Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

YANGA KUWAFUATA WAARABU MEI 03, YAJIPANGA KWA USHINDI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya kimataifa Yanga wanatarajiwa kuondoka nchini Mei 03 kwa ajili ya mchezo wao wa kwanza wa kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya USM Alger nchini Algeria.

Yanga iliyoingia katika hatua makundi ya kombe la Shirikisho baada ya kuwaondoa Welayta Dicha itashuka dimbani Mei 07 kupambana na USM Alger ikiwa ni mchezo wa kwanza wa kundi D.

Baada ya kumalizika kwa mchezo wa jana dhidi ya Simba kumalizika, Yanga sasa wanaweka nguvu zao zote kwenye mashindano hayo ili kuhakikisha wanazidi kufanya vizuri.

Mkuu wa Kitengo wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga Dismas Ten amesema kuwa kwa sasa nguvu zote wanaelekeza katika mchezo wao wa kombe la Shirikisho kwa ajili ya kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye mechi yao ya kwanza.

Ten amesema kuwa Yanga wataondoka nchini kupitia Dubai na kisha kuelekea nchini Alger ili kuwahi kufika nchini humo pamoja na kuzoea hali ya hewa.

Yanga kwa sasa inayosimamiwa na kocha msaidizi Shadrack Nswajigwa imekuwa na matokeo sio mazuri toka kuondoka kwa kocha mkuu George Lwandamina kuachana na timu hiyo na michezo minne ambayo imesimamiwa na msaidizi wake ameshindwa kuwapa ushindi.
 
Ikumbukwe hivi sasa Yanga ndiyo timu pekee inayoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo ya kimataifa baada ya Simba kuondoshwa na Al Masry SC kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga ilipangwa kundi moja 'KUNDI D' na timu za U.S.M Alger, Rayon Sports na Gor Mahia FC kwenye hatua ya makundi baada ya kuindosha Wolaita Dicha SC ya Ethiopia kwa jumla ya mabao 2-1.

YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwasilisha  hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha  kwa Wizara hiyo kwa mwaka 2018/19  Bungeni mjini Dodoma mapema leo.
 Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu akitoa maelezo Bungeni  mapema leo kuhusu mikakati ya Serikali kuhusu kufikisha umeme katika vijiji vyote hapa nchini.
 Mbunge wa Mwanga Prof. Jumanne Maghembe akichangia hoja ya  Bajeti ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kuhusu mikakati inayoweza kusaidia kuendelea kukuza kiwango cha elimu hapa nchini.
 Naibu Waziri wa  Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Mhe. Elias Kuandikwa akijibu swali Bungeni  mjini Dodoma kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kujenga miundo mbinu  hapa nchini.
 Wageni mbalimbali walihudhuria Bunge wakiwemo Skauti  wakifuatilia kipindi cha maswali na majibu mapema leo Bungeni mjini Dodoma.
 Naibu  Waziri wa Fedha Dkt. Ashatu Kijaji akisisitiza jambo kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe leo mjini Dodoma.

(Picha zote na MAELEZO)

WAZIRI WA MADINI AAGIZA RIPOTI YA TEITI IPELEKWE KWA CAG KWA AJILI YA UCHUNGUZI

$
0
0
*Ni baada ya kubainika kwa tofauti ya zaidi ya Shilingi bilioni 30 ambayo ni pungufu ya fedha ambayo Serikali imekiri kupokea.

