Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

Kifo cha Mwalimu Mponda wa TaSUBa chaigusa Serikali

$
0
0

Na Anitha Jonas – WHUSM
Serikali imetoa  pole kwa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo kwa kumpoteza Mwalimu mahiri John Mponda aliyekuwa balozi  wa tasnia ya Sanaa nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza katika ibada ya kumuaga marehemu huyo iliyofanyika katika Chuo cha TaSUBa Wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kumuaga kwani anatarajiwa kuzikwa kijiji cha Mbalizi Mkoani Mbeya.

“Tunatambua mchango wa Mwalimu John Mponda katika tansia ya sanaa nchini na kupitia wanafunzi waliyopita katika mikono yake pamoja na vikundi vya vijana alivyovianzisha ambavyo amekuwa akivifundisha kazi za sanaa, hakika tumempoteza mtu makini,”alisema Mhe.Shonza.

Akiendelea kuzungumza  katika msiba huo Mheshimiwa Shonza  aliwasihi wasanii waliyopata mafunzo kutoka kwa mwalimu huyo kuwa mabalozi  kwa wasanii wenzao na kuwashauri misingi iliyobora katika katika kukuza na kuendeleza kazi za sanaa. 
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha TaSUBa Dkt.Herbert Makoye alisema kuwa marehemu mwalimu Mponda ameondoka katika kipindi walichokuwa wanamuhitaji sana kwani kwasasa taasisi hiyo ipo katika maandalizi ya Tamasha la Utamaduni la Bagamoyo ambalo nilakimataifa na hufanyika kila mwaka na yeye  alikuwa mratibu na mpaka mauti yanamfika alikuwa akiwa shughulikia maandalizi hayo. 
“Kwa hakika msiba huu ni pigo kwa taasisi yetu na mwalimu huyu alikuwa kiungo miongoni mwetu na alifanya kazi yake kwa weledi na kujituma alikuwa ni mtu aliyeipenda kazi yake ,’’alisema Dkt.Makoye.

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Mkufunzi wa Sanaa katika Chuo cha Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) marehemu Mwl. John Mponda leo  kabla ya ibada ya kumuaga kwa ajili ya safari ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika Mbalizi mjini Mbeya.

WAKAZI DAR KUPATA MAJI YA UHAKIKA IFIKAPO 2020

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam Kisare Makori amehitimisha maadhimisho ya Wiki ya maji jijini yenye kauli mbiu ya Hifadhi Maji na Mifumo ya Ekolojia kwa Maendeleo ya Jamii.

Ametumia hitimisho la maadhimisho hayo kufungua mradi mdogo wa utakatishaji maji taka katika eneo ya Mburahati jijini.Akizungumza leo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Makori amesema maji yanayopatikana jijini kwa sasa ni asilimia 75 pekee na hadi kufikia mwaka 2020 maji yatapatikana kwa asilimia 95 na kufikia mwaka 2025 wakazi wote wa jiji watapata maji kwa asilimia 100.

Akizungumzia kuhusu mafanikio ya miradi maji Makori amesema miradi inayotekelezwa na DAWASA na DAWASCO katika mradi wa Ruvu chini ni lita milioni 270 kutoka lita milioni 182 zinazalishwa kwa siku na kuhudumia wakazi wa Bagamoyo, Kawe na maeneo ya jirani na mradi wa Ruvu juu lita 196 kutoka lita milioni 82 zinazalishwa kwa siku na kuhudumia wakazi wa maeneo ya Kibaha, Mbezi, Ubungo na maeneo ya jirani. 

Amesema zaidi ya visima 20 vimechimbwa na kunufaisha wakazi wa Kimbiji Mpera na maeneo yake.Amepongezwa wananchi kwa kukubali kuunganishwa na huduma ya maji kutoka laki 123,000 hadi kufikia 228,000.Pia amewataka wananchi kushiriki shughuli za usafi licha ya kuwa na asilimia 10 tu ya wakazi wanaopata huduma hiyo na amehaidi hadi kufikia 2020 asilimia 30 ya wakazi watafikiwa na huduma hiyo.

Makori amesema mwaka 2017 hadi mwaka 2020 miradi 50 ya uondoaji maji taka itajengwa Jangwani na kusaidia maeneo yenye wakazi wengi, mlipuko wa magonjwa na watu wenye kipato kidogo.

