Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

WATAKIWA KUWEKA MIKAKATI ENDELEVU KUBORESHA AFYA ZA WANAOWAHUDUMIA

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi wametakiwa kujiweka tayari katika kujadili changamoto na kuibua mikakati endelevu ili waweze kuboresha huduma za afya kwa watu wenye uhitaji, askari pamoja na familia zao.

Hayo yamesemwa leo asubuhi katika hoteli ya SG Resort iliyopo jijini hapa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili ya wakuu wa vituo tiba vya Polisi Tanzania pamoja na wafanyakazi na watumishi wa JSI kuhusiana na uboreshaji utoaji wa huduma za afya katika kukabiliana na jukumu la kupambana na uzuiaji wa maambukizi ya VVU na UKIMWI.

Alitoa wito kwa Madaktari, Wauguzi na watumishi wengine wanaofanya kazi katika Zahanati na vituo vya afya kuendelea kuwatambua wenye maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa kuwapima, kuwaanzishia dawa na kuhakikisha wote walioanza matibabu wanaendelea kutumia dawa kwa kipindi chote cha uhai wao.

Kamanda Mkumbo aliendelea kuwakumbusha washiriki wa mkutano huo kuendelea kuwahudumia wananchi kwa uadilifu na utunzaji mkubwa wa siri za wateja wanaopatiwa huduma za VCT/CTC ikiwa ni sehemu ya kiapo chao juu ya taaluma yao.

Naye Mganga mkuu wa Kikosi cha Afya cha Jeshi la Polisi nchini Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Msenga, alisema kwamba lengo la semina hiyo ambayo inawezeshwa na JSI/AIDS FREE ni kujitathmini namna ya utoaji huduma bora kwa askari, familia zao pamoja na wananchi wengine wanaotumia vituo hivyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akiwahutubia wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi kutoka maeneo mbalimbali nchini wakati wa ufunguzi wa semina iliyofanyika katika hoteli ya SG Resort iliyopo jijini Arusha.
Baadhi ya wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi kutoka katika vituo mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo ambayo ulifunguliwa na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo kwa niaba ya IGP.
Mgeni rasmi wa ufunguzi wa semina kuhusiana na VVU na UKIMWI kwa wataalamu wa vituo vya afya vya Polisi nchini Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa semina hiyo. Kulia kwake ni Mganga Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Dr. Charles Msenga na kushoto kwake (aliyevaa suti) ni Mkurugenzi wa AIDS FREE Dr. William Nyagwa.
Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha.



UTAFITI WA MATUMIZI,MAPATO KAYA BINAFSI KUTAMBUA VIASHIRIA VYA KIUCHUMI

MGODI BUZWAGI WAZINDUA MAKTABA SHULE YA SEKONDARI BUGISHA KAHAMA

$
0
0
Mgodi wa dhahabu wa Acacia Buzwagi umezindua maktaba iliyogharimu shilingi milioni 22.4 kwenye shule ya sekondari Bugisha iliyopo katika kata ya Mondo wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa lengo la kusaidia wanafunzi na walimu kuchangia katika kuboresha ubora wa elimu inayotolewa.

Maktaba hiyo imezinduliwa leo Alhamis Februari 8,2018 na Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na kuhudhuriwa pia na Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu.

Hii ni maktaba ya pili katika wilaya ya Kahama kuzinduliwa na mgodi huo ambapo mwaka 2017 mgodi wa Buzwagi ulianzisha maktaba ya jamii katika kata ya Kagongwa ili kutoa rasilimali za elimu ya aina mbalimbali kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati uzinduzi huo, Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu maktaba hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi kutoka jamii inayouzunguka mgodi wa Buzwagi.
Alisema kupitia mpango wa Acacia wa maendeleo ya jamii wameamua kushirikiana na shirika la kimataifa la Read International kuboresha jengo moja la shule hiyo na kuliwekea samani kwa ajili ya matumizi ya maktaba.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akikata utepe kuzindua rasmi jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha. Katikati ni Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu.Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akifuatiwa na diwani wa kata ya Mondo Kija Peja
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia vitabu katika maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu wakisoma vitabu ndani ya maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Muonekano wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha lililoboreshwa na mgodi wa Buzwagi kwa kushirikiana na Read International - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

MAGAZETI YA IJUMAA LEO FEBRUARY 9,2018

SIDO YATANGAZA VITA KWA WADAIWA SUGU

$
0
0
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam limetangaza vita kwa wale wadaiwa sugu kulipa madeni yao kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada. Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga wakati akizindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wateja wao.

