Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI MKUTANO WA AU NCHINI ETHIOPIA

$
0
0
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amehudhuria katika Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli. Januari 29, 2018. 
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) na Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa (katikati) nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) na Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa (katikati) nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahi jambo na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mke wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mjumbe Maalum na Mwenyekiti wa Umoja wa Africa Nchini Sudan, Prof. Joram Biswaro, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. 

5 YEARS DEATH ANNIVERSARY

$
0
0




Moses Tito Kachima


BORN:27th January 1945                  DIED: 29th January 2013



Gone but not forgotten. Your presence lingers in our life. God blessed us with your presence and now you’re not here with us but we have an angel to watch over us and heaven has also gained an angel. Years have passed but you’ll always be missed.

May your soul rest in eternal peace, Amen. 

SERIKALI KUTOWAFUMBIA MACHO WANAOJIHUSISHA NA UVUVI HARAMU

$
0
0

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais ,Dk.John Magufuli imeapa kutowafumbia macho viongozi au watu wanaojihusisha na shughuli za uvuvi wa kutumia zana haramu zilizopigwa marufuku.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega alipokuwa akiteketeza zana za uvuvvi haramu zilizomakatwa hivi karibuni katika Wilaya za Busega mkoani Simiyu na Magu mkoani Mwanza.

Amesema kuwa hakuna atakayesalimika katika sakata hilo endapo tu akibainika kutumia zana haramu za uvuvi.Ameongeza kuwa Serikali ina dhamira kubwa na wavuvi katka ufanyaji wa shughuli zao na ndio maana imeamua kupiga marufuku zana zote haramu kwa lengo la kusaidia kizazi kijacho ili nacho kije kinufaike na raslimali za Taifa hili.

,"Hivyo idara ya uvuvi kamwe hautomfumbia macho kiongozi yeyote yule ambaye anajishughulisha na biashara hiyo kwa kigezo cha kuwa yeye ni kiongozi.“Kwa yule atakayebainika kuwa ni kiongozi au mtu mwenye fedha zake anajihusisha na uvuvi haramu ambao Serikali inatumia fedha nyingi kukabiliana nao basi cha mtema kunde atakiona juu yake kwani zana zake zitachomwa,faini na yeye kuchukuliwa hatua za kisheria,” amesema.

Aidha Ulega amewataka wavuvi kuendelea kusalimisha zana haramu kabla ya kukumbwa na dhahma kubwa itakayowapeleka mahali pabaya zaidi ya hali ya sasa jinsi ilivyo.Pia amewahakikishia upatikanaji wa zana zinazohitajika mapema kwani tayari wamesha anza kupokea maombi mengi ya mashirika yanayohitaji kusambaza zana halali katika nchi yetu kwa madhumuni ya kuokoa rasilimali za majini zilizokuwa zikipatwa na shinda nyingi kutoka kwa wavuvui wasiokuwa waaminifu.

Kwa upande wake Msimamizi wa Kamati Maalumu ya kuthibiti na kupambana na uvuvi haramu Kanda ya Simiyu na Mwanza, Nchama Marwa amemuhakikishia Naibu Waziri kuwa hakuna uonevu wa aina yeyote ile unaofanywa na kikosi hicho kuhusu kuwawajibisha wale wanaoendelea na shughuli hiyo kwa kujifisha .Ameongeza kuwa kuna wavuvi ambao wanasalimisha na wengine bado wanaendelea kuvua kwa kujifisha laniki ni lazima tu watawakamata na sheria ya uvuvi itafuata mkondo wake bila kinyongo wala uonevu wa aina yeyote ile.

Aidha kiongozi huyo wa kikosi maalumu aliwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa kazi zao kwa Naibu Waziri na kumweleza kuwa kuwa mpaka sasa wamekamata nyavu haramu za makila 33121,nyavu za dagaa175,makokoro ya sangara119.Pia nyavu za timba 3,sangara wabichi kilo 1071,sangara kayabo3463, watu hao waliokamatwa na kikosi kazi wametozwa faini kulingana na kile walichokamatwa nacho na kufikia kiasi cha Sh.milioni 767.