 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makori akizungumza katika  maadhimisho ya wiki ya maji jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makori (alievaa kofia ya kijani) akipanda mti katika mradi wa kuchaata maji taka.
 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makori akiweka jiwe la msingi la ujenzi katika mradi wa kuchaata maji taka.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makori  aiwa ameambana na viongonzi mbalimbali wakigangua eneo la mradi huo.

TANESCO YAWATOA HOFU WATEJA WAO, YASEMA HAKUNA TATIZO KATIKA LUKU

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco)limekanusha taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii  inayodai kutakuwa na tatizo katika mfumo wa manunuzi ya LUKU kuanzia Machi 25 hadi Aprili 5 mwaka huu.

Taarifa hiyo ya kutunga inadai kutokana na hali hiyo wateja wanunue umeme wa kutosha katika kipindi hicho.

Tanesco kupitia Ofisi ya Uhusiano imesema taarifa hizo si za kweli na uzushi wenye nia ya kupotosha umma kwani haijatokea taarifa yoyote kuhusu hitilafu katika mifumo ya manunuzi ya LUKU.

"Ikumbukwe kwamba taarifa kutoka Tanesco hazitolewi na mtu binafsi bali ofisi ya uhusiano iliyo chini idara ya Mkurugenzi Mtendaji ambayo ni msimamizi wa utoaji taarifa za shirika hili,"imesema taarifa ya Tanesco.

Imewaomba wateja wote wa Tanesco waipuuze taarifa hiyo kwani haina ukweli wowote ."Wateja wote mnaombwa kuendelea kutumia huduma za umeme kama kawaida."

SERIKALI YA TANZANIA NA MALAWI KUANDAA KONGAMANO LA BIASHARA NA UWEKEZAJI JIJINI MBEYA

MSAADA TUTANI

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk Hassan Abbas atuzwa

$
0
0
 Katibu wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA) Merinah Millensasha (kulia) akimkabidhi cheti cha pongezi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk Hassan Abbasi (katikati) kwa kutambua kazi ya Uzalendo anayofanya,  kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Wazee na Watoto wa asasi hiyo, Mohamed Shaban.

How To Cook Chips Mayai

Michuzi TV: TIRA YAZIFUTIA LESENI KAMPUNI NNE ZA UDALALI WA BIMA


RAIS MAGUFULI, WAZIRI WA ULINZI WA ISRAEL WAFANYA MAZUNGUMZO IKULU

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Ulinzi wa Israel Avigdor Lieberman mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Israel Avigdor Lieberman Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao na ujumbe kutoka nchini Israel uliokuwa ukiongozwa na Waziri wa Ulinzi wa Israel Avigdor Lieberman Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Waziri wa Ulinzi wa Israel Avigdor Lieberman wa kwanza (kushoto kwake) Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi wa nne kutoka (kulia) Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Florence Turuka wa kwanza kushoto aliyesimama mstari wa nyuma pamoja na Viongozi wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na makamanda mbalimbali kutoka makao makuu ya Jeshi.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Cancer Case in Tanzania: Room for Development

$
0
0
  Today Tanzania is facing a cancer crisis with as many as 35,000 new cases expected to be diagnosed a year. 
  In spite of the emergence of cancer as a serious national problem, there are only two cancer hospitals in the country. 
  The largest cancer disease hospital is the Ocean Road Cancer Institute (ORCI), located in Dar-es-salam. The Institute handles nearly 3,000 new cancer patients and up to 10,000 follow-up cases annually. Up to 20% of ORCI's patients are children, who are usually treated with both chemotherapy and radiotherapy. The ORCI is equipped with diagnostic imaging services and cancer screening. 
  However, regular screening and early diagnosis is not a common event in Tanzania. Only a small number of patients from all over the country can afford to travel to Dar-es-salaam for cancer check-up. 

The United Republic of Tanzania National Health Policy advocates the right for cancer patients to be treated free of charge. Prior to diagnosis, patients are required to cover for themselves the expenses related to screening of cancer and any other necessary medications which are not covered by the government.
  In general, this challenging situation with cancer patients can be alleviated by opening of new screening centers and nuclear medicine facilities which are indispensable for cancer diagnostics and treatment.  

