Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

MICHUZI TV: IGP SIRRO AZITAKA TAASISI MBALIMBALI NCHINI KUKEMEA VITENDO VYA UBAKAJI KWA KUTOA ELIMU


WANAWAKE GAIRO WAONGOZA KIMKOA KUJIFUNGUA WAKIWA NA UMRI CHINI YA MIAKA 20

0
0
Na John Nditi, Gairo
WANAWAKE wajawazito 2,600  sawa na asilimia 27 kati ya 9,577 waliojifungulia  zahanati na vituo vya afya  kwa mwaka 2017 katika halmashauri ya wilaya ya Gairo , mkoani Morogoro walibainika  kuwa  chini  umri wa  miaka 20.

Hali hiyo ilisababisha  kujitokeza  kwa vifo  vitokanavyo na uzazi pingamizi unaochagiwa na uchungu mkali,  kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua  na kifafa cha mimba.

Mratibu wa Afya  ya Mama na Mtoto wa wilaya ya Gairo, Edifonzia Mhafigwa alisema hayo   wakati akiwasilisha taarifa katika   mkutano wa kujadili utoaji wa elimu kuhusu kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi kwenye   siku ya  Utepe Mweupe ambayo  kimkoa ilifanyika  katika  kata ya Ukwamani , wilayani humo.

Mbali na changamoto hiyo, wanawake wajawazito waliojifungulia kwa wakunga wa jadi  kwa mwaka 2017 walifikia 1,270 , waliojifungulia njiani  ni 108 , waliojifungulia nyumbani ni 180 na kwenye  Zahanati walikuwa ni 3,482.
 Katibu Tawala wa wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro, Adam Bibangamba ( aliyesimama) akitoa hotuba yake ya  ufunguzi wa mjadala wa elimu  juu ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi kwa  wanawake wajawazito  na kupinga mimba za utotoni  wakati wa siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kata ya Ukwamani , wilayani humo. ( Picha na John Nditi).
Mkazi wa  Kata ya Ukwamani , wilaya ya Gairo akichangia mada
  Baadhi ya wananchi  wa kata ya Ukwamani , wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro wakisiiliza na kusoma vipeperushi vya  elimu  ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo  na uzazi vya akina mama wajawazito na kupinga mimba za utotoni, wakati wa mjadala wa uelimisghaji jamiii  siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kwenye kata hiyo.
Wazee wa  kata ya Ukwamani, wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro ( mstari wa mbele ) wakiwasikiliza wataalamu wa afya ( hawapo pichani) wakati wa utoaji wa elimu  ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi kwa  akina mama wajawazito na kupinga vita  kujifungulia kwa wakunga wa jadi na  mimba za utotoni, wakati wa siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kwenye kata hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO WA MAJADILIANO MUNYONYO KAMPALA

0
0
Bw. Plasduce Mbossa katikati Mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kushoto yake ni Bi. Lydia Mallya ambaye pia ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania pamoja na Bi. Judith Nzamba aliyevaa gauni la Bluu mfanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania wamesimama katika banda lao la maonesho ya Miundombinu ya Usafiri yanayofanyika katika viwanja vya Speke Resort Munyonyo-Uganda.
Wapili kutoka kulia Mhe. Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na wataalam wengine wa sekta ya Afya walioshiriki katika Mkutano wa Majadiliano wa sekta ya Afya katika ukumbi wa mikutano wa Speke Resort Munyonyo-Uganda.
Washirika wa Maendeleo kutoka nchi mbalimbali duiani wa sekta ya Miundombinu ya Usafiri walioshiriki katika mkutano wa majadiliano unaofanyika katika viwanja vya Speke Resort Munyonyo-Uganda.
Baadhi ya Washiriki wa Tanzania katika Mkutano wa Majadiliano wa sekta ya Afya walioshiriki katika mkutano huo unaoendelea kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Speke Resort Munyonyo-Uganda.

IN LOVING MEMORY

WAFUASI 28 CHADEMA WAFIKISHWA KORTINI KWA KUTUHUMIWA KUFANYA MKUSANYIKO ISIVYOHALALI

0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

WATU 28, wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia Chadema (ChADEMA), wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kukusanyika isivyo halali.

Mbele ya Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa, watuhumiwa hao wote wanadaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu huko Kinondoni katika eneo la Mkwajuni lililopo katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walifanya mkusanyiko usio wa halali kinyume cha sheria.

