Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109587 articles
Browse latest View live

MAMA SALMA, BASHE, MSUKUMA, LUSINDE WAMUOMBEA KURA MTULIA KINONDONI

0
0
Na Said Mwishehe, Glogu ya jamii

WABUNGE kutoka majimbo mbalimbali nchini kupitia Chama ChaMapinduzi (CCM), wamewaomba wananchi wa jimbo la Kinondoni jijiniDar es Salaam kuhakikisha Februari 17, mwaka huu wanamchaguamgombea ubunge wa chama hicho, Abdallah Mtulia katika uchaguzi
mdogo jimboni humo.

Wamesema Mtulia ndio chaguo sahihi kwa wananchi wa Kinondoni nakwamba akiwa mbunge watashirikiana naye katika kufanikishachangamoto za wananchi zinapata ufumbuzi wake.Pia wameeleza namna ambavyo wabunge wa CCM  wamekuwa wamojabungeni katika kupigania maendeleo ya wananchi tofauti na wabungewa upinzani ambao kila kitu wao ni kupinga hata liwe jambo lamaendeleo.

Wakizungumza kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika wanja wa People Kigogo wilayani Kinondoni jijini, wabunge hao waCCM wamewaomba wananchi kutofanya makosa kwenye uchaguzi huohuku wakitoa sababu mbalimbali za kwanini Mtulia anastahili kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Mgeni rasmi  kwenye kampeni hizo ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) amewaomba wananchikumchagua Mtulia kwani ndio mgombea sahihi na wanaamini akiwambunge watashirikiana naye kutatua kero za wananchi.
 
"Nimekuja kuzungumza na ninyi kuwaomba tarehe 17,siku yaJumamosi wote mkamchague Mtulia, lakini si tu kumchagua lazimatuseme kwanini mumchague Mtulia.Ndio mgombea mwenye sifa zoteza kuwa mbunge wa Kinondoni,"amesema Bashe.

Pia amesema kwenye kampeni hizo wapo wanaotoa hoja kuwa Serikali ya CCM haitaki mfumo wa vyama vingi, ambapo amefafanua hoja hiyo haina maana yoyote kwani mwaka 1992 licha ya watanzania wengi kutaka mfumo wa chama kimoja uendelee lakini uamuzi ulitolewa wa kuingia mfumo vyama vingi.

"Mwaka 1992, watanzania walipata fursa ya kuchagua tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi au laa.Waliotaka vyama vingi walikuwa asilimia 20 na waliosema chama kimoja kiendelee walikuwa asilimia 80."Mwaka 1995 tukafanya uchaguzi wa vyama vingi na CCM ikashinda, hivyo CCM hatuna hofu na mfumo wa vyama vingi na ndio maana tumeendelea kushinda katika kila chaguzi.

"Pia wapo wanaotoa hoja CCM hakuna demokrasia hili nalo halina ukweli.CCM demokrasia ipo tena ya kutosha.Ndani ya CCM tunaweza kutofautiana kimtazamo, tunaweza kutofautiana kwa hoja na wakati mwingine tukashikana mashati lakini ukweli utabaki tunafanya hayo yote kwasababu ya demokrasia tuliyonayo,"amesema Bashe.


BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 12.02.2018

VOA Swahili: Duniani Leo 12th February 2018

MAMA SALMA KIKWETE ATOA BUSARA ZAKE KWA MTULIA SAID MAULID NA WANA KIGOGO

SLIMMING OIL YA KUONDOA KITAMBI & KUPUNGUZA UNENE NA UZITO.