Naye Boniface Mkama Mkazi wa Nyamikoma wilayani Busega ameipongeza Serikali kwa kuwasaidia na vitendo vya kinyama vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya wavuvi wenzao.Hivyo ameiomba kuwawaishia tu zana sahihi ili waendelea na shughuli zao za kila siku za uvuvi.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ,Abdullah Ulega akishiriki shughuli ya kuteketeza zana haramu za uvuvvi zilizokamatwa hivi karibuni katika wilaya za Busega mkoani Simiyu na Magu mkoani Mwanza.
Mkuu wa wilaya za Busega,Tano Seif Mwera akishiriki shughuli  la kutekeza  zana haramu za  uvuvvi zilizomakatwa hivi karibuni katika wilaya za Busega mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ,Abdullah Ulega akizungumzana na wavuvi juu ya kiongozi au mtu mwenye fedha zake anajihusisha na uvuvi haramu zana zake zitateketezwa na yeye atachukuliwa hatua za kisheria.Picha na Emmanuel Massaka.

MKAZI WA JIJI LA MWANZA AJISHINDIA MILIONI 40 ZA TATUMZUKA

$
0
0
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Khadija Nyembo akimkabidhi mfano wa hundi  mkazi wa Buswelu,Ilemela,jijini Mwanza, Gibson Gratian Erasms,aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 40 kwenye mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka uliofanyika jumapili iliyopita (Jackpot ya Jumapili).
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Khadija Nyembo akiwa katika picha ya pamoja na Mkazi wa Buswelu,Ilemela,jijini Mwanza, Gibson Gratian Erasms,aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 40 kwenye mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka uliofanyika jumapili iliyopita (Jackpot ya Jumapili),sambamba na baadhi ya viongozi wa Ofisi ya Wilaya na pamoja na ndugu wa mshindi huyo.

MPINA AAGIZA VIWANDA VYA SAMAKI KANDA YA ZIWA VICTORIA VIANZE KAZI IFIKAPO JULAI MWAKA HUU.

$
0
0
Na John Mapepele, Mara.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameagiza viwanda vinne vya kuchakata samaki na mazao yake vilivyofungwa katika Mikoa ya Mwanza na Mara kuanza kazi mara moja ifikapo Julai Mosi mwaka huu, ambapo amewataka wamiliki kupeleka mipango kazi ya namna ya kuvifufua kabla ya kufikia mwezi Machi mwaka wizarani kwake.

Alivitaja viwanda hivyo kuwa ni Tan Perch Limited na Supreme Perch Limited vilivyopo Mwanza na Mara Fish Packers Limited na Prime Catch Limited katika mkoa wa Mara.Waziri Mpina alizungumza hayo jana wakati alipokuwa kwenye ziara ya kikazi mkoani Mara na Mwanza kukagua operesheni maalum ya kutokomeza uvuvi haramu kanda ya Ziwa Victoria inayofanywa na kikosi kazi maalum alichokiunda hivi karibuni.

“Mimi kama Waziri mwenye dhamana ya Sekta ya Uvuvi nchini niliyepa kulinda raslimali za uvuvi nitahakikisha kwamba ulinzi wa raslimali hizi ni wa kudumu, na usio na mwisho hadi uvuvi haramu utakapoisha hapa nchini” alisisitiza Mpina 

