Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

Awamu ya pili Zabuni mradi wa Ujenzi Bwawa la Kuzalisha Umeme teigler's Gorge zafunguliwa leo

$
0
0
 Na Greyson Mwase, Dar es Salaam.

Zabuni kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme wa Megawati 2100 la Steigler's Gorge katika Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji zimefunguliwa  leo tarehe 02 Februari, 2018.



Akizungumza wakati wa ufunguzi wa zabuni hizo kwenye Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Manunuzi kutoka Wizara ya Nishati, Amon MacAchayo amesema zabuni hizo ni za Awamu ya Pili kutokana na kukosekana kwa mshindi katika Awamu ya Kwanza iliyotangazwa mapema mwaka jana.



Alisema kuwa, katika awamu ya kwanza jumla ya kampuni 81 zilinunua nyaraka za zabuni ambapo nakala moja ilikuwa inauzwa kwa shilingi 200,000 lakini ni kampuni nne tu zilifanikiwa kurejesha maombi na kuongeza kuwa kampuni zote nne hazikuwa na  vigezo vinavyohitajika hali iliyopelekea kutangazwa upya kwa zabuni tarehe 19 Desemba, 2017 katika vyombo vya habari  vya ndani na nje ya nchi.



MacAchayo aliongeza kuwa, katika awamu ya pili kampuni 17 zilijitokeza katika ununuzi wa nyaraka kwa gharama ya shilingi 500,000 kwa kila moja ambapo mpaka siku zinafunguliwa ni kampuni tano tu zimerejesha nyaraka zenye maombi ya zabuni.



Alisema hatua inayofanyika kwa sasa ni ufanyaji wa tathmini ya zabuni hizo na kusisitiza kuwa mara baada ya kukamilika kwa tathmini ya zabuni hizo waombaji wote watajulishwa mshindi na baada ya hapo zitafuata taratibu za mazungumzo, barua na kuandaa mkataba kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi mara moja.Aliwataka kampuni zilizowasilisha maombi kuwa watulivu wakati zoezi la tathmini likiendelea.
 Mkurugenzi wa Idara ya Manunuzi kutoka Wizara ya Nishati, Amon MacAchayo (mbele) akizungumza na wawakilishi wa kampuni mbalimbali zilizoomba zabuni kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme katika Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji kwenye ofisi za Wizara ya Nishati jijini Dar es Salaam tarehe 02 Februari, 2018

 Mtaalam wa Manunuzi kutoka Wizara ya Nishati, Jackson William (kulia) akieleza jambo kwenye ufunguzi huo. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Manunuzi kutoka Wizara ya Nishati, Amon MacAchayo na aliyekaa kushoto ni mwakilishi wa kampuni zilizoomba zabuni,  Khaled Makkawy kutoka kampuni ya  The  Arab Contractors

 Sehemu ya wajumbe wakifuatilia zoezi la ufunguaji wa zabuni kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme katika Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji katika kikao hicho.

Wataalam kutoka Idara ya Manunuzi, Wizara ya Nishati wakifungua nyaraka mbalimbali za zabuni katika kikao hicho.


DINI YA MAREHEMU, KINGUNGE KUFAHAMIKA SIKU YA MAZISHI YAKE

UGENI MAHAKAMA YA JUU NCHINI GUATEMALA WAKUTANA NA JAJI MKUU WA TANZANIA

$
0
0
Na Mary Gwera

Katika mwendelezo wa Utekelezaji wa Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (5) (2015/2016-2019/2020), Mahakama ya Tanzania inaendelea na jitihada za kupata uzoefu na ujuzi kutoka katika Mahakama mbalimbali duniani zilizopiga hatua katika maboresho ya huduma ya utoaji haki kwa wananchi.

Haya yamejidhihirisha kufuatia ugeni wa Maafisa wa Mahakama waliowasili kutoka nchini Guatemala kwa mualiko wa Mahakama ya Tanzania kushiriki katika Hafla ya Siku ya Sheria nchini, iliyofanyika Februari 01, 2018 vilevile Mahakama ya Tanzania kupata maoni na ushauri zaidi wa jinsi ya kuendelea kuiboresha Mahakama nchini kwa manufaa ya wananchi ambao ndio walengwa Wakuu.

