Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110104 articles
Browse latest View live

MBUNGE MGIMWA:WATENDAJI KAMATENI WAZAZI WOTE AMBAO HAWAWAPELEKI WATOTO WAO SHULE

$
0
0
Na Fredy Mgunda,Mufindi. 


Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini amewataka viongozi wa vijiji na kata kuwachukulia hatua za kisheria wazazi wote ambao hawataki kuwapele shule watoto wao wakifaulu mitihani ya shule ya msingi kwenda shule ya sekondari. 

Akizungumza na blog hii mbunge Mahamuod Mgimwa alisema kuwa sasa imefika mwisho kwa watoto wa jimbo la Mufindi Kaskazini kuwa soko la wafanyakazi wa kazi za ndani wakati wanauwezo wa kuwa viongozi hapo baadae.

“Nasema tena haiwezekani kila mfanyakazi ukifika daresalaam utasikia katoka Iringa jimbo la Mufindi Kaskazini sasa sitaki kusika swala hilo na wazazi wanaofanya hivyo nitawachulia hatua za kisheria serikali ya awamu ya tano inataka kuwa na wasomi wengi ili kuasaidia maendeleo ya nchi”alisema Mgimwa

Mgimwa alisema kuwa wazazi wa jimbo la Mufindi la Mufinda watafungwa kwa kuwapeleka watoto wao kufanya kazi za ndani pindi wamalizapo shule ya msingi au sekondari kufanya hivyo kunadumaza maendeleo yao.

“Haiwezekani mwanafunzi amefaulu halafu mzazi anampeleka kufanya kazi za ndani siwezi kukubali hata kidogo maana nimegundugua wazazi wengi hawapendi watoto wao waendelee kusoma badala yake wanataka wakafanye kazi za ndani narudia kusema mtoto akifaulu asipopelekwa shule nitamchulia hatua za kisheria huyo mzazi” alisema Mgimwa.
Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahamuod Mgimwa akizungumza na viongozi wa kata ya Kibengu kuhusu maswala mbalimbali ya kimaendeleo sambamba na kutoa maagizo mbalimbali ambayo yatasaidia kuchochea maendeleo ya kata ya hiyo na jimbo hilo kwa ujumla
Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahamuod Mgimwa na viongozi wengine wakisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya kata ya Kibengu
Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahamuod Mgimwa akiangalia moja ya mradi wa ujenzi wa vyoo 
Diwani wa kata ya Kibengu Zakayo Kilyenyi akiwa na viongozi wa kata ya hiyo mara baada ya kutoka kwenye kikao na mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini.



Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akagua Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.

$
0
0
Shirika la Umeme Tanzania limeagizwa kumchukulia hatua Mkandarasi ambaye ni kampuni ya wazawa ya JV State Grid Electrical & Technical Works Ltd aliyekuwa akitekeleza Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Pili (REA II) Mikoa ya Mbeya na Songwe kwa kushindwa kukamilisha katika baadhi ya maeneo kwa mujibu wa makubaliano.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ametoa agizo hilo Januari 5, 2018 kwenye mkutano na wananchi wa Kijiji cha Utengule Usongwe, Mbeya Vijijini alipokuwa kwenye ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Umeme Vijijini.

Mgalu alitoa agizo hilo kufuatia taarifa ya Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Benedict Bahati ambaye alimueleza kuhusu kampuni hiyo iliyokuwa ikitekeleza Miradi katika Wilaya za Mbarali, Rungwe, Kyela na Ileje kushindwa kukamilisha miradi yake kama ilivyopaswa kulingana na mkataba. 

