Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110149 articles
Browse latest View live

DC TEMEKE AHIMIZA WAENDESHA BODABODA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

$
0
0
Na Emmanuel ,Globu ya Jamii

MKUU wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Felix Lyaniva amewataka madereva wa pikipiki na Bajaj kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu na viatu wakati wanapoendesha vyombo vya moto.

Amesema lengo ni kuepuka ajali zinazosababishwa na madereva wazembe na kuwataka kufanya kazi kwa kuzingatia sheria zilizopo.

Lyaniva ameyasema hayo jana , wakati wa utambulishaji rasmi wa mfumo wa namba utakaowatambulisha madereva pikipiki na bajaji katika vituo vyao mbalimbali katika katika Kata ya Kibondemaji, Mbagala Jijini Dar es salaamu uliofadhiliwa na Diwani wa Kata hiyo Abdallah. 

Diwani huyo ameshirikiana na Kampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaji Association (TAMOBA) kwa ajili ya kuzisajili Pikipiki na Bajaji katika mfumo wa GPS utakaowawezesha kujua Pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani na kuweza kupatikana kwa haraka zaidi.Akizungumza zaidi Lyaniva amewapiga marufuku mgambo wa wilaya hiyo kutokamata pikipiki na Bajaj kwani wengi wao wamekuwa wakikamata pikipiki hizo bila ya kuzingatia sheria.

Amesena kazi ya kukamata bodaboda itafanywa na askari wenye weledi na wenye kujua sheria za usalama barabarani.Lyaniva pia amewapongeza TAMOBA kwa kuwafikia madereva bodaboda na bajaj kwani walikuwa na wasiwasi wa kuibiwa vyombo vyao na kuporwa na majambazi.

Ameongeza Diwani huyo ameleta maendeleo makubwa na mazuri katika Kata hiyo na pia TAMOBA imeleta usalama mzuri kabisa wa kisasa kwa kuwa madereva hao watafanya kazi zao wakiwa hawana wasiwasi wa kuibiwa Pikipiki zao na mali zao wawapo katika majukumu yao hayo pamoja na abiria wao.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe Felix Lyaniva akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kuzingatia sheria za usalama Barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu na viatu wakati wanapoendesha vyombo vya moto,jana jijini Dar es Salaam.(picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba akizungumza na akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kufanya kazi kwa kuzingatia sheria zilizopo, jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Utumishi wa TAMOBA Bw. Erasto Lahi akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kuzisajili Pikipiki na Bajaj katika mfumo wa GPS utakaowawezesha kujua Pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani na kuweza kupatikana kwa haraka zaidi, jana jijini Dar es Salaam.
Semu ya madereva wa pikipiki na Bajaj piki na Bajaj wakiwa kwenye mkutano utambulishaji rasmi wa mfumo wa namba utakaowatambulisha madereva pikipiki na bajaji katika vituo vyao mbalimbali vya Kata ya Kibondemaji, Mbagala Jijini Dar es salaamu.


BENKI YA CRDB YADHAMINI MKUTANO MKUU WA GS1

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, kwa kutambua udhamini wa benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Global Standard (GS1), taasisi hiyo inajishughulisha na uwekaji wa Barcodes katika bidhaa za kitanzania ili ziweze kukubalika katika soko la kimataifa na pia kuwa mdau wa kufanikisha sekta ya viwanda nchi mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania, Gideon Mazara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei,akizungumza katika Mkutano wa Mkuu wa Taasisi ya GS1 ambao ni watumiaji wa Simbomilia (Barcodes).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto), akiwa na baadhi ya watendaji wa benki hiyo katika mkutano wa Mwaka wa taasisi ya GS1.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benmki ya CRDB, Tully Mwambapa akiteta jambo na Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo, Frederick Nshakanabo, katika mkutano huo. 
Mkutano ukiendelea.

MICHUZI TV: WAJASIRIAMALI WANAWAKE WANUFAIKA NA MAFUNZO YA MKE WA MANDELA

USAJILI KILI MARATHON WAPATA MUAMKO MKUBWA MLIMANI CITY

$
0
0
Usajili wa mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon zinazotarajiwa kufanyika jumapili ijayo mjini Moshi umekuwa mkubwa huku wakazi wa Dar es Salaam na mikoa ya jirani wakimiminika kukamilisha zoezi hilo na kupokea namba zao za ushiriki.

Zoezi hilo limefanyika kwa ukamilifu Jumamosi na Jumapili katika Viwanja vya Mlimani City ambao walidhamini eneo hilo la kujisajili kama njia ya kuunga mkono juhudi za kukuza na kuendeleza michezo hususan riadha.

“Tumeridhishwa sana na muitikio wa watanzania na kwa kweli mwaka huu muamko ni mkubwa zaidi kwani mbio hizi zimezidi kuwa maarufu na kubwa mwaka hadi mwaka,” allisema Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli ambaye bia yake ndio mdhamini mkuu wa mbio hizi.

