Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

TUZO ZA SZIFF KUFANYIKA APRIL MOSI, STAA WA BEINTEHAA NDANI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) zinatarajia kufanyika April Mosi mwaka huu, huku msanii maarufu kutoka nchini India wa tamthilia ya Beintehaa Pritika Rao 'Aliyah' akitarajiwa kuwa mgeni mwalikwa kuja kushuhudia utowaji wa tuzo hizo.

Hayo yamesemwa wakati wa utangazaji wa vipengele vinavyoshindanishwa katika upatikanaji wa washindi wa tuzo hizo vikiwa katika makundi 19 ikiwemo tuzo ya chaguo la watazamaji (viewers Choice Awards).

Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi mtendaji wa Azam Media Tido Mhando amesema kuwa SZIFF ni tuzo za kwanza kubwa kabisa kufanyika nchini ikiwa ni katika malengo mojawapo ya kuibua na kuendeleza tasnia ya Sanaa ya maigizo na filamu ambapo filamu shiriki kutoka Tanzania, Kenya, Burundi, Rwanda na DRC Kongo zimeingia kwenye kinyang'anyiro hicho.

"Timu nzima ya tuzo za SZIFF waliweza kupita mikoa yote nchini na waliweza kupata filamu nyingi sana mikoani na hata nje ya nchi ikiwemo Kenya,Burundi,Rwanda na DRC na zikiwa zimeingia katika kinyang'anyiro cha ushiriki wa tuzo hizo kubwa nchini ikiwa ni mara ya kwanza,"amesema Mhando.

Mhando amesema kuwa SZIFF imejikita zaidi katika filamu zenye maudhui ya kiswahili ambapo takribani filamu 143 zilifanikiwa kupambanishwa na kuruka kila siku kupitia chaneli ya Sinema Zetu na watazamaji waliweza kupata fursa ya kupiga kura.

Kwa upande wa Msimamizi wa tuzo za SZIFF Zamaradi Nzowa amesema kuwa tuzo hizi ni kubwa na mbali na washindi kupata tuzo pia wataweza kuondoka na kitita cha pesa taslimu na utambulisho maalumu na kipekee kwenye soko la tasnia ya filamu ukanda wa Afrika Mashariki na Kati pamoja na nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara.

"Tuzo za SZIFF zitaweza kuitangaza nchi yetu sehemu mbalimbali sambamba na lugha ya kiswahili na pia washindi watajinyakulia pesa taslimu kwani filamu zaidi ya 500 ziliweza kuchujwa kwa vigezo vilivyokuwa vimeweka na majaji wetu ambao hawakuweza kutangazwa hadharani," amesema Zamaradi.

Katika kuweza kuwapata washiriki na washindi mbalimbali,Azam Tv waliweza kushirikiana na COSOTA, BASATA pamoja na bodi ya filamu nchini katika safari ya mchakato mzima wa kuwania tuzo za SZIFF ulioanza rasmi Januar Mosi mwaka huu na kumalizika Machi 12 ambapo filamu zaidi ya 500 zilipokelewa na kuchujwa kwa kutumia vigezo vya kisheria na ubora wa maudhui.

Baadhi ya tuzo zinazowaniwa ni pamoja na Best film, best director, best actor, best actress, best commedian na Best screen play. Zingine ni best editing, best original music, best cinematography hizo zikiwa katika filamu ndefu,filamu fupi pamoja na makala.
Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando akizungumza na wanahabari wakati kutangaza vipengele vya tuzo za Sinema Zetu Film Festival (SZIFF)  inayotarajiwa kufanyika April Mosi Mwaka huu na muigizaji wa tamthilia ya Beintehaa Pritika Rao 'Aliyah' akitarajiwa kuwa mgeni mwalikwa. Kulia ni Mkurugenzi msaidizi wa Azam Media Jacob Joseph.

 Jaji Mkuu wa Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) Martin Mhando akitaja vipengele vyinavyowaniwa katika tuzo hizo zitakazofanyika April Mosi. Kulia ni Msimamizi wa Tuzo hizo Zamaradi Nzowa
 Baadhi ya Wana habari wakifuatilia mkutano huo
  Msimamizi wa tuzo za Sinema Zetu Film Festival (SZIFF) Zamaradi Nzowa akielezea jambo kwa wanahabari wakati wa utajaji wa vipengele 19 vinavyowaniwa kwenye tuzo hizo

TUMEJIANDAA VILIVYO TAMASHA LA PASAKA CCM KIRUMBA APRILI 1-JOHN LISSU

$
0
0
*Awaambia wakazi wa Kanda ya Ziwa wafike kuona burudani, Msama awahakikishia usalama, maandalizi yamekamilika

Na Said Nwishehe,Globu ya jamii

MWANAMUZIKI maarufu wa nyimbo za Injili John Lissu amewaomba mashabiki wa muziki huo na Watanzani kwa ujumla hasa wakazi wa Kanda ya ziwa kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Aprili 1 mwaka huu.

