Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu MAJALIWA amwakilisha Rais Magufuli Mkutano wa Viongozi Wakuu Nchi za Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Comoros, Azali Assoumani, kwenye ndege ya shirika la Ethiopian Airline, wakiwa safarini kueleke Ethiopia, katika Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU, Waziri Mkuu, anamwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahigawakati alipo wasili kwenye uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Addis Ababa, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU Nchini Ethiopia. Januari 28, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Afrika KusiniJacob Zumakwenye hafla ya miaka 100 ya kumkumbuka Rais wa kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisainiwa kitabu cha kumbukumbu, cha Rais wa kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na Rais wa Afrika KusiniJacob Zumakwenye hafla ya miaka 100 ya kumkumbuka Kiongozi huyo, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS DKT. MAGUFULI ASALI IBADA YA JUMAPILI KANISA KATOLIKI LA MTAKATIFU PETRO JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishukuru mara baada ya kushiriki Sakramenti Takatifu katika Ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishukuru kwa kusali pamoja na Mke wake Mama Janeth Magufuli, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa mara baada ya wote kwa pamoja kushiriki Sakramenti Takatifu katika Ibada ya Jumapili iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Wanakwaya kutoka Chuo cha Ardhi jijini Dar es Salaam wakiimba kwenye Ibada hiyo ya Jumapili ilifanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Paroko Msaidizi wa Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Fr. Asis Mendokta akihubiri katika Ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua Nakala za CD ya kwaya kutoka Chuo cha Ardhi mara baada ya Ibada. Kushoto ni Mke wake Mama Janeth Magufuli akifurahia.
PICHA NA IKULU

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU ATEMBELEA GHALA LA KUHIFADHI VIFAA VYA MAAFA DODOMA

$
0
0
Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Tafiti) Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Bashiru Taratibu akitoa maelezo kuhusu ghala la kuhifadhi vifaa vya maafa kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora alipotembelea kuangalia hali ya ghala hilo.Afisa Ugavi Hospitali ya Mkoa wa Dodoma Bw. James Mashaka akionesha moja ya kifaa cha kuhifadhi maji wakati wa maafa (Collapse can jelly) kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora alipotembelea Ghala la kuhifadhi vifaa vya Maafa.Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akifuatilia maelezo ya ghala la kuhifadhia vifaa vya maafa kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Tafiti) Idara ya Uratibu wa Maafa Bw. Bashiru Taratibu alipotembelea kukagua hali ya ghala hilo.Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akifuatilia baadhi ya taarifa zinazohusu ghala la kuhifadhi vifaa vya maafa lililopo Dodoma.Muonekano wa moja ya Ghala la kuhifadhi Vifaa vinavyotumika wakati wa Maafa lililopo Dodoma.

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA,SERIKALI ZA MITAA YAPONGEZA UJENZI HOSPITALI WILAYA YA KILOLO

$
0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imepongeza ujenzi wa majengo mbalimbali ya kutolea huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.

Kamati hiyo imetoa Pongezi hizo wakati walipotembelea Kilolo na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali hiyo.Wabunge wamepongeza kazi inayofanywa na wakandarasi kwani ipo katika ubora mzuri na kiwango cha kuridhisha.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Mwanne Mchemba aliyeongoza Waheshimiwa hao amesema “naipongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, uongozi na watumishi kwa ujumla kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, ujenzi ni wa kiwango cha juu na thamani ya fedha inaonekana”.

Kamati imeagiza Halmashauri kuhakikisha inakamilisha majengo yote kwa wakati ili huduma ianze kutolewa mara moja.Ameongeza kuwa ni vizuri kipindi hiki ambacho ujenzi unaendelea Halmashauri ijipange kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba, vitendanishi na dawa pamoja na kuajiri watumishi.

Naye Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege ameziagiza Halmashauri zote nchini ambazo hazina Hospitali za Wilaya zianze taratibu za ujenzi mara moja ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini.

