Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110079 articles
Browse latest View live

MHE SAMIA SULUHU AHUDHURIA MKUTANO WA SADC TROIKA EXTRA JIJINI LUANDA, ANGOLA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amemuwakilisha Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC aliyemaliza muda wake kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda umefanyika hapa Luanda, leo tarehe 24 Aprili, 2018. 
Mkutano huu umeitishwa baada ya mashauriano kati ya Mheshimiwa Dkt. Cyril Ramaphosa, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini na Mwenyekiti wa SADC na Mhe. João Lourenço, Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikino ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC Mkutano huu umetanguliwa na kikao cha Mawaziri ambacho kilifanyika jana tarehe 23 April 2018. 
Mkutano huu ulihusisha nchi wanachama sita tu wa SADC Double Troika na Viongozi wafuatao walihudhuria, Mhe. Dkt. Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa Summit, Mhe. João Lourenço , Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama – (SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation),Mhe. Hage Geingob, Rais wa Namibia na Makamu Mwenyekiti wa Summit, Mhe. Edgar Lungu, Rais wa Zambia na Makamu Mwenyekiti wa SADC Organ, Mfalme Mswati III, Mfalme wa Swaziland na Mwenyekiti wa Summit anayetoka; Mheshimiwa Joseph Kabila Kabange, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Mheshimiwa Thomas Thabane, Waziri Mkuu wa Lesotho walialikwa na walihudhuria.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda, Luanda Angola.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja Wakuu wa Nchi na Serikali muda mfupi kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda, Luanda Angola. 
Wengine pichani kutoka kushoto ni Mheshimiwa Thomas Thabane, Waziri Mkuu wa Lesotho  Mhe. Edgar Lungu, Rais wa ZambiaRais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Rais Joseph Kabila, Mfalme Mswati IIIMfalme wa Swaziland  Mhe. Dkt. Cyril Ramaphosa Rais wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa Summit, Mhe. João Lourenço  Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama – (SADC Organ on Politics, Defence and Security Cooperation),   Mhe. Hage Geingob Rais wa Namibia na Makamu Mwenyekiti wa Summit
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifuatilia kwa makini  Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda, Luanda Angola. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza mara baada ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili wa SADC kuhusu hali ya Usalama katika Kanda kumalizika mjini Luanda Angola. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

TPDC KUWANUFAISHA WANANCHI KWA GESI ASILIA MAJUMBANI

$
0
0
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi mradi wa uunganishaji wa gesi asilia kutoka katika bomba kubwa la gesi asilia linalomilikiwa na TPDC kwenda kwenye bomba dogo la usambazaji wa gesi asilia kutoka Ubungo hadi Mikocheni ambalo nalo linamilikiwa na TPDC ili kuongeza kiasi cha gesi asilia katika bomba hilo kwa lengo la kuwafikia watumiaji wengi zaidi. 

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Mhandisi Kapuulya Musomba akikabidhi jukumu la ujenzi wa mradi wa uunganishwaji wa gesi asilia kutoka kwenye bomba kubwa la kusafirisha gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam katika eneo la Valvu namba 15 (Block Valve Station-BVS) ambapo ndipo bomba hilo litarajiwa kujengwa hadi eneo la Ubungo Maziwa litakapounganishwa na bomba dogo la usambazaji wa gesi asilia kuelekea Mikocheni Dar es Salaam. 

“Leo ni siku kubwa sana kwetu kama Kampuni ya Mafuta ya Taifa tunapokabidhi rasmi jukumu la ujenzi wa miundombinu ya kutoa gesi asilia kutoka kwenye bomba letu kubwa kwenda kwenye bomba letu dogo la usambazaji wa gesi asilia kazi ambayo itafanywa na kampuni ya SINOMA ambayo faida yake kubwa ni kulipa uwezo wa kubeba na kusambaza gesi nyingi zaidi itakayoruhusu uunganishwaji zaidi wa gesi asilia kwa watumiaji wapya katika maeneo yote ambayo bomba hilo linapita yaani Ubungo, Sinza, Chuo Kikuu, Survey, Mwenge na Mikocheni” alifafanua Kaimu Mkurugenzi. 

Akizungumzia wanufaika wa mradi huo pindi utakapokamilika, ndugu Musomba amesema kuwa, pamoja na kuendelea kusambaza kwa watumiaji wa zamani ambao ni MM I, MM II, MM III, TanPack na Iron and Steel wateja wapya watakaonufaika ambao tayari wameshakubaliana ni Coca Cola kwanza Limited na BIDCO na nyumba 70 katika awamu ya kwanza na kwamba wanatarajia kuunganisha kwa viwanda zaidi vitakavyokuwa tayari kwa muda wowote. 

