Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

MKUTANO WA MAWAZIRI WA SEKTA MALIASILI,MAZINGIRA WA JUMUIYA AFRIKA YA MASHARIKI WAFANYIKA LEO JIJINI ARUSHA

$
0
0
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakati wa mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (kulia) akisaini baadhi ya makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. Wanaoshuhudia ni Mawaziri wa Mazingira kutoka Uganda na Kenya.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (wa pili kulia) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Bi. Katerina Rangnitt wakiangalia baadhi ya michoro ya katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mradi huo ya katuni unafadhiliwa na Serikali ya Sweden kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakimsikiliza mmoja ya wachora katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Picha ya pamoja ya baadhi ya wajumbe wa mkutano huo.(PICHA ZOTE NA HAMZA TEMBA-WMU)

MBIVU NA MBICHI KWA WANYOGE WA RC MAKONDA KUFAHAMIKA KESHO.

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda anawaalika Wananchi wote waliofika kwenye Wiki ya Sheria na kusikilizwa Kero na malalamiko yao na jopo la Wanasheria kufika ukumbi wa Diamond Jubilee siku ya kesho February 10 kuanzia Saa mbili asubuhi kwaajili ya kupata mrejisho wa malalamiko waliyowasilisha kwa Wanasheria. 

Tayari maandalizi ya tukio hilo yamekamilika kwa 100%, unachotakiwa wewe ni kuwahi mapema ili uweze kujua hatma ya malalamiko yako.

Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dar es salaam. 

HAKIMU WA KWELI NI MUNGU.

MICHUZI TV LIVE: USIKU WA LADY IN RED NDANI YA UKUMBI WA KING SOLOMON JIJINI DAR

AKIBA YA FEDHA ZA KIGENI YAONGEZEKA-MAJALIWA

$
0
0
*Asema rekodi hiyo haijawahi kufikiwa kwa miaka minne

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema akiba ya fedha za kigeni imeongezeka na kufikia dola za Marekani bilioni 5.91 kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa kwa takriban miaka minne kuanzia mwaka 2013 hadi 2016.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Februari 9, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Waziri Mkuu amesema mbali na kuongezeka kwa akiba ya fedha za kigeni, pia thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi imekuwa takriban dola za Marekani bilioni 8.695 ikilinganishwa na wastani wa dola bilioni 8.828 kwa miaka mitatu iliyopita.Hata hivyo Waziri Mkuu ameongeza kuwa utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha nusu mwaka ni wa kuridhisha ambapo ukusanyaji wa mapato ulifikia Sh. trilioni 12.95 sawa na asilimia 82.8 ya lengo lililopangwa katika kipindi hicho. 

Amesema matumizi ya fedha hizo yameelekezwa katika kugharamia shughuli mbalimbali za Serikali za kuhudumia wananchi na miradi ya kipaumbele ambayo ni kuanza kwa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Standard Gauge.Pia kugharamia Mpango wa Elimumsingi Bila Malipo, kugharamia Mpango wa Ununuzi wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi na utekelezaji wa miradi ya usambazaji maji vijijini na mijini na usambazaji wa umeme vijijini kupitia REA.

Miradi mingine ni ununuzi wa meli za abiria na mizigo katika maziwa, ukarabati na ujenzi wa baadhi ya viwanja vya Ndege na kujenga na kuendeleza maeneo ya uwekezaji wa viwanda katika mikoa mbalimbali nchini.“Hakika kwa mafanikio haya tuna kila sababu ya kumpongeza Rais Dkt. John Magufuli kwa uongozi wake mahiri na juhudi anazofanya za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma muhimu na maendeleo ya haraka.”

Waziri Mkuu amesema  Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha kuwa inatekeleza ahadi zake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba malengo yaliyowekwa kwa mwaka 2017/2018 yanafikiwa kwa kiwango kikubwa. Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha na kujenga misingi na mifumo imara ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa lengo la kuwa na mapato endelevu kwa ajili ya kugharamia matumizi yake. 

