Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110120 articles
Browse latest View live

PICHA MBALIMBALI ZA AROBAINI YA MSIBA WA MZEE KINGUNGE NA MKEWE

$
0
0

 Ndugu wa Marehemu Kingunge Ngombalemwilu wakiwa katika picha ya pamoja mara bada ya kuhitimisha arobaini katika makaburi ya kinondoni Dar es Salaam.
 Mtoto Maraehemu Mzee Kingunge Gombalemwili , Kinjeketile Ngombale akiwa na mkewe akiweka shada la maua kwenye kaburi la babayake wakati wa kuhitimisha arobaini ya msiba wa Baba yake na Mama yake katik amakaburi ya kinondoni jijini Dar es Salaam.
 Ndugu wa Marehemu Mzee Kingunge  Ngombalemwilu wakiwa wamekusanyika katika kuomboleza arobaini ya msiba  katika makaburi ya kinondoni.

Waziri Mwakyembe atembelea Maeneo yaliyotumika harakati za Ukombozi na ya kihistoria Mkoani Iringa

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (watatu kushoto) akiwasili katika makumbusho ya Mtwa Mkwawa yaliyopo Kalenga kwa ajili ya kuona naoma makumbusho hiyo inavyohifadhi na kuendeleza historia ya shujaa Mkwawa aliyepigana vita vya msituni wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka kwa utumwa wa wajerumani jana Mkoani Iringa. Watatu kulia ni Mratibu wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika Bibi. Ingiahedi Mduma
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) akiangalia fuvu la Mtwa Mkwawa alipotembelea makumbusho ya Mkwawa yaliyopo Kalenga kwa ajili ya kuona naoma makumbusho hiyo inavyohifadhi na kuendeleza historia ya shujaa Mkwawa aliyepigana vita vya msituni wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka kwa utumwa wa wajerumani jana Mkoani Iringa.
Mtaalamu kutoka makumbusho Mkwawa (kulia) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrion Mwakyembe (wapili kulia) baadhi ya vifaa alivyotumia Mtwa Mkwawa wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka katika utumwa wa wajerumani jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa ameshika silaha za jadi alizokuwa anatumia Mtwa Mkwawa wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka katika utumwa wa wajerumani jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiangalia kaburi la Mtwa Abdul Adam Sapi Mkwawa alipotembelea makaburi ya machief kutoka ukoo wa Mkwawa jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.

SHULE ZA AL MUNTAZIR, KSIJ KUTOA ELIMU K WA WATOTO WENYE UMRI WA ZAIDI YA MWAKA MMOJA HADI 18

$
0
0
SHULE za Al Muntazir zinaendeshwa chini ya mwamvuli wa KSIJ- Central Board of Education na hutoa  Elimu kwa watoto wenye umri kati ya mwaka mmoja na nusu hadi wenye umri wa miaka 18. 

Mifumo mbali mbali ya Elimu ya shule za Al Muntazir inaanzia wale wachanga tunawaita toodlers kuendelea Shule ya awali, msingi, sekondari na mwisho ngazi ya juu ya sekondari yaani A- levels.

 Shule za Al Muntazir zinasikia fahari kwani  hadi sasa zinatoa elimu kwa wanafunzi zaidi ya 4500 na kutengeneza ajira zaidi ya 400 za walimu na wasio walimu. Shule za Al Muntazir zinajulikana kwa kupenda kwao mafanikio na kupigania UBORA.

Moja kati ya miradi ambayo KSIJ- Central Board of Education imeanzisha kwenye hii miaka ya karibuni ni uendeshaji wa  shule ya wanafunzi  wenye mahitaji maalumu ya Al Muntazir kwa kifupi tunaiita (AMSEN) ambayo ilianza rasmi mwaka 2013, na kwa miaka 5 tu imefanikiwa kuelimisha wanafunzi zaidi ya  75.

AMSEN inatoa huduma hii ya Elimu  katika mazingira yenye madarasa na vifaaa vya kutosha na kukidhi mahitaji, chumba chenye nafasi na vifaa vya kutosha kwaajili ya (OT) Ocupational Therapy, speech na lugha, aqual therapy pool na uwanja wa michezo wa kutosha.

Shule hii ya watoto wenye mahitaji maalum AMSEN Wanatoa mafunzo na Elimu kwa watoto wenye ugumu katika kujifunza, usonji, dyslexia, Down Syndrome, Cerebral Palsy na nyinginezo za aina hizo.