0
0
Kwa   mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, suala   la  kitambi, unene  na /ama  uzito  ulizo zidi  linasababishwa  na uwepo  kwa  kiasi  kikubwa  cha  mafuta  kwenye  mishipa  ya  damu.
SLIMMING  OIL  ni  dawa  ya  asili  inayo  saidia  kumaliza  tatizo  la  kitambi, unene  na  uzito  ulio zidi kwa  kusafisha  mishipa ya  damu  kwa  kuyeyusha  na   kuondoa  mafuta yasiyo  hitajika  ama  mafuta  ya  ziada  yaliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  damu.
VILEVILE : SLIMMING  OIL  pia  inasaidia  kutibu  na  kumaliza  kabisa  tatizo  la  kutokwa  na  chunusi  za  usoni, vipele  na  majipu mwilini  pamoja  na  tatizo  la  kutokwa  kwa  vipele sugu  katika  eneo  la  chini  ya  kisogo (kichogo )  linalo  tokana  na  kunyolewa  kwa  kutumia  mashine  ambazo  hazijafanyiwa  usafi.
Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO NATIONAL  HOUSING.
Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  0766  53  83  84.
Kwa  taarifa  na  maelezo zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyinginezo,  tutembelee  kupitia :

Maafisa Habari, TEHAMA ni Mawakala wa Mabadiliko

0
0
Na. Atley Kuni OR TAMISEMI.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Joseph Nyanda amewataka Maafisa habari na TEHAMA nchini kutekeleza majukumu yao kwakuzingatia Weledi, maarifa na ubunifu kwakuwa wao ni Mawakala wa mabadiliko.

Akifungua kikao cha siku nne mkoani humo kilicho andaliwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kwakushirikiana na Mradi wa uimarishaji wa mifumo ya umma PS3, na kushirikisha maafisa habari na TEHAMA kutoka mikoa ya Mara na Arusha, amewatahadharisha maafisa hao kuwa endapo watazembea kutekeleza wajibu wao wa msingi kwa weledi basi watu wengine watapotosha umma.

“Kila mmoja miongoni mwenu anayo dhamana yakutangaza mambo mazuri yanayofanywa na serikali, lakini mkikaa kimya ninyi kama sauti za taasisi zenu watu wasio wema watapotisha maudhui hayo na mwisho wa siku kuchafua taswira ya serikali” amesisitiza Nyanda.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano serikalini, Rebbeca Kwandu, akizungumza kabla yakumkaribisha Mgeni rasmi, amewataka maafisa hao kubadilika katika utendaji wao mara baada ya mafunzo ya mfumo huo juu ya uendeshaji wa tovuti.

“Mwanzoni tulipoanzisha tovuti hizi, hatukuwa na muongozo ambao ni dira ya uendeshaji lakini mara baada ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kuandaa muongozo huu kwakushirikiana na wadau wetu PS3 ni imani yangu tutabadilika” amesema Kwandu na kuongeza kuwa uwepo wa tovuti bila ya uwepo wa habari haina maana.

Akizungumza kwa niaba ya Mradi wa PS3 Mkurugenzi anayeshughulia utawala bora na Ushirikishwa wa wananchi Dkt. Peter Kilima, amekiri kuwa Maafisa habari na Maafisa TEHAMA ndio roho ya taasisi, hivyo ushirikishwa hasa kwenye vikao vya maamuzi itakuwa ni fursa kwao kuchuja na kuujuza umma mambo mazuri ya nchi.

Awali akitoa Salaam za Idara ya habari maelezo, Mkurugenzi Msaidizi wa habari na picha Thadeus Rhodney, amesema kuwa ili kutangaza mambo mazuri yanayofanywa na serikali lazima maafisa habari wawe na zana (tools) za utendaji kazi na zana yenyewe katika mustakabali wa sasa kwa ngazi za Mikoa na mamlaka za Serikali za Mitaa ni Tovuti.

“Wafadhali PS 3 wametuwezesha kuwa na mfumo wa Government Website Fremwork (GWF) tumieni hizi tovuti kama tools ya kuujuza umma.