 "Leo tunazindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wadaiwa sugu wote wa SIDO hatutakuwa na huruma juu ya hili maana hawa ndiyo wanarudisha maendeleo ya shirika nyuma, kuna waliokopa, walipanga kama haujalipa deni lako ujue tunakupa siku 14 tu baada ya hapo sheria itachukua mkondo wake," amesema Mkurugenzi Maganga. 

Meneja Macdonald Maganga amesema wadaiwa ni wale waliopewa maeneo maalumu ya viwanda kwa ajili ya kufanyia kazi zao na waliopatiwa huduma ya fedha kwa mkopo na kushindwa kurejesha kwa wakati. “Kuna ambao wamekaa miaka mingi au miezi mingi bila kurejesha fedha kwetu kama shirika inatuathiri kwa sababu hatuwezi kuwahudumia wengine,” amesema Maganga. Maganga amesema wanadai jumla ya sh. milioni 350 kutoka kwa wadaiwa zaidi ya 77. 
 Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akitoa uamuzi wa wao kuwaweka kampuni ya udalali ya Yono Auction kwa ajili ya kwenda kukamata wadaiwa sugu wote. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela akitoa tamko la siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni. 
Meneja wa SIDO mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akiongoza wafanyakazi na viongozi wa Yono kupita mlango kwa mlango wakati wakizundua kampeni ya kudai madeni "LIPA DENI LAKO SIDO, KUWA MZALENDO'. 

DUKA LA VIFAA VYA UJENZI LAFUNGULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMPUNI  ya Kimataifa ya Kohler ya bidhaa bora za ujenzi imefungua duka la kusambaza bidhaa  zake katika Kampuni ya ABC Emproria jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Rais wa Kampuni hiyo Kanda ya Bara ya Kusini Asia na EMEA, Salil Sadanandan amesema kampuni imeamua kuingia katika soko la Tanzania kutokana na kufanya utafiti na kubaini kuwa ni moja ya nchi katika ukanda wa Afrika Mashariki sekta ya ujenzi inakuwa kwa kasi.

“Kutokana na kasi ya kukua kwa sekta ya ujenzi nchini tumeona kuna umuhimu wa kusogeza huduma ya upatikanaji wa bidhaa za Kohler kwa urahisi wakala wetu wa ABC  Emporio ambayo ina uzoefu mkubwa wa kuuza na kufunga vifaa vya ujenzi , huu ni mwendelezo wa kupanua masoko yetu barani Afrika ambao tayari wana matawi katika nchi za Kenya na Uganda” Amesema Sadanandan .

Nae Rais wa Kampuni  ya ABC Emporio, Muhamed Hadani amesema kuwa wanajivunia kuwa mawakala wa kuuza bidhaa za Kohler pia ni fursa pekee kwa watanzania kupata bidhaa hizo kwa gharama nafuu
 Rais wa Kampuni ya Kohler Kanda ya Bara ya Kusini Asia na EMEA, Salil Sadanandan akizungumza na waandishi habari kuhusiana na ufunguaji wa duka la vifaa vya ujenzi leo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Kampuni  ya ABC Emporio, Muhamed Hadani akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na usambazaji wa bidhaa za Kohler leo jijini Dar es Salaam.
 Msemaji wa Kampuni ya ABC Emporio, Matha Majura akizungumza na wandishi wa habari  kuhusiana na kampuni huyo inavyofanya kazi hapa nchini.
Muonekano wa duka la vifaa vya ujenzi lililofunguliwa leo jijini Dar es Salaam.

ALIYEKUWA KAMISHINA MADINI KORTINI KWA TUHUMA ZA KUTUMIA MADARAKA VIBAYA

$
0
0
  Na Karama Kenyunko, Blogu ya Jamii.

Aliyekuwa Kaimu Kamishna wa Madini nchini, Ally Samaje amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu tuhuma za Matumizi mabaya ya madara.