Alisema wana uhakika washiriki watazidi 10,000, idadi ambayo ilifikiwa mwaka jana. “Mwaka huu sisi kama Kilimanjaro Premium Lager tunawakumbusha wateja wetu kuwa twende Moshi kushiriki, tufurahie bia yetu namab moja baada ya kukimbia lakini pia tukumbuke kutoendesha vyombo vya moto huku tukiwa tumetumia kilevi,” alisema Meneja huyo.

Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael alisema wao kama wadhamini wa mbio za kilometa 21wameona muamko mkubwa na wanatarajia washiriki wengi zaidi katika mbio hizo za half marathon.

Mbio za mwaka huu, ambazo zinaandaliwa na Wild Frontiers na Dep Blue Media na kuratibiwa kitaifa na kampuni ya Executive Solutions, zitafanyika katika Chuo Kikuu Cha Ushirika Moshi (MoCU) Machi 4 kuanzia saa 12 asubuhi.
Wakazi wa Dar es Salaam wakijiandikisha kushiriki katika mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon zitakazofanyika Mjini Moshi Machi 4, mwaka huu. Zoezi hilo lilifanyika katika viwanja vya Mlimani City.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU ILIYOFANYIKA KATIKA KANISA LA KIGANGO CHA MLIMANI WILAYANI CHATO

$
0
0
  Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akishiriki Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita Februari 25, 2018.
 Rais Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akipiga makofi baada ya mahubiri kutoka kwa Padre Alex Bulandi wakati wa Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita Februari 25, 2018.

Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia waumini wa kanisa hilo mara baada ya kukaribishwa na Padre Alex Bulandi wakati wa Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25, 2018.
  Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akimshukuru Padre Alex Bulandi baada ya kusalimia wakati wa Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato Mhe.Medradi Kalemani akiwasalimia waumini wa kanisa wakati wa Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Padre Alex Bulandi baada ya Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Nishati amabaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato Mhe. Medrad Kalemani mara baada ya Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.


PICHA NA IKULU.

BITEKO AUTAKA MGODI WA KATAVI NA KAPUFI KUAJIRI WATANZANIA

$
0
0
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko ameupa Siku 14 Mgodi wa Dhahabu wa Katavi & Kapufi uliopo Mkoani Katavi kuhakikisha uwe umekamilisha taratibu za kuajiri Watanzania na kupunguza wafanyakazi wa kigeni kwenye nafasi ambazo Watanzania wanazimudu kama Sheria inavyoelekeza.

Alitoa agizo hili jana Tarehe 24 Februari, 2018 alipofanya ziara kwenya mgodi huo ili kujionea shughuli zinazofanyika katika mgodi huo.

Taarifa ya mgodi iliyowasilishwa kwake ilibainisha kuwa jumla ya wageni 48 wameajiriwa na huku 36 kati yao wakiwa hawana ujuzi na wanafanya shughuli ambazo Watanzania wanamudu, ikiwemo ya ulinzi.

Biteko alisema dhamira ya Serikali ni kuona Watanzania wananufaika na Sekta ya Madini kwa namna mbalimbali ikiwemo ya kujipatia ajira kwenye migodi na kwamba suala hilo la kuajiri wageni kwenye nafasi wanazomudu Watanzania halivumiliki.

Alimuagiza Mkuu wa Wilaya na Afisa Madini kuhakikisha wanalifuatilia jambo hilo na liwe limemalizika baada ya wiki mbili kuanzia Tarehe 24 Februari, 2018 na apatiwe mrejesho wake.
aibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Lilian Matinga (katikati) wakati wa kukagua shughuli ziazofanyika kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Katavi & Kapufi Ltd uliopo Mkoani Katavi.
 Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa pili kulia) akitembelea maeneo mbalimbali ya Mgodi wa Dhahabu wa Katavi & Kapufi Ltd uliopo Mkoani Katavi ili kujionea shughuli zinazoendelea mgodini hapo. Wa pili kulia ni Mbia na Makamu Mwenyekiti wa Mgodi wa Katavi & Kapufi Ltd, Sebastian Kapufi
 Moja ya eneo la mitambo kwenye mgodi wa Dhahabu wa  Katavi & Kapufi Ltd uliopo Mkoani Katavi