Mwendesha Mashtaka wakili wa Serikali, Faraji Nguka leo akisoma mashtaka amedai, lengo la mkusanyiko huo wakiwa na nia ya kufanya uvunjifu wa amani na kusababisha taharuki kwa wananchi.

Hata hivyo, washtakiwa wote wamekana kuhusika kwenye tukio hilo na baadhi yao wameweza kutimiza mashati ya dhamana ambayo yamewataka kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja atayesaini bondi ya shilingi milioni moja na nusu.

 Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Machine 8, mwaka huu.

Baadhi ya majina ya watuhumiwa hao ni, Tabitha Mkude, Haji Lukwambe, Emmanuel Kimoi, Mohammed Juma, Hussein Mnombo, Abdallah Hamisi, Hussein Kidela, Paulo Kimaro, Brayan Morris, Hussein Nguli na Edina Kimaro.

Wengine ni Fatuma Ramadhani, Asha Kileta, Salha Ngondo, Ally Rajabu, Raphael Mwaipopo, na Athumani Mkawa.
WATU 28, wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia Chadema (CHADEMA), wakiwa wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kukusanyika isivyo halali.

WAZIRI JAFO APANIA KUBORESHA SEKTA YA AFYA KWA WAKINAMAMA WAJAWAZITO KWA KUJENGA VITO VYA AFYA

0
0
Na Victor   Masangu, Chole  Kisarawe   
WAKINAMAMA  wajawazito katika kijiji  cha Kihare kata ya Maluwi Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani  waliokuwa wanakabiliwa na changamoto katika sekta ya afya kutokana na  ukosefu wa kutokuwa na  wodi maalumu  ya kujifungulia kwa  kwa kipindi cha  muda mrefu na kuwalazimu kutembea umbari wa kilometa 15 kufuata huduma hatimaye kilio chao kimepata mkombozi baada kukamilika kwa jengo la wazazi.

Aisha Ramadhani na Fatma Iddy ni baadhi ya wakinamama ambao walisema kwa miaka mingi wamekuwa wanateseka pindi inapofika wakati wa kujifungua kutokana na zahanati ya Kihare ambayo  walikuwa wanaitumia katika kupata huduma ya matibabu ilikuwa haina jengo la wodi ya wazazi hivyo ilikuwa inawalazimu kufunga safari ya umbari wa kilometa 15 kwa kutumia usafiri wa baiskeli,pikipiki au wakati mwingine kutembea kwa  miguu.

Walisema  kwamba hapo awali walikuwa wanapata shida kubwa wakati wa kujifungua kutokana  na kutokuwepo kwa wodi ya kujifungulia hivyo walikuwa wanachanganywa na wagonjwa wengine wa kawaida kitu hali ambayo ji hatari kwa afya zao na mtoto, hivyo wameipongeza serikali ya awamu ya tano na juhudi za Mbunge wa jimbo lao  kwa kuamua kujenga jengo hilo ambalo litakuwa ni msaada mkubwa katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wake Mganga mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jonathan Budenu  amekiri kuwepo kwa changamoto ya wakinamama wa kijiji cha Kihare  kutembea umbari mrefu wa kilometa 15 kwa ajili ya kwenda kufuata huduma ya kujifungua katika kituo cha afya chole,ambapo kwa sasa wameanza harakati za ujenzi wa  wodi kwa kutumia  za halmashauri pamoja na michango ya wananchi.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi  Selemani Jafo amebaini kuwepo kwa hali hiyo wakati alipokwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi ya wazazi katika zahanati ya Kihare ambapo  amesema kwamba katika kukabiliana na changamoto hiyo imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vitatu vya afya.

Jafo alibainisha kuwa serikali ya awamu ya tano lengo lake kubwa ni kuhakikisha inaborsha sekta ya afya hivyo ujenzi wa vituo hivyo vya afya vitaweza   kupunguza adha ya wagonjwa hususan kwa  wakinamama wajawazito kwa wananchi wa Wilaya ya Kisarawe.

“Kwa kweli katika hili la wakinamama wajawazito wamekuwa wakipata shida kubwa sana, kwani wakti mwingine wanasumbuka ya kufuata huduma ya afya kwa kutembea umbali mrefu, hivyo tumetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 500, kwa kila ujenzi wa  kituo cha afya kimoja nah ii kwa kweli itapunguza sana adha ya wakinamama waliyokuwa wakiipata pamoja na wananchi wote kwa ujumla,”alisema Jafo.