Waziri Mpina alipata fursa ya kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Ulinzi ya Mkoa huo, wananchi katika maeneo tofauti na hatimaye kushiriki katika zoezi la kuchoma nyavu haramu ambapo hadi sasa zaidi ya nyavu zenye thamani ya shilingi bilioni nne zimechomwa moto katika zoezi linaloendelea la kudhibiti uvuvi haramu mkoani Mara.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye miwani ) akishirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent Anney na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Bi Anarozy Nyamubi kuteketeza nyavu haramu zilizokamatwa na kikosi kazi maalum alichokiunda hivi karibuni katika wilaya ya Musoma kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Emanueli Bulayi akishuhudia tukio hilo leo.(Na John Mapepele) 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Joelson Mpina akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Anarozy Nyamubi baada ya kuteketeza nyavu haramu katika Wilaya ya Butiama leo. 
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent Anney akimwaga mafuta kwenye nyavu haramu ili kuzichoma moto katika kijiji cha Bwai Kumusoma wilayani Musoma leo. 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Joelson Mpina akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Bwai Kumusoma wilayani Musoma leo ambapo alishiriki zoezi la kuchoma nyavu haramu zilizokamatwa na kikosi kazi cha kudhibiti uvuvi haramu Kanda ya Ziwa Victoria alichokiunda hivi karibuni, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent Anney akisoma majina ya Wavuvi Haramu 

MAJINA YA VYUO YABADILISHWA ZANZIBAR

$
0
0
Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kiliunganishwa na Chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar cha Chwaka, Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar cha Maruhubi na Chuo cha Afya cha Mbweni kwa sheria No. 7 ya mwaka 2016
Kutokana na muungano huo, majina ya taasisi hizo yamebadilika na kua kama inavyoonekana kwenye jadweli hapa chaini

  S/NO
JINA LA ZAMANI
JINA JIPYA
     1
Chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar
Skuli ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.
     2
Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar
Taasisi ya Utalii ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
     3
Chuo cha Afya
Skuli ya Afya na Tiba ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar

Hivyo, mawasiliano yote yanayohusu taasisi hizi yapelekwe kwa anuani ifuatayo:-

Makamu Mkuu wa Chuo
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
S.L.P. 146
Tunguu – Zanzibar.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

KIGWANGALLA AWATAKA WALIOVAMIA KIWANJA MAMLAKA HIFADHI YA NGORONGORO KILICHOPO NJIRO WAJIANDAE KISAIKOLOJIA

$
0
0

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akipata maelezo ya eneo la kiwanja chenye hati namba 4091 kilichopo Njiro Jijini Arusha ambacho kimevamiwa na watu mbalimbali na kuanzishwa makazi yenye kaya 82 ndani ya eneo hilo kutoka Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dk. Fredy Manongi (katikati). Eneo hilo ni mali ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na hati halisi ya eneo hilo ipo kwa jinala Bodi ya Utalii Tanzania. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la kiwanja chenye hati namba 4091 kilichopo Njiro Jijini Arusha ambacho kimevamiwa na watu mbalimbali na kuanzishwa makazi yenye kaya 82. Eneo hilo ni mali ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na hati halisi ya eneo hilo ipo kwa jinala Bodi ya Utalii Tanzania.
  Meneja wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Egidius Mweyunge (kulia) akimuongoza Waziri Kigwangalla kukagua eneo hilo.
Dk. Kigwangalla akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukagua eneo hilo.

DKT. MWAKYEMBE: TUMEJIPANGA, LAZIMA TURUDI NA MEDALI JUMUIYA YA MADOLA


SHUGHULI ZA KIBINADAMU ZAATHIRI UZALISHAJI UMEME NYUMBA YA MUNGU

$
0
0

Na Rhoda James, Kilimanjaro

Imeelezwa kuwa, shughuli za Kibinadamu zinazofanywa kuzunguka Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Nyumba ya Mungu zimeendelea kuathiri uzalishaji wa nishati hiyo kutokana na kukosekana maji ya kutosha.