Aidha akieleza kuhusu utaratibu wa uunganishwaji wa gesi asilia kwa watumiaji Mhandisi Musomba ameeleza kuwa, “Utaratibu ni wa kawaida sana kikubwa mteja tarajiwa anatakiwa kuwasilisha barua ya maombi ya gesi asilia kisha wataalam kufanya utafiti wa namna ya kumuunganishia mteja gesi hiyo na kwa upande wa watumiaji wa majumbani tunashauri pia nyumba kadhaa kuungana pamoja na kuleta barua kisha taratibu za kiutalamu za namna ya kuwafikishia gesi asilia zifanyike.” 

Kwa upande wake Meneja Mkuu Msaidizi wa SINOMA, Lu Xiaoqiang ambao ndio Wakandarasi walioshinda zabuni ya ujenzi wa mradi huo amesema kuwa, “Leo ni siku ya furaha kwa kuwa tumeweza kupata nafasi ya kutekeleza mradi wa TPDC wa ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka eneo la Ubungo bomba ambalo tunaamini litasaidia kukuza uchumi wa nchi nzuri ya Tanzania kwa kusambaza nishati viwandani na majumbani.” 
Akizungumzia gharama za matumizi ya gesi asilia majumbani Mhandisi Musomba amefafanua kuwa, “Matumizi ya gesi asilia ni ya gharama nafuu kulinganisha na mkaa na gesi za mitungi-LPG ambapo kwa mtumiaji wa gesi za mitungi mfano wa Kilo 15 ambayo itatumika kwa mwezi mmoja kama akitumia gesi asilia atatumia hadi miezi miwili na hivyo kuokoa karibu nusu ya gharama ya matumizi ya nishati majumbani lakini pia gesi asilia ni nyepesi kuliko hewa na hivyo kuwa salama zaidi kwa matumizi hata pale inapovuja kwa kuwa hupotea hewani.

” Jukumu la kusambaza gesi asilia ni la msingi kwa maeneo ya uchumi imara wa viwanda na hivyo TPDC inaendelea kufanya tafiti za kitaalamu za usambazaji wa gesi asilia katika maeneo mengine ya nchi yakiwemo Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Tanga na Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba akieleza kwa kina Mradi Mpya wa Kuunganisha gesi asilia kutoka bomba kubwa hadi kwenye bomba dogo la Ubungo Mikocheni mradi ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miezi miwili. Piv
Meneja Mkuu Msaidizi wa SINOMA, Lu Xiaoqiang akielza kwa waandishi wa habari namna watakaovyotekeleza ujenzi wa Miundombinu hiyo kwa ufanisi na wakati kadiri ya masharti ya mkataba. Pembeni yake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Ubungo Tanesco, Sophia Fitina akielezea jinsi walivyoupokea mradi huo tokea umeingia katika eneo lao.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mhandisi Kapuulya Musomba (wa tatu toka kushoto) akiwa na  Meneja Mkuu Msaidizi wa SINOMA ndugu Lu Xiaoqiang (anayemfuatia Kushoto) pamoja na wafanyakazi wanaotekeleza mradi huo. 

TLS NI CHAMA CHA UMMA KIFANYE KAZI KWA MUJIBU WA SHERIA - JAJI MKUU

$
0
0
Na Lydia Churi, Magreth Kinabo-Mahakama
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) ni taasisi ya Umma na siyo binafsi hivyo amekitaka kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kisheria kwa kushirikiana na Mahakama na kuacha kujiingiza kwenye masuala ya uanaharakati na siasa.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Jaji Mkuu amesema TLS ni chama huru cha kitaaluma kwa kuwa kilianzishwa kwa mujibu wa sheria kufanya kazi kwa manufaa mapana ya Umma.
“Hatuwezi kukubali chama hiki kikajisemea kuwa wao ni chama binafsi na tukakubali...Dhana ya ubinafsi haipo”, alisisitiza Jaji Mkuu.

Alisema jukumu la TLS ni Kuisaidia Serikali na Mahakama kuhusu mambo yoyote yanayogusa sheria, utawala wa sheria na kazi za kisheria na akaongeza kuwa dhana hii ndiyo inayoiunganisha Taasisi hiyo na Mahakama ya Tanzania.