Lissu ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia Tamasha la Pasaka ambalo mwaka huu litafanyika Uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza siku ya Aprili 1 na Aprili 2 litafanyika mkoani Simiyu katika uwanja vya Halmashauri mjini Bariadi.

Mwanamuziki huyo ameeleza kuwa wanamuziki mbalimbali maarufu wa muziki wa Injili ndani na nje ya Tanzania wataonesha vipaji vyao vya kuimba,hivyo kikubwa ni wakazi wa Kanda ya ziwa kujitokeza kwa wingi siku hiyo.

Tamasha hilo ambalo huwa linaandaliwa na Kampuni ya Msama Promotion kupitia Mkurugenzi Mkuu Alex Msama ,wamehakikisha kuwa kutakuwa na  idadi kubwa ya wanamuziki wa Injili ili watu  wataofika kwenye tamasha hilo wapate burudani inayoambatana na ujumbe wenye kumpendeza Mungu

"Tunawaomba wakazi wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla tukutane uwanja vya CCM Kirumba siku ya Aprili 1 mwaka huu,wanamuziki wa Injili tumejiandaa vizuri,mashabiki karibuni muone kile ambacho tumekiandaa kwa ajili yenu.

" Siku hiyo mashabiki wa muziki wa Injili watarajie  mambo makubwa zaidi hasa kwa kuzingatia ukubwa wa Tamasha hilo nwa kwamba linafanyika wakati wa Pasaka na mwaka huu tupo Kanda ya Ziwa kwa mara ya kwanza,"amesema John Lissu.
  Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. lex Msama kushoto  akifafanua kuhusu maandalizi ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika kanda ya ziwa Aprili 1 na 2 mwaka huu, mapema leo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar,kulia ni mmoja wa waimbaji mahiri wa nyimbo za Kiroho (injili) John Lissu akifurahi jambo kwenye mkutano huokuhusu maandalizi ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika kanda ya ziwa Aprili 1 na 2 mwaka huu.

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. lex Msama kushoto  na Mwanamuziki wa Injili John Lissu wakiimba wimbo  wakati walipozungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika kanda ya ziwa Aprili 1 na 2 mwaka huu.

RC TABORA: FICHUE RAIA WA KIGENI AMBAO WATAJIANDIKISHA KUPATA VITAMBULISHO VYA TAIFA.

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
MKUU  wa Tabora Aggrey Mwanri amewataka wakazi wa Wilaya ya Urambo kuwa makini kwa kutoa taarifa sahihi wakati wa zoezi la uandikishaji kwa ajili ya vitambulisho vya Taifa ili watu wasiostahili wasije wakajipenyeza na kupatiwa vitambulisho bila kustahili.

Akizungumza katika Kijiji cha Ussoke Mlimani alisema kuwa wananchi wanatakiwa kufichua watu wote wasio raia ambao wanataka kujiandikisha ili waweze kupata vitambulisho kinyume cha sheria.

Mwanri alisema huku nyuma Urambo katika sehemu ya Ulyankulu ilikuwa Makazi ya wakimbikizi kutoka nchi jirani na kuongeza kuwa upo baadhi yao wakawa wameshajipenyeza katika maeneo mbalimbali mkoani humo bila kufuata taratibu.

Alisema ni jukumu la kila mkazi wa Urambo ambaye ni mzalendo kufichua mbinu chafu kama zitaka kufanyika ili kuficha ukweli wa mtu kwa makusudio ya kutaka kumpa kitambulisho mgeni.

Mwanri alisema ili zoezi hilo liwe na tija kwao na Taifa ni vema wananchi wakatoa ushirikiano kwa watendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), viongozi wa Wilaya wanapomtilia shaka mtu anayetaka kujiandikisha ili uchunguzi ufanyike kuzuia udanganyifu huo.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa Wakazi wote wa Mkoa huo ambao wana sifa kuendelea kujitokeza kwa wingi kwenda katika maeneo yalipopangwa ili kujiandikisha kabla ya muda wa mwisho wa zoezi hilo.

Alisema kitendo cha baadhi ya watu kupenda kujiandikisha siku za mwisho kimekuwa kikisababisha msongamano na usumbufu kwa wananchi na kuongeza ili kuepuka ili waende mapema vituoni.

Balozi wa Kuwait azuru Shule ya Sekondari ya Old Tanga

$
0
0
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem amezindua kituo cha kompyuta katika Shule ya Sekondari ya Old Tanga ikiwa ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi huo unaofahamika kwa jila la “KITUO CHA KOMPYUTA KATIKA KILA TAASISI YA ELIMU”. kituo hiki ni cha pili kuzinduliwa nchini na Ubalozi huo kufuatia kile cha awali kilichozinduliwa mwaka jana katika Taasisi ya Taaluma Chuo Kikuu Dar es Salaam.

