Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

KAIMU MGANGA MFAWIDHI HOSPITALI YA KITETE ASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI WA KITAALAMU

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT

19 MACHI 2018

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo imeamua kumsimamisha Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Kitete Dkt. Nassoro Kaponta ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizotolewa na wananchi dhidi ya Hospitali hiyo.

Maazimio hayo yalitolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri mara baada ya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa Kitete.

Alisema Dkt Kaponta anasimamisha sio kama yeye katenda kosa bali ni katika uwajibikaji ili kupitisha Kamati Maalumu ya Kuchunguza Kitaalamu (Therapeautic Committee) kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa tuhuma zilizotolewa na wananchi kuhusu mwenendo wa wa Watumishi wa Hospitali hiyo ambaye yeye alikuwa akiisimamia.

Mwanri alitaja baadhi ya tuhuma ni pamoja na lugha chafu kutoka kwa baadhi ya Wauuguzi wanazitoa kwa wakimama wajawazito wanapokwenda kupatiwa huduma ya kujifungua, wagonjwa kudaiwa rushwa na baadhi ya wafanyakazi na vifo wa wakinamama vinavyotokana na uzembe.

Alisema pamoja na Kamati hiyo kuchunguza mambo ya Kitaaluma pia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) Mkoani Tabora imepewa jukumu la kuchunguza tuhuma zinazotolewa na wananchi wanaoenda kutibiwa pale za rushwa na lugha chafu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MKUTANO WA NNE WA BARAZA KUU LA CHAMA CHA ZAPSWU WAFANYIKA ZANZIBAR

$
0
0

 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafayakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania TALGWU, Obadia Mwakasitu akizungumza katika Kikao cha Baraza la nne la ZAPSWU huko katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi
 Mgeni rasmi wa Kikao cha Baraza kuu la nne la Chama cha Wafayakazi wa Sekta ya Umma, Mw. Khamis Mwinyi ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi ZATU akiwahutubia washiriki wa wa Kikao hicho.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafayakazi wa Sekta ya Umma Zanzibar akizungumza machache na kumkaribisha mgeni Rasmi katika kikao cha Baraza kuu la nne la Chama hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Zanzibar.
 Washirki wa kikao cha Baraza kuu la nne la Chama Wafayakazi wa Sekta ya Umma Zanzibar wakiimba nyimbo maarufu ya Mshikamano katika kikao hicho.
Picha ya pamoja ya Wajumbe walioshiriki kikao cha Baraza kuu la nne la Chama cha Wafayakazi wa Sekta ya Umma Zanzibar ZAPSWU. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar 

HOTUBA YA RAIS WA TFF ALIPOZUNGUMZA NA WAHARIRI WA HABARI ZA MICHEZO LEO JIJINI DAR

$
0
0
UTEKELEZAJI WA TFF KATIKA MAENEO MBALIMBALI

Ndugu Waandishi wa Habari,Sekretarieti ya TFF, Watanzania wote wanaotuangalia na kutusikiliza,mabibi na mabwana habari za asubuhi.

Naomba nianze kwa kumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana mahali hapa siku ya leo tukiwa wazima wa Afya,Lakini pia nichukuwe nafasi hii kuishukuru Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dr.Joseph Pombe Magufuli kwa ushirikiano mkubwa ninaoupata katika uendeshaji wa mpira wa miguu, nimekuwa karibu sana na Serikali kuhakikisha juhudi zetu za kuendeleza mpira zinafanikiwa kwa kasi kubwa sana na mafanikio ya ujio wa Rais wa FIFA ni kielelezo cha karibuni kuonyesha ushirikiano mkubwa tunaoupata toka kwa Serikali hasa Waziri mwenye dhamana ya michezo Mh.Dr,Harrison Mwakyembe na timu yake.

Lakini niwashukuru kwa nafasi ya kipekee ndugu zangu Waandishi wa Habari kwa kazi kubwa mnayoifanya kuhabarisha umma kuhusu habari za mpira wa miguu,Pia pongezi zenu kwa kazi nzuri mliyoifanya wakati wa ujio wa FIFA, mlifanya kazi kubwa sana kutangaza ziara ya Rais wa FIFA, mmetupa heshima kubwa sana.