Waziri Jafo akiwa  katika ziara yake ya kikazi  Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani ambapo ameweza kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu, miundombinu, afya maji, pamoja na kuweza kukutana na viongozi, watendaji , pamoja na kungumza na wananchi wa vijiji,vitongoiji, kata kwa lengo la kuweza kusikiliza changamoto wanazokabiliana nazo kwa lengo la kuweza kuzitatua.
 Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi, Seleman Jafo akizungumza na baadi ya viongozi na watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo katika sekta ya afya, maji, barabara, pamoja na elimu pamoja na kuzungumza na wananchi.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais  Tamisemi,  Seleman Jafo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya wauguzi na madaktari wa  halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi mbali mbai ya maendeleo pamoja na kuzungumz na wananchi.(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)

WAFUASI 28 CHADEMA WAFIKISHWA KORTINI KWA KUTUHUMIWA KUFANYA MKUSANYIKO ISIVYOHALALI

0
0

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

WATU 28, wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kukusanyika isivyo halali.

Mbele ya Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa, watuhumiwa hao wote wanadaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu huko Kinondoni katika eneo la Mkwajuni lililopo katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walifanya mkusanyiko usio wa halali .


Mwendesha Mashtaka wakili wa Serikali, Faraji Nguka leo akisoma mashtaka amedai, lengo la mkusanyiko huo wakiwa na nia ya kufanya uvunjifu wa amani na kusababisha taharuki kwa wananchi.

Hata hivyo, washtakiwa wote wamekana kuhusika kwenye tukio hilo na baadhi yao wameweza kutimiza masharti ya dhamana ambayo yamewataka kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakaesaini bondi ya shilingi milioni moja na nusu.

 Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 8, mwaka huu.

Baadhi ya majina ya watuhumiwa hao ni, Tabitha Mkude, Haji Lukwambe, Emmanuel Kimoi, Mohammed Juma, Hussein Mnombo, Abdallah Hamisi, Hussein Kidela, Paulo Kimaro, Brayan Morris, Hussein Nguli na Edina Kimaro.

Wengine ni Fatuma Ramadhani, Asha Kileta, Salha Ngondo, Ally Rajabu, Raphael Mwaipopo, na Athumani Mkawa.


Katika mkusanyiko huo, Mwafunzi wa mwaka wa kwanza wa chuo cha NIT Aquilina Akwelini aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala, polisi bado wanaendelea na uchunguzi kujua chanzo cha kifo chake.
WATU 28, wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia Chadema (CHADEMA), wakiwa wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kukusanyika isivyo halali. Picha na Mody

KAMISHANA MPYA WA POLISI ZANZIBAR AJITAMBULISHA KWA RAIS SHEIN

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti  wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Kamishna Mpya wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Bw. Mohamed Haji Hassan alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha baada ya uteuzi wake na dhamana alizopewa.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti  wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Kamishna Mpya wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Bw. Mohamed Haji Hassan alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha baada ya uteuzi wake na dhamana alizopewa. (Picha na Ikulu)

NAIBU WAZIRI MADINI ATUA MKOANI SONGWE KWA ZIARA YA KIKAZI

0
0
Na Mathias Canal, Songwe
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko leo 22 Februari 2018 ameanza ziara ya kikazi katika Mkoa wa Songwe ambapo pamoja na mambo mengine atatembelea na kukagua eneo la mgodi tarajiwa wa Bafex linalotarajiwa kuanza uchimbaji wa Madini ya dhahabu.

Maeneo mengine atakayotembelea ni pamoja na mgodi wa uchimbaji dhahabu wa Shanta Gold Mine uliopo katika kata ya Saza, Wilayani Songwe ambapo atazungumza pia na wafanyakazi wa mgodi huo.

Sambamba na hayo pia Naibu Waziri wa Madini atazungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano ulioandaliwa Mara baada ya kutembelea maeneo ya uchimbaji.