Hadi sasa ujenzi uliofanyika ni wa majengo matano ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje; jengo la maabara; jengo la huduma ya mionzi; jengo la huduma ya afya ya uzazi na mtoto; na jengo la wagonjwa wa ndani. Ujenzi wa majengo haya hadi kukamilika unatarajia kutumia kiasi cha fedha shilingi bilioni 4.4.

Aidha, mradi mzima wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo utagharimu Tsh. Bil 12.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa ikiwasili katika Hospital ya Kilolo kukagua ujenzi wa Hospital ya Wilaya.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa ikipokea Taarifa ya Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Kilolo ilipofanya ziara ya Ukaguzi wa Katika Mradi huo.
Huu ndio muonekano wa Sehemu ya Jengo la Hospital ya Wilaya ya Kilolo inayoendelea kujengwa.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat Kakunda(Pili Kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikalinza Mitaa wakati wa Ziara katika Mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Kilolo.

WAZIRI MKUCHIKA AVUTIWA NA MIRADI YA TASAF

$
0
0
Estom Sanga-Singida 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mhe. George Mkuchika amepongeza hatua ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kubuni utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wananchi katika ujenzi wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao. 

Mhe. Mkuchika amesema utaratibu huo siyo tu kwamba unapunguza gharama bali unawafanya wananchi kuithamini miradi hiyo na kuitunza kutokana na kutumia nguvu na jasho lao katika kuitekeleza. 

Waziri huyo ameyasema hayo mwishoni mwa juma baada ya kutembelea kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida ambako alikagua jengo la zahanati lililojengwa na TASAF kwa kuwashirikisha wananchi kijijini hapo. 

Aidha Mhe. Mkuchika ameupongeza mkoa wa Singida kwa kusimamia zoezi la uandikishaji Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kwa uaminifu na hivyo kupunguza kwa kiwango kikubwa idadi ya Watu wasiostahili kujumuishwa kwenye Mpango huo kinyume cha utaratibu. 
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akitoka katika jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida lililojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo. 
Mwonekano wa jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida iliyojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo ikiwa ni mkakati wa TASAF wa kuboresha huduma za Afya kwa walengwa wake na wananchi wa eneo hilo. 
Waziri Mkuchika akipanda mche wa mti katika eneo la Zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida iliyojengwa na TASAF na wananchi . 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika (aliyesimama mbele ya kamera) akiwahutubia baadhi ya watumishi wa sekretarieti ya mkoa wa Singida wakati alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. 
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akikagua jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika wilaya ya Singida jengo lililojengwa na TASAF ikiwa ni mkakati wa kuwasogezea huduma ya Afya wananchi na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.



NDOA ZA UTOTONI BADO NI TATIZO KUBWA TANZANIA NA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Na,Jumbe Ismailly SINGIDA 

TATIZO la ndoa za utotoni katika Tanzania na nchi za Afrika Mashariki limeonekana ni tatizo kubwa sana katika maeneo hayo ambapo kitakwimu inaonyesha kuwa kati ya mikoa kumi bora Mkoa wa Shinyanga unaongoza kwa kuwa na asilimia 59 na Mkoa wa Singida umeshika nafasi ya nane kwa kuwa na asilimia 42.

Meneja wa Shirika la kidini lisilokuwa la kiserikali la World Vision Tanzania (WVT) Kanda ya kati,Faraja kulanga aliyasema hayo kwenye uzinduzi wa mpango wa kutokomeza mimba za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.

Alifafanua kwamba kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Tanzania Demokratic Health Survey ya mwaka 2010 inaonyesha kitakwimu kwamba tatizo la ndoa za utotoni,Mkoa unaoongoza ni Mkoa wa Shinyanga wenye asilimia 59 huku Mkoa wa Singida ukiwa na assilimia 42 na hivyo kushika nafasi ya nane katika mikoa hiyo kumi bora.