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

FIFA na CAF kuendelea kufikiria namna ya kuisaidia Zanzibar

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) Gianni Infantino na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) Ahmad Ahmad wakiri kuelewa hali ya Zanzibar pamoja na kuzingatia Sheria wamesema wanaona mazingira Maalum ya Zanzibar.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali serikali iliyozungumza na Marais hao wa mashirikisho ya mpira wa miguu kwa ngazi ya bara la Afrika na Dunia walipofika nchini hivi karibuni kwa ajili ya kufanya mkutano wao wa kuandaa ajenda za mkutano mkuu wa dunia.
‘’Marais hao walisema kuondolewa kwa Zanzibar katika uanachama wa CAF kulizingatia sheria zinazosimamia Shirikisho hilo lakini pamoja na hayo waliamua kuiachia  Zanzibar kuendelea kufaidika na  fursa zote wanazopatiwa wanachama wa CAF  isipokuwa kuwaruhusu kupiga kura, pia wanasema wataangalia zaidi ya hilo maeneo mengine namna ya kuisaidia Zanzibar,''Dkt.Harrison Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza katika Mkutano huo Mheshimiwa Mwakyembe alisisitiza kuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alieleza kwa ufasaha mgogoro huu wa soka kwa viongozi hao wenyedhamana na mashirikisho hayo nao kumuelewa ambapo walisisitiza kuhitaji serikali kuendelea kushauriana nao katika suala hilo.
Pamoja na hayo nae Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia aliwasihi wapenzi wa soka nchini kuendelea kuwa watulivu kwani suala hilo linashughulikiwa na viongozi wa ngazi za juu nao wanalifahamu

Makamu Mwenyekiti wa UWT afanya ziara katika Mkoa wa Magharibi Unguja

$
0
0
Na Is-Haka Omar, Zanzibar.
VIONGOZI na watendaji wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi(UWT) Tanzania wameshauriwa kuendeleza utamaduni wa kuwatembelea wananchi ili kuibua kero zinazowakabili na kuzifanyia kazi kwa mujibu wa matakwa ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya  mwaka 2015/2020.

Pia wametakiwa kuzitendea haki dhamana za uongozi walizonazo katika medali za kisiasa kwa kuhakikisha CCM inazidi kuwa Chama bora na imara chenye sera , taratibu na misingi ya maadili yanayokidhi matakwa ya wananchi wote bila ya ubaguzi wa kidini na kikabila.

Ushauri huo umetolewa kwa wakati tofauti na Waasisi na viongozi wa zamani wa UWT katika mwendelezo wa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa Umoja huo Taifa Ndugu Thuwayba Kisasi, katika Mkoa wa Magharibi Unguja.

Akizungumza mwasisi wa UWT aliyewahi kushika nyadhifa mbali mbali ndani Umoja huo na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM Taifa Bi.Mariam Hengwa (75) hapo nyumbani kwake kwa Mchina mwisho, amesema Chama Cha Mapinduzi kipo ngazi za chini kwa wananchi hivyo viongozi hao wapange utaratibu wa kuwatembelea wananchi mara kwa mara.

Bi. Mariam amesema viongozi wa UWT wanatakiwa kubuni mipango mbali mbali ya kimaendeleo itakayoongeza Ari na utendaji kwa Akina Mama wa Umoja huo, na kuwavutia wanawake wa upinzani kujiunga na CCM.
 MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Kisasi (kushoto) akisikiliza kwa makini nasaha za muasisi wa UWT Bi. Salama Majaliwa alipotembelewa nyumbani kwake Mwera na uongozi wa Umoja huo.
 MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Kisasi (kushoto) akisikiliza kwa makini nasaha za muasisi wa UWT, Bi. Mariam Hengwa(aliyekuwa katikati akizungumza) alipotembelewa na UWT yumbani kwake Kwa mchina-Mombasa Unguja.
 MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Kisasi (kulia) akisikiliza kwa makini nasaha za muasisi wa UWT, Bi. Rufea Juma Mbarouk(kushoto) alipotembelewa na UWT nyumbani kwake Mbweni Unguja.
MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Kisasi (kulia) akimkabidhi zawadi muasisi wa UWT, Bi. Rufea Juma Mbarouk(kushoto) alipotembelewa na UWT nyumbani kwake Mbweni Unguja.




WANANCHI 300 WA KITONGOJI CHA KINACHERE,HANANG WAANZA UJENZI WA KISIMA NA TENKI LA KUHIFADHIA MAJI YA MVUA

$
0
0
Na Jumbe Ismailly -HANANG    


WANANCHI  300 wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,tarafa ya Simbay,wilayani Hanang,Mkoani Manyara kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Hanang wameanza ujenzi wa kisima na tanki la kuhifadhia maji ya mvua ili waweze kuondokana na adha ya kufuata huduma hiyo  umbali wa zaidi ya mita 400 kutoka kwenye makazi yao.
Mwenyekiti mstaafu wa Kijiji hicho,Peter Qwendo alisema mradi huo utakapokamilika unatarajia kugharimu zaidi ya shilingi milioni 49 na kwamba kati ya kiasi hicho cha fedha nguvu za wananchi ni asilimia kumi ya gharama za mradi huo kwa kufanyakazi ya kukusanya mawe,mchanga,kokoto,kuchota maji na kumwagilia.
Aidha Qwendo ambaye pia ni mmoja wa watu waliokwenda nchini Kenya kupata mafunzo juu ya usimamizi wa shughuli hiyo,alisema wananchi hao wanaoishi katika kaya 107 wamekuwa wakiifuata huduma hiyo katika Kitongoji cha Ghata kilichopo umbali wa takribani kilomita 14 kwenda na kurudi.
ananchi wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,Tarafa ya Simbay wakifanya kazi za mikono kuhakikisha mradi huo unakamilika katika kipindi cha mwezi mmoja na kuanza kunufaika na huduma ya maji safi na salama.
bunge wa Jimbo la Hanang,Dk.Mary Nagu akiungana na wananchi wa Kitongoji cha Kinachere kufanyakazi za kukusanya na kusomba mchanga wa kujengea kisima pamoja na tenki la kuhifadhia maji ya mvua na kuahidi kuchangia lori tano za mchanga.
mafundi wa kujenga kisima wakiendelea na kazi ya kusuka nondo za kisima kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wake katika kipindi cha mwezi mmoja.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)
Ni Mbunge wa Jimbo la Hanang,Mkoani Manyara,Dk.Mary Nagu(wa kwanza kutoka kushoto) akipata maelezo mafupi ya mradi wa ujenzi wa kisima na tenki la kuhifadhia maji ya mvua kutoka kwa msimamizi wa mradi huo,Apolei Wilbrod.

