Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110129 articles
Browse latest View live

Tamasha la Tukuza Utalii Tanzania lazinduliwa Jijini Arusha

$
0
0

Na.Vero Ignatus Arusha. 

Katibu mkuu baraza la Sanaa Tanzania amewataka wazazi na walezi wa hapa nchini kuwalea watoto na kuhakikisha kuwa wanaishi katika maadili ili kuzuia mmomonyoko wa maadili.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha la kwanza la Tanzania Tukuza Utalii Genesis 1,Godfrey Ngereza alisema kuwa tanzania imebarikiwa kwa tunu mbali mbali hivyo watanzania hawana budi kuzitunza na kuzilinda.

Aidha alisema kuwa wazazi hawana budi kuwafundisha watoto uzalendo na kuhakikisha kuwa tamaduni zilizopo haziishi."Waswahili walisema samaki mkunje Angali mbichi tukiwalea watoto vizuri ni ngumu kuona maadili yanamomonyoka kwa kuwa tutakuwa tumetengeneza watoto wema" Alisema Godfrey

Kwa upande wake Raisi wa Mtandao wa wasanii wa nyimbo za Injili Tanzania(TAGOANE)Dkt.Godwin Maimu Nnyaka alisema kuwa watoto yatima hawahitaji mavazi na chakula peke yake bali kujengewa msingi bora wa maisha yake.
Katibu mkuu mtendaji Baraza la sanaa nchini( Basata)Godfrey Mngereza akiwa anazungumza katika ufunguzi wa Tamasha hilo.Picha zote kwa Idhini ya Vero Ignatus Blog
Rais wa Mtandao wa Wasanii wa wasanii wa Muziki wa Injili Tanzania na maandili nchini Tanzania (TAGOANE) Dkt.Godwin Maimu akiwa anazungumza katika ufunguzi wa Tamasha la Tukuza utalii Tanzania lililozinduliwa rasmi Jijini Arusha.
Mgeni rasmi Katibu Mkuu mtendaji kutoka Baraza la sanaa nchini (BASATA) pamoja na Rais wa Tagoane nchini wakikata keki kama ishara ya Ufunguzi wa Tamasha la Kuza Utalii Tanzania .
Mgeni rasmi kutoka Baraza la sanaa la Taifa (Basata)Godrey Mngereza akifurahi pamoja na watoto yatima katika tamasha lililoandaliwa na Tagoane Jiiini Arusha.
Meza kuu Rais wa Tagoane,Katibu Mkuu mtendaji kutoka Baraza la Sanaa nchini (Basata)Katibu mkuu Tagoane,na wakurugenzi wa vituo vya kulelea watoto yatima Jijini Arusha.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog.


KAMPUNI YA PiMAK YAFUNGUA DUKA KUBWA LA KUUZA VYOMBO VYA MAHOTELINI JIJINI ARUSHA

$
0
0
Na Pamela Mollel,Arusha

KAMPUNI ya kimataifa ya PiMAK inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli , imefungua duka kubwa jijini Arusha kwaajili ya kuwarahisishia watumiaji wa vyombo hivyo kuvipata kwa wakati

Akizungumza katika uzinduzi wa duka hilo la kisasa Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwepo kwa duka hilo hapa Tanzania tayari ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa mahoteli

Kimambo alisema kuwa kampuni ya PiMAK kuja kuwekeza nchini itasaidia ajira lakini pia kuwainua wajasiriamali wadogo wenye ndoto ya kufika mbali.“Kuna hawa wajasiriamali wadogo ambao wanajihusisha na maswala ya upishi watapata fursa ya kutanua biashara zao kwa kuwa tayari vifaa vinapatikana kiurahisi”alisema Kimambo

Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez alisema, kampuni hiyo yenye makao yake Uturuki imeamua kufungua maduka hapa Nchini Tanzania kwaajili ya kuwarahisishia wateja wake ambao walikuwa wakiagiza vyombo hivyo nje ya nchi.

Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo katikati akifungua duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAK ambao ni watengenezaji na wauzaji wa bidhaa hiyo ,Duka hilo lilifunguliwa juzi eneo la njiro jijini Arusha,Kulia ni Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez ( Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)

Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo ambaye alikuwa mgeni rasmi akiingia katika duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAKambao ni watengenezaji na wauzaji wa bidhaa hizo ,Duka hilo lilifunguliwa juzi eneo la njiro jijini Arusha,kulia ni Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro

Kulia ni Mbunge wa Arusha Godbless Lema akiteta jambo na Mkurugenzi wa hoteli ya Gold Crest ya Mwanza na Arusha Mathias Manga mara baada ya kuwasili katika ufunguzi wa duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAK 

Meneja Mkuu wa kampuni ya PiMAK ya kimataifa inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa mbalimbali vya mapishai kwenye mahoteli akitoa maelezo kwa mteja aliyetembelea duka hilo

Muonekano ndani ya duka hilo.

Watanzania wanaoishi Saudi Arabia wakutana kwa majadiliano

$
0
0
Na Mwandishi Maalum, Saudi Arabia

Jumuiya ya Watanzania waishio Jeddah nchini Saudi Arabia ' Tanzania Welfare Society' hivi karibuni ilifanya Mkutano wa pamoja wa wanajumuiya Watanzania na Wanadiaspora. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Mgaza. Aidha, mkutano huo ulihudhuriwa na Spika Mstaafu wa Balaza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Pandu Amir Kificho ambaye alikuwa mgeni rasmi. Mhe. Pandu Amir Kificho alikuwa nchini Saudi Arabia kutekeleza ibada ya 'Umrah' katika miji ya Makkah na Madina.