Kituo cha Kompyuta katika Shule ya Old Tanga kimeunganishwa na huduma ya mtandao ili kuhamasisha wanafunzi juu ya matumizi ya teknolojia kwa kupitia kompyuta zinazopatikana ndani yake ili kufanikisha utekelezaji wa mipango ya elimu kwa njia za kieloktroniki.
Wakati huo huo Balozi Al-Najem amezindua uwanja wa mpira wa miguu,  mpira wa wavu na pia  kuahidi kusaidia na kugharamia ujenzi wa viwanja hivyo  kwa kubadilisha eneo ambalo lilikuwa limetelekezwa na kulifanya viwanja vya michezo.

Pia Balozi aligawa geloni za kuhifadhia maji za lita 22 kwa kila darasa katika Shule ya Sekondari ya Old Tanga kuwarahisishia wanafunzi kupata maji safi na salama badala ya kusongamana na kusukumana katika kisima ambacho kilizinduliwa na balozi miezi michache iliyopita.
 Hii ni ziara ya pili kufanywa na Balozi wa Kuwait katika Shule ya Sekondari ya Old Tanga baada ya ziara ya kwanza mwezi Desemba mwaka jana ambapo alizindua kisima ikiwa ni mwendelezo wa mradi wa Ubalozi “KISIMA CHA MAJI KATIKA KILA SHULE” kwa ushirikiano na Taasisi ya Direct Aid ya Kuwait.
Katika ziara ya mwisho Balozi alifuatana na maafisa mbalimbali akiwemo mwenyekiti wa Bodi ya Shule na meya wa zamani wa Tanga Bwana Salim Kisauyi, mkurugenzi wa jiji la Tanga na afisa elimu waliowakilishwa na afisa Taaluma Bhoke Robin na afisa elimu wa Kata Furaha Godfrey na mwakilishi wa Meya wa sasa.

ABIRIA WANUSURIKA KIFO KUFUATIA KUPINDUKA KWA BASI LA KIMOTCO NDANI YA MTO

$
0
0
Basi la Kampuni ya Kimotco (pichani) lililokuwa likitoka Musoma,kwenda Arusha kupitia Mugumu,limepinduka katika mto unaodaiwa kuwa na viboko ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo William Mwakilema amethibitisha kupata taarifa ya tukio hilo leo Machi 16,na kusema kuwa katika ajali hiyo hakuna majeruhi wala vifo,na kuwa abiria wote wako juu ya basi.

Jitihada za kuwaokoa mmoja mmoja zinaendelea.Baada ya basi hilo kusombwa na maji abiria wote walitokea juu ya madilisha ya basi na kukaa juu yake,kwani halikuzama lote,jitihada za kuwaokoa zinaendelea  mpaka sasa,ambapo zaidi ya abiria wanne  wametolewa.

TAARIFA ZAIDI TUNASUBIRI KUTOKA MAMLAKA HUSIKA 

 Baadhi ya abiria wakiwa juu ya basi hilo mara baada kupinduka,wakiokolewa mmoja mmoja na Lori kama ionekavyo pichani
Basi likiwa limepundika kwenye mto ndani ya hifadhi ya serengeti.

RC MAKONDA AZINDUA WIKI YA MAJI KWA MKOA WA DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na wenyeviti wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani pamoja na Wafanyakazi wa Dawasa ambao wameudhuria  kwenye uzinduzi wa wiki ya maji kwa mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere hapa jijini. 
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya maji kwa mkoa wa Dar es Salaam ambapo alisema ni vyema Dawasco wakaongeza usambazaji wa maji katika mkoa huo hili kusaidia ukuaji wa maendeleo ya Viwanda hapa nchini.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa DAWASCO, Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza wakati wakati wa uzinduzi wa wiki ya maji kwa mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika leo.

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala , Edward Mpogolo akizungumza na wadau wa maji waliofika katika uzinduzi wa wiki ya maji kwa mkoa wa Dar es Salaam, pia alieleza mafanikio ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kipindi cha Miaka Miwili.
 Baadhi wafanyakazi wa Dawasa na DAWASCO waliohudhuria kwenye uzinduzi wa wiki ya maji  kwa mkoa wa Dar es Salaam.
Sehemu ya Wenyeviti wa Serikali ya Mtaa wa  mkoa wa Dar es Salaam waliohudhuria uzinduzi wa Wiki ya Maji kwa Mkoa wa Dar es Salaam

TIDO MHANDO AELEZEA UBALOZI WA LULU TUZO ZA SZIFF.

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mkurugenzi wa Azam Media Tido Mhando amesema kuwa baada ya balozi wa Tuzo za Sinema Zetu internationa Film Festival Elizabeth Michael 'Lulu' kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela hawajatafuta mbadala wake.

Mhando amejibu swali aliloulizwa wakati wa utangazaji wa vipengele vya tuzo za SZIFF zinazotarajiwa kufanyika April Mosi mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam.

