ya usafiri kidijitali barani Ulaya na Afrika imezindua rasmi huduma zake jijini Mwanza huku mamia ya madereva wakiwa tayari wamesajiliwa kwa ajili ya kutoa huduma katika maeneo yote ya jiji.

Katika kusherekea uzinduzi wa huduma hiyo, Taxify inatoa punguzo la asilimia 50 kwa abiria kuanzia tarehe 28 Mei, 2018 mpaka mwisho wa mwezi wa sita mwaka huu. Gharama za usafiri kwa kipindi hiki ni:- Kuanza safari ni TZS 700, Kwa kilometa ni TZS 460, Kwa dakika ni TZS 70 huku gharama ya chini kabisa ya safari ikiwa ni TZS 2,000.

“Mwanza ni jiji lenye watu zaidi ya milioni 3.5, barabara nzuri zenye ubora, Huduma bora ya mitandao inayopatikana kirahisi na maelfu ya magari. Tulifanikiwa kupokea maombi mengi kutoka kwa wakazi wa jiji hili waliokuwa na shauku ya kutumia huduma yetu lakini huduma yetu ilikuwa bado haijafika jijini hapa, jambo hili limetusukuma kuzindua rasmi huduma yetu leo jijini hapa. 

Mamia ya madereva wameshasajiliwa kwenye jukwaa letu na tayari tumeshaona mamia ya safari ambazo zimefanyika hata kabla ya uzinduzi rasmi. Mwanza ipo tayari kwa huduma ya usafiri kwa njia ya mtandao na tunaimani kuwa huduma hii itafanya vizuri katika jiji la ‘Rock City’ alisema Remmy Eseka, Mkuu wa Operesheni, Taxify Tanzania.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Ms. Mary Tesha ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya Taxify iliyozinduliwa hivi karibuni jijini humo. Jiji la Mwanza sasa limeingia kwenye ligi ya miji ya kisasa duniani baada ya kuingia rasmi kwa Kampuni ya Taxify inayotoa huduma ya usafiri kidijitali.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taxify, Kanda ya Afrika Mashariki, Shivachi Muleji (kushoto) akikabidhi fulana kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Ms. Mary Tesha ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya Taxify iliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza. Jiji hilo sasa limeingia kwenye ligi ya miji ya kisasa duniani baada ya kuingia rasmi kwa Kampuni ya Taxify inayotoa huduma ya usafiri kidijitali.
Meneja Uendeshaji wa Taxify nchini Tanzania, Remmy Eseka akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya Taxify hivi karibuni jijini Mwanza. Jiji hilo limeingia kwenye ligi ya miji ya kisasa duniani baada ya kuingia rasmi kwa Taxify, Kampuni inayotoa huduma ya usafiri kidijitali.
Meneja wa Taxify Kanda ya Ziwa, Milumbilwa Kipimo akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hafla ya uzinduzi ya huduma ya Taxify hivi karibuni jijini Mwanza. Jiji hilo limeingia kwenye ligi ya miji ya kisasa duniani baada ya kuingia rasmi kwa Taxify, Kampuni inayotoa huduma ya usafiri kidijitali.
Msanii wa muziki wa hiphop, Fareed Kubanda a.k.a Fid Q akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma ya Taxify iliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza. 

Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wafikiatamati

$
0
0
Mhe. Mhandisi Stella Manyanya Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji akifuatilia Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji la Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea.

Mkutano huu ulilenga kujadili na kutolea ufumbuzi masuala mbalimbali yakiwemo ya kiforodha, ambayo yamekuwa kikwazo katika ufanyaji wa biashara za kuvuka mipaka katika Jumuiya.Mkutano huu uliofanyika kuanzia tarehe 25 hadi 30 Mei, 2018 na kuhudhuriwa na nchi zote wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifikia tamati tarehe 30 Mei, 2018 jijini Arusha.
Prof. Adolf Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akizungumza kwenye Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji uliofanyika jijini Arusha.
Kutoka kushoto ni Mhe. Dkt. Pindi Chana Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Prof. Adolf Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (Mb) Naibu Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji, na Bw. Benard Haule Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji, na Sekta za Uzalishaji wakifuatilia mkutano 
Maza Kuu ikiongoza Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji uliokuwa ukiendelea jijini Arusha 
Prof. Adolf Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto) akisaini taarifa ya Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara,Viwanda,Fedha na Uwekezaji. Kushoto Bw. Eliah Chilangazi Afisa Biashara kutoka Wizara ya Biashara, Viwanda, na Biashara 
Prof. Adolf Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto), Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (Mb) Naibu Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji (Katikati), na Bw. Benard Haule Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji, na Sekta za Uzalishaji (kulia) wakishauriana jambo 
Prof. Adolf Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mhe. Dkt. Pindi Chana Balozi wa Tanzania nchini Kenya wakifuatilia mkutano 
Waheshimiwa Mawaziri, Mabalozi na Watendaji wa Serikali wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano 

KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO,MHANDISI AISHA AMOUR AONGOZA WAJUMBE WA KAMATI YA MAAFA KUTEMBELEA BWAWA LA NYUMBA YA MUNGU

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro,Mhandisi Aisha Amour akiwa ameongozana na wajumbe wengine wa Kamati ya Maafa kutembelea Bwawa la Nyumba ya Mungu lililopo wilayani Mwanga ambalo linatajwa ujazo wake wa maji wa kawaida umepitiliza na kusababisha Mafuriko kwa wakazi waishio kando ya Bonde la Mto Pangani.
 Mhandisi ,Aisha Amour akitizama kina cha Maji katika Bwawa la Nyumba ya Mungu kilichofikia Mita za ujazo 689.88 . 
 Sehemu ya Bwawa la Nyumba ya Mungu. 
 Baadhi ya wakazi wa vijiji vya jirani na Bwawa la Nyumba ya Mungu wakitumia usafiri wa Mitumbwi kusafiri kutoka upande mmoja kwenda upande wa Pili. 

 Sehemu ya Mapitio ya Maji baada ya kujaa katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ,maji haya yanaelekea katika maeneo ambayo yapo makazi na mashamba ya watu yaliyopo pembezoni mwa Bonde la Mto ,Pangani. 

WALIOKAIDI KUHAMA KWENYE MAENEO YENYE MAFURIKO SAME SASA KUKAMATWA

$
0
0

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.


SERIKALI imetoa siku mbili kwa wananchi waliosalia katika Vijiji vya Ruvu Mferejini na Ruvu Marwa wilayani Same ,Mkoani Kilimanjaro vilivyozingirwa na maji kuondoka mara moja na kwamba watakao kaidi wataondolewa kwa kutumia nguvu na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Zaidi ya watu wapatao 2000 wamelazimika kuyahama makazi yao baada ya kufikwa mafuriko kutokana na mvua kubwa za masika zinazoendelea kunyesha huku eneo lililoathirika zaidi na mvua hizo ni ukanda wa tambarare wa wilaya ya Same unaopakana na Bwawa la Nyumba ya Mungu.

Licha ya Idadi hiyo ya watu kuyahama makazi yao lakini bado wapo waliokaidi kuondokana na hapa Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Same ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Wilaya hiyo ,Rosemerry Senyamule ,ikatoa agizo.

Serikali imetenga maeneo kando ya milima iliyopo katika kitongoji cha Mferejini kwa ajili ya Kambi za Muda kwa watu waliokosa Makazi ,Clouds Habari imefika katika Kambi hizo na kujionea maisha mapya ya wahanga wa mafuriko huku misaada ya kibinadamu ikihitajika zaidi .
Licha ya kukosekana kwa baadhi ya huduma katika eneo hili bado wananchi hawa wanahitaji msaada wa hali na mali ili angalau kuweza kunusuru Maisha yao kutokana na Baridi kali ,Mbu na hata wanyama wakali wakiwemo Nyoka.

Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi ,Aisha Amour ni miongoni mwa baadhi ya viongozi waliowatembelea wahanga wa mafuriko kwa ajili ya kutoa pole . 

Mafuriko katika vijiji hivi yanatajwa kuwa hutokea kila baada ya Miaka 10 na kwamba mara ya mwisho yalitokea mwaka 2008 huku chanzo kikitajwa kuwa ni kujaa kwa Bwawa la Nyumba ya Mungu ambapo ujazo ulifikia Mita za ujazo 689.88 ambazo kwa sasa zimeanza kupungua hadi kufikia mita za ujazo 689.80 baada ya maji kuanza kuelekea kwenye maeneo ya makazi kwa kupitia mto Pangani.

Wananchi Jamii ya Massai pia ni miongoni mwa waathirika wa Mafuriko hayo. 

MAONESHO YA TAASISI ZA KITAFITI

Viewing all 110158 articles
Browse latest View live




Latest Images