Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

Kind reminder: Haba na Haba Dance Festival Start on Friday, 11th - 12th May 2018

$
0
0
 Dear Friends and Partners,

Haba na Haba team would like to take this opportunity to give you a kind reminder for our coming  HABA NA HABA – DAR ES SALAAM INTERNATIONAL DANCE FESTIVAL MAY 2018, to be held on Friday - Saturday 11th and 12th May 2017. The festival will bring together great traditional and contemporary dance performances from a number of different groups from local and international artists/dance group. 

Let’s join together to celebrate and support traditional and contemporary dance, dancers, choreographers and the whole dance sector in the city of Dar es Salaam, Tanzania.

We are very happy to welcome you all, and encourage you to spread the word about this coming dance event for this remain 4 days before we start enjoying and celebrating traditional and contemporary dance performance. 

#Saving_our_Dance_Heritage_Dance_Without_Boundaries

Please find attached poster of all event will be happened during the festival,  

Date: 11th and 12th May 2018
Venue: NAFASI ART SPACE, Mikocheni, Dar es Salaam
Time: 7:30pm - 10:00pm
YOU ARE ALL WELCOME | KARIBU SANA
SEE YOU THERE.



HANARI ZA UMOJA WA MATAIFA LEO MEI 7, 2018

JAFO AITAKA MANISPAA YA UBUNGO IJITATHMINI

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo ameitaka manispaa ya Ubungo ijitathimini katika usimamizi wa mapato na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. 
Jafo amesema hayo alipokuwa katika ziara ya kukagua shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo jijini Dar es salaam. 

Akizungumza katika ziara hiyo, Waziri Jafo ameonesha kusikitishwa na manispaa hiyo kuonyesha dalili za wazi kushidwa kufunga mifumo ya kielectroniki katika maeneo yote  ya  kituo cha afya cha Palestina chenye watu wengi wanao hudumiwa. 

Amesema katika eneo la mapokezi pekee ndilo walilofunga mfumo wa kielekroniki kitendo ambacho kinakosesha mapato  makubwa kwa serikali ambapo kwasasa amejulishwa kwamba zinakusanywa sh.milioni mbili kwa mwezi. 

"Hali hii iliyojitokeza katika kituo cha Palestina kutotumika kikamilifu mifumo ya kielektroniki kunaashiria hata katika vyanzo vingine kuna uwezekano mkubwa wa upotevu wa mapato ya Manispaa ya Ubungo," amesema Jafo

Kufuatia hali hiyo, Waziri Jafo ameagiza mfumo wa GotHomis ufungwe katika maeneo yote ifikapo Mei 30 mwaka 2018. Aidha, Waziri Jafo amemtaka mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Kayombo kusimamia vyema utekelezaji wa miradi katika manispaa hiyo.

Hata hivyo amesema anakusudia kuunda timu ya uchunguzi na ufuatiliaji kutoka TAMISEMI ili kujiridhisha mwenendo wa ukusanyaji wa mapato pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa fedha ambazo Halmashauri hiyo imepokea hadi sasa.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akizungumza na wafanyabiashara alipotembelea Soko la Shekilango kuangalia ujenzi uliofanyika.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akikagua utoaji huduma katika kituo cha Afya cha Palestina Manispaa ya Ubungo.

Wafanyabiashara wa soko la Shekilango wakiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo katika ukaguzi wa soko hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akikagua mfumo wa maji taka uliokarabatiwa katika Kituo cha Afya Palestina Manispaa ya Ubungo.

Mark Zuckerberg's senate hearing highlights

SITAKI UKANJANJA KATIKA UJENZI WA STENDI YA MABASI MBEZI LUIS - WAZIRI JAFO

$
0
0
WAZIRI  wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amewaonya watu ambao ni makanjanja wa miradi ya maendeleo kwamba hatasita kuwachukulia hatua kali za kisheria huku akisema hatarajii kuwaona katika mradi wa stendi ya mabasi ya mikoani inayotarajiwa kujengwa Mbezi Luis jijini Dar es salaam.