Akitolea ufafanuzi suala hilo,Mhando amesema kuwa mchakato wa kumpata balozi wa SZIFF kwa hiyo baada ya matatizo ya Lulu hawakuona umuhimu wa kupata mtu mwingine ,kwani muda haukuwa rafiki kwao.

"baada ya kutokea kwa matatizo kwa balozi wetu wa SZIFF Lulu, ambapo ili kumpata mwakilishi mwingine kunachukua muda mrefu hatukuona umuhimu wa kufanya hivyo na kuacha tuendelee na mchakato wa tuzo zetu ambazo tayari ulikua umeshaanza,"amesema Mhando.

Tuzo za SZIFF zilizinduliwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Harrison Mwakyembe ikiwa ni katika mchakato wa awali kabisa wa timu ya SZIFF kwenda mikoani kwa ajili ya kutafuta filamu mbalimbali huku balozi wa tuzo hizo Lulu akitambulishwa kwa mara ya kwanza kabisa.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akifurahia jambo na aliyekuwa Balozi wa Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu (SZIFF) Bi. Elizabeth Michael alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa tuzo hizo Oktoba mwaka jana jijini Dar es Salaam. Tuzo hizo zinaratibiwa na Azam Media zinatarajiwa kutolewa  April Mosi ambapo zinazoshirikisha filamu za Kiswahili.

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA UHAMIAJI


AZAM WAANZA MAANGAMIZI YA KUMUUA MTIBWA KOMBE LA FA

$
0
0
AZAM WAANZA MAANGAMIZI YA KUMUUA MTIBWA KOMBE LA FA

Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.

Kikosi cha Azam FC, kimeanzamaandalizi ya kuivaa Mtibwa Sugar huku Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Idd Cheche akiahidi mchezo mzuri na kuondoka na ushindi kwenye mtangane wa robo fainali ya kombe la Azam Sports HD dhidi ya Mtibwa Sugar.

Mchezo huo wa hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) unatarajia kufanyika Uwanja wa Azam Complex Machi 30 mwaka huu saa 1.00 usiku, ambapo tayari kikosi cha Azam FC kimeshaanza maandalizi tokeo jana jioni.

“Mashabiki waendelee kutusapoti kwa sababu mchezo wa mpira unahitaji sapoti, mchezo wa mpira una wachezaji, una viongozi, una mashabiki na mashabiki ndio wanaoongeza chachu ambayo inakuja kufanya mchezo uwe pendwa duniani.

“Kwa hiyo mashabiki waje kwa wingi watusapoti na sisi tutahakikisha tunawapa furaha ile ambayo wanaitarajia, watarajie mchezo mzuri na wenye ushindi,” alisema Cheche.

Cheche aliyewahi kuwa Kocha Mkuu wa timu ya vijana ya Azam FC (Azam U-20) kabla ya desemba mwaka juzi kupewa nafasi hiyo timu kubwa, alisema mchezo huo utakuwa ni tofauti sana na ule waliocheza kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu na kutoka sare ya bao 1-1.

“Mchezo wa ligi ni tofauti na FA, huu ni mchezo wa mtoano (knockout) lazima mmoja afungwe kama mnatoka sare mnafika kwenye hatua ya penalti lakini sisi tunataka kuhakikisha mchezo tunaumaliza ndani ya dakika 90 lakini kikubwa mno kwanza ni kuanza kuwajenga wachezaji wetu mazoezini kwa sababu mazoezi ndiyo yatatupelekea kufanya vizuri huu mchezo kwa hiyo tuko makini kuhakikisha watu wanafanya mazoezi vizuri ili mechi iweze kuwa nyepesi kwetu,” alisema.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TRC YANUNUA VICHWA 11 VYA KUVUTA MABEHEWA

$
0
0
Na  Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CSHIRIKA la Reli Nchini (TRC) imeingia mkataba wa ununuzi vichwa vya trein 11 na kampuni ya Progress Rail Locomotives (PRL) ya Marekani ili kuweza kuongeza idadi ya vichwa katika shirika hilo
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo,  Masanja Kadogosa amesema kuwa ununuzi wa vichwa hivyo itafanya shirika kuwa vichwa 47.
Amesema walikuwa na vichwa 29 ambavyo kwa mahitaji vilikuwa havitoshi lakini kwa sasa shirika linatakuwa vichwa vya kutosha katika kutoa huduma nzuri kwa wateja wa Trein.
Amesema kuwa vichwa vitafanya majaribio katika awamu tatu ambapo ya kwanza ni kuangaliwa na watalaam katika ubora wake na awamu nyingine kuviwasha na kupakia tani 700 toka Dar es Salaam pamoja na hatua ya tatu kupakia tani 1200 toka  Morogoro hadi Kigoma na Mwanza.
Kadogosa amesema serikali imeokoa zaidi dola 8,800,000 kwa  kila kichwa kutoka dola 3 200,000 kutokana na na mazungumzo ya kamati.
 Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa Meneja wa Kanda wa Nchi za Afrika zilizo Jangwa la Sahara wa Kampuni ya Progress Rail Caterpillar, Barend Hanekom wakibadilishana mikataba mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano 
Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa Meneja wa Kanda wa Nchi za Afrika zilizo Jangwa la Sahara wa Kampuni ya Progress Rail Caterpillar, Barend Hanekom wakionesha mikataba kwa waandishi habari mara baada ya kusaini jijini Dar es Salaam.

KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII YAVUTIWA NA MIRADI YA TASAF MKOANI SIMIYU.

$
0
0

NA ESTOM SANGA- BARIADI

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii wamefanya ziara mkoani Simiyu na kuvutiwa na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Miradi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF-mkoani humo.

Wajumbe hao walianza ziara yao kwa kusomewa taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambapo Katibu Tawala wa Mkoa huo , Jumanne Sagini aliwajulisha Wajumbe hao kuwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF,umekuwa chachu muhimu katika kuleta maendeleo ya wananchi katika mkoa huo mpya.

Amesema kupitia Mpango huo Walengwa wameboresha maisha kwa kuendelea kujenga mkazi bora, kuchimba visima vya maji, uanzishwaji wa mashamba ya pamba ili kujiongezea kipato huku pia sekta za Afya na Elimu zikiendelea kunufaika na utekelezwaji wa Miradi ya TASAF.

Wakiwa katika Wilaya ya Maswa ,mkoani humo, Wajumbe hao walioongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Stephen Rweikiza, walipata fursa ya kutembelea baadhi ya kaya za Walengwa ambako walishuhudia mafanikio ya ujenzi wa Nyumba ya mmoja wa Walengwa wa TASAF ,Monica Kwilasa katika kijiji cha Shanwa ambaye ametumia sehemu ya ruzuku aliyopata kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kuboresha Makazi yake.

Kama Wahenga wasemavyo “ Kuona ni kuamini” Wajumbe wa kamati hiyo walionyesha kushangazwa na mafanikio ya Mlengwa huyo ambaye aliwajulisha namna alivyotumia fedha alizozipata kutoka TASAF kuanzisha biashara ndogo ndogo iliyomwongezea kipato na kumwezesha kujenga nyumba kwa matofali ya saruji na kuezeka kwa mabati.

Akizungumza na Walengwa na Wananchi katika eneo la shule ya Sekondari ya Nyalikulungu ambako pia TASAF imejenga majengo, Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Rweikiza,amesema mafanikio yaliyoanza kupatikana katika utekelezaji wa Mpango huo ni kielelezo cha namna Serikali inavyopiga vita umaskini kwa kutumia mbinu mbalimbali ambazo amesema zinapaswa kuungwa mkono na wananchi. Zifuatazo ni picha za ziara hiyo ya kamati ya huduma za jamii ya bunge.
Wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya huduma ya Jamiii wakiwa mbele ya nyumba iliyojengwa na mmoja wa Walengwa kwa ruzuku ya TASAF Bi. Monica Mwalu, (aliyekamata karatasi) katika kijiji cha Shanwa wilayani Maswa . Aliyevaa kofia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika.
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za jamii,Mhe. Venance Mwamoto (aliyevaa koti) akitoka ndani ya nyumba iliyojengwa na mmoja wa walengwa kwa ruzuku ya TASAF.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Wakikagua moja ya Majengo yaliyojengwa na TASAF katika shule ya Sekondari ya Nyalikulungu katika wilaya ya Maswa mkoani Simiyu.
Waziri Mkuchika (aliyevaa kofia ) na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya huduma za Jamii wakikagua zoezi la ilipaji wa ruzuku kwa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Shanwa Wilayani Maswa ruzuku ambayo imeanza kuboresha maisha yao kwa kiwango kikubwa.
Baadhi ya Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Shanwa wilaya ya Maswa wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya huduma za jamii Mhe. Steven Rweikiza( hayupo pichani) wakati kamati hiyo ilipokagua miradi ya TASAF mkoani Simiyu. 

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

TCRA:EPUKENI KUWEKA TAARIFA NYINGI ZINAZOWAHUSU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII

$
0
0

Na.Vero Ignatus. Arusha

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Katika kuadhimisha siku ya walaji duniani inayo adhimishwa kila mwaka machi 15,imetoa mafunzo kwa waalimu wanafunzi zaidi ya 300 katika chuo cha ualimu Monduli mkoani Arusha.

Akizungumzia Madhumuni ya kutoa elimu hiyo Kaimu meneja wa Mamlaka ya mawasiliano kanda ya Kaskazini Francis Msungu amesema ni katika jitihadha zilezile za serikali za kuhakikisha kwamba inamlinda mlaji kwa kumpa elimu juu ya haki na wajibu wawatumiaji wa huduma za mawasiliano kwaajili ya kuleta maendeleo.