Wanajumuiya walipata fursa ya kusikiliza hotuba zilizotolewa na Balozi na Spika Mstaafu wa Balaza la Wawakilishi. Vile vile waliweza kuuliza maswali na pia kutoa maoni na ushauri. 

Katika hotuba zilizotolewa wanajumuiya walisisitizwa kuwa na umoja na uzalendo kwa Tanzania. Walitakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanachangia maendeleo ya Tanzania. Habari zimeletwa na Mwandishi Maalumu wa Jeddah, Saudi Arabia. Kwa Picha na matukio mengine zaidi angalia youtube kupitia 'Prince eddycool' 
Kutoka Kushoto Afisa Utawala wa Konseli Kuu ya Jeddah Ali Mohamed, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Mgaza, Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanziabar Mhe. Pandu Amir Kificho ambaye alikuwa mgeni mwalikwa, Kaimu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio mji wa Jeddah Bw. Salim Ali Shatri.
Baadhi ya Watanzania na wanadiaspora wa Jeddah wakiwa katika picha na meza kuu baada ya mkutano.
Watanzania na Wanadiaspora wa Jeddah wakisikiliza hotuba katika hoteli ya Trident.

MLAWI-TBC YAONGEZA USIKIVU MIPAKANI

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WADAU WA SEKTA YA UWINDAJI WA KITALII NCHINI, YAONGEZEA MIAKA MIWILI YA UMILIKI WA LESENI ZA VITALU

$
0
0
Na Hamza Temba, Dodoma

Serikali imesikia kilio cha wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii nchini na kuamua kuongeza muda wa miaka miwili ya umiliki wa leseni za vitalu 95 vya uwindaji wa kitalii ambazo zilikuwa ziishe muda wake tarehe 31 Desemba mwaka huu (2017).

Uamuzi huo umefikiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati wa kikao cha majumuisho na watendaji wa Wizara hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkuano wa wadau wa sekta hiyo ulioandaliwa na Wizara hiyo mjini Dodoma jana.

Akizungumzia uamuzi huo Dk. Kigwangalla alisema, lengo ni kuwapa muda wawekezaji hao ili waweze kujiandaa na mabadiliko ya mfumo mpya wa utowaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada ikiwemo kurudisha baadhi ya gharama za uwekezaji walizoweka katika vitalu hivyo.

Awali akizungumza katika mkutano huo wa wadau Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis alimuomba Waziri Kigwangalla kuwaongezea muda wa umiliki wa leseni zao kuanzia miaka mitano au mitatu na nusu ili waweze kurudisha gharama za uwekezaji walizowekeza katika vitalu hivyo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, makambi na vifaa vyake pamoja na maji.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi na Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki (kulia).  
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla.

Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis (kulia) akiwasilisha mapendekezo yake katika mkutano wa wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada.
Mdau wa sekta ya uwindaji wa kitalii, Dk. Licky Abdallah akizungumza katika mkutano huo. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KUBENEA ATOA MILIONI 14 ZA MFUKO WA JIMBO KUJENGA VIVUKO VIWILI MABIBO

$
0
0
   Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akikabidhi fedha kwa ajili ya kulipia kivuko kilichokuwa watu wakilipishwa 200 kwa kila wakipita.
 Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akizungumza na wakazi  wa Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi, ambapo aliweza kutoa kiasi cha Shilingi Milioni 14 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja na kuamua kununua kivuko cha mtu Binafsi ili watu waweze kupita bure kuliko awali ambapo walikuwa wakilipishwa shilingi 200.
  Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea  akiwa katika mitaa ya  Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi
  Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akitembea na wakazi  wa Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi
 Mmoja ya wakazi wa mabibo akiwasilisha hoja yake kwa mbunge wa jimbo la Ubungo Saed Kubenea wakati alipofanya ziara ya kusikiliza kero za Wananchi
 Mmoja ya wakazi wa mabibo akiwasilisha hoja yake kwa mbunge wa jimbo la Ubungo Saed Kubenea wakati alipofanya ziara ya kusikiliza kero za Wananchi.

URA SACCOS YAKABIDHI VIFAA TIBA KWA HOSPITALI ZA JESHI LA POLISI

$
0
0
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijani, akikata utepe kuashiria uzinduzi na kupokea Vifaa Tiba kutoka URA Saccos
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijani akifanyiwa kipimo cha Presha na Sukari kutoka kwa Afisa Muuguzi PC Stella Sizya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Polisi Kilwa Road.
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijani  akioneshwa baadhi ya Vifaa  tiba vilivyotolewa na URA Saccos
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijani akisaini karatasi za makabidhiano ya Vifaaa na  Naibu Kamishna Azizi Mohamed ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa cha URA Saccos/

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAVUNDE AWATAKA POLISI JAMII KUUNDA VIKUNDI VYA UZALISHAJI MALI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde amewataka Vijana ambao wanashiriki katika mafunzo ya Ulinzi shirikishi kupitia Polisi Jamii kuunda vikundi vya uzalishaji mali ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato.

Mavunde ameyasema hayo leo wakati akifunga mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma.