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WAZIRI wa Madini Angella Kairuki amezindua rasmi Ripoti ya Nane ya Taasisi ya Uhamasishaji uwazi na uwajibikaji katika rasilimali za madini mafuta na gesi asilia nchini Tanzania(TEITI) kwa mwaka 2015/2016 ambayo inazungumzia ulinganishi wa mapato  ya Serikali na malipo ya kampuni za madini, mafuta na gesi asilia huku akitoa maagizo  kwa taasisi hiyo kuhakikisha ripoti hiyo inapelekwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) baada ya kubainika kuna tofauti ya  zaidi ya Shilingi bilioni 30.
Amefafanua Ripoti ya TEITI inaonesha kuwa kuanzia Julai 1 mwaka 2015 hadi Juni mwaka 2016 kunaonesha jumla ya Sh.434,627,874,380 zimepokelewa serikalini kutoka kampuni 55 za madini , mafuta na gesi asilia zilizoshiriki kwenye mchakato huo wa ulinganishi ambapo kampuni hizo zinaonesha zililipa  serikalini Sh 465,164,747,725 na hivyo kusababisha tofauti kati ya malipo kuwa ni pungufu Sh 30,536,873,345 chini ya fedha ambazo Serikali inakiri kupokea.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Waziri Kairuki amepongeza kazi nzuri ya TEITI ya kukamilisha ripoti hiyo lakini ni lazima ifahamike imekuaje imejitokeza tofauti hiyo ya fedha na hivyo ametoa maelekezo taarifa hiyo ipelekwe kwa CAG kwa ajili ya uchunguzi kama kifungu 18(1) cha sheria ya TEITI ya mwaka 2015 kinavyotoka.
"Tunataka hii ripoti iende kwa CAG ili tujue nini ambacho kimetokea na ni vema kazi hiyo ikafanyika kwa wakati,"amesema Waziri Kairuki.
Pia amesema ripoti hiyo  inaonesha sekta ya madini imechangia kwa asilimia 85 na sekta ya mafuta na gesi asilia ikionesha kuchangia asilimia 15 ya mapato ya Serikali kwa mwaka 2015,2016.
Amefafanua kuwa yote ambayo yamependekezwa na kamati ya TEITI yatafanyiwa kazi kwa haraka ili kuhakikisha yale ambayo yamesemwa yanafanyika kama ambavyo wamependekeza kwa maslahi ya Watanzania wote huku akielezea hatua kadhaa ambazo Serikali inachukua kuhakikisha madini yananufaisha wananchi wote.
Waziri Kairuki ameeleza nchi yetu ilijiunga katika mpango wa kimataifa wa Uwazi katika sekta ya uchimbaji wa rasilimali ambapo lengo lake kuu lilikuwa kuhakikisha mapato yanayopatikana katika sekta hiyo yanajulikana wazi kwa wananchi bila kificho.Hivyo  Serikali na kampuni za madini yanawajibika kutoa taarifa zake kwa umma ili ufahamu kilichopatikana na hatimaye wataweza kuhoji ni kwa namna gani wanafanufaika na rasilimali hizo.
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipo ya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16 leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mwenyekiti wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi wa Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini Mafuta na Gesi Asilia nchini Tanzania(TEITI), Augustina Rutahiwa akizungumzia mchakato ulivyofanyika ili kupata ripoti iliyonzuri wakati wa uzinduzi wa ripoti ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipoya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila akizungumzia serikali ivyojipanga kulinda madini ya hapa nchini kuwanufaisha hasa wazawa wakati wa mkutano wa uzinduzi wa ripoti ya nane ya TEITI uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Msimamizi wa kujitegemea, Symphorian Malingumu akiwasilisha ripoti ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipo ya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16 leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ripoti ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipo ya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16 leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila pamoja na baadhi ya wajumbe kutoka Makampuni, Asasi za Kiraia na Taasisi za Serikali wakiwa wameshika ripoti ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipo ya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16  mara baada ya kuzinduliwa leo.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe kutoka Makampuni, Asasi za Kiraia na Taasisi za Serikali walioshiriki katika mchakato wa ripoti  ya nane ya TEITI  ya ulinganishi wa Mapato ya Serikali na Malipoya Kampuni za Madini, Mafuta na Gesi asilia kwa mwaka wa fedha 2015/16 leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

USHINDI DHIDI YA YANGA, MANARA AWASHUKURU MASHABIKI

$
0
0
 Assalaam Aleikum.

Salaam zangu za Mei Mosi

Kwanza sote tumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma anaendelea kutupa uhai na uzima hadi siku ya leo.
Hakika pumzi hii ndio inatufanya tufurahi na kuhuzunika pamoja,pia ndio inayotufanya tuweze kuandika na kusoma maandiko mbalimbali ikiwemo andishi hili dogo

Jana pale uwanja wa taifa palifanyika mechi kubwa kabisa ktk ukanda huu wa Afrika Mashariki. Simba na Yanga zote za hapa jijini Dar.

Sio vyema kurejea kuwapa matokeo ila Alhamdulillah klabu yangu ya Simba imefanikiwa kushinda na kujisogeza karibu kabisa na ubingwa wa ligi kuu nchini

Nimeandika kujisogeza kwa kuwa bado hatujatwaa ubingwa.kwa sasa tunahitaji points tano tu ili tuweze kutawazwa ubingwa huu unaosubiriwa kwa hama na washabiki wote kote nchini

Kiukweli hzi points tunazohitaji tutazisaka kwa tahadhari zote na kwa kutambua kiu ya wanasimba.. tutaingia kwenye michezo ilobaki kwa nguvu kubwa na kwa umakini wa hali ya juu,sambamba na kuwaheshimu wapinzani wetu

Ukiachana na hayo nna vitu vwili very special nataka kuvisema hapa

Kwanza ni shukran kwa washabiki wetu..ktk maisha yangu yote nilioishi sijapata kuona washabiki kama wa Simba..
Ni watu wasikivu mno na wenye subira na upendo wa hali ya juu,ni watu wanaopenda futboll halaf ndio timu yao,wana ustaarabu uliopitiliza na wenye mapenzi yasio na shaka kwa klabu yao,

Kwenye ustaarabu huwa natolea mfano wa kitendo cha kutoa back pass kwa mchezaji Hassan kesi wakati akiichezea Simba kwa Donald Ngoma wa Yanga na kutufunga goli la kizembe zaid ktk historia ya derby hii

Inawezeka kabisa ilikuwa ni bahati mbaya,ila kilichostaajibisha muda mchache ujao mchezaji huyo alihamia Yanga tena kwa maneno mabaya ya dharau na kebehi..naapa Wallah kitendo kile ingekuwa kwa wenzetu kessi angeuhama mji huu na kurudi Morogoro (tamka Mrogoro)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

NAIBU WAZIRI NDUGULILE AZINDUA BODI MPYA YA USHAURI WA HOSPITALI ZA WATU BINAFSI

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile  akizindua Mwongozo wa viwango vya Msingi kwa vituo vya kutolea huduma za Afya katika ukumbi wa LAPF leo Jijini Dodoma.Kushoto kwake ni Msajili wa Hospitali Binafsi Dkt. Pamela Sawa.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akizindua kanuni za sheria ya uongozi wa hospitali za watu binafsi katika ukumbi wa LAPF leo Jijini Dodoma.Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara hiyo Dk Otilia Gowele na Kulia ni Msajili wa Hospitali Binafsi Dkt. Pamela Sawa.
 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akizindua Mwongozo wa viwango vya Msingi kwa vituo vya kutolea huduma za Afya katika ukumbi wa LAPF leo Jijini Dodoma. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara hiyo Dk Otilia Gowele na Kulia ni Msajili wa Hospitali Binafsi Dkt. Pamela Sawa.
 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Dkt.Faustine Ndugulile akimkabidhi cheti cha shukrani kwa aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Ushauri wa Hospitali za watu  binafsi Dkt.Mohamed Ally Mohamed katika ukumbi wa LAPF leo Jijini Dodoma.
  Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi mpya ya ushauri wa hospitali za watu binafsi mara baada ya kuizindua leo katika ukumbi wa LAPF leo Jijini Dodoma.
Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO-DODOMA.

IGP SIRRO AFANYA UKAGUZI WILAYANI MUFINDI

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, mhe. Jamhuri William (kushoto) wakati alipofanya ziara ya kikazi na kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo mkoani Iringa leo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akisalimiana na Maofisa wa Polisi wakati alipofanya ziara ya ukaguzi na kuzungumza na Maofisa na askari wa wilaya ya Mufindi mkoani Iringa leo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na askari wa vyeo mbalimbali wilayani Mufindi mkoani Iringa leo, wakati akiwa kwenye ziara ya ukaguzi pamoja na kuona changamoto walizonazo askari wa Jeshi hilo na kuwataka kufanyakazi kwa kuzingatia sheria na taratibu. Picha na Jeshi la Polisi

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA ULIVYADHIMISHA SIKU YA MUUNGANO

$
0
0
Mhe. Baraka Luvanda (kulia), Balozi wa Tanzania nchini India akimpokea Mhe. Shri Vijay Goel, Waziri wa Nchi, Masuala ya Bunge na Takwimu wa India katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Tanzania iliyofanyika jijini New Delhi tarehe 26 Aprili 2018. 
Mhe. Baraka Luvanda (kulia), Balozi wa Tanzania nchini India akiwa katika mazungumzo na Mhe. Shri Vijay Goel, Waziri wa Nchi, Masuala ya Bunge na Takwimu wa India kabla ya kuanza rasmi kwa hafla ya kuadhimisha Siku ya Muungano wa Tanzania. 
Balozi Luvanda akiwahutubia washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Muungano wa Tanzania.
Balozi Luvanda akigongesheana glasi na Waziri wa Nchi, Masuala ya Bunge na Takwimu wa India ikiwa ni ishara ya kuutakia mema Muungano wa Tanzania uweze kudumu milele. 
Mhe. Shri Vijay Goel, Waziri wa Nchi, Masuala ya Bunge na Takwimu wa India (katikati) akionesha jarida kuhusu miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini India na kuzinduliwa rasmi katika hafla hiyo. 
Hafla ikiendelea 
Mhe. Baraka Luvanda (kulia), Balozi wa Tanzania nchini India akimkabidhi zawadi ya kinyago Mhe. Shri Vijay Goel, Waziri wa Nchi, Masuala ya Bunge na Takwimu wa India. 
Picha ya pamoja. 

DK. KIGWANGALLA ATOA OFA YA MAPUMZIKO YA FUNGATE YA ALI KIBA KATIKA HIFADHI ZA WANYAMAPORI

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa ofa maalum kwa Mwanamuziki, Ally Kiba, mke wake na wasaidizi wake ambao ni mdogo wake Abdu Kiba na mkewe kupumzika katika Hifadhi ya Taifa atakayoichagua wakati wa fungate yake ili aweze kufurahi vivutio vya utalii vilivyopo na hivyo kuhamasisha utalii wa ndani. Ametoa ofa hiyo jana wakati wa harusi ya msanii huyo iliyofanyika katika ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa sherehe hiyo na Waziri wa Afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mbunge wa Viti Maalum, Neema Mgaya.
 Picha ya pamoja katika sherehe hiyo iliyojumuisha Bwana Harusi, Ali Kiba, mke wake na wapambe wake na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali akiwemo Mbunge wa Viti Maalum, Mama Salma Kikwete, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimum, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mwenyekiti wa UVCCM Kheri James.
Picha ya pamoja ya maharusi na viongozi wa chama na Serikali pamoja na Gvana wa Jiji la Mombasa, Rashid Bedzima (wa pili kulia).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiteta jambo na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na  Wanamuziki, Ommy Dimpoz na Hamisi Mwanjuma MwanaFA.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifurahia jambo na Msemaji wa Klabu ya Simba, Haji Manara na Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa sherehe hiyo.