Akiwatambulisha wageni hao kwa Mhe. Jaji Mkuu wa Tanzania, Februari 1 katika Ofisi ya Mhe. Jaji Mkuu, Mahakama ya Rufani Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga alisema kuwa takribani miaka mitatu sasa baadhi ya Maafisa wa Mahakama nchini walifanya ziara nchini Guatemala kwa lengo la kujifunza ni kwa namna gani Mahakama nchini Guatemala imefanikiwa katika utoaji wa huduma zake.

“Mhe. Jaji Mkuu, tulichojifunza na tukaona ni vyema kuiga kutoka Guatemala ni pamoja na huduma ya Mahakama inayotembea ‘mobile court’, ufanyaji kazi wa Mahakama kwa masaa 24, kuweka mbele matumizi ya teknolojia katika shughuli zake  n.k, hivyo tumeona ni vyema pia kwa Mahakama nchini kupata utaalamu/uzoefu kutoka kwa wenzetu jinsi ya kuweza kutekeleza haya,” alisema Bw. Kattanga.
  Jaji Mkuu wa Tanzania (pichani) akiwa katika mazungumzo na Wageni hao (hawapo pichani), katika mazungumzo yao Mhe. Jaji Mkuu amefurahishwa na hatua iliyofikiwa na Mahakama nchini Guatemala.
 Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akiongea jambo na Wageni hao, Mhe. Wambali aliwaelezea Wageni hao juu ya Mfumo wa Mahakama nchini.
  Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (aliyeketi mbele) akiwa pamoja na baadhi ya Wahe. Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Jaji Kiongozi, Mtendaji Mkuu na Ugeni kutoka Mahakama nchini Guatemala pindi Wageni hao walipomtembelea Mhe. Jaji Mkuu ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Jaji Mkuu aliyemaliza muda wake wa Mahakama nchini Guatemala, Mhe. Osvaldo Mendez akizungumza jambo.
 Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia, Bw. Waleed Malik akiongea jambo katika kikao hicho.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MWANANCHI MWENYE ULEMAVU YUSUF ABDULRAHMAN NDEMANGA AKABIDHIWA BAJAJI ALIYOAHIDIWA NA RAIS MAGUFULI

$
0
0
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Bw. Gerson Msigwa wakimwongoza mlemavu wa maungo Bw. Yusuf Abdulrahman Ndemanga kwenye Bajaji ambayo aliahidiwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli walipokutana wakati wanavuka kwenye pantoni ya MV Kigamboni Agosti 25, mwaka jana, kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa Februari 2, 2018
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimkabidhi mlemavu wa maungo Bw. Yusuf Abdulrahman Ndemanga Bajaji ambayo aliahidiwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli walipokutana wakati wanavuka kwenye pantoni ya MV Kigamboni Agosti 25, mwaka jana, kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa Februari 2, 2018. Kulia ni ke w Bw. Ndemanga, Bi. Hawa Mohamed.
mlemavu wa maungo Bw. Yusuf Abdulrahman Ndemanga na mkewe Hawa Mohamed Wakiondoka na Bajaji ambayo aliahidiwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli walipokutana wakati wanavuka kwenye pantoni ya MV Kigamboni Agosti 25, mwaka jana, kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa Februari 2, 2018. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Yusuph Abdulrahman Ndemanga ambaye ni mlemavu wakati alipomkuta ndani ya jengo la abiria lililopo upande wa Magogoni kabla ya kuvuka na Pantoni kuelekea katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam Agosti 25, mwaka jana. Bw. Ndemanga alimuomba Rais msada wa kupatiwa Bajaji ili ajimudu kiusafiri na kiuchumi.

Picha na IKULU

UPDATES ZA MSIBA WA MAREHEMU MZEE NGOMBALE MWIRU - KUZIKWA JUMATATU MAKABURI YA KINONDONI, DAR ES SALAAM

TUSIIME YATESA TENA KIDATO CHA NNE

$
0
0
Shule ya Tusiime imeendelea kufanya vizuri katika matokeo ya kitaifa ya kidato cha nne kwa kufaulisha asilimia 100 ya watahiniwa wake wote 303.

Kwenye matokeo yaliyotangazwa jana na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), shule hiyo imeendelea kufaulisha wanafunzi wake wote kwa ufaulu wa juu huku ikiwa na idadi kubwa ya wanafunzi kuliko shule zote 100 bora kitaifa.Shule hiyo ilikuwa na wanafunzi 303 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, kati ya hao, wanafunzi 59 wamepata daraja la kwanza, wanafunzi 161 daraja la pili na wanafunzi 62 daraja la tatu na 21 tu ndio wamepata daraja la nne.