Hayo yalielezwa na Kaimu Meneja wa Kituo Clarance Mahunda wakati Waziri wa Nishati, Subira Mgalu alipofanya ziara Kituoni hapo mwishoni mwa wiki na kueleza kuwa, hivi sasa kituo hicho kinazalisha megawati 3.5 hadi 4 tofauti na uwezo wake wa kuzalisha megawati 8 kwa saa 24.“Shughuli za binadamu zikiwemo kulima, kuchunga ngo’mbe na uvuvi kumepelekea uzalishaji wa umeme katika kituo hiki kuwa hafifu, kitu ambacho kinasababisha ukosefu wa maji ya kutosha hivyo kuzalisha umeme pungufu,” alisema Mahunda.

Pia, Mahunda alimweleza Naibu Waziri wa Nishati kuwa, japokuwa zipo juhudi mbalimbali zambazo zimefanyika kuzuia athari hizo ikiwemo kushirikisha wadau mbalimbali kama Pangani Water Basin pamoja na taasisi mbalimbali za Serikali, lakini baado kituo hicho kinazalisha megawati 3.5 hadi 4. 

Aidha, Mahunda alieleza kuhusu utendaji wa Kituo hicho na kusema kuwa ni mzuri kutokana na kufanyika ukarabati mkubwa uliofanyika mwezi Oktoba na Novemba,2017 na hivyo kupelekea mashine zote kufanya kazi ipasavyo.Pia aliongeza kuwa, kwa sasa kituo hicho kinasafirisha umeme kwa njia mbili za Msongo wa Kilovoti 66 kuelekea Kiungi na njia nyingine ni Umeme kusafirishwa kwa Msongo wa Kilovoti 33 kupitia Mwanga na Mkuyuni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati alizitaka Mamlaka kuanzia Serikali za Mtaa hadi Mkoa na wananchi wanaozunguka maeneo ya kituo hicho kuhakikisha wanatunza mazingira yanayozunguka kituo hicho kwa kulinda vyazo vya maji ili kupata maji ya kutosha wakizingatia umuhimu wa nishati ya umeme kwa maendeleo ya watu na Taifa.

“Nimeelezwa kuwa kina cha maji hakiruhusu mashine zote kuzalisha umeme, na hii ni kwa sababu ya shughuli za binadamu ambazo zinaendelea pembezoni mwa Bwawa la maji yanayotumika kuzalisha umeme huo,”aliongeza Mgalu.Mgalu aliongeza tatizo la shughuli za kibinadamu limeviathiri pia vituo vingine za kuzalishia umeme vya Hale na Pangani na hivyo kupelekea upungufu katika kuzalisha umeme kutokana na kina cha maji kupungua.

Aidha, Mgalu aliitaka TANESCO pamoja na Serikali za Mitaa kuendelea kuwaelimisha wananchi wanaozunguka maeneo hayo ili kuwezesha kituo husika kuzalisha umeme kwa viwango vinavyo takiwa.
Kaimu Meneja wa Kituo cha Nyumba ya Mungu TANESCO, Clarance Mahunda akitoa maelezo kuhusu utendaji wa kituo hicho kwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa pili kulia). Wengine katika picha ni Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati Makao Makuu na wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Kaimu Meneja wa Kituo cha Nyumba ya Mungu TANESCO, Clarance Mahunda akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati). Wengine katika picha ni Watumishi wa Wizara ya Nishati na kutoka Mkoa wa Kilimanjaro.
Kaimu Meneja wa Kituo cha Nyumba ya Mungu TANESCO, Clarance Mahunda (katikati) akitoa maelezo kuhusu Bwawa la maji linalotumika kuhifadhia maji katika Kituo cha Nyumba ya Mungu. Kushoto ni Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu na kulia ni Katibu wa Naibu Waziri, Ngerenja Mgejwa.


MADARASA YA NYASI, TEMBE, UDONGO YASITUMIKE KATIKA SHULE ZOTE NCHINI-WAZIRI JAFO

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi ambao kwenye maeneo yao bado kuna wanafunzi wanasomea katika madarasa ya Tembe ama yalioezekwa Nyasi au kujengwa kwa Udongo kuhakikisha wanaacha mara moja kutumia madarsa hayo na kujenga madarasa bora.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya nne ya Uongozi wa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi yanayotolewa kupitia ofisi ya Rais Tamisemi kwa kushirikiana na Taasisi ya Uongozi yenye lengo la kujenga uwezo wa viongozi kuweza kutawala kwa ufanisi.