Inahudumia watoto wenye umri kuanzia make 3 hadi 22.  Shule hii inatoa huduma ili kukidhi matarajio ya watoto hawa wenye mahitaji maalumu ili wajitahidi kufikia malengo yao katika harakati za kujipatia ajira kila mmoja kwa jinsi ya upekee wake alivyo umbwa na Mwenyezi Mungu.

Shule ya AMSEN iliyopo chini ya mwamvuli wa KSIJ- Central Board of Education imekua ikiandaa matembezi ya hiari  kwa muda wa miaka 4 mfulurizo ili kuweka alama ya siku ya usonji Duniani.Matembezi haya ni ishara ya juhudi katika kueneza ujumbe wa kuwafanya watu wote watambue na kuelewa kuhusu watoto wenye mahitaji maalumu.

Mwaka huu tena tumeandaa matembezi kwa mara ya 5  kwa kauli mbiu isemayo “TUWAPENDE NA TUWALINDE”

Kuwapenda na kuwalinda siyo tu kwa kuwaweka ndani na  kuwapa mahitaji mbali mbali wanayo hitaji, bali ni kwa kwa kuwapatia elimu na mafunzo ili waweze kujitegemea na kuonyesha ulimwengu kwamba wanaweza kufanya yote ambayo watoto wengine wa kawaida wanafanya napengine zaidi yao.

Na hiki ndicho ambacho haswa KSIJ Central Board of Eduacation ,kupitia shule ya watoto wenye mahitaji maalumu ya Al Muntazir imekua ikifanya na inataka watoto hawa wapate maisha yenye heshima na yaliyotulia.

Kwa mantiki hiyo basi napenda  kuwaalika   wazazi wakiambatana na watoto wao pamoja na umma yote ya watanzania popote walipo waungane nasi siku ya tarehe 25 Machi 2018 ili kutuunga mkono katika matembezi haya yatakayoanzia kwenye viwanja vya shue ya Msingi ya Al Muntazir Wavulana  iliyopo Barabara ya Barak Obama na kumalizikia kwenye viwanja vya shule ya msingi ya  Al Muntazir Wasichana iliyopo Barabara ya Umnoja  wa mataifa.

Naomba mtambue kuwa  peke yetu hatuwezi kufikia malengo BALI kwa  pamoja tutaweza.
NITATEMBEA KWAAJILI YA WATU WENYE USONJI WEWE JEeee?

WAZIRI MKUU ASHUHUDIA MCHEZO WA KIRAFIKI VIJANA WA NGORONGORO HEROES NA MOROCCO

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Morocco nchini, Abdelilah Benryane, walipokutana  kushuhudia mchezo wa kirafiki wa kimataifa, Timu ya Taifa Vijana  walio chini ya Umri wa miaka 20 (Ngorongoro Heroes )na Timu ya Morocco. Ambao umefanyika jana kwanye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam March 18, 2018. 
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya mashabiki wa Tanzania na Morocco walio kuja kushudia mchezo wa kirafiki wa Kimataifa  wa Timu ya Taifa Vijana  walio chini ya Umri wa miaka 20 (Ngorongoro Heroes )na Timu ya Morocco.Kushoto kwa Waziri Mkuu ni Balaozi wa Morocco Nchini Tanzania ,Abdelilah Benryane . mchezo huo umefanyika jana kwanye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam March 18, 2018.

VLADIMIR PUTIN ASHINDA KWA KISHINDO URAIS URUSI

$
0
0
Rais wa Urusi Vladimir Putin wa Chama cha Independent.

Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
RAIS wa Urusi Vladimir Putin wa Chama cha Independent kwa mara nyingine ameibuka mshindi wa kiti cha urais kwa muhula mwingine wa miaka sita.

Putin ameibuka na ushindi mnono wa zaidi ya asilimia 77, akiwamwaga Pavel Grudinin wa Communist party na Vladmir Zhirinovsky wa Chama cha "LDPR" katika uchaguzi uliofanyika jana Machi 18 mwaka huu.

Putin (65) alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuongoza taifa hilo mwaka 2000 ambapo alihudumu kwa mihula miwili na akachaguliwa kuwa Waziri Mkuu kwa muhula mmoja.