Mkuu wa shule ya sekondari Tusiime, Emil Rugambwa, alifurahia sana matokeo hayo akisema ni mafanikio makubwa ikizingatiwa kuwa shule hiyo ilikuwa na idadi kubwa ya watahiniwa ambayo ni zaidi ya mara tatu ya watahiniwa wa baadhi ya shule zilizoingia kumi bora.

“Kwetu haya ni mafanikio makubwa sana kwani kufaulisha wanafunzi 212 kwa daraja la kwanza na la pili si jambo jepesi ni la kupongeza, nawapongeza walimu wangu na uongozi wa shule kwa matokeo haya mazuri, sisi tulikuwa na wanafunzi 303 na wamefaulu vizuri “ alisema Rugambwa.

“Shule yetu siyo ya vipaji maalum hivyo inachukua wanafunzi wenye uwezo wa kawaida sana kitaaluma na kuwajengea mazingira wezeshi ya kila mmoja kutimiza ndoto yake na mwisho wake wanafaulu mitihani yao ya kitaifa,” alisema

Naye Mkurugenzi wa shule hizo, Albert Katagira, alisema matokeo hayo mazuri yanatokana na dhamira waliyonayo kama taasisi kuhakikisha vijana wa Tanzania wanapata elimu bora katika mazingira yaliyo safi na salama.

“Napenda kuwathibitishia wazazi na wadau wote wa elimu kuwa shule za Tusiime zitaendelea kutoa elimu bora hapa nchini kama sehemu ya mchango wake kwa jamii ya watanzania kuandaa rasilimali watu wenye maarifa, ujuzi na weledi kwa manufaa yao, familia zao na taifa kwa ujumla,” alisema.

Alisema katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, shule hizo zimeweka mikakati mizuri iliyohakikisha kwamba kila mwanafunzi aliyejiunga na shule hizo anafaulu mitihani yake ya kitaifa.
Mkuu wa shule ya Tusiime, Emil Rugambwa, akimkabidhi zawadi ya kitabu mwanafunzi wa shule hiyo, Godson Ezekiel aliyepata daraja la 1.8 kwenye matokeo ya kidato cha nne. Wanafunzi 59 wamepata daraja la kwanza, wanafunzi 161 daraja la pili na wanafunzi 62 daraja la tatu na 21 tu ndio wamepata daraja la nne.
Mwanafunzi Godson Ezekiel wa shule ya Tusiime aliyepata daraja la kwanza 1.8 kwenye matokeo ya kidato cha nne akiwa na wenzake shuleni hapo mara baada ya kuzawadiwa kitabu na Mkuu wa shule hiyo. Emil Rugambwa. Wanafunzi 59 wa shule hiyo walipata daraja la kwanza, wanafunzi 161 daraja la pili na wanafunzi 62 daraja la tatu na 21 tu ndio wamepata daraja la nne
Mratibu wa kidato cha nne shule ya Tusiime, Mitala Innocent akiwasomea wanafunzi wa shule hiyo matokeo ya kidato cha nne shuleni hapo ambapo wanafunzi wa shule hiyo 59 wamepata daraja la kwanza, wanafunzi 161 daraja la pili na wanafunzi 62 daraja la tatu na 21 tu ndio wamepata daraja la nne.

MAKAMU WA RAIS AWAPA POLE FAMILIA YA RUBANI WA SERIKALI KAPTENI BOMANI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amehudhuria msiba wa Rubani wa Ndege za Serikali, Marehemu Kapteni Dominic Bomani aliyefariki jana kwa ajali ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume .
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha kumbukumbu cha maombelezo ya Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa pole Rosemary Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 akamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rosemary Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani, wengine pichani ni mtoto wa marehemu Joanitha Bomani (kulia) na Dada wa marehemu Stella Bomani(kushoto) wakati alipoenda kuwapa pole nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

AZAM FC YAANZA TAMBO KUELEKEA MCHEZO DHIDI YA NDANDA

$
0
0
Na Agness Francis, Globu ya Jamii 
MABINGWA wa Afrika Mashariki na Kati Azam Fc  wanatarajia kushuka dimbani kesho kuumana na  Wanakuchere NdandaFc katika mchezo wao wa marudiao raundi ya pili, Ligi kuu Tanzania Bara utakaochezwa Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari AzamFc  Jaffary Iddy Maganga, amesema katika mtanange huo utakaoanza saa 10 jioni, kikosi chake kitawakosa wachezaji wake mahiri 5.