“Viongozi wangu nataka Mkakusanye mapato ya ndani kwa nguvu zote na Fedha hizo mzitumie kwenye miradi ya maendeleo na kwa wale ambao mpaka leo wanafunzi wanasomea kwenye mazingira duni hawana madarasa bora watoto wanasomea kwenye madarsa ya Tembe, mengine yameezekwa kwa Nyasi nahitaji muelekeze Nguvu katika ujenzi wa madarasa bora na hayo ya Tembe yotoweke kabisa; Mjenge madarasa ambayo wanafunzi watajiskia fahari kusoma”Alisema Waziri Jafo.

Waziri Jafo hakusita kuwakumbusha Viongozi  kuhusu Usimamizi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Afya 212 vinavyoendelea kujengwa hivi sasa katika ameneo yote yote Nchini.

Niwapongeze baadhi ya Wakurugenzi ambao mpaka sasa wamefanya kazi nzuri sana ya Usimamizi wa ujenzi wa Miundombinu hiyo ya Afya wameshakamilisha ujenzi na wamejenga mpaka Njia za kutembelea(Walk Way) katika vituo hivyo na nataka mpaka Tarehe 30 April 2018 Kila Halmashauri iliyopokea Fedha za ujenzi wa Miundombinu ya Afya iwe imekamilika.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akifungua mafunzo ya Wakuu wa Wilaya na Wakugenzi wa Halmashauri yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais Tamisemi kwa ushirikiano wa Taasisi ya Uongozi yanayofanyika kwa siku Tano Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe. Josephat Kandege akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI kufungua mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri.
 Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Prof. Joseph Semboja akiwasilisha taarifa ya Utangulizi wakati wa mafunzo ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri
Mkuu wa Wilaya ya Londido Mhe. Daniel Chongolo (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe wakati wa mafunzo ya Uongozi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MBULU YAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA MABILIONI KUKAMILISHA VIPAUMBELE VYAKE

$
0
0
Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, limepitisha shilingi bilioni 43.983 za mapendekezo ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga akizungumza baada ya kupitishwa bajeti hiyo, alisema vipaumbele vyake ni elimu, afya, maji, kilimo na mifugo. Kamoga alisema bajeti hiyo imezingatia vipaumbele vya vijiji, kata, halmashauri, mkoa, mpango wa pili wa maendeleo ya Taifa na dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025. 

Alisema vipaumbele vingine ni mikakati na sera mbalimbali za kisekta, maelekezo mbalimbali ya viongozi wakuu wa kitaifa, na ahadi ya Rais John Magufuli alizozitoa wakati wa kampeni wilayani Mbulu. Alisema halmashauri hiyo imejikita katika kuongeza mapato ya ndani kwa kuimarisha vyanzo vilivyopo, kubuni vyanzo vipya na kuimarisha mfumo wa kielectroniki. 

"Halmashauri imejikita katika mpango bora wa matumizi ya ardhi kwa makazi, biashara, viwanda vidogo, maeneo ya malisho ya mifugo, kilimo, hifadhi ya mazingira na uhifadhi wa vyanzo vya maji," alisema Kamoga. Mbunge wa jimbo la Mbulu Vijijini, Flatei Massay alipongeza kupitishwa kwa bajeti hiyo ambayo imekidhi kuondoa changamoto mbalimbali. 

Massay alisema bajeti hiyo imegusa sekta mbalimbali ikiwemo elimu ya msingi, sekondari, kilimo, mifugo, ushirika, umwagiliaji, afya na maji. Alisema anatarajia wananchi wa jimbo hilo watapiga hatua kubwa ya maendeleo kupitia utekelezaji wa miradi ya mpango wa bajeti iliyopishwa na madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo. 