Jafo ameyasema hayo alipotembelea eneo linalotarajiwa kujengwa stendi hiyo eneo la Mbezi Luis jiji Dar es salaam. Ujenzi wa stendi hiyo unatarajiwa kuanza kujengwa miezi michache ijayo baada ya jiji la Dar es salaam kupata fedha Sh. bilioni 50 kutoka serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI. 

Akizungumza katika eneo hilo, Jafo amesema kuna baadhi ya watu wanapoona miradi mikubwa kama hiyo huwa wanapanga mikakati ya kuhujumu au kujipatia fedha kwa kufanya ufisadi.

"Wataofanya hivyo waelewe wazi  hawatabaki salama," amesisitiza  Waziri Jafo

Aidha, Jafo amesisitiza kauli ya Rais Dk.John Magufuli aliyoitoa wakati akizindua stendi ya mabasi ya Msamvu kwamba katika ujenzi wa stendi zote lazima zizingatie mahitaji ya wadau mbalimbali hususan Mama na baba Nitilie ili waweze kujipatia fedha kutokana na uuzaji wa chakula. 
Naye, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam  Zipora Liana amemuahidi Waziri Jafo kwamba stendi hiyo itakuwa ya mfano barani Afrika kwani itajengwa kisasa zaidi.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akiwa na Viongozi wa mkoa wa Dar es salaam na wilaya ya Ubungo katika ukaguzi wa eneo la ujenzi wa Stendi ya Mbezi Luis.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akikagua mipaka ya eneo la ujenzi wa Stendi ya Mbezi Luis.
 Viongozi mbalimbali wakisikiliza maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo kuhusu ukaguzi wa eneo la ujenzi wa Stendi ya Mbezi Luis.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akipata maelezo ya eneo linalotarajiwa kujengwa stendi ya mabasi ya kisasa ya Mbezi Luis.

INTRODUCING NEW SONG FROM AMINI - SIJUI (OFFICIAL VIDEO)

TANZANIA YATAJWA KUWA BUSTANI YA EDEN NA CHIMBUKO LA MWANADAMU WA KALE DUNIANI

$
0
0

Hatimaye utata uliokuwa ukiendelea duniani kwa watafiti wa mambo ya kale kuhusiana na mahali mwanadamu wa kwanza alipotokea umemalizika baada ya jopo la wataalam liloundwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kufuatia ushahidi wa vinasaba kubaini kuwa binadamu huyo alitokea barani Afrika huku ikidaiwa kuwa ni Tanzania eneo la Olduvai Gorge.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya ufugaji nyuki aloiutisha kujadili maendeleo ya sekta hiyo Jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.

Amesema  utafiti huo umeshirikisha wataalamu kutoka mataifa mbalimbali duniani na kuwa kumalizika kwake kutaiwezesha sekta ya utalii nchini kukua kwa kasi sambamba na kuongeza pato la taifa.

Wananchi MBEYA watakiwa kufanya mazoezi

$
0
0
Taasisi ya Mo Dewji imekuwa miongoni mwa wadhamini ambao kwa kushirikiana na Taasisi ya Tulia Trust wamewezesha kufanyika Tulia Marathon 2018, ikiwa ni mara ya pili kufanya hivyo baada ya mbio za mwaka jana ambazo zilikuwa na mafanikio makubwa.

Akizungumza katika mbio hizo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla alisema watu wengi hawana utaratibu wa kufanya mazoezi jambo ambalo sio zuri kiafya na hivyo kuwataka wananchi kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao.

Aidha Makalla alimpongeza Naibu Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Mwanzilishi wa Taasisi ya Tulia Trust, Dkt. Tulia Ackson kwa kuanzisha mbio hizo ambazo zinasaidia sana mkoa huo kuboresha sekta ya afya na elimu. 

“Michezo ni muhimu sana kwa afya zetu … tujifunze na sisi tuanze kufanya mazoezi sababu ni muhimu sana kwa afya zetu. Mimi hapa nilipo sijawahi kuumwa maralia tangu nikiwa kidato cha kwanza lakini sababu nafanya mazoezi. Ukiwa unafanya mazoezi magonjwa haya ya pressure unaachana nayo,” alisema na kuongeza.