Ofisi Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Mradi wa Uimarishaji mifumo ya umma chini ya mradi wa PS3 wanaendesha Mafunzo ya nanna bora ya uendeshaji wa tovuti za serikali ambapo Maafisa habari pamoja na Maafisa TEHAMA wapatao 418 nchini kote watapatiwa mafunzo
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara,Raphael Joseph Nyanda akifungua Semina kwa Maafisa hao wa Mkoa wa Mara na Arusha.
Dkt. Peter Kilima, Mkurugenzi wa Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Wananchi kutoka PS3, akizungumza wakati wa Mafunzo hayo
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari Maelezo anayeshghulikia Habari na picha akitoa Salama za Idara wakati wa Semina hiyo.

ARDHI YASABABISHA MGOGORO KATI YA FAMILIA NA SERIKALI MJINI GEITA

0
0

Na Joel Maduka ,Geita.

Familia ya Bw Mlelemi Mashirungu inayoishi mtaa wa Mkolani Kata ya Nyankumbu wilayani Geita imeilalamikia serikali kwa kuanzisha ujenzi wa shule ya msingi Shinde kwenye shamba la ukoo huo lenye ukubwa wa ekari 20 bila makubaliano na serikali ya Halmashauri ya mji wa Geita .

Msimamizi wa eneo hilo Bw Sizya Mashirungu amesema eneo la ujenzi wa shule hiyo lilitengwa na serikali ya kijiji kabla ya kubadilishwa na kuwa mitaa lakini ameshangazwa na kitendo cha serikali kuanzisha ujenzi katika eneo lake bila makubaliano.

Bw Mashirungu alisema eneo hilo limeanza kumilikiwa na ukoo tangu mwaka 1991 baada ya Baba yao mzazi kufariki na kwamba limekuwa likitumika katika shughuli za kilimo.

“Anayezungumza kuwa hii ni hifadhi akuna ofisi yoyote ambayo ilishawai kufika kuweka pingamizi juu ya eneo hili na mshangaa mwenyekiti ambaye anangangania kuwa eneo hili ni la hifadhi yani huu ni utapeli kabisa na mimi sitakubaliana na maamuzi ambayo yanataka kuchukuliwa na serikali juu ya matumizi ya eneo hili”Alisema Mlelemi.
Baadhi ya eneo ambalo linalalamikiwa na Sizya Mashirungu kuvamiwa na kujengwa shule na serikali kinyume na makubaliano kati yake halmashauri ya Mji wa Geita. 
Mwenyekiti wa mtaa Shinde Bw Makoye Mumilambo akizungumza juu ya malalamiko ambayo yametolewa na Bw,Sizya Mashirungu juu ya kutaka kutahifishwa eneo la familia na serikali ya mtaa huo. 
Eneo linalolalamikiwa likiwa tayari limeshaanza kuchimbwa Msingi kwaajili ya ujenzi wa shule ya Msingi ya Shinde. 

Wakazi Mwananyamala wavutiwa na huduma za 'One Stop Centre' za CRC

0
0
BAADHI ya wananchi wanaoishi Mwananyamala 'A' jijini Dar es Salaam wamevutiwa na huza huduma za pamoja kwa waathirika kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ‘One Stop Center’ na msaada wa ushauri kisheria zilizotolewa jana na Kituo cha Usuluhishi – CRC.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi waliopata huduma hizo kwenye Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mwananyamala 'A' walisema wamefurahishwa na kitendo cha CRC kusogeza huduma hizo eneo lao jambo ambalo limewavutia wakazi wengi.

