Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
Mwasisi wa Twist - Chubby Checker akionesha inavyochezwa

Article 7

$
0
0

  



Registration is NOW open for CISA and CISM Review Class for the forthcoming CISA exam on 14th December, 2013. Our Reviews are due to begin on Monday 2nd September, 2013 to Thursday 17th October, 2013 (Monday to Friday) for weekday courses, and Saturday 2nd November 2013 – Sunday 8th December 2013 for weekend classes. Both the weekday and the weekend options will be for a total duration of 75 hours.
The review classes focus exclusively on the essential areas covered in the CISA or CISM exam. A series of sample exam questions that provide participants with a "feel" of the format and the types of questions encountered on the exam.


Our trainers are qualified Professionals with technical experience, skills and knowledge of specific domain(s). Participants will gain an overall understanding of the relevant CISA/ CISM Examination DOMAINS.


Study Materials

Our Courses utilize official ISACA presentations and study materials provided by ISACA. We will inform you about recommended materials upon your enrolment.

Fees- 1,000,000 Tshs.  per Participant


For more details about the course and online registration visit our website www.isaca.or.tz or contact - info@isaca.or.tz


 WARNING:

Any training institution offering review has to be approved by ISACA  before it begins to offer review classes.

USAILI WA KUTAFUTA MODELS WATAKAOSHIRIKI KWENYE ALLY REHMTULLAH 2014 COLLECTION FASHION SHOW WAFANYIKA JIJINI DAR.

$
0
0
DSC_0037
Meza kuu ya Majaji walioshiriki katika Usaili ya kutafuta Models watakaoshiriki kwenye Ally Rehmtullah 2014 Collection Fashion show kutoka kushoto ni Meneja Mkuu wa Alliance Autos, wakala wa Volkswagen nchini, Alfred Minja, Ally Hassan, Mrembo na mwigizaji maarufu nchini Wema Sepetu, Mwandaaji wa Onyesho hilo ambaye pia ni Mbunifu wa Mavazi nchini Ally Rehmtullah, Mwanamitindo Jamillah Nyangasa, Sarah Raqey.
Mbunifu wa mitindo maarufu hapa nchini Ally Rehmtullah amefanya maandalizi ya awali ya fashion show yake itayofanyika Agosti 30,  mwaka huu katika Hoteli ya Serena ambapo zaidi ya wanamitindo 30 wasichana na wavulana watashiriki katika maonyesho hayo kabambe.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi kwenye mahojiano maalum Rehmtullah amesema kwenye onyesho la mwaka huu wasichana watashiriki 20 na wavulana 10 ambao watavaa mavazi mbalimbali yaliotengezwa na kubuniwa na Rehmtullah mwenyewe kwa kuzingatia mila na desturi za Kiafrika.
Katika mchujo huo majaji watano watashiriki kuchagua warembo wenye mvuto, kujiamini na wenye kuwa na muonekano mzuri kwenye jukwaa ili kuwavutia wageni waalikwa ambao watakuwa ni wabunge, mawaziri na viongozi mbalimbali.
Rehmtullah alilisitiza mwaka huu kwamba onyesho la mitindo ya mavazi yatafana baada ya kudhamini wa makampuni kadhaa makubwa hapa nchini.
DSC_0050 
Pichani juu na chini ni Models wa kike wakipita mbele ya majaji wakati wa Audition ya kutafuta washiriki watakaonyesha mavazi kwenye Onyesho la Mavazi la Ally Rehmtullah 2014 Collection.
DSC_0049
DSC_0053
DSC_0082
Pichani juu na chini ni Models wa kiume wakipita mbele ya majaji kwa ajili ya kuchaguliwa kushiriki kwenye Ally Rehmtullah 2014 Collection Fashion Show.
DSC_0080
DSC_0069
DSC_0071

NMB emerge the best Bank in Tanzania

TIMU YA POLISI YAFIKA SALAMA KATIKA JIJI LA WINDHOEK NCHINI NAMIBIA

$
0
0
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi,Windhoek Namibia.

Hatimaye timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo ya Nane ya Umoja wa wakuu wa majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO) nchini Namibia imefika salama na imeanza mazoezi mepesi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza jumatatu tarehe 19 mwezi Agosti mwaka huu.

Timu hiyo ambayo ni tishio katika michezo hiyo kutokana na historia yake ya ushindi katika mashindano yaliyotangulia imekuwa kivutio kila inapopita huku kila mmoja akitaka kusalimiana nayo.