“Kwa maana kwamba ule utafiti huwa unakwenda kuuliza kila nyumba na wakiuliza katika kila nyumba mama alipata ujauzito katika umri gani,wale waliopata mimba katika umri chini ya miaka 18 ilikuwa ni asilimia 59.”alifafanua Kulanga.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Eliasi Tarimo alipokuwa akizindua mpango wa mapambano dhidi ya ndoa za utotoni kwenye ukumbi wa Kanis Katoliki,mjini Singida.
baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa semina ya mapambano dhidi ya ndoa za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki,mjini Singida. 
baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa semina ya mapambano dhidi ya ndoa za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki,mjini Singida. 
Meneja wa World Vision Tanzania (WVT) Kanda ya kati,Faraja Kulangwa akiwasilisha mada juu ya madhumuni ya semina hiyo kwa wananchi waliohudhuria kwenye ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.


SERIKALI KUPIMA MAENEO YAKE YOTE MWAKA HUU KUEPUSHA MIGOGORO NA WANANCHI

$
0
0
Na. Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi amezitaka Wizara, Taasisi za Serikali na Vyombo vyote vya Umma kupima maeneo yao na kuyawekea alama za mipaka ili kuepusha maeneo hayo kuvamiwa na wananchi.

Waziri Lukuvi amesema hayo mara baada ya kukagua maeneo yaliyo na migogoro ya ardhi katika manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Aidha Mheshimiwa Lukuvi akiambata na Naibu wake ambaye ni mbunge wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza walitembelea maeneo yaliyovamiwa na wananchi ya Polisi Kigoto-Kirumba lililovamiwa na wananchi, Uwanja wa Ndege wa Mwanza na eneo la Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Nyamirolerwa katika manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kutokana na kujionea uvamizi huo wa maeneo hayo, Waziri Lukuvi amezitaka taazizi zote za serikali kupima maeneo yao ili wananchi waweze kutambua maeneo ya Serikali wasiweze kuyavamia jambo ambalo huzaa migogoro.

Hata hivyo Waziri Lukuvi amewataka wananchi waliojenga ndani ya hifadhi ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuondoa maendelezo yao ndani ya siku saba kabla kuchukuliwa hatua kwakuwa ni wavamizi na hawaruhusiwi kukaa karibu na eneo linalorusha na kutua vyombo vya anga jambo ambalo ni hatari kwao na usalama wa vyombo hivyo.

"Hawa waliojenga ni wavamizi na watambue hivyo majibu tutatoa badaye nini tutafanya lakini wajue maisha yao siyo ya hapo ndani ya uwanja," alisema lukuvi.Na katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi William Lukuvi amezitaka halmashauri zote nchini kukamilisha zoezi la ukusanyaji wa kodi ya Ardhi kabla ya tarehe 30 mwezi Aprili mwaka huu.

CHUO CHA KODI KUWAJENGEA UWEZO MAWAKALA WA FORODHA ZANZIBAR

$
0
0
Na Oliver Njunwa- Dar es Salaam

Chuo cha Kodi (ITA) pamoja na Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB), vimeingia katika makubaliano ya kushirikiana katika kuwajengea uwezo Mawakala wa Forodha Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya hafla fupi ya kutiliana saini makubaliano hayo, iliyofanyika hivi karibuni katika Chuo cha Kodi jijini Dar es salaam, Mkuu wa Chuo hicho Prof. Isaya Jairo amesema kwamba, makubaliano hayo ni muhimu kwani kila upande una watalaam wa kutosha kuwasaidia Mawakala wa Forodha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“ITA inajivunia utaalam wake wa kufundisha na ZFB ina utaalamu katika masuala ya kiforodha. Kwa hiyo wote kwa pamoja tutashirikiana ili malengo ya makubaliano haya yaweze kufikiwa”, alisema Prof. Jairo.

Prof. Jairo aliongeza kuwa, katika makubaliano hayo, Chuo cha Kodi kitatoa mafunzo ya muda mfupi na utaalamu wa masuala ya forodha kwa ZFB ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na Mawakala wa Forodha wanaofanya kazi kwa weledi.