Coclyin Usibadilike - (Official Video)

TANZANIA KUFAIDIKA NA MRADI MAENDELEO YA KIJAMII KUTOKA KOREA KUSINI

$
0
0
 Na Mwandishi Wetu- Dodoma
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inategemea kunufaika na mradi maalum kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ lenye makazi yake nchini Korea ya Kusini kuhusu utoaji wa mafunzo ya kuiwezesha jamii kuwa na tabia, fikra na mtazamo  chanya ili kuwa na ari na hamasa ya kufikia mabadiliko ya kweli na endelevu katika kujiletea maendeleo ya jamii yenyewe na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika Kikao kati ya Serikali na Shirika hilo Katibu Mkuu Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga amesema  kuwa Mradi huu ni muhimu sana katika jamii ya watanzania kwani utasaidia kubadilisha fikra za watanzania katika kukuza ari na raghba ya kujiletea maendeleo wenyewe katika maeneno yao.

Bibi Sihaba ameongeza kuwa elimu hii itasaidia kuimarisha fikra chanya kwa watanzania wote kujitambua na kuona kuwa maendeleo ya kweli na endelevu yanatokana na ufahamu, uelewa na utashi wa wananachi waliojitoa kufanya kazi za maendeleo kwa kushirikiana na Serikali yenyewe ili kutatua changamoto zilizopo na hivyo  kujifikia maendeleo jumuishi kwa manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Aidha, akizungumza wakati akitoa elimu hiyo kwa ujumbe wa Menejimenti ya Idara kuu Maendeleo ya Jamii, Katibu Mkuu wa Shirika la ‘International Youth Fellowship’ Dkt. Hun Mok Lee amesema kuwa mabadiliko ya fikra ni muhimu katika mendeleo ya Taifa lolote na kama Tanzania inataka kuendelea zaidi inabidi ianze kutoa elimu itakayosaidia kuwajenga na kubadili fikra za watoto na vijana kuhusu utashi wao wa kutatua vikwazo na changamoto ili kujiletea maendeleo yao wenyewe.
  Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akizungumza na wadau wa kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini wakati walipofika katika Ofisi za Wizara Jijini Dodoma kuwasilisha Mpango maalum kuhusu Umuhimu wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo.
 Katibu Mkuu  Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini Dkt. Hun Mok Lee (kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika hilo hapa Tanzania Jeon Hee Young wakitoa mafunzo kwa Menejimenti ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii kuhusu uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo Jumuishi. 
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Bi. Magreth Mussai akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Wizara na wadau wa Maendeleo kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga na Menejimenti yake wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo wa Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika kujiletea Maendeleo Jumuishi kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
 Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TAARIFA KWA UMMA

AZAKI TANO ZA KIRAIA WAPONGEZA RIPOTI YA NANE YA TEITI, WASHAURI FEDHA ZA MADINI ZITUMIKE KULETA MAENDELEO

$
0
0
 Na Said Mwishehe, Blog ya jamii
AZAKI tano kwenye Kamati ya Taasisi ya Uhamasishaji, Uwazi na uwajibikaji katika rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia nchini Tanzania(TEITI) zimpongeza Ripoti ya Nane ya taasisi huku wakishauri fedha zinazopatikana kwenye madini zitumike kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kesho.

Kwa mujibu wa Azaki hizo zisizo za kiserikali ambazo ni Publish What You Pay(PWYP-TZ), Gender and Disability , Interfaith base, Trade Union na Corventional NGO,s ambazo si za kiserikali

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu ripoti hiyo ambayo imezinduliwa rasmi na Waziri wa Madini Angella Kairuki, Mjumbe wa TEITI kutoka Azaki hizo za kiraia anayewakilisha Taasisi za kidini, Grace Masalakurangwa amesema baada ya kuzinduliwa kwa ripoti hiyo ni vema ikafikishwa kwa umma.

Ambapo wamefafanua ni vema pia ripoti hiyo ikawekwa kwenye lugha rahisi na nyepesi kueleweka na kwa kufanya hivyo itasaidia watu wengi zaidi na wa makundi mbalimbali kuichambua.

"Tumewaita waandishi wa habari kwa lengo la kuwaelezea namna ambavyo tumefurahishwa na kupongeza  ripoti ya TEITI ambayo imezinduliwa leo. Ombi letu kwao ni vema ripoti hiyo ikawekwa kwenye lugha rahisi ili iweze kuchambuliwa," amesema Masalakurangwa kwa niaba ya azaki hizo ambazo zimesisitiza uzinduzi ni jambo moja na wananchi kutoa maoni yao ni hatua nyingine.

Pia ametoa ombi sasa umefika wakati wa Serikali kutunga kanuni kuhusu sekta ya madini ingawa wanatambua sheria ya madini ya mwaka 2015 ipo lakini wanaamini kukiwa na kanuni kutasaidia kwani sheria hiyo inazungumza kwa upana zaidi.