Aidha, Jaji Mkuu amewataka viongozi wa TLS kushirikiana na Mahakama pamoja na Mihimili mingine ya dola  na kuacha malumbano kwenye vyombo vya habari kwa kuwa hayawasaidii kuendeleza chama hiki muhimu kwa wanasheria nchini.
Jaji Mkuu pia amewashauri viongozi wa chama hicho kumuheshimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuwa Sheria na Kanuni zote ni lazima zipitie kwake.
Alisema Mamlaka ya Baraza la Uongozi la TLS katika Kutekeleza Majukumu ya Umma ni kusaidia kuboresha elimu ya sheria na taaluma ya Sheria Tanzania na kuwawezesha wanataaluma wa sheria kupata elimu ya ziada ya sheria kwa kadri mabadiliko yanayotokea nchini na duniani.

Majukumu mengine ya TLS ni pamoja na kuwawakilisha, kuwatetea na kuwasaidia wanasheria Tanzania kuhusu mazingira ya kufanya kazi za kisheria na kuwasaidia wananchi wa Tanzania katika masuala ya kisheria yanayogusa Sheria.

TLS ni Taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria za nchi kabla ya Uhuru na kukubalika kuendelea kuwepo kama Taasisi ya Kisheria kwa malengo ya kuanzishwa kwake kuelekezwa kwenye manufaa ya umma kwa kushirikiana na Mahakama, Bunge, pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chama hiki kilianzishwa kwa Sheria ya Baraza la Kutunga Sheria (Legislative Council) Namba 30 ya 1954 na ni moja ya Sheria nyingi za iliyokuwa Tanganyika kabla ya Uhuru, ambazo kwa mujibu wa Kifungu cha 4 cha Katiba ya Tanganyika  ziliruhusiwa kuendelea kutumika Tanganyika ilipopata Uhuru Disemba 9 mwaka 1961 kama Sheria za Tanganyika huru.

MSANII DIAMOND KUTOA BURUDANI KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI

$
0
0
Msanii nyota wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz, kwa kushirikiana na kampuni ya Coca-Cola ametangaza kuwa ameshiriki kuimba wimbo utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 uitwao Colours. 

Wimbo huo uliotungwa na mwanamuziki Jason Derulo wa Florida, Marekani, Diamond ameshiriki kuweka maudhui ya lugha ya Kiswahili na umetayarishwa na prodyuza Nahreel kwa kushirikiana na maprodyuza kutoka nchi nyingine chini ya udhamini wa kampuni ya Coca-Cola. 

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, amesema anayo furaha kupata fursa ya kushiriki kuimba kuimba wimbo wa mashindano haya makubwa ya kidunia na kuitangaza Tanzania na lugha ya Afrika bila kusahau tasnia ya muziki kwa ujumla. 

“Kwangu hii ni nafasi nyingine ambayo najivunia kuipata ya kutangaza muziki wa kitanzania sambamba na lugha ya Kiswahili kwa kuwa sehemu niliyoshiriki kuimba nimetumia lugha ya taifa la Tanzania ambayo inazidi kupata umaarufu mkubwa duniani”alisema Diamond.

Kwa upande wake Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola ambayo ni moja ya mdhamini wa mashindano haya makubwa ya soka duniani inayo furaha kwa msanii kutoka nchini Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano haya. “Tuna imani Watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano haya”alisisitiza. 

Prodyuza nguli wa muziki nchini na kanda ya Afrika Mashariki, Nahreel ,ambaye ameshiriki kutengeneza wimbo huu aliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa jitihada mbalimali ambazo imekuwa ikifanya kuwanyanyua wasanii wa hapa nchini ambapo mbali na Diamond naye ameshiriki kwenye tukio hili kubwa. 
“Ninayo furaha ya kufanya kazi na Diamond kwa mara nyingine katika tukio hili kubwa la mashindano ya Kombe la Dunia na najivunia heshima kubwa tuliyopewa”
 Msanii Diamond akiongea katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es alaam (katikati) ni Sealouise Shayo, Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini (kulia) ni Meneja wake Sallam SK.
 Msanii Diamond na Nahreel katika mkutano wa waandishi wa habari, wengine ni maofisa wa Coca-Cola na mameneja wa msanii Diamond.
Maofisa wa Coca-Cola wakiwa katika picha ya pamoja na Diamond na Nahreel baada ya mkutano na waandishi wa habari.