“Pamoja na jukumu kubwa mlilonalo na ulinzi na usalama wa raia na mali zao,lakini pia mhakikishe mnatumia mkusanyiko wenu kuunda vikundi vya uzalishaji mali ili kujiongezea kipato na kutengeneza nafasi za Ajira zaidi,”amesema

Mavunde amewataka vijana hao kuyatumia vyema mafunzo waliyopata kwa kuwa waadlifu,waaminifu na wazalendo kwa Taifa lao na kusimama mstari wa mbele kuhakikisha Taifa hili linaendelea kuwa na AMANI na UTULIVU.

Naye, Kamanda wa Mkoa wa Polisi wa Dodoma,SACP Gilles Muroto amewataka Vijana zaidi kujitokeza katika Ulinzi shirikishi ili kuimarisha usalama na amani katika mkoa wa Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde akifunga mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde akisalimiana na viongozi mbalimbali alipokuwa akifunga mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde akiwa na Kamanda wa polisi Dodoma Gilles Murotop wakikagua gwaride katika ufungaji wa mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma.
Vikundi vya Ulinzi shirikishi
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde akitoa cheti kwa mmoja wa washiriki wa mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde akimvisha utambulisho mmoja wa washiriki wa mafunzo ya Ulinzi shirikishi yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI ATEMBELEA TBC-ARUSHA

$
0
0
Msimamizi wa Kituo cha kurushia matangazo ya TBC Fm na TBC Taifa cha Namanga mkoani Arusha Ndg. Joseph Nchinga (kushoto) akitoa maelekezo ya mtambo mpya wakurushia matangazo ya TBC Fm na TBC Taifa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan P. Mlawi (wa kwanza kulia) wakati alipotembelea kituo hicho kilichopo eneo la Namanga mkoani Arusha leo tarehe 28/12/2017. Kituo hicho kimekamilika na kimeongeza usikivu wa TBC Fm na TBC Taifa kwa umbali wa Kilomita 45 kwa pande zote mbili za mpakani mwa Tanzania na Kenya.
Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kanda ya Arusha Ndg. Gerald G. Uisso (kulia) akimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan P. Mlawi mtambo mpya wa kurushia matangazo ya TBC Fm na TBC Taifa wakati alipotembelea eneo ambalo mtambo huo umefungwa mtaa wa Njiro jijini Arusha leo tarehe 28/12/2017. Mtambo huo utaongeza usikivu wa TBC Fm na TBC Taifa kwa kanda ya Arusha. 
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan P. Mlawi (katikati) akimuelekeza jambo Mkandarasi wa Kampuni ya Alkan CIT Ngd. Ali Mohamedi (Kulia) wakati alipokagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi mpya za Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) zinazojengwa eneo la Njiro jijini Arusha leo tarehe 28/12/2017. Kampuni ya Alkan CIT ndiyo inayojenga ofisi hiyo ambapo ujenzi unatarijiwa kukamilia mwezi Januari 2018. Kushoto ni Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kanda ya Arusha Ndg. Gerald G. Uisso.
Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kanda ya Arusha Ndg. Gerald G. Uisso (kushoto) akimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan P. Mlawi chumba kitakacho tumika kama studio za TBC FM na TBC Taifa wakati alipo kagau maendeleo ya ujenzi wa ofisi za kanda za shirika hilo zilizoko Njiro jijini Arusha leo tarehe 28/12/2017. Bi Susan ametembelea eneo hilo kukagua hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa ofisi mpya za TBC kanda ya Arusha, ujenzi huo unatarijiwa kukamilika mwezi januari 2018.
Eneo la ofisi ya Shirika la Utangazaji la Taifa TBC linaloendelea na ujenzi lililopo Njiro mkoani Arusha. Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi.Susan P. Mlawi alitembelea eneo hilo kujionea maendeleo ya ujenzi yaliyofikiwa leo Tarehe 28/12/2017.PICHA NA 
OCTAVIAN KIMARIO-WHUSM

SERIKALI INAVYOZIDI KUBORESHA MIUNDOMBINU KWA WANANCHI WAKE.

$
0
0
 Kivuko cha zamani cha Mto Kankoko kilichopo  Wilaya ya Uvinza  mkoani Kigoma kilichokuwa kikitumika kuvusha watu, magari pamoja na mizigo kikiwa kimewekwa kando baada kuharibika mara kwa mara na kuwa kikwazo cha usafiri kwa wakazi wa eneo hilo.
Kivuko cha Kisasa katika Mto Kankoko Wilaya ya Uvinza  mkoani Kigoma kilichokuwa kikitumika kuvusha watu, magari pamoja na mizigo hii ikiwa ni jitihada za serikali  katika kuboresha huduma za jamii  .

VIONGOZI 10 WA VYAMA VYA USHIRIKA WAKAMATWE NA KUHOJIWA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evaristy Ndikilo ameagiza jeshi la polisi mkoa kuwakamata viongozi wa vikundi 10 vya usimamizi wa Korosho vilivyofanya udanganyifu kwa wanunuzi wa korosho na kufanya wafanyabiashara kutaka kususa Korosho hizo.

Akizungumza wakati wa mkutano na wadau wa korosho wilaya ya Mkuranga, Ndikilo amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya vikundi vya wakulima kuweka mawe na mchanga katika magunia ya korosho ili kupata uzito mkubwa kwa lengo la kumdanganya mnunuzi na vikundi hivyo vinapaswa kutoa maelezo juu ya Korosho wanazozipeleka katika maghala yao.