Ndugu zangu, leo nitaongelea mambo makubwa mawili ili waTanzania wapate kufahamu kinachoendelea katika mchezo wa mpira wa miguu hapa nchini.Moja nitaongelea kuhusu mambo ambayo tumeyafanya kwa kipindi cha miezi saba nilichokuwepo madarakani lakini la pili ni mambo yanayoendelea sasa hivi kwenye Shirikisho.


MAWAZIRI WA AFYA KUTOKA NCHI 10 WAJADILIANA NAMNA YA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA AFYA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii

MAWAZIRI wa Afya kutoka nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini wamekutana nchini Tanzania kwa ajili ya kujadili namna ya kuboresha huduma za afya na hasa katika utambuzi na kubaini magonjwa ya mlipuko.

Pia mawaziri hao wamekutana kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika utoaji na usimamizi bora wa huduma za afya.Mbali ya mawaziri pia wadau wa sekta ya afya kutoka kwenye baadhi ya mashirika wameshiriki mkutano huo.

Kupitia mkutano huo wa afya wa 65 nchi zisizo na uzoefu zitajifunza kutoka nchi ambazo zinafanya vizuri katika utoaji huduma,usimamizi na kutathimi ambapo washiriki wakiwamo mawaziri wa afya pamoja na wadau wa afya wameendelea kubadilisha uzoefu kupitia mada mbalimbali zinazoendelea kutolewa na watoa mada.

Kwa Tanzania, mwenyeji wa mkutano huo ni Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ni miongoni mwa wanaoshiriki mkutano huo unaojadili masuala ya afya kwa nchi hizo.

Kauli mbiu katika mkutano huo inasema "Ushirikiano wa sekta ya afya katika kupata mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu(SDG's)" na mkutano huo huo utakaofanyika kwa siku tatu inasema hivi.

Hivyo nchi mbalimbali wameelezea namna ambavyo wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali katika sekta ya afya.Mwakilishi kutoka nchi ya Uganda pamoja na kuelezea ambavyo wamefanikiwa katika sekta ya afya lakini changamoto kubwa ipo katika ajali za barabarani ambazo nyingi zinatokana na uendeshaji usifuata sheria unaofanywa na waendesha pikipiki.

Akizungumza kwenye mkutano huo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema nchini Tanzania kuna mikakati mbalimbali ya kuboresha huduma za afya.Pia ameelezea hivi karibuni watazindua chanjo ya kansa kwa msichana wa kike kuanzia miaka 9 hadi miaka 13.

Amesema lengo ni kukabiliana na tatizo la ugonjwa wa kansa na lengo la Serikali ni kuhakikisha ugonjwa wa kansa unapungua.Wakati wa mkutano huo pia wamejadili sera mbalimbali kwa kila ambazo zipo kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya.

DC SHINYANGA AFUNGA MAFUNZO VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI WANAWAKE NA VIJANA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefunga mafunzo kwa vikundi vya wajasiriamali vya wanawake na vijana manispaa ya Shinyanga yaliyolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kutumia vizuri fedha za mikopo walizopewa na manispaa hiyo.

Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo katika ofisi za manispaa ya Shinyanga na kuhudhuriwa na wanawake na vijana 60 kutoka vikundi 20 vya wajasiriamali ambao wamepata mikopo ya shilingi milioni 125.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo leo Jumatatu Machi 19,2018 Matiro aliwataka vijana na wanawake hao kutumia fedha walizopewa kwa malengo waliyokusudia na kuhakikisha wanaanzisha viwanda vidogo vitakavyoinua uchumi wao.

“Tumieni mikopo hii kwa ajili ya kuanzisha viwanda vidogo ili kumuunga mkono rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli anayetaka Tanzania iwe nchi ya viwanda,pale mnapokwama tafadhali wasilianeni na viongozi wa serikali,tutawasaidia na pia tutatembelea miradi yenu ili tujue mnachofanya”,alisema Matiro.

