Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109922 articles
Browse latest View live

VANESSA MDEE AACHIA ALBAMU YAKE YA KWANZA

$
0
0
 Mwanamziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa albamu yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la Money Mondays itakayofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
 Msanii wa kimataifa Mohombi Nzasi Moupondo "Mohombi" akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa albamu ya kwanza ya Vanessa Mdee inayokwenda kwa jina la Money Mondays pamoja na ushirikishwaji wake kwenye baazi ya nyimbo za kwenye albamu hiyo.

MWANAMUZIKI maarufu nchini katika muziki wa Bongo Fleva Vanessa Mdee hatimaye amezindua albamu yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la Money Mondays.

Albamu hiyo imezinduliwa jijini Dar es Salaam leo na miongoni mwa wanamuziki walishuhudia sherehe za uzinduzi wa albamu hiyo ni msanii wa kimataifa Mohombi.

Kwa kukumbusha Mohombi siku za karibuni ameshinda tuzo ya kimataifa ya Grammy mwenye uraia wa Sweden na Congo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Vanessa amesema katikka albamu hiyo wameshirikishwa nyota kadhaa wa muziki akiwamo Joh Makini, Caspper Nyovest wa Afrika Kusini, Konshens wa Jamaica na nyota wa tuzo ya kimataifa ya Grammy Mohombi.

Amesema albamu hiyo ni ya kwanza kwake na tayari imeshapata umaarufu mkubwa kutoka kwa mashabiki na kutabiriwa kuwa moja ya albamu kubwa kwa mwaka 2018.

Uzinduzi  wa albamu hiyo umesimamiwa na kuratibiwa na Mikito App ambao wameonesha sapoti kubwa.”Sambamba na wadhamini wengine kama Mdee Music ,GSM Travel and Tours,Hyatt Kilimanjaro hotel na Henney”.

Pia ametumia uzinduzi wa albamu yake mpya yenye nyimbo kama Kwangu njo ailiyomashirikisha Mohombi amethibitisha ubora wa muziki wake na kipaji chake katika kuimba kwa hisia.

Vanessa Mdee kwa siku za karibuni amekuwa moja ya wasanii wakike wenye uwezo mkubwa kimuziki na amefanikiwa kutikisa katika anga la muziki wa kimataifa kupitia nyimbo zake kadhaa.

Wakati akiwa leo ndio ameizindua albamu hiyo tayari imeshaana kutajwa kuwa moja ya albamu bora ambazo zilikuwa zikitarajiwa na mashabiki.

Katika kuhakikisha kila kitu kinakwenda vema , anatarajia kufanya ‘Party’ maalum leo katika hoteli ya Hyatt Dar es Salaam kwa waalikwa maalumu kwa ajili ya kuisikiliza albamu hiyo na mgeni rasmi atakuwa Mohombi.

Harmonize atoa Msaada wa Fimbo kwa Wasioona Mtwara.

$
0
0

Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Rajab AbdulKahal maarufu Harmonize ametoa Msada wa Fimbo30 kwa Chama cha Wasioona Kilichopo Mkoa wa Mtwara Zenye Thaman ya Shilingi Million1 na Laki8 kama njia mojawapo ya kuwafariji walemavu wa macho katika kipindi hiki cha Sikukuu.

Katika Salam zake Hamornize amesema alipata taarifa ya kuwa chama Hicho kinauhitaji wa Fimbo kwa ajili ya Matumizi ya Kutembelea hivyo kuamua Kuleta Fimbo hizo ambapo Mahitaji ya Fimbo kwa kiasi kikubwa yanahitajika.

Aidha amewaomba baadhi ya Wadau wenye uwezo kujitokeza na kutoa Msaada ili kupunguza changamoto ambazo zinawakabili watu wenye ulemavu wa Macho.

Akizungumzia Kuhusiana na ziara yake Mkoani Mtwara Harmonize anasema bado Ataendelea Kutoa Msaada kulingana na anachopata na ataendelea kutembea asasi mbalimbali zenye mahitaji maalum ili kuweza Kusaidi.
 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Harmonize katika Picha ya Pamoja na chama cha watu Wasioona Mkoani Mtwara Mara baada ya kukabidhi Msaada wa Fimbo kwa walemavu wa Macho Mkoani Mtwara.
 Harmonize akimuongoza Kushuka Ngazi katibu wa Chama cha Wasioona Ally Ismail katika Makabidhiano ya Msaada wa Fimbo za kutembelea kwa watu wenye Ulemavu.


 Harmonize akiwa na Rafiki yake Sarah Akiongea na Wanachama wa Chama cha watu Wasioona kabla ya Kukabidhi Fimbo30 kwa ajili ya kutembelea.
Msanii wa Muziki wa kizazi Kipya Harmonize akimkabidhi Fimbo 30  katibu wa chama cha Wasioona Mkoani Mtwara Ally Ismail.

WATANZANIA WAOMBWA KUSHIRIKI MKESHA MKUBWA WA KITAIFA, MAOMBI MAALUMU

$
0
0
Said Mwishehe, Blogu ya jamii
WANZANIA wameombwa kushiriki katika mkesha mkubwa kitaifa ambao pia utatumika kufanya maombi maalumu kumuombea Rais John Magufuli.