“Niseme tunafaidika sana kupitia Trulia Trust kwa mambo ambayo anayafanya, anaupenda mkoa wetu ameboresha miundombinu katika elimu na afya. Alianza kwenye ngoma na sasa anafanya Tulia Marathon na kutokana na marathon hii anakwenda kusaidia afya na elimu.”

Naye Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Rachel Chengula alisema wameamua kushirikiana na Tulia Trust ili kusaidia kuokoa maisha ya Watanzania ambao wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na kukosa huduma bora za afya.

“Tunatambua kwamba maisha ya mwanadamu yanaanza mimba inapotungwa hivyo ni muhimu sisi kama sehemu Watanzania tuliojengwa katika misingi ya upendo kuona ni muhimu kushirikiana na serikali na wadau wengine kama Tulia Trust kuweka mazingira bora ya wodi za uzazi ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi nchini,

“Tunapongeza hatua ambazo zinachukuliwa na serikali za kukarabati vituo vya afya katika Halmashauri mbalimbali nchini kwa kujenga na kukarabati majengo ya upasuaji, wodi za wazazi na watoto pamoja na maabara. Tunaamini jitihada hizi zitasaidia kupunguza vifo vya kina mama na watoto nchini,” alisema Chengula.

Awali akizungumza kuhusu Tulia Marathon 2018, Dkt. Tulia alisema fedha ambazo zimepatikana katika mbio za mwaka huu zitatumika kusaidia kuboresha sekta ya elimu na afya kama ilivyokuwa mwaka jana na lengo lao ni kushirikiana na serikali ili kuwezesha wananchi wapate huduma bora za kiafya na elimu bora.

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Mwanzilishi wa Taasisi ya Tulia Trust, Dkt. Tulia Ackson akiongoza wanariadha waliojitokeza kukimbia katika Tulia Marathon 2018 zilizofanyika Jijini Mbeya.
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Mwanzilishi wa Taasisi ya Tulia Trust, Dkt. Tulia Ackson akielezea mafanikio ambayo Tulia Marathon iliyapata kwa mwaka uliopita na mipango ya mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akizungumza namna Tulia Marathon inawasaidia kuboresha sekta ya afya na elimu na kutoa pongezi kwa Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.


MASHINDANO YA SIRRO CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI KIBITI

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akimkabidhi mpira mmoja wa Viongozi wa timu zinazoshiriki mashindano ya Sirro Kibiti mwaka 2018 katika uwanja wa Samora Kibiti wakati wa uzinduzi wa michezo hiyo uliofanyika jana. Mashindano hayo yanashirikisha timu 16 kutoka Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Migomba kutoka Wilayani Rufiji wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Sirro Kibiti mwaka 2018 katika uwanja wa Samora Kibiti. Mashindano hayo yanashirikisha timu 16 kutoka Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akiwasalimu wakazi wa Kibiti wakati wa Sherehe za ufunguzi wa mashindano ya Sirro Kibiti mwaka 2018 katika uwanja wa Samora Kibiti. Mashindano yanayoshirikisha timu 16 kutoka Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
Msanii Malima Ndolela (Mzee wa Ndolela) akitumbuiza wakati wa Sherehe za ufunguzi wa mashindano ya Sirro Kibiti mwaka 2018 katika uwanja wa Samora Kibiti. Mashindano yanayoshirikisha timu 16 kutoka Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
Msanii Man Prince akitumbuiza wakati wa Sherehe za ufunguzi wa mashindano ya Sirro Kibiti mwaka 2018 katika uwanja wa Samora Kibiti. Mashindano yanayoshirikisha timu 16 kutoka Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji.

TAPSEA ANNUAL MEETING

World Bank launches trainings on new Environmental and Social Framework (ESF)

$
0
0
DAR ES SALAAM, May 8, 2018 - Workshops to support the implementation of the new World Bank Environmental and Social Framework (ESF) kicked off today in Dodoma.

The workshops, which will take place over four days (May 8 -11) in Dodoma and Dar es Salaam, bring together government representatives, development partners as well as stakeholders from civil society organizations from Tanzania and Malawi, with the aim of providing them with a comprehensive understanding of the new environmental and social requirements the World Bank will be applying to investment projects it finances starting October 2018.