Amesema agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja kwani kufanya udanganyifu kwa zao la korosho ni kuhujumu uchumi kufuatia zao hilo kuongoza kwa kuleta fedha za kigeni na zao namba moja linaloangaliwa na serikali hivyo haliwezi kuchezewa

Amesema agizo hilo linaenda sambamba na kuwakamata wanunuzi wa korosho walioshinda mnada na kuchelewesha malipo kwa wakulima ndani ya siku 4.

"Sitachelea kumkamata yeyote atakae kwamisha mchakato wa kukuza zao hili katika mkoa wangu, walio na haki yao kulipwa walipwe stahiki zao kwa wakati na kuweza kufanya maendeleo yao.

Amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya wakulima au wasimamizi wa vikundi Wanauza korosho awali zinakua na ubora wa juu na mnunuzi anapokuja kuchukua baada ya kulipia anakuta ubora umebadilika kutoka ngazi ya juu hadi ngazi ya chini jambo linaloonesha kuna mchezo unaofanywa na viongozi na kufanya korosho ishindwe kupata soko.

Aidha ametangaza kuwa msimu wa korosho unaokuja hakutakuwa na uhifadhi usio rasmi wa korosho na korosho zote zitahifadhiwa katika maghara matatu tu kwa mkoa ili kulinda ubora wa korosho na kudhibiti udanganyifu.

Alisema tabia ya udanganyifu unayofanywa na baadhi ya vikundi ndio chanzo cha wakulima kucheleweshwa mafao yao ili kumpisha mnunuzi kujiridhisha kabla ya kulipia jambo ambalo linakwamisha maendeleo ya wakulima.

"Mtu anaehujumu wakulima wa korosho hao wanahujumu uchumi wa nchi na ni lazima wapambane na mkono wa Serikali kwani Kwa sasa zao la korosho ni miongoni mwa mazao yanayoongoza kukuza pato la taifa"alisema.

Nae Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mkuranga Abdallah Ulega amemuomba mkuu wa mkoa kuwasaidia wakulima ambao wanastahili kupata fedha zao kupatiwa kwa muda ili kuharakisha maendeleo.

Alisema Kupima korosho ndani ya muda mfupi na kubaidi kubadilika kwa ubora ni wazi kuwa  kuna jambo ambalo ni muhimu kutafutiwa ufumbuzi.

"Mimi nitashirikiana vizuri kusimamia wakulima kutafuta ufumbuzi wa uharibifu na wizi dhidi ya mazao yao kwani  wanaoumia ni wananchi ambao ndo wengi kuliko waharibifu" alisema.

Meneja mkuu wa Chama cha Msingi mkoa wa Pwani (COLLECU) Seif Upara amesema jitihada zaidi zinaendelea kuhakikisha wakulima wanapatiwa elimu zaidi kuhusu mfumo wa Stakabadhi Gharani ili kuboresha usimamizi wa zao hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evaristy Ndikilo akizungumza na watendaji wa Halmashauri ya Mkuranga na Viongozi wa chama Ushirika juu ya Korosho kuchelewa kulipwa wakulima.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga akizungumza hali halisi ya zao la Korosho.
Meneja wa Coreku, Seif Upallah akizungumza hali ya uendeshaji minada ya Korosho.
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evaristy Ndikilo akisalimiana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mkuranga Abdallah Ulega mara baada ya kuwasili katika ofisi ya  Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga.picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.

UHAMIAJI TANGA YAWAONYA VIONGOZI WA VITONGOJI NA VIJIJI VILIVYOPO MIPAKANI WANAOUZA ARDHI KWA WAGENI

$
0
0

VIONGOZI wa Vitongoji na Vijiji vilivyopo kwenye mipaka mkoani Tanga wameonywa kuacha tabia ya kuuza ardhi kwa wageni wanaofika kwenye maeneo yao badala yake hakikishe wanatoa taarifa wanapowaona watu wasiowajua ili kuweza kukomesha vitendo vya wahamiaji haramu.

Hayo yalisemwa na Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga Crispian Ngony’ani wakati akizungumza na vyombo habari ambapo alisema viongozi hao wamekuwa ni tatizo kubwa badala ya kukemea vitendo vya wahamiaji haramu lakini wamekuwa wakiwakumbatia kwa kuwapatia ardhi jambo ambalo ni kosa kisheria.

Alisema utafiti walioufanya mpakani mwa Kenya na Tanzania Horohoro wamebaini idadi kubwa ya wakenywa wameuziwa ardhi katika maeneo hayo na wanaishi nchini kinyume cha sheria huku akiwataka viongozi hao kuachana na vitendo hivyo kabla hawajakamatwa na kupelekwa kwenye vyombo vya dola.

“Tatizo kubwa viongozi wa vitongoji na vijiji badala ya kumemea uuzaji wa ardhi kinyemele hivyo napenda kutoa onyo kwao kuacha tabia hiyo kwani sisi kama idara ya uhamiaji tupo macho kuhakikisha wale wote wanaohusika na vitendo hivyo tunawachukulia hatua “Alisema.