Mkesha huo unatarajia kufanyika Desemba 31 mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru uliopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Askofu Dk. Godfrey Malassy  kwa niaba ya Tanzania Fellowship of Churches amesema mwaka huu ni mwaka wa pekee kwa Taifa la Tanzania kufuatia matendo makuu ambayo Mungu ameitendea nchini yetu.

“Na hasa ni kutokana na kazi njema inayofanywa na Serikali ya Awamu ya tano chini uongozi wa Rais Magufuli na wasaidizi wake wote kuonesha mwanga na dira katika usimamizi wa rasilimali zote za Taifa.

“Tunamshukuru Mungu kwamba amesikia maombi yetu Watanzania. Leo watanzania na ulimwengu mzima ni mashahidi wa Tanzania mpya yenye amani na utulivu unaotoa fursa kwa wananchi wote kufanya kazi kwa bidii na kujenga uchumi,” amesema Dk.Malassy.

Ameongeza mwaka 2017 ni mwaka wa kipekee kwa Taifa, hivyo ni fursa adhimu kwa Watanzania wote kukusanyika nchini nzima kwa sauti moja kusimama pamoja usiku wa Desemba 31 kumshukuru Mungu kwa kutuvusha mwaka huu.

“Hivyo tuombe kwa ajili ya kuukaribisha mwaka 2018. Mwaka huu tunasababu muhimu kitaifa kumuombea Rais Magufuli kwa jukumu kubwa alilokabidhiwa na kila Mtanzania kuongoza Taifa letu la Tanzania,”amesema.

Amefafanua maono ya mkesha mkubwa kitaifa utakaombatana na maombi maalum kwa Taifa umelenga Taifa liwe na amani na utulivu toka kwa Mungu wa amani aliye hai.

“Hakuna amani bila Mungu yeye ndiye mtoa amani kwa watu wote wamchao kwa kusudi lake. Mungu analokusudia na Taifa hili,”amesema.

Amesema amani ni msingi wa maisha ya mwanadamu na bila amani maisha yanakuwa magumu.

Ametaja mikoa mingine ambayo mkesha huo utafanyika Desemba 31 mwaka huu ni Dodoma, Kilimanjaro, Mwanza, Iringa, Ruvuma, Singida, Morogoro na Zanzibar
Viongozi wa kamati ya maandalizi wakiongozwa na Askofu, Dk.Godfrey Malasy(wa tatu kulia) wakizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu mkesha mkubwa kitaifa unaotarajia kufanyika Desemba 31 mwaka huu katika mikoa 10 nchini.

WAZIRI MKUU AWASILISHA TAMKO LA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema amekwishawasilisha tamko la maadili ya viongozi wa umma kwenye Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma tangu jana (Alhamisi Desemba 28, 2017).
Akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Namahema ‘A’ wilayani Ruangwa mkoani Lindi leo jioni (Ijumaa, Desemba 29, 2017), Waziri Mkuu amesema fomu hizo zilipokelewa jana na amekwishapatiwa barua ya kupokea tamko hilo.
“Nimewaita hapa ili kuthibitisha kuwa nimetekeleza takwa hilo la kisheria na tayari Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi ya Umma imekiri kupokea tamko langu kwa barua hii hapa,” alisema Waziri Mkuu huku akionyesha barua hiyo ambayo ilisainiwa na Jaji Harold Nsekela, Desemba 28, 2017.
“Kwa kuzingatia mfano ulioonyesha na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ninawaagiza viongozi wote wanaotakiwa kujaza fomu hizo kwa mujibu wa sheria wafanye hivyo na kuziwasilisha ifikapo tarehe 31 Desemba, 2017 saa 10 jioni,” alisisitiza Waziri Mkuu.
Alisema anawakumbusha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu wote na viongozi wote walioko kwenye ngazi za uteuzi wahakikishe wanatimiza takwa ambalo liko kwa mujibu wa kifungu cha 9 na cha 11 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya Mwaka 1995.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwatakia Watanzania wote heri wakati wanaposubiri kumaliza mwaka 2017 na kuwatakia heri na fanaka katika maeneo waliyopo wanapojiandaa kuupokea mwaka 2018.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, DESEMBA 29, 2017.



Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akionyesha barua aliyopokea kutoka kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,wakati akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Namahema ‘A’ wilayani Ruangwa mkoani Lindi leo jioni Ijumaa, Desemba 29, 2017.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Dekula Band performs their song called Liverpool live on Flimpoman's Show.