Mwendesha Mashtaka wakili wa Serikali kutoka Takukuru, Leornad Swai amedai, mshtakiwa Samaje ambaye pia alikuwa Katibu wa Bodi ya umUshauri wa Madini, ametenda kosa la kwanza kati ya Aprili 9 na June 21, mwaka 2013.

Imedaiwa mbele ya Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa kuwa, mshtakiwa Samaje akiwa katika utendaji wa kazi zake alitumia madaraka yake vibaya kwa kushindwa kuitisha mkutano wa hiyo bodi na kupata ushauri wake kwa kuzingatia maombi ya leseni ya madini Namba HQ-P26114 kwa ajili ya (Gamestone and Associated minerals) yakiwamo madini ya Graphite na Marble katika eneo la Mererani, Wilaya ya Simanjiro Mkoa Wa Manyara.

Imedaiwa mahakamani hapo kuwa maombi hayo yaliwasilishwa na Kampuni ya Tanzanite one mining ltd na State mining Corporation.

 Kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha sheria ya madini no. 14 ya mwaka 2010  kwa lengo la kuipatia faida kampuni hizi kwa kupata eneo la madini ambalo ni kilometa 7.6.

Katika shtaka la pili, Swai alidai kuwa Aprili 16 mwaka 2013 mshtakiwa Samaje alitumia vibaya madaraka yake kwa kutoa maelekezo kwa Kamishna Msaidizi wa leseni na Haki za Madini John Nayopa kuandaa leseni kuchimba madini ya Gemstones ikiwamo Tanzabite,Graphite na Marble bila ya kuzingatia mfumo wa uendeshaji wa taarifa za madini wa Cadastie (MCIMS) wa Wizara ya Nishati na Madini wa eneo la kilometa 7.6 lililopo Mererani wilaya  Simanjiro.

Ilidaiwa kitendo hicho ni kinyume na kifungu cha 49(2)(b) cha sheria ya madini namba 14 ya 2010 na kusababisha kampuni hizo kupata faida ya leseni  za kuchimba madini.

Hata hivyo, mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na ameachiwa huru kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

Mahakama ilimtaka mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye anuani zinazojulikana watakaosaini bondi ya milioni 50.

Kesi imeahirishwa hadi Februari  28 mwaka huu,

WAHAMIAJI HARAMU 77 WAFIKISHWA KAHAKAMANI

$
0
0
Wahamiaji haramu 77 kutoka nchini Ethiopia wamefika leo katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, hata hivyo hawakuweza kusomewa mashtaka yoyote baada ya mkalimani kutotokea mahakamani hapo.

TAARIFA

WADAU MBALIMBALI WAKUTANA KUJADILI MADHARA YATAKONAYO NA NDOA ZA UTOTONI

$
0
0
 Mwanasheria  na Wakili wa Masuala ya haki za Watoto, Gebra Kambole akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Wadau  wanaopinga ndoa za utotoni katika mkutano Maalum ulioandaliwa na Tasisi ya Msichana Initiative  Dar es Salaam, katika Mkutano huo wadau wameweza kujadili na kupitia Rufaa iliyowekwa na Mwanasheria Mkuu juu ya kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama kuu kuwa Mtoto wa Miaka 15 awezi kuolewa.
 Afisa Mawasiliano wa , Eileen Mwalongo, akizungumza jambo kuhusiana kupinga ndoa za utotoni wakati wa kikao cha Wadau kujadili Rufaa ya Mwanasheria Mkuu dhidi ya Hukumu ya kesi ya kupinga ndoa kuanzia miaka 15.
 Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao cha Wadau kupinga Rufaa ya Mwanasheria Mkuu kupinga hukumu ya Mahakama kuu juu ya ndoa kuanzia miaka 15.
 Sehemu ya Wadau walioshiriki katika kikao cha Wadau kupinga Rufaa ya Mwanasheria Mkuu kupinga hukumu ya Mahakama kuu juu ya ndoa kuanzia miaka 15 wakimsikiliza Mwanasheria Gebra Kambole.

REGROW KICHOCHEO CHA KUFUNGUA UTALII KANDA YA KUSINI

$
0
0

Na Hamza Temba - Dodoma
..........................................................
Serikali imeanza utekelezaji wa mkakati wa kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini unaohusisha upanuzi wa maeneo ya kijeografia yenye vivutio pamoja na mazao ya utalii ili sekta hiyo ichangie zaidi kwenye pato la taifa na kuondoa umaskini katika jamii.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati akijibu hoja mbalimbali za wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma.