Alisema viongozi hao badala ya kukemea uzaji wa haramu ardhi kwa wageni wao wamekuwa mstari wa mbele kuwakarabisha kwenye maeneo hayo bila kutambua kufanya hivyo ni makosa kisheria hivyo kuwaonya kuacha vitendo vya namna hiyo mara moja.

“Pindi wanapomuona mgeni au raia anauza ardhi watoe taarifa kwenye vyombo vinavyo husika ikiwemo idara ya uhamiaji tukishirikiana kwa mtindi huo tutaweza  kukomesha vitendo vya watu kuvamia ardhi yetu na kuishi kinyume cha sheria tu “Alisema Ofisa Uhamiaji huyo.

Wakati huo huo,Ofisa Uhamiaji huo alisema katika kipindi cha mwaka 2017 wamekamatwa watanzania 61 kwa kuvunja sheria za uhamiaji ambapo kosa kubwa ni kushiriki vitendo viovu vya kuwasafirisha wahamiaji hao katika maeneo mbalimbali na kuwaingiza nchini.

Alisema hasa wahamiaji ambao ni raia kutoka nchini Ethiophia
wanaonekana wana biashara kubwa sana kwa baadhi ya watu mkoani Tanga kwa kwenda nchini Kenya  kuwachukua kwa kufanya udalali na kuwapitisha kwenye njia za panya hadi kwenye maeneo wanayotaka kufika.

Aidha alisema kutokana na hali hiyo idara hiyo imeweka mikakati kabambe ya kuhakikisha wanakomesha vitendo vya namna hiyo kwa kuongeza udhibiti wa watu wanaoingia nchini kwa kushirikiana na vyombo vya vyengine vya dola.

Hata hivyo alisema katika kipindi hicho kesi 28 zimefunguliwa ambazo zilikuwa zinawahusu watanzania na zilizokuwa zikiendelea ni 10,nne zilikwisha,mbili zilifutwa na moja iko kwa wakili wa serikali na nyengine moja ipo uhamiaji.(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

Waziri Jafo avitaka vituo vyote vya Afya kutengeneza bustani za kupumzikia

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo(katikati) akikagua ujenzi wa miundombinu ya Afya katika Kituo cha Afya Makole kilichopo katika Manispaa ya Dodoma.

Nteghenjwa Hosseah, TAMISEMI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amevitaka vituo vyote vya Afya Nchini sambamba na hospital za Wilaya kutengeneza bustani ya kupumzikia kwa wagonjwa wanaosubiria matibabu katika maeneo hayo. Waziri jafo ameyasema hayo wakati akikagua Ujenzi wa miundombinu ya Afya katika Kituo cha Afya Makole kilichopo Manispaa ya Dodoma na kuutaka uongozi wa Kituo hicho kutenegenza bustani ya kisasa pamoja na kupanda miti ya kutosha ili kutunza matunzingira lakini kupendezesha eneo la hospital.

“Hili Agizo liende kwa Vituo vyote Nchini pamoja na Hospital za Wilaya zilizoko chini ya TAMISEMI kuhakikisha wanaekeleza maelekezo haya katika ameneo yote nataka hospital iwe sehemu ya kupa faraja mgonjwa kwa kupata huduma nzuri lakini pia kusubiria huduma hiyo katika maeneo yanayovutia wakati wote” Alisema Waziri Jafo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo(Kushoto) akimsikiliza Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole kuhusiana na maendeleo ya ujenzi wa kituo cha Afya.

Akikagua majengo matano yanayojengwa katika Kituo hicho cha Afya na kusimamiwa na TAMISEMI Waziri Jafo amesema ameridhishwa na Ujenzi wa miundombinu hiyo ya Afya katika Hospital ya Makole kwani umefuata ramani zilizotolewa na Wizara, unajengwa kwa ubora na uko ndani ya muda wa Utekelezaji.

“Hivi ndio ninavyotaka wataalamu wangu kujiongeza katika baadhi ya maeneo mfano hapa Mmejenga Mabara kubwa kulingana na wingi wa wagonjwa mnaowahudumia kwa siku sasa sio kwa sababu ramani imeonyesha maabara ndogo basi kila mtu anafuata hivyo hivyo ni lazima tujiongeze kulingana na mahitaji ya ameneo yetu ya huduma” Alisema Waziri Jafo.

Akizungumzia maendeleo ya mradi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole amesema Ujenzi huu umesema ujenzi wa Maabara, chumba cha Upasuaji, Wodi ya Kina Mama, Nyumba ya Mganga pamoja na Ukarabati wa Kichomea Taka utakamilika mapema mwezi February 2017 na Fedha zilizopokelewa kwa ajili ya ujenzi huo zitatosha na kukamilisha ujenzi wa miundombinu yote.

Kituo cha Afya Makole ni miongoni mwa vituo 211 Nchini vilivyopokea/vitakavyopokea Fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Afya lengo ikiwa ni kuboresha Miundombinu ya Afya ili kuweza kutoa huduma bora kwa watanzania.
Jengo la Maabara kama linavyoonekana likiwa katika hatua ya Lenta.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo(kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi(katikati) baada ya ukaguzi wa ujenzi wa miundombinu ya Afya Katika Kituo cha Afya Makole.
Ujenzi wa Chumba cha Kuhifadhia Maiti ukiwa katika hatua ya Lenta.