WHO YAWAJENGEA UWEZO WATENDAJI TFDA NA WATAALAMU WA DAWA KATIKA VIWANDA

SPIKA NDUGAI ATEMBELEWA NA WAKURUGENZI WATENDAJI WA CLOUDS MEDIA GROUP, MULTICHOICE TANZANIA NA UJUMBE WA BUNGE LA MALAWI

$
0
0
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na wageni wake Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Ndg. Joseph Kusaga (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji, Multichoice Tanzania Ndg. Maharage Chande (kulia) walipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza na mgeni wake Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Ndg. Joseph Kusaga (katikati) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji, Multichoice Tanzania Ndg. Maharage Chande
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akipeana mikono na Mkurugenzi Mtendaji, Multichoice Tanzania Ndg. Maharage Chande (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Ndg. Joseph Kusaga 
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na mgeni wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kutoka Bunge la Malawi Mhe. Kamlepo kalua (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. Kulia ni Naibu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, Ndg. Thomas Makiwa. PICHA NA OFISI YA BUNGE

JESHI LA MAGEREZA KUNOGESHA SHEREHE MAADHIMISHO YA MUUNGANO DODOMA

BENKI YA CBA YAKUTANA NA WATEJA WAKE JIJINI ARUSHA

$
0
0
Na Pamela Mollel,Arusha

UKATA wa fedha katika uwekezaji na kukuza biashara ya utalii mkoani hapa umepata tiba baada ya Commerial Bank of Africa, kusema itashirikiana na wafanyabiashara kuwapa mikopo hadi kufikia dola za Marekani milioni 50 kwa atakayetaka.

Mkuu wa Idara ya Masoko wa benki hiyo, Julius Konyani, alisema wafanyabiashara 500 katika sekta ya utalii mkoani hapa kila mmoja anaweza kukopeshwa dola za Marekani milioni 50.Alisema hayo katika ya katika chakula cha jioni walichoandaa kwa ajili ya kubadilishana nao mawazo na wateja wao.

“Mteja mmoja anaweza kukopeshwa dola za Marekani milioni 50, tunaweza kuwakopesha wateja 500 hapa Arusha kila mmoja kiasi hicho cha mkopo hapa,” alisema.Alisema benki yake imefanya utafiti kwa mikoa mbalimbali kuangalia fursa zilizopo kama vile kilimo na utalii, na hivyo, imejipanga kuwawezesha wateja hao kukopa kiasi wanachohitaji ili kuendeleza na kukuza uwekezaji katika mkoa yao.

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Benki ya Commerial Bank of Africa (CBA) Tanzania, Gift Shoko akizungumza na wadau wa benki hiyo katika hafla fupi ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo katika hoteli ya Mt. Meru jijini Arusha, huku akiwajulisha hatua mbalimbali za kibenki zilizoboreshwa kwa wateja wao (Habari picha na Pamela Mollel Arusha)
Wadau wa benki ya Commerial Bank of Africa,CBA wakiwa katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Arusha kwa lengo la kuwajulisha hatua mbalimbali walizozifikia huku wateja wao wakipata wasaa wa kueleza changamoto zinazowakabili.
Mkurugenzi Mkuu Mendaji wa Be Gift Shoko kushoto akizungumza na mmoja wa wadau wa benki hiyo jijini Arusha 
Mkuu wa Idara ya Masoko wa benki ya CBA, Julius Konyani akizungumza katika hafla ya chakula cha jioni na wadau wa benki hiyo jijini Arusha kwa lengo la kuwajulisha hatua mbalimbali walizozifikia huku wateja wao wakipata wasaa wa kueleza changamoto zinazowakabili.

Wadau wa benki hiyo wakiwa katika hafla ya chakula cha jioni jijini Arusha.


How nuclear technologies helped Zanzibar to improve rice quality

$
0
0
Though economic development in Zanzibar has been associated with tourism, agriculture contributes greatly to the Islands' economy and food security. In Zanzibar agriculture is the main source of income for around 70 percent of the population.
Zanzibar's agricultural sector received a boost last year, with horticulture recording a 10 percent growth.Today the horticultureis one of the fastest growing and vibrant subsector on the island.  Though its returns are much lower than the $63 million that Zanzibar earns annually from cloves  —  its main export —  horticulture offers new opportunities for farmers, especially given the fluctuating clove prices.

Six years ago, nearly 80 percent of vegetables consumed in the Isles were sourced outside Zanzibar; however, with the growth of the tourism industry and the constant demand from restaurants and hotels, Zanzibar farmers are gradually taking up vegetables and fruit as a source of income.