Alisema Serikali haitowafumbia macho Wakandarasi walioshindwa kukamilisha utekelezaji wa Miradi waliyokabidhiwa kwa mujibu wa makubaliano na aliliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikisha Mkandarasi huyo anapatikana na hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yake kwa mujibu wa makubaliano ya awali.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Utengule Usongwe, Mbeya Vijijini (hawapo pichani) alipokuwa kwenye ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Utengule Usongwe, Mbeya Vijijini wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) akimsikiliza Mbunge wa Mbeya Vijijini, Oran Njeza (kulia aliyesimama) wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Utengule Usongwe, Mbeya Vijijini (hawapo pichani) alipokuwa kwenye ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Mtinika (aliyesimama) akizungumza wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa tatu kushoto waliokaa) ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akiagana na Mbunge wa Mbeya Vijijini, Oran Njeza (kulia) mara baada ya kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Utengule Usongwe, Mbeya Vijijini wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Mbeya. Kushoto ni Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Benedict Bahati.

WANANCHI WA BUCHI-MBWERA WILAYANI KIBITI MKOA WA PWANI KUPATA DARAJA LA KUDUMU

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, Kibiti.
Wananchi wa Kata ya Mbuchi Tarafa ya Mbwera Wilayani Kibiti  mkoa wa Pwani kwa kipindi kirefu wametaabika na adha ya kukosa Daraja linalounganisha vijiji hivyo viwili vyevye wakazi zaidi ya elfu 24.
Kukosekana kwa Daraja hilo kumepelekea kukatika kwa mawasiliano ya Uhakika baina ya wananchi wa Mbuchi na wale wa upande wa Pili wa Bwera, kuongeza gharama za maisha na hata kupelekea maafa kwa wakina mama wanaojifungua na wagonjwa kwa sababu ya kukosa njia rahis na nafuu ya kuwafikisha katika huduma za Matibabu.
Vijiji hivyo ambavyo vimetengenishwa na Mto Mberambe ambao ni Tawi la Mto Rufiji na kutengeneza Delta ya Kaskazini tangu kuanzishwa kwake havijawahi kuwa na Daraja la kuwaunganisha katika shughuli zao za kila siku za kila siku za kujiletea Maendeleo.
Wananchi wa maeneo haya wamekuwa wakitumia Mitumbwi kuwavusha kutoka eneo moja hadi Lingine na huku wakitozwa Tsh 200 kwa safari moja na Pikipiki kutozwa Tsh 1000 kwa safari; Huduma hiyo hupatikana kuanzia saa kumi ba mbili asubuh hadi saa kumi na mbili jioni.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(katikati) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng.Evarist Ndikilo na viongozi wengine wa Mkoa huo wakati wa ziara yake ya kuweka jiwe la msingi katika Daraja la Mbuchi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akimpa MKandarasi maelekezo juu ya umuhimu wa daraja la Mbuchi kukamilika kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu kutokana na hali adha wanayoipata wananchi wa maeneo hayo kwa hivi sasa.
Hawa ni wananchi wa kijiji cha Mbwera wakivuka kwa kutumia Mtumbwi kuja kijiji cha Mbuchi kwa ajili ya shughuli mbalimbali hii ni kutokana na kukosekana kwa daraja linalounganisha vijiji hivyo lakini kwa sasa Ujenzi wa daraja hilo umeanza na utakamilika baada ya mwaka mmoja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akimskiliza Meneja wa TARURA Wilaya ya Kibiti kuhusu maendeleo ya Ujenzi wa Daraja la Mbuchi.

Zanzibar to Organize a Half Marathon race to Promote Gender Mainstreaming, Attain Sustainable Development Goal

$
0
0
More than 300 Zanzibari  women, men, girls and boys are expected to participate in the race ZANZI HALF scheduled to take place on February 4th, 2018 in Stone Town in the Isles.
ZANZI HALF is an international standard sporting and cultural event featuring a half marathon of 10 km and 5 km distances to be staged for the first time in the East African archipelago of Zanzibar with ethe view to highlighting women's empowerment and gender equality. 
The race is a response to the 2030 agenda for sustainable development with a call out for action in the world, and is organized by the local interfaith women´s program Upendo Means Love and the Danish NGO and running community Right to Movement in collaboration with ZIFF, Zanzibar International Film Festival (ZIFF) and Zanzibar Amateur Athletic Association (ZAAA). 
Women and girls are at the very heart of the agenda in an acknowledgement that their participation is crucial as a pre-condition for the achievement of sustainable development, says one of the organizer,Ms Lotte Bredholt. The race will bring together women and men from the grass root level united in a movement that will translate into further action, transforming gender norms by challenging existing traditional roles, taboo and break down stereotypes showing women and girls as active agents of change and peace. However, sustainability and equality is only achievable if women and men work together.