Vilevile, kuwa na usimamizi madhubuti wa ukusanyaji wa mapato ambao utasaidia kupanua wigo na kudhibiti ukwepaji wa kodi kupitia urasimishaji wa shughuli za uchumi kwa kuwezesha ukuaji wa biashara katika sekta ndogo na za kati ambazo ndiyo mihimili wa kuzalisha ajira na kukuza uchumi.Akizungumzia kuhusu viashiria mbalimbali vya kiuchumi, Waziri Mkuu amesema vinaonesha kwamba hali ya uchumi ni nzuri na pato la Taifa katika kipindi cha Julai hadi Desemba, 2017 lilikua kwa wastani wa asilimia 6.8. 

“Hali hii inaashiria kwamba tuna matarajio makubwa ya kufikia lengo la mwaka la ukuaji wa asilimia 7.0. Sekta zilizochangia kwa kiwango kikubwa katika ukuaji huo ni habari na mawasiliano, uchimbaji madini, biashara, ujenzi na uzalishaji viwandani.”


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
IJUMAA, FEBRUARI 9, 2018.

MAKAMU WA RAIS AANZA ZIARA YA SIKU NNE MKOANI IRINGA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo ameanza ziara ya siku nne mkoani Iringa ikiwa na lengo la kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo na kuzindua mradi wa kuendeleza utalii ukanda wa kusini mwa Tanzania – REGROW.

Mara baada ya kuwasili mkoani Iringa , Makamu wa Rais alifungua wodi mpya katika Zahanati ya Kising’a ambapo aliwaomba wananchi wote wajiunge na mfuko wa bima ya Afya ili waweze kunufaika na huduma bora za afya.“niwaombe sana ndugu zangu kila mmoja ahakikishe ana bima ya afya, bima ya afya ndio mkombozi wako, unapopata mavuno yako weka pesa ya bima ya afya”

Makamu wa Rais alitoa pongezi kwa Wananchi hao kwa mwamko wa kuchangia ujenzi na kutoa eneo lakini pia pongezi kwa umoja wa makampuni ya Asas kwa ufadhili wa shilingi za kitanzania milioni 125.Makamu wa Rais alisema Ilani ya CCM inatuagiza kujenga zahanati katika kila kijiji hivyo ujenzi wa Wodi hii katika Zahanati ya Kising’a ni utekelezaji wa maagizo ya Ilani hiyo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi waliojitokeza wakati wa ufunguzi wa wodi katika zahanati ya Kising’a mkoani Iringa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya uendeshaji na uzalishaji wa kiwanda cha Ivori Food & Bevarage cha Iringa kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Bw. Suhail Esmail Thakore. (Picha na ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya utengenezaji wa viungo katika kampuni ya GBRI inayozalisha bidhaa za mboga mboga zinazojulikana kama Eat Fresh mjini Iringa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyeshwa baadhi ya bidhaa za mboga mboga za Eat Fresh na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GBRI Bi. Hadija Jabir.




Introducing "Nimekuzoea" (Official Video) by Mbosso

BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA 09.02.2018

INTRODUCING "ALELE" OFFICIAL AUDIO BY MBOSSO


VOA Swahili: Duniani Leo 9th February 2018

Article 1

RAIS DKT. MAGUFULI AWAANDALIA SHEREHE YA MWAKA MPYA MABALOZI WANAOWAKILISHA NCHI ZAO HAPA NCHINI (DIPLOMATIC SHERRY PARTY) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam Ijumaa jioni Februari 9, 2018 kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kuwakaribisha Mabalozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya kuanza kwa hafla ya kukaribisha mwaka mpya kwa Mabalozi hao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Dkt. Augustine Mahiga katika picha ya pamoja na  Mabalozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika Hafla ya kukaribisha Mwaka mpya 2018 kwa mabalozi hao (Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika Ikulu.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Dkt. Augustine Mahiga katika picha ya pamoja na  wawakilishi wakazi wa Jumuiya mbalimbali za kimataifa wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika Hafla ya kukaribisha Mwaka mpya 2018 kwa mabalozi hao iliyofanyika Ikulu.
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

DUKA LA VIFAA VYA UJENZI LAFUNGULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMPUNI  ya Kimataifa ya Kohler ya bidhaa bora za ujenzi imefungua duka la kusambaza bidhaa  zake katika Kampuni ya ABC Emproria jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Rais wa Kampuni hiyo Kanda ya Bara ya Kusini Asia na EMEA, Salil Sadanandan amesema kampuni imeamua kuingia katika soko la Tanzania kutokana na kufanya utafiti na kubaini kuwa ni moja ya nchi katika ukanda wa Afrika Mashariki sekta ya ujenzi inakuwa kwa kasi.

