Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU AHIMIZA KILIMO CHA KAHAWA

$
0
0
*Asisitiza kahawa iuzwe kwa mfumo wa ushirika
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wananchi wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wajikite kwenye zao la kahawa ili wawe na zao mbadala la biashara.

Ametoa wito huo leo (Ijumaa, Januari 5, 2017) wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Lipokela na vijiji jirani, wilayani Songea mara baada ya kukagua shamba la kahawa la Aviv Tanzania lenye ukubwa wa hekta 1,990.

“Limeni kahawa ili mpate fedha sababu zao hili ni la biashara. Kahawa ni miongoni mwa mazao matano ya biashara ambayo Serikali ya awamu ya tano imeamua kuyawekea mkazo ili yaweze kuongeza tija kwa wakulima na kuinua uchumi wa Taifa”.

“Tumeamua kuweka mkazo kwenye mazao matano ya pamba, kahawa, chai, korosho na tumbaku kwa sababu yanaleta tija na kuliingizia Taifa fedha za kigeni,” alisema na kuongeza:

“Tumefanya tathmini na tumegundua udhaifu mkubwa mkubwa katika usimamizi wa mazao haya ndani ya Serikali kuanzia ngazi ya Halmashauri.”
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifafanuliwa jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Molam Tanzania Limited, Medappa Mg, wakati alipotembelea Shamba la Kahawa la AVIV lililopo kwenye kijiji cha Lipokela Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, Waziri Mkuu yupo Mkoani Ruvuma  kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Januari 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipewa ufafanuzi wa miche ya Kahawa,  na mkulima wa zao hilo wakati akikagua kitalu cha miche ya kahawa katika Shamba la Kahawa la AVIV lililopo kwenye kijiji cha Lipokela Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, Waziri Mkuu yupo Mkoani Ruvuma  kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Januari 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi miche ya Kahawa, Mkulima wa zao hilo, Remigius Njovu,i nayotolewa bure na Kampuni ya Molam Tanzania Limited, kwa wakulima wa zao la Kahawa, baada ya kukagua kitalu cha miche ya kahawa katika Shamba la Kahawa la AVIV lililopo kwenye kijiji cha Lipokela Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, Waziri Mkuu yupo Mkoani Ruvuma  kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Januari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi miche ya Kahawa, Mkulima wa zao hilo, Remigius Njovu,inayotolewa bure na Kampuni ya Molam Tanzania Limited, kwa wakulima wa zao la Kahawa, baada ya kukagua kitalu cha miche ya kahawa katika Shamba la Kahawa la AVIV lililopo kwenye kijiji cha Lipokela Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, Waziri Mkuu yupo Mkoani Ruvuma  kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Januari 5, 2018. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BALOZI MTEULE WA UFARANSA AWASILISHA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frédéric Clavier.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frédéric Clavier baada ya Mhe. Balozi kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho. Wawili hao pamoja na mambo mengine walizungumzia masuala ya uwekezaji ambapo Ufaransa inahitaji kuongeza uwekezaji wa makampuni yake hapa nchini ili kuunga juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Ujumbe wa Wizara ulioshiriki mazungumzo hayo. Kutoka kulia ni Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Bi. Mindi Kasiga; Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. Jacob Msekwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Balozi Mteule wa Ufaransa wakiendelea na mazungumzo yao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiteta jambo na Balozi Mteule wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frédéric Clavier mara baada ya wawili hao kubadilishana mawazo kuhusu namna ya kuimarisha uhusiano baina ya nchi zao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Ufaransa nchini Tanzania, Mhe. Frédéric Clavier wa pili kutoka kushoto. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia) na Naibu Balozi wa Ufaransa, Bw. Alexandre Peaudeau.

MKURUGENZI WA NURU FUNERAL SERVICES PAUL BEDA MOSHI AFARIKI DUNIA

$
0
0
TANZIA
Familia ya Bwana Paul Beda Moshi inasikitika kutangaza kifo cha baba yao mpendwa Paul Beda Moshi Mkurugenzi wa Nuru Funeral Services, kilichotokea siku ya Jumatano tarehe 3/1/2018.