WAZIRI MKUU AAGIZA MAAFISA KILIMO WASAMBAZWE

$
0
0
*Ataka takwimu za kahawa ziwe tayari ifikapo Feb. 28

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Mji na Wilaya za Mbinga wahakikishe kuwa wanaunda kanda za kilimo na kuwasambaza maafisa kilimo wao badala ya kuwaacha wakae maofisini.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Ijumaa, Januari 5, 2018) wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja na Halmashauri ya Mji wa Mbinga, kwenye ukumbi wa Jumba la Maendeleo, mjini Mbinga.

“Mkurugenzi wa TC na DC chuja maafisa kilimo ulionao na uhakikishe wanabakia watatu tu. Abaki DALDO, mtu wa horticulture na mthamini, wengine wote wasambaze kwenye kanda ili wasimamie wakulima wakiwa huko huko. Hili litekelezwe na Mkuu wa Wilaya ulisimamie” alisema.

Aliwataka maafisa kilimo wa zao la kahawa waende vijijini na kufanya sensa ili waweze kubaini wana wakulima wangapi wanaozalisha kahawa. “Afisa kilimo wa wilaya lazima ujue kijiji kina wakulima wangapi wa kahawa, na wana ekari ngapi? Na katika ekari hizo, ana miche mingapi? Hii itaisaidia Serikali ijue inahitaji dawa za aina gani, mbolea kiasi gani na miche mingapi kwa wakulima wake,” alisema.

“Ninataka hizi takwimu ziwe zimekamilika ifikapo tarehe 28 Februari, mwaka huu,” alisisitiza.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia mche wa Kahawa, wakati alipotembelea kituo cha utafifti wa zao la kahawa (TACRI) kilichopo kwenye kijiji cha Ugano Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Dkt. Deusdedit Kilambo. Januari 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kitalu cha miche ya Kahawa, wakati alipotembelea kituo cha utafifti wa zao la kahawa (TACRI) kilichopo kwenye kijiji cha Ugano Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Dkt. Deusdedit Kilambo na katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme Januari 5, 2018
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia kahawa kwenye mashine ya kusagia kahawa, wakati alipotembelea kiwanda cha kahawa cha Mbinga Coffee kilichopo Mbinga Mjini Wilayani Songea, Mkoani Ruvuma, kushoto ni Meneja Uzalishaji Rabiel Ulomi na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. Januari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia sampuli za kahawa kwenye, wakati alipotembelea kiwanda cha kahawa cha Mbinga Coffee kilichopo Mbinga Mjini Wilayani Songea, Mkoani Ruvuma, kulia ni Meneja Uzalishaji Rabiel. Januari 5, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na Watumishi wa Halmashauri ya Mbinga, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma. Januari 5, 2018.

 KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YA KUTANA NA WADAU WA SANAA KUJADILI KUHUSU SUALA LA MAVAZI KWA WASANII

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na Wadau wa Sanaa (hawapo pichani) kuhusu nini kifanyike kwa mavazi ya wasanii sababu ya kuwepo kwa wasanii wengi wanaovaa mavazi yanayokiuka na maadili ya kitanzania katika kikao chake na wadau mbalimbali wa Sekta ya Saana nchini kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam, kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo na Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza (kulia).
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wadau wa Sanaa (hawapo pichani) kuhusu Sheria ya Filamu nchini inayosema lolote linalotoka nje ya nchi,Michezo ya kuigiza na kazi yoyote ya kisanii inayotengenezwa hapa nchini kusawili hali halisi ya kitanganyika, katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Kulia) kujadili nini kifanyike kutokana na kuwepo na mmomonyoko wa maadili katika mavazi kwa wasanii.