Among various harvesting crops the most popular one is also rice. In recent years the demand for the grain was so high that Zanzibar started to import nearly 80% of the rice it needed. Farmers say they could close that gap if they had adequate agricultural extension services to guide them on the use of fertilizers and other modern technology.

Zanzibar's Ministry of Agriculture and Natural Resources elaborated special strategy with a view of increasing to try to increase rice production by developing irrigation systems, training farmers and introducing improved varieties of rice.

The local farmers decided to made improvements by employing a mutation induction to make rice seed more resistant to diseases, water shortages or high level of salinity in the soil.

Mutation is a natural process, and can take years. In this case safe level of irradiation can significantly speed up the process.  

In order to cultivate more varieties a special biotechnology laboratory on the island has been equipped in Zanzibar with special technologies. The nuclear technology application help local farmers to go forward and create modified seeds resistant to large number of diseases.

By increasing the local production of rice through the introduction of improved and new varieties, Zanzibar can reduce its dependence on imports, save money and create more jobs.


RAIS DKT.MAGUFULI ANATARAJIWA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO UHURU WA HABARI NCHINI

$
0
0
Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
RAIS wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk. John Mgufuli  kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu ikiwa ndio kilele chake na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.

Ambapo  wageni  zaidi ya 300 wanatajiriwa kuhudhuria  hafla hiyo wakiwepo wadau , wanahabari  ,wabunge na taasisi mbalimbali ambapo kimataifa Afrika  inafanyika Nchini Ghana Accra zaidi ya nchi 100  zitawakilisha katika hafla hiyo.

Akizungumza  jjjini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi  ya vyombo vya habari Kusini mwa Jangwa la Sahara Salome Kitomari amesema katika siku hizo watazungumzia umuhimu wa  uhuru wa habari, utawala bora kwa waandishi wa habari na  wanasheria kama Mahakama kuwa na uhuru  wa kusimamia kesi za jinai za kuwa na uwazi kwa wanahabari vilevile na kukumbusha kutekeleza majukumu katika  uandikaji wa habari kuwa sahihi.

Aidha Makamo wa Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Jane Mihanji amesema wao wamekuwa na jukumu la kuwaweka pamoja waandishi wa  habari  na kuwapa mafunzo na  kuwapatia  vitendea kazi.
Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.
Makamu wa Rais wa  Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Jane Mahanji akizungumza na waandishi wa habari namna wanavyokwenda begakwabega na waandishi kwa kuto semina ili kutoa habari zenye faida kwa Taifa.
Mkurugenzi wa  Tanzania Media Foundation (TMF) Fausta Musokwa akizungumza na waandishi wa habari wanavyochangia kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari kwa kutoa pesa ili vyombo hivyo vijiendeshe.
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumza na waandishi wa habari kuhusuumoja wa Mataifa unavyodhamini mchango mkubwa wa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea siku ya uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BENKI YA ACCESS YATOA MSAADA KOMPYUTA 10, MEZA PAMOJA NA VITI SHULE YA SEKONDARI TURIANI KINONDONI

$
0
0
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akikabidhi moja ya kompyuta 10 kwa Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam zilizotolewa na benki ya Access kwa shule hiyo Baadhi ya vitu vingine vilivyotolewa na benki ya Access kwa shule hiyo ni pamoja na viti 10na meza za kompyuta 10 wanaoshuhudia tukio hilo kulia ni Mwanafunzi Amina Ibony wa kidato cha IV na Nasib Masenga Kidato cha IV.
2
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akiwa na Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam mara baada ya kukabidhi kompyuta hizo kutoka kulia ni Benedig Mfoi Meneja Uendeshaji Camara Education Foundation Tanzania.
4
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akimsikiliza Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akisoma risala ya shule mara baada ya kupokea kompyuta 10 kutoka Benki ya Access ya jijini Dar es salaam.
5
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Turiani wilaya ya Kinondoni wakitumia kompyuta mara baada ya kukabidhiwa na benki ya Access leo jijini Dar es salaam.