Mara baada ya kuwasili katika Mkoa wa Songwe Mhe Biteko amesifu juhudi za mbunge wa Jimbo la Songwe Mhe Philiph Mulugo kutokana na uwajibikaji mkubwa katika kuwasemea wananchi wa jimbo hilo hususani katika kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia sekta ya Madini.
Naibu Waziri wa Madini, Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza mara baada ya kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Songwe kwa ajili ya ziara ya siku mbili ya kikazi katika mkoa wa Songwe, Leo 22 Februari 2018.
Naibu Waziri wa Madini, Mhe Doto Mashaka Biteko akisisitiza jambo mbele ya Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Songwe, na Kamati ya  siasa ya CCM Wilaya hiyo mara baada ya kuwasili Mkoani Songwe kwa ziara ya kikazi, Leo 22 Februari 2018.
Mkuu wa wilaya ya Songwe, Mhe Samwel Jeremiah akieleza changamoto za wachimbaji wadogo katika Wilaya hiyo mbele ya Naibu Waziri wa Madini, Mhe Doto Mashaka Biteko wakati akisoma taarifa ya Mkoa wa Songwe kwa niaba ya mkuu wa Mkoa huo, Mhe Chiku Galawa, Leo 22 Februari 2018.

MEYA DAR AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MAMEYA WA MAJIJI YA AFRICA KUBADILISHANA UZOEFU

0
0

Na Said Nwishehe,Globu ya Jamii

MEYA wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kuna mambo mengi ya kujifunza na kubadilisha uzoefu kutoka kwa Majiji mbalimbali Barani Afrika kuliko majiji ya nchi za Ulaya.

Mwita amesema hayo leo, wakati akielezea ujio wa Meya wa Jiji la Blantyre nchini Malawi Wild Ndipo ambaye amekuja kwenye Jiji la Dar es Salaam akiambatana na viongozi wengine kwa lengo la kuja kubadilisha uzoefu kwenye nyanja mbalimbali.

Akizungumzia ujio wa Meya wa Jiji la Blantyre nchini Malawi,Mwita amesema kwenye mkutano wa mameya wa majiji mbalimbali ya Afrika uliofanyika nchini Afrika Kusini,walikubaliana kujenga utaratibu wa kutembeleana wao kwa wao.

Amesema kwa majiji ya Afrika kuna mambo ya kujifunza hasa kwa kuzingatia kuna mambo mengi yanafafana na hasa kwenye miundombinu ya barabara,elimu,afya na kilimo.Amefafanua kwa Majiji ya Ulaya mengi yamejengwa miaka 200 iliyopita na mingine zaidi hapo na kwa mazingira hayo hakuna cha kujifunza lakini kwa majiji ya Afrika kuna mengi ya kujifunza kwani hata umri wa majiji hayo unafafana.

Hivyo ujio wa Meya wa Malawi ni wa umuhimu zaidi kwani pamoja na mambo mengine watabadilisha uzoefu na kuweka mikakati ya kuboresha Majiji yao.Ameongeza Jiji la Dar es Salaam na Jiji la Blantayre wameingia uhusiano wa urafiki kwenye lengo la kubadilisha mbibu na uzoefu kwenye mambo mbalimbali.

Mwita amesema ugeni huo ukiwa jijini Dar es Salaam watatembelea miradi ya maendeleo na kwa leo wamefanya mradi wa kutembelea mradi wa mabasi yaendayo haraka kwa lengo la kujifunza namna unavyoendeshwa.Kwa upande wa Ndipo ambaye ni Meya wa Jiji la Malawi amesema Jiji la Dar es Salaam kuna mengi ya kujifunza,hivyo wamepanga kutembelea maeneo mbalimbali ya mradi.

Pia amesema kubwa zaidi kesho watapata nafasi ya kushiriki kwenye kikao cha Baraza la Jiji,hivyo kuna kitu watajifunza.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akizungumza leo, ujio wa Meya wa Jiji la Blantaya nchini Malawi (kulia) ambaye amekuja kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali jijini

NAIBU WAZIRI DK. NDUGULILE AFANYA ZIARA WILAYA YA SHINYANGA KUKAGUA HUDUMA ZA AFYA

0
0


Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amepiga marufuku dawa za serikali kuonekana zikiuzwa kwenye maduka ya watu binafsi kwani serikali haitaki kuingia kwenye matatizo ya uhaba wa dawa kwenye sehemu zake za kutolewa huduma ya afya. 

Dk. Ndugulile amepiga marufuku dawa za serikali kuonekana zikiuzwa kwenye maduka ya watu binafsi wakati wa ziara yake ya kikazi katika wilaya ya Shinyanga, Februari 21,2018 akikagua shughuli za huduma za afya zinavyotolewa kwa wananchi pamoja na kutoa hamasa kwa jamii kujiunga na Bima ya afya ya jamii CHF iliyoboreshwa.