Katibu wa Shirikisho la Muziki Tanzania ambaye ni Mwanamuziki Mkongwe John Kitime akisisitiza kuwepo kwa Kampeni ya Kitaifa kusisitiza suala la mavazi yenye kulinda utamaduni wetu katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) kujadili suala la mavazi kwa wasanii na taifa kwa ujumla.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini Stara Thomas akichangia mada ya kuhusu mavazi ya heshima kwa wasanii nchini katika kikao kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani).Na Anitha Jonas – WHUSM

RAIS DKT MAGUFULI AMJULIA HALI MZEE KINGUNGE HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

$
0
0

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali  mwanasiasa mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika wodi ya Mwaisela, hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam akitibiwa majeraha baada ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam.
Hali ya Mzee Kingunge inaendelea kuimarika
 

PROF.NDURU AWAAGA BoT KWA UJUMBE MZITO

$
0
0

*Baadhi ya wafanyakazi washindwa kuvumulia watokwa machozi,
*Mwenyewe asema Gavana Prof Luoga ni mtu sahihi,apewe ushirikiano

Said Mwishehe Globu ya jamii

HATIMAYE Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Profesa Benno Nduru ameagwa rasmi na wafanyakazi wa benki hiyo ambapo baadhi yao wakajikuta wanashindwa kuvumilia kiasi cha kutokwa machozi huku mwenyewe akitumia nafasi hiyo kuacha ujumbe mzito kwa wafanyakazi na Gavana mpya wa BoT, Profesa Floranc Luoga.

WAFANYAKAZI BoT WATOKWA MACHOZI

Wafanyakazi wamesema Prof.Nduru amekuwa Gavana wa BoT kwa miaka 10 na sasa amemaliza muda wake na kukabidhi nafasi hiyo kwa  Prof.Luoga ambaye kwa mujibu wa ratiba ataanza rasmi kazi Jumatatu ya keshokutwa.

Hivyo wafanyakazi wa BoT waliamua kuandaa sherehemu maalumu kumuaga Prof.Nduru na kisha kumkaribisha rasmi Prof.Luoga. Sherehe hizo zilifanyika katika ukumbi uliopo kwenye benki hiyo juzi.

Kwa sehemu kubwa katika tukio hilo wawakilishi mbalimbali wa BoT wamepata nafasi ya kumzungumzia Prof.Nduru namna ambavyo amefanya kazi zake kwa uzalendo mkubwa na alitoa nafasi ya kuwapa nafasi wafanyakazi kila mmoja kuonesha uwezo wake katika eneo analofanyika kazi.

Pia wamemuelezea namna ambavyo amerudisha heshima ya BoT ambayo wakati anaingia ilikuwa imeanza kupoteza heshima.Wafanyakazi hao hawakusita kuelezea namna  alivyomakini na mwenye kutumia weledi kutekeleza majukumu ya benki hiyo kwa maslahi ya nchi na Watanzania wote.

Hata hivyo wimbo rasmi wa kumuaga Prof.Nduru ulisababisha baadhi ya wafanyakazi kushindwa kuvumilia.Maneno yaliyokuwa yanaelezwa dhidi ya namna alivyoishi nao BoT na sasa anawaacha yalikuwa na ujumbe wenye kugusa moyo wa kila aliyekuwepo ukumbini.


WAZIRI MKUU AKEMEA MADUDU USHIRIKA MBINGA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa Mbinga Mjini, kwenye mkutano wa hadhara aliyouitisha kwenye Uwanja wa Michezo Mbinga Mjini Wilayani Songea, Mkoani Ruvuma. Januari 5, 2018.