Ibada ya kuuga mwili wa marehemu itafanyika siku ya Jumapili tarehe 7/1/2018 nyumbani kwake Kawe Mlalakuwa karibu na viwanja vya Lugalo Golf Club jijini Dar es Salaam, mazishi yatafanyija siku ya jumatatu ya tarehe 8/1/2018 nyumbani kwake Rombo Tarakea Mbomai.

Bwana ametoa Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe.

Kwa mawasiliano zaidi na jinsi ya kufika piga +255714270410 na +255713775238

RC WANGABO AZIAGIZA KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA KUSIMAMIA USAMBAZAJI WA PEMBEJEO.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezitaka kamati za ulinzi na usalama ngazi ya Mkoa kushirikiana na za Wilaya kusimamia usambazaji wa mbolea ili kufikia malengo ya kuzalisha chakula kwa wingi katika mkoa baada ya kutokea upungufu wa mbolea za kupandia (DAP) na za kukuzia (UREA) katika Mkoa.

Ameagiza hayo katika kikao cha kutafuta suluhisho la upatikanaji wa mbolea Mkoani Rukwa baada ya taarifa za upatikanaji wa mbolea hizo kutoridhisha hasa katika kipindi hiki cha msimu wa kilimo ambapo asilimia 80 ya wananchi wa Mkoa wa Rukwa wanategemea kilimo kujipatia kipato cha kujiendesha Kimaisha.

Amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya kilimo ilichukua hatua za makusudi kubadili mfumo wa ruzuku uliokuwa ukiwafaidisha wakulima wachache kupitia vocha za pembejeo na hatimae kupitia mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) iliweka mfumo wa uuzaji na usambazaji wa mbolea kwa uagizaji wa pamoja na kutoa bei elekezi kwa kila Halmashauri.

Ameongeza kuwa hali ya upatikanaji wa mbolea Mkoani Rukwa si ya kurudhisha na kubainisha kuwa hadi kufikia tarehe 3/1/2018 Mkoa umepokea mbolea ya kupandia (DAP) tani 3,746.6 kati ya tani 47,869 upungufu ni tani 44,122.9 na mbolea ya kukuzia (UREA) tani 2,599.6 kati ya mahitaji ya tani 49,669 na kuwa na upungufu wa tani 47,069.4.

“Ndugu zangu hivi sasa tuko vitani, na adui yetu ni upatikanaji wa pembejeo, kwahiyo hapa Mkoa mzima tuungane tuwe kitu kimoja, tulidhibiti hili jambo, haya ni maagizo mbolea yoyote inayokuja hapa katika ngazi ya Mkoa, kamati ya ulinzi na usalama lazima isimamie, sio suala la Sekretariet hya Mkoa peke yake, lazima tujue kama mbolea hiyo imefika ama la,” RC Wangabo alisisitiza.

Aidha amewataka mawakala wa mbolea Mkoani humo kuhakikisha wanaagiza mbolea ya kutosha kutoka nje ya mkoa ili wasambazaji wadogowadogo waweze kuisambaza mbolea hiyo katika vijiji vya halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa.

Akiwawakilisha mawakala wa usambazaji wa mbolea mkoani humo Mmiliki wa Kampuni ya usambazaji Ikuwo General Enterprises Sadrick Malila amesema kuwa upungufu mkubwa uliopo ni upatikanaji wa mbolea ya kukuzia (UREA) na sio mbolea ya kupandia (DAP) ambayo mpaka sasa ana tani 200 katika ghala lake peke yake, na kuiomba serikali kuongeza shilingi 1000 katika bei elekezi ili kufidia usafirishaji wa mbolea hizo.

Mmoja wa Wakulima waliohudhuria katika kikao hicho Godfrey John ameiomba serikali kwa kushirikiana na mawakala hao kuongeza kasi ya upatikanaji wa mbolea hiyo ili kunusuru maisha ya wanarukwa wanaotegemea kilimo kujikimu kimaisha.