Mwanasheria wa halmashauri hiyo, Honoratus Mulokozi alisema bajeti hiyo kabla ya kupitishwa imezingatia sheria namba 9 ya serikali za mitaa ya mwaka 1982.Mulokozi alisema sheria hiyo ilifanyiwa marekebisho Januari mosi mwaka 2000 inayotaka kufuata sheria, kanuni na taratibu, wakati wa kuandaa bajeti. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akizungumza baada ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kupitisha mpango wa bajeti ya shilingi bilioni 43.983 za mwaka wa fedha wa 2018/2019. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akielezea vipaumbele vya mpango wa bajeti ya Halmashauri hiyo. 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Joseph Mandoo akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo baada ya kupitisha mpango wa bajeti ya shilingi bilioni 43.983 za mwaka wa fedha wa 2018/2019. 

JAJI MKUU AZINDUA KITUO CHA MAFUNZO, HABARI KUWAJENGEA UWEZO WATUMISHI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

JAJI Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma amezindua Kituo cha Mafunzo na Habari za Mahakama kilichopo Kisutu Dar es Salaam ambacho kitasaidia kuwajengea uwezo watumishi  wa Mahakama.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika mapema leo jijini Dar es Salaam Jaji mkuu amesema kituo hicho kina malengo kadhaa ikiwemo kuhakikisha haki inawafikia wananchi na walengwa kwa urahisi zaidi.

Amesema katika kituo jicho kuna vielelezo vingi vya mahakama kutekeleza majukumu yake kwa vitendo, kuwajengea uwezo  watumishi wa mahakama hasa kujifunza mambo ambayo kwa Bahati mbaya hawakusoma wakiwa chuoni.Amesema Tehama inarahisisha kazi kwa sababu kutoa haki kwa kutumia tehama wanawafikia wananchi wengi kwa urahisi zaidi.

Prof.Juma amesema kituo hicho ambacho kimejengwa kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kitakuwa na maeneo mapya kabisa ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi na watumishi wa mahakama ambayo ni Makosa ya Mtandaoa, Makosa yanayotokana na miamala ya simu  na Dawa za kulevya

Amesema mahakimu na waendesha mashtaka wakipata mafunzo hayo watakuwa na uelewa mmoja katika kutoa haki." Makosa hayo matatu yanahitaji ushiriki wa vyombo vya nje, kuna sheria nyingi za kimataifa zinagusa sheria zetu za Tanzania" amesema Ptof.Juma.

Amesema kwa sasa wanapata  taarifa za Mahakama kutoka katika mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu lakini bado hawajaweza kupata taarifa katika mahakama zote nchini na kuwataka watumishi wa mahakama wawasaidie kukusanya taarifa hizo.Kwa upande wa Mkurugenzi Mkazi wa benki ya Dunia, Bella Bird amesema mfumo huo huo mpya utasaidia kuwafikia wananchi wengi kwa urahisi zaidi.

Naye Mkuu wa Chuo cha Lushoto  Paul Kihwelu amesema kwa mara ya kwanza Mahakama imejenga kituo cha mafunzo ambacho ni msingi mzuri wa kuwepo kwa uhuru wa mahakama kwa kuwajengea uwezo watumishi.

"Mafunzo ya mwanzo ya tehama yatatolewa pia kwa wadau mbalimbali wakiwemo wanafunzi, Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru)" amesema.