Mwaka 2012 Putin   alichaguliwa kuwa Rais na ni kipindi ambacho mihula ya uongozi iliongezwa kutoka miaka 4 hadi 6.

Ushindi huo unamfanya Vladimir Putin kwa Rais wa urusi hadi 2024.

UONGOZI Institute to hold first graduation ceremony for Postgraduate Diploma in Leadership

$
0
0
Dar es Salaam: The graduation ceremony for the first group of graduates of the UONGOZI Institute Post-Graduate Diploma (PGD) in Leadership is scheduled to take place on 21st March 2018 at the Institute’s premises, where a total of 30 participants will be graduating.

This first group of graduates comprises of senior police officers who were selected from different regions of the United Republic of Tanzania. The Diploma program, encompassing 10 modules, focuses on enhancing leadership competencies in 3 areas, Making Strategic Choices, Leading People and Other Resources and Excelling in Personal Leadership Qualities.

The graduation ceremony will be officiated by Hon. George H. Mkuchika (MP), Minister of State, President’s Office, Public Service and Good Governance. Minister of Home Affairs, Hon. Mwigulu Nchemba (MP) and the Inspector General of Police, Mr. Simon Sirro, will also be in attendance.

“We are pleased to note that 97% of the police officers that began the training will graduate. This has been an intensive and challenging programme, and the discipline and commitment they have shown is a true testament of their leadership capacity” said Prof. Semboja, CEO of UONGOZI Instiute.

UONGOZI Institute and Aalto University Executive Education of Finland have jointly been running the one-year Post-Graduate Diploma in Leadership, an executive programme that is designed to equip senior government officials with the necessary skills and competencies to provide sustainable solutions through effective leadership.

“Since we started this course back in April 2017, I have learnt a lot on how to solve challenges of all sorts whenever they come across my office. It is a very useful training, not only for police officers, but it needs to be offered to all other public servants across the country,” said Mr. Benedict Michael Kulyamba, Chief of the Human Resource Division of the Tanzania Police Force and one of the graduates.

The graduation ceremony will also be attended by 32 participants from the second cohort of the Post-Graduate Diploma in Leadership, scheduled to begin at the end of March. The second cohort includes senior government officials from various Ministries and Public Agencies.

MSAJILI AZITAKA NGOs KUWASILISHA TAARIFA

$
0
0
MASHIRIKA yasiyo ya Kiserikali nchini (NGOs) yaaswa kuwasilisha taarifa za Mwaka kwa mujibu wa Kifungu Na. 29 cha Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 na Kanuni Na. 10 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2004 (GN 152, 2004) kabla ya tarehe 15 Aprili, 2018.

Hayo yameainishwa katika taarifa ya Msajili wa Mashirika yasiyo ya kiserikali Marcel Katemba kwa vyombo vya habari  jijini Dar es Salaam leo. Taarifa hiyo inaeleza kuwa “Mashirika yasiyo ya kiserikali kuwasilisha Taarifa za Mwaka kwa mujibu wa Kifungu Na. 29 cha Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 na Kanuni Na. 10 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2004 (GN 152, 2004), kama ilivyorekebishwa na Kanuni Na. 6 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2014 (GN 8, 2015)”.

 “Taarifa hiyo ijumuishe Taarifa za utendaji kazi, Taarifa za fedha zilizokaguliwa, NGO Fomu Na.10 na Stakabadhi ya malipo ya ada ya mwaka” 

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Mashirika yatakayoshindwa kutekeleza agizo hili ndani ya kipindi tajwa, yatachukuliwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutozwa faini. 

GESI YALETA KIZAAZAA, WATU WATANO WANUSURIKA KIFO KIDONGO CHEKUNDU - RPC SHANNA

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

WATU watano wamenusurika kifo baada ya nyumba kuteketea kwa moto, katika kitongoji cha Kidongo Chekundu kata ya Magomeni wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani. Hili ni tukio la pili linalohusiana na janga la moto kutokea ndani ya wiki moja mkoani hapo ambapo machi 11, nyumba ya Makulata Petro iliungua huko Magwila wilaya ya Chalinze na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi wawili .

Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna alielezea tukio hilo, limetokea machi 18 saa 5:30 asubuhi . Alisema  ,moto huo umeteketeza nyumba hiyo na kwasasa majeruhi hao wanapatiwa matibabu hospitali ya wilaya ya Bagamoyo .