Dk. Ndugulile alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha (2017-18) serikali kwenye bajeti ya wizara hiyo ya afya imetenga jumla ya shilingi bilioni 270, tofauti na mwaka wa fedha (2015-16) ambapo zilikuwa milioni 30 hivyo hawatarajii kusikia sehemu za kutolewa huduma zake za kiafya kuwa zina upungufu wa dawa.

Akiwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga na Kituo cha Afya cha Kambarage manispaa ya Shinyanga na kukagua bohari za dawa, Dk. Ndugulile alitoa tahadhari kwa wauguzi kuwa ni marufuku dawa hizo za serikali kukutwa zinauzwa kwenye maduka ya watu binafsi na ikibainika watachukuliwa hatua kali.

“Serikali ya awamu hii ya tano imedhamiria kuboresha huduma za afya hapa nchini, na ndio maana hata bajeti yake imetolewa ni ya fedha nyingi hivyo sisi kama wizara husika hatutarajii kuwepo kwa upungufu wa dawa kwenye sehemu za huduma za afya”,alieleza.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika bohari ya dawa kwenye kituo cha afya kata ya Kambarage mjini Shinyanga. Picha zote na Marco Maduhu na Steve Kanyefu
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa ameshika kopo la dawa katika bohari ya dawa kwenye kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga na kusisitiza kuwa dawa zenye nembo ya dawa za serikali MSD hazitakiwi kutoka nje ya hospitali za serikali.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsalimia mgonjwa katika kituo cha Afya Kambarage mjini Shinyanga huku akiangalia dawa alizopewa mgonjwa na kupiga marufuku wagonjwa kuambiwa dawa hakuna na kwenda kununua kwenye maduka ya dawa ya watu binafsi.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulileakikagua chumba cha upasuaji katika kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga, na kuagiza jengo hilo lifanyiwe marekebisho ili kuendana na hadhi ya chumba cha upasuaji, sababu haliridhishi kuendana na huduma ambayo itakuwa ikitolewa.

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MAHAFALI YA 34 YA CHUO KIKUU HURIA

0
0

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki matembezi ya mahafali ya 34 ya Chuko Kikuu Huria pamoja na Mkuu wa chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda (kulia) kuelekea kwenye uwanja wa Halmashauri ya  Bariadi kwenye sherehe za mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Huria Tanzania Profesa Rwekaza Mukandala wakati wa mahafali ya 34 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye uwanja wa Halmashauri ya Bariadi mkoani Simiyu. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

 Sehemu ya Wanafunzi waliohitimu katika Chuo Kikuu Huria wakiwa kwenye sherehe za mahafali ya 34 ya chuo hicho. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

BIL.1.7 KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU SIMIYU

0
0
Uwekezaji katika sekta ya elimu Nchini kupitia mpango wa kuinua ubora wa elimu (EQUIP-Tanzania) ambao umelenga kuboresha mchakato wa kufundisha na matokeo ya kujifunza kwa watoto nchini umeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa Mkoani Simiyu.

Uwekezaji huo ambao unafadhiliwa na serikali ya Uingereza kupitia Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) umeleta ufanisi wa elimu na kufanya viwango cha ufaulu kuwa juu kutoka asilimia 36 mwaka 2013 mpaka asilimia 68 2017.

Na katika kutimiza hayo Jumla ya kiasi cha shilingi Bil 1.7 kutoka DFID kupitia mradi wa kuinua ubora wa Elimu Nchini (Equip) zimetolewa kwa Serikali ya Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu Mkoani humo .

Akizungumzia nia ya serikali ya Uingereza wakati wa mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan , Mkuu wa DFID-Tanzania Elizabeth Arthy alisema wametoa kiasi hicho cha fedha kwa serikali ya Mkoa wa Simiyu ili kuhakikisha wanatatua changamoto ya miundombinu iliyopo.

Arthy alisema kuwa kiasi hicho cha fedha ambacho kinatarajiwa kutumika katika kuboresha miundombinu hiyo na kujenga vyumba vya madarasa, ofisi za walimu pamoja matundu ya vyoo kitasaidia kwa kiasi kikubwa kuleta ufanisi wa utoaji elimu kwa walimu na wanafunzi.