TAFF YAMSHUKURU RAIS MAGUFULI KWA MSAADA WAKE WA MATIBABU YA MSANII WASTARA

MSEMAJI WA JESHI LA ZIMAMOTO,UOKOAJI NCHINI ATEMBELEA CHANNEL TEN

$
0
0
 Mwandishi wa habari na mtangazaji mwandamizi wa African Media group Ltd inayosimamia Vyombo vya utangazaji Channel ten na Magic Fm, Bw. Kibwana Dachi akifafanua jambo kwa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mkaguzi Joseph Mwasabeja (wa pili kulia) wakati wa ziara yake ya kujitambulisha tangu alipoteuliwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 29/01/2018.
 Msemaji Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mkaguzi Joseph Mwasabeja (katikati) akipata maelezo kutoka kwa mtangazaji mwandamizi wa Channel Ten na Magic fm, Kibwana Dachi katika studio za Channel Ten, (kushoto) ni Damian Muheya na Nasibu Mgosso (kulia) wakiwa ni Maafisa habari wa Jeshi hilo wakati wa ziara yake ya kujitambulisha tangu alipoteuliwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 29/01/2018.
 Mkuu wa Kitengo cha kurusha matangazo Channel Ten, Bw. Abdallah Lugisha akitoa ufafanuzi jinsi mitambo ya kurusha matangazo inavyofanya kazi kwa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mkaguzi Joseph Mwasabeja akiwa ameambatana na Maafisa habari wa Jeshi hilo wakati wa ziara yake ya kujitambulisha tangu alipoteuliwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 29/01/2018.
 Msemaji Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mkaguzi Joseph Mwasabeja akijibu swali kutoka kwa mtangazaji wa Magic Fm Salma Msangi katika kipindi cha Busati wakati wa ziara yake ya kujitambulisha tangu alipoteuliwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam mapema leo tarehe 29/01/2018. Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji).
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA - JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

Jafo Apiga Marufuku Madarasa ya Udongo na Tembe.

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halamshauri zote nchini kuhakikisha wanajenga madarasa yenye ubora na Viwango kuondokana na tatizo la baadhi ya Wilaya kuwa na majengo ya udongo na tembe.

Jafo ametoa agizo hilo leo Mjini Dodoma alipokuwa akifungua mafunzo ya uongozi ya siku tano kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi toka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara yanayondelea katika ukumbi wa Hazina mkoani humo.

"Sitaki kuona madarasa ya udongo, tembe na watoto kusomea nje, hakikisheni matumizi ya mapato ya ndani yanagusa na kujibu matatizo ya wananchi," alisisitiza Jafo.Jafo amewataka Wakuu wa Wilaya kuhakikisha matumizi ya mapato ya ndani katika Halmashauri zao yanatumika katika miradi mbalimbali ya wananchi ikiwemo ujenzi wa madarasa ili kuondokana na uwepo wa madara ya udongo na tembe katika halmashauri zote hapa nchi.

Aidha amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kufanya maamuzi ya haraka mara wanapopokea fedha za miradi ya maendeleo, kauli hii imetokana na baadhi ya wakurugenzi kuwa na uzembe katika kufanya maamuzi hivyo kuchelewesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilaya zao na Taifa kwa ujumla.


RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI MTEULE DKT. WILBROD,MAAFISA WAKUU WA JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WANAOTARAJIWA KUSTAAFU

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa kabla ya kuzungumza na wanahabaari Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam. 
  Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa akizungumza na Wanahabari mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari mara baada ya kufanya mazungumzo na Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari mara baada ya kufanya mazungumzo na Balozi Mteule Dkt. Wilbrod Slaa Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo kabla hajaanza kuwatambulisha Maafisa Wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (hawaonekani pichani) ambao wanatarajia kustaafu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo ambaye aliambatana na Maafisa Wakuu (sita)  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambao wanatarajiwa kustaafu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Maafisa Wakuu (sita) wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania  wanaotarajiwa kustaafu ambao ni Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania Luteni Jenerali James Mwakibolwa wanne kutoka (kulia), Meja Jenerali Michael Isamuhyo watatu kutoka (kulia) Brigedia Jenerali Aron Robert Lukyaa wapili kutoka (kulia), Kanali Peter Samuel Sameji wa kwanza (kulia).  Wengine katika picha ni Brigedia Jenerali William Ephraim Kivuyo wapili kutoka kushoto na Brigedia Jenerali Elizaphani Lutende Marembo. PICHA NA IKULU