Akifafanua kuhusu fedha ambazo zinapatikana kwenye eneo la madini, mafuta na gesi asilia ni vema Serikali ikahakikisha zinatumika katika kufanya mambo yenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho na kueleza wao ni miongoni mwa wajumbe wa kamati ya TEITI lakini wanayo nafasi ya kuchambua na kutoa maoni yao kuhusu ripoti ambayo imezinduliwa.
 Mjumbe wa TEIT kutoka Asasi za Kiraia anayewakilisha Taasisi za Kidini, Grace Masalakurangwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti iliyozinduliwa na  Waziri wa Madini, Angellah Kairuki leo Jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe kutoka PWYP-TZ, Petro Ahham akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uwajibikaji wa serikali kwenye rasilimali za Tanzania ili kuwanufaisha wazawa.

Benki ya Exim yaendelea kushika nafasi ya tano

$
0
0
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Exim Bank Tanzania, Selemani Ponda akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu matokeo ya benki ya mwaka 2017. Kushoto kwake ni Kaimu Afisa wa operation David Lusala na Kulia ni Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha Issa Hamisi.

BENKI ya Exim imeendelea kubaki katika nafasi ya tano kwa ukubwa ikiwa na rasilimali zenye thamani ya shilingi trilioni 1.6 zitokanazo na ukuaji wa amana kutoka kwa wateja.

Ikiwa ni Benki ya kwanza nchini kufungua Benki tanzu nje ya nchi, Benki ya Exim imeendela kufanya vizuri pia huko ughaibuni. Benki tanzu ya Jibuti ni ya nne kwa ukubwa nchini humo wakati ile ya Komoro ni ya pili visiwani humo. Jibuti ilipata faida ya shillingi billioni 6.5 wakati Komoro walipata faida ya shilingi bilioni 4.8.  Marejesho ya mtaji kwa benki hizo yamekuwa juu zaidi ya kiwango kilichotarajiwa kwa asilimia 50 na 40 kwa Jibuti na Komoro.

Nchini Uganda, ambapo kuna Benki tanzu pia, Benki imeendelea kufanya vizuri na kupunguaza kiwango cha hasara. “Ni mataraji yetu kuwa Uganda itafuata nyayo za Jubuti na Komoro, hivyo kuanza kutengeneza faida kubwa mwaka 2018”, alisema Kaimu Mkurugenzi mkuu, Bwana Selemani Ponda.

Katika mahesabu ya mwaka 2017, faida jumla itokanayo na shughuli za kibiashara nchini Tanzania ziliathirika kidogo kutokana na  mikopo mibaya na pia taratibu mpya za kiuhasibu lenye kuhitaji tengo zaidi kwenye mikopo mibaya. Hata hivyo, matokeo ya kifedha ya biashara mbalimbali katika utendaji nchini Tanzania ukiondoa kuharibika kwa mikopo, Benki imeweza kupata faida ghafi  ya shilingi bilioni 39 kutokana na ongezeko la tengo kwenye mikopo mibaya faida ilishuka mpaka shilingi bilioni 9.6.

“Benki imejivunia kuwa na benki tanzu nje ya nchi, hivyo kuwa na wigo mpana wa kutengeneza faida kutokana na hali nzuri ya uchumi katika nchi husika”, aliongeza kaimu mkurugenzi mkuu, bwana Selemani Ponda.

Exim itafuta mikopo yenye mingine zaidi robo ya kwanza ya mwaka 2018 kufuatana na taratibu mpya za kibenki na kufanya uwiano wa mikopo mibaya kuboreka kutoka asilimia 14.63 mpaka asilimia 8.95. Kaimu mkurugenzi mtendaji bwana Selemani Ponda amethibitisha jitihada za Benki za kuendelea kuboresha ubora wa mikopo kwa lengo la kufikia uwiano wa chini ya asimlimia 5% mpaka mwisho wa mwaka huu.

Bring a friend to DICOTA convention

$
0
0
DICOTA understands the importance of friendship for attendees participating in it's convention. Because of that, this year DICOTA offers discounted convention rates, so that everyone can bring a friend to the 2018 Seattle Convention.

To register for the bring a friend discount offer, visit here.

Offer ends May 15th

SPIKA NDUGAI ATEMBELEA KIWANDA CHA ASASI KILICHOPO MKOANI IRINGA

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai akiendelea na ziara yake kiwandani hapo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai akimsikiliza Bw. Fuad Abri Mkurugenzi wa Kiwanda cha maziwa cha ASAS wakati akitoa maelezo alipokembelea kiwanda hicho na kukagua uzalishaji pamoja na shughuli zingine za uzalishaji wa Bidhaa mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo leo mjini Iringa katikati ni MNEC wa CCM mkoa wa Iringa Bw. Salim Abri na wa pili kutoka kulia ni Mbunge wa jimbo la Kilolo Mh. Venance Mwamoto.
Fuad Abri Mkurugenzi wa Kiwanda cha maziwa cha Asas akitoa maelezo wa kwa Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai wakati alipokembelea kiwanda hicho na kukagua uzalishaji pamoja na shughuli zingine za uzalishaji wa Bidhaa mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo leo Mjini Iringa , Ahmed Salim mmoja wa wakurugenzi wa ASAS na Mbunge wa jimbo la Kilolo Mh. Venance Mwamoto.
ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakiendelea na kazi.
Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai wakati akionyeshwa moja ya bidhaa zinazozalishwa na kiwanda cha ASAS wakati alipokembelea kiwanda hicho na kukagua uzalishaji pamoja na shughuli zingine za uzalishaji wa Bidhaa mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo leo wa pili kutoka kushoto ni MNEC wa CCM Mkoa wa Iringa na anayefuatia ni Ahmed Salim Mmoja wa wakurugenzi wa ASAS.
MNEC wa CCM mkoa wa Iringa Bw. Salim Abri akizungumza na Spika wa Bunge ofisini kwake wakati Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai alipotembelea kiwanda cha Maziwa cha ASAS leo.