DIAMOND AMWAGA ZAWADI KWA MASHABIKI WAKE JIJINI DAR LEO

$
0
0
Msanii Nyota wa Bongofleva Afrika Mashariki na kwingineko Diamond Platnum akimkabidhi mmoja wa masahabiki wake baada ya kujishindia manukato (pafyume) ya CHIBU,mara baada ya kushiriki promosheni ya 'nogewa ushinde' inayoendelea kuchezeshwa kupitia bidhaa yake ya Karanga,ambayo pakiti yako moja huuzwa shilingi 300/= tu . 
Msanii Nyota wa Bongofleva Afrika Mashariki na kwingineko Diamond Platnum akimkabidhi mmoja wa masahabiki wake baada ya kujishindia simu ya mkunoni aina Samsung J7,mara baada ya kushiriki promosheni ya 'nogewa ushinde' inayoendelea kuchezeshwa kupitia bidhaa yake ya Karanga,ambayo pakiti yako moja huuzwa shilingi 300/= tu . 
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya aka Bongofleva hapa nchini Abdull Nassib almaarufu kwa jina la Diamond Plutnum akiwataja washindi mbalimbali waliojinyakulia zawadi kupitia promosheni ya karanga zake iitwayo 'Nogewa Ushinde',hafla hiyo imefanyika mapema leo jijini dar na kuhudhuriwa na mashabiki wake lukuki.
Msanii Nyota wa Bongofleva Afrika Mashariki na kwingineko Diamond Platnum akimkabidhi ufunguo mmoja wa masahabiki wake baada ya kujishindia piki piki mara baada ya kushiriki promosheni ya 'nogewa ushinde' inayoendelea kuchezeshwa kupitia bidhaa yake ya Karanga,ambayo pakiti yako moja huuzwa shilingi 300/= tu . 
Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya aka Bongofleva Abdull Nassib almaarufu kwa jina la Diamond platnumz akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mapema leo jijini Dar,mara baada ya kugawa zawadi mbalimbali kwa washindi wa promosheni inayoendeshwa kupitia karanga zake (diamondkaranga) inayoitwa 'nogewa ushinde',Diamond Platnumz amemwaga zawadi hizo kede kede kwa washindi wa promosheni hiyo zaidi ya 30,zikiwemo  piki piki,Manukato (pafyumu ya CHIBU),simu mbalimbali

DC, MBUNGE MUHEZA WASHIRIKIANA NA WANANCHI KUANZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA HIYO

$
0
0
MKUU wa wilaya ya Muheza, Mhandisi Mwanasha Tumbo,Mbunge wa Jimbo hilo,Balozi Adadi Rajab na wakazi wa wilaya hiyo wakishirikiana kwa pamoja wameanza kuchimba msingi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya katika Kijiji cha Lusanga Kata ya Lusanga ambayo itasaidia kuondoa changamoto ya kutokuwepo kwa kipindi cha miaka 37.

Hatua ya viongozi hao ina lengo la kuandika historia tokea wilaya hiyo ilipoanzishwa mwaka 1974 ambapo wananchi walikuwa wakitegemea kupata huduma za matibabu kwenye hospitali ya Teule Muheza kutoka maeneo mbalimbali kabla ya kufikiria kuanzishwa kwa hospitali hiyo ambayo itakayogharimu zaidi ya bilioni 11.

Akizungumza wakati akishiriki zoezi la uchimbaji wa mtaro wa Hospitali hiyo na kupokea mifuko ya saruji 600 ya Lucky kutoka kwa Kampuni ya kuzalisha Saruji ya Kisarawe, Mhandisi Mwanasha alisema waliamua kufanya hivyo kutokana na kuwepo kwa changamoto ya huduma ya afya ambayo ilimlazimu wakati ameteuliwa kuiongozi wilaya hiyo kukutana na wadau kuweza kuona namna ya kuweka mikakati ya kupatikana kwake.

Aidha kutokana na kuwepo kwa hospitali ya wilaya walikuwa wakilazimika kutimia hospitali ya teule Muheza tokea ilipoanzishwa lakini imeonekana kuzidiwa na watu wanaohitaji huduma hasa ukizingatia pia zahanati na vituo vya afya vipo vichache huku wananchi wakiongezeka.

“Nilibaini changamoto ya hospitali ya wilaya wakati nilipokuwa nikifanya vikao kwa kuzunguka kata zote nikaona tatizo la huduma ya afya ni kubwa sana na hivyo kuonekana kuna haja ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Muheza lakini hata kwenye baraza la madiwani suala hilo lilizungumzwa”Alisema
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo akichimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya hiyo itakayojengwa eneo la Kijiji cha Lusanga wilayani humo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo Like Gugu wakishuhudia tukio hilo.
Mbunge wa Jimbo la Muheza,Balozi Adadi Rajabu akichimba mtaro kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo eneo la Lusanga wilayani humo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo,Like Gugu
Sehemu ya wananchi wakishiriki katika uchumbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA


MBUNGE MGIMWA AKABIDHI MIFUKO 400 YA SARUJI NA BATI 150 KWA AJILI YA UJENZI NA UKARABATI WA MAJENGO YA SHULE NA ZAHATI ZA KATA YA MAPANDA

$
0
0

Na Fredy Mgunda,Mufindi.

Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa amekabidhi jumla ya mifuko ya saruji 400 na bati 150 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa madarasa ya shule za msingi pamoja na zahati za Kata ya Mapanda kwa lengo la kuboresha maendeleo ya wananchi wa jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, alisema kuwa niliomba kuwa mbunge kwa lengo la kuwatumikia wananchi hivyo najitahidi huku na kule kuhakikisha natimiza azma yangu ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa jimbo la Mufindi Kaskazini.