"...Binafsi nimevutiwa na kitendo cha huduma kama hii kutolewa eneo letu, mimi nilikuwa na kesi kuna mtu anataka kunidhulumu kiwanja kesi yangu inaendelea lakini baada ya kuona kuna huduma hizi nimekuja kupata msaada wa kisheria na nimeshauriwa cha kufanya...,"alisema Bi. Nzela Khamis akizungumza mara baada ya kuhudumiwa.
Mwanasheria wa Kituo cha Usuluhishi–CRC, Suzan Charles (kulia) akitoa huduma kwa baadhi ya wateja waliojitokeza kwenye zoezi la utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa waathiriwa wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na huduma zingine muhimu kwa kundi hilo Mwananyamala 'A' jana jijini Dar es Salaam.
Afisa wa Polisi na Mratibu wa Kituo cha One Stop Center (OSC) Amana, Bi. Christina Onyango (kulia) akimsikiliza mmoja wa wateja waliofika kupata huduma leo Mwananyamala 'A' jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wahudumu wa afya kwenye kituo hicho akitoa huduma kwa mmoja wa wateja waliofika kupata huduma.
Shughuli za utoaji huduma kwa baadhi ya wateja waliojitokeza kwenye zoezi la utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa waathiriwa wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na huduma zingine muhimu kwa kundi hilo Mwananyamala 'A' jijini Dar es Salaam zikiendelea.

Shughuli za utoaji huduma kwa baadhi ya wateja waliojitokeza kwenye zoezi la utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa waathiriwa wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na huduma zingine muhimu kwa kundi hilo Mwananyamala 'A' jijini Dar es Salaam zikiendelea.



ALICHOKISEMA NAIBU WAZIRI WA UJENZI, KWANDIKWA KWA TAASISI YA TARURA

MAGAZETI YA LEO JUMNNE FEBRUARI 13, 2018

TIGO YATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA PROMOSHENI YA NYAKA NYAKA BONUS.

0
0
Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ya Tigo Tanzania, leo imewazawadia washindi 36 wa promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus simu aina ya Tecno R6 zenye uwezo wa 4G. 

Akitangaza washindi hao wa kwanza 36 waliopatikana katika promosheni hiyo inayoendelea kwa kipindi cha miezi mitatu, Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael alibainisha kuwa washindi 13 wanatoka Dar es Salaam, na wengine ni wakaazi wa mikoa ya Morogoro, Pwani, Tanga, Dodoma, Mtwara, Iringa, Mwanza na Arusha. 

‘Ofa hii kabambe ni sehemu ya ubunifu wa Tigo unaoendana na mahitaji ya wateja na utakaowezesha kila mtu kufurahia huduma bora za mtandao wa Tigo 4G wenye kasi zaidi na ulioenea zaidi nchini,’ alisema.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kati) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam alipotangaza washindi wa kwanza wa simu za Tecno R6 zenye uwezo wa 4G katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa. Kushoto ni Mtaalam wa Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza.
 Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kulia) akimzawadia  Saidi Abdallah Popote wa Tabata, Dar es Salaam simu aina ya Tecno R6 yenye uwezo wa 4G aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus, huku akishuhudiwa na baadhi ya washindi wengine. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa.
 Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kati) akimzawadia  Advera Revelian Kyaruzi wa Tegeta, Dar es Salaam simu aina ya Tecno R6 yenye uwezo wa 4G aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus, huku akishuhudiwa na baadhi ya washindi wengine. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAYA 408 KUFANYIWA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI YA KAYA BINAFSI MKOANI MWANZA

DIAMOND,HAMISA MOBETO WAFUNGA JALADA MATUNZO YA MTOTO

0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

HATIMAYE jalada la kesi ya madai ya matunzo ya mtoto lililofunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa watoto na Mwanamitindo maarufu nchini, Hamisa Mobeto dhidi ya mwanamuziki, Naseeb Abdull 'Diamond Platinumz' limefungwa rasmi.

Akizunguma leo na waandishi wa habari baada ya kutoka mahakamani Diamond amesema, walifika mahakamani hapo kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ili upande wa Ustawi wa Jamii na Mahakama ziwe sawa ili kesho na kesho kutwa kisije kikazungumzwa kitu kingine cha uongo.

"Tunategemea, mtoto wetu aje kuwa mtu fulani ama kiongozi, hivyo nawashauri wazazi wa kiume na wa kike wajitahidi kuweka majivuno yao pembeni wanapokuwa na migogoro na wasimuingize mtoto", amesema Diamond.