“Since the World Bank issued its current safeguard policies nearly 20 years ago, setting the standards for Multilateral Development Banks in protections for people and the environment, we have seen that investment projects are more sustainable and have a greater impact when the environment is protected, and when communities are engaged,” says Bella Bird, World Bank Country Director for Tanzania, Malawi, Somalia and Burundi. “The new ESF builds on this solid foundation and places more emphasis on the utilization of country systems for sustainable results.”

The ESF is the result of the most extensive consultations ever conducted by the World Bank, with nearly four years of analysis and engagement around the world with governments, development experts, and civil society groups, reaching nearly 8,000 stakeholders in 63 countries. The new framework provides a broad coverage of environmental and social issues, including important advances on transparency, non-discrimination, social inclusion, public participation and accountability. The ESF also places more emphasis on building Borrower governments’ own capacity to deal with environmental and social issues.

The World Bank’s environmental and social policies aim to ensure that the people and the environment are protected from the potential adverse impacts of the projects it finances — such as building a road, connecting people to electricity, or treating waste water. The policies help identify, avoid, and minimize harm to people and the environment. They require the borrowing governments to address certain environmental and social risks in order to receive World Bank support for investment projects.

The ESF is expected to go into effect October 2018, and will progressively replace the World Bank’s current Safeguards policies.

MICHUZI TV: MZEE MAJUTO AFIKA SALAMA NCHINI INDIA, MWANAE AELEZEA WALIVYOPOKELEWA

SHONZA - SERIKALI KUJENGA KITUO CHA MICHEZO TANGA

Mkazi wa Zanzibar ashinda bidhaa zenye thamani ya Tsh. milioni 1 kutoka Jumia

$
0
0
Mkazi wa visiwani Zanzibar, Bi. Patricia Philipo amejishindia vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka Jumia kupitia kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ katika mwezi uliopita wa Aprili. 

Mshindi huyo alipatikana kupitia kampeni iliyoendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. Wateja walitakiwa kupendekeza mtu wao wa karibu ambaye waliona anastahili nyumba yake kupendezeshwa na Jumia kwa kupatiwa ofa ya vyombo vya ndani.

Bi. Patricia Philipo aliibuka mshindi baada ya mchumba wake Bw. Mwalim Juma Kumpendekeza ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa.

“Mimi ni mteja mzuri wa Jumia kwa sababu naitumia mara kwa mara kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali ambazo zimekuwa zikinifika mpaka ninakoishi Zanzibar. Baada ya kuliona hili shindano, niliona ni vema nimpendekeze mwenzangu ashinde. Ukizingatia tupo kwenye maandalizi ya ndoa yetu, suala la mahari pamoja na vyombo vya ndani ni gharama hivyo ushindi wake ungekuwa na mchango mkubwa kwenye shughuli yetu,” alisema Bw. Juma ambaye ni mchumba wa mshindi wa kampeni hiyo, Bi. Patricia.

“Sikuwa na wasiwasi kwamba endapo angeshinda asingeweza kupatiwa zawadi zake. Kwa sababu hapo nyuma kulikuwa na mashindano kadhaa kama vile ‘Treasure Hunt’ kipindi cha Mobile Week, wateja walikuwa wanashinda simu na kukabidhiwa bila ya ubabaishaji wowote,” alimalizia Bw. Juma.

Akielezea furaha yake mara baada ya kutangazwa mshindi Bi. Patricia Philipo amesema kuwa, “kusema ukweli hapo mwanzo sikutarajia kama ningeweza kushinda kutokana na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wangu. Kuna wakati nilitaka kukata tamaa kwa sababu mwenzangu alikuwa ameniacha mbali, mashabiki wake walikuwa wanamuunga mkono na kuwashirikisha wengine kwa kiasi kikubwa.”
Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni moja,Mkazi wa visiwani Zanzibar, Bi. Patricia Philipo mara baada ya kujishindia vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka Jumia kupitia kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ katika mwezi uliopita wa Aprili.

Bi. Patricia Philipo aliibuka mshindi baada ya mchumba wake Bw. Mwalim Juma Kumpendekeza ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akizungumza mapema leo jijini Dar kuhusu ushindi wa Mkazi wa visiwani Zanzibar, Bi. Patricia Philipo (hayupo pichani) aliyejishindia vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka Jumia kupitia kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ katika mwezi uliopita wa Aprili.Pichani kushoto ni Mchumba wa mshindi,Bw. Mwalim Juma. 