“Nimetoa jumla ya mifuko ya saruji 400 na bati 150 kwa ajili ya kuhamasisha ujenzi na ukarabati wa madarasa katika shule na zahati za kata hii ikiwa ni mwamzo tu nitaendelea kutoa saruji nyingine na bati hata vitu vingine ili kulifanya jimbo la Mufindi Kaskazini kupata maendeleo kwa kasi” alisema Mgimwa

Mgimwa alisema kuwa halmashauri ya Mufindi imeshaanda mpango kabambe ambao utakuwa msaada mkubwa kuchochoe maendeleo kwa kasi huku serikali ikiendelea kufanya jitihada za kuhakikisha wananchi wanapata maji ya kutosha na kuitumia vizuri ardhi ya halmashauri hiyo kwa kufanya maendeleo.
Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa akiwa na diwani wa kata ya Mapanda Obed Kalenga na mwenyekiti wa kijijicha Ihimbo wakati wa kueleza vitu gani ambavyo amevifanya kwenye kata hii kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa kata ya Mapanda 
Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa akiwa kwenye moja ya darasa ambalo litakarabatiwa kutumia mfuko wake wa jimbo ili liwe kwenye kiwango kinachotakiwa 
Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua majengo ya shule na kuangalia majengo yapi yanastahili kukarabatiwa
Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa akiwa kwenye moja ya zahati ambayo inatakiwa kufanyiwa ukarabati ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa kata ya Mapanda.



DKT MWANJELWA ATOA SIKU MOJA KWA WAFANYABIASHARA WALIOFUNGA MAGHALA YA MBOLEA LA SIVYO KUNYANG'ANYWA LESENI

$
0
0
Na Mathias Canal, Morogoro

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa leo Disemba 29, 2017 amewaagiza wafanyabiashara wa mbolea kote nchini walioweka mgomo wa kupeleka mbolea kwa wakulima kufikia 30 Disemba 2017 wawe wamefungua maghala yao kwa ajili ya kuwauzia mbolea wakulima.

Alisema endapo wafanyabiashara hao wasipofanya hivyo serikali itawanyang'anya leseni zao haraka iwezekanavyo ili kuruhusu wafanyabiashara wenye uwezo wa kufanya jukumu hilo pasina kuwaumiza wakulima kutokana na bei ghali ya mbolea.

Mhe Mwanjelwa ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) Mara Baada ya kubaini kuwa kuna wafanyabiashara ambao wameanza kufunga maghala kwa madai ya kupanda kwa mbolea katika soko la Dunia.

Alisema kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria na kuijaribu serikali kwani malalamiko yao ya kupanda kwa bei katika soko la Dunia hayana tija kwani mbolea zote zilipo nchini tayari wakishanunua kipindi soko likiwa kwenye unafuu mkubwa.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Katikati) akikagua mbegu zilizohifadhiwa ghalani kabla ya kuanza kusambazwa alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Wakala wa Mbegu Dkt Sophia Kashenge Kilenge (Kulia) na Meneja uzalishaji Wakala wa Mbegu Ndg Charles Levi (Kushoto). Picha Zote Na Mathias Canal 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Mkurugenzi Wakala wa Mbegu Dkt Sophia Kashenge Kilenge alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo baada ya kukagua baadhi ya mashine za mbegu alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua namna mbegu za mazao mbalimbali zilivyohifadhiwa alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017. 

SERIKALI KUWASHUGHULIKIA WANAOTUMIA TAKWIMU ZISIZO RASMI

NAIBU WAZIRI SHONZA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA ARUSHA

$
0
0
 Askari wa wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Majid Kijaji (kushoto) akimfafanulia   Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa kwanza kulia) kuhusu fuvu la Fisi alipotembelea hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Bi. Mery Kirombo (wa kwanza kulia) akimpatia maelezo mafupi kuhusu hifadhi hiyo  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) muda mfupi kabla ya kuanza kwa safari ya kuhamsisha utalii katika hidadhi hiyo leo tarehe 29/12/2017 mkoani Arusha. Katikati  ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Ndg. Godifrey Mngereza. Safari hiyo iliandaliawa na Taasisi ya Mtandao wa Wasanii wa  Musiki wa Njili hapa Nchini (TAGOANE)

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa pili kulia waliokaa nyuma)  akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Tengeru English Medium katika eneo la Ngurudoto Crater  alipotembelea  hifadhi ya Taifa  ya Arusha (Arusha National Park) iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017. Kushoto kwake ni msanii wa maigizo Kingwnedu na kulia kwake ni Rais wa TAGOANE Dkt. Godwin Maimu , taasisi ya TAGOANE ndiyo iliyo ratibu safari hiyo ya siku moja ya kuhamasisha utalii wa ndani nchini.
 Afisa Utalii na Masoko wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg.  Nicholaus Mahimbi (kulia) akimfafanulia  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) kuhusu mabaki ya fuvu la Nyati lililopo katika eneo la Ziwa Dogo la Momella wakati Mhe. Shonza alipotembela hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani nchini. 
 Askari wa wanyama pori wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha Ndg. Agustino Kombwa (wa kwanza kulia) akimpa maelekezo ya namna ya kupanda mlima Meru  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa kwanza kushoto)alipotembela hifadhi hiyo iliyoko mkoani Arusha leo tarehe 29/12/2017 kama juhudi za kuhaasisha utalii wa ndani nchini.Kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Ndg. Godfrey Mngereza na Dkt. Godwin Maimu Rais wa taasisi ya TOGOANE. Taasisi ya TAGOANE ndiyo iliyo ratibu safari hiyo.
PICHA NA OCTAVIAN KIMARIO-WHUSM.


MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO DECEMBER 30,2017

BURIANI ALHAJ SHEIKH AHMED ISLAM

$
0
0
Na Ramadhani K. Dau, Malaysia

Ilikuwa siku ya Jumamosi tarehe 23 Disemba 2017, majira ya saa 5 usiku kwa saa za Malaysia nilipopata ujumbe mfupi wa sms kutoka kwa Sheikh Issa Othman, maarufu Mufti wa London, Imam wa Masjid Maamur ukiniarifu msiba wa mzee wetu Sheikh Ahmed Islam. Ujumbe wake ulikuwa mfupi sana: “Mzee wetu Ahmed Islam amefariki sasa hivi. Maiti inaletwa msikitini hivi sasa. Maziko kesho In Shaa Allah. Innallillahi Wainnaillahi Raajiuun”.
Mara tu baada ya kupata taarifa hiyo na baada ya kumtakia maghfira mzee wetu, nikajua kuwa kwa mara nyingine tena umeniangukia wajibu wa kuandika Taazia ya mtu ambaye namfahamu, namheshimu na alikuwa na ukaribu sana na mimi. Nimeshawahi kuandika huko nyuma kuwa kuandika Taazia ni jambo zito na gumu sana. Kila niandikapo hutamani sana Taazia hiyo iwe ndio ya mwisho.

 Lakini kwa mipango Yake Mwenyezi Mungu, najikuta nashindwa kukwepa wajibu huo. Hata hivyo, mara hii nilidhani ningeweza kuukwepa wajibu huo kwa kumuomba rafiki yangu na ndugu yangu mwanahistoria maarufu Sheikh Mohamed Said aandike Taazia hiyo nami nilikuwa tayari kumpa maelezo yoyote ambayo yangemsaidia katika uandishi wake. Pamoja ya kuwa alikubali kuifanya kazi hiyo, Mohamed alisisitiza kuwa lazima na mimi niandike. Kwa jinsi ya msisitizo aliouweka Sheikh Mohamed, nimejikuta kwa mara nyingine tena  nalazimika kuandika Taazia hii huku nikiwa na moyo wa huzuni sana kwa kuondokewa na mzee wangu ambaye alikuwa mithili ya baba yangu mzazi.
Marehemu mzee Ahmed Islam ana mambo mengi na sura nyingi. Wapo wanaomfahamu kama ni miongoni mwa wazee maarufu na viongozi katika jamii ya Waislamu, wapo wanaomfahamu kama mtaalamu wa masuala ya Rasilimali Watu (Human Resources) na wapo wanaomfahamu mzee Ahmed Islam kama mwana michezo mahiri.
Marehemu mzee Ahmed Ijhad Islam alizaliwa Zanzibar tarehe 22 Disemba 1930 akiwa ni mtoto pekee wa Sheikh Ijhad Islam na bibi yetu Bi Maryam Mussa. Kwa bahati mbaya, mzee Ijhad Islam alifariki wakati mzee Ahmed akiwa mdogo na hivyo akalelewa na mama yake. Baada ya msiba huo, bibi yetu Bi Maryam aliolewa na kupata mtoto mmoja wa kike ambaye jina lake ni Zerah. 
Baada ya kumaliza masomo yake ya msingi na Sekondari kwenye Government School (sasa Ben Bella) Zanzibar mwaka 1948, ilipofika mwaka 1957 marehemu mzee Ahmed Islam alikwenda Cornwall, Uingereza kuchukua masomo katika fani ya Mawasiliano yaani Telecommunications. Wakati huo alikuwa ameajiriwa na kampuni ya Cable and Wireless (C&W) ambako alikuwa Meneja Msaidizi (Assistant Manager). Kampuni hii ilikuwa ndiyo kampuni kubwa ya mawasiliano Afrika Mashariki. Baada ya kurudi masomoni, marehemu aliendelea na kazi yake na baada ya kampuni ya C&W kumezwa na Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki (East African Post and Telecommunication), mzee Islam akahamia Dar es Salaam mwaka 1970. 
Akiwa Dar es Salaam mzee Islam alifanyakazi katika Shirika hilo na baada ya mgawanyiko yakaundwa Mashirika mawili tofauti; Shirika la Posta (TPC) na Shirika la Simu (TTCL). 
Marehemu mzee Islam alihamishiwa TTCL hadi alipostaafu mwaka 1986 akiwa katika nafasi ya Mkurugenzi wa Rasilimali Watu yaani Director of Manpower. Baada ya kustaafu, marehemu alifanyakazi Ubalozi wa Ufaransa kwa mkataba wa miaka 3. Wakati wa uhai wake, mzee Islam amefanya mengi katika fani mbalimbali ikiwa ni pamoja na uongozi wa dini, ujenzi wa nchi, uendelezaji wa michezo na utoaji nasaha kwa Taasisi na vijana mbalimbali katika masuala ya ndoa na kujiendeleza kwenye elimu ya juu.  
Kwa upande wa dini, marehemu ametoa mchango mkubwa sana. Miongoni mwa matunda ya kazi yake ni usimamizi wa ujenzi wa Masjid Maamur iliyopo Upanga, Dar es Salaam. 
Kwa wanaokumbuka vizuri jiografia ya Upanga, kabla 1987 pale palipojengwa Masjid Maamur hapakuwa na msikiti. Lakini kwa kushirikiana na wazee wenziwe marehemu mzee Islam aliweza kusimama kidete katika kusimamia ujenzi wa Masjid. Si wengi wanaofahamu kuwa ujenzi wa Masjid Maamur ulianza na msukusuko mkubwa kwa sababu kulikuwa na mwanajeshi ambaye alikuwa amepanga kwenye nyumba ya jirani ambayo ilikuwa inamilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Wateja wa Tigo pekee wanafurahia bonasi za bure kwa bando zote