Kwa msimu wa 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulilima Hekta zipatazo 556,975.9 na kuvuna tani 1,109,055.6 za mazao ya chakula kati ya hizo mahindi yalikuwa tani 710,602. Kwa msimu huu wa Kilimo wa 2017/18 Mkoa  umelenga kulima jumla ya eneo la Hekta 554,310.6 na kuvuna tani 1,669,746.2 za mazao ya chakula.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na wadau wa kilimo Mkoa wa Rukwa (hawapo kwenye picha) katika Kikao kilichowajumuisha Wataalamu wa kilimo ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Kamati za ulinzi na usalama ya Mkoa na Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wao, Mawakala wa usambazaji wa mbolea wakubwa na wadogo pamoja na  wakulima. 

KOZI YA MULTI MEDIA ITASAIDIA KUONGEZA UFANISI KWA WAANDAAJI FILAMU NCHINI-WAZIRI MWAKYEMBE

$
0
0
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo imeahidi kuwasaidia wanafunzi wanasoma kozi ya Multi Media kupata nafasi za mafunzo kwa vitendo katika sehemu mbalimbali pale inapowawia vigumu kupata nafasi hizo.
Kauli hiyo imetolewa jana na Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipotembelea Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT) kwa lengo la kufahamu  kozi ya Multi Media inayotolewa na chuo hicho namna gani inaweza kusaidia  uandaaji wa filamu nchini.
‘’Kozi hii ya Multi Media ni moja ya masomo yanaweza kuisaidia sekta ya filamu kupata taswira mpya tofauti na ilivyosasa kwani wataalamu hawa wakitumiwa vizuri katika kuandaa filamu  za hapa nchini wanaweza kuleta mabadiliko kwani kwa sasa sekta hiyo ina changamoto kubwa ya kukosa waandaji wenye weledi’’Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza katika ziara hiyo Dkt.Mwakyembe aliwapongeza wanafunzi wa chuo hicho kwa kuonyesha weledi pale walipokuwa wakijibu  maswali waliyoulizwa  kuhusiana na namna wanaweza kuboresha uandaaji wa filamu ambapo wanafunzi watatu tofauti walijibu kwa ufasaha.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) akipongeza uongozi wa chuo cha Teknolojia Dar es Salaam kwa kuaandaa vijana wenye weledi katika uandaaji wa filamu alipotembelea chuo hicho  jana jijini Dar es Salaam kwa lengo la kukutana na wanafunzi wanaosoma kozi ya Multi Media,kutoka kulia ni Mkuu wa Chuo cha DIT Prof.Preksedis Ndomba na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Bibi. Joyce Fissoo (kushoto).
 Mkuu wa Chuo cha DIT, Prof.Preksedis Ndomba (kulia) akitoa taarifa ya maendeleo ya kozi ya Multi Media inayotolewa na chuo hicho inavyoweza kusaidia sekta ya filamu kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) alipotembelea chuo hicho jana jinini Dar es Salaam kujionea namna kozi ya Multi Media inaweza kusaidia sekta ya filamu katika uandaaji.
 Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Bibi Joyce Fissoo akiuliza swali kwa baadhi ya wanafunzi wanasoma kozi ya Multi Media katika Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (hawapo pichani) namna gani wanaweza kuboresha uandaaji wa filamu, katika ziara ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) chuoni hapo jana jijini Dar es Salaam (watatu kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha DIT Prof.Preksedis Ndomba.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe(wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT) jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea chuo hicho kwa ajili ya kufahamu kozi ya Multi Media inavyoweza kusaidia sekta ya Filamu nchini, na wapili kulia ni Mkuu wa Chuo cha DIT Prof.Preksedis Ndomba pamoja na  Katibu Mtendaji  Bodi ya Filamu nchini Bibi Joyce Fissoo (wapili kushoto). Na Anitha Jonas –WHUSM

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Msemaji wa Jeshi la Polisi afanya ziara BBC

$
0
0
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Barnabasi Mwakalukwa akiagana na meneja wa ushirikiano wa BBC Media Action, Agnes Kayuni mara baada ya kumaliza mazungumzo na watendaji wa BBC Media Action leo alipo watembelea ofisini kwao kwa lengo la kuimarisha ushirikiano. (Picha na Jeshi la Polisi)
Studio Meneja wa shirika la utangazaji la BBC, Peter Mfalila akimuonesha Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Barnabasi Mwakalukwa namna studio ya BBC Dar es salaam inavyofanya kazi. (Picha na Jeshi la Polisi