Alisema kwa upande wa mkakati wa kupanua jeografia ya vivutio vya utalii nchini Serikali itafungua utalii wa ukanda wa kusini kwa kuboresha vivutio na miundombinu ambapo tayari imesaini mkataba wa mkopo nafuu kutoka benki ya dunia wa milioni 150 za kimarekani sawa na zaidi ya Shilingi bilioni 340 za kitanzania kwa ajili ya mradi wa REGROW ambao utasimamia maliasili na kuendeleza utalii wa ukanda wa kusini.

Alisema kupitia mradi huo jumla ya viwanja vya ndege 15 vitaboreshwa ndani ya Pori la Akiba la Selous na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na uwanja wa ndege wa Nduli uliopo mjini Iringa. Maeneo mengine yatakayoboreshwa katika hatua ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huo ni Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa na Mikumi.

"Mradi huo utaboresha pia usafiri wa reli kwa kuimarisha kituo cha Matambwe ambacho ni kitovu cha utalii katika Pori la Akiba la Selous",. Alisema Dk. Kigwangalla.

Akizungumzia upanuzi wa mazao ya utalii, alisema sekta hiyo kwa muda mrefu imekuwa ikitegemea zaidi utalii wa wanyamapori huku ukiegemea zaidi katika ukanda wa kaskazini kwa zaidi ya asilimia 90.

Alisema kwa sasa Serikali itapanua wigo wa mazao hayo ya utalii ambapo mwezi Septemba kila mwaka utakuwa mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa Tanzania (Urithi Festival) kwa ajili kuimarisha utalii wa kiutamaduni na kuhamasisha utalii wa ndani.

Alisema Serikali kupitia Wizara yake itaimarisha pia utalii wa fukwe na utalii wa mikutano.Awali Dk. Kigwangalla alisema sekta ya Utalii ina mchango mkubwa katika uchumi wa taifa ambapo huchangia asilimia 17.6 ya pato la taifa, asilimia 25 ya mapato yote ya fedha za kigeni na asilimia 12 ya ajira zote nchini.

Alisema pamoja na mafanikio hayo sekta hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uvamizi kwenye maeneo ya hifadhi na kuegemea zaidi kwenye vivutio vya ukanda wa kaskazini huku vivutio vya kanda nyingine vikiwa havichangii ipasavyo kwenye pato la taifa.

Jeshi la Polisi nchini latakiwa kuziachia pikipiki ilizozishikiria mda mrefu

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi nchini kuziachia pikipiki ambazo wamezishikilia kwa mda mrefu na zina makosa madogo waziachie na wasikae nazo kwa mda mrefu mpaka zikawa vyuma chakavu.

Dk Mwigulu amesema yale yenye makosa makubwa kama uhalifu wa kivita, madawa ya kulevya, na wale wanaotelekeza wabaki nazo na wafanye utaratibu wa kuwapeleka mahakani au kuziteketeza na zenye makosa madogo wazitatua haraka na kuwarudishia na kuwapa elimu wamekosea wapi.

“Wapeni masomo wamekosea wapi walekezeni na waliowabishi waelekebisheni lakini tusirundike tukatengeza vyuma chakavu kwa hivi vitu ambavyo utatuzi wake tunawo, tutumie huu mkono wakutatua kwa yale ambayo yapo ndani ya mamlaka yetu” alisema Dk Mwigulu

Alisema kuwa ipo haja ya vijana sasa kufundishwa zaidi kuhusu sheria ya usalama barabarani ili kupunguza ajali ya pikipiki na mlundikano wa pikipiki katika vituo vya polisi nchini kwani kila napopita kita vituo vya polisi hukuta pikipiki ni nyingi na makosa yao ni madogomadogo.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba akikagua pikipiki ambazo zimeshikiliwakatika kituo cha polisi pangani. ameagiza polisi nchini kuziachia pikipiki ambazo wamezishikilia kwa mda mrefu na zina makosa madogo waziachie na wasikae nazo kwa mda mrefu mpaka zikawa vyuma chakavu.