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

ESRF, Ubalozi wa Sweden na UDSM waandaa Mdahalo wa Uchumi Jumuishi

$
0
0
TANZANIA itahitaji kutengeneza mkakati mpya wa maendeleo na kuachana na falsafa za zamani kama itataka kufikia ustawi na kuwa nchi yenye kipato cha Kati.
Mkakati huo katika; masoko, rasilimali na uwezeshaji unatakiwa kuwezesha sera za maendeleo zilizo endelevu kwa kuangalia zaidi changamoto tofauti za maendeleo na kuzikabili kabla ya kuzitumia kubadili harakati za maendeleo.
Kauli hiyo imo katika mdahalo uliofanyika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na kuongozwa wataalamu wa uchumi.
Walisema katika mdahalo huo kwamba mkakati wa zamani kuhusu maendeleo kwa kutegemea kuzalisha bidhaa na kuziuza nje una vikwazo vingi hasa katika uzalishaji kutokana na masuala ya teknolojia na hivyo mkakati utakaokuwa jumuishi, unaoratibu kilimo, madini na huduma unaweza kuwezesha kukua kwa uchumi kama ilivyokuwa katika mkakati wa zamani wa uzalishaji kwa ajili ya kupeleka nje.
Wamesema katika mkakati huo mpya serikali inatakiwa kufanya wajibu mkubwa kufanya mabadiliko ya kimfumo na kimkakati kuelekea uchumi jumuishi ambapo kila mwananchi atashiriki.
Uchumi huo hautategemea uzalishaji wa viwandani pekee bali uchumi wa kisasa unaozingatia huduma ambao katika awamu ijayo kilimo cha kisasa nchini Tanzania kitakuwa sehemu ya mkakati huo.
Wanazuoni hao wamesema kwamba mafanikio ya kuwa na uchumi jumuishi kwa nadharia za sasa zinategemea mpango mkakati wa maendeleo wenye kuangalia mambo mengi yatakayowezesha kuwa na ukuaji jumuishi, unaoshirikisha na kuzingatia uwiano wa masoko, serikali na jamii.
Walisema taratibu hizo mpya duniani zitasaidia kuwa na uchumi wenye mafanikio unaobadili maisha ya watu kwa kuangalia changamoto mbalimbali ikiwamo vifo na kutengeneza mfumo mpya wenye kuzingatia uwezo na mahitaji.    
 Profesa wa Uchumi wa Chuo Kikuu Cornel, Ithaca na aliyekuwa mchumi wa Benki ya Dunia  Prof. Kaushik Basu akiwasilisha mada kuhusu misingi ya maendeleo kwa kuzingatia sosholojia na saikolojia ya watu wakati wa mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
 Aliyekuwa mchumi wa zamani wa Benki ya Dunia kutoka Chuo Kikuu cha Columbia, Prof. Joseph Stiglitz akiwasilisha mada kuhusu kutoka uzalishaji unaolenga soko la nje hadi ukuaji uchumi jumuishi wa karne ya 21 kwa taifa la Tanzania wakati wa mdahalo uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
 Mwenyekiti  wa mdahalo kutoka kigoda cha Mwl. Julius Nyerere, Prof. Benno Ndulu akiongoza mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mkuu wa Idara ya Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jehovaness Aikaeli akitoa neno la shukrani kwa washiriki wa mdahalo kuhusu uchumi  jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akizungumza na kituo cha Habari cha ITV kuhusu mdahalo huo na manufaa yake kwa Tanzania na kwa sekta ya uchumi wakati wa mdahalo kuhusu uchumi  jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Baadhi ya  washiriki wakitoa maoni ya mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Sehemu ya washiriki wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Meza kuu katika picha ya pamoja na wadau mara baada ya kumalizika kwa mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa UDSM mara baada ya kumalizika kwa mdahalo kuhusu uchumi jumuishi uliowezeshwa na ESRF kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Sweden uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

PAMOJA NA MVUA KUBWA KUNYESHA WANANCHI WAENDELEA KUJITOKEZA KUSAJILIWA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0
Usajili wa Vitambulisho vya Taifa mkoani Morogoro umeendelea kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kusajili pamoja na changamoto kubwa ya mvua ambayo imeharibu miundombinu na kufanya baadhi ya maeneo kutofikika kwa kirahisi.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sanganjelu Kata ya Madege wilayani humo Afisa Usajili Wilaya ya Gairo Ndg. Godwill Mwamanga amewahimiza wananchi wanaoshiri zoezi hilo kuwa makini wanapojaza taarifa zao kwa kuhakikisha wanajaza taarifa sahihi naza kweli ili kuepukana na usumbufu hapo baadae.