Amesema kufanya hivyo kwa namna moja ama nyingine ina muathiri mtoto.
"Nilazima kuweka majivuno pembeni ya matatizo yetu binafsi kwa kuwa yana muumiza mtoto, ni lazima muangalie ni namna gani mnatengeneza mazingira mazuri ya kuweza kumlea na kumsaidia mtoto,"amesema.

Naye, Wakili wa Mobeto, Walter Godluck amesema ustawi wa jamii unasaidia katika usuluhishi wa kesi za watoto ambazo zinahusu malezi ambapo baba na mama wanakubalina ni jinsi gani wanaweza kulea mtoto.

Amesema, leo wameleta ripoti ya usuluhishi mahakamani hapo ambapo kesi ya msingi ya matunzo ya mtoto ilifunguliwa.Amesema, malalamiko waliyoyaleta kuhusu matunzo ya mtoto upande wa pili wameridhia na wameona kuna haja ya kuyafanyia kazi na kwamba kiasi cha fedha walichokubaliana nacho wamekiweka kifamilia.

Wakili huyo amesema wazazi wamekubali kushughulikia malezi ya mtoto, na kuwa Diamond yupo tayari kumlea mtoto na atafanya hivyo kwa uwezo wake .Huku akicheka kuashiria furaha, Hamisa Mobeto amesema" kuhusu maamuzi nimeefurahia nayo, sababu panda zote mbili tulikaa tuka discuss na tukakubaliana nayo, nashukuru kila mtu ameridhia nayo ameridhika nayo na yamekwisha" amesema Mobetto.

Mobeto alifungua kesi ya matunzo ya mtoto mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine alikuwa anaiomba Mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi.

Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto alikuwa akiiomba Mahakama imuamuru Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.

AGPAHI YATOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA KISAIKOLOJIA KWA WAHUDUMU WA VITUO VYA TIBA NA MATUNZO MWANZA

0
0
Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limeendesha mafunzo kuhusu msaada na huduma za kisaikolojia kwa wahudumu wa jamii wanaosaidia kazi katika vituo vya tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) vilivyopo katika halmashauri za wilaya mkoani Mwanza. 

Mafunzo hayo ya siku tano yanayokutanisha wahudumu wa jamii kutoka halmashauri za wilaya za Ilemela,Kwimba, Magu,Buchosa,Misungwi,Sengerema na Nyamagana yanafanyika kuanzia Jumatatu Februari 12,2018 hadi Ijumaa 16 Februari ,2018 katika ukumbi wa Midland Hotel jijini Mwanza.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, Mratibu wa Kudhibiti Ukimwi mkoa wa Mwanza Dk. Pius Masele alisema mafunzo hayo yatawasaidia watoa huduma ngazi ya jamii kuboresha huduma katika vituo vya afya kwenye maeneo yao.

“Kupitia mafunzo haya mtaweza kuwaunganisha wateja na huduma mbalimbali za kijamii ili kuhakikisha kunakuwepo uendelevu wa huduma kwenye vituo vya tiba na matunzo ikiwa ni pamoja na kuwarudisha kwenye huduma wateja waliopotea”,alisema Dk. Masele.
Mratibu wa Kudhibiti Ukimwi mkoa wa Mwanza Dk. Pius Masele akifungua mafunzo kuhusu msaada wa huduma za kisaikolojia kwa wahudumu wa jamii. Kulia ni Afisa Miradi Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Mwanza, Cecilia Yona.
Dk. Masele akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo watumie mafunzo wanayopewa ili wakaboreshe huduma kwenye vituo vya tiba na matunzo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada ukumbini.
Afisa Miradi Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Mwanza, Cecilia Yona akielezea malengo ya mafunzo ya huduma na msaada wa kisaikolojia na maana yake kwa wahudumu wa jamii.

KILOMBERO YAWAWEZESHA MAELFU WAZEE WASIOJIWEZA HUDUMA ZA CHF ILIYOBORESHWA

0
0

Na John Nditi, Kilombero.