ZIARA YA MWENYEKITI WA CCM WILAYA YA UBUNGO LUCAS MGONJA

$
0
0
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya UbungoLucas Mgonja akizungumza na viongozi wa Wilaya hiyo katika Mkutano wa ndani uliofanyika jana katika Kata ya Msigani wilayani humo, ikiwa ni sehemmu ya ziara yake ya kuimarisha uhai wa Chama. Kushoto ni Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo Salum Kally
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo Lucas Mgonja akishauriana jambo na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo Salum Kally wakati wa kikao hicho
 Katibu wa UVCCM Kata ya Msigani Reinhard Chicano akisalimia baada ya kutambulishwa
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Msigani Godlove Mondo akifungua kikao hicho
 Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Ubungo Mbarouk Masoud akifanya utambulisho wa viongozi waliofuatana na Mwenyekiti Mgonja kwenye kikao hicho
 Wajumbe kwenye kikao hicho wakishangilia jambo kuliunga mkono.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, DK. HAMISI KIGWANGALLA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA TFS

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ameugiza uongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kukabidhi eneo la Kilomita za mraba 25,000 kutoka kwenye Hifadhi ya Msitu wa Morogoro unaosimamiwa na wakala huyo kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Makao Makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Ametoa agizo hilo jana akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani Morogoro ambapo alimuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi kuzikutanisha taasisi hizo ndani ya siku saba zijazo ili kukamilisha mchakato wa kumega eneo hilo na kukabidhiwa kwa Mamlaka hiyo ili taratibu za ujenzi ziweze kuanza.


Aidha, ameuagiza uongozi huo wa TFS kuweka vigingi vya mpaka katika eneo la hifadhi hiyo ya msitu ndani ya siku 30 zijazo huku akitoa muda huo huo kwa wananchi wote waliovamia eneo hilo kuondoka mara moja kwa hiari yao wenyewe kabla ya kuondolewa kwa nguvu.


Katika hatua nyingine, Dk. Kigwangalla amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala hiyo, Prof. Dos Santos Silayo kukabidhi mbao zaidi ya 400 zilizokamatwa hivi karibuni mkoani Morogoro baada kuvunwa kinyume cha Sheria kwa uongozi wa Mkoa huo ili zisaidie kutengeneza madawati ya shule za msingi.


Pamoja na mbao hizo amemuagiza pia mtendaji huyo kukabidhi kwa uongozi wa mkoa huo magunia 350 ya mkaa yaliyokamatwa katika kituo cha Tazara yakiwa yanasafirishwa kinyume cha Sheria ili yasambazwe kwenye shule za Sekondari mkoani humo.


Dk. Kigwangalla alitoa maagizo hayo jana wakati akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Morogoro inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Dk. Steven Kebwe, ambapo alimuomba kusimamia zoezi hilo la ugawaji kikamilifu ili walengwa waweze kufikiwa.



Katika ziara hiyo ametembelea pia bonde la Kilombero ambalo ni chanzo kikubwa cha maji yanayotengeneza Stieglers Gorge ambapo Serikali ya awamu ya tano itajenga mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa megawatts 2100.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pilia kulia) akisalimiana na viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, muda mfupi baada ya kuwasili makao makuu ya mamlaka hiyo mkoani Morogoro jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pilia kulia) akisalimiana na viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, muda mfupi baada ya kuwasili makao makuu ya mamlaka hiyo mkoani Morogoro jana.
Dk. Kigwangalla akizungumza na watumishi wa TAWA wakati wa ziara hiyo.

DKT MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

$
0
0
Na Mathias Canal, Mbeya

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa amemuagiza Mrajis Mkuu wa Maendeleo ya Ushirika nchini kuanza uchunguzi mara moja kwenye SACCOS ya Wakulima wa mpunga Madibila iliyoko Wilayani Mbarali, Mkoani Mbeya ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya Watendaji waliohusika na upotevu wa fedha pamoja na matumizi mabaya ya madaraka.