Katibu Mkuu Mambo ya Nje akutana na Mwakilishi wa Aga Khan

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akizungumza na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Aga Khan, Bw. Amin Kurji alipomtembelea katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Februari 2018.
Mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Bw. Kurji yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano na shughuli za maendeleo ambazo zimekuwa zikifanywa na Shirika la Aga Khan nchini katika kuhudumia wananchi hususan katika sekta ya Afya na Elimu. 
Mazungumzo yakiendelea, kulia ni wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

JESHI LA POLISI MKOA WA RUVUMA LATOA ELIMU JUU YA USALAMA BARABARANI.

$
0
0
Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani mkoa wa RUVUMA, limeendesha kampeni ya zuia ajali barabarani katika shule ya msingi ZIMANIMOTO iliyopo katika manispaa ya SONGEA

KAMATI YA MAJI YAVUNJWA KWA UBADHIRIFU WA FEDHA

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameivunja Kamati ya maji ya kata ya Didia iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutokana na kufanya ubadhirifu kwenye mradi wa maji wa kisima kirefu. 

Kamati hiyo inadaiwa kutafuna pesa za mradi ulioanza kujengwa mwaka 2013/2014 na kukabidhiwa mwaka 2016 na kugharimu shilingi milioni 400.16 umeshindwa kuendelea kuhudumia wananchi mara baada ya kifaa kimoja kuharibika na kukosekana pesa za matengezo na kuufanya mradi kutaka kufa. 

Akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Didia jana Februari 8,2018 mkuu wa wilaya aliamua kuvunja kamati hiyo na kuagiza wajumbe wa kamati hiyo wakamatwe. “Kamati hii kuanzia sasa nimeivunja na ninaagiza jeshi la jadi Sungusungu watu hawa watafutwe wakamate na wapelekwe Polisi sababu ni wahujumu uchumi na kisha wapewe muda wa kizirudisha pesa zote walizozitafuna kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria,” alisema Matiro. 

Hata hivyo mara baada ya kuivunja kamati hiyo ya maji, alisimamia zoezi la wananchi kuchagua viongozi wengine sita wa mpito kupitia mkutano huo wa hadhara kwa kuchaguliwa na wananchi wakiongozwa na mwenyekiti wake Katunge Njile, huku akiagiza viongozi wote wa vitongoji kuitisha mikutano ya hadhara na kuchagua wajumbe wawili wawili ambao wataunda kamati ya maji ya kudumu. 

Pia aliagiza kila kaya kwenye kata hiyo ya Didia yenye wakazi 4112 wachange shilingi 3000, fedha ambazo zitasaidia kununua kifaa kwenye mradi huo wa maji chenye gharama ya shilingi milioni 3.7, ili uanze kufanya kazi na kuondoa adha ya wananchi kutumia maji machafu sambamba na kumtua ndoo kichwani mwanamke. 

Naye aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya maji Selemani Msabaha, alikiri kuwa walishindwa kuendesha mradi huo mara baada ya pesa kukosekana ambapo mpaka sasa kwenye akaunti kuna shilingi 129,000. Kwa mujibu wa mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo Sumbukeni Malela kamati hiyo ilikuwa ikikusanya hadi shilingi milioni 17 na walikuwa hawafanyi vikao na hakuna listi za manunuzi ya vifaa vinapoharibika na kwamba kiasi cha shilingi 984,600 hazijulikani zilipo. 
Mkuu wa wilaya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wananchi wa Kata ya Didia Shinyanga na kuivunja kamati ya maji kutokana na kufanya ubadhirifu wa fedha na kukwamisha mradi huo kutofanya kazi tena. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog 
Wananchi wa kata ya Didia wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. 
Aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati ya maji iliyovunjwa kata ya Didia Selemani Msabaha akizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro na wananchi na kukiri mradi huo wa maji Didia kuwa umeshidwa kuendelea kutoa huduma mara baada ya fedha za matengenezo Shilingi milioni 3.7 kukosekana 
Mkaguzi wa ndani wa halmashuri ya Shinyanga vijijini Sumbukeni Malela ,akieleza jinsi ubadhirifu wa fedha ulivyotumika kwenye mradi huo wa maji Didia.Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog 

BoT YAWAASA WAANDISHI KUTOA UCHAMBUZI WA KINA TAARIFA ZA FEDHA ZA MABENKI

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mtwara

SEMINA ya siku tano ya waandishi wa Habari za Uchumi, Biashara na Fedha iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania, Idara ya Uhussiano na Itifaki, imemalizika leo Februari 5, 2018 mkoani Mtwara.