Mkuu wa Chuo cha Kodi pia amesema kwamba lengo la vyuo sio kupata fedha bali kutoa wataalamu wa kutosha ambapo uwezo wa Chuo hupimwa kwa idadi ya wanafunzi wanaohitimu na aina ya sifa walizonazo.

Aidha, Prof. Jairo ameiomba ZFB kulinda hadhi ya jina la Chuo cha Kodi kwani kina jina zuri kutokana na uzoefu wake wa kutekeleza makubaliano ya ushirikiano na taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB) Omar Hussein Mussa wakibadilishana hati za makubaliano ya ushirikiano katika kuwajengea uwezo wanachama wa ZFB.
Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar Omar Hussein Mussa wakizungumza na wajumbe wa Kamati ya Makubaliano kutoka Chuo cha Kodi (Kulia) na Zanzibar (kushoto) kabla ya kusaini hati za makubaliano katika chumba cha mikutano ITA.
Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB) Omar Hussein Mussa (wa pili Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala Tanzania (TAFFA) Stephen Ngatunga (wa kwanza kulia) katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ushirikiano mara baada ya kusaini makubaliano ya kuwajengea uwezo mawakala wa Forodha Zanzibar. (PICHA ZOTE NA OLIVER NJUNWA).




WACHEZAJI 12 GOLF LUGALO WAAANZA VYEMA MWAKA 2018

$
0
0
Wapiga golf 12 akiwemo aliyekuwa Mkuu wa majeshi ya Ulinzi jenerali Mstaafu George Waitara wameanza vyema mwaka kwa kuibuka washindi katika michuano ya Golf inayofanyika kila baadaya Miezi Mitatu ambapo kwa mwaka 2018 ndio ya kwanza.

Katika mashindano hayo yaliyokuwa na msisimko na kushirikisha wacheza golf 73 kutoka katika makundi matano ambayo ni Watoto(Juniors), Seniors, Wanawake Divisheni A, B na C huku idadi kubwa ya wanawake wakiendelea kujitokeza.

Katika kundi la Divisheni A Mshindi aliiibuka Seif Mcharo ambaye ni miongoni mwa Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Golf baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 71 akifuatiwa na Kapteni Kibuna Shaabani aliyepata Mikwaju ya Jumla 74 huku Divisheni B Mshindi akiibuka Likuli Juma Baada ya Kupata mikwaju ya Jumla 70 akifuatiwa na Michael Lotich aliyepiga 74.

Kwa Upande wa Kundi C Sajini Taji John Msey aliibuka mshindi baada ya kupata Mikwaju ya Jumla 76 akifiuatiwa na Balozi Sai Kapale aliyepiga mikwaju ya Jumla 81 wakati katika kundi la wanawake Habiba Juma aliibuka Mshindi na kueneleza historia ya yake ya kufanya vyema baada ya kupiga mikwaju ya jumla 76 na kumshinda Mwenzie Lilian Mwaulambo kwa Count Back baada ya kufungana kwa Mikwaju 76.

Katika kundi la Senior Jenerali Mstaafu George Waitara alibuka mshindi Baada ya kupata net ya 72 akifuatiwa na Brigedia Jenerali Mstaafu Julius Mbilinyi aliyepata Net ya 76 huku katika kundi la Watoto Zabron Hamis aliibuka mshindi kwa mikwaju ya jumla 70 na kufuatiwa na Karimu Ismail aliyepiga 74.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu ya Golf ya Lugalo Brigedia jenerali Mstaafu Michael Luwongo alisema ni mashindano ya kwanza kwa mwaka 2018 lakini yameweza kuitoa Dira ya mwelekeo wa Wachezaji.

Pia aliahidi kuendelea kuwekeza katika kuibua Wachezaji wapya na kuendeleza waliopo ikiwemo kuhakikisha wanashiriki Michuano mbalimbali ya Kimataifa na Kitaifa na kiletea heshma nchi na klabu ya jeshi ya Lugalo.