Mhe Mwanjelwa alitoa agizo hilo Jana Disemba 4, 2018 wakati akipokea taarifa ya kilimo ya Wilaya ya Mbarali akiwa katika ziara yake ya kikazi Wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe Reuben Mfune alimueleza Mhe Mwanjelwa kuwa katika SACCOS ya Madibila kumekuwa na hasara kubwa kutokana na matumizi mabaya ya madaraka kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika.Hivyo alimuomba Naibu Waziri kuwachukulia hatua za kinidhamu haraka viongozi wote waliosababisha hasara kwenye vyama hivyo vya ushirika baada ya uchunguzi kufanyika katika kipindi cha siku 14.

Aliongeza kuwa taarifa ya ukaguzi iliwasilishwa kwa Mrajis wa vyama vya ushirika kwa barua Kumb Na. MDC/C.20/10/89 tarehe 23/01/2017 lakini mpaka sasa hazijachukuliwa hatua zozote za kinidhamu jambo ambalo linafifihisha shughuli za wananchi kujipatia maendeleo endelevu.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Mbarali wakati wa ziara yake ya kikazi kukagua shughuli za maendeleo, Jana Januari 4, 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe Reuben Mfune mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya siku moja, Jana Januari 4, 2018. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mbarali mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya siku moja, Jana Januari 4, 2018. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Mbarali wakati wa ziara yake ya kikazi kukagua shughuli za maendeleo, Jana Januari 4, 2018







MAKONDA AENDELEZA FARAJA KWA WAANDISHI WA HABARI.

$
0
0

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda , Leo amehaidi Kuijengea Nyumba ya Vyumba Vinnie (4) Familia ya Mwandishi (mpiga picha) wa Magazeti ya Serikali TSN wanaochapisha Magazeti ya Habari Leo na Daily News Marehemu Athumani Hamis ambae amezikwa Leo katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam. 

Ahadi hiyo Imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TSN Dkt. Yonaz kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda ambae aliombwa kuisadia familia ya Marehemu ambayo ina watoto Wanne wanaosoma uku wakiwa wanaishia kwenye Nyumba ya kupanga kutokana na Baba yao kuugua kwa zaidi ya Miaka 10 na hivyo kushindwa kufanya kazi. 

 Dkt. Yonaz amesema Mhe Makonda kwa kutambua mchango wa tasnia ya Habari hususani waandishi wa Habari amekubali kujenga Nyumba hiyo kama kielelezo cha Kumuenzi Marehemu Athumani ambae katika Uhai wake alikuwa Mpiga Picha Mahiri wa Magazeti ya Serikali nchini. 

 Hatua hii imepokelewa kwa Furaha na baadhi ya waandishi wa Habari ambao wamesema Kitendo cha Makonda kukubali Kuijengea Nyumba Familia ya Marehemu Athumani mbali na kuwafuta Machozi ya Huzuni, Bali kimekuwa ni fundisho Tosha kwa Baadhi ya waandishi ambao walikuwa Wakimchukia Mhe Paul Makonda pasipo sababu za Msingi, na kukifananisha Kitendo hiki na Ukamilifu wa Maandiko katika vitababu vitakatifu yanayotutaka TUWAPENDE ADUI ZETU.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda (katikati) akizungumza na Mhariri Mtendaji wa  Magazeti ya Serikali TSN Dkt. Jimmy Yonaz  kulia na Kaka wa Marehemu Athuman Hamis Dkt. Ibrahim Msengi nyumbani kwake Sinza Kijiweni jijini Dar es salaam.

KASI YA MADIWANI JIMBONI KWA MCHUNGAJI MSIGWA KUJIUZULU INATISHA , YUPO KATIBU WA CHADEMA MKOA

$
0
0
Diwani  wa kata ya  Mwangata Anjelus Mbogo kushoto   akizungumza na  wanahabari  leo  baada ya  kujiuzulu kwake wengine ni katibu kata  ya  Mwangata Tumaini Gwivaha  na aliyekuwa katibu wa mkoa wa Iringa Chadema Oscar Ndale  ambao  wote  wamejiuzulu  leo
Katibu wa  Chadema  mkoa wa Iringa Oscar Ndale  katikati  akiwa na diwani wa Mwangata  Anjelus Mbogo na katibu kata  ya  Mwangata  Tumaini Gwivaha  baada ya  kujiuzulu  leo

Na MatukiodaimaBlog.