“Kutokana na kasi ya kukua kwa sekta ya ujenzi nchini tumeona kuna umuhimu wa kusogeza huduma ya upatikanaji wa bidhaa za Kohler kwa urahisi wakala wetu wa ABC  Emporio ambayo ina uzoefu mkubwa wa kuuza na kufunga vifaa vya ujenzi , huu ni mwendelezo wa kupanua masoko yetu barani Afrika ambao tayari wana matawi katika nchi za Kenya na Uganda” Amesema Sadanandan .

Nae Rais wa Kampuni  ya ABC Emporio, Muhamed Hadani amesema kuwa wanajivunia kuwa mawakala wa kuuza bidhaa za Kohler pia ni fursa pekee kwa watanzania kupata bidhaa hizo kwa gharama nafuu
 Rais wa Kampuni ya Kohler Kanda ya Bara ya Kusini Asia na EMEA, Salil Sadanandan akizungumza na waandishi habari kuhusiana na ufunguaji wa duka la vifaa vya ujenzi leo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Kampuni  ya ABC Emporio, Muhamed Hadani akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na usambazaji wa bidhaa za Kohler leo jijini Dar es Salaam.
 Msemaji wa Kampuni ya ABC Emporio, Matha Majura akizungumza na wandishi wa habari  kuhusiana na kampuni huyo inavyofanya kazi hapa nchini.
Muonekano wa duka la vifaa vya ujenzi lililofunguliwa leo jijini Dar es Salaam.

MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO FEBRUARY 10,2018

TUME ya Uchaguzi yavikumbusha vyama vya siasa kwasilisha orodha ya mawakala wao

$
0
0

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevikumbusha vyama vya siasa ambavyo vimesimamisha wagombea ubunge na udiwani katika majimbo mawili na kata tisa kuwa kesho (Februari 10) ndio siku ya mwisho ya kuwasilisha orodha ya mawakala wao kwa wasimamizi wa uchaguzi.


Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Bw. Ramadhan Kailima amesema hatua hiyo ni kwa mujibu wa kifungu namba 57 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi (Sura ya 343) na kifungu namba 58 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa (Sura ya 292) ambazo zinabainisha kuwa majina ya mawakala  wa vyama vya siasa yanatakiwa kuwasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi siku saba kabla ya uchaguzi.


“Uchaguzi utafanyika tarehe 17 Februari 2018, hivyo siku saba kabla ya uchaguzi ni kesho (tarehe 10 Februari), hivyo nivisihi vyama vyote vya siasa vilivyosimamisha wagombea, kama vikitaka kuweka mawakala  kwenye uchaguzi huo, vipeleke orodha yao yaani utambulisho wa barua na kesho Jumamosi ndio siku ya mwisho.


“Ikifika tarehe 11 yaani Jumapili wasimamizi wa uchaguzi hawataruhusiwa kupokea orodha ya mawakala wa vyama vya siasa,” amesisitiza Kailima na kuongeza kuwa orodha hiyo ya mawakala kwa mujibu wa sheria iwe inaonesha jina la wakala, anuani yake na kituo ambacho chama kimependekeza wakala aende kusimamia.


KUKAMILIKA UWANJA WA NDEGE CHATO KUTAFUNGUA FURSA ZA UTALII GEITA

$
0
0
Na Joel Maduka-Chato

Kukamilika kwa ujenzi wa uwanja mkubwa wa ndege wilayani Chato mkoani Geita unatarajia kuwavutia watalii wengi kutembelea kivutio cha hifadhi ya Taifa cha Rubondo Kilichopo mkoani humo .

Ujenzi wa uwanja huo umeanza rasmi mwezi wa Septemba mwaka jana na unatarajia kukamilika Juni mwaka huu.Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini (TANAPA), Jenerali Mstaafu George Waitara wakati alipotembelea uwanja huo pamoja na wajumbe wa bodi hiyo na baadhi ya watendaji kwa nia ya kujionea maendeleo ya ujenzi huo ambao umeelezwa kukamilika kwa asilimia 65.