Aidha aliwataka vijana na wanawake kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo kwenye halmashauri za wilaya ,mikopo ambayo haina masharti magumu wala riba kubwa ukilinganisha na taasisi za kifedha (benki).“Msikubali kukata tama kwamba maisha ni magumu,hata siku moja serikali haiwezi kugawa pesa kwa mtu mmoja mmoja,anzisheni vikundi vya ujasiriamali,kisha ombeni mikopo kwenye halmashauri,pesa zipo”,aliongeza Matiro.
Washiriki wa mafunzo kwa vikundi vya wajasiriamali vya wanawake na vijana  wa manispaa ya Shinyanga wakiwa wamesimama baada ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kuingia ukumbini kwa ajili ya kufunga mafunzo hayo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasisitiza wanawake na vijana kutumia kwa malengo yaliyokusudiwa pesa za mikopo walizopata
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiimba wimbo kuhusu wanawake ...."Wanawake wote hongeraa...."

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Diwani mwingine wa Chadema Arusha Ajiuzulu na kujiunga na CCM

$
0
0
Diwani wa kata ya Kaloleni Halmashauri ya jiji la Arusha, Ndg.Emmanuel Kessy wa CHADEMA (pichani kati) amejiuzulu uanachama na udiwani mapema jana na kutangaza kujiunga na chama cha CCM, kwa kile alichoeleza kuwa amefanya hivyo ili kuunga mkono juhudi za Mh.Rais Magufuli.Diwani huyo amepokelewa na Katibu mwenezi wa Wilaya ya Arusha Mjini Ndg.Abrahamu Mollel pamoja Katibu Hamasa wa Vijana Mkoa wa Arusha Ndg. Omary Lumato

KESI YA ALIYEKUWA MHASIBU WA TAKUKURU KUANZA KUSIKILIZWA APRILI 10

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

Kesi dhidi ya Mhasibu  Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Godfrey Gugai anayedaiwa kuwa na  utajiri wa kutisha kwa kumiliki mali zenye thamani ya Sh. 3 bilioni ambazo haziendani na kipato chake kuanza kusikilizwa mapema mwezi ujao.

Hayo yameelezwa leo Machi 20, 2018 na wakili wa serikali kutoka Takukuru, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba. 

"Mheshimiwa kesi hii leo ilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini upelelezi umekamilika, tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuja kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali (PH).

Kufuatia taarifa hiyo, hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Aprili 10, mwaka huu. Kwa ajili ya washtakiwa kusomewa Maelezo ya awali.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera

Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Gugai na wenzake wanasota mahabusu kutokana na kukabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.

MASHINDANO YA 'CASTLE LAGER 5s' YAANZA KUTIMUA VUMBI JIJINI DAR

$
0
0
Mchezaji wa team Z,ya Ilala akijaribu kuwatoka wachezaji wa team Kiba wakati wa Bonanza la Castle 5s(5-aside) lililofanyika Viwanja vya Sigara Tabata mwishoni mwa wiki.Bingwa katika mashindano hayo ataiwakilisha inchi ya Tanzania katika mashindano ya Afrika yanayotarajiwa kufanyka Zambia.
Mchezaji wa team Kiba,ya Ilala akijaribu kuwatoka wachezaji wa team Simba wakati wa Bonanza la Castle 5s(5-aside) lililofanyika Viwanja vya Sigara Tabata mwishoni mwa wiki.Bingwa katika mashindano hayo ataiwakilisha inchi ya Tanzania katika mashindano ya Afrika yanayotarajiwa kufanyka Zambia.
Mchezaji wa timu Kiba,ya Ilala akijaribu kufunga wakati wa mechi ya Bonanza dhidi ya timu Simba wakati wa Bonanza la Castle 5s(5-aside) lililofanyika Viwanja vya Sigara Tabata mwishoni mwa wiki.Bingwa katika mashindano hayo ataiwakilisha inchi ya Tanzania katika mashindano ya Afrika yanayotarajiwa kufanyka Zambia. 