  With advanced nuclear technologies, Tanzanian doctors will be able to deliver more precise diagnosis, treatment and be able to evaluate treatment given to cancer patients. Specialists at ORCI are now able to employ more innovative 3D scanning of tumors, that detects the abnormal cells at early stages with more accuracy than the scanners of previous generation.  
  Once the tumor is identified, medical specialists are able to use modern technology such as contouring computer software to define and separate the healthy tissue from affected one in order to apply radiation and medical isotopes in a more accurate way to minimize exposure to healthy tissues and organs. .

  Tanzanian government is exerting considerable efforts to tackle health issues with new strategies and programs at all levels, starting from preparation of specialists capable to deliver professional service. Compared to other East African countries, Tanzania is the only country with the highest number of nuclear medicine specialists even though their number is still very low.
  Nuclear medicine specialty involves the use of facilities such as PET/CT (Positron Emission Tomography/Computer Tomography) and currently PET/MRI(Positron Emission Tomography/Magnetic Resonance Imaging), Hybrid SPECT/CT (Single Photon  Emission Computed Tomography),Thyroid Uptake System and so on.

CLICK HERE TO READ MORE 

WATOTO WA WAFUGAJI WAGUSWA NA SOKO LA KIMKAKATI LA MIFUGO LONGIDO

$
0
0

Katika kijiji cha EWORENDEKE, kata ya KIMOKOUWA, Wilayani LONGIDO mkoani ARUSHA, kijiji hicho kipo takriban kilomita 4 kutoka Namanga, mpaka wa Tanzania na Kenya.

Hapo kuna Soko la Kimkakati la mifugo Longido, linalohusika na uuzaji wa mifugo kutoka mikoa takribani 7 ya hapa nchini Tanzania. Wafugaji huuza mifugo hiyo hapa nchini na nchi za jirani, soko hilo ambalo limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), limekuwa ni neema kwa watoto wa kaya zinazozunguka soko hilo.

Watoto wa wafugaji wa jamii ya kimaasai ambao ndiyo wanufaika wa soko hilo wameguswa na uwepo wa soko hilo kwa kupata maziwa ya mbuzi bure. Watoto hao hukamua maziwa hayo kutoka kwa mbuzi ambao hufikishwa sokoni hapo muda wa jioni na kusubiri kuuzwa usiku ambapo mnada wa mifugo kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi hufanyika sokoni hapo.

Mratibu wa Kitaifa wa Program ya MIVARF,Walter Swai, amebainisha kuwa tangu Program hiyo ianzishwe kutekelezwa rasmi mwaka 2011, katika mikoa yote ya Tanzania bara na Zanzibar imekuwa ikichochea faida nyingi, zaidi ya malengo mahususi yaliyokusudiwa na Program ambayo, ni kufanikisha azma ya Serikali ya Tanzania ya kuongeza kipato kwa wananchi pamoja na uhakika wa chakula kwa kaya zenye kipato cha chini hususan maeneo ya vijijini.
 Baadhi ya watoto wa wafugaji, kijiji cha Eworendeke, kata ya Kimokouwa, Wilayani Longido wakipata maziwa kwa ajili ya matumizi yao kwa kukamua bure mbuzi waliofikishwa muda wa jioni katika Soko la kimkakati la mifugo Longido kuuzwa, Soko hilo limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
 Mmoja wa watoto wa wafugaji, kijiji cha Eworendeke, kata ya Kimokouwa, Wilayani Longido akipata maziwa kwa ajili ya matumizi yake kwa kukamua bure mbuzi waliofikishwa muda wa jioni katika Soko la kimkakati la mifugo Longido kuuzwa, Soko hilo, limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