ULEGA AHIMIZA UJENZI WA SHULE KWA WANANCHI KUJITOLEA

$
0
0


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amewataka maafisa maendeleo kutembelea vijijini ili kuhamasisha maendeleo katika kaya za vijiji kutokana baadhi vijiji kuwa nyuma kimaendeleo.

Kutofika kwa watendaji kuhamasisha maendeleo kunasababisha wananchi kuona serikali haifanyi kazi. Amesema kuwa vijiji vikiwezeshwa vitaleta maendeleo kwa haraka kwani serikali ya awamu ya tano inaitaji kusonga mbele bila kumwacha mwananchi yeyote nyuma katika ukuaji wa uchumi.

Akizungumza katika kijiji cha nyangunguti na Mkenge Kata ya Beta wilayani Mkurunga ,amesema maofisa wa maendeleo wanatakiwa kukimbizana na kasi ya maendeleo kwani muda wa kukaa ofisini umekwisha.

Amesema ili kuimarisha serikali na kumsaidia Rais Dk.John Pombe Magufuli ,watendaji wawe chachu ya maendeo kwa kuwafikia wananchi moja kwa moja. Kwa upade wa wananchi wa kijiji cha Nyangunguti wamemuomba Naibu Waziri huyo kuendelea kuhamasisha maendeleo ili vijiji vikue kwa kasi

Katika ziara ya Vijiji hivyo ameahidi kutoa Mifuko 130 ya saruji ,Mifuko 100 ikiwa ni sehemu ya kuchangia ujenzi wa shule mpya na 30 katika kijiji cha Mkenge kwa ajili sakafu ya shule ya kijiji hicho. Aidha ametoa fedha tasilimu sh.100000 kwa ajili wanafunzi yatima wa kijiji cha Nyangunguti.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Nyangunguti.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akisalimina na mmoja wa watoa huduma mara baada ya kuwasili katika Zahanati ya kijiji cha Mkenge Mkoa wa Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akionesha karatasi namna ya udanganyifu wa Korosho unaosababisha soko la zao hilo kuwa na tatizo.
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri Ulega .Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII AFANYA ZIARA KATIKA HIFADHI YA SAADANI

$
0
0
Wananchi wa Kitongoji cha Uvinje kilichomo ndani Hifadhi ya Taifa ya Saadani iliyopo wilayani Bagamoyo Mkoani wa Pwani wamesema hawapo tayari kuhama wala kulipwa fidia ili kupisha hifadhi hiyo.

Kitongoji hicho, ambacho ni kati ya vitongoji nane vya Kijiji cha Saadani, kilitakiwa kiondolewe tangu mwaka 2005 baada ya hifadhi hiyo kupandishwa daraja kutoka pori la akiba na kuwa hifadhi kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 281 la Septemba 16, 2005.

Akizungumza mbele ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Bagamoyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga wakati alipofanya ziara jana katika kijiji hicho aliwambia wananchi hao kuwa lengo la ziara yake ni kutaka kuwasikiliza juu mgogoro huo na sio kuwahamisha.

‘Mimi ni mgeni kidogo kwenye Wizara hii, Nimekuja kuangalia sio kuwahamisha kwa kuwa sijui eneo hili lina ukubwa kiasi na lina kaya ngapi lakini nimekuja kutembelea hifadhi na maeneo yote yenye changamoto. ‘’ alisema.Alisema amefika kwa ajili ya kuwasikiliza ili aweze kujua jinsi mgogoro ulivyo kwa sababu hakutaka kusikia upande mmoja wa TANAPA pekee.

Naye , Kaimu Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, Hassan Akida alisema wakazi wa eneo hilo hawapo tayari kuhama na wala kulipwa fidia kwa vile ni ardhi yao tokea enzi za mababu zao.’‘Tumesema hapa ndo kwetu mnataka kutuhamisha mtupeleke wapi wakati sisi tumezoea maisha yetu hapa’’ alisema Akida.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akioneshwa ramani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani na Mwakilishi wa Mkuu wa Hifadhi za Taifa, Vitalis Kuluka huku akishirikiana kuonesha eneo hilo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo,Erica Yigella ( wa pili kulia) mahali kilipo Kitongoji cha Uvinje ambapo wakazi wa eneo hilo wamegoma kuhama ndani ya hifadhi hiyo na wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea hifadhi hiyo jana. Wa kwanza kulia ni Afisa Wanyamapori, Godfrey Maro na Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani, Stephano Msumi na pande wa kulia nyuma ya Katibu Tawala ni Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa, Fredrick Mofulu 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( wa pili kulia ) akizungumza na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani , Stephano Msumi ( katikati) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea hifadhi hiyo jana kwa ajili ya kujionea changamoto mbalimbali zinazoikabili . Wa kwanza kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo, Erica Yigella, Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Vitalis Kuluka, wa tatu kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa, Fredrick Mofulu 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza jana na Wananchi wa Kitongoji cha Uvinje ambao wamegoma kuhama ndani ya hifadhi hiyo, wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea kwa ajili ya kuzungumza nao ili kujua ukubwa tatizo la mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka 10 sasa .
Bango lililopo katika geti la Gama linalokuelekeza sheria na taratibu ukiwa unaingia katika Hifadhi ya Taifa ya Saadani iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Year-End Highlights: JMK PARK REACHES 100,000 REGISTERED USERS IN 2017!!