HALMASHAURI ya wilaya ya Kilombero , mkoani Morogoro wamewakatia  kadi za   Mfuko wa Afya ya Jamii  (CHF ) iliyoboreshwa  wazee wasiojiweza zaidi ya 7,800 waliopo katika  kata  26  ili kuwawezesha kupata  huduma bora za matibabu katika vituo vya  Afya, Zahanati na hospitali na wategemezi wao.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri  hiyo , Dennis Londo   alisema hayo  mbele ya  Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari, kabla ya zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa baadhi ya wazee wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.

Londo  alisema   kuwa , hadi sasa  kiasi cha Sh milioni 13.3 zimetumika  kwa ajili ya mpango wa kuwakatia wazee wasiojiweza  bima  ya  afya ya CHF Iliyoboreshwa.Hata hivyo alisema , halmashauri hiyo imejipanga  kuhakikisha wazee wanapatiwa bima ya Afya CHF iliyoboreshwa na lengo  ni  kuwafikia  wazee wasiojiweza  zaidi ya  15,000  katika kata zote 26.

“ Halmashauri ya wilaya hii imejipanga vyema na inatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM  na miongoni mwa mam ohayo ni kundi la wazee wasiojiweza wamenufaka na huduma ya bima  ya afya” alisema Londo.
 Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( wapili  kushoto) akimkabidhi kadi ya bima ya afya ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Iliyoboreshwa mzee  Petro Karubandika mkazi wa kata ya Mlimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero  wakati wa zoezi la ugawaji  kadi  hizo kwa wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba na (  kushoto) ni  mkuu wa wilaya ya Kilombero, James Ihunyo na ( watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilombero, Dennis Londo.
 Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( wapili kushoto) akimkabidhi kadi ya bima ya afya ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Iliyoboreshwa   Nelasi Nyingi , mkazi wa kata ya Mlimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero  wakati wa zoezi la ugawaji  kadi  hizo kwa wapatao  2,100 kutoka  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba (  kushoto ) ni mkuu wa wilaya ya Kilombero, James Ihunyo na ( watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilombero, Dennis Londo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri   ya Kilombero , Dennis Londo  ( kulia) akitoa maelezo mafupi ya mapango wa kuwakatia bima ya afya wazee  wasiojiweza kwa  Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari ( wapili kutoka kushoto) wakati wa  zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa  wazee wapatao  2,100 wa  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.
Baadhi ya wazee wa kata saba za tarafa ya Malimba , halmashauri ya wilaya ya Kilombero wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu tawala mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari  ( hayupo pichani) wakati wa  zoezi la ugawaji  kadi za CHF Iliyoboreshwa  kwa  wazee wapatao  2,100 wa  vijiji 23 vya kata saba za Tarafa ya Mlimba.  ( Picha na John Nditi).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO

0
0
Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza kumfungia  Juma Nyoso wa Kagera Sugar kwa kosa la kupiga shabiki baada ya mchezo kati ya timu yake dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Kaitaba, mkoani Kagera.

Akitolea ufafanuzi hukumu hiyo, Ofisa habari wa TFF Clifford Ndimbo amesema kamati ya nidhamu iliketi na kujadili masuala mbalimbali ya nidhamu ikiwemo suala la beki wa timu ya Kagera Juma Nyoso kumpiga shabiki wakati wa mchezo wao dhidi ya Simba uliochezwa mwanzoni mwa mwaka huu.

Ndimbo amesema  "Kamati ya nidhamu ya TFF iliweza kukaa na kulijadili masuala mbalimbali ya nidhamu pia  ilijadili shauri ambalo lilifikishwa kwenye kamati hiyo ambalo lilimuhusu mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyoso kuhusu tukio lake ambalo lilitokea kwenye mchezo uliozikutanisha Kagera Sugar na Simba kwenye uwanja wa Kaitaba," amesema.