Mshindi huyo alipatikana kupitia kampeni iliyoendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. Wateja walitakiwa kupendekeza mtu wao wa karibu ambaye waliona anastahili nyumba yake kupendezeshwa na Jumia kwa kupatiwa ofa ya vyombo vya ndani. 
Afisa Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Hadija Natalia Tuwano pamoja na Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey wakimsikiliza kwa makini Mchumba wa mshindi,Bw. Mwalim Juma akitoa ushuhuda wa namna alivyompendekeza Mchumba wake na kujishindia vyombo vya ndani mbele ya Waandishi wa Habari mapema leo jijini Dar,Mwalimu Juma alimpendekeza mchumba wake Bi. Patricia Philipo ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa.

NG'UMBI AVISHWA RASMI CHEO CHA BRIGEDIA JENERALI

$
0
0
Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
BALOZI wa Tanzania nchini China Mbelwa  Kairuki kwa niaba ya Makao Makuu ya Jeshi amemvisha  rasmi Kanali R.C Ng’umbi  cheo kipya cha  Brigedia Jenerali.

Brigedia Jenerali Ng’umbi  ambaye pia ni Mwambata Jeshi katika Ubalozi wa Tanzania  nchini China , ni miongoni mwa maofisa  27 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopandishwa vyeo  tarehe 12 Aprili mwaka ,2018 na Rais na Amiri Jeshi  Mkuu Dkt. John Magufuli.

 Akizungumza Mara baada ya kuvalishwa Cheo hicho jana Mei 7 , Brigedia Jenerali  alimshukuru Amiri Jeshi Mkuu  Dk. Magufuli  pamoja na uongozi wa Makao Makuu ya Jeshi kwa kupandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali.

Tukio hilo lilifanyika  katika ofisi za  ubalozi wa Tanzania nchini China  na kuhudhuriwa na maofisa  pamoja na watumishi  kutoka ofisi  za Ubalozi  pamoja na familia zao.
 Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa  Kairuki kwa niaba ya Makao Makuu ya Jeshi akimvisha  rasmi Kanali R.C Ng’umbi  cheo kipya cha  Brigedia Jenerali katika hafla iliyofanyika kwenye ubalozi wa Tanzania nchini China.
  Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa  Kairuki, Brigedia Jenerali, R.C Ngumbi  wakiwa katika picha ya pamoja  na Maafisa na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.
  Brigedia Jenerali R.C Ngumbi akiwa katika  picha ya pamoja  na Balozi Mbelwa Kairuki, Maafisa na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.

CSI WAHIMIZA USHIRIKIANO ILI KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI, WAELEZEA UMUHIMU WA WAKUNGA KATIKA KUTOA HUDUMA ZENYE HESHIMA

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
SHIRIKA la Childbirth Survival International (CSI) limesema ipo haja kwa wakunga wote nchini kutoa huduma yenye heshima kwa mama mjazito ili ajifungue salama huku likitoa ombi kwa Serikali kuendelea kutoa fedha katika sekta ya afya kwa lengo la kupunguza vifo kwa mama wajawazito na watoto.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la CSI Stella Mpanda wakati anazungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wakunga Duniani ambapo kwa Tanzania maadhimisho hayo yalifanyika kitaifa mkoani Morogoro na kauli mbiu ilikuwa inasema "Ukunga ni chachu ya huduma bora kwa akina mama".


Amesema kutokana na kauli mbiu hiyo Shirika la CSI linaungana na wakunga wote nchini na duniani kwa ujumla kuhakikisha wakunga wanatoa huduma bora zenye ustadi kwa mama mjazito na lengo ni kuhakikisha mama anajifungua salama.

Mpanda amesema ili kupunguza vifo vya mama mjazito na watoto ni vema jamii ya Watanzania kwa pamoja wakashirikiana kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake na kufafanua mashirika yanatakiwa kutimiza wajibu wao, Serikali na wananchi nao kutimiza wajibu wao na  kwa kufanya hivyo CSI inaamini vifo hivyo vitapungua.