JESHI LA POLISI TABORA LAMKAMATA MGANGA WA JADI ANAEPIGA RAMLI CHONGANISHI KWA JAMII

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limefanikiwa kumkamata mganga wa Jadi mwenye kupiga ramli chonganishi na kusababisha Mauaji ya mama mmoja aliyefahamika kwa jina la NDILU MBOGOSHI, Miaka 65, Msukuma, Mkulima, Mkazi wa Shilabela Kata ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua Mkoa wa Tabora, ambaye aliuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kichwani. Mara baada ya tukio hilo upelelezi ulifanyika na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora liliweza kubaini na kumkamata mganga wa jadi huyo ambaye amefahamika kwa jina la THERESIA PAULO, 57YRS, MSUKUMA, mganga wa jadi na mkazi wa ISAGEGE-SASU Tarafa ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua.
 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Tabora SACP Wilbroad Mutafungwa akitoa taarifa za kukamatwa kwa Mganga wa Jadi anayepiga ramli chonganishi na kusababisha Mauaji.
Picha hapo juu: Mganga aliyekamatwa akiwa pamoja na vifaa vyake vya kazi ambaye anapiga ramli chonganishi iliyosababisha Mauaji huko Ulyankulu Mkoa wa Tabora.Picha na Habari toka kwa Omar Matesa @ RPC TABORA

Je! Unajua unaweza kupata bei bora za soko kwa shamba lako la kuzalisha kwa kutumia mtandao wa simu?

$
0
0
Je! Unajua unaweza kupata bei bora za soko kwa shamba lako la kuzalisha kwa kutumia mtandao wa simu? Tazama na ujifunze jinsi wengine wanavyofanya.




KIKAO CHA RAIS MAGUFULI,WAFANYABISHARA KIWE CHACHU YA MAENDELEO KATIKA NCHINI

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KWA Ujinga wangu naomba niseme mapema tu, mimi si mfanyabiashara ila 
nimekuwa karibu kwasababu nanunua bidhaa za wafanyabishara.

Nanunua bidhaa za wafanyabishara kulingana na mahitaji yangu ya kila 
siku.Ndio ukweli maana maisha yangu ni kwamba nikijipata vijesenti naenda dukani nanunua nachojitaji.Kwa kuwa nimekuwa karibu na wafanyabishara , nikiri nimekiwa nikifuatilia 

mambo yao mbalimbali.Hata wanapotoa malalamiko yao kuhusu kukwamishwa kwa mambo yao nimekuwa nikisia.Malalamiko ya tozo kubwa za kodi kwenye masuala ya biashara nayo nimekuwa nikiwasikia wafanyabishara wakilalamika.

Nawasikia kwasababu mbali ya kuwa ni sehemu ya mteja wao , bado nami ni Mtanzania ambaye nashukuru Mungu ni muumini wa kufuatilia kila jambo nchini kwetu.Hata Rais wangu Dk.John Magufuli wakati unatoa maagizo kwa Waziri wa Fedha na Mpango kukaa na Mamalaka ya Mapato Tanzania(TRA)kuangalia namna ya tozo za kodi.

Ukasema kuwa kodi zimekuwa kubwa kiasi cha kufanya kuwa kero.Ukaeleza 
namna ambavyo unataka kodi iwe jambo la heshima kwa Taifa na si kuwa kero kwa mlipaji.Kwa Ujinga Wangu baada ya kusikia utakutana na wafanyabishara kutoka maeneo mbalimbali nchini.Nikasema kwenye mazungumzo hayo lazima kitaeleweka.

Rais Magufuli ukaamua kutoa nafasi ya kila mfanyabishara kutoa dukuduku lake.Nakumbuka kwenye mkutano huo ambao wewe uliongoza ulieleza namna ambavyo unataka kumsikia kila mmoja wao.Wafanyabishara nao kwa kuwa kuna mambo ambayo yalishikuwa kero kwao waliamua kusema kila kitu.Hakuna ambacho wamekificha maana waliona ndio sehemu pekee ya wao kusikilizwa.

Wakaeleza changamoto ambazo wanakutana nazo kutoka kwa TRA.Wakaeleza namna ambavyo wanaojihusisha na biashara ya mazao kuharibikia njiani.Wakaeleza namna ambavyo wanatamani Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya biashara.

Wafanyabishara hao wakaelezea mambo mengi.Wakaeleza namna ambavyo wanaamini kikao hicho kati yao na Rais kitakuwa na mafanikio makubwa.Kama nilivyotangulia kueleza awali mimi si mfanyabiashara lakini nimevutiwa na mazungumzo kati ya pande hizo mbili.
 Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara ITNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  alipokuwa akiendesha  mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam hivi karibuni .