Watoto 6 Wawashiwa Vifaa vya Usikivu (Cochlear Implant)

$
0
0
Watoto sita ambao wamewekewa vifaa vya usikivu Januari mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo wameanza kusikia kwa mara ya kwanza baada ya kuwashiwa vifaa hivyo.

Kuwashwa kwa vifaa hivyo kumeleta furaha kwa wazazi kwani wameshuhudia watoto wao wakisikia sauti kwa mara ya kwanza na hivyo kuwajengea matumaini ya watoto hao kuanza maisha mapya.

Zoezi la kuwawashia vifaa hivyo (Switch On) limefanyika leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalaam kutoka Medel Austria ambao ndio wasambazaji wa vifaa hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari , Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio Dkt. Edwin Liyombo amesema watoto hao walifanyiwa upasuaji wa upandikizaji kifaa cha usikivu Januari mwaka huu ambapo zaidi ya asilimia 80 ya upasuaji huo ulifanywa na watalaam wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .

‘’Watoto hawa wataanza maisha mapya ya kusikia sauti mbalimbali katika mazingira yanayowazunguka baada ya kuunganisha vifaa hivi na kuviwasha’’. Amesema Dkt. Liyombo

Akifafanua amesema mbali na watoto hao sita lakini pia watoto wengine watano ambao walifanyiwa upasuaji huo mwaka jana na wengine sita ambao walifanyiwa upasuaji huo nchini India nao wamekuja kufuatiliwa maendeleo yao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kupewa ushauri wa kitaalam. 

Akielezea ukubwa tatizo Dkt. Liyombo amesema takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinaonesha kuwa katika watoto 1,000 wanaozaliwa, inakadiriwa kuwa watoto watano wanazaliwa na tatizo kubwa la usikivu .

Pia amesema MNH ipo kwenye mchakato wa kuanzisha utaratibu wa kuwachunguza watoto wachanga ili kubaini mapema wenye matatizo yakutosikia.

Kwa upande wake Muwakilishi kutoka Medel Fayaz Jafar amesema upasuji huo umekua na mafanikio makubwa kwakua katika awamu hiyo kumekua na mabadiliko kwani asilimia kubwa ya upasuaji umefanywa na watalaam wa MNH na kwamba hatua hiyo ni ya kuridhisha.

Huduma ya Upandikizaji wa kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) ilizinduliwa Juni 7 , 2017 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu hivyo Tanzania imekuwa nchi ya pili kutoa huduma hiyo katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Kenya. Aidha Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo kupitia Hospitali ya Umma ambayo ni Muhimbili yenye hadhi ya ubingwa wa hali ya juu.
Mtaalam wa Huduma ya Usikivu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mathayo Majogoro Alfred (katikati) akiunganisha kifaa cha usikivu cha nje na cha ndani ili mtoto Matilda Katobesi aweze kusikia kwa mara ya kwanza. Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo akifuatilia na kushoto ni mama wa mtoto huyo, Angelina Cosmas.
Mtoto Matilda kwa mara ya kwanza leo tarehe 24, Januari, 2018 akianza kutamka baadhi ya maneno baada ya kufundishwa na mtaalamu wa sauti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuwasha kwa mara ya kwanza vifaa vya usikivu kwa watoto waliofanyiwa upasuaji na kupandikizwa vifaa hivyo katika hospitaili hiyo. Kuanzia kushoto ni Mkuu wa Idara ya Macho, Dkt. Baruani, Katibu wa Umoja wa Watoto na Wazazi Wanaonufaika na Vifaa vya Usikivu nchini, Bupe Mwakalambile na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Wateja, Bwana Aminiel Aligaesha.
Wazazi wakisubiri kuashwa kwa mara ya kwanza kwa vifaa vya usikivu katika hospitali hiyo.
Mtaalamu wa Sauti, Fayaz Jaffer akionyesha kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) kwa waandishi wa habari ambacho kinapandikizwa kwa mtoto mwenye tatizo la kusikia. Kulia ni Paul Khalil kutoka Kampuni ya Medel. Kuanzia kushoto ni Dkt. Edwin Liyombo, Dkt. Baruani, Bi. Bupe Mwakalambile na Bwana Aminiel Aligaesha wakiwa kwenye mkutano huo leo.

serikali yatakiwa kuzitambua kazi za wanawake katika mipango ya Taifa

$
0
0
NA VICENT MACHA - DAR ES SALAAM.