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA ‘DOLA’ KUANZIA JANUARI 1 MWAKA 2018

$
0
0
* WATALII KURUHUSIWA KWA KIBALI MAALUMU


Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Hali ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/18 ambapo alitoa agizo kwa vyombo vya ulinzi kuwakamata wanaowalazimisha watanzania kufanya malipo kwa Dola badala ya Shilingi, mkutano ulifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

Na Said Mwishehe,Blogu ya  Jamii
SERIKALI imepiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni ikiwamo ‘dola’ kuanzia Januari 1 mwaka 2018, na kueleza bei zote za huduma na bidhaa zitangazwe kwa Shilingi ya Tanzania.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk.Philip Mpango wakati anaelezea mwenendo wa hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/2018.

Dk.Mpango kabla ya kutoa agizo hilo,amefafanua suala la matumizi ya fedha za kigeni sambamba na Shilingi ya Tanzania nchini linasimamiwa na Sheria ya Usimamizi wa fedha za kigeni ya mwaka 1992, sheria ya Benki Kuu ya Tanzania(BoT) ya mwaka 2006, na tamko la Serikali ya mwaka 2007 kuhusu matumizi ya fedha za kigeni kulipia bidhaa na huduma katika soko la ndani.

Amesema matumizi ya fedha za kigeni sambamba na Shilingi ya Tanzania wakati wa kufanya miamala mbalimbali yanaweza kuwa na athari kiuchumi ikiwa pamoja na kudhoofisha thamani ya shilingi.

“Sheria iliyopo kwa sasa haikatazi jambo hili bali inasisitiza sarafu ya Tanzania ndio fedha halali na mtu au taasisi yoyote itakayekataa kuupokea malipo ya shilingi yetu tutachukua hatua za kisheria.

“Hata hivyo suala hili limeendelea kuwa kero kwa wananchi kutokana na ugumu wa kusimamia matakwa ya sheria.Inafahamika kuwa baadhi ya wateja wanapewa kiwango cha thamani  ya kubadilisha fedha ambacho kiko juu kuliko thamani halisi iliyoko kwenye soko,”amesema.

Ameongeza hali hiyo inaumiza zaidi mteja husika. Hivyo suala hilo linahitaji kufanyiwa marekebisho ya sheria.”Ili kukabiliana na hali kero kama hizo wakati utaratibu wa kurekebisha sheria unaendelea ,Serikali inaagiza yafuatayo kuaniza Januari 1,mwaka 2018.”
Kwa mujibu wa Dk.Mpango maagizo hayo ni bei zote nchini kutangazwa kwa Shilingi.Bei hizo zinajumuisha kodi ya nyumba za kuishi na maofisi.

Pia bei ya ardhi, gharama za elimu na afya, bei za vyombo vya usafiri na vifaa vya kieletroniki.

Amesema vyombo vya dola vihakikishe vinasimamia maagizo hayo na watakaoendelea kutoza huduma na bidhaa kwa fedha za kigeni wachukuliwe hatua.

Ameongeza kwa bei ambazo walengwa wake wakuu ni watalii au wateja wasio wakazi zinaweza kutangazwa kwa fedha za kigeni na malipo yake yanaweza kufanyika kwa fedha za kigeni.

“Bei hizo zinajumuisha gharama za usafirishaji kwenda nje ya nchi kupitia Tanzania, gharama za mizigo bandarini kwenda nje ya nchi, gharama za viwanja ndege na visa kwa wageni.

“Na gharama za hotelikwa watalii kutoka nje ya nchi.Hata hivyo walipaji wanaotumia fedha za kigeni watambuliwe kwa vitambulisho vyao kama pasi ya kusafiria na nyaraka za usajili kwa kampuni.

“Viwango vya kubadilisha fedha vitakavyotumika katika kuweka hizo bei katikka sarafu mbili viwekwe wazi na visizidi vile vya soko.

“Ifahamike kuwa ni benki na maduka ya fedha za kigeni tu yanayoruhusiwa  kupanga viwango vya kubadilisha fedha kutokana na ushindani katika soko la fedha za kigeni kupanga viwango vya kubadilisha fedha, amesema Dk.Mpango.

Ametumia nafasi hiyo kueleza mkazi yoyote wa Tanzania asilazimishwe kulipia bidhaa au huduma yeyote hapa nchini kwa fedha za kigeni na vyombo vya dola viwachukulie hatua za kisheria wale wote watakaobainika kukiuka maagizo hayo ya Serikali.

WAZIRI MPINA APOKEA RIPOTI YA KAMATI NDOGO ALIYOIUNDA KWA SIRI KUTATHMINI UTENDAJI WA SEKTA YA UVUVI KATIKA ZIWA VICTORIA

$
0
0

 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Luhaga Mpina (kulia) akipokea ripoti ya Kamati Ndogo ya kutathmini utendaji wa sekta ya Uvuvi katika Ziwa Victoria kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhandisi Bonaventure Baya anayeshuhudia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia uvuvi, Dk.  Yohana Budeba hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dodoma jana.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Luhaga Mpina(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati Ndogo ya kutathmini utendaji wa sekta ya Uvuvi katika Ziwa Victoria baada ya kukabidhi ripoti yako mjini Dodoma jana. Kushoto ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhandisi Bonaventure Baya Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi,  Dk Yohana Budeba
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Luhaga Mpina akiwashukuru wajumbe wa Kamati Ndogo ya kutathmini utendaji wa sekta ya Uvuvi katika Ziwa Victoria baada ya kupokea ripoti hiyo mjini Dodoma jana.  Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia uvuvi Dk. Yohana Budeba
Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya kutathmini utendaji wa sekta ya Uvuvi katika Ziwa Victoria,  Mhandisi  Bonaventure Baya (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya  Mifugo na Uvuvi  anayeshughulikia uvuvi, Dk Yohana Budeba mara baada ya kukabidhi ripoti yake kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Luhaga Mpina hayuko pichani Dodoma jana.