Katika kuadhimisha siku ya walaji wameitumia kutoa elimu juu ya haki, na wajibu wa watumiaji wa huduma za mawasiliano kama sehemu ya walaji,tahadhari za kuchukua katika mawasiliano hususani mitandao.

Msungu amesema kwamba walaji,ni kundi kubwa la kiuchumi ambalo huwa linaadhirika na kuathiri maamuzi ya kiuchumi yanayofanywa na mataifa na makampuni ya kibiashara."Sisi kundi hili la walaji ni kundi lile ambalo maoni yetu huwa suala la kusikilizwa kwa makini katika maamuzi ambayo yanafanywa ya kiuchumi" alisema.

Kwa upande wake Mhandisi Mwandamizi wa Masafa (TCRA) Jan Kaaya ametoa tahadhari kwa jamii kutokuweka taatifa nyingi zinazowahusu kwenye mitandao kwani siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi la uhalifu ambalo wanatumia mitandao kufuatilia taarifa za watu.Jan amesema ni muhimu kuhakikisha unapoweka taarifa ako katika mitandao hii ya kijamii,usiweke taarifa zako nyingi zinazomiwezesha mtu kuzitumia hizohizo katika kukudhuru wewe mwenyewe.

Mwanasayansi wa Masafa kutoka Mamlaka ya mawasilianoTanzania kanda ya kaskazini Julius Filex Mwanasayansi wa Masafa kutoka Mamlaka ya mawasilianoTanzania kanda ya kaskazini Julius Filex amezungumzia suala la uninuzi wa simu na kisema kuna sheria ya Mawasiliano ya kieletroniki na posta ya mwaka 2010/ambayo inamtaka mnunuzi wa simu kuhakikisha baadhi ya vitu kabla hajakabidhiwa simu.

Ahakikishe amepewa risiti,garantii ya mwaka mzima,auziwe simu ikiwa kwenye box lake,pia aangalie simu yake ni bandia ama la kwa kutumia *#06

Kaimu Meneja Mamlaka ya Mawasiliano kanda ya Kaskazini Francis Msungu
Mhandisi Mwandamizi wa Masafa (TCRA) Jan Kaay akizungumza na waandishi wa habari.Picha na Vero Ignatus Blog.
Kaimu mkuu wa chuo cha Ualimu Monduli Jesca Moiro akizungumza katika mafunzo hayo kama mwenyeji wa wanafunzi waalimu.Picha na Vero Ignatus Blog.Mwanasayansi wa Masafa kutoka Mamlaka ya mawasilianoTanzania kanda ya kaskazini (wa kwanza kulia) Julius Filex akizungumza na waalimu wanafunzi katika chuo cha ualimu Monduli ,(kushoto )Afisa kutoka (TCRA) Osward Octavian akionyesha vitabu ambavyo ni muongozo kwa watumiaji wa mawasiliano.Picha na Vero Ignatus Blog.
Kaimu Meneja Mamlaka ya Mawasiliano kanda ya Kaskazini Francis Msungu akisisitiza jambo katika mafunzo hayo.Picha na Vero Ignatus Blog.

Baadhi ya washiriki ya mafunzo hayo yaliyoandaiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania( TCRA) nakufanyika katika chuo cha Ualimu Monduli mkoani Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YATEMBELEA MGODI WA SEKENKE

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Murad SadickA (Kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Bw. Emmanuel Lwehaula wakati wa ziara ya kutembelea mgodi wa Sekenke one Mkoani Singida.
Sehemu ya Waheshimiwa Wabunge wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira wakiangalia zoezi la uchenjuaji wa dhahabu kwa kutumia zebaki mara baada ya kutembelea mgodi wa Sekenke one Mkoani Singida.
Sehemu ya wachimbaji wadogo wadogo wa Sekenke one wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola (hayupo pichani) alipopata fursa ya kuzungumza nao na kusisitiza suala la usafi wa mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akifafanua vifungu vya Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 kwa watendaji wa Wilaya ya Iramba na kuwataka kuisimamia ili kudhibiti vitendo vya uchafuzi wa Mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akisalimiana na Bw. Dotto Roman Selasini Afisa Uhamiaji wa Wilaya ya Iramba mara baada ya kuwasili katika Mgodi wa Senkenke One ulipo katika Kijiji cha Nkonkilangi, Kata ya Ntwike, Tarafa ya Shelui, Wilaya ya Iramba akiongozana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kutembelea mgodi huo kwa lengo la kujionea hali ya mazingira mgodini hapo.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE MAMBO YA NJE YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI MBALI MBALI WILAYANI RUANGWA MKOANI LINDI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia) wakati alipowasili kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali na ukarabati wa mabweni ya wafungwa leo tarehe 17 Machi, 2018 Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Cosato Chumi akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Ndg. Rajab Bakari (kushoto) akifafanua jambo pale kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama ilipokuwa inakagua miradi mbali mbali na ukarabati wa mabweni ya wafungwa leo tarehe 17 Machi, 2018 Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi. Katikati ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Mussa Zungu

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE

TAGCO WAIKUMBUKA SHULE YA FAMILIA YA MZEE LAIBON MTO WA MBU MKOANI MANYARA.