*Aagiza uchunguzi ufanyike kuanzia leo, maafisa wa MBICU, MBIFACU kikaangoni
*Apiga marufuku ununuzi wa kahawa kwa mfumo wa MAGOMA
*Aitisha kikao cha wadau wa kahawa Dodoma Jan. 14

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amebaini madudu kwenye Vyama Vikuu vya Ushirika vya Mbinga (MBICU na MBIFACU) na kuagiza uchunguzi ufanyike kuanzia leo.

“Nikiondoka hapa jukwaani, viongozi wote wa zamani na wa sasa waripoti kwa Mkuu wa Wilaya, na OCD hakikisha ofisi za chama hazifunguliwi hadi kesho asubuhi (leo) kazi itakapoanza, ili wasije kubadilisha nyaraka kwenye ofisi yao. Timu yangu ya uchunguzi iko hapa Mbinga, kesho waende wote kwenye ofisi hizo,” alisema huku akishangiliwa na wananchi.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Ijumaa, Januari 5, 2018) wakati akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mbinga, kwenye viwanja vya CCM, mjini Mbinga.

“Natambua kuwa MBICU ilishakufa ikiwa na madeni makubwa na mkaunda tena MBIFACU, ambayo nayo inasuasua, lakini viongozi wote hawa watafutwe, waje waonane wa timu  yangu na waeleze fedha za chama zimeenda wapi na kama walizikopea zilifanya nini,” alisisitiza.

Alisema timu hiyo ya uchunguzi itakiangalia chama hicho na kukifumua chote, na wote wakaobainika kuhusika watachukuliwa hatua za kinidhamu. “Tunataka MBICU na madeni yenu yaliyoko kwa Msajili wa HAZINA yajulikane, tunataka turudishe hoteli yetu, mashamba yetu na majengo yetu,” alisema.

CCM YATEUA WAGOMBEA UBUNGE KINONDONI NA SIHA

$
0
0
UCHAGUZI WA MARUDIO KATIKA KATA NNE ZA MANZASE (CHAMWINO), KIMAGAI (MPWAPWA), ISAMILO (MWANZA) NA MADANGA (PANGANI)
PAMOJA NA MAJIMBO YA SIHA (KILIMANJARO) NA KINONDONI (DAR ES SALAAM)
____________________


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kuujulisha umma wa wanachama wa CCM kuwa kimepokea taarifa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa kutakuwa na uchaguzi wa marudio katika Kata na Majimbo yaliyotajwa hapo juu. 

Wanachama wote wenye sifa za msingi kwa mujibu wa Katiba ya Nchi na waliokidhi vigezo vya uanachama kwa mujibu wa Katiba ya CCM na Kanuni zake wanahamasishwa kujitokeza ili kuomba ridhaa ya Chama kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi huu wa marudio isipokuwa na kama inakavyoelekezwa na taarifa hii. 

Aidha Chama kimejipanga kufanya kampeni za kistaarabu na kisayansi, na zilizosheheni siasa za hoja na zinazojikita katika kushughulika na shida za wananchi na hatimaye kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huu wa marudio. Kwa maana hii, msisitizo unawekwa kwa wanao omba ridhaa ya kugombea, vikao vya uchujaji na mapendekezo, na vikao vya uteuzi kuzingatia Misingi ya Maadili na kuhakikisha waombaji wana akisi uaminifu, uadilifu, uchapakazi, heshima kwa watu, ukubalifu wa imani, siasa na itikadi ya CCM, nidhamu kwa chama na wawe watu ambao umma wa wananchi unawatambua kwa nafasi yao katika jamii inapokuja katika kushughulika na shida zao.