TIC YAKUTANA NA WAWEKEZAJI WA NYANDA ZA JUU KUSINI

NGOs ZATAKIWA KUJIHAKIKI KUTAMBULIKA NA SERIKALI

BENKI YA ACCESS YATOA MSAADA WA KOMPYUTA 10 MEZA PAMOJA NA VITI KWA SHULE YA SEKONDARI TURIANI KINONDONI

$
0
0
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akikabidhi moja ya kompyuta 10 kwa Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam zilizotolewa na benki ya Access kwa shule hiyo Baadhi ya vitu vingine vilivyotolewa na benki ya Access kwa shule hiyo ni pamoja na viti 10na meza za kompyuta 10 wanaoshuhudia tukio hilo kulia ni Mwanafunzi Amina Ibony wa kidato cha IV na Nasib Masenga Kidato cha IV.
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akiwa na Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam mara baada ya kukabidhi kompyuta hizo kutoka kulia ni Benedig Mfoi Meneja Uendeshaji Camara Education Foundation Tanzania.
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akizungumza mara baada ya kukabidhi kompyuta hizo kulia ni Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona akimsikiliza Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akisoma risala ya shule mara baada ya kupokea kompyuta 10 kutoka Benki ya Access ya jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Turiani wilaya ya Kinondoni wakitumia kompyuta mara baada ya kukabidhiwa na benki ya Access leo jijini Dar es salaam.
Meneja Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Bw. Simon Sijaona na Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam wakiwaelekeza namna ya kutumia kompyuta hizo mara baada ya kukabidhiwa shuleni hapo leo.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakifurahia wakati walipopewa taarifa ya kuletewa kompyuta hizo na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Izungo Angalo kutoka Benki ya Access ya jijini Dar es salaam.
Bw. Izungo Angalo Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari ya Turiani Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam akitoa taarifa ya kupokelewa kwa kompyuta 10 kutoka Benki ya Access.

KUMBUKUMBU

$
0
0
DR. FRANCIS MW. MSELLEMU 
1941- 1996 

Baba, Ni Miaka 22 sasa tangu uondoke hata bila ya kutuambia neno la KWAHERI! Maisha yetu hayajawahi kuwa rahisi bila uwepo wako, Baba. Japo watu wanatuona tukicheka , hawajui ni kiasi gani mioyo yetu inahuzunika kwa kukukosa malezi, mapenzi na uwepo wako wewe. Hata hivyo tunamshukuru MUNGU kwa kuendelea kutulinda, kututunza na kutubariki. Ameedelea kuwa kweli kwetu Mume wa Mjane na Baba wa Yatima. Tunakuombea Pumziko la Milele, na tukiamini kwamba siku moja tutakutana na tutaimba Halleluya pamoja na wewe mbinguni. Unakumbukwa daima na Mke wako Mpendwa Kodawa Mikaline Msellemu - ‘Mama K’ kama ulivyo kuwa umezoea kumuita, Watoto, Wakwe zako, pamoja na Wajukuu. Ndugu , Jamaa na Marafiki nao hawajakusahau. ‘Mamillioni Wanaitegemea’

-Pumzika kwa Amani DAD!

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kufanya ziara nchini

$
0
0
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Ayodeji Adesina atafanya ziara ya siku nne (4) nchini kuanzia tarehe 25 hadi 28 Aprili, 2018 kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Lengo la ziara ya Dkt. Adesina nchini ni kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Benki hiyo ambayo imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya miradi ya miundombinu nchini.

Akiwa nchini, Mhe. Dkt. Adesina ataonana kwa mazungumzo rasmi na Mhe. Rais Magufuli pamoja na kuzindua Barabara kutoka Dodoma kwenda Babati hafla itakayofanyika katika eneo la Mradi wa Barabara wa Mayamaya-Mela- Bonga Wilayani Kondoa.

Aidha, Dkt. Adesina atatembelea Mtambo wa Kusafirisha Umeme wa Iringa kwenda Shinyanga pamoja na Kituo Kidogo cha Umeme cha Zuzu cha Mkoani Dodoma.

Dkt. Adesina ambaye ameambatana na Makamu wa Rais wa Benki hiyo anatarajiwa kushiriki Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanzania yatakayofanyika Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2018. Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zinazoongoza kwa kupokea misaada kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kupitia Mfuko wa Maendeleo wa Benki hiyo (ADF). Aidha, tangu kuanzishwa kwa Benki hiyo hapa nchini mwaka 1971, Tanzania imenufaika kwa kiasi cha zaidi ya Dola za Marekani bilioni 3.5 huku miradi ya maendeleo ya miundombinu ikipewa kipaumbele.

Aidha, hadi kufikia mwezi Novemba 2017 Benki ya Maendeleo ya Afrika imekuwa ikitekeleza miradi 25 yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 1.9. Kati ya miradi hiyo, 22 ni ya Sekta ya Umma yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.8 huku miradi mitatu (3) ikiwa chini ya Sekta Binafsi kwa thamani ya Dola za Marekani milioni 187.0.