Amewataja wachezaji hao ni Himidi Mau, Waziri Junior, Joseph Mahundi, Joseph Kimwaga na Aboubakar Salum  maarufu  kama (Sure Boy) anayetumikia adhabu ya kadi Nyekundu aliyoipata wakati wa mechi dhidi ya Mabingwa watetezi Tanzania Bara  Yanga SC. 

"Licha ya kuwakosa wachezaji hao, tuko vizuri na kikosi chetu ni kipana chenye uwezo mkubwa, tutahakikisha tunapambana vikali dhidi ya Wanakuchere ili tunachukue pointi 3,"amesema Jaffary Maganga. 

Kwa upande wake Kocha Mkuu wa Azam Fc  Aristica Cioaba amesema kuwa wamejiandaa vema kwa mchezo huo kiakili, kimwili huku akitamba kuwa kikosi chake kiko kwenye mazingira mazuri.
Afisa Habari AzamFc,  Jaffary Iddy Maganga akizungumza na waandishi wa habari katika kuelekea   Mtanange  wa patashika nguo kuchanika pale Uwanja  wa Azam Complex Chamazi wakiwa wenyeji wa NdandaFc  katika kuuchapa mchezo  wao wa Marudiao raundi ya 2 Ligi kuu Tanzania Bara.

BALOZI MWAPACHU AMLILIA KINGUNGE KWA UJUMBE MZITO

$
0
0
Na Balozi Juma Mwapachu

BALOZI Juma Mwapachu ameamua kuandika tanzia ambayo ameamua kumuelezea mwanasia mkongwe na maarufu nchini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ambaye amefariki dunia leo.

Amemuelezea kwa kirefu ambapo anaanza kwa kusema "LEO alfajiri nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha ndugu yetu Kingunge Ngombale Mwiru. 

Kifo chake ni pigo kubwa kwa familia yake ambayo ni wiki chache tu tarehe 4 Januari, kilifiwa na mama yao, Peras Ngombale Mwiru, mke wa Ngombale Mwiru. 

Tanzania nzima bila kujali misimamo ya siasa haina budi kuwa na majonzi mazito kwa kuondokewa na Comrade Ngombale Mwiru. Alikuwa shujaa wa siasa tangu TANU hadi kifo chake. 

Nilimfahamu kwa karibu nilipochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TANU Youth League, Chuo Kikuu, Dar es Salaam kwa kipindi 1967/68. Yeye alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa TANU Youth League, Makao Makuu. 

Joseph Nyerere alikuwa Katibu Mkuu na Moses Nnauye alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi. Nilibahatika nami kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya  TANU Youth League. 

Tangu kipindi hicho Ngombale ananiona Comrade. Hata siku ile ya sala ya kumuaga mama Peras pale St Peters Church aliponiona akitoa smile kubwa alinipa mkono akiniita 'Comrade '. 

Mwaka 1991 Ngombale alichaguliwa na CCM kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kupendekeza Sera na Mwelekeo wa Chama na nchi katika miaka ya 90.

Mimi, Iddi Simba na Reginald Mengi tuliteuliwa kuwa wanakamati. Report yetu iliyokubaliwa kwa kishindo na Mkutano Mkuu wa CCM hapo 1992 baada ya kuwasilishwa na Ngombale kwa fasaha kubwa ndiyo iliyojenga misingi ya mageuzi  ya uchumi nchini.

Wakati wa kazi hiyo Ngombale akawa karibu sana nami akitambua kwamba nilikuwa pia mjumbe wa Tume ya Nyalali kuhusu Chama Kimoja au tuingie kwenye Vyama Vingi. 

Comrade Ngombale alikuwa rafiki wa karibu sana wa Professor Ahmed Mohiddin, Mkenya aliyependwa sana na Mwalimu Nyerere kutokana na maandiko yake kuhusu ujamaa. 

Mohiddin ana undugu na familia ya mke wangu. Sote tuliyokuwa karibu ya Ngombale tulimuita Susilov kutokana na kuwa 'ideologue' wa TANU na CCM. Susilov alikuwa ideologue wa Soviet Union Communist Party. 

Tanzania imempoteza jabari wa siasa. Kwangu nimempoteza Mwalimu na rafiki . Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi.  

Amin.
Balozi Juma Mwapachu

MATOKEO YA LIGI DARAJA LA KWANZA LEO

$
0
0

FDL KUNDI B

Mawenzi-0 Vs Coast-2

Mufindi-1 Vs Polisi Tz-2

Mbeya Kwanza-3 Vs Polisi Dar-1

JKT Mlale-0 Vs KMC-1

MSIMAMO
1) KMC-28
2) Coast-26
3) Jkt Mlale-25
4) Polisi Tz-24
5) Mbeya Kwanza-22
6) Mufindi-13
7) Mawenzi-8
8) Polisi Dar-5

KMC ya Dar es Salaam na Coast Union ya Mjini Tanga zimepanda ligi kuu zikiungana na JKT Tanzania.

POLISI DAR imeshuka rasmi ligi daraja la kwanza.

Shilingi milioni 208 zanufaisha kaya maskini TASAF Kishapu

$
0
0
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi.
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imetoa sh. milioni 208.5 kwa ajili ya kuwezesha kaya maskini katika kipindi cha Januari hadi Februari.
Mratibu wa TASAF wilaya hiyo, Sospeter Nyamuhanga amebainisha hayo jana ambapo amesema fedha hizo zimetolewa kwa ajili ya kaya 5959 katika vijiji 78 vilivyopo wilaya humo.Alisema kuwa zoezi hilo limeendelea kupata mafanikio kutokana na walengwa wengi kufanyia kazi elimu wanayopewa kuhusu matumizi sahihi ya fedha hizo wanazowezeshwa.
Nyamuhanga aliongeza kuwa kutokana na ufuatiliaji unaofanyika nyakati tofauti baadhi ya kaya zimeonesha mabadiliko kimaisha ambapo zimetumia fedha hizo kuboresha maisha yao kwa kufanya shughuli mbalimbali za kujipatia kipato.
Alifafanua kuwa katika kaya hizo imebainika kuwa wanufaikaji wameweza kununua mifugo ikiwemo mbuzi, kondoo  na kuku huku wengine wakifanya biashara ndogondogo.Aidha, alisema baadhi ya walengwa tayari wamebadilisha aina za makazi yao kutoka nyumba za tembe na nyasi za awali na kuanza kujenga nyumba za kisasa za bati hali inayoleta matumaini katika miradi kama hii.
“Lengo la mpango wa TASAF siku zote ni kuziwezesha kaya maskini kujikwamua kiuchumi na ndiyo maana mara kwa mara katika mazoezi haya tunatoa elimu ili kuwaelekeza namna bora kutumia fedha wanazowezeshwa,” alisema.
 Zoezi la uwezeshaji Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) likiendelea katika kijiji cha Mwigumbi kata ya Mondo ambapo mmoja wa walengwa akiwawezeshwa ruzuku.
 Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Sospeter Nyamuhanga (wa pili kulia waliosimama) akipata maelezo kuhusu zoezi hilo alipofika kufanya ufuatiliaji kijiji cha Wela kata ya Uchunga.
 Sehemu ya walengwa wa TASAF wakiwa katika zoezi la uwezeshaji kwenye kijiji cha Mwigumbi kata ya Mondo.
Zoezi likiendelea katika kijiji cha kijiji cha Wela kata ya Uchunga.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MHAGAMA: MUSWADA SHERIA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII KUNUFAISHA WATUMISHI WA UMMA

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema kupitishwa kwa muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii utasaidia kuwanufaisha watumishi wa umma kwa kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati na wenye tija.

Amebainisha hayo wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) walipokutana Mjini Dodoma katika warsha ya siku tano kuanzia Januari 29 hadi Februari 02, 2018 kujadili masuala ya wafanyakazi nchini.

Waziri Mhagama alieleza kuwa, kupitiswa kwa muswada ni moja ya utekelezaji wa takwa la Ibara ya 11 kifungu kidogo cha kwanza cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulipoona umuhimu wa kuweka mifumo ya hifadhi ili Watanzania wapate manufaa hasa siku za uzeeni.

“Maamuzi ya kuwa na Muswada huu umezingatia taratibu zote za kisheria ikiwemo Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Sera ya Hifadhi ya Jamii, Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani unaoongoza katika maswala ya Hifadhi ya Jamii”.Alisisitiza Mhagama.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Rayal Village Dodoma Februari 01, 2018.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Dodoma.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Erick Shitindi akionesha ishara ya umoja na mshikamano wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) uliofanyika Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) wakifuatilia ujumbe kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) aliowasilisha katika mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) Bw. Suleiman Kikingo akichangia hoja wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la chama hicho uliofanyika Ukumbi wa Royal Village Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Baraza Kuu la Taifa uliofanyika Dodoma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YAFUTA TOZO ZAIDI YA 80,ADA 139 KATIKA MAZAO YA KILIMO

TRA YAZIFUNGIA HOTEL TATU IKIWEMO NAFF HOTEL NA KITUO CHA MAFUTA MKOANI MTWARA

$
0
0
Mamlaka ya mapato mkoani Mtwara (TRA) imezifungia hotel tatu mkoani humo pamoja na kituo cha kuuza mafuta kwa kushindwa kulipa kodi ya malimbukizo ya madeni.

Hotel zilizofungiwa ni Naff Beach, Naf blue, BNN pamoja na kituo cha Mnarani Petrol Station ambao kwa pamoja wanadaiwa zaidi ya Shilingi bilioni moja ,ambazo ni malimbukizo ya madeni ya nyuma kwa kipindi cha miaka mitatu.

Afisa mwandamizi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Mtwara, Flavian Byabato amesema zoezi hilo ni endelevu kwa mkoa mzima.

“Ni madeni ambayo yametokana na ukaguzi kwa kipindi cha miaka mitatu nyuma,kikubwa walipe kodi,tunafungia kwa mambo mbalimbali kama malimbikizo ya madeni ya muda mrefu,matumizi sahihi ya mashine za EFD katika kutoa na kudai risiti sahihi inayoakisi gharama halisi ya malipo na kutii sheria za kodi kama kutunza kumbukumbu,”amesema Byabato

Byabato amesema endapo wadaiwa watashindwa kulipa madeni yao watachukua hatua nyigine kama kukamata mali au kuwapeleka mahakamani,kama hawatajitokeza kuomba na kuahidi ni lini watalipa madeni kwani hakuna aliyejitokeza kufanya hivyo.

Aidha amesema pia yapo maduka madogo ambayo yamefungiwa na kwa sasa wako wilayani Masasi wanaendelea na ukaguzi.

Pichani hoteli ya Naff Beach ikiwa imezungushiwa utepe na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

RC MTAKA AHIDIWA USHIRIKIANO NA BALOZI WA IRELAND,INDONESI NCHINI TANZANIA

$
0
0
Na Mathias Canal

Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock amemuahidi Mkuu wa Mkoa wa simiyu Mhe Antony Mtaka kuendeleza ushirikiano na Mkoa wa Simiyu ili kuboresha sekta ya Afya kupitia Irish Aid.

Balozi huyo ameyasema hayo wakati wa mazungumzo ya pamoja na Mhe Mtaka ambapo tayari kwa pamoja wamekubaliana kuanza kutekelezwa wa kusudio hilo tarehe 6 Februari 2018 kwa kuanza na timu ya wataalamu kufika Mkoani humo ili kuanza haraka shughuli hiyo.

Balozi H.E Ambassador Paul Sherlock amemuahidi Mhe Mtaka kuwa tayari nchi yake ya Ireland imekusudia kwa dhati kushirikiana vyema na Mkoa huo huku akisisitiza kuendelea kushirikiana zaidi pia katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo kwenye sekta ya Mifugo, Kilimo na Utalii.

Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock ametoa kauli hiyo ya kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka za kutoka kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo uwekezaji wakati alipokutana na kufanya mazungumzo leo 2 Februari 2018 katika.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kushoto) akimkabidhi Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Prof Ratlan Pardede Mwongozo wa uwekezaji Mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kulia) akifurahia jambo na Muwakilishi Mkaazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi Jacqurline Mahon.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kulia) akisalimiana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock ofisini kwake Jijini Dar es salaam.



MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA GODWIN KUNAMBI AKABIDHI VITAMBULISHO KWA MMACHINGA 140

$
0
0
Na Ramadhani Juma-Ofisi ya Mkurugenzi

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi amekabidhi vitambulisho kwa Wafanyabiashara ndogo maarufu kama m Machinga wanaofanya shughuli zao katika soko la jioni ili waweze kufahamiana wakati wa biashara zao na hata kusaidia kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama.