$
0
0

DAR ES SALAAM, Tanzania – 29 December 2017 – Just in time to celebrate the end of 2017, Samwel Wilson Milli became the 100,000th new user to register at the Jakaya M. Kikwete Youth Park (JMK Park) on 19th December, it was announced today by the park’s Director, Mark Sequeira. This major milestone comes just in time to mark a year of exciting highlights at the facility.  In just two years since its opening, the Park, which is fully funded by Symbion Power, has become an epicenter of activity in the lives of the many young boys, girls and adults throughout Dar as Salaam.

Mr. Milli, 18 years old, and now a fan of JMK Park, is pursuing his education in economics, geography and mathematics. To mark the occasion, JMK Park gave Samwel the opportunity to show off his fancy footwork on the full pitch, by organizing an exclusive football match for him and his friends. Their team, known as “Bunju Sports” won 4-0 against ‘Mburahati FC”.  It was a first time visit to JMK Park for both U18 teams as well as the first time any of them had ever played on a professional football pitch.

Mr. Sequeira said, “JMK Park has continued to grow as a vital part of the community in Dar es Salaam. Reaching this landmark 100,000 number of registered individual users reflects the enormous impact that JMK Park has on the community and is also a testament to the commitment of a talented and highly trained staff, as well as to the wide range of free programs that are available.”

The following are a selection of highlights that took place at JMK Park during 2017:

  • Celebrated 100,000 registered individual users!

  • JMK Park hosted a wide range of events including, International Day of the Girl; Malaria International Day; World AIDS Day; Day of African Child and many more.

  • JMK Park was proud to host a visit by Olympic Gold Medalist and FIFA Women’s World Cup champion Alex Morgan and Orlando City SC midfielder Servando Carrasco of Major League Soccer who visited Tanzania in December as part of the U.S. Department of State Sports Envoys program.  They held soccer clinics and JMK Park and spoke to students from a variety of local schools.

  • Coach training development programs for more than 85 coaches with expertise in basketball, football, volleyball, hockey, and Grassroot Soccer Zinduka training.

FOOTBALL
  • Grassroot Soccer Zinduka and Skillz Girl programs provide important health and lifestyle educations to participating boys and girls.  In 2017, over 3000 kids completed the programs.

  • U16 Academy players were selected to participate with the Tanzania National Football team to compete in the CAF Gabon Tournament as well as selected U15 Academy players who were invited to train with the Tanzanian National Team and participate in the U17s AFCON Tournament to be hosted in Tanzania in 2019.

  • Launched JMK Park Football Academy and a dedicated JMK Park Girls Team.

  • The JMK Park Elite Football Academy in Association with Sunderland AFC, brought home the winning trophy from the prestigious Chipkizi Cup 2017 East African Tournament U17 Boys in Arusha for the U17s competition.

BASKETBALL
  • Jr. NBA program doubled to include 900 participating boys and girls, and a total of 60 teams, with Aga Khan Boys and Juhudi Girls winning the 2017 championship.

  • Launched the JMK Park Elite Basketball Training Academy program for U16s and U18s.  Participants were selected after open tryouts were held for kids aged 15 – 18.

  • Hosted a range of tournaments and coach training clinics including, the male/female wheelchair basketball tournament; Open Tournament where 39 teams from Kenya, Arusha, Bagomoyo participated.

  • Hosted coaching clinics and basketball camps including one with former NBA player, Hasheem Thabeet.

Paul Hinks, CEO Symbion Power said, “JMK Park has been a huge success and I am very proud to see how it has continued to grow and become part of Dar es Salaam. The fact that in just two short years 100,000 people have registered, tells us that more parks (just like JMK Park) are needed across the country. It is our hope that other firms which operate in Tanzania will also sponsor the construction of similar facilities, which help to provide much needed free programs and services.  I’d like to thank Mark and the fantastic and dedicated team of coaches and administrators for all their efforts in making JMK park what it is today.”                                                                              

The Park’s range of free sport and education programs have continued to grow and expanded into what is now a diverse time table of 16 different programs designed to engage children on and off the field with skills-based athletic coaching and lifestyle education including programs focused on HIV/AIDS and Malaria awareness.