SERIKALI imetakiwa kuzitambua kazi za kutoa huduma zinazotekelezwa na wanawake na kuziingiza katika Mipango ya Taifa kwani zinaweza kusaidia kuongeza pato la Taifa.

Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia (TGNP) Bi. Lilian Liundi alipokuwa akitoa Mhuktasari wa Kongamano la Wanawake na Uongozi.

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika siku ya jumanne ya tarehe 27 Mlimani City jijini Dar es salaam, likihudhuriwa na wanawake mbalimbali walio katika nafasi za uongozi na waliostaafu.Mkurugenzi huyo alisema kuwa kuna haja ya serikali kuzitambua shughuli mbalimbali zinazotolewa na wanawake kama huduma kwa lengo la kujipatia kipato kwani uchunguzi umebaini kuwa wanawake hutumia muda wa masaa 10 mpaka 15 kwa siku kwa shughuli hizo hivyo wanakosa muda wa kufanya shughuli za kujipatia kipato.

Aidha Mkurugenzi huyo aliendelea kusema kuwa lengo kuu la Kongamano hilo ni wanawake kwa pamoja kuweza kujadili namna gani wataweza kuongeza nafasi za uongozi na maamuzi kwani bado hawajaweza kufikia lengo ambalo ni 50 kwa 50.

Lakini pia kuweza kusherekea, kupongezana na kuajadili changamoto mbalimbali anazokutana nazo mwanamke katika Nyanja ya elimu, afya na umiliki wa ardhi swala ambalo bado ni changamoto kubwa kwa wanawake wengi hivi sasa. Bi. Lilian aliendelea kusema kuwa kutakuwa na kuenzi na kukumbuka mchango uliotolewa na wanawake ambao walikuwa katika ngazi za uongozi maamuzi kuanzia ngazi ya jamii mpaka taifa.

Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo anatarajiwa kuwa Waziri msataafu Mama Marry Nagu, lakini pia kutakuwa na wadau zaidi ya 250 wanawake kwa wanaume viongozi wa sasa na wastaafu katika kuhakikisha kongamano hilo linaleta tija kwa jamii yetu.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo jijini Dar es salaam katika mkutano na waandishi kuhusu kongamano la Wanawake Uongozi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi wa katikati akiwa na jopo la wafanyakazi wa shirika hilo pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki katika kuandaa Kongamano la Wanawake na Uongozi. 
Waandishi wa habari wakiendelea na kazi yao.
                        

NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA ASHUHUDIA UZINDUZI HUDUMA ZA KISASA KITUO CHA AFYA NYAMWAGA TARIME

$
0
0
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akilakiwa nawananchi wakati alipokwenda kushuhudia uzinduzi wa huduma za kisasa katika kituo cha Afya cha Nyamwaga kilichopo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara wakati wa ziara yake mkoani humo mbali na mambo mengine kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi na kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akiangalia vifaa vilivyopo katika kituo cha afya cha Nyamwaga kilichopo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akitoa nasaha wakati alipokwenda kushuhudia uzinduzi wa huduma za kisasa katika kituo cha Afya cha Nyamwaga kilichopo Wilaya ya Tarime mkoa wa Mara.
Baadhi ya wananchi wakisikiliza nasaha zilizokuwa zikitolewa na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula wakati wa uzinduzi wa kituo cha afya cha Nyamwaga kilichopo Tarime mkoa wa Mara.
Baadhi ya wananchi wakisikiliza nasaha zilizokuwa zikitolewa na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula wakati wa uzinduzi wa kituo cha afya cha Nyamwaga kilichopo Tarime mkoa wa Mara.
Sehemu ya majengo ya kituo cha Afya cha Nyamwaga kilichopo Tarime mkoa wa MaraPICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI-WANMM