Kamanda Shanna aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Emmanuel Nangu (33) mfanyabiashara ambaye ameungua miguu na mke wake Victoria Mushi (32) aliyejeruhiwa kifuani na mikononi. Mwingine ni msichana wa kazi Jovina Mapinduzi (16) aliyeungua miguuni na mapaja.

Aidha kamanda huyo alisema ,moto huo ulipotokea mitungi miwili ya gesi ilipasuka na kuruka juu na kupasua paa kisha kutoka nje na kuwajeruhi pia wapita njia ambao ni Msafiri Mohammed (36) na Hadija Juma (22) ambaye anuvunjika mguu.

"Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na kinachunguzwa licha ya kuwa na dhana mbili juu ya moto huo moja ni mitungi ya gesi na tatizo la umeme," alisema Shanna.

Alieleza wananchi wanapaswa kuangalia miundombinu ya umeme kwani baadhi ya nyumba ni michakavu.

"Kikosi cha zimamoto kinapaswa kutoa elimu kwa wananchi ili kutambua mitungi ya gesi ambayo haina matatizo " alifafanua kamanda Shanna.

Kamanda Shanna alisema, shirika la umeme (Tanesco) linapaswa kutoa elimu kwa jamii juu ya kufanya marekebisho ya miundombinu ya umeme kwenye nyumba zao. Aliwaasa wenye nyumba kutoa elimu kwa wadada na wakaka wanaowaweka kufanya kazi kwenye nyumba zao ,ili kujua matumizi ya gesi na vyombo vya umeme.

ATAKAYEHUJUMU UJENZI WA MRADI WA MAJI TOKA ZIWA VICTORIA KUKIONA - RC MWANRI

$
0
0
SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imesema itamchukulia hatua kali mtu yoyote atakayebainika kuhujumu utekelezaji wa Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Mkoani humo wenye gharama ya bilioni 600 kwa ajili ya kusaidia kutoa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa leo wilayani Nzega na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wakati alipotembelea na kukagua mradi huo unaotoa maji katika Kijiji cha Solwa mkoani Shinyanga kupeleka mkoani Tabora ambapo wilaya za Nzega, Igunga, Uyui na Tabora mjini zitanufaika na mradi huo wa maji kutoka ziwa Victoria unaotekelezwa kwa muda wa miezi thelathini.

Alisema kuwa Serikali haitamfumbia macho mtu yeyote atakayebainika kuwa na nia ovu ya kutaka kuiba vifaa mbalimbali ambavyo vinatumiwa na wakandarasi katika kujenga mradi huo ambao ni muhimu sana kwa ajili ya wakazi wa maeneo mbali ya Tabora.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza na Mkandarasi na wananchi baada ya kutembelea na kukagua mradi wa maji kutoka ziwa Victoria jana ambapo mradi huo unaotoa maji katika Kijiji cha Solwa mkoani Shinyanga kupeleka mkoani Tabora ambapo wilaya za Nzega,Igunga,Uyui na Tabora mjini zitanufaika na mradi huo wa maji kutoka ziwa Victoria unaotekelezwa kwa muda wa miezi thelathini. 

Mwanri alisema kuwa hadi sasa kazi inaendelea ambapo Mkandarasi ya kampuni ya L & T yupo kazini akiendelea na shughuli ya kuunga na kufukia mabomba ardhini na kueleza kuwa hujuma yoyote ambayo inaweza kujitokeza inaaweza kusababisha mradi kuchelewa kumalizika kusababisha wakazi wa maeneo ambao yalikuwa yapate huduma hiyo kuendelea kupata matatizo ya maji.

Alisema kuwa kama kuna matatizo yoyote wanayopata kama vile wizi wa vifaa ni vema wakaeleza ili uongozi wa Mkoa uweze kuchukua hatua mapema kwa ajili ya kuendelea kuwawekea mazingira mazuri ya ujenzi wa mradi huo na kuongeza kuwa kama watapata matatizo na kunyamaza na muda wa kukamilisha mradi utafika wakiwa bado hawajakamilisha Serikali haitasikiliza.
Mkuu wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari baada ya kuungana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo pichani) kutembelea na kukagua mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria jana ambapo mradi huo unaotoa maji katika Kijiji cha Solwa mkoani Shinyanga kupeleka mkoani Tabora ambapo wilaya za Nzega,Igunga,Uyui na Tabora mjini zitanufaika na mradi huo wa maji kutoka ziwa Victoria unaotekelezwa kwa muda wa miezi thelathini.