Katika kesi hiyo Nyoso alituhumiwa kwa kosa la kumpiga shabiki na kupelekea kupoteza fahamu baada ya kumalizika kwa mchezo kinyume na kanuni za ligi kuu zinazozungumzia uungwana katika mchezo wa kosa 'Fair Play'.

Katika hukumu hiyo iliyotolewa na Kamati waliweza kupitia ripoti ya kamishna wa mchezo huo ambapo imeweza kuelezea  tukio hilo ambapo  Nyoso wakati anaelekea vyumbani aliweza kupishana na shabiki aliyekuwa anapuliza vuvuzela na kusababisha Nyoso kusimama na kuanza kumpiga shabiki huyo kwa kutumia kiatu na baadaye akamuinamisha na kuanza kumpiga kwa kutumia goti.

"Kwa upande wa Kamati iliweza kumuita Nyoso na kujitetea na kwa upande wake alikana madai yanayomkabili ya kumpiga shabiki na kudai kuwa amlikunja na sio kumpiga," amesema Ndimbo

Baada ya kumsikiliza utetezi wake Kamati imeweza kumtia hatiani Nyoso kwa kupitia kanuni ya ligi kuu na pia waliweza kupitia  taarifa za nyuma za mchezaji huyo na kuona kuwa Nyoso  aliwahi kuadhibiwa kwa makosa ya utovu wa nidhamu. 

Nyoso amepewa adhabu ya kukosa mechi tano na faini ya Sh.milioni moja.

BASATA KUZICHUKULIA HATUA BENDI ZISIZOSAJILIWA

0
0
Na Agness Francis, Globu ya jamii 

BARAZA la Sanaa Tanzania (BASATA) kutatua kero ya wasanii wa dansi kwa kuwachukulia hatua wanamuziki wa ndondo bendi zisizosajiliwa hapa nchini. 

Bendi hizo zimejitokeza kwa wingi kufanya shoo kwenye kumbi mbali mbali ya starehe kwa kuimba kopi ya nyimbo za wasanii hao na kusababisha muziki huo kushuka. Akizungumza na Michuzi Blog leo katika Ukumbi wa BASATA Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bendi ya Twanga Pepeta Asha Baraka amesema muziki huo wa dansi umekuwa hauna faida kwao.

Amefafanua hasa wanapokwenda kufanya shoo kwenye makumbi wateja wanakuwa wachache wanakimbilia huko kwenye hizo bendi zilizoibuka kufanya matamasha yasio na kiingilio. 

Aidha Asha Baraka amesema"Kwa wasanii wetu pia wapo wanaoshusha muziki huo kwa msanii kutoka kwenye bendi iliyosajiriwa na kujiunga na hizo bendi zisizofahamika kufanya shoo kama kawaida."Badala yake huleta sintofahamu kwa mameneja kuambiwa wamegawanya bendi ikiwa jambo hilo si la kweli," amesema Asha Baraka.

Ameongeza matokeo yake kusababisha kupungua kwa kipato na biashara inakuwa ngumu,kwani hakuna faida inayopatikana kutokana na hawa ndondo bendi waliojitokeza kufanya kazi hiyo.

Wakati huohuo vilevile Mkurugenzi wa MPOAFRIKA Mpondoli Mwakabana, amewataka BASATA kuwapigania huko ngazi za juu ili kuongezewa muda katika shughuli zao za biashara za makumbi ya starehe na itapelekea hata hizo bendi ziweze kukodishwa badala ya ya zile ndondo ambazo huwa kama deiwaka.

AWESO ATAKA MIRADI YA MAJI IKAMILIKE KWA WAKATI

0
0
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso akikagua bomba la DAWASCO linalosambaza Maji ya Ruvu Juu iliyopo maeneo ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso akikagua Mradi wa visima 20 eneo la Kisarawe II katika mji wa Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso aendelea na ziara ya kukagua maendeleo ya Miradi ya Maji Mji wa Kigamboni Jijini Dar es salaam.