Pia amezungumzia umuhimu wa jamii kutambua vidokezo hatari kwa mama mjazito ambavyo husababisha vifo iwapo atachelewa kwenda hospitali na kueleza vidokezo hivyo mama ,baba na wananchi wanapaswa kuvitambua kwani itasaidia katika kupunguza vifo hivyo vinavyotokea wakati wa kujifungua kwa baadhi ya akina mama.

Amefafanua Shirika la CSI kwa muda mrefu limekuwa likitoa mafunzo ya elimu ya uzazi salama kwa jamii ambapo pia wamekuwa na programu maalumu zinazolenga kuwajengea uwezo wakungwa ili watoe huduma bora na zenye ustadi wa hali ya juu na kusisitiza wataendelea na jukumu hilo kwani dhamira yao ni kuona vifo vitokanavyo na uzazi vinapungua au kwisha kabisa nchini na duniani kwa ujumla.

"CSI tumekuwa na jukumu la kutoa mafunzo kwa wakunga ili waendelee kutoa huduma bora.Pia tumekuwa tukitoa mafunzo kwa vijana na mabinti kuhusu stadi za maisha pamoja na jinsi ya kujilinda hasa kwa watoto wa kike ili wafikie malengo yao.

"Tunaamini tukiendelea kushirikiana katika eneo hili tutapunguza changamoto ambazo mama mjazito anazipitia wakati wa kujifungua.CSI tunalo jukumu la kuiona jamii ya Watanzania linapofika suala la uzazi linakuwa jambo lenye kufurahiwa na kila mmoja wetu badala ya kuibua hofu kwa jamii kwa kuwaza iwapo mama atajifungua salama au laa.Tutaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine kuhakikisha tunapunguza vifo kwa mama wajawazito na watoto,"amesema Mama Stella Mpanda ambaye pia ni mwanzilishi wa CSI akishirikiana na Profesa Tausi Kagasheki.

Halmashauri ya Kishapu yakabidhi maabara kwa Shule ya Mangu

$
0
0
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu imekabidhi jengo la maabara kwa Shule ya Sekondari Mangu iliyopo Kata ya Shagihilu baada ya ujenzi wake kukamilika.
Maabara hiyo iliyokamilika gharama ya thamani ya Sh. Milioni 10.1 linatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa wanafunzi wa shule hiyo wa mchepuo wa sayansi kwa vitendo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mang’era Mang’era akikabidhi jengo hilo alisema litachochea ufaulu wa wanafunzi ambao awali walikosa mazoezi ya vitendo.
Alisema lengo la Halmashauri ni kuhakikisha elimu inakua na hivyo inaendelea kuboresha miundombinu ya shule zake ikiwemo ujenzi wa maabara kwa ajili ya sayansi.
Mang’era Mang’era aliwataka walimu na wanafunzi kuwa kitu kimoja na kuitendea haki maabara hiyo kwa kushirikiana ili wawe na ufaulu mzuri katika mitihani inayohusisha mazoezi ya vitendo.
Alisema kuwa ufaulu kwa wanafunzi katika shule hiyo na zingine utafaleta sifa kwa wananchi wa kata hiyo pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwa ujumla.
Mang’era ambaye pia ni Afisa Mipango aliwataka wanafunzi kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii ili kuweza kufikia malengo yao ya baadaye katika kitaaluma. 
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mang’era Mang’era akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la maabara Shule ya Sekondari Mangu.
 Viongozi mbalimbali wakiangalia maabara ya Shule ya Sekondari Mangu baada ya kuziduliwa rasmi na kukabidhiwa baada ya ujenzi wake kukamilika.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mang’era Mang’era (kulia) akiwa na Afisa Elimu Sekondari, Paul Kasanda wakiangalia vifaa mbaimbali vya maabara hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mang’era Mang’era akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mangu (hawapo pichani) wakati wa makabidhiano ya jengo la maabara.
 Diwani wa Kata ya Shagihilu, Mhe. Mohamedi Amani akitoa neno la shukrani katika hafla hiyo.
 Muonekano wa maabara hiyo wakati viongozi mbalimbali walipotembelea baada ya kufunguliwa rasmi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

FAMILIA YALALAMIKA NYUMBA KUVUNJWA BILA KUFUATA SHERIA, WAMUOMBA MAKONDA AWASAIDIE HAKI ITENDEKE

$
0
0
Na Emmanuel Masaka, Globu ya jamii.