Mwanri aliwataka Wakuu wote wa Wilaya na Watendaji wote ambapo mradi huo unapita kuhakikisha wanasimamia ili isije ikatokee hujuma yoyote na kama ilitokea wakamate watu wote wanatuhumiwa.

Naye Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkama Bwire alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo upo ndani ya utekelezaji na tayari hata malipo ya fidia kwa wananchi  waliopitiwa maeneo yao na mradi yamekwishafanyika. Alisema wananchi 204 ambao maeneo yanapitiwa na Mradi huo na kukabainika kuwa wanatarajiwa kulipwa milioni 890.5 zitatumika  kama fidia  kwa wananchi hao

Alisema kuwa jumla ya milioni 760 zimeshalipwa kwa wananchi zaidi ya 162 ambao maeneo yao yalikwishafanyiwa tathmini.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Nzega alisema wananchi wa wilaya yake wanaupokea Mradi huo kwa furaha kwa kukamilika kwake kutasaidia kuwaondolea tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama ya uhakika. Mradi huu wa Maji unatarajia kuwanufaisha wakazi wa Mkoa wa Tabora wapatao milioni moja ambao watakuwa na uhakika wa maji safi na salama.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na Taka Manispaa ya Tabora (TUWASA) Mkama Bwire akitoa ufafanuzi juu ya ulipaji fidia wakati utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria jana mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri kutembelea na kukagua mradi huo.
Baadhi ya Mafundi wa Kampuni ya L & T wakiwa kazini wakiendelea na shughuli ya kuunga na kufukia mabomba ardhini kwa ajili ya kupeleka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tabora.

RAIS DKT MAGUFULI AENDESHA MKUTANO WA 11 WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara ITNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwasili kuendesha mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 19, 2018. Kulia kwake ni   Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Joakim Mhagama na kushoto kwake ni  Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel 
 Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara ITNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Dkt. Reginald Mengi  alipowasili kuendesha mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 19, 2018. 
 Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara ITNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa meza kuu  na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa  Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu Mhe. Jenista Joakim Mhagama na kushoto kwake ni  Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel  na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Dkt. Reginald Mengi  akijiandaa kufungua  mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 19, 2018.  
 Sehemu ya Mawaziri, Wabunge na wafanyabiashara wakiwa katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara unaoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 19, 2018.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

UFAFANUZI WA BASATA KUHUSU KUFUNGIA KAZI ZA SANAA ZILIZOKOSA MAADILI

JWTZ – KUJENGA VIWANDA KATIKA KAMBI ZA JKT

$
0
0
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo akimuelekeza kitu Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme ambaye ameshika punje za mahindi kiganjani kwake, alipotembelea kiwanda cha kisasa cha kuchakata mahindi cha kikosi cha JKT Mlale Songea Mkoani Ruvuma.

 “ Tunakikosi cha JKT Mbalali kilichopo Mbeya kinalima zao la kahawa na niwazalishaji wazuri wa zao hilo napotutajenga kiwanda cha kuchakata kahawa ili tuwe na Kahawa Product ya JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA ,Tunasambaza viwanda hivi kwa faida ya wananchi wa Tanzania, kwa maendeleo yao ,kwa maendeleo yetu wote, tunaimani tumeanza kuthubutu,tunaimani tutaweza ”

MAKAMU WA RAIS AKISHIRIKI UJENZI WA SEKONDARI MICHEWENI5

$
0
0

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki ujenzi wa skuli ya Sekondari Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mwonekano wa ujenzi wa skuli ya Sekondari Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba

TIGO TANZANIA NA UBER WAUNGANA KULETA OFA MPYA KWA WATEJA WA DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari(wa pili kushoto) akipeana mikono na Meneja Mkuu wa Uber Afrika Mashariki, Loic Amado(wa pili kulia) mara baada ya kuingia makubaliano ya kipekee yatayowafaidisha watumiaji wa Tigo wakaotumia huduma za usafiri za Uber kwa kutumia Uber App bure. Kulia ni Mkurugenzi Mkaazi wa Uber Tanzania, Alfred Msemo na kushoto ni Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha wa Tigo, Hussein Sayed kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar Es Salaam jana.

Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali nchini, Tigo Tanzania imeingia katika makubaliano ya kipekee na kampuni ya kiteknologia ya Uber. Kuanzia leo, wateja wote wa Tigo watatumia huduma za Uber App bure! Makubaliano haya ya aina yake yatawafaidi watumiaji wa huduma za usafiri za Uber pamoja na madereva waliojiunga na mfumo huo. 


“Tigo ni nembo pana ya biashara katika soko la Tanzania na tuna wajibu wa kuzindua njia bora zaidi kwa wateja kujumuika katika maisha yanayowazingira. Makubaliano haya na Uber yanaboresha bidhaa na huduma ambazo wateja wetu wanafurahia katika maisha yao ya kila siku,” Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo, Simon Karikari alisema. 
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari (kushoto) akizungumza katika hafla ya kuingia makubaliano ya kipekee yatayowafaidisha watumiaji wa Tigo wakaotumia huduma za usafiri za Uber kwa kutumia Uber App bure, iliyofanyika jijini Dar Es Salaam leo. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkaazi wa Uber Tanzania, Alfred Msemo, Meneja Mkuu wa Uber Afrika Mashariki, Loic Amado pamoja na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha wa Tigo, Hussein Sayed.

Naye Alfred Msemo, Mkurugenzi wa Uber alisema, “Tunafurahia makubaliano haya na Tigo yatakayowawezesha watumiaji na madereva wa huduma za Uber waliojisajili na mtandao wa Tigo kutumia huduma ya Uber App bure kwenye simu zao za mkononi bila tozo lolote la gharama za data. 

Uber ni mfumo wa simu za kisasa unaowezesha watu kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa kubonyeza kitufe tu! Lengo kuu la Uber ni kuwezesha usafiri salama, wa uhakika na kwa gharama nafuu kwa kila mtu, kila sehemu. Makubaliano haya yatawahamasisha maelfu ya wakaazi wa Dar es Salaam ambao wamejisajili na mtandao wa Tigo kutumia Uber App kwa ajili ya huduma za usafiri jijini Dar es Salaam,’ Msemo alibainisha. 
Kampuni hizi mbili zitashirikiana katika bidhaa na promosheni zitakazoboresha huduma kwa wateja wa sasa na wa siku zijazo. Tigo na Uber nchini Tanzania wanatarajia kutangaza ofa zaidi kabambe zitakazowawezesha wateja kufurahia huduma za Uber jijini Dar es Salaam ambapo huduma za Uber zinapatikana kwa sasa. 

KAMATI YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA YATEMBELEA CHANZO CHA MAJI - IFUNDA

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge Biashara na Mazingira mwishoni mwa wiki imetembea chanzo cha Maji ‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya Ifunda, Mkoani Iringa.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Innocent Bashungwa ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Iringa kwa jitihada zao za kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya kunyweshea mifugo ili kuendelea kulinda vyanzo vya maji na kuwataka kuondoa miti iliyopo pembezoni mwa chanzo hicho ambayo inanyonya maji kwa wingi.
Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola amezitaka Halmashauri na Wilaya zote nchini kupanda miti kwa wingi ambayo ni rafiki kwa mazingira. “Endapo tutapanda miti kwa wingi, tutaendelea kuwa na mvua za kutosha na kila Halmshauri zinatakiwa kuwa na Sheria ndogo ndogo za Mazingira”
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza amewataka waheshiwa wabunge kuwa mstari wa mbele kuhimiza kilimo cha umwagiliaji kwa kutimia ‘matone’ ili kupunguza matumizi ya maji katika maeneo yao.

 Diwani wa Kata ya Ifunda Bw. Elicus Chumila Ngwetta akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mara baada ya kutembelea eneo la Ifunda na kujionea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichohifadhiwa vizuri. Uhifadhi wa vyanzo vya maji ni muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola.
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Kangi Lugola akifafanua jambo mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Kamati ya Bunge mwishoni mwa wiki ilipata fursa ya kutembelea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya Ifunda, Mkoa wa Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza akiwaonyesha waheshimiwa wabunge wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya mifugo kunywa maji katika eneo la Ifunda ikiwa ni jitahada za Mkoa huo kuhifadhi vyanzo vya maji. 