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusuano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Laiboni iliyopo Mto wa Mbu mkoani Manyara ,Rashid Mohamed msaada wa Madaftari 2500 kwa ajili ya wananfunzi wanaosoma katika shule hiyo.
Mwenyekiti wa TAGCO ,Pascal Shelutete na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali ,Dkt Hassan Abbas wakigawa Daftari kwa wanafunzi wanaosoma katika shule ya Msingi Loibon.
Mwenyekiti TAGCO ,Pascal Shelutete akizungumza mara baada ya kukabidhi Msaada huo.Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusuano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akipeana mkono na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Laibon ,Rashid Mohamed wakati akikabidhi msaaada wa Matenki mawili ya kuhifadhia maji shuleni hapo .kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo.
Mwenekiti wa TAGCO ,Pascal Shelutete akizungumza jambo na Wanafunzi wanaosoma katika shule ya Msingi Loibon.
Moja ya majengo ya Shule ya Msingi Loibon iliyojengwa na Mfugaji wa Jamii ya Kimaasai,Loibon Ole Mapii baada ya Mungu kumjalia watoto Zaidi ya 200 na wajukuu Zaidi ya 400 na kulazimika kujenga shule kwa ajili ya familia yake.
Wenyeji wa eneo ilipo shule hiyo Jamii ya Wafugaji wa Kimasaai waliandaa Nyama kwa ajili ya ugeni uliotembelea shule hiyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete na maafiwa Habar wenzake wakingojea kipande cha nyama .Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Arusha.

BILIONI TANO KUKAMILISHA MIRADI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

$
0
0
BILIONI tano kukamilisha miradi ya Manispaa ya Kigamboni ambayo ni Ujenzi wa Zahanati, kituo hc afya pamoja na ujenzi wa barabara ya kuelekea Daraja a Mwalimu Nyerere.

Akifafanua kabla ya kuanza kutembelea miradi hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa yaa Kigamboni, David Sukali amesema kuwa miradi hii kutimiza irani ya chama cha mapinduzi ambazo ziliahidiwa katika uchaguzi wa mwaka 2015. 

Pia manispaa ya kigamboni inamradi wa kugawa pikipiki kwa kata za manispaa ya Kigamboni ambapo kila kata itapata pikipiki tano ambazo zitakuwa kwaajili ya vijana wa kata hizo kwaajili ya kujipatia kipato tofauti na wanavyoingia mikataba wanayoingia wanapata shida kubwa katika kikidhi mahitaji ya mikataba yao. 

Miradi ya Manispaa ya Kigamboni ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kimbiji, ujenzi wa barabara ya kwenda Daraja la Nyerere, ujenzi wa Ofisi za Manispaa hyo pamoja na ujenzi wa Zahanati. 

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa yaa Kigamboni, David Sukali akizungumza na umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na wafanyakazi wa Manispaa ya Kingamboni wakati wakielekea kwenye ukaguzi wa utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa kituo cha Afya cha Kimbiji katika Manispaa ya Kigamboni pamoja na ofisi za Manispaa hiyo jijini Dar es Salaam.
Mchumi wa Manispaa ya Kigamboni, Maximillian Manyuka akisoma matumizi  ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha afya cha Kimbiji, ofisi za Manispaa ya Kigamboni pamoja, ujenzi wa Zahanati pamoja na ujenzi wa barabara ya kuelekea daraja la Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Musa Kilakala akizungumza na wafanyakazi wa Manispaa ya Kigamboni na baadae kueekea kukagua utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha afya cha Kimbiji, ujenzi wa barabara ya kuelekea Daraja la Nyerere, ujenzi wa Zahanati pamoja na ujenzi wa ofisi za Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, David Sukali (Mwenye suti ya  Bluu) akitoa maelekezo  kwa vijana wa  Mkoa wa Dar es  salaam na Viongozi wa vijana wa Manispaa ya Kigamboni katika Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kimbiji katika Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam
 Ujenzi ukiendelea katika Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha afya cha Kimbiji katika manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam,Musa Kilakala  akisaidiana na Wajenzi wa Kituo cha Afya cha Kimbiji kutandaza nondo katika ujenzi wa kiuo hicho.
 Viongozi wa UVCCM mkoa wa Dar es Salaam na Wilaya ya Temeke akitembelea kwenye mradi wa ujenzi wa Ofisi za Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
 Msanifu Majengo, Edwin Mwangasa(Mwenye tishet Nyekundu)Akitoa maelezo jinsi Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Manispaa ya Kigamboni utakavyo kamilika pamoja na changamoto zinazomkabiri mhandisi huyo.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Musa Kilakala  akisaidiana na mafundi kuweka nondo katika ujenzi wa ofisi za Manispaa ya Kigamboni.
Uonekano wa Majengo ya Ofisi za Manispaa ya Kigamboni zitakapokamilika hapo baadae.