MAGAZETI YA JUMATATU LEO FEBRUARY 26,2018

TRA: SASA UNAWEZA KULIPA KODI YA MAJENGO KIELEKTRONIKI

$
0
0
Na: Veronica Kazimoto,Dar es Salaam,
Wito umetolewa kwa wananchi wote kuanza kulipa Kodi ya Majengo ya mwaka 2017/18 mapema kwa kuwa ulipaji wa kodi hiyo umerahisishwa  ambapo wanaweza kulipa kwa kutumia njia ya kielektroniki.
Akizungumza jijini Dar es Salaam hivi karibuni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kichere alisema hakuna muda utakao ongezwa ifikapo Juni 30, mwaka huu na badala yake faini itatozwa kwa kila mmiliki wa jengo atakayechelewa kulipa kodi hiyo.
“Kama mamlaka hatuoni sababu ya kuongeza muda wa kulipa Kodi ya Majengo ifikapo tarehe 30 Juni 2018 kwasababu tumewarahisishia wananchi ulipaji wa Kodi hii ambapo wanaweza kupata ankara ya malipo kwa majengo yaliyosajiliwa kwenye tovuti ya TRA au simu ya mkononi na kufanya malipo katika tawi lolote la Benki ya NMB au CRDB popote nchini au kwa njia ya mitandao ya simu ya Mpesa, Tigopesa au Halopesa”, alisema Kichere.
Kamishna Mkuu Kichere alisema kuwa, wananchi wafuatilie matangazo ya namna ya kulipa Kodi ya Majengo kwa njia ya kielektroniki katika mitandao ya kijamii na kwenye vyombo mbalimbali vya habari au wafike katika ofisi za TRA zilizo karibu na maeneo yao nchi nzima wapate utaratibu wa kulipa kodi hiyo kielektroniki.
Kichere aliongeza kuwa Kodi ya Majengo inalipwa kwa mujibu wa Sheria hivyo, ni muhimu wananchi walipe mapema kodi hiyo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza mwishoni ikiwa ni pamoja na msongamano wa watu.
“Natoa wito kwa wananchi kwamba, wasisubiri mpaka mwisho ndio waanze kupanga foleni kwenye ofisi za TRA, wanatakiwa kulipa kuanzia sasa hivi katika ofisi zetu na wanaweza kulipa kwa kutumia njia ya kielektroniki kama nilivyoeleza hapo awali, kinyume na hapo itatubidi tutoze faini kwa atakayechelewa kulipa kodi hii ya majengo,” alisisitiza Kichere.
Kodi ya Majengo hulipwa kuanzia mwezi Julai mosi ya mwaka wa fedha husika hadi Juni 30 ya mwaka unaofuatia kwa kufuata Sheria, kanuni na taratibu,  hivyo, muda huu ni muafaka kwa wananchi kuanza kulipia kodi ya majengo mpaka ifikapo tarehe 30 Juni, 2018.

KATIBU CHADEMA KATA YA MAILMOJA ATIMKIA CCM

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

WIMBI la baadhi ya viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) limezidi kuwakumba hapa nchini baada ya katibu wa CHADEMA kata ya MailMoja Mjini Kibaha Mohamed Hashim kuhamia CCM.

Pamoja na hayo wanachama wengine wa CHADEMA na ACT Wazalendo wapatao tisa nao walirejea CCM na kukabidhi kadi zao kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ramadhan Maneno.

Hayo yalijiri Kongowe wilayani Kibaha wakati Maneno alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa wilayani humo.Maneno alisema, kwa sasa wapinzani wameshatambua vyama hivyo kuwa hakuna jipya hivyo wameamua kumuunga mkono Rais Dk John Magufuli ambaye anatatua kero na changamoto zilizokuwa zinawasumbua wananchi.

“Hichi ndicho kielelezo cha kumkubali kiongozi wetu wao wenyewe wameona kinachofanyika na kasi na mabadiliko ya kimaendeleo iliyopo,” alisema Maneno.Alisema kuwa wanaCCM wanapaswa kukiimarisha chama kwa kuhakikisha wanalipa ada zao kwa wakati kwani ili mwanachama awe hai lazima alipe ada zake .

“Tunawanachama 38,000 kwenye Mji wa Kibaha lakini waliolipa ada ni wanachama 8,000 pekee ,,:;si sawa lazima wanachama watakeleze jukumu lao hilo ili kujenga chama,” alisisitiza Maneno.Alielezea kwa sasa viongozi waendelee kuhamasisha wananchi kujiunga CCM kwani mtaji wa chama ni kuongeza wanachama wapya.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akizungumza jambo na baadhi ya  viongozi ,wa CCM Mjini Kibaha na halmashauri ya mjini hapo wakati wa ziara yake mjini humo .
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akisalimiana na  baadhi ya  viongozi ,wa CCM Kata ya Kongowe na Mjini Kibaha kabla ya mkutano nao ,kuzungumzia masuala mbalimbali ya Chama wakati wa ziara yake mjini humo .(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akipokea kadi kutoka kwa katibu wa CHADEMA kata ya MailMoja Mohamed Hashim aliehamia CCM wakati mwenyekiti huyo alipokuwa akizungumza na baadhi ya wanachama na viongozi ,katika mkutano huo wanachama wengine Tisa kutoka upinzani walijiunga na Chama hicho.(picha na Mwamvua Mwinyi).