Kati ya miradi yote, miradi ya maendeleo ya miundombinu inachukua asilimia 73 ambapo kati yake miradi ya Barabara ni asilimia 51, Maji na Usafi wa Mazingira asilimia 12 na Nishati asilimia 10. Asilimia 27 zilizosalia zinasaidia miradi ya sekta binafsi hususan katika kilimo na ustawi wa jamii.

Imetolewa na: 
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, 
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
 Dar es Salaam, 24 Aprili, 2018

KITENGO CHA MAGONJWA YA DHARURA MUHAS WAZINDUA KITABU KWA AJILI YA KUFUNDISHIA

$
0
0
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Andrea Barnabas Pembe akizindua kitabu kwa ajili ya kuwafundishia wanafunzi wanaosoma mwaka wa nne katika fani ya udaktari hasa wale wa Magonjwa ya Dharura hafra iliyofanyika ukumbi wa ukumbi wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Andrea Barnabas Pembe akizindua kitabu kwa ajili ya kuwafundishia wanafunzi wanaosoma mwaka wa nne katika fani ya udaktari hasa wale wa Magonjwa ya Dharura hafra iliyofanyika ukumbi wa ukumbi wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Tiba ya Dharura na Ajali wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dk. Hendry Sawe ambaye ni mtunzi wa kitabu hicho na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura akipongezwa na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Andrea Barnabas Pembe mara baada ya kumaliza uzinduzi.

BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI ZAIDI

MWENYEKITI HALMASHAURI YA MOROGRO ATAJA MBINU KUTUA MIGOGORO YA ARDHI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

IMEELEZWA watu pekee wanaoweza kumaliza migogoro ya ardhi nchini ni pande mbili ambazo zipo kwenye mgogoro na si vinginevyo na hata watalaam wanapokwenda basi ni kwa ajili ya kuweka mipaka tu.

Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Halmashaui ya Wilaya ya Morogoro, Kibena Kimu wakati wa ufunguzi wa mdahalo wa haki za ardhi wilayani Morogoro uliondaliwa na Shirika la mradi la PELUM Tanzania.

Mdahalo huo unaofanyika kwa siku mbili na kushirikisha vijiji vitano vya Mikese Lubungo, Newland na Mfumbwe vya wilayani humo ambapo Kimu amefafanua haiweze kumaliza siku bila kupata taarifa ya mgogoro wa ardhi kutoka kati ya wakulima na wafugaji au kijiji na kijiji, kuhusu mipaka.

Ambapo kila mmoja anakidai kuingiliwa na mwenzake na hata watalaamu wakienda na GPS wanakuwa na wakati mgumu kutatua mgogoro huo.

"Nimekuwa nikiwashauri wakae pande zote mbili zinazolumbana kuhusu ardhi na wanapokubaliana inakuwa rahisi kumaliza mgogoro na watalaam wa ardhi wanakuwa sehemu ya mashahidi tu,"amesema.

Ameongeza elimu inayotolewa na PELUM kuhusu kutambua rasilimali ardhi na namna gani ya kumiliki na kuwa na uwezo wa kushughulikia migogoro ya ardhi inayojitokeza imesaidia sana wananchi.

"Kwani vijiji vyote vina mabaraza ya ardhi lakini elimu waliyopata pengine haijatosheleza. Nawashukuru PELUM kwa kazi wanayofanya na elimu wanayotoa ya kusimamia matumizi bora ya ardhi kwenye halmashauri yetu ya Morogoro.

"Rasilimali pekee tuliyonayo watanzania ni ardhi kitu ambacho nchi zingine hakipo.Tumeona ujio wa watu wengi wakija kwa ajili ya kuchukua na kumiliki na kuwekeza kwenye miuondombinu ya ardhi yetu, tusipokuwa na uwezo wa kumiliki ardhi, tunaweza kuja kuwa watumwa kwenye nchi yetu,"amesema.

Amefafanua watu wanaendesha maisha yao kwa kilimo na hali ya kawaida na kusisitiza mpango unaofanywa na PELUM wa kuwapimia vipande vya ardhi wananchi wa kawaida na kuwatengenezea hati miliki za kimila ni jambo la msingi.

"Hati hizo za kimila zitawawezesha wananchi kwenda kukopa na kuenedeleza au kuwekeza kwenye maendeleo yetu na kutengeneza viwanda vidogo.