RAIS DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI MZEE KINGUNGE NGOMBALE MWIRU PAMOJA NA WAGONJWA WENGINE WALIOLAZWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali mwanasiasa mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa kwa ajili ya matibabu katika Wodi ya Mwaisela iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akiwajulia hali watoto wawili Mapacha walioungana Maria na Consolata ambao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)kwa ajili ya Matibabu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akisali pamoja na watoto wawili Mapacha walioungana Maria na Consolata ambao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)kwa ajili ya Matibabu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa Mohamed Janabi pamoja na wafanyakazi wengine wa Taasisi hiyo mara baada ya kutembelea wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wapishi wanaofanya kazi ndani ya Hospitali ya Muhimbili wakati akitoka kuona wagonjwa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Kaka wa Profesa Anna Tibaijuka ajulikanye kwa jina la Richard Kajumulo ambaye amelazwa katika Wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na manesi wanaohudumia wagonjwa katika Wodi ya ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Nasoro Rashid aliyelazwa katika Wodi ya ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali mzee Hamadi Lila aliyekuwa akilia kwa furaha mara baada ya kumuona Rais alipofika katika wodi ya Sewahaji.

PICHA NA IKULU

MBUNGE WA CHALINZE MH. RIDHIWANI KIKWETE AONGOZA MAZISHI YA MWENYEKITI WA KIJIJI CHA HANDOGO CHALINZE

$
0
0
TANZIA 

Jana Tarehe 5 Januari 2017 Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Rhidhiwani Kikwete ameshiriki Ibada ya Msiba wa Rafiki yake na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Hondogo, Kata ya Mandela,Halmashauri ya Chalinze Ndg. Omar Ramadhani. Mh. Ridhiwani amesema Hakika ni Msiba mkubwa sana kwake na wana Chalinze na Mungu amlaze Mahala pema Peponi. Marehemu Omary Ramadhani, Amin.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Rhidhiwani Kikwete akishiriki kuomba dua katika msiba wa marehemu Omary Ramadhani.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Rhidhiwani Kikwete akishiriki kuomba dua katika msiba wa marehemu Omary Ramadhani.
Baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wakishiriki katika mazishi ya Marehemu Omary Ramadhani.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete na Baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wakishiriki katika mazishi ya Marehemu Omary Ramadhani.
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiweka mchanga katika kaburi wakati wa mazishi ya Marehemu Omary Ramadhani.

WAZIRI UMMY AKABIDHI MIFUKO 200 YA SARUJI KWA SHULE YA SEKONDARI MAWENI.

$
0
0
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga katikati akipokea cheti cha kutambua mchango wake kusaidia maendeleo ya Jiji la Tanga kutoka kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi kushoto ni Diwani wa Kata ya Maweni,Joseph Calvas 
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi kulia akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wao katika kuinua sekta ya elimu kwenye Kata ya Maweni Diwani wa Kata hiyo kushoto Joseph Calvas 
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi katika akimshukuru WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga kulia kwa kusapoti elimu katika Jijini hilo baada ya kupokea mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya Sekondari Maweni 
Afisa Elimuy Sekondari Jiji la Tanga,Lusajo Gwakisa akizungumza na waandishi wa habari ambapo walimshukuru WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga kulia kwa kusapoti elimu katika Jijini hilo baada ya kupokea mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya Sekondari Maweni 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga akisaini kitabu cha wageni katika shule ya Sekondari Maweni Jijini Tanga katikati Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Ramadhani Posi.

PROF.ELISANTE AFANYA ZIARA MKOANI MOROGORO.

$
0
0
Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel afanya ziara ya kikazi mkoani Morogoro na kutembelea kiwanda cha 21 Century pamoja na kiwanda cha Abood Seed Oil Industry Ltd vyote vya mjini Morogoro.

katika hotuba yake Prof. Elisante amesifu utendaji wa kazi wa viwanda hivi na kluwataka kuongeza juhudi ya uzalishaji wenye tija na kuthamini wafanyakazi.