STENDI YA KISASA MAILMOJA - KIBAHA KUKAMILIKA MWEZI MACHI

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

STENDI ya mabasi ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani inatarajiwa kukamilika Machi baada ya mkandarasi wa kuongezewa muda kutokana na mradi huo kukumbwa na changamoto kadhaa.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Renatus Makoye msimamizi wa ujenzi wa stendi hiyo kutoka kampuni ya Mhandisi alipokuwa akielezea maendeleo ya ujenzi huo kwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoani Pwani Ramadhani Maneno ambaye alikwendakukagua mradi huo .Alisema awali mradi huo ulitarajiwa kukamilika Novemba mwaka jana.

Makoye alisema kuwa stendi hiyo ambayo imegharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.9 itakuwa ikihudumia wasafiri wa mabasi ya kwenda mikoani pamoja na mabasi madogo ya Daladala yanayofanya safari zake ndani ya mkoa imefikia hatua za mwisho.

"Awamu ya kwanza ilikuwa ni ujenzi wa fensi, choo na kituo cha polisi, awamu nyingine ni ujenzi wa sehemu ya mabasi kupaki na sehemu za magari binafsi," alisema Makoye.Alieleza ujenzi huo umezingatia viwango ambapo sehemu ya mabasi makubwa ujenzi wake ni kiwango cha zege huku ile ya mabasi madogo imejengwa kiwango cha lami.

Mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Ramadhan Maneno aliishukuru serikali kwa kuwa na taasisi na benki ya dunia ambao ndiyo waliofadhili wa ujenzi huo.Alielezea kwamba thamani ya fedha zimetumika kwa usahihi.

Maneno alisema ujenzi wa mradi wa stendi utainua uchumi wa mkoa wa Pwani na kuwataka watumiaji wa stendi hiyo kuitunza ili iweze kudumu na kutoa huduma nzuri.Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Jeniffer Omolo alisema baadhi ya majengo yatajengwa ikiwa ni pamoja utawala litajengwa na vibanda vya kukatia tiketi sehemu za abiria kusubiria mabasi, migahawa na majengo ya huduma mbalimbali za kijamii.

Omolo alisema baadhi ya majengo hayajajengwa kutokana na fedha kutokuwa ya kutosha kuweka vitu vyote hivyo .Alisema lengo lao ni kuwa na stendi ya kisasa ambayo ina huduma zote.
 Hali halisi ya ujenzi unavyoendelea katika stendi Mpya ya kisasa inayojengwa mjini Kibaha Mkoani Pwani.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Pwani ,Ramadhani Maneno (wa tatu kutoka kulia) akimsikiliza mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Jennifer Omolo (wa pili kutoka kulia)wakati alipokuwa akitoa taarifa ya miradi ya soko la Loliondo na ujenzi wa stendi Mpya ya kisasa katika ziara ya siku moja aliyoifanya mwenyekiti huyo mjini humo.

SOLOMONI MUKUBWA,CHRISTINA SHUSHO WATHIBITISHA KUNOGESHA TAMASHA LA PASAKA 2018 KANDA YA ZIWA

$
0
0

Waimbaji wa nyimbo za Kiroho (Injili), Afrika Mashariki na Kati Christina Shusho na Solomon Mukubwa wanatarajiwa kuwaburudisha kiroho vilivyo,watakapokuwa wakitumbuiza katika jukwaa la Tamasha la Pasaka 2018,ambalo safari hii linafanyika Kanda ya Ziwa,mkoa wa Mwanza na Simiyu. 

Akiwatangazia Mashabiki wa Tamasha la Pasaka jijini Dar Es Salaam hapo jana,Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw, Alex Msama alisema kuwa mbali ya uzinduzi wa Mwimbaji Nyota wa nyimbo za Injili,Rose Muhando pia waimbaji hao wamethibitisha kuzindua na kuzitangaza nyimbo zao mpya.

Msama amesema kuwa Waimbaji hao wana  nyimbo nzuri na zenye kumuimbia,kumsifu na kumtukuza Mungu,nyimbo ambazo anaamini zitavuta hisia za wengi watakapozikia.

"Solomoni Mukubwa na Shusho wote hawa hawajasikika muda mrefu katika majukwaa,hivyo wakazi wa Kanda ya Ziwa wakae mkao wa kuzifurahisha roho na wajitokeze kwa wingi katika maonesho hayo yatakayofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Aprili 1 na Uwanja wa Halmashauri mjini Bariadi mkoani Simiyu Aprili 2 mwaka huu",alisema Msama.
Mkurugenzi wa Msama Promotions Ltd,Alex Msama akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na maandalizi ya tamasha la pasaka linalotarajiwa kurindima Kanda ya Ziwa.

DC SOPHIA MJEMA AELEZEA UMUHIMU WANAWAKE,VIJANA KUPATIWA ELIMU YA UKOPAJI MIKOPO

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya Jamii

MKUU wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema , amemuagiza Mwwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Kata ya Liwiti Salima Fumbwe kuandaa vijana na wanawake wa kata hiyo kwa lengo la kupatiwa elimu ya uchukuaji wa mikopo ya Serikali na kisha kuirejesha.