Mkuu huyo alieleza kuwa tangu shirika lake lianze kusaidia katika Elimu ,Mkoa wa Simiyu umeweza kupata mafanikio makubwa na ya haraka ambayo yamesaidia kuuweka Mkoa katika nafasi nzuri Kitaifa katika matokeo ya mitihani ya kuhitimu elimu ya Msingi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka aliuelezea mpango wa kuinua ubora wa elimu Tanzania kwa Mkoa wake kuwa ni mpango ambao umeweza kuleta mabadiliko makubwa ya kukuza viwango vya ufaulu wa wanafunzi.

Mtaka anaeleza wanalishukuru shirika la maendeleo ya uingereza (DFID) kupitia mpango wa kuinua ubora wa elimu kwa kuona kuwa Tanzania na Mkoa wake unahitaji msaada huo wa kuinua kiwango cha ufaulu pamoja na uboreshaji wa mazingira ya elimu.

Amesema kupitia msaada huo wa fedha kiasi cha shilingi Bil 1.7 zilizotolewa kwao na shirika la DFID kwa mwaka huu za kuboresha mazingira ya elimu ,zitawasaidia kujenga vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo ambavyo vyote hivyo ni changamoto kubwa Mkoani kwake.

Anaongeza kuwa kupitia fedha hizo anaanimi tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo utapungua kwa kiasi kikubwa na kwamba atasimamia vema fedha hizo ili ziweze kutumika ipasavyo.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mheshimiwa Anthony Mtaka akimuelezea Makamu wa Raisi utekelezaji wa mpango wa EQUIP-Tanzania mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza nchini Tanzania Bibi Elizabeth Arthy akizungumza mbele ya makamu wa Rais juu ya mchango wa serikali ya Uingereza katika kuboresha elimu.
Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza nchini Tanzania Bibi Elizabeth Arthy akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa shule ya msingi Gamondo A iliyoo wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Bibi Elizabeth Arthy alipotembelea shule ya msingi Gamondo A mkoani Simyu, kuona utekelezaji wa mpango wa EQUIP-Tanzania.

KASESELA, ASIA JUMA WATINGA KARIAKOO KUPATA UZOEFU NAMNA BORA YA KUSIMAMIA MACHINGA

0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akisalimia wananchi baada ya kutambulishwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (watatu kushoto) alipowapeleka Kasesera na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah katika eneo la biashara za Machinga katika Mtaa wa Kongo, Kariakoo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kupata uzoefu wa namna Wilaya ya Ilala ilivyofanikiwa katika kuboresha mazingira na kuwaweka pamoja machinga hao katika shughuli zao. Wapili kushoto ni Katibu Tawala wa Ilala Edward Mpogolo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akimtambulisha Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah kwa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Baadhi ya kinamama wakimweleza kero Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema alipokuwa na ugeni huo
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akiwa katika Mtaa wa Kongo kujionea shughuli mbalimbali zinavyoendesha na Machinga wa Kariakoo

VITUO MAALUM VYA UCHENJUAJI KUJENGWA KATIKA MAENEO YA WACHIMBAJI WADOGO NCHINI

0
0
Na Zuena Msuya, Geita.

Serikali  inadhamiria kujenga vituo maalum vya uchenjuaji na kuvizungushia ukuta katika kila eneo lenye wachimbaji wadogo ili kudhibiti wizi na uuzwaji holela wa madini ya dhahabu katika maeneo hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila alisema hayo Februari 20, 2017 mkoani Geita ,wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Mfano na Mafunzo kwa wachimbaji wadogo kinachojengwa katika eneo la Rwamgasa mkoani humo.

Prof. Msanjila alisema kuwa vituo hivyo vitakapojengwa vitarahisisha ukusanyaji wa mapato na kuwasaidia wachimbaji kuuza dhahabu yao kwa bei halisi na kudhibiti walanguzi katika maeneo ya wachimbaji.
Vilevile alifafanua kuwa utaratibu unaotumiwa na wachimbaji wadogo hivi sasa kuchenjua dhahabu, umekuwa ukipoteza dhahabu nyingi ikilinganishwa na utumiaji wa njia za kisasa: Pia hakuna kumbukumbu sahihi na taarifa zilizo wazi zinazoonyesha soko halisi la uuzaji wa dhahabu inayochimbwa na wachimbaji wadogo katika maeneo mbalimbali nchini.