Katibu Mkuu ameeleza kuwa Serikali inapenda kuona muelekeo mzuri wa Viwanda kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025 hivyo ni jukumu la wenye Viwanda kuongeza uzalishaji wenye tija ambapo kwa upande wa serikali kazi yetu ni kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji na kuondoa vikwazo vya kufanya shughuli.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel akiangalia pamba iliyosokotwa kushoto kwake ni ndugu Gevaronge Miyombe, Mchumi Wizara ya Viwanda na kulia kwa katibu mkuu ni ndugu Deus Rwegasira Msimamizi Mkuu, Idara ya Usokotaji katika kiwanda cha 21 Century cha mjini Morogoro.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel akiangalia mashine ya usokotaji wa nyuzi pembeni ni ndugu Deus Rwegasira, Msimamizi Mkuu -Idara ya Usokotaji katika kiwanda cha 21 Century cha mjini Morogoro.
Wafanyakazi wa kiwanda cha 21 Century cha mjini Morogoro

WANANCHI WA GAIRO WAFURAHIA UJENZI WA BARABARA YA LAMI

$
0
0

Wananchi wa Wilaya ya Gairo wametoa shukrani zao za pekee kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuweza kuwawezesha kupata barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 3.5.

Hayo yamezungumzwa na Kata ya Magoweko mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa ziara ya viongozi wa wilaya ya Gairo walipofanya ukaguzi wa barabara hiyo ambayo kwa sasa ipo hatua za mwisho kumalizika."Wana Gairo tunapenda kutoa shukrani zetu kwa Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli kwani barabara ya lami ni muujiza hatukuwahi kuota kama itatokea," walisema wakazi hao.

Viongozi hao ambao ni Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Shaidi Mchembe, Mbunge wa Gairo Mhe. Ahmed Shabiby, Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Bw. Shabani Sajilo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Meneja TARURA. Bw. Simon, Wajumbe KUU (W) nk walifanya ziara hiyo kufuatia mvua kubwa zinazoendelea Wilayani.

Aidha dhumuni rasmi la ukaguzi huo ilikuwa ni kuhakikisha ujenzi huo unaisha kwa wakati ambapo barabara inatakiwa kukabidhiwa Januari mwaka huu.Barabara hiyo ni matokeo ya ahadi ya aliyekuwa Waziri wa Ujenzi ambaye kwa sasa ni Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa Gairo miaka mitatu iliyopita kwenye mkutano wa hadhara ambao Mgeni Rasmi alikuwa rais wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.


Mkuu wa Wilaya Gairo, Mhe. Siriel Shaidi Mchembe (aliyevaa kiti jekundu la drafti) akimuonyesha Mbunge wa Gairo Mhe. Ahmed Shabiby madhara ya miundombinu kwa mvua zinazoendelea kunyesha Wilayani humo.
Mbunge wa Gairo, Mhe. Ahmed Shabiby, akielezea hali ya barabara kwasasa na jinsi ilivyokuwa zamani.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Bi. Agnes Mkandya akifafanua jambo.
Kaimu Meneja wa Tanroads Mkoa wa Morogoro, Kilian akielezea jambo mbele ya viongozi wa wilaya ya Gairo walifika kutembelea barabara hiyo kujionea eneo lililoadhiriwa na mvua..

Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini Tanzania (TARURA), Gairo Bw. Simon akielezea jambo wakati wa ziara hiyo. Pembeni kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Shaidi Mchembe na (wa kwanza kulia) ni Mbunge wa Gairo, Mhe. Ahmed Shabiby wakiwa na viongozi wengine.

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AZINDUA UMEME KISIWA CHA FUNDO PEMBA LEO

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiondoa kipazia kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Mradi wa Usambazaji wa Umeme katika Kisiwa cha Fundo kisiwani Pemba ikiwa katika shamra shamra za sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika kisiwa hicho huko Fundo Wilaya ya Wete.(Picha na Ikulu) .
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akiwahutubia Wananchi wa Kisiwa cha Fundo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Umeme.(Picha na Ikulu).