Timu hiyo inaundwa na wanamichezo 67 ambao wanacheza Mpira wa miguu wanaume, Mpira wa pete Wanawake, Riadha wanaumwe na wanawake na mchezo wa Vishale (Dats).

Michezo hiyo itashirikisha Nchi kumi na nne (14) katika michezo mbalimbali na lengo la michezo hiyo ni kujenga ushirikiano wa Majeshi ya Polisi kwa nchi wanachama wa SARPCCO katika kukabiliana na uhalifu.
timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo ya Nane ya Umoja wa wakuu wa majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO) nchini Namibia,wakipiga jalamba wakati wa kujiandaa na mashindano hayo.
Timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo nchini Namibia ikiwa kwenye picha ya pamoja na Baadhi ya Wenyeji wao.

TANAPA YAFUNGA RASMI AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA UJANGILI KWA UHARAKA KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA RUAHA

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akikagua gwaride la Kikundi cha Kukabiliana na Uhalifu kwa Haraka (Rapid Response Team) kilichohitimu mafunzo yao katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha mwishoni mwa wiki.
Wahitimu wa RRT wakiapa Kiapo cha Utii mbele ya Mgeni Rasmi Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi.
Wahifadhi wakifuatilia kwa makini zoezi la uhitimishwaji wa mafunzo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Hifadhi ya Ruaha Dk. Christopher Timbuka, John Shemnkunde, Mtango Mtahiko na Godwell Meing’ataki.
Mkurugenzi wa Uhifadhi wa TANAPA Martin Loibooki akisoma maelezo kuhusu mafunzo hayo kwa mgeni rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akiongea na wahitimu.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

WARSHA YA WIKI MOJA KWA REDIO ZA JAMII NCHINI KATIKA KUTEKEKELEZA MRADI WA DEMOKRASIA NA AMANI WA UNESCO UNAOFADHILIWA NA UNDP YAMALIZIKA WILAYANI SENGEREMA

$
0
0
IMG_2789
Meneja wa mradi wa Amani na Demokrasi (DEP ) kutoka UNESCO Courtney Ivins akizungumza na Mameneja na Wakurugenzi wa redio za jamii kupata tathmini ya warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa Juma wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
IMG_2743
Washiriki wakijadiliana katika makundi mambo mbalimbali ya kuboresha kwenye redio jamii zao katika utekelezaji wa mradi wa DEP kuelekea uchaguzi 2015 wakati wa kuhitimisha warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa Juma.IMG_2825
Mameneja na Wakurugenzi wa redio za jamii nchini kwenye picha ya pamoja na wawezeshaji mara baada ya kumalizika kwa warsha ya wiki moja kwa ajili ya kuwaanda redio za jamii kuendesha mijadala ya Amani na Demokrasi kuelekea uchaguzi 2015 iliyoandaliwa na shirika la UNESCO na kufadhiliwa na UNDP.

POMBE HARAMU AINA YA GONGO YAKAMATWA NDANI YA BASI HUKO MASASI MKOANI MTWARA IKISAFIRISHWA

$
0
0
Na Elvan Limwagu wa Globu ya Jamii,Masasi 

Basi dogo la kubeba abiria liitwalo BUTI LA ZUNGU lenye Namba za Usajili T510CFM aina ya Toyota Costa jana (18/8/2013) lilikamatwa na Polisi maeneo ya Njenga Ndanda na kufikishwa katika Kituo cha Polisi Ndanda baada ya kupekuliwa na kukutwa na Madumu 5 ya Pombe haramu aina ya Gongo yakiwa yamefichwa chini ya siti.

Madumu hayo ambayo yalifungwa vizuri ndani ya mabox na juu yake kufunikwa kwa mifuko myeusi ya nylon pasipo kutoa harufu kabisa.

Basi hilo linalofanya safari zake kati ya Lindi – Masasi lilikamatwa majira ya saa 9 alasiri likisafiri kutoka Masasi kwenda Lindi. Baada ya upekuzi mmiliki wa mzigo huo hakujitokeza na Makondakta walishindwa kumtaja mwenye mzigo huo na hivyo Kondakta mmoja aitwaye ALLY alishikiliwa katika kituo hicho kwa kuisaidia Polisi. Basi hilo ambalo lilibeba abiria nikiwemo “mimi” liliruhusiwa kuendelea na safari saa 9:55 alasiri.
Askari Polisi wa Kituo cha Ndanda wakiendelea na ukaguzi kwenye basi hilo.
Mara madumu kadhaa yakaonekana na kuanza kushushwa.
Hili ndio basi lenyewe lililokuwa limebeba kilaji hicho haramu.
Hivi ndivyo kilivyokuwa kimehifadhiwa kilaji hicho,tena kwa ustaji mkubwa ili kisibainike.
Wadau wakidiskasi jambo.

