Na Agness Francis Blogu ya Jamii
BAADA ya Taifa Stars kuchapwa mabao 4-1 dhidi ya Algeri wakiwa ugenini sasa wanawakaribisha nyumbani kikosi cha timu ya Taifa ya Jamuhuri kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wao wa kirafiki.
Mchezo huo wa aina yake kati ya timu hizo mbili utachezwa kesho Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni na kiingilio kwa VIP ni Sh.5000 na viti vya mzunguko na vyenye rangi ya Chungwa ni Sh.1000.
Akizungumza leo Dar es Salaam, Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa Stars Hemedi Moroccoleo, amesema mchezo utagumu kwao lakini amewahakikishia Watanzania kupata ushindi katika mchezo huo.
"Tunatarajia kufanya vizuri katika mchezo wa kesho ili kupata ushidi ili kusogea mbele kuwa kwenye nafasi nzuri tutajitahidu kadri ya uwezo wetu kupambana kwa kuwa wenzetu wacongo wako vizuri na makini katika mchezo wa Soka" amesema kocha Morocco.
Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Hemedi Morocco akizungumza na waandishi wa habari Leo katika makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) kuhusu maandalizi ya kumenyana na Timu ya Taifa ya Jamuhuri ya Kidemokrasiya ya Congo katika mchezo wa kirafiki utakaochezwa kesho uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa Timu ya Congo, IBenge Florent akizungumza na wandishi wa habari leo katika makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania (TFF) akizungumzia ujio wao pamoja na maandalizi katika mchezo huo wa kirafiki dhidi ya Timu hizo mbili utaokachezwa katika Dimba la Uwanja wa Taifa Jijini Da ea Salaam.
Mchezaji wa Taifa Stars, Himidi Mau akizungumza na wandishi wa habari kwa ni aba ya wenzake kuelekea kesho kwenye dimba la uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki na Kikosi cha Congo Leo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania (TFF).
Nahodha wa Kikosi cha Timu ya Congo, Benic Adobe akizungumza na wandishi wa habari leo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhusu maandalizi ya mechi hiyo itakayochezwa kesho katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA