Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA PASIPOTI MPYA YA TANZANIA YA KIELEKTRONIKIA

$
0
0



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Januari, 2018 amezindua mfumo wa uhamiaji mtandao (e-Immigration) ambao utasaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa mipaka ya nchi, kudhibiti ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali na kuimarisha utoaji wa huduma za kiuhamiaji kwa raia wa Tanzania na wageni wanaoingia na kuishi hapa nchini kwa madhumuni mbalimbali.






Kabla ya kuzindua mfumo wa uhamiaji mtandao Mhe. Rais Magufuli amekagua teknolojia iliyotumika katika mfumo huo ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa alama za vidole na baadaye kupatiwa pasipoti mpya ya kielektronikia (e-Passport) ambayo pia imeanza kutolewa leo.
Pasipoti mpya za kielektronikia pia zimetolewa kwa viongozi wengine wakuu wa Serikali, Bunge na Mahakama wa Tanzania Bara na Zanzibar, waliohudhuria uzinduzi huo.





 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akionesha kwa furaha passipoti yake mpya  ya kielektronikia baada ya kuipokea kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018. Kushoto ni Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na kushoto kwa Waziri ni Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Dkt. Peter Makakala.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli   akionesha kwa furaha passipoti yake mpya  ya kielektronikia baada ya kuipokea kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018. 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli  akiiangalia  kwa furaha passipoti yake mpya  ya kielektronikia baada ya kuipokea kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli  akipokea passipoti yake mpya  ya kielektronikia  kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018. 
 Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein  akipokea pasipoti yake mpya ya kielektronikia kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018.  
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akionesha kwa furaha passipoti yake mpya  ya kielektronikia baada ya kuipokea kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akiweka sahihi kwa ajili ya kujipatia pasipoti yake mpya  makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018.  
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli  akiwa na  Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akisubiri hatua inayofuata  baada ya kuweka sahihi kwa ajili ya kujipatia pasipoti yake mpya ya kielektronikia makao makuu ya Idara ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018.   PICHA NA IKULU

MKUNGU WA NDIZI TUNAUZA 15000/- SOKO LA MABIBO-WAFANYABISHARA

$
0
0
Na Neemalisa Nambeye, Globu ya Jamii

WAFANYABISHARA wa ndizi katika soko la Mahakama ya Ndizi lililopo Mabibo jijini Dar es Salaam wamesema kuwa katika soko hilo bei ya mkungu mmoja wa ndizi wanauza Sh.15000 ambayo iko chini zaidi ukilinganisha na masoko mengine.

Wakizungumza leo na Michuzi Blog sokoni hapo, baadhi ya wafanyabiashara ya ndizi wamesema wanauza bei hiyo kutokana na wingi wa ndizi zinazofika sokoni kwao lakini pia kule ambako wananunulia bei ya manunuzi iko chini.

Imefahamika wakati bei ya mkungu wa ndizi ikiwa Sh.15000 kwenye soko hilo masoko mengine likiwamo soko la Buguruni jijini Dar es Salaam baadhi ya wafanyabiasha wanauza mkungu mmoja wa ndizi kati ya Sh. 30,000 hadi Sh.35.000.

Wafanyabiashara hao wa soko la Mahakama ya Ndizi wameeleza kuwa idadi ya wanunuzi wa ndizi ni kubwa sokoni hapo lakini kikubwa ambacho wanajivunia ni wingi wa ndizi zilizopo.

"Bei yetu iko tofauti na maeneo mengine,hapa kwetu mkungu mmoja tunauza Sh.15000 lakini masoko mengine bei iko juu kidogo.Sababu kubwa tunakofuata ndizi tunanunua kwa bei yenye unafuu na hivyo nasi kurudisha unafuu huo wa bei kwa wateja wetu,"wamesema wafanyabiashara hao.

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AHIMIZA MAHAKAMA KUTENDA HAKI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi ameitaka Mahakama kutenda Haki bila kufungwa na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha Haki kutendeka.

Pia ameitaka kutoa fidia ipasayo, kukuza usuluhishi ipasavyo, kukuza usuluhishi baina ya watu husika katika migogoro  na watoe haki bila kujali sababu za hali ya mtu kijamii ama kiuchumi

Waziri Kabudi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akifunga maonesho ya Wiki ya Sheria ambayo kilele chake kinatarajiwa kufanyika kesho katika Viwanja vya Mahakama vya Chimala jijini. Kauli mbiu katika siku ya sheria mwaka huu inasema, Matumizi ya Tehama katika utoaji haki kwa wakati na kuzingatia maadili.

Waziri Kabudi pia ameitaka Mahakama ipunguze kuchelewesha kesi bila sababu za msingi na iongeze kasi ya usikilizwaji wa Mashauri kwa 

Ameongeza Wizara inathamini maonesho ya siku ya sheria na maendeleo yanayofanywa na Mahakama katika kuendeleza kuboresha mfumo wa sheria na kwamba Mahakama imekuwa ya kwanza kubadilika katika sekta ya sheria. Hivyo Wizara itahakikisha maboresho ya mahakama yanafanikiwa.

Kabla ya ufungaji wa maonesho hayo, Waziri Kabudi pia amezindua  Mahakama ya Mwanzo na Mahakama ya Wilaya Kigamboni.

Akizindua jengo hilo la Mahakama lililogarimu zaidi ya Sh.milioni 500  Prof.Kabudi amesema, mkakati wa Mahakama hadi kufikia mwaka jana walikuwa wanahitaji  Mahakama Kuu 19, Mahakama za Hakimu  Mkazi 14, Mahakama za Wilaya 109, Mahakama za Mwanzo 3003 huku wakiwa na uhitaji mkubwa wa ukarabati wa mahakama nyingi nchini. 

Aliipongeza Mahakama kwa ubunifu, umakini na ufanisi waliouonesha kwa kufanya utafiti wa kutumia Moladi na ujenzi bora, imara na wenye gharama nafuu. Prof. Kabudi pia ameipongeza mahakama kwa kujenga majengo hayo katika wilaya mpya, hasa Kigamboni na amewataka kutafuta viwanja zaidi ili jitihada za kuongeza mahakama Kigamboni zifanyike kwa kuwa ipo moja tu.
Waziri wa katiba na Sheria, Profesa Pamalagamba Kabudi akizungumza na wananchi pamoja na watumishi wa Mahakama wakati wa uzinduzi mahakama ya mwanzo na Wilaya ya Kigamboni, kulia kwake ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania, Ferdnandi Wambari na kulia kwake ni Jaji Mkuu  Kuu Zanzibar Omary, Othaman Makungu.
 Waziri wa katiba na Sheria Profesa Pamalagamba Kabudi akipanda mti katika jengo jipya la mahakam ya mwanzo na Wilaya ya Kigamboni, baada ya kumaliza kuzindua mahakama hiyo mpya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

NHIF YATOA USHAURI KWA WANANCHI, YAPOKEA MALALAMIKO

$
0
0
Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umeshiriki katika Wiki ya Sheria kwa kutoa ushauri na kupokea malalamiko mbalimbali kutoka 
kwa wananchi waliofika kutembelea mabanda hayo kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Katika kuelekea maadhimisho ya wiki ya sheria kesho, maonesho hayo yaliyoanza  Jumapili ambapo  NHIF wameweza kutoa huduma ya 
upimaji magonjwa yasiyoambukizwa sambamba na ushauri nasaha kwa wananchi mbalimbali.

Mtaalamu wa Kisukari kutoka Hospitali ya Amana Dk.Natalius Kapilima amesema wananchi wengi waliojitokeza kupata huduma ya vipimo wamekutwa wana uzito mkubwa unaotokana na ulaji usiofaa na kutokufanya mazoezi ya viungo vya mwili Magonjwa yaliyokuwa yanapimwa katika banda la NHIF ni kisukari, presha (BP), uwiano wa uzito na urefu wa mtu pamoja na maambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU) na takribani wananchi 170 waliweza kupata huduma hiyo.

NHIF wameweza kuandikisha wanachama wapya wanaotaka kujiandikisha na mfuko huo wa bima hususani kwa TOTO afya Kadi kwa ajili ya watoto wadogo chini ya miaka 18.

Nesi Catherine Moshi akiwa anachukua kipimo cha damu kutoka kwa mwananchi aliyefika kwenye banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika maonyesho ya wiki ya Sheria nchini.
Afisa wa Sheria kutoka Makao Makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Tamasha Magongo akimuelekeza mwananchi aliyefika kwenye band lao alipoleta malalamiko yake.


Mfanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Victor Wanzagi akitoa maelezo kwa mwananchi aliyefika kwenye banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika maonyesho ya wiki ya Sheria nchini.

Mtaalamu wa Kisukari kutoka Hospitali ya Amana Dr Natalius Kapilima akimsikiliza mwamachi aliyefika kwenye banda la Mfuko wa Taifawa Bima ya Afya (NHIF) katika maonyesho ya wiki ya sheria nchini.

KAMATI YA MAADILI TFF YAMUADHIBU MJUMBE BODI YA LIGI

$
0
0
Na Agness Francis Globu ya jamii.

KAMATI ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) imemfungulia mashitaka Mwenyekiti wa Abajalo FC na Mjumbe wa Bodi ya Ligi Edgar Chibula kwa tuhuma ya kuikashifu na kuidhalilisha Kamati ya Bodi ya Ligi ya TFF katika vyombo vya  Habari ambapo ni kinyume na sheria. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam,Ofisa Habari wa TFF Clifford Ndimbo amesema kuwa  Chibura alishitakiwa Februari 28 mwaka huu kwa kosa la  kuzungumza maneno yasiofaa kwa kuidhalilisha bodi hiyo katika vyomba vya habari ikiwa ni kinyume na kufungu cha sheria  cha 50(1), (2) na (6) cha Katiba ya TFF toleo  la mwaka 2015,pia ni kinyume na sheria kanuni za maadili  toleo  la 2013.

Aidha Ndimbo amesema kwenye  shauri  hilo mtuhumiwa  huyo hakuhudhuria, isipokuwa alileta  utetezi wake kwa njia ya maandishi 
ambapo Sekretarieti ya TFF ilitoa ushahidi wa sauti(clip)  ya mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha redio hapa nchini. 

Ambapo kwenye mahojiano hayo mtuhumiwa alisikika akizungumza maneno hayo yasio na maadili katika maendeleo ya mpira wa miguu. 

Ndimbo amesema kutokana na utovu wa nidhamu  na kosa la kuzungumza maneno ya kuikashifu  Bodi ya Ligi ya Mpira wa Miguu TFF,  Kamati imeamua asijuhusishe na shughuli  zozote za mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja pamoja na faini ya Sh.milioni 3  chini ya kufungu cha  73 (4) kanuni za maadili ya TFF toleo 2013.

RAIS MAGUFULI AMJULIA HALI MSANII MKONGWE KING MAJUTO HOSPITALINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimjulia hali msanii mkongwe Amri Athumani maarufu kama King Majuto aliyelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimjulia hali msanii mkongwe Amri Athumani maarufu kama  King Majuto aliyelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimjulia hali msanii mkongwe King  Amri Athumani maarufu kama Majuto aliyelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018

VIGOGO TFF KUHUDHURIA MKUTANO MKUU CAF

$
0
0
Na Agness Francis, Globu ya Jamii 
VIONGOZI wa tatu wa ngazi za juu katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) wanatarajia kuhudhuria mkutano mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika(CAF).

Taarifa ya TFF iliyotolewa leo jijini Dar es Salaam imesema mkutano huo utafanyika Februari 2 mwaka huu nchini Morocco.

Imesema viongozi watakaohudhuria ni Rais wa Bodi ya Ligi ya Mpira wa Miguu Tanzania Wallace Karia, Makamu wa Rais wa TFF Michael  Wambura na Kaimu  mkuu wa Bodi hiyo Kidao Wilfred.

DK. KIGWANGALLA AELEZA HATMA YA WAVAMIZI KATIKA HIFADHI YA BONDE LA MTO KILOMBERO


KING MAJUTO AUZUNGUMZIA UONGOZI WA RAIS MAGUFULI

$
0
0
*Amwambia alikuwa wa kwanza kumtabiria atakuwa  Rais 
*Amsifu misimamo yake, namna alivyorudisha nidhamu ya kazi

Na Ripota Wetu, Globu ya jamii

GWIJI wa maigizo nchini Amri Athuman a.k.a Mzee Majuto, amesema anamuomba Mwenyezi Mungu ampe umri mrefu Rais ,Dk.John Magufuli kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kuwatumikia Watanzania huku akielezea kufurahishwa kwake na namna ambavyo amerudisha ambavyo amerudisha nidhamu ya watu kufanya kazi.

King Majuto amefafanua wakati Dk.Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi yeye alikuwa wa kwanza kumtabiria kuwa kuna siku atakuwa Rais wa Tanzania na ndicho ambacho kimetokea na ukweli anajisikia furaha sana kutokana na utendaji kazi wa Rais na kila mtu amekuwa na adabu na anatambua nchi sasa ina viongozi.

King Majuto ametoa kauli hiyo leo akiwa Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam baada ya  Rais Magufuli kwenda kumjulia hali .King Majuto amelazwa hospitalini hapo kwa ajili ya kupata matibabu.Akizungumza mbele ya Rais Magufuli, King Majuto amesema kuwa  yeye alikuwa wa kwanza kumtabiria Dk.Magufuli kuwa akipata urais nchini itasonga na kweli sasa nchi yetu inakwenda vizuri.

"Nilitabiri huyu akiwa Rais mambo yatakucha na kweli sasa mambo yamekucha.Tumempata Rais na si masihara kwani watu wamekuwa na adabu,wanajua nini maana ya kazi na wanafanya kazi kweli.Na sisi wazee tunafarijika sasa hivi , tumepata rais si masihara na watu wanaadabu zao.

"Watu wanajua nini kazi na wanafanya kazi.Na sisi waze  tunafarijika sasa hivi leo, kama hivi viwanda vimetapakaa.Umekuwa Rais mwenye misimamamo na hiki ndicho ambacho tunajivunia maana si wote wenye misimamo.Najisia raha sana na namuomba Mungu akupe maisha marefu,"amesema King Majuto.

Wakati anaanza kuzungumza na Rais,King Majuto amesema "Uongozi wa Rais Magufuli sijui lakini Mwenyezi Mungu ampe maana kuna sehemu amezikamata haswa haswa na watu wanaelewa hii nchi ina viongozi.Sasa ni kazi tu,"Amesema kuna watu walikuwa wanaita fedha jero lakini sasa wanaiita Sh.500 na hata wale waliokuwa wanafoji vyeti ili wapate kazi lakini sasa hawana nafasi hata akiwa amefanya kazi kwa miaka 20 akibainika amefoji cheti ataondoka.

 "Yaani raha sana, mtu kafoji vyeti nje hata kama amekaa miaka 20, nafurahishwa sana na uongozi wako.Umekuwa mzazi kwetu na si kwa wasanii tu bali kwa Watanzania wote,"amesisitiza King Majuto.

Akizungumzia uongozi wa Rais Magufuli ,King Majuto amesema kuwa misimamo yake imesaidia watu kufanya kazi na kutoa mfano alipofika Muhimbili alipokelewa vizuri na madaktari na kupata vipimo na ndani ya muda mfupi tu akawa amepeta huduma."Nahisi ujio wako hapa hospitali kuna watu watakuwa wamejikojolea  kutokana na kuifahamu misimamo yako.Kwa kweli ni raha sana,"amesema King Majuto.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimjulia hali msanii mkongwe King  Amri Athumani maarufu kama Majuto aliyelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam leo Januari 31, 2018

CCM KIBAHA MJINI YAKAMIA KUUZIKA UPINZANI UCHAGUZI 2019/2020

$
0
0

Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mjini Kibaha, Mkoani Pwani ,Maulid Bundala amezitaka jumuiya zote za CCM na chama kijumla ziungane kuendelea kuisemea serikali na utekelezaji wa ilani ili waliozoea kukosoa wakose ya kusema.

Aidha amewaasa wanachama na viongozi wa chama wilayani hapo,kujipanga ili kuuzika upinzani katika chaguzi zijazo 2019/2020.Akifungua baraza la jumuiya ya wazazi ya CCM Mjini Kibaha ,wakati jumuiya hiyo ikiadhimisha miaka 41 ya CCM ,Bundala alisema wanaCCM wasiwe watu wakusemewa bali wajifunze kusema wenyewe.

Alisema wawe wamoja na kukiimarisha chama ili ikifika 2019-2020 mitaa na kata zote ziwe mikononi mwa Chama hicho.“Tembeeni kifua mbele ,macho mita 100 bila kuogopa ,elezeni anayofanya mwenyekiti wetu wa CCM Taifa na rais Dk.John Magufuli”

“Msisubiri kusemewe na watu wasiolitakia mema taifa letu,tusingojee wapinzani wazushe hoja zinazopotosha kwa wananchi na kuikosoa serikali” alisema Bundala.Bundala aliwaasa viongozi wa chama kila mmoja kwa nafasi yake kumsaidia Mh.Rais kusimamia utekelezaji wa ilani katika ngazi za chini .

Aliwataka kuondoa uoga kwa kuwasimamia na kuwakosoa pale wanapokosea watendaji ,madiwani na halmashauri .“Tusimwachie Rais pekee asimamie mambo yote peke yake ,tukikaa nyuma nyuma ndio maana tunauziwa mbuzi kwenye gunia ,tuhakikishe halmashauri zinatimiza miradi pia huduma stahiki kwa wananchi” alisema Bundala.

Bundala aliomba vijana waache kukaa vijiweni,kucheza pool wajitume ili kujikomboa na umasikini.Hata hivyo ,alieleza viongozi wa chama nao wasiwe wababaishaji wafanyekazi ama biashara na kazi kwani wao ni mfano wa kuigwa.Nae mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Kibaha Mjini ,Edwin Shunda alisema wamejipanga kurejesha mitaa na kata 2019-2020 .Shunda alisema ,pia wanatarajia kuondokana na hali ya kuwa tegemezi kwa kuanzisha miradi ya jumuiya hiyo .

Katika maadhimisho hayo ,jumuiya hiyo ilifanya usafi eneo la chama Mjini Kibaha ambapo pia aliyekuwa mgombea wa udiwani kupitia CUF ,kata ya Kongowe ,2015,Mathas Kambi alijiunga na CCM.
Mwenyekiti wa Jumuiya wa Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha Mjini,Edwin Shunda (mwenye kofia) akishirikiana na wajumbe wa jumuiya hiyo kufyeka katika mazingira ya jengo la chama hicho wakati wa maadhimisho ya kutimiza miaka 41 ya chama hicho wilayani Kibaha leo,yaliyofanya na jumuiya ya wazazi Mjini hapo
Mwenyekiti wa Jumuiya wa Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha Mjini,Edwin Shunda (mwenye kofia) akishirikiana na wajumbe wa jumuiya hiyo kuzoa takataka na kuweka katika vifaa vya kubebea uchafu katika mazingira ya jengo la chama hicho wakati wa maadhimisho ya kutimiza miaka 41 ya chama hicho wilayani Kibaha leo,yaliyofanywa na jumuiya hiyo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha,Maulid Bundala (katikati) akikabidhi kadi ya CCM kwa Aliyekuwa Mgombea wa udiwani kupitia Chama cha Wananchi (CUF) 2015,kata ya Kongowe ,Mathas Kambi (anaepokea kadi) baada ya jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Kibaha kufanya usafi katika jengo la chama hicho wakati wa maadhimisho ya kutimiza miaka 41 ya chama hicho wilayani Kibaha leo,Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Kibaha mjini, Edwin Shunda.Picha na Mwamvua Mwinyi.

Wafanyakazi JKC Wapewa Mafunzo na kampuni ya Medtronic ya Mfumo wa Umeme wa Moyo (Electrocardiogram – ECG)

$
0
0
Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwtete (JKCI) Peter Kisenge na Prof. Ahmed Osman wa Broward General Medical Centre ya nchini Marekani wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa Moyo wa bila kufungua kifua na kumuwekea kifaa maalum cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (pace maker) ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo yaliyoandaliwa na kampuni ya Medtronic tawi la Kenya ambao ni watengenezaji wa vifaa tiba vya magonjwa ya Moyo.
Prof. Ahmed Osman kutoka Broward General Medical Centre ya nchini Marekani akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo ya mfumo wa umeme wa Moyo (Electrocardiogram –ECG) kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo yaliyoandaliwa na kampuni ya Medtronic tawi la Kenya ambao ni watengenezaji wa vifaa tiba vya magonjwa ya Moyo.
Viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kampuni ya Medtronic ambao ni watengenezaji wa vifaa tiba vya magonjwa ya Moyo wakati wa mafunzo ya mfumo wa umeme wa Moyo (Electrocardiogram – ECG) kwa wafanyakazi wa JKCI yaliyoandaliwa na kampuni hiyo.
Prof. Ahmed Osman kutoka Broward General Medical Centre ya nchini Marekani akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi mfumo wa umeme wa Moyo (Electrocardiogram –ECG) unavyofanya kazi mwilini wakati wa mafunzo hayo yanayoenda sambamba na vitendo ya siku tano yaliyoandaliwa na kampuni ya Medtronic tawi la Kenya ambao ni watengenezaji wa vifaa tiba vya magonjwa ya Moyo.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Prof. Ahmed Osman (hayupo pichani) kutoka Broward General Medical Centre ya nchini Marekani akiwafundisha jinsi mfumo wa umeme wa Moyo (Electrocardiogram -ECG) unavyofanya kazi mwilini.Picha na JKCI

SERIKALI KUZIFIKIA KAYA ZOTE MASIKINI NCHINI

$
0
0
Serikali imepanga kuimarisha Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambao umo ndani ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ili kuzifikia kaya zote masikini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) amesema Bungeni leo wakati akijibu swali kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.

“Serikali ipo katika hatua za mwisho za kuanza kuandaa sehemu ya pili ya TASAF Awamu ya Tatu ambayo itaendelea kwa miaka mingine mitano” Mhe. Mkuchika amesema na kuongeza Serikali inaelewa yapo maeneo yenye kaya zenye vigezo vya umasikini na uhitaji ambavyo bado havijafikiwa.

Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ulianza mwaka 2013 na unatekelezwa katika Halmashauri 159 za Tanzania Bara, na Unguja na Pemba lakini si katika vijiji, mitaa na shehia zote. 

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI,
OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA.
TAREHE 31 JANUARI, 2018.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akijibu swali kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini Bungeni leo.

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 31.01.2018

Majaliwa arejea kutoka kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika nchini Ethiopia

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim, kwenye Hoteli ya Radisson Blue, mjini Addis Ababa, wakati akiondoka kurejea Dar es salaam, kushoto ni Mke wa Salim Ahmed salim,  Mama Amne Salim, Waziri Mkuu alikua Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 30, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiagana na Rais wa Comoros, Azali Assoumani, ndani ya ndege ya shirika la Ethiopian Airline, wakiwa wanarejea kutoka kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja AU, Januari 30, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, nje ya ndege ya shirika la Ethiopian Airline, wakati akiwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam  kutoka kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja AU, Januari 30, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MISS UNIVERSITY WAPAGAWISHA WANA MBEYA.


Ban Ki-moon ashiriki ufunguzi wa Ubalozi wa Tanzania Jamhuri ya Korea Kusini

$
0
0
 Mheshimiwa Matilda Masuka Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea akiwakaribisha na kuwashukuru wageni waalikwa waliohudhuria kwa wingi kwenye ufunguzi rasmi wa Ofisi za Ubalozi tarehe 31 Januari 2018. Awali Tanzania ilikuwa inawakilishwa nchini humo kutokea Japan. Mheshimiwa Balozi Matilda Masuka aliteuliwa Desemba 3, 2016 na baadaye kuapishwa kuwa Balozi wa kwanza mwenye makazi yake Mji Mkuu wa Seoul, Jamhuri ya Korea. 
 Mheshimiwa Lim Sung-nam, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea akizungumza kwa niaba ya Serikali yake wakati wa ufunguzi rasmi wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo. Kwenye salamu zake za ufunguzi, Mheshimiwa Sung-nam amesifu jitihada za Serikali ya Tanzania kukuza uchumi na kusifu ushawishi na karisma ya Balozi Masuka ambayo imewezesha kuvutia Mabalozi na wanadiplomasia wengi Jijini Seoul kushuhudia ufunguzi wa ofisi za Ubalozi.

 Mheshimiwa Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mstaafu akihutubia wageni waliofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania. Mheshimiwa Ki-moon, ambaye alitambulishwa kama rafiki mkuu wa Tanzania nchini humo, alipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufanikiwa kusimika bendera ya Tanzania nchini mwake baada ya miaka 25 ya uhusiano mzuri wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi.  
 Picha ya pamoja baada ya Waziri Mahiga na Mheshimiwa Sung-nam  kukata utepe na kuzindua rasmi majengo hayo. Kutoka kushoto ni Bw. Park Young min, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika; Mhe. Silvester Bile, Kiongozi wa Mabalozi wa Afrika na Balozi wa Ivory Coast; Mhe. Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mstaafu; Mhe. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje Tanzania; Mhe. Lim Sung-nam, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Korea Kusini; Mhe. Matilda Masuka, Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini; na Mhe. Salim Alharthy, Kiongozi wa Mabalozi na Balozi wa Falme ya Oman nchini Korea ya Kusini.  

 Picha ya pamoja na Mabalozi wanawake wanaoziwakilisha nchi mbalimbali kwenye Jamhuri ya Korea na picha ya Mabalozi kutoka nchi za kiafrika walioko nchini Korea Kusini. 
 Picha ya pamoja baada ya Waziri Mahiga na Mheshimiwa Sung-nam  kukata utepe na kuzindua rasmi majengo hayo.

GOLIKIPA ALIYELALAMIKA NJAA KUHOJIWA NA TFF

ILANI aliyosaini Dk. Kigwangalla leo kuhusu waliovamia kiwanja chenye hati namba 4019 kilichopo Njiro, Jijini Arusha

UNNewsKiswahili: Jarida la Habari Januari 31, 2018

WABUNIFU WA MAVAZI WAZINDUA CHAMA CHAO

Viewing all 110025 articles
Browse latest View live


Latest Images