HOTUBA YA RAIS DKT.JOHN POMBE MAGUFULI WAKATI WA MKUTANO WA 11 WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA 19 MARCH 2018

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATOA NENO KWA MAWAZIRI WA AFYA WA AFRIKA MASHARIKI,KATI NA KUSINI

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii

SERIKALI ya Tanzania imewahakikishia mawaziri wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki,Kati na Kusini kuwa itaendelea kuisaidia sekretarieti ya ECSA yenye makao makuu yake jijini Arusha.

Imesema kuwa inatambua majukumu ya Sekretarieti hiyo katika sekta ya afya huku ikiwaomba mawaziri hao na wadau wengine kuboresha mifumo ya afya ili kusaidia kuondoa changamoto zinazojitokeza wakati wa utoaji wa huduma bora za afya.

Akizungumza Dar es Salaam jana jioni wakati anafungua Mkutano wa 65 wa Mawaziri wa Afya kutoka Afrika Mashariki,Kati na Kusini,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ni jukumu la Serikali ya Tanzania kuendelea kuwa mwenyeji na kusaidia sekretarieti ya ECSA.Waziri Mkuu amesema pia mawaziri hao katika mkutano huo unaondelea jijini Dar es Salaam wajadili mambo yote muhimu yanayohusu sekta ya afya na kufafanua wasiache hata jambo moja nyuma na zaidi ni nini kifanyike kuboresha sekta ya afya.

"Niwaombe mawaziri wa afya ambao mmekutana katika mkutano huu ,wekeni mikakati yenye lengo la kuboresha sekta ya afya na kuangalia namna ya kuondoa changamoto ambazo zinakuwa vikwazo katika utoaji wa huduma bora za afya."Boresheni mifumo ya afya na kubwa zaidi ifikapo mwaka 2030 tuwe tumefikia malengo ya Maendeleo Endelevu(SDG's) katika eneo la afya.

"Jukumu la Serikali ya Tanzania ni kuendelea kusaidia na kuwa mwenyeji wa sekretarieti ya ECSA-HC," amesema Waziri Mkuu Majaliwa.Ametumia mkutano huo kuwataka mawaziri hao na wadau wengine wa afya ambao wamedhuria mkutano kuweka mkakati wa namna ya kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama TB na magonjwa ya kuambukiza.

Mbali ya kuzungumzia mambo yanayohusu uboreshaji wa huduma za afya,Waziri Mkuu Majaliwa amewaomba washiriki kabla ya kuondoka watembelee vivutio vya utalii vilivyopo nchini.Kwa upande wa baadhi ya washiriki wa mkutano wameelezea hatua wanazochukua kuboresha sekta ya afya huku wakiisifu Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dk.John Magufuli ambavyo upo imara katika usimamizi mzuri wa mambo mbalimbali.Kauli mbiu ya mkutano huo wa 65 kwa mawaziri hao wa afya unasema Ushiriki wa sekta ya afya katika kupata mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu(SDG's).
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akifungua Mkutano wa kimataifa wa masuala ya Afya, uliohudhuliwa na Mawaziri kutoka nchi za Afrika Mashariki, Afrika ya kati na Afrika ya Kusini.

MAGAZETI YA JUMANNE LEO MARCH 20,2018

WAZIRI WA MAJI AZUNGUMZIA UMUHIMU WA KUKABILIANA NA UHARIBIFU WA VYANZO VYA MAJI, MAZINGIRA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema ni muhimu kuwekwa mikakati ya kukabiliana na uharibifu unaoendelea katika vyanzo mbalimbali vya maji na misitu nchini.

Mhandisi Kamwele amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani na kwa Tanzania lengo lake ni kuangalia uwezekano wa kuwapatia maji safi na salama kwa watanzania wote.

Aidha ameeleza mkakati wa kuvuna maji ya mvua ili kupata maji shuleni kupitia matanki na visima vya kujenga ambapo anaamini itasaidia kuondoa changamoto ya uhaba wa maji shuleni.

Pia ameeleza mafanikio katika suala la maji na majengo katika shule za Kirumba na Isenyi jijini Mwanza pia katika ujenzi wa vyoo na vyumba kwa wanafunzi wa kike.