‘Nawasihi sana muwe wakweli kwenye taarifa zinazohusu umri, makazi na uraia wenu ili taarifa zitakazo kusanywa zikajenge mfumo madhubuti wa Utambuzi wa Taifa wenye taarifa sahihi za watu” alisisitiza

Kwa sasa zoezi la Usajili linaendelea katika Kata ya Madege na Lesha ambapo Kata zingine za Msingisi, Rubeho, Chanjale, Iyogwe, Italagwe na Mkalama zimekamilisha zoezi. Kata za Nongwe, Gairo, Chagongwe, Chakwale, Kibedya, Idibo, Nongwe, Mandege, Chagongwe, Ukwamani, Magoweko na Ngiloli zitaendelea na zoezi kwa kuzingatia ratiba ya usajili iliyotangazwa na Mamlaka.

Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa 21 inayoendelea na zoezi la Usajili na Utambuzi wa Watu lenye kulenga kuwapatia wananchi Vitambulisho vya Taifa.
Wananchi wa Kata ya Madege wakikatiza barabara kubwa ya Taragwe iliyojaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha; kuelekea kwenye vituo vya Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwenye Kijiji cha Sanganjelu wilani Gairo.

Wananchi wa kijiji cha Iyogwe wakisikiliza maelekezo ya utaratibu wa kusajiliwa kutoka kwa Msimamizi wa kituo ambaye hayupo pichani.


Ndg. Juma Ally mkazi wa Kata ya Iyogwe Wilaya ya Gairo – Morogoro akipigwa picha na kuchukuliwa alama zake za kibaiolojia wakati zoezi la Usajili likiendelea.


Wananchi wakazi wa kijiji cha Kilama wilaya ya Gairo mkoani Morogoro wakisikiliza kwa makini majina yao yakisomwa kuelekea kwenye chumba cha Usajili ikihusisha hatua ya kupigwa picha, kuweka alama za vidole na saini kileketroniki kwa kutumia mashine maalumu za kukusanya taarifa.


Afisa Usajili Wilaya ya Gairo Ndg. Godwill Mwamanga akizungumza na wananchi wakati wa kukagua maendeleo ya shughuli za Usajili kwenye kijiji cha Ngayaki kata ya Leshata.

FAO NA USAID TANZANIA WAIPIGA TAFU SERIKALI KUKINGA KICHAA CHA MBWA

$
0
0

Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (wa tatu kushoto) akizungumza jambo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) Fred Kafeero (katikati) na Mwakilishi Shirika la Misaada la Marekani (USAID), Dk. Patrick Swai wkati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa chanjo ya Kichaa cha mbwa kwa kwa ajili ya kuzuia ugonjwa huo kwa Wilaya ya Moshi iliyopo mkoani Kilimanjaro, ambayo imeripotiwa kuwa na tatizo hilo hivi karibuni. Hafla hiyo imefanyika wizarani hapoleo Aprili 30 2018 jijini Dar es Salaam. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)

Kiongozi wa Timu wa FAO, Florunso Fesina akitoa mada kuhusu utafiti uliofanywa na shirika hilo kwa madhara yasababiswayo na mifugo kutopewa chanjo hasa mbwa na paka wakati wa hafla ya shirika hilo kukabidhi msaada wa chanjo ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa kwa wizara ya Mifugo na uvuvi jjini Dar es Salaam leo.

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula na kilimo Duniani (FAO) Fred Kafeero (wa tatu kulia) na Mwakilishi shirika la Misaada la Marekani (USAID), Dk. Patrick Swai (wa pili kulia) wakionesha moja ya bango litakalotumika wakati wa tiba na na chanjo katika hafla ya kukabidhi msaada wa chanjo ya Kichaa cha mbwa kwa Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (wa tatu kushoto) kwa ajili ya kuzuia ugonjwa huo kwa Wilaya ya Moshi iliyopo mkoani Kilimanjaro, ambayo imeripotiwa kuwa na tatizo hilo hivi karibuni. Hafla hiyo imefanyika wizarani hapo jana jijini Dar es Salaam. Pamoja nao ni watendaji waandamizi wa wizara

Sehemu ya washiriki wa hafla hiyo wakifuatilia mada.

Kiongozi wa Timu wa FAO, Florunso Fesina akitoa mada kuhusu utafiti uliofanywa na shirika hilo kwa madhara yasababiswayo na mifugo kutopewa chanjo hasa mbwa na paka wakati wa hafla ya shirika hilo kukabidhi msaada wa chanjo ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa kwa wizara ya Mifugo na Uvuvi jjini Dar es Salaam leo. 

WANANCHI WAHAMASISHWA KUWAPELEKA WATOTO WAO KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

SERIKALI mkoani Kigoma imewataka viongozi mbalimbali kuwa mfano katika zoezi la kuhamasisha wananchi kuleta watoto wao wenye umri chini ya miaka 14 kwenye chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi.