WANAWAKE WATAKIWA KUCHANGAMANA HILI WAWEZE KUJIKWAMUA KIUCHUMI

$
0
0
 Aliyekuwa Mkurugenzi wa Tantrade Tanzania,Jacqueline Maleko akizungumza wakati wa usiku wa Wanawake na tunzo kwa Mwanamke aliyefanikiwa kwa mwaka 2018 iliyoandaliwa na Tasisi ya Shangwe ambapo wanawake kutoka sehemu mbalimbali walikutana na kuzungumza mambo ya ujasilimali na namna ya kuvuka kutoka hatua moja hadi nyingine.
 Mkurugenzi wa Tasisi ya I-learn East Afrika ,Noela Bomani(Kulia) Akikabidhi tunzo kwa Mwanamke aliyefanya vizuri na kuwa kivutio katika mafanikio yake katika kipindi cha mwaka 2017/2018 Joyce Ibengwe ambaye ni mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko  Kutoka kwa Tasisi ya waajiri nchini(ATE).
 Mshindi wa Tunzo ya Mwanamke aliyefanikiw akwa mwaka 2017/2018 Joyce Ibengwe ambaye ni mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko  Kutoka kwa Tasisi ya waajiri nchini(ATE).akizungumza namna alivyopitia mpaka kufikia hatua hiyo kutoka kuitwa mama na watu mpka mke wa mtu.
 Meneja Bima ya magari kutoka shirika la Bima ya Taifa (NIC) Emakulata Mwaitege, akizungumza umuhimu wa Wanawake kujiwekea bima katika biashara zao na maisha yao hili waweze kusimama tena pindi majanga yanapowakuta.

MAKAMU WA RAIS AFANIKISHA UCHANGIAJI UJENZI HOSPITALI YA MUHEZA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana aliwezesha kupatikana kwa shilingi bilioni moja na milioni mia saba kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

Katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais aliwapongeza uongozi wa Wilaya ya Muheza na mkoa wa Tanga pamoja na wananchi kwa kuamua kujenga hospitali yao ya wilaya ili kuboresha hali ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Makamu wa Rais alisema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuimarisha ubora wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kupunguza idadi ya vifo vya watoto kutoka kiwango cha vifo 66 kati ya vizazi hai 1,000 hadi kufikia kiwango cha angalau vifo 40 kati ya vizazi hai 1,000. Aidha, Serikali imedhamiria kupunguza vifo vya wanawake wajawazito kutoka 556 kwa mwaka 2017 katika vizazi hai 100,000 hadi kufikia 292 ifikapo mwaka 2020.

Sambamba na hilo Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo tuna mkakati wa kujenga, kukarabati na kupanua miundombinu ya Vituo vya afya 208 ili kuimarisha utolewaji wa huduma mbalimbali za afya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza  wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
  aziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela(kushoto) akimkabidhi Makamu wa Rais zawadi mara baada ya kumalizika kwa zoezi la uchangiaji jana kwenye hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam​

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DK.MWIGULU AWATAKA WANAFUNZI KUACHA KUTENGENEZA TAASWIRA MBAYA KWA SERIKALI

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii.

WAZIRI wa Mambo ya ndani, Dk.Mwigulu Nchemba amewataka wanafunzi kuachana na harakati za kutengeneza taswira mbaya za Serikali badala yake kuwa na mitazamo chanya.

Dk.Mwigulu ameyasema hayo jana katika kongamano la UNILIFE lililofanyika Chuo cha Biashara (CBE), ambalo liliandaliwa na Mbunge wa Viti maalum, Ester Mmasi.
Amesema wanafunzi hawatakiwi kufanya harakati ili wawe adui wa Serikali kwani yenyewe haina muda wa kushughulikia mashinikizo ya wanafunzi.

"Nilishawahi kufanya harakati nikiwa chuoni na nilipewa jina la Chifu..majina yangu yamekuja kujulikana nikiwa serikalini lakini nilikuwa napinga baadhi ya ajenda za Taifa ambazo niliona hazina manufaa," amesema Dk. Mwigulu.

Amesisitiza wanafunzi wengi kwa sasa wamekuwa wakiitafuta taswira mbaya ya Serikali bila kuangalia masuala mengine yanayopaswa kuungwa mkono.

"Kuwa kijana mwema chuoni sio kwa kuwa kimya bali kuwa na mitazamo chanya na ukiona mwanazuoni anabisha jambo jema ujue kuna kasoro," amesema.
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images