VODACOM YAOMBA RADHI WATEJA WAKE KUTOKANA NA HITILAFU ILIYOKEA HIVI KARIBUNI

NBC yazindua Huduma ya Mawasiliano ya papo kwa papo ya wateja (Hotline Service)

$
0
0
Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Maharage Chande akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma ya mawasiliano ya papo kwa papo (Hotline Service) kati ya mteja wa benki hiyo na maofisa wa benki nhuduma itakayopatikana ndani ya matawi ya NBC. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Maharage Chande (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja cha benki hiyo, Jane Dogani (kushoto), wakifurahia wakati mmoja wa wateja wao, Amin Juma (katikati) akijibiwa swali alilouliza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo.
Meneja Mahusiano wa NBC Tanzania, Eddie Mhina akiongoza shughuli za uzinduzi wa huduma ya Hotline Service ya Benki ya NBC katika Tawi la Corporate jijini Dar es Salaam. Huduma hiyo pia kwa sasa inaweza kupatikana katikan matawi mengine.

hepi besdei ya kuzaliwa mdau Fortunata

$
0
0
 Keki ya Fortunata ambayo ilikuwa maalumu kwenye siku yake ya kuzaliwa ambayo alikula pamoja na wafanyakazi wenzake wa LAPF ,Dodoma.
 Fortunata akimlisha keki rafiki yake Scola
 Wakati wa kugonga glasi kama ishara ya kumpongeza Fortunata kwa kuongeza umri zaidi katika sherehe ndogo iliyofanyika kwennye Pub maarufu ya Ngonyani , Dodoma.
Fortunata akimimina champaigne kwa wafanyakazi wenzake wa LAPF waliojumuika nae siku ya kuzaliwa kwake iliyofanyika hivi karibuni,Dodoma.

MSIBA WA NEMELA PHILLIP MANGULA NYUMBANI KWAO OYSTERBAY, DAR ES SALAAM, LEO

news alert: mtoto wa kike aokotwa upanga jijini dar es salaam leo, amehifadhiwa kituo kidogo cha polisi cha salender

$
0
0

Mtoto wa kike mwenye umri unaokadiriwa kuwa miaka 3 ama 4 anayesema anaitwa Manka ameokotwa leo na wasamaria wema maeneo ya Upanga jijini Dar es salaam na kupelekwaa katika kituo kidogo cha polisi cha Salender ambako hadi tunaenda mitamboni alikuwa amehifadhiwa hapo. Juhudi za kuwatafuta wazazi wake ama wanafamilia zinaendelea na wito umetolewa kwa yeyote anayemfahamu mtoto huyu ama wazazi wake aende kituoni hapo.

Mkurugenzi wa Mipango wa Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Sera za Uhamiaji atembelea Balozi Dr. Kamala ofisini kwake Brussels

$
0
0
Mkurugenzi wa Mipango wa Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Sera za Uhamiaji Bi. Chantal Lacroix akimweleza Balozi wa Tanzania Jumuiya ya Ulaya Dr. Diodorus Buberwa Kamala maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa ushirikishaji wa sekta binafsi katika masuala ya Uhamiaji  utakaofanyika Arusha tarehe 18 na 19, Septemba 2013. Mazungumzo yamefanyika katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania Ubelgiji na Jumuiya ya Ulaya, Brussels leo.

New England Umoja Organization (NEU) event cancelled

$
0
0

 On behalf of the New England Umoja Organization (NEU) and its leadership, we regret to inform you that, our annual event which was planned for 8/24/13 has been cancelled due to circumstances which are beyond our control.
We sincerely regret the inconvenience this will cause. While the organization may not be able to compensate the leadership is asking for your understanding and patience as we works to improve the organization and its functions in the community. 
We would like to thank all of you for continued support.