"Tunawachimbaji wadogo wa dhahabu wengi sana nchini hii, na wanapochimba wanapata dhahabu lakini ukiwauliza wanauza wapi dhahabu yao hakuna majibu sahihi, pia ukiuliza bei kila mmoja anamajibu yake, na kwa mtindo huu wanaikosesha serikali mapato, hali hii haikubaliki lazima idhibitiwe" alisisitiza Msanjila.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila, akishuka chini ya mgodi uliojengwa katika Kituo cha Mfano na Mafunzo ili kujiridhisha na ujenzi huo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila( katikati) akiwa chini ya mgodi uliojengwa katika kituo cha Mfano na Mafunzo kilichopo Rwamgasa, mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila,( tatu kulia) na maafisa kutoka wizara ya madini na serikali ya kijiji waakiwa juu ya sehemu ya mtambo wa uchenjuaji katika Kituo cha Mfano na Mafunzo ,wakifanya ukaguzi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila, (tatu kushoto) na alipotembelea mgodi wa Mwenyekiti wa Wachimbaji Wadogo mkoani Geita (GEREMA) Christopher Kadeo( tatu kulia).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS WA FIFA, GIANN INFANTINO AWASILI NCHINI TANZANIA

RAIS MAGUFULI AHUDHURIA MKUTANO MAALUM WAKUU WA NCHI JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (EAC) UNAOFANYIKA KAMPALA NCHINI UGANDA

0
0







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika Mkutano huo Maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaofanyika Kampala nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wa nne kutoka kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir wakati Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulipokuwa ukipigwa katika ukumbi wa mkutano uliopo katika eneo la Munyonyo Kampala nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wanne kutoka kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir wakati wa mkutano huo Maalumu wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unao endelea jijini Kampala.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni akifungua Mkutano huo maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Kampala nchini Uganda.
Wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya a Afrika Mashariki wakifatilia hotuba mbalimbali katika Mkutano huo maalum.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

FIRST NATIONAL BANK YAENDESHA MKUTANO KUJADILI UCHUMI

0
0
 Afisa Mtendaji Mkuu wa FNB Tanzania, Warren Adams akizungumza na wadau pamoja na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo kwenye mkutano wa kujadili uchumi unaofanyika kila mwaka nchini. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.  Mwendeshaji wa mkutano na Mchambuzi wa Masuala ya Uchumi Barani Afrika kutoka Rand Merchant Bank ya Afrika Kusini, Neville Mandimika akizungumza na wadau kutoka sekta mbalimbali katika mkutano ulioendeshwa na First National Bank na kujadili uchumi unaofanyika kila mwaka nchini.
Wadau kutoka sekta mbali mbali wakihudhuria katika mkutano wa kujadili uchumi unaofanyika kila mwaka nchini ulioendeshwa na First National Bank Tanzania jijini Dar es salaam leo.

TANZANIA YANG'ARA KATIKA VITA DHIDI YA RUSHWA

0
0
Tanzania, Rwanda Zang’ara EAC Vita ya Rushwa .

MISIMAMO thabiti ya Rais John Pombe Magufuli katika masuala mbalimbali ya maendeleo ya Taifa imezidi kuleta mafanikio ambapo ripoti mpya katika mapambano dhidi ya rushwa imeonesha Rwanda na Tanzania kuongoza katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika mapambano dhidi ya rushwa kwa mwaka 2017. 

Kwa mujibu wa Ripoti ya Tathmini ya Hali ya Rushwa (Corruption Perception Index) iliyotolewa jana Februari 21, 2018 na Taasisi ya Transparency International, juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano Tanzania chini ya Dkt. John Pombe Magufuli katika kupambana na rushwa zimezidi kuzaa matunda katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. 

Taarifa hiyo iliyokusanya takwimu za mwaka mzima wa 2017 zinaonesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi chache zilizopanda kwa kiasi kikubwa katika kupambana na rushwa huku nyingi nyingi zikishuka au kubaki pale pale. 

Wakati mwaka 2016 Tanzania ilikuwa ya 116 duniani, katika ripoti hiyo mpya Tanzania imepanda kwa nafasi 13 na kuwa ya 103 huku ikizizidi kwa mbali nchi kadhaa kubwa duniani katika utafiti huo uliohusisha mataifa 180. 

BENKI KUU YAFAFANUA KUHUSU RIBA YA DHAMANA

Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images