“ Kiukweli niseme kazi kubwa sana ambayo imefanyika ya ujenzi wa uwanja huu utakuwa na faida kubwa sana kwaajili ya mambo ya utalii na mambo mengine kama ya biashara na suala jingine kubwa ni kuibua vivutio vingine tupate watalii wengi zaidi , tunatarajia utakapokamilika utaleta manufaa sana katika sekta mbali mbali zikiwemo za utalii na biashara mkoani Geita na mikoa ya jirani,”alisema Waitara.

Kwa upande wake, Mhandisi wa ujenzi wa uwanja huo,Makuye Muhinga,Alisema uwanja huo wenye barabara ya kutua ndege (run a way ) yenye urefu wa Mita 300 upo kwenye hatua nzuri na kwamba wanatarajia kukamilisha mwaka huu ujenzi wa uwanja.
Mwenyekiti wa wa Bodi ya Shirika la kuhifadhi Wanyamapori Tanzania (TANAPA), Jenerali Mstaafu,George Waitara akizungumza na Mhandisi wa ujenzi wa uwanja huo,Makuye Muhinga juu ya mikakati ambayo inaendelea ya ujenzi wa uwanja wa ndege Wilayani Chato mkoani Geita,wakati walipoutembelea. 
Barabara ya kutua ndege (run away) yenye urefu wa Mita 300 ambayo kwa sasa hipo kwenye hatua nzuri za mwisho kukamilika. 
Baadhi ya watendaji na wajumbe wa Bodi ya TANAPA wakikagua ujenzi wa mradi wa uwanja wa Ndege Wilayani Chato Mkoani Geita. 
Mwenyekiti wa bodi ya hifadhi za Taifa nchini (TANAPA), Jenerali Mstaafu,George Waitara akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Chato (Katikati) Shaaban Ntarambe pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi ,Robert Gabriel Luhumbi wakati walipofika na kujionea ujenzi wa uwanja wa ndege ambao unajengwa Wilaya ya Chato unavyokwenda kwa kasi. 
Mhandisi wa ujenzi wa uwanja huo,Makuye Muhinga akizungumza na Mwenyekiti wa bodi ya hifadhi za Taifa nchini (TANAPA), Jenerali Mstaafu,George Waitara pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel,Juu ya hatua ambazo wamezifikia hadi sasa za ujenzi wa uwanja wa Ndege. 



INTRODUCING "TUHESHIMIANE" BY MR NICE

TANFAS YAWEKA MIKAKATI YA KUINUA VIWANDA NCHINI

Introducing "Thomas Sankara" by Mr Teacher

Rais Magufuli ampandisha cheo na kumteua Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar

WAZIRI MKUU AMJULIA HALI MWENYEKITI WA CWT SINGIDA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtembelea na kumpa pole Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu (CWT) mkoa wa Singida Mwalimu Aron Jumbe aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

Akiwa hospitalini hapo leo (Jumamosi, Februari 10, 2018), Waziri Mkuu amefarijika baada ya kumkuta Mwenyekiti huyo na wagonjwa wengine waliolazwa kwenye taasisi hiyo wakihudumiwa vizuri.

Pia Waziri Mkuu amewajulia hali mabinti pacha walioungana Consolata na Maria Mwakikuti ambao nao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwapa pole wagonjwa hao na kuwaeleza kwamba Serikali inadhamira ya dhati kuhakikisha inaboresha huduma za afya na kwamba madaktari wataendelea kuwahudumia vizuri ili kuhakikishia afya zao zinaimarika na kurejea katika shughuli zao za kila siku

Kwa upande wake, Mwalimu Jumbe alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutenga muda wake na kwenda kumjulia hali. Aliwashukuru madaktari na wauguzi wa taasisi ya JKCI kwa huduma nzuri wanazompatia tangu alipofika hospitalini hapo.

Kwa upande wao Maria na Consolata walishukuru kwa msaada wa huduma za matibabu wanazozipata na kwa sasa wanaendelea vizuri. Pia walimshukuru Waziri Mkuu kwa kwenda kuwajulia hali na kumtakia kheri katika shughuli zake


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, FEBRUARI 10, 2018.
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images