Ameshukuru Benki ya dunia, Serikali ya Korea  na Mpango wa maendeleo Ufaransa kwa ushirikiano wao katika suala la maji na utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji ni lazima.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza wakati wa kufungua Mkutano wadau wa maji uliandaliwa na benki ya Dunia nchini uliokwenda kwa jina la 'TANZANIA WASH POVERTY DIAGNOSTIC' uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.
 Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Malawi na Burundi, Bella Bird akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Maji na Umwagiliaji kufungua mkutano huo muhimu kwa ajili ya maji Tanzania.
 Mwasilishaji wa mada juu ya kupinga umaskini na uhaba wa maji  Mchumi wa Benki ya Dunia, George Joseph akizungumza na wadau wa maji waliofika katika mkutano huo.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini(TUDARCO), Prof.  Uswege  Minga  akizungumzia na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa utunzaji wa maji na na mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na baadae.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAKAZI WA KATA TANO DAR WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUINGILIA KATI UBOMOAJI WA NYUMBA ZAO

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii
WAKAZI wa Kata  tano  wa Jiji la Dar es Salaam wamemuomba Rais Dk. John Magufuli kuingilia kati ubomoaji wa  nyumba kata hizo katika kupisha ujenzi wa bomba la Maji la Ruvu.

Kata zitazoathirika kwa makazi katika upanuzi wa ujenzi wa bomba la Ruvu Juu ni Wazo, Salasala, Bunju Mbweni pamoja na Mabwepande

Akizungumza na waandishi wa habari mkazi wa Salasala Dk. Julian Bujugo amesema hawapati usingizi tangu walivyoambiwa wavunje nyumba zao wakati sheria inawalinda.

Amesema sheria ya mwaka 2001 ya Dawasa katika ujenzi wa mabomba yao ni mita tano (5) lakini sasa wameambiwa ni mita 15 ambazo hiziko katika sheria 

Bujugo amesema kuwa katika suala hilo walitaka kwenda mahakamani lakini waliona wazungumze ili kuweza kusema kwa Serikali kitu ambacho kinawatatanisha kuhusu  uboaji huo.

Amesema kuwa Rais Dk.Magufuli ni mtetezi wa wanyonge,hivyo kwa wakazi wa kata tano jicho lao ni kwa Rais na  sheria inawafanya kuwa halali.

Bujugo amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuangalia suala lao kwani hawana sehemu ya kukimbilia.
Mkazi wa Salasala na Diwani wa Kata ya Magomeni, Dk.Julian Bujugo akizungumza na waandishi habari kuhusiana na ubomoaji wa nyumba zao ambapo ni kinyume cha sheria  jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA HOSPITALI YA ABDALLA MZEE PEMBA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro kuwachukulia hatua mara moja askari polisi ambao wamekiuka maadili na taratibu za jeshi hilo katika mkoa wa Kusini Pemba.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa kuwekwa kwa jiwe la msingi wa ujenzi wa nyumba 36 za askari polisi katika eneo la Mfikiwe, wilaya ya Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba. Makamu wa Rais alitoa pongezi kwa Jeshi la Polisi nchini kwa kuhakikisha nchi inakuwa tulivu na yenye amani pia alitoa pongezi kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Hamad Masauni kwa kusimamia vyema zoezi la ujengaji nyumba za Polisi.

Makamu wa Rais pia alitoa pongezi kwa kampuni ya Twiga Cement kwa kutoa Saruji mifuko zaidi ya elfu sita pamoja na kampuni za Shubash Patel kwa kuchangia vifaavingine vya ujenzi. Awali Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Nchini Mhandisi Hamad Masauni alipongeza Jeshi la Polisi kwa kupambana na biashara haramu ya madawa ya kulevya na kusema yeyote atakayevunja sheria achukuliwe hatua bila kujali wadhifa au umaarufu wake.

Kwa Upende wake Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini ameahidi kufanya kazi kwa taratibu na sheria lakini pia alitoa wasihi kwa wanasiasa wanaochochea vurugu kwani wao watachukuliwa kama wahalifu na si wanasiasa. Ziara ya Makamu wa Rais imekamilika leo ambapo pia alitembelea Hospitali ya Abdala Mzee ambapo alijionea vifaa vya kisasa vilivyowekwa na huduma bora zinazotolewa.