HOSPITALI DAR ZABAINIKA KUWA NA WAGONJWA WENGI WALIOKUFA KWA VIFO VYA MALARIA, UKIMWI

$
0
0
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

 HOSPITALI za Mkoa wa Dar es Salaam zimebainika zilikuwa na wagonjwa wengi ambao walikufa kutokana na malaria, Ukimwi , ajali, maambukizi ya bakteria kwenye damu, upungufu wa damu, saratani na kifua kikuu(TB) ukifuatiwa na mkoa wa Morogoro. 

 Imefahamika malaria na upungufu wa damu ulichangia vifo vingi kwenye kundi la watoto chini ya miaka mitano na vifo kutokana na Ukimwi na Kifua Kikuu viliathiri zaidi kundi la watu wazima, vifo vinavyotokana na ajali viliathiri zaidi kundi kubwa la vijana wakati saratani ziliathiri makundi ya umri wote. 

 Hayo yameelezwa  jana jijini Dar es Salaam na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) wakati ikielezea matokeo ya utafiti wa vifoo vinavyotokea katika hospitali za Tanzania. Imeelezwa na NIMR taarifa za vifo ni moja ya vyanzo muhimu vya takwimu katika kupanga mipango na kuandaa sera ya afya ambapo uchambuzi wa takwimu katika makundi ya magonjwa ya kuambukiza, magonjwa yasiyoambukiza na kundi la ajali na majeraha ulionesha tofati kubwa kati ya mikoa na mikoa. 

 Utafiti huo umebaini mikoa ya Pwani, Geita na Katavi imeonekana kuathirika zaidi na magonjwa ya kuambukiza na utapia mlo. Wakati vifo kutokana na ajali na majeraha viliathiri zaidi mikoa ya Rukwa, Tabora, Singida na Kigoma. Kundi la magonjwa yasiyoambukiza limeathiri zaidi mikoa ya Ruvuma, Manyara, Dar es Salaam na Mwanza.

 "Kati ya mwaka 2006 na mwaka 2015, mikoa ya Kanda ya Kati (Dodoma, Singida, Manyara) mikoa ya kaskazini (Arusha na Kilimanjaro) ndiyo iliyobeba mzigo mkubwa wa vifo vilivyosababishwa na maradhi ya mifumo ya kupumua, upungufu wa damu uliathiri zaidi mikoa ya Dodoma, Simiyu na Mtwara,"imesema. Imeeleza utafiti umeanisha changamoto katika ukusanyaji, uchanganuzi na matumizi ya takwimu katika hospitali zilizopo nchini na kumekuwa na matumizi hafifu ya majina rasmi ya magonjwa kwa kutumia mwongozo wa kimataifa. 

 "Vyanzo vikuu vya vifo hospitalini nchini Tanzania ni pamoja na malaria, maradhi yanayoathiri mfumo wa kupumua, Ukimwi, upungufu wa damu na magonjwa ya moyo. "Kumekuwa na ongezeko kubwa la vifo vya watoto wachanga na magonjwa ya mfumo wa kupumua katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. 
Mganga Mkuu wa Serikali, Prof Muhammad Bakari Kambi akizungumza wakati akifungua mdaharo uliowahusisha wataalamu mbali mbali kujadili ni kitu gani kinasababisha vifo katika hospitali, kufuatia utafiti uliofanywa na  Taasisi ya Taifa Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu (NIMRI). Kupitia matokeo ili kutoa ushauri wa kisera ili serikali iweze kutilia mkazo ambapo Prof. Kambi amesema changamoto inazikumba hospitali nyingi ni magonjwa yasiyoambukiza yamekuwa ni changamoto kubwa inayopelekea kuzigharimu sana. Kaimu Mkurugenzi wa NIMRI akimkaribisha mgeni rasmi. 
 Washiriki kutoka taasisi mbali mbali za serikali na hospitali za mikoa wakifuatilia kwa makini.

MBUNGE NYAMAGANA AWEKA MIKAKATI YA KUIBUA,KUENDELEZA MPIRA WA WAVU

$
0
0
Na Zainabu Nyamka,Globu ya jamii

MBUNGE wa Jimbo la Nyamagana  Stanlaus Mabula ameweka mkakati wa kuibua, kukuza na kuendeleza mpira wa wavu ili  uwe ajira. 