JWTZ – KUJENGA VIWANDA KATIKA KAMBI ZA JKT

$
0
0
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo akimuelekeza kitu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme ambaye ameshika punje za mahindi kiganjani kwake, alipotembelea kiwanda cha kisasa cha kuchakata mahindi cha kikosi cha JKT Mlale Songea Mkoani Ruvuma. “ Tunakikosi cha JKT Mbalali kilichopo Mbeya kinalima zao la kahawa na niwazalishaji wazuri wa zao hilo napotutajenga kiwanda cha kuchakata kahawa ili tuwe na Kahawa Product ya JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA ,Tunasambaza viwanda hivi kwa faida ya wananchi wa Tanzania, kwa maendeleo yao ,kwa maendeleo yetu wote, tunaimani tumeanza kuthubutu,tunaimani tutaweza ”

Wagonjwa 25 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua katika kambi maalum ya matibabu

$
0
0
Na Mwandishi Maalum

Jumla ya wagonjwa 25 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua katika kambi maalum ya matibabu ya siku sita inayofanyika  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Upasuaji huo unafanywa na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya nchini Australia.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo jijini Dar es Salaam  Daktari bingwa wa upasuaji wa  moyo na mishipa ya damu ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya upasuaji Bashir Nyangasa alisema wagonjwa watakaofanyiwa upasuaji watoto ni  15 na watu wazima 10.

Dkt. Nyangasa alisema kambi hiyo imeenda  sambamba na upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wagonjwa 65 kati ya hao watoto 35 na watu wazima  30. Wagonjwa ambao wamefanyiwa uchunguzi na hawatafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo watafanyiwa upasuaji na madaktari wa JKCI.

“Watoto tunaowafanyiwa upasuaji ni wale wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo ambayo ni matundu na mishipa ya damu kutopitisha damu  vizuri katika moyo na kwa watu wazima tunapandikiza mishipa ya damu kwenye moyo (CABG – Coronary Artery Bypass Grafting) na kubadilisha milango ya moyo miwili hadi mitatu iliyoziba au haifungi vizuri.

Kabla ya kuanza kwa kambi hiyo kulikuwa na mafunzo ya kiuguzi ya siku tano ya utoaji  huduma bora kwa  wagonjwa wa upasuaji wa moyo  yalitolewa na Taasisi ya Open Heart International kwa  wauguzi 30 wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete.

Hadi sasa wagonjwa wanne wameshafanyiwa upasuaji wa moyo  kati ya hao watoto wawili na watu wazima wawili na hali zao zinaendelea vizuri.

KAMATI YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA YATEMBELEA CHANZO CHA MAJI, IFUNDA

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge Biashara na Mazingira mwishoni mwa wiki imetembea chanzo cha Maji ‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya Ifunda, Mkoani Iringa.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Innocent Bashungwa ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Iringa kwa jitihada zao za kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya kunyweshea mifugo ili kuendelea kulinda vyanzo vya maji na kuwataka kuondoa miti iliyopo pembezoni mwa chanzo hicho ambayo inanyonya maji kwa wingi.

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola amezitaka Halmashauri na Wilaya zote nchini kupanda miti kwa wingi ambayo ni rafiki kwa mazingira. “Endapo tutapanda miti kwa wingi, tutaendelea kuwa na mvua za kutosha na kila Halmshauri zinatakiwa kuwa na Sheria ndogo ndogo za Mazingira”.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza amewataka waheshiwa wabunge kuwa mstari wa mbele kuhimiza kilimo cha umwagiliaji kwa kutimia ‘matone’ ili kupunguza matumizi ya maji katika maeneo yao.
Diwani wa Kata ya Ifunda Bw. Elicus Chumila Ngwetta akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mara baada ya kutembelea eneo la Ifunda na kujionea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichohifadhiwa vizuri. Uhifadhi wa vyanzo vya maji ni muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akifafanua jambo mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Kamati ya Bunge mwishoni mwa wiki ilipata fursa ya kutembelea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya Ifunda, Mkoa wa Iringa.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akisisitiza jambo mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mara baada ya kutembelea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kinachopeleka maji yake Mto Lyandembela ambao nao unamwaga maji Ruaha Mkuu mwaka mzima, Mto ambao ni muhimu sana kwa ustawi wa viumbe hai. Kushoto ni Mhe. Hawa Mwaifunga na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Innocent Bashungwa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza akiwaonyesha waheshimiwa wabunge wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya mifugo kunywa maji katika eneo la Ifunda ikiwa ni jitahada za Mkoa huo kuhifadhi vyanzo vya maji.