Akizungumza jana Brigedia Jenerali Marko Gaguti ambaye ni mkuu wa wilaya ya Buhigwe kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu , Emmanuel Maganga, wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo kimkoa iliyofanyika wilayana hapa,alisema njia ya kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na kupata chanjo, kutokufanya ngono katika umri mdogo, kubeba ujauzito katika umri mdogo pamoja na kuwa na wanaume zaidi moja.

"Njia ya pili ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini dalili za awali ili kupata matibabu mapema,"alisema .Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mwanamvua Mlindoko alisema katika wilaya yake kuna jumla ya watoto 1325 wenye umri kati ya miaka 9 hadi 14.

Alisema katika wilaya yake inatarajia kutoa chanjo kwa watoto 4974 na kwamba kufikia Desemba mwaka huu watakuwa wametoa chanjo kwa watoto hao kwa asilimia 100.

Diwani wa kata ya Kazuramimba Nuru Kashakali, alisema amejitolea kuzunguka katika shule zote za msingi zilizopo kata yake ili kuwahamasisha watoto hao kujitokeza katika zoezi la kupatiwa chanjo.

Nao baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Uvinza Agustina Nzobanya mkazi wa Kazuramimba alisema yeye atahakikisha Watoto wake wote wanapatiwa Chanjo na kuendelea kuhimiza wananchi kuwaleta watoto wao ili kuepuka gharama zinazoweza kujitokezapindi wapatapo Ugonjwa huo.
Brigedia Jenerali Marko Gaguti ambaye ni mkuu wa wilaya ya Buhigwe kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia jenerali mstaafu , Emmanuel Maganga, akizindua chanjo ya kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi mapema jana wilayani humo.
 Brigedia Jenerali Marko Gaguti ambaye ni mkuu wa wilaya ya Buhigwe kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu , Emmanuel Maganga, akizungumza jambo mbele ya wananchi (hawapo pichani),mapema jana wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi

Mahusiano mazuri kati ya mwajiri na mfanyakazi kunaleta tija –Mwalwis

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Mahusiano mazuri kati ya wafanyakazi na waajiri ndio kunafanya kazi kufanyika na nchi kuweza kukua kiuchumi kutokana na uzalishaji unaofanyika.

Hayo aliyasema Mkurugenzi Msaidizi  wa Idara ya Kazi, Andrew Mwalwis wakati kutoa zawadi kwa wafanyakazi wa Kiwanda cha Lake Cement kilichopo Kimbiji jijini Dar es Salaam, amesema kuwa kuendelea kwa kiwanda kunatokana na wafanyakazi kuwa na ari ya kufanya kazi.

Amesema kuwa kama kuna migogoro katika kiwanda hakuna uzalishaji ambao unaweza kupatikana na mwisho wa siku kiwanda kinafungwa.

Mwalwis amesema kuwa waajiri lazima wafuate sheria za nchi katika kulinda masilahi ya wafanyakazi na ndipo tunaweza kujenga uchumi wa viwanda pamoja na kusaidia watanzania katika suala la ajira.

Nae Afisa Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Utawala wa Lake Cement, Giridhar Jadhao amesema kuwa wamejiwekea utaratibu wa kutoa zawadi kwa wafanyakazi kila siku ya wafanyakazi ili kuongeza tija na wengine kuweza kufanya vizuri.

Nae Afisa Rasilimali wa Kiwanda hicho, Julieth Domel amesema kuwa wafanyakazi wamekuwa na ari ya kufanya kazi na kufanya kiwanda kuendelea kuwepo.

Amesema kuwa ataendelea kuhakikisha wafanyakazi na wanaendelea kuwa  na moyo wa kufanya kazi na kiwanda kuendelea kutoa huduma.
 Mkurugenzi wa Idara ya Kazi Andrew Mwalwis akizungumza katika kiwanda cha Lake Cement wakati wa utoaji wa zawadi kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho, Kimbiji jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Utawala wa Lake Cement, Giridhar Jadhao akizungumza kuhusiana na wafanyakazi wa kiwanda hicho wanavyojitoa katika kufanyakazi ,Kimbiji jijini Dar es Salaam.
 Afisa Rasilimali Watu wa Kiwanda cha Lake Cement, Julieth Domel akizunngumza kuhusiana na wafanyakazi kufuata sheria za kazi.
 Mwenyekiti wa Tawi la Wafanyakazi wa Kiwanda hicho, Emmanuel Mayunga akizungumza kuhusiana na masilahi ya wafanyakazi katika kiwanda hicho na uchangiaji katika mifuko ya hifadhi ya Jamii.
 Afisa Rasilimali wa Watu  wa Lake Cement, Ahmed Mustafa akipokea zawadi kwa niaba ya mfanyakazi mwenzake katika utoaji zawadi kwa wafanyakazi wa kiwanda cha Lake Cement.
 Afisa Usalama Mahala Pakazi katika Kiwanda cha Lakr Cement. Amina Likati akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wa mwaka katika kiwanda hicho.
Sehemu ya wafanyakazi wakati utoaji wa kiwanda cha Lake Cement
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images