IDADI ya  madiwani  wa  chama  cha  Demokrasia na  maendeleo  (chadema)  jimbo la  Iringa  mjini  kujiuzulu  imezidi  kuongezeka   na  kufikia madiwani  saba   sasa  baada ya watatu kujiuzulu ndani ya  wiki  hii pamoja  na katibu  wa chadema mkoa  wa Iringa  Oscar Ndale  .

wakati diwani wa Kwakilosa na Ruaha  walijiuzulu kwa pamoja    juzi diwani  wa Mwangata  Anjelus Mbogo alijiuzulu leo   pamoja na  katibu  wa mkoa  wa  chama  hicho  na katibu  kata  wa  Chadema Mwangata  Tumaini Gwivaha .


wakitangaza  azma  ya  kujiuzulu  kwao nafasi hiyo   mbele ya waandishi  wa  habari  Mbogo  na  Ndale  walisema   kuwa  kujiuzulu  kwao kumetokana na mahusiano mabaya  ya  kufifisha maendeleo  kwenye kata  yake pamoja na mabavu  ya  viongozi w juu wa Chadema .

kati  yake na  viongozi wa  juu wa Chadema  hicho akiwemo  mwenyekiti wa kanda ya  Nyasa Mchungaji  Peter  Msigwa  ambae  ni  mbunge wa   jimbo  la  Iringa mjini pamoja  na  uongozi wa juu wa Chadema  ukiongozwa na mwenyekiti  wake  Taifa Freeman  Mbowe.


"  Vyama  vya  siasa  vipo  vingi  kuna  CUF , ACT  Wazalendo  na  CCM  hivyo  nitachagua  ni  chama gani  kitanifaa  kufanya  siasa  zangu ila  hata  CCM nipo  tayari  hakuna  ubaya "

Alisema  kuwa  mbunge Msigwa  amekuwa  akimfanyia  diwani  mwenzao Joseph Lyata figisu  figisu toka  akiwa naibu meya  wa Manispaa ya  Iringa na  hofu ya mbunge  Msigwa  ni baada ya  kuhisi kuwa anautafuta  ubunge wa  jimbo  hilo mwaka  2020 .

Diwani  Mbogo alisema  kwa  sasa atabaki  mwanasiasa   huru  na  iwapo  mbunge  Msigwa na mstahiki meya  Alex Kimbe wataondoka  hata  leo  chadema basi atarejea  Chadema  ila  kama   wataendelea  kubaki hatarudi  kamwe .

Kwa  upande  wake aliyekuwa  katibu  wa Chadema  mkoa ,Ndale  alisema  kuwa kuyumba  kwa chadema  Iringa mjini  kumesababishwa na mbunge   kutokuwa na ushirikiano mzuri  na  wenzake na mara  kadhaa  wamekuwa  wakimuonya ila  bado  anaendelea  na kuwa  Mbowe pia  amesababisha  kujiuzulu kwake  nafasi hiyo  na  kwa  sasa  atajiunga na  CCM .

Ndale  alisema aliomba kujiunga na  CCM na amekubaliwa na  hivyo ataendelea na  Siasa  kupitia CCM huku akisema uhai  wa Chadema  Iringa  mjini  umefika  mwisho .

Kwa  upande  wake Joseph Lyata  aliyekuwa  diwani kata ya  Kwakilosa  alisema siasa ndani ya  Chadema kwake  imemshinda hivyo ameamua  kuondoka  ndani ya  chama  hicho na  kuwa  mwanasiasa  huru .

Msimamizi  wa  uchaguzi jimbo la Iringa  mjini  Omary  Mkangama ambae  ni kaimu  mkurugenzi wa Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa amethibitisha  kupokea  barua  za madiwani watatu ndani ya  wiki  hii  kutoka  Chadema  ambao  wamejiuzulu nafasi zao Tandesy  Sanga wa kata ya  Ruaha , Joseph  Lyata kata ya Kwakilosa na Anjelus Mbogo  wa kata ya Mwangata  .