RAIS Dkt Magufuli akutana na Maafisa Wakuu sita wa JWTZ wanaotarajiwa kustaafu

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo kabla hajaanza kuwatambulisha Maafisa Wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (hawaonekani pichani) ambao wanatarajia kustaafu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo ambaye aliambatana na Maafisa Wakuu (sita)  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambao wanatarajiwa kustaafu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Maafisa Wakuu (sita) wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania  wanaotarajiwa kustaafu ambao ni Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania Luteni Jenerali James Mwakibolwa wanne kutoka (kulia), Meja Jenerali Michael Isamuhyo watatu kutoka (kulia) Brigedia Jenerali Aron Robert Lukyaa wapili kutoka (kulia), Kanali Peter Samuel Sameji wa kwanza (kulia).  Wengine katika picha ni Brigedia Jenerali William Ephraim Kivuyo wapili kutoka kushoto na Brigedia Jenerali Elizaphani Lutende Marembo. PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI MKUTANO WA AU NCHINI ETHIOPIA

$
0
0
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amehudhuria katika Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli. Januari 29, 2018. 
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) na Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa (katikati) nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) na Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa (katikati) nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahi jambo na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mke wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mjumbe Maalum na Mwenyekiti wa Umoja wa Africa Nchini Sudan, Prof. Joram Biswaro, nje ya ukumbi wa Nelson Mandela mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU. Januari 29, 2018.

WAZIRI ATAKA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI KUPELEKA WATUMISHI TPSC KUPIGWA MSASA

$
0
0
Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Dkt.Henry Mambo (wa pili kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo huku Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt.(Mstaafu) George Mkuchika (wa tatu kushoto) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kukitembelea chuo hicho tawi la Singida mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Chuo cha utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) tawi la Singida, Sijali Kolojelo akisoma risala ya mafanikio na changamoto za TPSC tawi la Singida wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt.(Mstaafu) George Mkuchika (katikati) alipotembelea TPSC tawi la Singida mwishoni mwa wiki kushoto kwa Waziri wa ni Mkuu wa TPSC Dkt. Henry Mambo.
Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Dkt.Henry Mambo aliyesimama akisoma risala fupi ya makaribisho kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt.(Mstaafu) George Mkuchika aliyekaa mara baada ya kuwasili TPSC tawi la Singida mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya watumishi wa TPSC tawi la Singida na wageni wengine wakimsiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt.(Mstaafu) George Mkuchika (hayupo pichani) mara baada ya kuwasili TPSC tawi la Singida mwishoni mwa wiki.

Wananchi Wapongeza Tanzania Kutajwa Kinara Uchumi Shirikishi

$
0
0
Wananchi Mkoani Dodoma wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali katika Kujenga uchumi shirikishi unaogusa maisha ya wananchi baada ya Tanzania kutajwa na Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum) kuwa nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara kuwa na uchumi Jumuishi.

Akizungumza katika Mahojiano maalum mjini Dodoma Bibi Anyangwe Lupembe amesema ni jambo la kupongeza kwa hatua hiyo kwani haya ni matunda na juhudi kubwa zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kama ujenzi wa reli wa reli ya Kisasa (Standard Gauge) na Uzalishaji umeme.

Akifafanua Lupembe amesema kuwa kila mwananchi kwa sasa anaelewa kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuwahudumia wananchi wanyonge kwa kuhakikisha kuwa huduma muhimu zinapatikana kama Madawa, Elimu, miundo mbinu hali inayowapa fursa wananchi kushiriki katika shughuli za uchumi ikiwemo uzalishaji kutokana na mazingira wezeshi yaliyopo kwa sasa.

Aliongeza kuwa kasi ya ujenzi wa miundombinu kama barabara inawawezesha wananchi kushiriki katika uzalishaji na shughuli za maendeleo katika maeneo mbalimbali hapa nchi, hivyo uchumi kumilikiwa na wananchi.

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images