Waziri Mahiga Apokea Nakala Za Hati Za Utambulisho kutoka Kwa Balozi Mteule Wa Uturuki Nchini

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Uturuki nchini, Mhe.Ali Dovutoglu. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Desemba 2017.
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Dovitoglu ambapo alimuhakikishia kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake pamoja na kumpongeza kwa kuteuliwa kwake kwa awamu nyingine kuiwakilisha Jamhuri ya Uturuki nchini.

MAVUNDE AZITAKA TAASISI BINAFSI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI WATU WENYE ULEMAVU

$
0
0
NAIBU waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde leo amekabidhi msaada wa fimbo za kisasa thelathini (30)kwa ajili ya watu wasioona wa mkoa wa Dodoma huku akitoa rai kwa taasisi binafsi na jamii kuweka utaratibu wa kusaidia makundi yenye mahitaji.

Msaada huo umetolewa na taasisi inayojishughulisha na kutoa huduma ya mikopo(NEXT GENERATION MICROFINANCE).

Akikabidhi msaada huo Mavunde ambaye ni mbunge wa Dodoma mjini ameipongeza taasisi hiyo kwa kutumia faida waliyoipata kusaidia watu wenye mahitaji maalum jambo ambalo linapaswa kuwa chachu kwa taasisi nyingine pia.

“Ndugu zanguni mlichokifanya leo kina maana kubwa sio duniani tu bali hata mbinguni,mmeona ni busara kutumia faida mliyoipata kwa ajili ya kusaidia wenzetu wenye mahitaji badala ya kutumia kufanya party,naomba utaratibu huu usiishie leo tu bali muendelee kugusa na makundi mengine yenye uhitaji,”alisema Mavunde.

Katika kusaidia makundi hayo ameiomba pia taasisi hiyo kusaidia chama cha waandishi wa habari wa mkoa wa Dodoma ili waweze kuwa na ofisi yao inayoendana na hadhi ya makao makuu.Ametoa rai pia kwa viongozi wa chama cha wasioona mkoa wa Dodoma kuhakikisha wanagawa fimbo hizo kwa walengwa bila ya upendeleo wowote.
Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi,vijana na ajira Anthony Mavunde akimkabidhi fimbo mwenyekiti wa chama cha wasioona mkoa wa Dodoma Omari Lubuva ikiwa ni msaada uliotolewa na Next Generation Microfinance.
Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi,vijana na ajira Anthony Mavunde akiwa na baadhi ya viongozi wa chama cha wasioona mkoa wa Dodoma na meneja wa Next Generation Microfinance wakijaribu kutumia fimbo zilizotolewa na taasisi hiyo kwa ajili ya watu wasioona mkoa wa Dodoma.
Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi,vijana na ajira Anthony Mavunde akizungumza wakati wa kukabidhi fimbo kwa ajili ya watu wasioona mjini Dodoma,kushoto kwake ni mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dodoma Neema Majule na kulia kwake ni meneja wa Next Generation Microfinance Sospeter Kansapa.
Katibu wa chama cha wasioona(TLB)mkoa wa Dodoma Enock Mbawa akizungumza wakati wa kupokea msaada wa fimbo kwa ajili ya watu wasioona,kushoto kwake ni meneja wa Next Generation Microfinance Sospeter Kansapa na kulia kwake ni mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Dodoma Bill Chidabwa.

TAARIFA YA UGAWAJI WA VITALU VYA UWINDAJI WA KITALII KWA NJIA YA MNADA

Deni la Taifa Liko Chini ya Ukomo wa Hatari – Dkt. Mpango

$
0
0

Na. Paschal Dotto.

Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imewatoa hofu wananchi kuhusu uvumi wa kuongezeka kwa deni la Taifa kwamba deni hilo ni himilivu na liko chini ya ukomo wa hatari.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philipo Mpango wakati akitoa mwenendo wa hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/2018 .

Dkt. Mpango alisema kuwa katika tathimini iliyofanyika mwezi Novemba mwaka huu inaonesha kuwa uwiano wa deni hilo na pato la Taifa ni asilimia 32.5 likilinganishwa na ukomo wa asilimia 56.“Katika kuangalia ukomo wa deni hili ambao uko chini, inaonesha kuwa deni hili ni himilivu katika kipindi cha muda wa kati na muda mrefu”, alisema Dkt. Mpango.