JMK Park’s founding partners, Symbion Power and Sunderland AFC, in collaboration with the NBA, developed the non-profit facility to provide free opportunities for education and skills training of Tanzanian youth that were not previously available. These programs help to contribute to improving the daily lives of children and the community.
 Sam Milli, JMK Park's 100,000th person to register, and his Bunju Sports team play against Mburahati FC in a friendly match at JMK Park.
 JMK Park coaches shown here with post-match Bunju Sports and Mburahati FC teams where Bunju won 4-0    
 The Juhudi School Girls Jr. NBA team celebrating their 2017 Championship win.
JMK Park Director, Mark Sequeira, Samwel Wilson Milli, 18, who became the 100,000th new user to register at JMK Park and Hababuu Omar, Head Coach, Football

TRA MKOANI PWANI YANASA TANI 26 ZA MIZIGO AMBAYO ILIKUWA IKISAFIRISHWA KINYEMELA BILA YA KUWA NA RISITI

$
0
0
NA VICTOR MASANGU, MKURANGA 

MAMLAKA ya mapato (TRA) Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani imefanikiwa kukamata tani 26 za mizigo ya aina mbali mbali ambayo ilikuwa imepakizwa katika malori mawili ya magari ikisafirishwa kinyemela kutokea kariakoo Jijini Dar es Salaam kuelekea mikoa ya kusini bila ya kuwa na risiti halali kinyume kabisa na sheria na taratibu za nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa TRA Wilaya ya Mkuranga Amosie Ernest alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa baada ya kuyakamata malori hayo walipoyapekuwa waliweza kubaini kuwa yamesheheni bidhaa nyingi ambazo hazijakatiwa risiti kwa mfumo wa mashine ya kielectroniki (EFD), hivyo walikuwa wanakwepa kulipa kodi.

“Ni kweli kwa sasa tupo katika msako mkali kwa ajili ya kuweza kugagua magari yote ambayo yanabeba miigo bila ya kuwa na risiti, na katika zoezi hili tumefanikiwa kuyakamata magari mawili makubwa ambayo yalikuwa yamebebeba mzigo ambao ulikuwa na bidhaa mbali mbali na baada ya kufanya uchunguzi tuliweza kuona kuwa kuna mapungufu makubwa kutokana na wahusika kutokuwa na risiti hivyo magari tumeyakamata yote,”alisema Ernest.

Pia alisema kwamba mizigo hiyo ambayo ilikuwa inasafirishwa kutokea maeneo ya kariakoo Jijijini Dar es Salaam kuelekea mikoa ya kusini ilikuwa na mapungufu makubwa kutokana na baadhi ya mizigo mingine ilikuwa haina risiti kabisa na baadhi ya mingine ilikuwa imekatiwa risiti kwa gharama ambayo ni ndogo ukilinganisha na bei iliyonunuliwa dukani.

Kwa upande wake Afisa elimu na huduma kwa mlipa kodi wa TRA Mkoa wa Pwani Kapera Bakari amebainisha kuwa thamani ya awali ambayo wameifanya wamebaini mizigo hiyo ambayo ina jumla ya thamani ya shilingi milioni 84 imekwepa kulipiwa kodi kihalali ni zaidi ya kiasi cha shilingi milioni 16 ambazo zilitakiwa kuingia serikalini.

Aidha Kapera alibainisha kuwa serikali ya awamu ya tano kwa sasa ipo macho katika kuhakikisha inakusanya mapato yake hivyo amewaasa wafanyabiashara wote Mkoa wa pwani kuachana na tabia ya kununua mizigo dukani bila ya kuwa na risiti ya aina yoyote kwani kufanya hivyo kunachangia kwa kiasi kikubwa kupoteza mapato kutokana na tabia ya ukwepaji wa kulipa kodi kwa kutumia mashine za EFD.

Mmoja wa madereva ambaye amekamatwa kutokana na kuhusika na tukio hilo ajulikanaye kwa jina la Hamis Abibu amesema kwamba mizigo ambayo alikuwa ameipakia katika gari yake akutambua lolote kama imenunuliwa bila ya kuwa na risiti ambazo zinastahili.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkuranga Sevelini Lalika ambaye nae alifika katika eneo la tukio ameipongeza TRA kwa juhudi wanazozifanya za kumuunga Rais wa awamu ya tano Dk,John Pombe Mgaufuli katika kuhakikisha wanakusanya kodi ipasavyo na kuwabana wale wote wenye tabia ya kukwepa kulipa kodi ya serikali kwa makusudi.

MALORI hayo mawili ya magari ambayo yamekamatwa na TRA yamekutwa yamesheheni bidha mbali mbali zikiwemo mikeka, viatu, mashuka, baiskeli,sabuni, spea mbali mbali za pikipiki, zimeingiza hasara ya zaidi ya kisi cha shiingi milini 16 kutokana na kukwepa kulipa kodi kihalali.

Michuano ya Kombe la Mapinduzi Kati ya Jamhuri na Mwenge Uwanja wa Amaan Zanzibar

$
0
0
 MSHAMBULIAJI wa Timu ya Jamhuri mwenye jezi ya njano Mussa Ali na beki wa Timu ya Mwenge Haysam Khamis wakiwania mpira wakati wa mchezo wao wa Michuano ya Kombe la Mapinduzi ilioaza kutimua vumbi leo katika Uwanja wa Amaan Zanzibar
MSHAMBULIAJI wa Timu ya Jamhuri Mussa Ali akimpita beki wa Timu ya Mwenge Yussuf Ali, katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi linalofanyka katika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya Mwenge ikiongoza kwa bao 1-0 kipindi cha pili cha mchezo. Picha na Othman Maulid Mapara
Viewing all 109922 articles
Browse latest View live




Latest Images