MAHAKAMA YAIPIGA KALENDA KESI YA UHUJUMU UCHUMI

0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeipiga kalenda kesi ya Uhujumu Uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh.Bilioni 2.4,  inayomkabili Mkurugenzi wa Tathmini ya Madini nchini,  Archard Kalugendo na mwenzake hadi Februari 27, mwaka huu.

Hatua hiyo, imekuja leo baada ya upande wa mashataka  uliokuwa ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Estazia Wilson kuieieleza Mahakama kuwa jadala la kesi hiyo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)

Karugendo na mwenzeke, Mthamini wa Madini ya Almasi wa Serikali, Edward Rweyemamu wanakabiliwa na shtaka la uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh.bilioni  2.4.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Godfrey  Mwambapa aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 27, mwaka huu itakapotajwa tena.

Inadaiwa kati ya Agosti 25 na 31, mwaka 2017  katika maeneo mbalimbali kati ya Dar es Salaam na Shinyanga, kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathamini  wa madini waliisababishia hasara Serikali kiasi hicho cha fedha.

PROGRAMU YA URITHI WA UKOMBOZI WA BARA LA AFRIKA KUIJENGEA HESHIMA TAIFA

0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM.

Serikali yatao Milioni Mia saba kwa ajili ya ukarabati wa Jengo lilokuwa Makao Makuu ya Wanakamati wanaopigania Uhuru wa kulikomboa Bara la Afrika ikiwa ni sehemu ya kuhifadhi historia ya Ukombozi wa Bara la Afrika.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipotembelea ofisi zinazoratibu programu hiyo ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika leo jijini Dar es Salaam kupata taarifa ya maendeleo ya programu hiyo.

‘’Tumepewa dhamana na heshima kubwa na Umoja wa Afrika ya kuhifadhi historia ya Ukombozi wa Bara la Afrika sababu ya Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere alivyopigania uhuru wa bara la afrika na kutoa ofisi jijini Dar es Salaam ambayo ilikuwa Makao Makuu ya wapigania Uhuru kutoka nchi mbalimbali za Afrika kukutania na kupanga mikakati hivyo ni vyema tuhifadhi historia hii,’’ Dkt.Mwakyembe.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa Habari  (hawapo pichani) kuhusu Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika ambao utakuwa ukikusanya na kuhifadhi historia ya ukombozi wa bara la Afrika alipotembelea yaliyokuwa Makao Makuu ya Ofisi za Wanakamati wa Ukombozi wa Bara la Afrika zilizopo jijini Dar es Salaam leo,kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Nicholaus Wiliam.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiwaeleza waandishi (hawapo pichani) kuhusu historia ya pikipiki aliyoshika kuwa ilikuwa ikitumiwa na Rais wa awamu ya kwanza wa Msumbiji Hayati Samora Machel katika kipindi cha kupigania uhuru wanchi yake, alipotembelea yaliyokuwa Makao Makuu ya Ofisi za Wanakamati wa kukomboa Bara la Afrika leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Historia na Makumbusho (JWTZ) Kanali Robert Mjange (wa pili kulia) akimweleza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (wa kwanza kulia) kuhusu hali ya jengo ambalo lilikuwa ni  Makao Makuu  yaliyokuwa yakitumiwa na viongozi mbalimbali  wa Afrika ambao walikuwa wanakamati wa kupigania Ukombozi wa Bara la Afrika hapo zamani, alipotembelea Ofisi zinazoratibu Programu ya Ukombozi  Bara la Afrika zilizopo jijini Dar es Salaam kupata taarifa ya maendeleo ya programu hiyo.

Mratibu wa Programu ya Urithi na Ukombozi wa Bara la Afrika Bibi Ingiahedi Mduma (katikati) akimwonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) jengo ambalo lilikuwa ni  Makao makuu ya Viongozi wa Kamati ya kupigania uhuru wa bara la afrika  hapo zamani ambalo linahitaji ukarabati kwa sasa  alipotembelea ofisi zinazoratibu programu hiyo leo jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 109587 articles
Browse latest View live




Latest Images