Makamu wa Rais pia aliweka mawe ya Msingi katika ujenzi wa madarasa katika skuli ya sekondari ya Ali Khamis Camp pamoja na ujenzi wa Tawi la Chama Cha Mapinduzi Ole. 

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Hafidh Jabir Ali mwenye umri wa miaka 3 aliyelazwa kutokana na kuungua na chai katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)  
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Rayna Abdala mwenye umri wa mwaka mmoja aliyelazwa kutokana na kuungua moto katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Dkt. Wuxiao Shu juu ya matibabu ya mguu wa mtoto AzarAli mwenye umri wa miaka aliyelazwa  katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi nje ya majengo ya hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba mara baada ya kukagua maendeleo ya hospitali hiyo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

UCSAF YAPEWA SIKU 14 KUWASILISHA RIPOTI YA HALI YA MAWASILIANO PEMBA

$
0
0
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye ameupa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) wiki mbili kwenda Pemba kukagua hali ya mawasiliano ya simu za mkononi na kuwasilisha taarifa hiyo ofisini kwake.
Mhandisi Nditiye ameyasema hayo akiwa kwenye ziara yake ya kikazi Zanzibar ya kukagua hali ya mawasiliano kisiwani humo na kutembelea taasisi za mawasiliano zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambapo suala la mawasiliano ni la muungano.
Nditiye amesema kuwa amepokea taarifa kutoka kwa wabunge wa Kisiwa cha Zanzibar kuwa hali ya mawasiliano kwenye kisiwa hicho sio nzuri na sehemu nyingine hakuna mawasiliano licha ya kuwa kuna minara ambayo inatoa huduma za mawasiliano ila kutokana na jiografia ya Pemba ambapo kuna milima na mabonde hivyo mawasiliano si ya uhakika. “Nawaagiza muende Pemba mkaainishe maeneo yote ambayo hayana mawasiliano na muwasilishe taarifa hiyo ofisini kwangu baada ya wiki mbili,” amesema Mhandisi Nditiye.
Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Ofisi ya Zanzibar Bi. Esuvatie-Aisa Masinga wakati akiwasilisha taarifa yake kwa Mhandisi Nditiye kuhusu majukumu ya ofisi yake ya usimamimizi na udhibiti wa mawasiliano na posta, amekiri kuwa yapo baadhi ya maeneo Pemba na Unguja ambapo hali ya mawasiliano sio nzuri na hairidhishi.
 Meneja Ofisi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Zanzibar, Bi. Esuvatie-Aisa Masinga akitoa taarifa ya hali ya mawasiliano Zanzibar kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kwanza kushoto) wakati wa ziara yake kisiwani humo
 Meneja Msaidizi Mtandao wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Zanzibar Bwana Mohamedi Ali Haji akimuonesha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kwanza kushoto) njia yanakopita mawasiliano kutoka Dares Salaam kuja Zanzibar wakati wa ziara yake kisiwani humo
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye ( wa kwanza kulia) akisikiliza kwa makini maelezo kutok akwa mfanyakazi wa TTCL kuhusu mwitikio wa wateja kwa huduma zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wakati wa ziara yake Zanzibar
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia) akitoa maelekezo kwa mwakilishi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Bwana John Munkondya kuhusu vituo vya mawasiliano vilivyopo Zanzibar wakati wa ziara yake kisiwani humo.
 Mfanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Zanzibar, Bwana Khalfan Mmkahirika akimuonesha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano namna scanner inavyofanya kazi ya kukagua mizigo na vifurushi vinavyosafirishwa na Shirika hilo ndani na nje ya nchi ili kulinda usalama wa raia na taifa wakati wa ziara yake Zanzibar. Mwenye koti nyeusi ni Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika hilo Bwana Hassan Mwang’ombe.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa ziara yake kwa taasisi za mawasiliano Zanzibar. Kushoto ni Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika hilo Bwana Hassan Mwang’ombe na kulia ni Mkurugenzi wa Huduma wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL) Bwana Hussein Selemani Nguvu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MFANYABIASHARA AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 2827