Katika simian hiyo iliyofunguliwa mwanzoni mwa wiki na Naibu Gavana wa Benki Kuu anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC), Bw. Julian Raphael Banzi, waandishi hao wamejifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya mfumo mpya wa kuandaa Sera ya Fedha, (Financial Monetary Policy), mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia, mifuko ya dhamana kwa wajasiriamali na dhamana za serikali. 

Mambo mengine ambayo waandishi hao kutoka vyombo mbalimbali vikiwemo, Redio, Luninga, Magazeti na Blogs ni kanuni mpya za usimamizi wa bureaux de change, usimamizi wa mabenki na taasisi za fedha na dhamana kwa mikopo ya nyumba (Mortgage Finance). 
Kaimu Mkurugenzi wa BoT, Tawi la Mtwara, Bi. Leticia Rweyemamu, akitoa hotuba ya kufunga semina ya sikju tano ya waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha, kwenye makao makuu ya tawi hilo Mkoani Mtwara leo Ijumaa Februari 9, 2018.
Kaimu Meneja wa Idara ya Uhusiano na Itifaki, BoT, Bi. Vicky Msina, akizungumza wakati wa hafla ya ufungaji wa semina hiyo.
Dkt. Suleiman Missango, Meneja Msaidizi-Idara ya Utafiti, Kurugenzi ya Sera za Uchumi na Utafiti, BoT, akiwasilisha mada kuhusu Government securities (Government Date Securities) , mwishoni mwa semina hiyo leo Februari 9, 2018.
Baadhi ya washiriki wakifurahia hotuba ya mgeni rasmi.
Meneja Msaidizi, Dawati la Kutatua Malalamiko ya wateja wa mabenki na taasisi za fedha, Benki Kuu ya Tanzania, (BoT) Bw.Ganga Ben Mlipano, akitambulishwa kwa wana semina kabla ya kuwasilisha mada ya mafanikio na changamoto za dawati hilo.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji na wana semina mwishonin mwa semina hiyo.

MKUU WA GEREZA UKONGA ASTAAFU UTUMISHI WA JESHI

$
0
0
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kushoto), akikwagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake wakati wa hafla ya kumuaga akistaafu utumishi wa jeshi hilo, Hafla hiyo imefanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila , akipunga mkono wa kwaheri wakati wa hafla ya kumuaga akistaafu utumishi wa jeshi hilo. Hafla hiyo imefanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Gwaride la heshima likipita mbele ya Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila, wakati wa hafla ya kumuaga kamishna msaidizi huyo iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kulia),akipongezwa na maafisa wa jeshi hilo baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo katika hafla iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila, akipongezwa na mkewe Yunisi Mwaisabila (kulia), baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo Cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Steven Mwaisabila (kushoto) akipongezwa na mjukuu wake baada ya kustaafu utumishi wa jeshi hilo wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika leo katika Viwanja vya Chuo Cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

SHONZA: Umiliki wa Viwanja vya Michezo nchini umezingatia Sheria

$
0
0
Na Lorietha Laurence-Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kama zilivyo taasisi nyingine kimefuata taratibu za ujenzi na umiliki wa viwanja vya michezo kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni zilizopo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza leo Mkoani Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Lupa Victor Mwambalaswa, lililohoji kuhusu viwanja vya michezo vinavyomilikiwa na Chama hicho.

“Ni vizuri ikafahamika kwamba mpaka sasa viwanja hivyo vinaendelea kutumika na umma wa watanzania kwa shughuli mbalimbali za kimichezo, kijamii na kiserikali sawa kabisa na Mipango ya Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka 1995, Sura ya 4 (i)-(ii)”

“kwa hiyo kuhusu suala la uporaji wa viwanja hivyo, CCM hakijafanya uporaji wowote kwa kuwa kinamiliki viwanja hivyo kihalali kwa mujibu wa sheria zilizopo hivyo ushiriki wa wananchi wenye mapenzi mema katika ujenzi wa viwanja hivyo hauondoi uhalali wa Chama cha Mapinduzi kumiliki viwanja hivyo”amefafanua Shonza.