Akieleza takwimu hizo, Waziri Mpango amesema kuwa mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, deni la Taifa lilifikia shilingi bilioni 47,823.1 ikilinganishwa na bilioni 42,552.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2016 ambapo kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 13,417.5 ni deni la ndani sawa na asilimia 28.1 na shilingi bilioni 34,405.6 ni deni la nje ambalo ni sawa na asilimia 71.9.Dkt. Mpango alisisitiza kuwa ongezeko hilo lilitokana na kupatikana kwa mikopo mipya ya nje na ndani ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maeneeleo.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa mradi wa umeme Kiwira (Kiwira Coal Mine), miradi ya uboreshaji wa huduma za maji kwa jamii, mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa kinyerezi na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege ambapo miradi hiyo itawezesha watanzania kufika uchumi wa kati wenye viwanda.“Mambo muhimu ya kujiridhisha nayo ni kwamba mikopo inayokopwa itumike katika kujenga uwezo zaidi wa kuzalisha mali na huduma nzuri kwa watanzania”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha Waziri Mpango amesema kuwa kufuatia hatua zinazochukuliwa na Serikali, ukwasi kwenye benki za biashara uliongezeka na kusaidia kupungua kwa riba ya mikopo baina ya mabenki na kufikia wastani wa asilimia 3.53 mwezi Novemba mwaka huu kutoka wastani wa asilimia 14.93 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017.

Vilevile riba za dhamana za Serikali zilishuka kutoka wastani wa asilimia 15.56 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017 hadi asilimia 8.76 mwezi Novemba, 2017 na kuongeza kuwa Serikali inatarajia kasi ya ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi itaanza kuimarika.Aidha, Dkt. Mpango amewaonya watu wanaotoa takwimu za uongo kuacha mara moja kwani wanaipotosha jamii, huku akiwataka waandishi wa habari kupata takwimu maalumu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ili kuweka takwimu sahihi.
Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Phillip Mpango akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu hali ya uchumi kwa mwaka 2017 leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dkt. Khatib M. Kazungu.

WAZIRI MPANGO AELEZEA HALI YA UCHUMI NA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2017/18

$
0
0
Na. Paschal Dotto.

Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imewatoa hofu wananchi kuhusu uvumi wa kuongezeka kwa deni la Taifa kwamba deni hilo ni himilivu na liko chini ya ukomo wa hatari.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philipo Mpango wakati akitoa mwenendo wa hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/2018 .

Dkt. Mpango alisema kuwa katika tathimini iliyofanyika mwezi Novemba mwaka huu inaonesha kuwa uwiano wa deni hilo na pato la Taifa ni asilimia 32.5 likilinganishwa na ukomo wa asilimia 56.

“Katika kuangalia ukomo wa deni hili ambao uko chini, inaonesha kuwa deni hili ni himilivu katika kipindi cha muda wa kati na muda mrefu”, alisema Dkt. Mpango.Akieleza takwimu hizo, Waziri Mpango amesema kuwa mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, deni la Taifa lilifikia shilingi bilioni 47,823.1 ikilinganishwa na bilioni 42,552.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2016 ambapo kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 13,417.5 ni deni la ndani sawa na asilimia 28.1 na shilingi bilioni 34,405.6 ni deni la nje ambalo ni sawa na asilimia 71.9.

Dkt. Mpango alisisitiza kuwa ongezeko hilo lilitokana na kupatikana kwa mikopo mipya ya nje na ndani ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maeneeleo.Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa mradi wa umeme Kiwira (Kiwira Coal Mine), miradi ya uboreshaji wa huduma za maji kwa jamii, mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa kinyerezi na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege ambapo miradi hiyo itawezesha watanzania kufika uchumi wa kati wenye viwanda.

“Mambo muhimu ya kujiridhisha nayo ni kwamba mikopo inayokopwa itumike katika kujenga uwezo zaidi wa kuzalisha mali na huduma nzuri kwa watanzania”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha Waziri Mpango amesema kuwa kufuatia hatua zinazochukuliwa na Serikali, ukwasi kwenye benki za biashara uliongezeka na kusaidia kupungua kwa riba ya mikopo baina ya mabenki na kufikia wastani wa asilimia 3.53 mwezi Novemba mwaka huu kutoka wastani wa asilimia 14.93 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017.Vilevile riba za dhamana za Serikali zilishuka kutoka wastani wa asilimia 15.56 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017 hadi asilimia 8.76 mwezi Novemba, 2017 na kuongeza kuwa Serikali inatarajia kasi ya ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi itaanza kuimarika.

Aidha, Dkt. Mpango amewaonya watu wanaotoa takwimu za uongo kuacha mara moja kwani wanaipotosha jamii, huku akiwataka waandishi wa habari kupata takwimu maalumu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ili kuweka takwimu sahihi.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Hali ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/18 ambapo alitoa agizo kwa vyombo vya ulinzi kuwakamata wanaowalazimisha watanzania kufanya malipo kwa Dola badala ya Shilingi, mkutano ulifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akitoa maelekezo kwa Benki nchini kuangalia namna ya kupunguza riba kwa wakopaji na pia kufuata vigezo stahiki kwa mkopaji ili kuondoa mikopo chechefu wakati wa mkutano kati yake na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (mbele) akiwa katika Mkutano na waandishi wa habari kuhusu hali ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/18 katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Susana Mkapa na Afisa Mwandamizi wa Wizara hiyo Bw. John Sausi wakizungumza jambo wakati wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) na Waandishi wa Habari kuhusu Hali ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/18 katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Maafisa Waandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakifurahia jambo wakati Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo aliangazia suala la hali ya Uchumi na kubainisha kuwa ni imara ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika Mashariki, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaabani (kushoto) akizungumza na wadau waliohudhuria Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) na waandishi wa habari katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam kulia.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)

Viewing all 110129 articles
Browse latest View live




Latest Images