$
0
0
*Ni baada ya kupatikana na hatia ya makosa 419 likiwemo la utakatishaji fedha

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu mfanyabiashara Stanley Mwaura kutumikia kifungo cha miaka miaka 2827 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa 419 ikiwemo utakatishaji  fedha.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya kumaliza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka na utetezi.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Shaidi amesema upande wa mashtaka kupitia mashahidi wake  15 waliofika mahakamani hapo kutoa ushahidi, wamethibitisha mashtaka pasipo kuacha shaka kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo.

Katika kesi hiyo mshtakiwa alijitetea mwenyewe.

Hakimu Shaidi amesema,  mshtakiwa huyo ana makosa 419, ambapo kosa la 1 hadi 99 ni kughushi, kosa la 100 hadi 198 ni kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kosa la 199 hadi 297 kujipatia nyaraka kwa njia ya uongo.  Huku kosa la 298 hadi 396 ni utakatishaji fedha na kosa la 397 hadi 419 ni kughushi.

Hakimu Shaidi amesema kuwa katika kosa la 1 hadi 99 Mahakama inamuhukumu mshtakiwa Murithi kwenda jela miaka 7 kwa kila kosa.

Katika kosa la 100 hadi 198 la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu Mahakama inamuhukumu kwenda jela miaka 7 kwa kila kosa.

Pia kosa la 199 hadi 297 mshtakiwa anahukumiwa kwenda jela miaka 7 kwa kila kosa.

Katika kosa la 298 hadi 396 mshtakiwa amehukumiwa kulipa faini ya Sh. milioni 100 kwa kila kosa sawa na Sh.bilioni 9.9 ama kutumikia kifungo cha miaka miaka 6 gerezani kwa kila kosa.

Pia kosa la 397 hadi 419 amehukumiwa kwenda jela miaka 7 kwa kila kosa.

"Mahakama imekutia hatiani katika makosa hayo 419 ambapo unahukumiwa kwenda jela miaka 7 kwa kila kosa ambapo jumla itakuwa miaka 2827 lakini adhabu hii itaenda sambamba ambapo utatumikia miaka 7 tu gerezani," amesema Hakimu Shaidi.

Miongoni mwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili mshtakiwa ni utakatishaji fedha ambapo inadaiwa kati ya February 6 na 7,mwaka 2012 maeneo ya Jiji la Dar es Salaam alijihusisha katika muamala wa kuhamisha fedha ambazo ni Sh.Mil 4.9 kinyume na sheria.

Pia inadaiwa kati ya April 30 na Mai 5, mwaka 2013 alihamisha kiasi cha Sh.milioni 6.5 kinyume na sheria.

TAFITI MBALIMBALI ZILIZOFANYWA NA WIZARA YA HABARI KUWASILISHWA KWA MAWAZIRI WA UTAMADUNI WA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA

$
0
0
Na Genofeva Matemu - WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe ameahidi kufikisha taarifa ya hatua ambayo Tanzania imefikia katika harakati za kutafiti na kuhifadhi kumbukumbu za ukombozi wa Bara la Afrika kwa mawaziri wa utamaduni wa nchi za kusini mwa Afrika ili nchi hizo wanachama ziweze kuendelea na hatua nyingine ya kuchangia katika ujenzi wa kituo cha kuhifadhi kumbukumbu hizo.
Waziri Mwakyembe ameyasema hayo leo Mkoani Mbeya alipofanya ziara kukagua maeneo yaliyotumika wakati wa harakati za ukombozi wa Bara la Afrika na kusema kuwa serikali ipo katika mpango ambao maeneo yaliyotumika katika harakati za ukombozi wa Bara la Afrika yatakarabati na kurejesha muonekano wake wa awali ili yasipotezi historia.
“Majengo yaliyotumika katika harakati za urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika ni sehemu ya historia na maeneo muhimu sana ambayo yanatakiwa kuboreshwa ili yaweze kuendelea kuwepo katika muonekano ule ule wa awali kwa lengo la kutokupoteza historia yake” amesema Mhe. Mwakyembe
Aidha Mhe. Mwakyembe amesema kuwa serikali imechukua wajibu wake wa kubaini maeneo yaliyotumika wakati wa harakati za ukombozi wa Bara la Afrika na kuwaomba viongozi wote nchi nzima kuendelea kubaini maeneo na vitu vilivyotumika katika harakati za ukombozi wa Bara la Afrika vilivyopo katika maeneo yao ili wizara   iyaendeleze kwa maslahi ya taifa na Afrika kwa ujumla.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Paul Ntinika (kulia) wakati wa ziara yake leo Mkoani Mbeya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto mwenye miwani) akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Paul Ntinika (kulia mwenye miwani ) alipotembelea eneo la Game lililotumika kama kambi ya wapigania uhuru wa Msumbiji leo Mkoani Mbeya wakati wa ziara yake kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika
Nyumba zilizopo katika eneo la Game zilizotumiwa na wapigania uhuru wa Msumbiji ambazo kwa sasa zinatumiwa na Idara ya Maliasili na utalii.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akimsikiliza Mratibu wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika Bibi. Ingiahedi Mduma (kulia) alipotembelea Nyumba ya Binti Matola aliyekuwa mwanaharakati na rafiki wa Mwalimu Nyerere ambaye aliweza kumhifadhi Hayati Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wakati wa ziara yake kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika leo Mkoani Mbeya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAKAGUA UJENZI WA OFISI ZA UHAMIAJI MKOANI MTWARA.

$
0
0
 Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na afisa uhamiaji Mkoa wa Mtwara, James Mwanjotile (kulia) wakati kamati hiyo ilipoenda kukagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara tarehe 19 Machi, 2018 Mkoani Mtwara.
 Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kulia) akipokelewa na katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto) wakati kamati hiyo ilipoenda kukagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara tarehe 19 Machi, 2018 Mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (katikati) akisisitiza jambo pale kamati hiyo ilipokuwa inakagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara tarehe 19 Machi, 2018 Mkoani Mtwara.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama wakimsikiliza kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara (hayupo kwenye picha) akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa katika kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Salum Rehani akizungumza jambo wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa katika kikao kilichofanyika  ofisini kwake Mkoani Mtwara.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

DC MTWARA AFUNGUA KONGAMANO LA WAJASIRIAMALI MJINI MTWARA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Mtwara Bw. Evod Mmanda akifungua kongamano la wajasiriamali katika ukumbi wa chuo cha ualimu Mtwara lililofadhiliwa na shirika la VSO. Lengo la kongamano hilo ni kuwajengea wajasiriamali hao uwezo na utayari wa kukamata fursa zitakazotokana na ugunduzi wa gesi unaoendelea katika mkoa huo na ukanda wa mikoa ya kusini kwa ujumla wake Kongamano hilo limefanyika leo 20.3.2018.
Wawasiliamali hao wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda hayupo pichani wakati akifungua kongamano la kuwajengea uwezo linalofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu mjini Mtwara. 
Mkuu wa wilaya ya Mtwara Bw. Evod Mmanda akiwa katika picha ya pamoja na wajasiriamali hao mara baada ya kufungua kongamano hilo mjini Twara leo.

TAZAMA SHEREHE ZA MKOMAULA KABILA LA WAYAO MKOANI RUVUMA

$
0
0
Kulia ni Sultani Mataka ambaye ni sultani wa tano wa kabila la wayao Tanzania akisalimiana na Mwandishi wa Ruvuma TV Nancy Mbogoro .
………………….
Kupitia kipindi cha Utalii cha Talii na Ruvuma TV tumekuandalia kipindi maalum kinachohusu Sherehe za asili za kabila la Wayao katika mkoa wa Ruvuma, Sherehe hizi zinakwenda kwa jina la Mkomaula, Sherehe hizi hufanyika kila mwaka na kuongozwa na Sultan Mataka ambaye ni Sultan wa tano wa kabila la Wayao Tanzania. Hii hapa chini Video yake.
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images