Brigedia Jenerali Mstaafu Luwongo aliwataka wanachama wa klabu hiyo kuendelea kuwa wanachama wenye nidhamu kama ilivyo ada ili kufanikiwa kuyafikia malengo yaliyokusudiwa.

WAKULIMA SKIMU YA UMWAGILIAJI MPUNGA NYAMAGOGO MANYONI WALALAMIKIA HALMASHAURI KUTELEKEZA KATAPILA

$
0
0
Na Jumbe Ismailly-Manyoni 

WAKULIMA wa skimu ya umwagiliaji mpunga ya Nyamagogo,iliyopo katika Kijiji cha Chikuyu,wilayani Manyoni,Mkoani Singida wameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kuitengeneza katapila lililokuwa likisaidia kusafisha mifereji ya kuoitisha maji kwenye mashamba hayo ili waweze kuongeza uzalishaji wa zao hilo ambao kwa sasa umepungua.

Mwenyekiti wa skimu hiyo ya umwagiliaji Nyamagogo,Abdallah Rajabu Maganga alisema katapila hilo ambalo limetelekezwa tangu mwaka 2012 kutokana na kukosekana kwa vipuli vinavyohitajika kulifufua kwa sababu kifaa hicho ni aina ya kizamani na hivyo matengenezo yake siyo rahisi na badala yake lingefaa kuuzwa kwa njia yam nada.

“Tatizo wanavyosema sema ni greda la kizamani unaona bwana spea zake hazipatikani sasa tunajiuliza wanaproses kwamba wanataka kuliuza unaona bwana sasa huyo unayemuuzia atalifanyia nini kama kweli ni greda la zamani ambapo hakauna spea”alifafanua Maganga.

Alifafanua mwenyekiti huyo wa (WAUWA) kwamba ili kuwasaidia wakulima wa zao hilo na kwa sababu sasa hivi dunia ni ya utandawazi spea zinapatikana sehemu yeyote pale hata kama Marekani wanaweza kwenda au kuagiza ili liweze kutengenezwa kwa manufaa ya wakulima hao wa skimu ya umwagiliaji.
baadhi ya Skimu za umwagiliaji mashamba ya mpunga Nyamagogo,wilayani Manyoni,Mkoani Singida yaliyoathirika kutokana na kujaa kwa maji ambayo hupeleka na mchanga na kusababisha mto kuwa juu na kuanza kukata mikato,kwa sababu ya kukosekana kwa katapila litakalotoa michanga na maji kufuata mkondo wake unaokubalika badala ya hivi sasa ambapo maji mengi yanapotea bure huku kipato chao kikishuka. 
baadhi ya mitaro iliyojaa mchanga pamoja na takataka na hivyo kusababisha maji kukosa mwelekeo na hivyo kusambaa ovyo kwenye maeneo mengine.
Katapila lililokuwa likiwasaidia wakulima wa skimu ya umwagiliaji mpanga Nyamagogo,wilayani Manyoni,Mkoani Singida kutojaa kwa maji ambayo hupeleka mchanga na kusababisha mto kuwa juu na kuanza kukata mikato,kwa sababu ya kukosekana kwa katapila litakalotoa michanga na maji kufuata mkondo wake unaokubalika badala ya hivi sasa ambapo maji mengi yanapotea bure huku kipato chao kikishuka.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).

KAMISHNA JENERALI MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATETA NA MAHABUSU GEREZA KEKO MAADHIMISHO WIKI YA SHERIA NCHINI

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiongea na Mahabusu wa Gereza Keko(awapo pichani) leo Januari 28, 2018 alipotembelea gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini.
 Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah akitoa taarifa fupi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa kabla ya kumkaribisha kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko(hawapo pichani).
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimsikiliza Mahabusu ambaye ni raia wa kigeni mara baada ya kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akikagua jiko la gesi katika Gereza la Mahabusu Keko. Jeshi la Magereza tayari limeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuachana na matumizi ya kuni kwa kutumia nishati ya gesi katika baadhi ya magereza nchini hivyo kutunza mazingira.