Mhagama: Kilimo cha miwa fursa kwa vijana

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye  Ulemavu  Mhe.Jenista Mhagama amewataka vijana kuchangamkia fursa zilizopo nchini na kuacha kulalamika kuhusu ukosefu wa ajira.
Akizungumza baada ya uzinduzi wa mradi wa shamba darasa kuwezesha wakulima wa nje (outgrowers) wa kiwanda cha Sukari cha Mkulazi  mwishoni mwa wiki katika eneo la Dumila wilayani Kilosa mkoani Morogoro,Waziri Mhagama amesema kundi la vijana linapaswa kuzifuata fursa zilipo na sio kusubiri kuletewa.
Waziri Mhagama amesema serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imejidhatiti kupunguza tatizo la ajira kwa kutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa lakini vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa wanapoteza muda mwingi katika mitandao ya kijamii.
“Takwimu zilizopo kwamba 56% ndio nguvu ya vijana,pia 60.7% ya ajira nchini zinapatika kwenye fursa zinazotokana na kilimo lakini vijana hawa hawataki kabisa kusikia habari za kilimo,” amesema Waziri Mhagama.
Waziri Mhagama amebainisha kuwa  serikali inaboresha mazingira ya kilimo kwa kutenga ardhi na mikopo kwa vijana lakini vijana bado wameonekana kutochangamkia fursa hiyo.
“Kujitokeza kwa vijana katika mradi huu ni wito kwa vijana wengine nchini kuelewa kuwa utajiri unapatikana shambani,njooni tutawapa mashamba mlime miwa na Mkulazi watawasaidia kufikia malengo yenu”, amesema waziri huyo huku akiwapongeza kikundi cha vijana wa KCL ambao walikutana katika mtandao wa ‘WhatsApp’ na kuamua kutafuta mashamba kwa ajili ya kilimo cha miwa.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu  Mhe.Jenista Mhagama akipanda miwa ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa shamba darasa kwa wakulima wa nje (Outgrowers) wa Wilaya ya Kilosa . Mpango huo unaratibiwa na kiwanda cha sukari cha Mkulazi kinachomilikiwa na PPF, NSSF pamoja na Jeshi la Magereza na unalenga kuwajengea uwezo wakulima ili kuzalisha miwa yenye ubora na kuiuza kiwandani hapo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye  Ulemavu Jenista Mhagama akisisitiza jambo baada ya kukagua shamba la miwa la kiwanda cha sukari cha Mkulazi-Mbigiro mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki. Wanaomsikiliza kutoka kulia ni Mkurugenzi wa NSSF Profesa Godius Kahyarara na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk.Steven Kebwe.Kushoto ni Mkurugenzi wa PPF Bw.Wiliam Erio. Kiwanda hicho kinachomilikiwa na PPF, NSSF pamoja na Jeshi la Magereza kinatarajiwa kutoa ajira 100,000 na pia kitazalisha tani 250,000 za sukari kwa mwaka.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAMATI YA USTAWI WA JAMII YA BARAZA LA WAWAKILISHI YAFANYA ZIARA KATIKA WIZARA YA AFYA ZANZIBAR.

$
0
0
 Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed akiikaribisha Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi ilipofika ofisini kwake Mnazi mmoja kwa ajili ya kutoa mrejesho wa ziara yake iliyofanya katika Vitengo vya Wizara hiyo.
 Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini akizungumza machache kabla ya Wajumbe wa Kamati yake kuchangia taarifa ya ziara yao kwa Vitengo vya Wizara hiyo.
 Katibu wa Wizara ya Afya, Asha Abdulla akisoma taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Wizara kwa kipindi cha mwezi Octoba-Disemba 2017/2018 mbele ya Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi.
 Mjumbe wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi, Mwanaasha Khamis Juma (katikati) akichangia taarifa iliyotolewa ya Kamati yao kwa Wizara ya Afya.
 Mjumbe wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi, Masoud Ibrahim ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Bububu akipitia taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Wizara ya Afya kwa kipindi cha mwezi Octoba-Disemba 2017/2018. Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Afya mnazi mmoja. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar.
Viewing all 110120 articles
Browse latest View live




Latest Images