SERIKALI KULIPA MADAI YA MALIMBIKIZO MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA KUANZIA KESHO

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akizungumza na waandishi wa Habari Kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari-Bunge mjini Dodoma (hawapo pichani) kuhusu hatua ya Serikali ya kuanza kulipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa Umma, kiasi cha shilingi bilioni 43.39 kuanzia Februari 10, 2018. Kushoto ni Kamishna Msaidizi-Bajeti, Bw. Emmanuel Tutuba na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (Utawala) Bi. Susan Mkapa (Picha-Wizara ya Fedha na Mipango)
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akizungumza na waandishi wa Habari Kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari-Bunge mjini Dodoma (hawapo pichani) kuhusu hatua ya Serikali ya kuanza kulipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa Umma, kiasi cha shilingi bilioni 43.39 kuanzia Februari 10, 2018. Kushoto ni Kamishna Msaidizi-Bajeti, Bw. Emmanuel Tutuba na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (Utawala) Bi. Susan Mkapa, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango wa Wizara hiyo Bw. Richard Mkumbo (Picha-Wizara ya Fedha na Mipango)
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akizungumza na waandishi wa Habari Kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari-Bunge mjini Dodoma (Hawapo Pichani)kuhusu hatua ya Serikali ya kuanza kulipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa Umma, kiasi cha shilingi bilioni 43.39 kuanzia Februari 10, 2018. Kushoto ni Kamishna Msaidizi-Bajeti, Bw. Emmanuel Tutuba na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (Utawala) Bi. Susan Mkapa, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango wa Wizara hiyo, Bw. Richard Mkumbo (Picha-Wizara ya Fedha na Mipango)

TAARIFA YA WAZIRI WA FEDHA KUHUSU MALIMBIKIZO YA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI


Ndugu Wawakilishi wa vyombo vya habari, nimewaiteni leo hii ili niwape taarifa fupi kuhusu malipo ya madai ya malimbikizo ya mishahara kwa Watumimishi wa umma waliokuwa na madai ili muweze kuufikishia umma wa Watanzania.
Serikali kupitia mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara (Human Capital Management Information System – HCMIS) kufikia tarehe 01 Julai 2017 ilikuwa na madai ya malimbikizo ya mishahara yenye jumla ya shilingi 127,605,128,872.81 kwa watumishi 82,111 Wakiwemo walimu 53,925 waliokuwa wanadai shilingi 53,940,514,677.23  sawa na asilimia 42.27 ya madai yote,   na wasiokuwa walimu 28,186 waliokuwa wanadai jumla ya shilingi 73,664,614,195.58 sawa na asilimia 57.73 ya madai yote. Madai haya yalikuwa ya muda mrefu mengine yakiwa ya kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2017
Madai haya yalijumuisha mishahara isiyolipwa, tofauti ya mishahara kutokana na kukaimu na nyongeza za mishahara zilizotokana na kupandishwa vyeo na kuchelewa kurekebishiwa mishahara.
MATOKEO YA UHAKIKI WA MADAI YA SHILINGI BILIONI 127,605,128,872.81 KWA WATUMISHI 82,111
  1. Madai ya watumishi 27,389 kati 82,111 yenye jumla ya shilingi  43,393,976,807.23 ikiwa ni asilimia 34 ya madai yote ya shilingi bilioni 127,605,128,872.81  yaliyohakikiwa yameonekana ni sahihi na yanastahili kulipwa bila marekebisho.
  1. Madai yanayostahili kulipwa yanajumuisha shilingi bilioni 16.25 kwa walimu 15,919 na shilingi bilioni 27.15 kwa watumishi wasiokuwa walimu  11,470
  1. Madai yote yaliyoonekana kuwa sahihi ya shilingi bilioni 43.39 yatalipwa pamoja na mshahara wa mwezi Februari 2018 kwa mkupuo mmoja. Malipo ya Madai haya ambayo mengine yana zaidi ya miaka kumi majina ya walipwaji wote yatatangazwa kwenye magazeti kuanzia kesho tarehe 10 Februari, 2018.
Kwa matokeo hayo ya uhakiki, mazoezi yaliyofanyika likiwemo  zoezi la kuwaondoa kwenye Mfumo wa malipo ya mshahara (“payroll”) watumishi hewa, vyeti feki na wasio kuwa na sifa na  uhakiki wa madai ya malimbikizo ya mishahara uliofanyika limeweza kuokoa jumla ya shilingi bilioni 84.22 ambazo ni sawa na asilimia 66 ya madai yote ya malimbikizo ya awali ya shilingi bilioni 127.61 yaliyokuwa kwenye mfumo ambazo bila zoezi  la uhakiki kufanyika zingelipwa wakati zilikuwa hazistahili kulipwa.
Serikali itaendelea kulipa madai ya watumishi kadiri yanavyojitokeza ili kuondokana na malimbikizo ya aina hii ambayo yanaweza kuisababishia Serikali hasara kwa kulipa madai yasiyostahili.