RAIS DKT MAGUFULI ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU JAJI MSTAAFU ROBERT KISANGA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Januari, 2018 ametia saini kitabu cha maombolezo na kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga (pichani) nyumbani kwa marehemu Oysterbay Jijini Dar es Salaam. 
Mhe. Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pia wametoa mkono wa pole kwa mke wa Marehemu Mama Maria Kisanga na kufanya maombi ya pamoja na familia ya marehemu. 
Jaji Mstaafu Robert Kisanga alifariki dunia tarehe 23 Januari, 2018 katika hospitali ya Regency Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa  Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 208.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakifanya maombi pamoja na mjane wa marehemu Mama Maria Kisangana mtoto wa marehemu Amani Kisanga na waombolezaji wengine baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  

NG'OMBE 341,098 WAPIGWA CHAPA SIMANJIRO

$
0
0
Ng'ombe 341,098 wamepigwa chapa Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ili kutekeleza agizo la Serikali la upigaji chapa mifugo kwa ajili ya utambuzi na kuepuka migogoro ya mara kwa mara. 

Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Zuwena Omary, aliyasema hayo juzi wakati akisoma taarifa kwa mkuu wa mkoa huo Alexander Mnyeti. Omary alisema lengo la wilaya hiyo ni kupiga chapa ng'ombe 437,925 hivyo wamefikia asilimia 79 hadi kufikia Desemba 31 mwaka jana. 

Alisema zoezi hilo lilitarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka jana ila baada ya serikali kuongeza muda hadi Januari 31 mwaka huu, watakuwa wamefanikiwa kukamilisha. Alisema wilaya hiyo ina mabwawa mawili ya Nyumba ya Mungu na Kidapash, ambayo shughuli za uvuvi zinafanyika na jitihada za kudhibiti uvuvi haramu zimefanyika. 

Kwenye sekta ya kilimo, umwagiliaji na ushirika alisema kuna ekari 346,000 zinazofaa kwa kilimo ambapo takribani ekari 144,00 hutumika kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara. "Mahitaji ya chakula kwa mwaka kwa wakazi wote ni tani 42,000 za nafaka na hali ya chakula ni ya kuridhisha kwenye maeneo mengi kwani wananchi wanatumia chakula kilichovunwa msimu wa Kilimo wa 2016/2017. 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti (wapili kulia) baada ya kupewa zawadi ya nguo ya jadi na wafugaji wa kata ya Naisinyai kwenye ziara yake Wilayani Simanjiro, kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Jackson Leskar Sipitieck na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Arnold Msuya. 



Mkazi maili 35 amuomba waziri wa afya msaada aokoe maisha ya mwanae

$
0
0
Bi Flora Liberia (33) akiwa yupo na mwanae Samweli Amos miaka (2)akiwa nyumbani kwake Maili 35 kata ya Visiga Halmashauri ya mji wa Kibaha mkoa wa Pwani.Picha na Vero Ignatus Blog.


Na.Vero Ignatus Pwani.

MKAAZI wa eneo la Maili 35 Kata ya Visiga katika Halmashauri ya Kibaha Mjini Bi Flora Liberia (30) ameelezea masikitiko yake kutokana na kutaabika na ulezi wa mtoto wake Amos Samwel mwenye umri wa miaka miwili na nusu ambaye tangu alipozaliwa viungo vyake havijakaza, hali iliyosababisha kukumbana na muuguzi aliyedai kuwa ni mfanyakazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambaye amekuwa akimlaghai na kutumia fedha zake kwa madai kuwa atamsaidia kumpatia matibabu mtoto huyo.

Ameongeza kwa kusema yeye hana ajira hivyo hulima vibarua vinavyomuwezesha kupata ujira mdogo ambao hujichangisha ili aweze kumpatia matibabu mtoto wake, ambaye tangu alipomzaa viungo vyake havijawahi kuwa imara kama ilivyo kwa watoto wengine anazungumza hayo kwa masikitiko .

Bi Flora ameomba msaada kutoka kwa Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Ummy Mwalimu ili kuweza kuokoa maisha ya mtoto wake.
Mtoto Samweli Amos miaka( 2) alizaliwa 2015 1/3 Zahanati ya mlandizi iliyopo Kibaha mkoa wa Pwani,akiwa ameketishwa katika kiti walichotengeneza wazazi kwa ajili ya kumketisha mtoto huyo kama inavyoonekana hapo.Picha na Vero Ignatus Blog.
Wa kwanza kushoto ni baba mzazi wa mtoto samweli ,Amos Hussein (39 mwenyeji wa Morogoro katikati ni Samwel Amos (2) wa kwanza kulia ni mama yake Flora Liberia (33 ) mwenyeji wa Kigoma,ila kwa sasa wanaishi mtaa mail 35 kata ya Visiga Halmashauri ya mji wa Kibaha mkoa wa Pwani.Picha na Vero Ignatus Blog.

Rais Shein Ahudhuria Chakula cha Mchana na Vijana wa Halaiki

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakijumuika na Vijana na Wanafunzi walioshiriki katika Halaiki ya kuadhimisha Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar
BAADHI ya Wanafunzi na Vijana walioshiriki katika sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar, wakijumuika katika hafla ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,kilichofanyika katika viwanja vya Vikosi vya KVZ Mtoni Zanzibar
BAADHI ya Vijana na Wanafunzi walioshiriki katika sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika viwanja vya Amaan Zanzibar
BAADHI ya Viongozi wa Halaiki wakiwa katika viwanja vya Vikosi SMZ wakishiriki katika hafla ya kuadhimisha Miaka 54 ya Mapinduzi Zanzibar.
BAADHI ya Wanafunzi na Vijana walioshiriki sherehe za maadhimisho ya Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar wakishiriki katika hafla ya chakula maalum cha mchana kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, katika kambi ya KVZ Mtoni Zanzibar.


BALOZI SOKOINE AKUTANA NA WATANZANIA UBELGIJI

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchi Ubelgiji Mh:Edward Joseph Sokoine katikati akiwa na baadhi ya watanzania waliofika jana kwenye kikao cha kusikiliza na kutafutia ufumbuzi kero za watanzania wanaoishi nje ya  Tanzania. {Picha zote na Maganga One Blog} 
Kiongozi wa Watanzani kitongoji cha Antwerpen nchini Ubelgiji ndugu Joseph Makani akimkaribisha Mh Balozi na maafisa Ubalozi alioambatana nao hapa jana,kutoka kushoto ni Afisa Ubalozi ndugu Shoo na upande wa kulia ni afisa ubalozi ndugu Juma Salum.Kikao kilikwenda vizuri kwani kila mmoja alipewa fursa ya kuuliza maswali. {picha zote na Maganga One Blog} 
Afisa Ubalozi ndugu Juma Salum{kulia}akitoa ufafanuzi wa swali aliloulizwa kuhusu maswala ya hati za kusafiria pindi mtu anapotaka kurudi nyumbani,alielezea kwa kirefu taratibu zinazotakiwa kufuatwa ili mtu kuepuka usumbufu. 
Mh Balozi akimsikiliza mmoja wa watanzania ndugu Omari Songambele {hayupo pichani}aliyetaka ufafanuzi kuhusu Uraia Pacha. 
Baadhi ya kina mama wa Kitanzania na nchi jirani walihudhuria mkutano uliowakutanisha na Balozi Sokoine 

Tanzania Yatabiriwa Makubwa Uchumi Jumuishi

$
0
0

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bibi. Bengi’i Issa akizungumza kuhusu katika mahojiano maalumu kuhusu kungara kwa Tanzania katika ukuaji wa uchumi jumuishi miongni mwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara jana jijini Dar es Salaam. (Picha na: MAELEZO).