Edith Max amemuomba Makonda kusaidia ili haki ipatikane na kufafanua nyumba yao imeporwa na moja ya taasisi na kisha kuiuza katika moja ya benki iliyopo nchini(jina tunalo).

Akieleza mkasa huo amedai familia yao ilikopa fedha Sh.milioni 30 katika benki hiyo na kudai walipotaka kulipa deni hilo walizungushwa na baadaye wakaambiwa kuna riba imeongezeka kutoka Sh.milioni 30, hadi Sh.million 90.

Amesema walikubali kulipa lakini kila wakifuatilia kulipa tena wakaendelea kuzungushwa hadi deni likafikia Sh.milioni 120 lakini walikubali kulipa fedha hiyo.Walipoenda kulipa wakabaini kuna udanganyifu umefanyika kwa kugushiwa hati ya mirathi na mtu asiyetambulika na familia.

Amefafanua familia fungua mirathi yake Januari 17 katika Mahakama ya mwanzo Kinondoni na Msimamizi wa mirathi hiyo Max Edmund Kafipa .Awali anasema, suala hili walilipeleka kwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Makonda wakati wa kampeni yake ya kuwasikiliza walidhurumiwa nyumba, viwanja na mashamba iliyofanyika Januari ambapo tarehe 30 pande zote ziliitwa na kujadiliana mbele ya wanasheria na uamuzi yao yanatarajiwa kutolewa Mei 7 mwaka huu.

Hata hivyo amesema kabla ya kuanza kuvunja nyumba hiyo wahusika walipewa uzio la kutovunja lakini nyumba hiyo ikavunjwa jambo ambalo ni kinyume na sheria."Wakili wao alitamka wazi kwa Makonda hana Mamlaka ya kuingilia mambo haya na hii nyumba tulikuwa tunaitaka muda mrefu,"amesema.

Ameongeza "jana walituita wa kasema wanataka watulipe fedha.Wakatuuliza mnataka tuwape bei gani ? tukasema tulipeni Sh.bilion 2, waomba wajadiliane lakini cha kushangaza wamekuka kuvunja nyumba yetu."Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mfaume AbdulKarim Gulam Shambe amekiri kuwepo kwa sakata hilo na kwamba wakati wanakwenda kuvunja nyumba hiyo walitoa taarifa wakati wameshaanza kuivunja.

  Msemaji wa familia hiyo Edith Max (kulia)akuonesha  nyumba hiyo  jana jijini Dar as Salaam.

ULEGA AZUNGUMZIA MRADI WA UMEME WA REA MKURUNGA,APONGEZA JUHUDI ZA VIONGOZI,WANANCHI

$
0
0
Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

NAIBU Waziri wa Mifugo Na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Mkuranga Aballah Ulega amekagua mradi wa Umeme vijijini(REA) Awamu ya 3 Union delta katika Vijiji viwil vya Mkokozi na Lugwadu katika Kata ya Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Akizungumzia mradi huo leo, Ulega amesema mradi huo ua umeme unatokana na uhudi za viongozi akiwemo Diwani  wa kata aa Mwandege Adolf Kohelo na yeye Mbunge wa jimbo la Mkuranga.

 Aidha Ulega Amewashukuru  wananchi wa vijiji hivyo kwa ushirikiano wao katika kufanikisha mradi huo."Nashukuru kwa kupokea  mradi na nimesikia kuna timu ya watu wa REA wapatao 60 ambao  mmewapa ushirikiano kwa kukubali kukakata miti yenu bila gharama.Mmenitia  moyo sana," amesema.

Pia amewaomba Watanzania kumuombea Rais Dk. John  Magufuli ili andelee kuwa na nguvu ya kuwatumikia wananchi wanyonge."Wanamkuranga hakuna zawadi nzuri ya kumpa Rais zaidi ya kumuombea," amesisitiza Ulega.