Akizungumza juzi wakati amekutana na wananchi wa kata ya Liwiti wilayani humo, Mjema ameelezea umuhimu wa vijana na wanawake kupata elimu inayohusu mikopo inayotolewa na Serikali na kisha kuirejesha ili wengine nao wakope.

" Salima kama kiongozi wa wanawake wa kata hii uje ofisini kwangu nikupatie maofisa maendeleo waje kutoa elimu ili vijana wapate fursa hiyo ya kupata mikopo ya Serikali.Muda wowote njoo pale ofisini,"DC Mjema amemueleza mwenyekiti huyo wa UWT.

Amesema fedha hiyo ya Serikali mara baada kuipata wakumbuke marejesho na kueleza wachukue mikopo hiyo na kuitumia kwa malengo maalum.Mjema amesema taratibu zote watapewa kupitia ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Liwiti kupitia maofisa maendeleo wa kata.

Pia amemuagiza Mwenyekiti huyo wa UWT kuweka utaratibu wa vijana wake ili kupata fursa hiyo kata ya Liwiti.Ameongeza anajua wapo vijana wengi wanashindwa kujishughulisha kutokana na kukosa mitaji,hivyo mikopo hiyo itawasaidia katika shughuli za ujasiriamali .

Kwa upande wake Fumbwe amempongeza Mjema aliyekuwa mgeni rasmi kuwa atahakikisha anafuatilia na kutekeleza maagizo ya Serikali."Tutaweka mpango maalum vijana na wanawake wote wa Liwiti waweze kuwa na fursa ya kukopa." Nitashirikiana na wanachama wenzangu na Katibu wangu wa UWT kuweka mazingira bora kwa wanawake wote,"amesema.

Amefafanua yeye kama kiongozi wa UWT msimamo wake ni kwamba wanawake wote wajikwamue kiuchumi ili wasiwe tegemezi .

KIPINDI MAALUM UWEZESHWAJI WA WANAWAKE KIUCHUMI KISARAWE PWANI

DIAMOND SOMA NILOCHOANDIKA KUHUSU WEWE NA ZARI, NAMUOMBA MUNGU ASIKURUDISHE ULIKOANZIA

$
0
0
Na said Mwishehe,Globu ya Jamii

NI ngumu kuzungumzia mahusoano ya kimapenzi ya watu wengine lakini kuna wakati unaamua kufumba macho na kuziba masikio useme japo kidogo.

Nikiri mahusiano ya kimapenzi wakati mwingine hukumbwa nachangmoto nyingi.Mungu nisaidie nifikishe ujumbe kwa ufasaha.Hata hivyo siri ya mtungi aijue kata.Wengine huwa ni wa kupata taarifa...bwana umesikia jamaa ameacha mpenzi au mke.

Wakati mwingine unaweza kuambiwa ndugu yangu yule mshikaji wako kaachwa na mkewe au mpenzi wake.Ni mambo ya kawaida kusikia waliokuwa na mapenzi moto na pengine kuwa ya mfano wa kuigwa yamefika tamati.Hata hivyo swali la msingi huwa watu wanataka kujua kwanini waliokuwa wanapendana wameachana.Hivyo sababu ndio huibua mjadala kwenye jamii.

Tena usiombe walioachana wakiwa ni watu maarufu na wenye kukubalika na kupendwa zaidi.Nikiri kwenye maisha yangu ya uandishi yaliyoanza rasmi mwaka 2001,sikuwahi kabisa kuandika chambuzi au maoni inayozungumzia wapenzi kuachana.

Sikuwa na sababu ya kufanya hivyo kwani ni maisha binafsi ya watu wawili walioamua kupenda na kukaa pamoja na hatimaye wakaamua kuachana.Kwa mazingira ya aina hiyo unatoa maoni au kuandika uchambuzi il iweje?Hivyo huwa napotezea na ndio maana hata hili la juzi la Mkuu wa Wilaya fulani(jina kapuni) kutumia mitandao ya kijamii kumpongeza mumewe kuongeza mke wa pili kichwani kwangu halikunisumbua maana halina uhusiano na maendeleo ya Watanzania.

Ingawa aliyesema ni kiongozi wa umma na matendo yake wakati mwingine yana nafasi ya kuigwa na wengine hasa yale matendo mema.Nikiri kabla kuvunja mwiko huu wa kutoandika habari za uhusiano wa kimapenzi,niliamua kufanya mawasiliano ya kutosha na halmashauri ya ubungo wangu mwisho wa siku moyo,mwili na akili vikakubaliana si dhambi kuelezea walau kidogo.

Naomba niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna yoyote ile kwani kwenye maisha yetu haya lile ambalo wewe unaliona haliko sawa kwa mwingine anaona zuri na kulipa maksi za juu.Ndio maisha ya binadamu yalivyo.Hivyo niombe msamaha kwa yule ambaye kwa namna moja au nyingine nitamkwaza.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110149 articles
Browse latest View live




Latest Images