New England Umoja 
Organization (NEU)

Madaktari bingwa kutoka China wajitambulisha kwa Rais wa Zanzibar leo

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na madaktari kutoka Jimbo la Jiangsu Nchini China waliofika Ikulu Mjini Zanzibar kusalimiana na Rais,madaktari hawa wataungana na Madaaktari wazalendo katika kutoa huduma katika Hospitali za Serikali Unguja na Pemba.
Baadhi ya Madaktari kutoka Jimbo la Jiangsu Nchini China waliofika Ikulu Mjini Zanzibar,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipozungumza na madaktari hao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa katika picha ya pamoja na madaktari kutoka Jimbo la Jiangsu Nchini China waliofika Ikulu Mjini Zanzibar kusalimiana na Rais,madaktari hawa wataungana na Madaaktari wazalendo katika kutoa huduma katika Hospitali za Serikali Unguja na Pemba.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

sheikh ponda apandishwa mahakamani mjini morogoro leo, asomewa mashitaka matatu

$
0
0

Sheikh Ponda Issa Ponda Akiondoka mahakamani mara baada ya kusomewa mashtaka matatu na kesi yake imehairishwa Hadi  tarehe 28.08.2013
Ulinzi Ukiwa umeimarishwa mahakamani leo 
Sheikh Issa Ponda Akiwa mahakamani mkoani Morogoro asubuhi ya leo Sheikh Ponda Amesomewa Mashtaka Matatu katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro Likiwemo la uchochezi alilolitoa Kwenye  Mkutano wa Hadhara Tarehe 10 mwezi huu ambapo inadaiwa alisema kwamba ”Ndugu waislamu Msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za Misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa Serikali ”katika viwanja vya shule ya kiwanja cha ndege Mkoani Morogoro. Baada ya kusomewa Mashitaka hayo Mahakama imesema Upelelezi Umekamilika na  Dhamana Imefungwa  na Amerudishwa Rumande Mpaka tarehe 28 mwezi huu ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa katika Mahakama ya Mkoa wa Morogoro..

WANADMV MAZOEZI YANAENDELEA LEO JUMATATU AUG 19, 2013 MEADOWBROOK PARK

$
0
0


WanaDMV yanaendelea leo Jumatatu Aug 19, 2013 kuanzia saa 11 jioni mazoezi yatafanyika Meadowbrook Park kwa ajili ya kucheza kwenye Labor Day Tounament itakayofanyika Aug 31, 2013 kama maelezo yanavyojieleza hapo chini na Jumapili Aug 25, 2013 tutacheza mechi ya kirafiki na Vitambi FC katika viwanja vya Layhill

Tafadhali tuzingatie muda na upatapo taarifa hii mtaarifu na mwenzio asante
VITAMBI FCand the greater DMV Kenyan community invites you to the Annual Labor Day Soccer Tournament. This is a family event to be held on Saturday August 31statLayhill Park, 14901 Layhill Road, Silver Spring. MD 20906.
The games begin at 11.00AM EST and promise to be action packed. This year’s event brings together local and non-local teams representing an array of African countries. Some of the featured teams are:


·         VITAMBI FC

·         WATEMBEZI FC (BALTIMORE)

·         DC FLAMES (MALAWI)

·         NEW JERSEY STARS

T        TANZANIA STARS DMV
Teams are required to be at the tournament site by 10:00AM EST

This event provides a fun opportunity for families to enjoy soccer, Bouncing castle, and field games for both children and adults. Food and refreshment will be available, especially the world famous Nyama Choma!


Local vendors are invited and encouraged to contact us for advertisement opportunities for their goods & services. This is a great opportunity to network while connecting with the community. Contact Erico at vitambifc@gmail.com with the subject “FAMILY COOKOUT” we will get back to you within 24 hours.



Thank you and we look forward to seeing you there!

HAJA YA HOJA: OGOPA MAPENZI YA KICHAWI:

$
0
0
Naitwa  Mama  Jessica, ni mwanamke mwenye  umri  wa  miaka  35, mkaazi  wa  Tabata, Dar  Es salaam.. Baada  ya  kuumizwa  sana    na  wanaume katika  mapenzi, niliamua  kutafuta  mganga wa  kienyeji, shoga  yangu  alinipeleka  kwa Mganga mmoja  anayeitwa  MUNGU  WAKABILI, ambaye  ni  Mtaalamu  aliyebobea   sana katika  masuala  ya  ULIMWENGU  USIO ONEKANA. 
Wakati naenda  kumuona  huyu  mganga, tayari  nilikuwa nimeanza  uhusiano  na  mwanaume mmoja lakini  na  yeye  akawa   haeleweki  heleweki. MUNGU  WAKABILI, alinipa  dawa   ya  mapenzi   ambayo  imenifanya  nijutie   kuitumia , kwani  baada  ya  kumfanyia  dawa  mwanaume  huyo, AMENIPENDA   KUPITA  KIASI! YANI AMEKUWA  KAMA   ZEZETA  KABISA! 
Alikuwa  na  mke  wa  ndoa na  watoto  watatu, ila amewatelekeza  wote   na  kuja  kuishi  na  mimi. Nyumba  aliyo jenga  na  mke  wake  ameiuza  na  kuninunulia  mimi  nyumba  nyingine   ili  tuishi  pamoja, kama  hiyo  haitoshi  alikuwa  na  magari  mawili  moja  amempa  mdogo  wangu  wa  kiume, jingine  ameliuza  na kunifungulia  duka  la  nguo  Kinondoni.   Ni mambo mengi  sana, yote  siwezi  kuelezea, ila kibaya  zaidi  ni kwamba, sasa  ameshindwa  kuendelea  na  biashara  zake,anataka  kuwa  na  mimi  wakati  wote  kwa  sababu  amekuwa  na  wivu  sana, anahisi akiniacha  hata  kwa  dakika  mbili tu nitaibiwa  na  mwanaume mwingine. Kibaya  kuliko  vyote  sasa  ndugu  wa  mume, mke  wake  na  ndugu  wa  mke wake, wameanza  kunitishia  maisha  yangu . 
Nilijaribu  kwenda  kumuomba  huyu MUNGU  WA  KABILI  anipe  dawa  ya  kumrudisha  huyu mwanaume  katika  hali  yake  ya  kawaida  lakini  amegoma  kufanya  hivyo, anasema yeye   hawezi  kuharibu dawa  aliyo kwisha  itengeneza tayari  na  kwamba  alinionya  mapema.. Hapa  nipo njia  panda  na  sijui  hatma  ya jambo  hili, natamani  nikimbie  mji  lakini  nashindwa.  
Nimeamua  kuandika  waraka huu  ili  kwanza, kuwaonya  wanawake  wenzangu  waachane  na   MAPENZI  YA  KICHAWI  ili  yasije  kuwakuta  kama  yaliyo nikuta  mimi, kwani naona  wanawake  wengi sana, wa  Dar  Es salaam, wanamkibilia  mtu  huyu  kwa  ajili  ya  kupata  dawa  za  mapenzi.. 
Nakuonya  usifanye  hivyo mwanamke  mwenzangu, kwani  mtu  huyu  licha  ya  kuwa  na  umri  mdogo  tu tena  wa  miaka  chini  ya  thelathini, lakini  dawa  zake  ni  za  hatari  sana  na  zina  nguvu  za  ajabu  sana! Usijaribu  kabisa  mwanamke  mwenzangu,  utaumbuka,kwani kila  mtu  atajua  umetumia  uchawi!  
 Lakini, pili, ninawaomba  wanawake  wenzangu  mnisaidie   kumshawishi     MUNGU  WA KABILI  ili  amrejeshe  huyu  mwanaume  katika  hali  yake  ya  kawaida.. 

MAMA SALMA KIKWETE APOKEA TUZO MAALUM TOKA TAASISI YA BEN TV DIPLOMATIC AWARDS 2012

$
0
0
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara akimkabidhi Tuzo ya Ben TV Diplomatic Awards-2012 Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ofisini kwake tarehe 19.8.2013. Tuzo hiyo ilitolewa kwa Mama Salma baada ya kuibuka mshindi miongoni mwa mataifa ya bara la Afrika, Caribean, Asia na Pacific kutokana na kazi za kuendeleza rasilimai watu hapa Tanzania.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akitoa hotuba fupi ya kushukuru mara tu baada ya kupokea Tuzo kutoka kwa Taasisi ya Bright Entertainment Network ya Uingereza iliyokabidhiwa kwake na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara tarehe 19.8.2013.
Mwnyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akipiga picha ya pamoja na Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo mara baada ya Waziri Mukangara kumkabidhi Tuzo hiyo.
Mke wa Rais na Mshindi wa Tuzo ya BEN TV DIPLOMATIC AWARDS-2012 Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara na baadhi ya wajumbe wa bodi ya WAMA, Mheshimiwa Zakhia Meghji, Makamu Mwenyekiti (kulia) na Mama Hulda Kibacha, Mjumbe wa bodi (kushoto).mara tu baada ya kupokea Tuzo hiyo ofisini kwake tarehe 19.8.2013.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dkt.Fenella Mukangara wakati akitoa maelezo mafupi kuhusiana na tuzo ya Ben TV Diplomatic Awards-2012 aliyopewa dhamana na Taasisi ya Bright Entertainment Network (BEN) ya Uingereza ya kumkabidhi Mama Salma Kikwete Tuzo hiyo katika jitihada zake za kuendeleza rasilimali watu katika Taifa kwa mwaka 2012.PICHA NA JOHN LUKUWI
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images