"  Kwa  mujibu wa  sheria  nitamuandikia barua mstahiki  meya  ili  yeye  aweze   kumwandikia waziri mwenye   dhamana  ambae ataijulisha   tume  wa Taifa ya  uchaguzi  ili  taratibu  nyingine  zifanyike "

Alisema  jimbo la  Iringa  linazo kata 18   kati  ya  madiwani hao CCM  ina madiwani  watano  pamoja na yule wa  Kihesa  aliyepita  bila kupingwa  itakuwa na madiwani  sita   huku  Chadema   itabaki na madiwani  9.

WIZARA YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA FAMILIA YA NGUZA VIKING (BABU SEYA) KURUDI KWENYE ANGA YA MUZIKI WAO

$
0
0

 Naibu Waziri wa Habari Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Studio ya Wanene na Wasanii Nguza Viking , Papii Nguza (Papii Kocha ) kwa ajili ya kurekodi mziki wa Live katika Studio Wanene.
 Msanii wa Muziki wa Dansi Nguza Viking akizungumza na Waandishi wa  Habari mara Baada ya kufanya Mazungumzo na Uongozi wa Wanene Studio na Naibu Waziri.
 Mwanamuziki wa Muziki wa Dansi Papii Kocha akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea Studio za Wanene na kufanya Mazungumzo  na mkurugenzi wa Studio na Naibu Waziri wa Habari Sanaa na Michezo Juliana Shonza
  Naibu Waziri wa Habari Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, akiteta na Mkurugenzi wa Wanene  Studio wakati wa mazungumzo  ya Kufanikisha wasanii hao kurekodi katiKa Studio hizo
Wasanii   wa  muziki wa Muziki wa Dansi Papii Kocha na Gunza Viking wakiwa wanatoka katika Studio za Wanene Mikocheni Dar es Salaam
--

RC Wangabo aziagiza kamati za ulinzi na Usalama kusimamia usambazaji wa pembejeo.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezitaka kamati za ulinzi na usalama ngazi ya Mkoa kushirikiana na za Wilaya kusimamia usambazaji wa mbolea ili kufikia malengo ya kuzalisha chakula kwa wingi katika mkoa baada ya kutokea upungufu wa mbolea za kupandia (DAP) na za kukuzia (UREA) katika Mkoa.

Ameagiza hayo katika kikao cha kutafuta suluhisho la upatikanaji wa mbolea Mkoani Rukwa baada ya taarifa za upatikanaji wa mbolea hizo kutoridhisha hasa katika kipindi hiki cha msimu wa kilimo ambapo asilimia 80 ya wananchi wa Mkoa wa Rukwa wanategemea kilimo kujipatia kipato cha kujiendesha Kimaisha.

Amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya kilimo ilichukua hatua za makusudi kubadili mfumo wa ruzuku uliokuwa ukiwafaidisha wakulima wachache kupitia vocha za pembejeo na hatimae kupitia mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) iliweka mfumo wa uuzaji na usambazaji wa mbolea kwa uagizaji wa pamoja na kutoa bei elekezi kwa kila Halmashauri.

Ameongeza kuwa hali ya upatikanaji wa mbolea Mkoani Rukwa si ya kurudhisha na kubainisha kuwa hadi kufikia tarehe 3/1/2018 Mkoa umepokea mbolea ya kupandia (DAP) tani 3,746.6 kati ya tani 47,869 upungufu ni tani 44,122.9 na mbolea ya kukuzia (UREA) tani 2,599.6 kati ya mahitaji ya tani 49,669 na kuwa na upungufu wa tani 47,069.4.

“Ndugu zangu hivi sasa tuko vitani, na adui yetu ni upatikanaji wa pembejeo, kwahiyo hapa Mkoa mzima tuungane tuwe kitu kimoja, tulidhibiti hili jambo, haya ni maagizo mbolea yoyote inayokuja hapa katika ngazi ya Mkoa, kamati ya ulinzi na usalama lazima isimamie, sio suala la Sekretariet hya Mkoa peke yake, lazima tujue kama mbolea hiyo imefika ama la,” RC Wangabo alisisitiza.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na wadau wa kilimo Mkoa wa Rukwa (hawapo kwenye picha) katika Kikao kilichowajumuisha Wataalamu wa kilimo ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Kamati za ulinzi na usalama ya Mkoa na Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wao, Mawakala wa usambazaji wa mbolea wakubwa na wadogo pamoja na wakulima. 