Kazi ya kusimika nguzo za umeme katika vijiji vya Lugwadu na Mkokozi ikiendelea kwa kasi.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega na Mbunge wa Mkuranga akiwaaga wananchi wa vijiji vya Mkokozi na Lugwadu katika ziara ya kukagua mradi wa umeme wa Rea Mkoani Pwani. Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi,Mbunge wa Mkuranga,Abdallah Ulega akimsikiliza Diwani wa Kata ya Mwandege,Adolf Kohelo katika ziara yake ya kukagua mrad wa umeme wa Rea Mkoani Pwani.

Chuo cha biashara cha Rungwe na Taasisi ya Yemco zimetiliana saini kuwajengea uwezo wajasiliamali

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
Chuo cha kimataifa cha Biashara na Ujasiriajari Rungwe na Taasisi ya Youth Empowerment and Mindset Change Organization (Yemco) leo zimetiliana saini mkataba wa makubaliano wa kuendeleza jamii na kuwajengea uwezo wa ujasiriamali vijana, akina mama na wanavicoba.

Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Rungwe, Dk Lenny Kasoga amesema makubaliano hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam,  yataongeza chachu ya kuboresha uwezo wa jamii na kuwa na wataalam wengine wenye ujuzi tofauti tofauti  katika maeneo ya ujasiriamali na kuleta maendeleo haraka hasa kwa vijana, akina mama na wanavicoba.

Amesema, Taasisi hizo  hazitajikita kwenye kutoa elimu ya ujasiriamali pekee Bali pia zitajihusisha katika kufanya tafiti kwa nia ya kutatua changamoto zinazojitokeza katika jamii na kutoa majibu.

Kasoga ambaye pia ni mhadhiri Mwandamizi wa uchumi na biashara amesema utekelezaji wa mkataba huo utakuwa na manufaa ikiwa ni pamoja na kuongea idadi ya wajasiriamali watakaokuwa na uwezo wa kubainisha fursa na kuzitumia vilivyo kwa kuanzisha biashara  za kati na zenye kuleta ajira na pato kwa Taifa.

Ameongeza kuwa ushirikiano huo unawezekana kutokana na dhamira ya Serikali katika kujenga mazingira bora ya kisera, kisheria na utendaji  yanayolenga kuleta maendeleo endelevu kwenye ujasiriamali  na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi.

Dk Kasoga aliwahakikishia wananchi kuwa ushirikiano huo utajikita kwenye kutengeneza ajira kwa vijana, akina mama na wanavikundi wa Vicoba kwa kuhakikisha viwanda vidogo na vya kati ambacho ni tofauti na vilivyopo vinaanzishwa.

"Nia yetu ni kuona wananchi na wadau wanashiriki ipasavyo na kwa usawa katika kujenga nchi yetu yenye fursa nyingine za kiuchumi." Alisema Dk Kasoga.

Mkurugenzi wa Yemco, Mohammed Bassanga alisema makubaliano hayo utoaji wa mafunzo hayo ya ujasiriamali na vicoba endelevu utahusisha na watu wenye ulemavu  ili waweze kujiletea maendeleo na kupambana na changamoto za kimaisha.

Alibainisha kuwa  makubaliano hayo yataxhangia juhudi za  serikali ya Muungano wa Tanzania katika kuchochea ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Mwakilishi wa bodi ya Chuo cha Rungwe, Mwanasheria Benjamin Mwakagamba alisema  ni Mara chache Taasisi binfsi zinaungana kufanya kazi ya kumsaidia jamii na kupongeza.
 Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Kimataifa cha Biashara na Ujasiriamali Rungwe Dk Lenny Kasoga akitiliana saini mkataba wa makubaliano ya kuendeleza jamii kwa kuijengea uwezo wa ujasiriamali  kwa vijana, akina mama na wanavicoba na Mkurugenzi wa Yemco Mohammed Bassanga wakishuhudiwa na mwakilishi wa bodi Chuo cha Rungwe Benjamin Mwakagamba na mwanasheria Isabella Mwaipopo.
Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Kimataifa cha Biashara na Ujasiriamali Rungwe, Dk Lenny Kasoga(wa pili kushoto)  akionyesha mkataba waliotiliana saini ya makubaliano na Mkurugenzi wa Yemco, Mohammed Bassanga(wa pili kulia)
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images