SERIKALI YAFANIKIWA KUREJESHA MALI ZA NCU, SHIRECU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imefanikiwa kurejesha mali tisa kati ya 10 za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU) ambazo zilichukuliwa kinyume cha taratibu na kuagiza watuhumiwa wachukuliwe hatua za kisheria.

Amesema mali moja iliyobakia bado inafanyiwa uchunguzi na mali mbili za Chama Kikuu cha Ushirika cha Shinyanga (SHIRECU) nazo pia zimepatikana lakini bado ziko kwenye hatua ya makabidhiano.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Februari 9, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Waziri Mkuu amezitaja mali za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU) zilizorejeshwa kuwa jengo la Nyanza Cooperative Union (1984) Ltd. maarufu kwa jina la “Transport House” au KAUMA House, lililopo katika kiwanja namba 242, Kitalu T, Mtaa wa Stesheni; kiwanda cha kusindika mafuta cha New Era Oil Mill, kilichopo katika eneo la Igogo; na jengo na viwanja vya Ashock Industries vilivyopo eneo la viwanda Igogo.

Nyingine ni majengo ya kilichokuwa kiwanda cha mkonge na dengu kilichopo eneo la Igogo kwenye kiwanja namba 41 na 79; jengo lililopo katika kiwanja kilichopo Isamilo namba 80, kitalu “D”; jengo lililopo katika kiwanja kilichopo Isamilo namba 110, kitalu “D” na ghala moja katika kiwanja namba 104, kitalu “A” kilichopo eneo la Igogo.

“Mali nyingine zilizorejeshwa ni jengo moja lililopo mjini Geita katika kiwanja namba 8 Kitalu “K”; jengo moja lililopo mjini Geita, katika kiwanja namba 24, Kitalu “K” na jengo lililopo Isamilo katika kiwanja namba 89 Kitalu “D”,” amesema Waziri Mkuu.

Kwa upande wa mali za SHIRECU, Waziri Mkuu amezitaja mali zilizopo kwenye hatua ya makabidhiano kuwa ni ghala lililopo Kurasini, Dar es Salaam na nyumba ya ghorofa tatu iliyopo kiwanja namba 1001 “BB” Ilala, jijini Dar es Salaam.

“Katika kusimamia misingi ya utawala bora na uwajibikaji wa watendaji wa vyama vya ushirika, Serikali inaendelea kufanya uchunguzi maalum kuhusu mikataba mibovu ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU), Chama Kikuu cha Ushirika cha Shinyanga (SHIRECU), Chama Kikuu cha Ushirika cha Kagera (KCU) na Chama Kikuu cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU). Vilevile, tunachunguza kushikiliwa kwa mali za ushirika bila kufuata utaratibu,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kuviamsha vyama vya ushirika vya msingi na vyama vikuu vilivyosinzia katika mikoa yote ili kujenga ushirika imara na kwamba juhudi na hatua hizo zinazochukuliwa na Serikali, zinalenga kuongeza imani, hamasa na uzalishaji wa mazao na kusimamia masoko yake, na hivyo, kuinua kipato cha wakulima sambamba na kuwapatia fursa ya kujiajiri wenyewe katika sekta ya kilimo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisoma hotuba ya kuahirisha bunge mjini Dodoma Februari 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Viewing all 109996 articles
Browse latest View live


Latest Images