India kuendelea kuwajengea uwezo Watanzania

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) ameiomba Serikali ya India kuendelea kuwajengea uwezo watumishi wa umma nchini.

Mhe. Mkuchika amesema hayo leo katika kikao na Balozi wa India nchini Mhe. Sandeep Arya ambaye ameahidi nchi yake kuendelea kutoa ufadhili katika fani mbalimbali kwa Watanzania.

“Watumishi kujengewa uwezo katika maeneo yanayohusu TEHAMA, Afya na Viwanda yatasaidia sana nchi yetu” Mhe. Mkuchika amesema mpango wa maendeleo wa Taifa wa 2025 unatilia mkazo viwanda ili kuleta mabadiliko ya uchumi na jamii.

Balozi Sandeep Arya kwa upande wake amesema nchi yake imepanga kwa siku za usoni kuendesha warsha na mafunzo kwa njia ya kieletroniki (e-corses) ambapo katika eneo la Afya amesema ili kujenga uwezo zaidi utafanyika utaratibu wa kubadilishana wataalam wa afya kati ya nchi yake na Tanzania.

“Tunapanga pia kuleta watalaam na kutoa mafunzo hapa Tanzania” Balozi Arya amesema na kuongeza kwa mwaka huu 2018 wameongeza mafunzo kuhusu vita dhidi ya madawa ya kulevya ikiwamo matumizi na usafirishaji wake.

Imetolewa na
Florence Lawrence
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano-UTUMISHI
05.01.2018
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb), katikati, akiwa katika kikao na balozi wa India nchini Mhe.Sandeep Arya, wa pili kutoka kushoto.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb), akiwa katika kikao na balozi wa India nchini Mhe.Sandeep Arya, wa pili kutoka kushoto

WAZIRI UMMY AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO KWA KLABU YA AFRICAN SPORTS

$
0
0
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu ametoa vifaa vya michezo kwa timu ya African Sports ya Tanga yenye thamani ya zaidi ya milioni 1.5 ikiwa ni mkakati kabambe wa kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri kwenye mashindano wanayoshiriki na hatimaye kucheza ligi daraja la kwanza msimu ujao.

Makabidhiano hayo yalifanyika leo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga wakati wa ufunguzi wa timu ya wanawake ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya wilaya ya Tanga ambapo alisema vifaa hivyo vitakuwa ni chachu ya timu hiyo kuweza kufikia malengo yao.

Aliyasema hayo mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa timu hiyo katika halfa iliyoshuhudiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa klabu ya African Sports ambapo alisema dhamira yake kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inarejea ligi daraja la kwanza na ile ya Coastal Union ihakikisha msimu ujao inarudi Ligi kuu.

“Niseme tu sisi tumejipanga kuhakikisha tunazirejesha timu hizi kwenye michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara tukianzia na timu ya Coastal Union lakini ndugu zangu African Sports mhakikishe mnarudi ligi daraja la kqwanza na baadae ligi kuu “Alisema 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katikati akimkabidhi vifaa vya michezo ambavyo ni viatu Mwenyekiti wa timu ya African Sports Awadhi Salehe Pamba ikiwa ni kuipa motisha timu hiyo kufanya vizuri kwenye michuano wanayoshiriki ili waweze kufanya vizuri na hatimaye kuweza kurejea daraja la kwanza na Ligi kuu kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga,Meja Hamisi Mkoba 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Klabu ya African Sports Awadhi Salehe Pamba leo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo.


KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA SOKO LA KONDE-PEMBA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipongezana na viongozi wengine mara baada ya ufunguzi wa soko la Konde lililopo Wilaya ya Micheweni, Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Sehemu ya wananchi waliohudhuria hafla fupi ya ufunguzi wa soko jipya la Konde lililopo Konde, Micheweni,Pemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa soko la Konde lililopo Wilaya ya Micheweni, Pemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume Pemba tayari kwa ufunguzi wa soko la Konde lililopo Wilaya ya Micheweni, Pemba. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Kimbunga bomb cyclone chaikumba New York na vitongoji vyake

Rais Magufuli amteua Mhe. Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini

MTU MMOJA AFA MAJI KWENYE MACHIMBO NZUGUNI 'A'

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images