"Hata pale wanapokuwa na changamoto za mvua na bei ya mazao basi wanaweza kuyafanya kuwa mazao ghafi na kuyatunza katika ubora mpaka pale yatakaposafirishwa,"amesema.

MABINTI WATAKIWA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA AJILI YA MANUFAA YA BAADAE

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu , Dkt Ave Maria Semakafu akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya siku ya Tehama kwa watoto wa kike Duniani ambapo alitumia muda huo kuwaasa mabinti kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa ajili ya manufaa yao ya baadae na kuacha kutumia kwa matumizi ambayo yatawagharimu kwani picha katika mitandao hazifutiki.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt Raynold Mfungahema  akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu katika Maadhimisho ya siku ya Tehama kwa Mtoto wa kike Duniani.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dkt. Ave Maria Semakafu, akipata maelezo juu ya Teknolojia ya Ununuzi wa pedi mtaani kwa shilingi 200 au katika shule za sekondari hili kuweza kumsaidia mtoto wa kike.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dkt. Ave Maria Semakafu akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi wa Masafa kutoka TCRA,Mhandisi Stella Bunyenza ni nmana gani gari hiyo inawez akufatilia masafa mbalimbali.
Sehemu ya Wadau  walioshiriki katika Maadhimisho ya siku ya Tehama kwa Mtoto wa kike Duniani.

MWANTIKA AANZA MAZOEZI MEPESI, YAKUBU MOHAMED KWENDA AFRIKA KUSINI KWA UCHUNGUZI ZAIDI- DAKTARI AZAM

$
0
0
Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.

BEKI wa timu ya Azam Fc David Mwantika, ameanza rasmi mazoezi ya wenzake wiki hii ikiwa baada ya kuugua ghafla uwanjani wiki tatu zilizopita.

Mwantika alipata hitilafu hiyo ya mwili dakika ya 65 wakati Azam FC ikicheza hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) dhidi ya Mtibwa Sugar kabla ya kukimbizwa Hospitali ya Mbagala Zakhem na kuhamishiwa Hospitali ya Wilaya ya Temeke, na baadaye ya Rufaa ya Muhimbili (MNH).

Baada ya kuhamishiwa Muhimbili na kutibiwa vema kabisa, iliwalazimu madaktari wa hospitali hiyo kumhamishia kitengo cha magonjwa ya moyo cha Taasisi ya Jakaya Kikwete na kufanyiwa vipimo ili kujua kama ana tatizo la aina hiyo.

Akizungumzia hali ya mchezaji huyo, Daktari wa Azam FC, Mwanandi Mwankemwa, alisema kuwa tayari wamepokea majibu ya vipimo hivyo vinavyoonyesha kuwa beki huyo hana tatizo la moyo akidai yupo fiti kabisa na ndio maana wamemruhusu kuanza mazoezi mepesi.

“Mwantika alipata huduma Muhimbili na akalazwa katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete na baada ya kufanyika uchunguzi wa kina kabisa na vipimo vya kina na kuangalia mishipa ya damu ya moyo imethibitika kwamba Mwantika hana tatizo la moyo.

“Na sasa amerudi tena na katika siku mbili hizi tulianza kuangalia uwezo wake wa kukimbia na uwezo wake wa pumzi kwa hiyo alianza mazoezi ya kukimbia kwa dakika 20, dakika 30 na leo (jana) amekimbia dakika 45,” alisema.

Mwankemwa alisema kuwa wiki ijayo beki huyo ataruhusiwa kuanza mazoezi ya kawaida na wenzake tayari kabisa kurejea katika ushindani.

Akizungumzia maendeleo ya beki Yakubu Mohammed, aliyevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia (fibula),  Mwankemwa alisema licha ya wiki nne kupita na kuondolewa hogo (P.O.P) bado beki huyo anasikia maumivu kwenye eneo hilo.

Daktari huyo alisema kutokana na hali hiyo, beki huyo atalazimika kwenda nchini Afrika Kusini kufanyiwa uchunguzi zaidi wiki hii muda wowote ili kujua tatizo linalomkabili.

“Baada ya kutolewa P.O.P imeonekana bado ule mguu una maumivu makali sana kwa hiyo uongozi uliamua kwamba aende naye akafanyiwe uchunguzi Afrika Kusini kwa hiyo  tutafanya taratibu za kutafuta Visa na Yakubu kama sio siku ya Jumatano ijayo au Alhamisi atakwenda kwa ajili ya matibabu Afrika Kusini,” aliongeza Mwankemwa.
Viewing all 110079 articles
Browse latest View live




Latest Images