Wafanyabiashara ndogo wapatao 140 wanaofanya shughuli zao katika eneo la Viwanja vya Nyerere wamekabidhiwa vitambulisho hivyo na Mkurugenzi huyo katika hafla fupi iliyofanywa katika viwanja hivyo mchana wa leo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Kunambi amewaasa wafanyabiashara hao kuwa na utamaduni wa kutunza akiba ili kukuza mitaji yao huku akiwaahidi kuwaboreshea mazingira ya kazi zao na kwamba hakuna kiongozi atakayewaondoa katika maeneo hayo mpaka watakapatiwa maeneo mbadala na rafiki kwa biashara zao.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (wa pili kulia) akimvisha kitambulisho rasmi mmoja ya Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo. Kulia ni Ofisa Masoko wa Manispaa hiyo Steven Maufi.
Baadhi ya Wafanyabiashara Ndogo wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akizungumza na Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (wa pili kulia) akimvisha kitambulisho rasmi mmoja ya Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo. Kulia ni Ofisa Masoko wa Manispaa hiyo Steven Maufi.

MBUNGE MGIMWA AFANIKISHA MASOMO KWA MTOTO MLEMAVU

$
0
0
Na Fredy Mgunda, Iringa

MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahamud Mgimwa amemwokoa mtoto wa kike ambaye ni mlemavu wa viungo kwa kumpeleka shule baada ya wazazi wake kushindwa gharama za masomo.

Mtoto huyo Rosemary Lutego ambaye ana umri wa miaka 15 alichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule yawasichana Iringa lakini alishindwa gharama za masomo na matumizi shuleni baada ya wazazi wake kukimbia jukumu la kumpeleka shule.Mbunge Mgimwa baada ya kugundua changamoto inayomkabili binti huyo licha ya kufaulu na kushindwa kujiunga na wenzake kuanza masomo ya kidato cha kwanza ndipo alipoamua kumsomesha katika shule maalum ya Wasichana Iringa ambayo ni mchanganyiko.

Mwanafunzi huyo alijulikana kama yuko nyumbani baada ya ziara ya kikazi aliyofanya mbunge Mahamud Mgimwa katika kata mbalimbali na kubaini uwepo wa mwanafunzi ambaye alikosa vifaa mbalimbali vya shule na kuamua kuchukua jukumu la kumsomesha hadi anamaliza shule.Mara baada ya kupata taarifa za mwanafunzi huyo,Mgimwa alizungumza na wazazi na walimu katika shule ya Msingi Ikweha na kuwataka uongozi wa kijiji cha Ikweha kuwatafuta wazazi hao na kuwapeleka katika vyombo vya sheria huku akichukua jukumu la kumnunulia vifaa vyote vinavyohitajika shuleni hapo.

Aidha aliwataka wazazi wote ambayo wana tabia ya kuwazuia watoto waliofaulu kujitokeza haraka kabla ya msako kuanza popote pale katika jimbo la Mufundi Kaskazini ambapo wawapeleke shule kutokana na sasa hakuna ada wala mchango katika shule za serikali.Aidha aliwataka wazazi kuacha tabia ya kuwafundisha watoto wao tabia ya kujifelisha katika mitihani ili waweza kuolewa wakati uwezo wa kufaulu upo kwa mtoto husika.

Akizungumza mara baada ya kupata msaada huo mtoto Rosemary Lutego alisema kuwa ndoto yake ya kupata elimu na kuweza kuja kuwasaidia wazazi wakeimeanza kupata mwanga kwani alidhani ndoto zake zimeishia darasa la saba.alimshukuru sana mbunge Mgimwa msaada huo mkubwa wa kufanikisha masomo yake kwani itakuwa mfano mkubwa wa wazazi wengine ambayo hawataki mtoto wa kike aende shule.