Mabula amebainisha haya  leo kwenye uzinduzi wa Mpira wa Wavu wenye jina la Mrajam Volleyball Championship inayohusisha  vikosi nane kutokea Mwanza, Zanzibar, Manyara, Mara,  Shinyanga na kilele chake kuwa Machi 25/mwaka huu.

Akiwakilishwa na Ahmed Misanga kwa niaba yake amesema mbunge wa Nyamagana amefarijika michuano hiyo kuja kufanyikia Nyamagana na kuweka historia kuwa michuano ya kwanza kufanyika katika uwanja uliozinduliwa wiki mbili zilizopita. 
"Mchakato wote wa upatikanaji wa wadau wa maendeleo ulitokana na jitihada zake na kuwezesha kujengwa uwanja huo uliogharimu Sh. 122,000,000.Amewaambia waandaaji ni heshima kubwa kupata mwaliko huo adhimu  na yupo tayari kushirikiana na vilabu vya mpira wa wavu jimboni humu kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji hivi na kuwa ajira.

Amefafanua  ofisi ya Mbunge wao ipo wazi,hivyo waende wakazungumze na kuweka  mkakati wa pamoja wa kudumu utakaokuwa chachu ya kuibua vipaji vya mpira wa Wavu, kuviendeleza na kuwa ajira ndani ya wilaya,  kimkoa, kitaifa na kimataifa.

" Maana kiu na furaha yangu nikuona mchezo wa wavu unakuwa ni zaidi ya mazoezi ya mwili bali unakuwa ajira,"amesema.Uzinduzi huu leo umezinduliwa na mgeni rasmi  Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mary Tesha aliyewakilishwa na Ofisa tawala.  

Wageni wengi ni ofisi ya Mbunge Ilemela iliyowakilishwa na Micheal Goyele, Wenyeviti wa Ilani vya mpira wa wavu Mwanza,  Tabora,  Mara. Vikosi vinane vinavyochuana nipamoja na:, Nyuki Zanzibar, Polisi Zanzibar, Ngorongoro Manyara, MTC jeshi Mwanza, Magu, Bunda, Shinyanga pamoja na kikosi kutokea Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustine Mwanza. 

Mshindi wa kwanza ataibuka na kitita cha shilingi million moja, mshindi wa pili atapata shilingi laki tano na mshindi wa tatu atapatiwa shilingi laki mbili. Wachezaji sita bora wataondoka navyeti pamoja na elfu 30.

MAKONDA AWAITA OFISINI KWAKE WANAWAKE WALIOTELEKEZWA NA WAUME ZAO

$
0
0
RC Paul Makonda


Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

MKUU wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda  amewataka wanawake wote waliotelekezwa na waume zao na hawapatiwi fedha za matunzo ya mtoto wafike ofisini  Jumatatu ya  Aprili 9 kwa lengo la  kupatiwa msaada wa kisheria.

Taarifa ya Makonda kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana amesema jopo la wataalamu wa sheria, maofisa ustawi wa jamii na askari Polisi kutoka dawati la jinsia wamejipanga ipasavyo kuwahudumia na kuhakikisha mzazi mwenza anatoa fedha kwa ajili ya matunzo ya mtoto.

"Huduma hii inatolewa bure chini ya uongozi thabiti wa Serikali ya Awamu ya Tano.Ewe mwanamke huu si wakati wa kulia wala kuteseka kwani Serikali yako itasimama na wewe hadi upate haki yako," amesema Makonda.

MATUKIO KATIKA PICHA KAMATI YA LAAC NA PAC MKOANI SINGIDA

$
0
0
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC),wakifuatilia mada kuhusu Mtazamo wa kikaguzi kutoka kwa Mkaguzi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Ndugu Athuman Mbuttuka katika semina iliyofanyika Mkoani Singida kwa ajili ya kuwajengea uwezo wajumbe hao.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC),wakifuatilia mada kuhusu Mtazamo wa kikaguzi kutoka kwa Mkaguzi wa ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Ndugu Athuman Mbuttuka katika semina iliyofanyika Mkoani Singida kwa ajili ya kuwajengea uwezo wajumbe hao.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Mary Chatanda akichangia hoja katika semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati hiyo, iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na kufanyika Mkoa wa Singida.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MARCH 23,2018

Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images