MAKAMU WA RAIS MSTAAFU DKT. BILAL AFUNGUA BARABARA YA FUONI MELI TANO KWARARA ZANZIBAR WAFANYIKA

$
0
0
Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Muhammed Gharib Bilal alipokata utepe kuashiria kufungua Barabara ya Kilomita Mbili ya Fuoni Meli Tano Kwarara.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.kushoto yake ni Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Baloz Ali Abeid Karume.
Barabara ya Fuoni Meli Tano Kwarara yenye urefu wa kilomita mbili iliofunguliwa na Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Muhammed Gharib Bilal.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Muhammed Gharib Bilal akikunjuwa kitambaa kuashiria kufungua Barabara ya Kilomita Mbili ya Fuoni Meli Tano Kwarara.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria katika Ufunguzi wa Barabara ya Kilomita Mbili ya Fuoni Meli Tano Kwarara.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Baloz Ali Abeid Karume akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Barabara ya Kilomita Mbili ya Fuoni Meli Tano Kwarara.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Muhammed Gharib Bilal akisisitiza jambo alipotoa hotuba ya ufunguzi wa Barabara ya Kilomita Mbili ya Fuoni Meli Tano Kwarara.Ikiwa Shamra Shamra za Maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

MAGAZETI YA JUMAPILI LEO JANUARY 7,2018

CCM YAWAHAMASISHA NA KUWAUNGA MKONO WANAFUNZI WA UALIMU (DUCE) WANAOJITOLEA KUFUNDISHA KATIKA SHULE ZA SERIKALI

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeipongeza Kamati ya Wanafunzi wanaojitolea kufundisha katika shule za Serikali na wanaosomea Masomo ya Ualimu katika Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu (DUCE) pamoja na Uongozi wa Tawi la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) chuoni hapo.

Kamati hiyo ya Wanafunzi wanaojitolea kufundisha katika shule za Serikali imekuwa na utaratibu wake mahususi ambapo wanafunzi wanaosomea ualimu Chuoni hapo hufundisha masomo mbali mbali ikiwamo yale ya Sayansi, Hisabati, na Uchumi katika shule za Serikali kuanzia shule za msingi na sekondari.

Awali akitoa neno la utambulisho na ufunguzi Mwenyekiti wa Kamati ya Wanafunzi wanaojitolea Ndg. Emijidius Cornel alieleza ushirikiano ambao wameupata kutoka kwa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na kwamba walichukua hatua hiyo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za ujenzi wa Taifa katika sekta ya elimu zinazofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Uongozi wa Ndg. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Naye Mwenyekiti wa Tawi la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg. Tweve Enock la Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) alipongeza Kamati ya Vijana wanaojitolea na kufafanua programu hiyo ya kujitolea ni sehemu ya mipango ya Tawi la Chama chuoni hapo kuunga mkono uharakishaji wa utekelezaji wa Sera za CCM na Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2015-2020.





DC WA MONDULI AKAGUA MIRADI MBALIMBALI NA KUTEMBELEA ENEO LILILOPATWA NA MAFURIKO

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Bw.IDD HASSAN KIMANTA, mapema jana Januari 06/2018 amefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo ya Tabia nchi katika wilaya ya Monduli. Miradi hiyo ina thamamani ya Tsh.705,360,698. Miradi ambayo imetekelezwa ni pamoja na Mradi wa Maji, Majosho ya kuogeshea mifugo, Mradi wa Mnada wa Kisasa wa kuuzia mifugo, Mradi wa kupunguza athari za Mafuriko. 

Mbali hivyo, mkuu wa wilaya alitembelea eneo lililopatwa na mafuriko yaliyo sababishwa na uchafu wa migomba iliokatwa na kutupwa hovyo. Hivyo amepiga marufuku kwa wakulima wa migomba kutotupa migomba kwenye mkondo wa maji ambao unakwenda kuziba madaraja na kuamuru aliesababisha adha hiyo kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mh.Idd Hassan Kimanta akikagua Mradi wa Majosho ya kuogeshea mifugo
Mradi wa Kisima cha maji ukiwa umekamilika
Mkuu wa wilaya alitembelea eneo lililopatwa na mafuriko yaliyo sababishwa na uchafu wa migomba iliokatwa na kutupwa hovyo.
Viewing all 110104 articles
Browse latest View live




Latest Images