Aliongeza kuwa wazazi wake walimwambia kuwa wanaenda kutafuta fedha za kununulia vifaa lakini hadi sasa hawakuweza kufanikisha hali iliyomlazimu abaki nyumbani wakati wanafunzi wengine wakiendelea na masomo."Namshukuru sana mbunge kwa kusikia na kuamua kugharamia masomo yangu ya sekondari nitahakikisha nasoma kwa bidii licha ya ulemavu wangu ili kuweza kuikomboa familia yangu katika umaskini." alisema 

DKT MWIGULU AZINDUA ZOEZI LA UANDIKISHAJI WANANCHI KUPATA VITAMBULISHO VYA URAIA MKOANI TABORA

$
0
0
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Dkt. Mwigulu Nchemba akizindua zoezi la uandikishaji wa wananchi kupata kitambulisho cha uraia mkoani Tabora kushoto kwake ni kaimu mkurugenzi mkuu wa NIDA Andrew Masawe na mkuu wa wilaya ya Tabora Queen Mlonzi. zoezi hilo lilifanyika leo katika wilaya ya Tabora
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watanzania kujiandikisha kupata kitambulisho cha Taifa kwani si zoezi la hiari ni lazima kwa mtanzania aliyeko ndani ya mipaka ya nchi ili kutambukiwa.
Waziri Mwigulu amewataka wananchi waache mazoea ya kutafuta kutambuliwa mpaka wanapokuwa na shida hasa za kutaka hati ya kusafiria au migogoro ya ardhi pale anapoambiwa yeye si raia wa Tanzania .
“Zoezi hili ni bure kujiandikisha na kupata kitambulisho pasitokee kiongozi yeyote wa wilaya na vijiji kuchangisha fedha wananchi ili wapate fomuza kujiandikisha na wala zoezi hili lisiunganishwe na siasa.”alisema Dkt.Mwigulu

MKUCHIKA AKUTANA NA MWAKILISHI WA UNICEF NCHINI

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na Mwakilishi wa UNICEF nchini Bi. Maniza Zaman alipomtembelea ofisini kwake jana.
Mwakilishi wa UNICEF nchini Bi. Maniza Zaman akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) alipomtembelea waziri huyo ofisini kwake  jana .

TAA Yakabidhi Gari Kituo Cha Zimamoto

$
0
0
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) jana imekabidhi gari aina Toyota Hilux kwa Idara ya Zimamoto na Uokoaji ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), ili kuchocheo ufanisi wa kazi.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela akikabidhi gari hilo katika hafla fupi iliyofanyika jana katika Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha JNIA, alisema litasaidia usafiri wa haraka kwenye matukio kwa Kamanda wa Zimamoto wa Viwanja vya Ndege Tanzania, Kamishna Msaidizi, Christom Manyoroga, ambaye awali alikuwa na gari kuukuu.

Bw. Mayongela alisema kuwa gari hilo lenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 80, mbali na kusaidia usafiri wa haraka kwenye matukio ya ndani ya kiwanja na nje endapo watatakiwa kutoa msaada, pia litasaidia shughuli mbalimbali za zimamoto na uokoaji.

Alisema Zimamoto ni miongoni mwa taasisi kubwa inayofanya kazi na TAA, hivyo ni jukumu la mamlaka kuhakikisha wanawezeshwa kwa vifaa na vitendea kazi ili waweze kufanya kazi kwa weledi.Pia Bw. Mayongela alisema mbali na msaada ya gari hilo TAA itatoa fedha kiasi Sh milioni 120 kwa ajili ya kuwapatia mafunzo wafanyakazi wa vituo vya Zimamoto vya viwanja vya ndege, ili weaweze kwenda na mabadiliko yanayotokea duniani.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (kushoto) akimkabidhi funguo ya gari, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania, Thobias Andengenye katika hafla iliyofanyika janao kwenye Kituo cha Zimamoto cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania, Thobias Andengenye akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa kikosi hicho na menejimenti ya TAA.
Gari aina ya Toyota Hilux alilokabidhiwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania, Thobias Andengenye na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela litakalotumiwa na Kamanda wa Kikosi cha ZImamoto na Uokoaji wa Viwanja vya Ndege Tanzania, Christom Manyoroga.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani cha Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Irene Sikumbili (kushoto) akiagana na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye  jana baada ya kukabidhiwa gari litakalotumiwa na Kamanda wa kikosi cha Zimamoto cha Viwanja vya Ndege Tanzania. Wengine kulia ni Mkuu wa Idara ya Manunuzi na Ugavi Bw. Mtengela Hanga na (katikati) Mkuu wa Idara ya Udhibiti Viwango Bw. Paul Rwegasha.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (kulia) akiagana na makamanda wa kikosi cha zimamoto na Uokoaji baada ya kukabidhi gari jana.


Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images