JAJI MKUU AWATAKA WATUMISHI KUONGEZA IMANI YA MAHAKAMA

$
0
0
Na Lydia Churi-Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewataka Watumishi wa Mahakama nchini kutoa huduma kwa kuzingatia Maadili, kuhakikisha kesi zinamalizika kwa wakati pamoja na kuacha vitendo vya rushwa ili kuongeza imani ya wananchi kwa Mhimili huo.

Akizindua wiki ya Sheria na Maonesho ya Elimu ya Sheria leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Jaji Mkuu alisema kuwa nguvu ya Mahakama ni imani ya wananchi na imani hiyo itaongezeka ikiwa hakuna rushwa, kuna maadili mema na kesi zitamalizika kwa wakati.

Jaji Mkuu pia amewataka wananchi kuacha kuilalamikia Mahakama na badala yake wachukue hatua kwa kuwataja watumishi wasiozingatia maadili kwa uongozi wa Mahakama.Aidha, amewashauri wananchi kujifunza na kuelewa taratibu za mashauri Mahakamani ili kurahisisha upatikanaji wa haki zao wanapozitafuta kwenye Mahakama mbalimbali nchini.

“Wananchi wengi wanakwenda kutafuta haki sehemu isiyohusika hivyo wanatakiwa kujifunza taratibu za Mahakama ili waweze kupata haki kwa wakati kwa kuwamuda mwingi unapotea kwa kutafuta haki mahali pasipostahili”, alisema Prof. Juma.Alisema hivi sasa Mahakama inaingia kwenye matumizi ya Teknolojia ya habari na Mawasiliano- TEHAMA hivyo matumizi haya yatamsaidia mwananchi kuweza kufahamu hatua zote za shauri lake lililopo Mahakamani.

Jaji Mkuu ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya Mnazi Mmoja ili kupata elimu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Mahakama na sekta ya sheria kwa ujumla.

Alisema, katika maonesho hayo, wananchi watapata nafasi ya kujifunza juu ya usuluhishi nje ya Mahakama, Mahakama inayotembea (Mobile Courts) pamoja na changamoto za upatikanaji wa haki zikiwemo upungufu wa Watumishi, Miundombinu, pamoja na vifaa.Akizungumzia taratibu wa usuluhishi wa kesi nje ya Mahakama (Mediation), Jaji Mkuu amesema wakati sasa umefika kwa wananchi kutumia utaratibu huo unaorahisisha upatikanaji wa haki na kuongeza kuwa Haki bora hupatikana kwa usuluhishi majumbani.

Aidha, kabla ya kuzindua wiki ya Sheria, Jaji Mkuu aliongoza Matembezi waliyowashirikisha watumishi wa Mahakama, wadau pamoja na wananchi kwa ujumla yaliyoanzia katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mpaka viwanja vya Mnazi Mmoja.

Matembezi hayo pia yalihudhuriwa na viongozi wa Serikali akiwemo Waziri wa wakati katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo Prof. Sifuni Mchome pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma akijiandaa kuanza Matembezi ya uzinduzi wa wiki ya Sheria leo jijini Dar es salaam. Kulia kwake ni mkewe akifuatiwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu na kushoto ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome pamoja na Askofu wa Kanisa la Anglican Nchini.
Gari linaloonesha Mfano wa Mahakama inayotembea. Hivi karibuni Mahakama ya Tanzania itaanzisha Mahakama zinazotembea (Mobile Courts) ili kupunguza mlundikano wa kesi Mahakamani.
Jaji Mkuu akiwa ndani ya gari hilo 

NEEC KUENDELEA KUWAWEZESHA WATANZANIA KUSHIRIKI SHUGHULIZA UCHUMI

MAGAZETI YA JUMATATU LEO JANUARY 29,2018

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images